Sitaki kuitwa nabii kwa hili

Sitaki kuitwa nabii kwa hili

lastman

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2011
Posts
402
Reaction score
226
Mimi bwana sitaki kuitwa nabii kwa hili kwa sababu nadhani kutokana na uongozi wa kifamilia, na tunaowaita wazee wa CCM wakati wa kutuchagulia rais.

Ila wakati taifa linaingia mikataba mibovu tunasahau kuna watu wazima kwa sababu mafungu ya chai yanafika.

Sasa kutokana na hila za wazee kumkata jaji, najua fika na nasema fika Bernard Membe, baba yake mdogo na Ridhiwani na mdogo wake J.Kikwete ndie Waziri mkuu anayefuata.

Gazeti la Mtanzania mwezi wa kwanza lilisema Magufuli ndo Rais na Paul Makonda kwenye bunge la Katiba alisema Samia Hassani ndio atakuwa Makamu wa Rais, na mimi nasema Benard Membe Waziri Mkuu iwapo serikali ya familia ya Kikwete Tanzania itapita.

Asante.

Team Jamiiforums
 
Mmmmh hawezi kufanya kosa Hilo hiki ni kipindi cha wachapa kazi PM atakuwa Mwakyembe ili amusaidie katika kutafsili ya sheria wakati Anaamua mambo mazito.
 
Tanzania inao MANABII wengi wa UONGO waliosemwa na Bwana Yesu Kristo.

Wapo manabii wengi wa uongo waliotabiri kwamba LAZIMA Lowassa atakuwa Rais wa JMT.

Tena wengine wakaenda mbali kwa kujiapiza kwamba kama Lowassa asipokuwa Rais wa JMT basi tuwatafute popote pale walipo tuwauwe.

Mimi nikajiuliza kama wanaamini UNABII wao, kwanini watupe taabu yote ya kuwatafuta ili tuwauwe, kwanini WASIJIUE wenyewe kuturahisishia kazi?

Halafu pia wanatuweka kwenye mtego wa kutenda jinai, kwani kwa mjibu wa sheria za JMT KUUA MTU kwasababu yeyote ile ni kosa la JINAI.
 
Tuiondoa hii fisiem madarakani,la sivyo Katiba pendezwa itarudishwa na kupitishwa hasa kwa mgombea mwenza yaani Samia Suluhu kama atakuwa makamu rais,ambaye mwanzo alikuwa makamu mwenyekiti wa BMK.ni hayo tu.
 
Mimi bwana sitaki kuitwa nabii kwa hili kwa sababu nadhani kutokana na uongozi wa kifamilia,na tunaowaita wazee wa ccm wakati wa kutuchagulia rais,ila wakati taifa lina ingia mikataba mibovu tuna sahau kuna watu wazima kwa sababu mafungu ya chai yanafika...Sasa kutokana na hila za wazee kumkata jaji,na jua fika na nasema fika Bernard membe,baba yake mdogo na ridhiwani na mdogo wake j.kikwete ndie waziri mkuu anae fata....gazeti la mtanzania mwezi wa kwanza lili sema magufuli ndo raisi,na paul makonda kwenye bunge la katiba alisema samia hassani ndo atakuwa makamu rais,na mimi na sema benard membe waziri mkuu iwapo serikali ya familia ya kikwete tanzania itapita..
asante..
team jamiiforum


Mkuu swala lako laweza kuwa la kweli . Mzee John Pombe Magufuri lazima Aibebe familia ya Mafisadi pamoja na familia ya Kikwete
 
Sitaki kua nabii pia: ccm itashinda ila membe sidhani kama atakuwepo. Huyu bw' magufuli naamini atavuruga system kubwa sana ya panga pangua
 
Membe atakuwa vp Waziri mkuu keshasema hatogombea ubunge jimboni kwake?
 
Mimi bwana sitaki kuitwa nabii kwa hili kwa sababu nadhani kutokana na uongozi wa kifamilia,na tunaowaita wazee wa ccm wakati wa kutuchagulia rais,ila wakati taifa lina ingia mikataba mibovu tuna sahau kuna watu wazima kwa sababu mafungu ya chai yanafika...Sasa kutokana na hila za wazee kumkata jaji,na jua fika na nasema fika Bernard membe,baba yake mdogo na ridhiwani na mdogo wake j.kikwete ndie waziri mkuu anae fata....gazeti la mtanzania mwezi wa kwanza lili sema magufuli ndo raisi,na paul makonda kwenye bunge la katiba alisema samia hassani ndo atakuwa makamu rais,na mimi na sema benard membe waziri mkuu iwapo serikali ya familia ya kikwete tanzania itapita..
asante..
team jamiiforum

Nabii mimi nakupinga,mimi nakuambia waziri mkuu ajaye ni Dr.Asha Rose Migiro.hutaki unaacha.
 
Mimi bwana sitaki kuitwa nabii kwa hili kwa sababu nadhani kutokana na uongozi wa kifamilia,na tunaowaita wazee wa ccm wakati wa kutuchagulia rais,ila wakati taifa lina ingia mikataba mibovu tuna sahau kuna watu wazima kwa sababu mafungu ya chai yanafika...Sasa kutokana na hila za wazee kumkata jaji,na jua fika na nasema fika Bernard membe,baba yake mdogo na ridhiwani na mdogo wake j.kikwete ndie waziri mkuu anae fata....gazeti la mtanzania mwezi wa kwanza lili sema magufuli ndo raisi,na paul makonda kwenye bunge la katiba alisema samia hassani ndo atakuwa makamu rais,na mimi na sema benard membe waziri mkuu iwapo serikali ya familia ya kikwete tanzania itapita..
asante..
team jamiiforum

Mbona Membe alishatangaza kuwa hagombei ubunge tena? Sasa huo uwaziri mkuu ataupataje?
 
......Unamaanisha Membe atakuwa Waziri Mkuu katika serikali itayaoundwa na Vyama vya Upinzani (UKAWA)?
 
Nabii mimi nakupinga,mimi nakuambia waziri mkuu ajaye ni Dr.Asha Rose Migiro.hutaki unaacha.

Dr Asharose hawezi kuwa sababu hawezi shinda jimbo lolote na PM lazima atoke miongoni mwa wabunge wa kuchaguliwa, pia kumbukeni Membe alishaaga jimboni kwake kuwa hatagombea ubunge hivyo mimi nampa nafasi kubwa Mwakyembe au Muhongo au Lukuvi mmoja wapo endapo atashinda ubunge anaweza fikiriwa but kumbukeni Magufuli hana kundi lolote nyuma yake kulingana na hali halisi ya mchakato hivyo atakuwa na nafasi ya uhuru zaidi wa kufanya maamuzi pasipo shinikizo
 
Mbona Membe alishatangaza kuwa hagombei ubunge tena? Sasa huo uwaziri mkuu ataupataje?[/QUOT


Ataupata kwa sababu ccm wamebadilisha mbinu,kwamba wazuri mkuu sio tena kiongozi wa wabunge,kwa hiyo atateuliwa hata kama hana madaraka yoyote..
 
Back
Top Bottom