Sisi walimu wa shule za msingi

Sisi walimu wa shule za msingi

Mssassou

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2015
Posts
1,537
Reaction score
597
Tumedanganywa sana na ahadi za CCM katika sekta yetu, tulihaidiwa mishahara inayoendana na maisha ya sasa, nyumba za kulala, kuboresha mazingira ya kufanyia kazi n.k.

Kwa muda wa miaka yote hiyo serikali ya CCM bado inawayawaya. Mbaya zaidi mnaleta Capitation katika shule zetu 90000 kila baada ya miezi minne tena shule hiyo iwe na idadi ya wanafunzi wasiopungua 600 chini ya idadi hiyo shule inaweza kupata 50000.

Katika pesa hiyo ya Capitation unapangiwa katika avifungu vinne;

1.Utawala

2.Ukarabati

3.Vifaa na

4.Mitihani

Kwa walimu wakuu wanapata shida sana kuziendesha shule hizo,hakuna madawati ya kutosha madarasani matokeo yake baadhi ya watoto wanakaa chini.

Kutokana na hali hiyo imetufanya sisi walimu kuichukia Serikali hii ya CCM kupita maelezo na tumejipanga vizuri kutoipigia kura CCM kwa ngazi zote za uongozi.

Maana sasa hatuna namna ni kutoipigia kura tu,kama tumeshindwa kupata mabadiliko ndani ya CCM tutayatafuta nnje ya CCM
.
 
Uzuri moja ni kuwa na mwaka huu mtadanganywa tena... kuna kila dalili

Mlidanganywa, mkafahamu mnadanganywa, mkakubali kudanganywa

Kwa kanunu ile ile, mtadanganywa tena na kwa maumivu yaleyale mtarudia mizaha ile ile.... "Shemeji unatuachaje"??
 
Wakati fulani inakuwa kama maigizo.... majuzi nimehudhuria kikao cha wazazi eti report inasomwa capitation iliyofika shuleni kwa miezi 6 iliyopita ni 321, 278. 65

Shule ina zaidi ya wanafunzi 700

Halafu kuna mtu ataniambia tumeboresha slimy yetu na mifumo yake..... ujuha mtupu
 
Walimu mnao uwezo wakuwashawish wananchi wafanye mabadiliko! Kama mmeamua kuungana mtasaidia kufanya mageuz mwez oktoba! Ila msikengeuke kwa vtshrt na vkofia na vikanga kutoka china
 
walimu msikubali ahadi hewa. muwe kama tomaso
 
Uzuri moja ni kuwa na mwaka huu mtadanganywa tena... kuna kila dalili

Mlidanganywa, mkafahamu mnadanganywa, mkakubali kudanganywa

Kwa kanunu ile ile, mtadanganywa tena na kwa maumivu yaleyale mtarudia mizaha ile ile.... "Shemeji unatuachaje"??

Shemeji katuacha na ugumu wa maisha,hatuulizi tena hilo swali jibu limepatikana
 
Walimu ndo kada ya watu wasiojitambua hata kidogo. Yaani wapo wapo tu bora liende. Hasa hawa wa shule za msingi yaani ni shiiiida...!

Sasa mnakuja hapa kulia lia wakati nyie ndo wezi wa kura kuisaidia CCM ishinde kipindi cha uchaguzi...? Shame on You...!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kazi ya ualimu hupaswi kuichukulia too serious ....la sivyo utaumia hahahah just take it easy halafu Fanya mambo yako mengi itainjoyi sana
 
Walimu ndo kada ya watu wasiojitambua hata kidogo. Yaani wapo wapo tu bora liende. Hasa hawa wa shule za msingi yaani ni shiiiida...!

Sasa mnakuja hapa kulia lia wakati nyie ndo wezi wa kura kuisaidia CCM ishinde kipindi cha uchaguzi...? Shame on You...!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Kibaka akiamua kuokoka kwa kumtumikia Mungu basi anatakiwa atiwe moyo na wala sikumkatisha tamaa
 
Mssassou

Nyinyi wenyewe mnafanya sekta yenu izaraulike. Chama kimekufa bado mnakikumbatia. Mkipewa nafasi ya kusimamia uchaguzi mnasahau yote mnayoyalalamikia sasa.
 
Last edited by a moderator:
Mssassou

Mkuu hilo ndio jambo la muhimu na kuwapa elimu walimu kulijua hilo ili october kuipiga ccm chini
 
Last edited by a moderator:
Walimu wenyewe wameshindwa kujipanga .maana kwanza waache kuwakombatia ccm madarakani hebu mabadiliko nyiewalma
 
Waalim walishazidiwa ujanja kwa kua mini Shwa mambo mengi hewa huku viongozi wao wakigeuza Chama Chao kua tawi la CCM watanyonywa hadi wakome
 
Kazi ya ualimu hupaswi kuichukulia too serious ....la sivyo utaumia hahahah just take it easy halafu Fanya mambo yako mengi itainjoyi sana

Hapo Sawa kabisa sababu serikali yenyewe haiko serious why kujifanya una mzuka nayo then Shule hakuna mahitaji ya. Msingi huku kupotezeana muda
 
unalamba mkopo na kazini huendi unatafuta kazi nyingine private au binafsi,unapiga kimya siyo mambo ya shemeji unatuachaje.
 
Tuungane watanzania wote jukumu la kumng'oa mkoloni mweusi linahitaji umoja wa hali ya juu,
 
Tumedanganywa sana na ahadi za CCM katika sekta yetu, tulihaidiwa mishahara inayoendana na maisha ya sasa, nyumba za kulala, kuboresha mazingira ya kufanyia kazi n.k.

Kwa muda wa miaka yote hiyo serikali ya CCM bado inawayawaya. Mbaya zaidi mnaleta Capitation katika shule zetu 90000 kila baada ya miezi minne tena shule hiyo iwe na idadi ya wanafunzi wasiopungua 600 chini ya idadi hiyo shule inaweza kupata 50000.

Katika pesa hiyo ya Capitation unapangiwa katika avifungu vinne;

1.Utawala

2.Ukarabati

3.Vifaa na

4.Mitihani

Kwa walimu wakuu wanapata shida sana kuziendesha shule hizo,hakuna madawati ya kutosha madarasani matokeo yake baadhi ya watoto wanakaa chini.Kutokana na hali hiyo imetufanya sisi walimu kuichukia Serikali hii ya CCM kupita maelezo na tumejipanga vizuri kutoipigia kura CCM kwa ngazi zote za uongozi.Maana sasa hatuna namna ni kutoipigia kura tu,kama tumeshindwa kupata mabadiliko ndani ya CCM tutayatafuta nnje ya CCM
.

Mmeongezewa mishahara mkuu Usijali.

Mishahara mipya ya mwezi wa saba hiyo hapo chini.

TGTS B/1 TSH.460,000/=

TGTS C/1 TSH.620,000/=

TGTS D/1 TSH.867,000/=

TGTS E/1 TSH.989,000/=

TGTS F/1 TSH 1,234,000/=

Kwa maelezo zaidi tembelea.

NB MUUNDO WA KADA YA UALIMU MSINGI UMEUHUISHWA KUTOKA B HADI G. www.pmoralg.go.tz
 
Walimu??? , yani hao ndo mazo*bie kabisa, na mwaka huu kama kawa watawasaidia kuiba kura, Huwa hawajielewi kabisaaa, kanga na t-shirt Za kichina basi huwamaliza kabisaaa
 
Back
Top Bottom