Kinumbo
JF-Expert Member
- Dec 8, 2019
- 3,189
- 5,819
Sio jambo la kufurahisha wala kufurahia kwa hali tuliyo kuwa nayo kiujumla, kuanzia namna ya tunavyo ishi kila siku. Dunia ya sana iko mbali na kwa haraka sana ila sisi watanzania tunaonekana bado sana ama hatuko tayari kwenda vile dunia iliko fika ama inako elekea. Inashangaza sana
Napenda tujadili kuhusu teknolojia, teknolojia inaonekana kwetu sisi bado tuko nyuma sana tofauti na mataifa mengine.
Staili ya maisha tunayo ishi imetufanya tudumae kimawazo hasa katika kutatua matatizo. Leo hii hapa Tanzania asilimia kubwa ya wananchi mitaani mpaka maofisini wanazungumza ama kujadili mambo yasio na mantiki yoyote ile katika dunia ya sasa.
Unakuta asilimia kubwa ya wananchi kuanzia asubuhi mpka muda wa kulala ni kupigizana kelele na mambo ya usimba na uyanga, siasa, wanawake na umbea tu.
Kweli kwa dunia tunayoilekea bado tunajadili ujinga kama huo? Yaani tunakaa na kupoteza muda wakati wenzetu huko wanafanya makubwa kila uchwao sisi tumebaki na kejeli za kijinga huko mitandaoni.
Wapo watano sema Serikali ndio imetufikisha hapa, naam kwa asilimia kubwa ni wao na hii ni kutokana kuwepo kwa sera mbovu hasa katika sekta ya elimu.
Hawa jamaa wanajiita viongozi hawana huruma kabisa na sisi wao wanajiangalia wenyewe tu, tuachane na hao jamaa maana hawana msaada wowote kwetu.
Nauliza sisi kama sisi tumechukua hatua ipi?
Duniani kumetokea mapinduzi makubwa mno ya teknolojia ila sisi hatujui tuko wapi na tunaelekea wapi. Leo hii huko China wana barabara inapita chini ya maji ila sisi kurusha tu satellite tumeshindwa wakati Kenya na Rwanda wamemeza.
Wapo watakao sema usilinganishe China na Tanzania, naam ni sahihi kabisa ila huoni taifa lako lina rasilimali nyingi kuliko hiyo China, sasa jiulize wamefanya nn mpaka wakupite. Akili mtu wangu
Leo hii kuna ishu ya Cryptocurrency, hii kitu nadhani kwa asilimia kubwa wengi wameisikia ama kuifahamu kabisa.
Cryptocurrency hii itakuja kuwa mapinduzi makubwa kwenye masuala ya kifedha hapo baadaye, je ni wangapi wana ufahamu kuhusu hii kitu na wako tayari?
Sisi Watanzania tumekalia mambo ya kipumbavu na kuacha mambo ya msingi, hatujifunzi vitu vipya wala ata kusoma vitabu hatutaki tupo tupo tu yaani inauma sana.
Sisi watanzania tunaelewa kwamba ukimaliza kidato cha nne ama ukifika chuo kikuu baasi umemaliza kila kitu hatutaki tena kujifunza ama kupanua mawazo yetu.
Sipo hapa kuongelea habari za Cryptocurrency ila nitatolea mfano tu. Wapo wadau mbalimbali wameleta mada kuhusu hii kitu lakini matokeo yake wakaitwa matapeli hii inaonyesha ni kiasi gani baadhi ya sisi watanzania hatuko tayari kujifunza, kujifanya tunajua na kupinga kumbe ujinga tu.
Niliwahi kutana na maneno mazuri sana katika moja ya kitabu cha mwandishi Robert Kiyosaki nanukuu "The most successful people in the world are the most rejected people in the world". Sisi watanzania tumekalia kupinga, kejeli na kuto kutaka kujifunza.
Unapinga Cryptocurrency wakati huo huo unatumia internet kwa miaka ya nyuma ilikuwa ngumu kuelewa ama kuamini ishu ya internet leo hii tunaitumia.
Nini kinakufanya usiamini Cryptocurrency wakati hayo ni matokeo ya teknolojia, vipo vingi vitakuja kwenye masuala ya teknolojia.
Mwenyezi Mungu ametujalia akili ili itumike kutatua matatizo yetu sio kupinga na kujadili masuala yasio na manufaa kwetu sisi kwa sasa na hapo baadaye.
