Kati ya matukio ambayo sitayasahau maishani mwangu ni tukio la kuoa mwanamke mchawi mkoani Tabora ktk kijijini cha Nkinga.
Mwanamke huyu mrembo ambaye tayari nina watoto naye ni mchawi hatari aliyejificha kwenye kivuli cha ulokole huku akiwa mwanakwaya wa kwaya ya Evangelical choir ktk kanisa moja kijijini hapo.
Niligundua uchawi wa mke wangu baada ya kutonywa na rafiki yangu juu ya tabia ya kutembea nje ya mke wangu.
Nikaamua kufuatilia na kubaini ukweli ,siku niliyopanga kumhoji mke wangu juu ya tabia yake nilishangaa kuona mwili wangu unapigwa na ganzi ya hofu kuu kupindukia.
Nikawa kila ninapomwona mke wangu namwogopa kabisa,nikamfuata rafiki yangu na kumweleza juu ya tukio lote akaniambia kuwa angenipa dawa ya kupaka machoni ili njionee mwenyewe jinsi ninavyoishi na mwanamke hatari.
Siku moja nikakutana na mdogo wake na mke wangu ambaye pia huimba kwaya ktk kanisa hilo akiwa na mdogo wake wanayeimba naye,nikataka kumwomba aongee na dadake ili aache kunisaliti.
Lakini nilishangaa kuona hata yeye naanza kumwogopa pia.
Siku iliyofuata rafiki akanipatia dawa nyeupe kama unga na kunielekeza namna ya kuitumia.
Usiku baada ya kuoga niliipaka hiyo dawa machoni tulipoenda kulala ghafla nilishangaa kumwona mke wangu akigeuka na kuwa joka kubwa na la kutisha pale kitandani.
Kisha ghafla tena akarudi ktk umbo lake la awali kama binadamu na akavaa kaniki nyeusi huku lile joka likiendelea kuwepo kitandani pale.
Nilitetemeka huku mkojo ukinitoka nikajikaza kupiga kelele kama nilivyokuwa nimeonywa.
PART -TWO itaendelea ujue nini kilitokea baada ya hapo
Sent from my VFD 301 using
JamiiForums mobile app