Sitaki wanaume wenye pesa

Sitaki wanaume wenye pesa

Kiukweli siwapendi wanaume wenye pesa awana utu kabisa wamejaa kiburi sana usaliti ,dharau Awana mapenzi ya dhati kabisa kwakuwa wanajiona wanauwezo wa kupata mwanamke yoyote wamtakaye wamekuwa wakibadilisha wanawake kama nguo unakuta mwanaume mmoja ana wanawake kama wote wamekuwa chanzo cha kueneza magonjwa. Wanajiona dunia ni yakwao kwakuwa wanaweza fanya chochote kwa kutumia pesa zao

Wanatumia mapungufu ya wanawake kupenda pesa ndo maan wanawatumia watakavyo. Wanawake pigeni kazi ukiwa na kipato chako ilo gari alilokuwa nalo utakuwa nalo nyumba sijui nn vyote vinatafutwa ukitafuta na kumtegemea mungu kwa Imani anakupa na unapata mwanaume wake mstaarabu mwenye hofu ya mungu

Heri kuwa na mwanaume masikini mwenye hofu ya mungu kuliko kuwa na mwanaume tajiri mweny hofu ya shetani anakuwa kama Bata maji Kila shimo la maji lazima atumbukize miguu alafu awaridhiki
So unataka ambaye ana pesa halafu hana hofu ya shetani au nimekuelewa vibaya?!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kauli ya meanaume mcha Mungu ni mfu.
Mapenzi sio dini wala ibada.
Mapenzi ni mahaba toka moyoni.
Unapotaka mcha Mungu ni dalili ya kuogopa kutendwa so unataka likondoo lililozubaa
Doooh Umeandika Rubbish brother.
Kumcha Mungu hakumfanyi mwanaume kuwa likondoo lililozubaaa.

Ila Kama unaamini...hivyo well and good.its your choice to believe in whatever.
 
Doooh Umeandika Rubbish brother.
Kumcha Mungu hakumfanyi mwanaume kuwa likondoo lililozubaaa.

Ila Kama unaamini...hivyo well and good.its your choice to believe in whatever.
Sikulaumu hujanielewa hata kidogo
 
Hakuna mwanamke atakaye kuunga mkono.
Chezea pesa wewe.😂😂
Pole lakini.
 
Mwanaume akiwa masikini huwa anaonekana mcha Mungu, subiri zimtembelee utaona kila rangi.
Pili masikini ni muongo kwani hujifanya mpole na mnyenyekevu kumbe mazingira humfanya awe hivyo.
Bora mara mia mwenye pesa na aliyezizoea utaigundua rangi yake halisi.

NB:
Upumbavu wa wanawake wengi, na hapa lazima niseme tena ni wapumbavu.
Hawatumii akili zao kutambua mwanaume sahihi ni yupi, wengi wanasubiri kuchaguliwa tu kama mafungu ya nyanya.
 
Kuna mtu yashamkutaa huku halafu kuna mtu nilisikia akisema wanaume tusio na hela tuna gubu na hela zetu za mawazo kwahiyo hataki hata kutusikia.

huyu mwingine anatutaka sisi tusio na hela,nikukumbushe tu kuwa sisi tusio na hela bado gubu letu halijaisha na hela zetu ni za mawazo vile vile.

kwahiyo unapokuja upande huu jiandae kisaikolojia usije anza kulia lia tena,maana saivi vilio ni vile vile tofauti ni sauti,hawa wanalia kwa sauti ya kwanza,wale wanalia sauti ya pili,halafu mstari wa kule nyuma wao kilio chao sauti ya tatu,Kwaya imetimia.

Mapenzi bana usipojua unataka nini,Raha tupu yani Raha bin burdaniiiiiii.....Ngoja nikasake kilio kingne huko.
 
Upumbavu wa wanawake wengi, na hapa lazima niseme tena ni wapumbavu.
Hawatumii akili zao kutambua mwanaume sahihi ni yupi, wengi wanasubiri kuchaguliwa tu kama mafungu ya nyanya.
Wengi wanaangalia vitu vya kijinga sana
 
Sio wote lakini, wapo wanaume wenye pesa na wana mapenzi ya dhati + wanaheshimu wanawake wao.

Kuna wanaume wamepaukaa ila kwa kiburi na dharau hawajambo, so hizo ni tabia tu za mtu binafsi, haihusiani na hela
naona umeamua kunisimanga
 
Back
Top Bottom