Yapo mengi ya kuyaandika ila nisiwachoshe ila tujitahidi kuwa tayari kwa mabadiliko ya dunia. Tutumie akili zetu kutatua changamoto zinazotukabili na pia tuwe tayari kujifunza sio kila kitu ni ubishi tu, asanteni.
Napenda tujadili kuhusu teknolojia, teknolojia inaonekana kwetu sisi bado tuko nyuma sana tofauti na mataifa mengine.
Staili ya maisha tunayo ishi imetufanya tudumae kimawazo hasa katika kutatua matatizo. Leo hii hapa Tanzania asilimia kubwa ya wananchi mitaani mpaka maofisini wanazungumza ama kujadili mambo yasio na mantiki yoyote ile katika dunia ya sasa.
Unakuta asilimia kubwa ya wananchi kuanzia asubuhi mpka muda wa kulala ni kupigizana kelele na mambo ya usimba na uyanga, siasa, wanawake na umbea tu.
Kweli kwa dunia tunayoilekea bado tunajadili ujinga kama huo? Yaani tunakaa na kupoteza muda wakati wenzetu huko wanafanya makubwa kila uchwao sisi tumebaki na kejeli za kijinga huko mitandaoni.
Wapo watano sema Serikali ndio imetufikisha hapa, naam kwa asilimia kubwa ni wao na hii ni kutokana kuwepo kwa sera mbovu hasa katika sekta ya elimu.
Hawa jamaa wanajiita viongozi hawana huruma kabisa na sisi wao wanajiangalia wenyewe tu, tuachane na hao jamaa maana hawana msaada wowote kwetu.
Nauliza sisi kama sisi tumechukua hatua ipi?
Duniani kumetokea mapinduzi makubwa mno ya teknolojia ila sisi hatujui tuko wapi na tunaelekea wapi. Leo hii huko China wana barabara inapita chini ya maji ila sisi kurusha tu satellite tumeshindwa wakati Kenya na Rwanda wamemeza.
Wapo watakao sema usilinganishe China na Tanzania, naam ni sahihi kabisa ila huoni taifa lako lina rasilimali nyingi kuliko hiyo China, sasa jiulize wamefanya nn mpaka wakupite. Akili mtu wangu
Leo hii kuna ishu ya Cryptocurrency, hii kitu nadhani kwa asilimia kubwa wengi wameisikia ama kuifahamu kabisa.
Cryptocurrency hii itakuja kuwa mapinduzi makubwa kwenye masuala ya kifedha hapo baadaye, je ni wangapi wana ufahamu kuhusu hii kitu na wako tayari?
Sisi Watanzania tumekalia mambo ya kipumbavu na kuacha mambo ya msingi, hatujifunzi vitu vipya wala ata kusoma vitabu hatutaki tupo tupo tu yaani inauma sana.
Sisi watanzania tunaelewa kwamba ukimaliza kidato cha nne ama ukifika chuo kikuu baasi umemaliza kila kitu hatutaki tena kujifunza ama kupanua mawazo yetu.
Sipo hapa kuongelea habari za Cryptocurrency ila nitatolea mfano tu. Wapo wadau mbalimbali wameleta mada kuhusu hii kitu lakini matokeo yake wakaitwa matapeli hii inaonyesha ni kiasi gani baadhi ya sisi watanzania hatuko tayari kujifunza, kujifanya tunajua na kupinga kumbe ujinga tu.
Niliwahi kutana na maneno mazuri sana katika moja ya kitabu cha mwandishi Robert Kiyosaki nanukuu "The most successful people in the world are the most rejected people in the world". Sisi watanzania tumekalia kupinga, kejeli na kuto kutaka kujifunza.
Unapinga Cryptocurrency wakati huo huo unatumia internet kwa miaka ya nyuma ilikuwa ngumu kuelewa ama kuamini ishu ya internet leo hii tunaitumia.
Nini kinakufanya usiamini Cryptocurrency wakati hayo ni matokeo ya teknolojia, vipo vingi vitakuja kwenye masuala ya teknolojia.
Mwenyezi Mungu ametujalia akili ili itumike kutatua matatizo yetu sio kupinga na kujadili masuala yasio na manufaa kwetu sisi kwa sasa na hapo baadaye.
Yapo mengi ya kuyaandika ila nisiwachoshe ila tujitahidi kuwa tayari kwa mabadiliko ya dunia. Tutumie akili zetu kutatua changamoto zinazotukabili na pia tuwe tayari kujifunza sio kila kitu ni ubishi tu, asanteni.