Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,157
- 4,454
Nilishaambiwa au kusikia mara kadhaa kwamba Mwanamke kashtaki kwa Mmewe kwamba kuna Mwanamme anamfuatilia/anamtongoza, matukio haya yapo ya aina kadhaa:-
1. Mwanamke kulalamika kwa Mmewe kwamba katongozwa na mtu anayemfahamu huyu mwanamke kaolewa na kaolewa na nani.
2. Mwanamke kulalamika kwa Mmewe kwamba katongozwa na Mwanamme asiyefahamu kwamba huyu Mwanamke kaolewa.
Kwa sisi ambao wake zetu hawajawahi kutuambia kama huwa wanatongozwa tubaki na picha gani?
1.Wake zetu hawatongozwi?
2.Wanatongozwa wanakataa lakini Wanapuuzia kutuambia?
3.Wanatongozwa wanakubali na kuifanya iwe siri?
Najaribu kuwaza tu kwasababu mimi mke wangu hajawahi kuniambia kwamba ametongozwa na mtu yeyote.
Kwa hiyo huwenda wake zetu pia wanatongozwa lakini hawatuambii tu
Kwani wewe ukitongoza huwa unamwambia?
Why?????
Kwa mila na desturi zetu, kabla ya mwanamke hajaolewa na au mara tu anapovunja ungo hupewa mafunzo maalumu
yanayojulikana kama unyago, msondo, nk. Katika mafunzo haya mwanamke anafundishwa namna ya kuishi na mume,
kumtunza mume na watoto, nakadhalika. Mwanamke hatarajiwi kuwa sababu ya fadhaa, wasiwasi, au hasira ya mumewe, hivyo hatarajiwi kumwelezea mumewe juu ya yeyote anayemtongoza au mahusiano yake ya siku za nyuma. Kikubwa anachotarajiwa ni kuwa mwaminifu kumkataa yeyote anayemtongoza na kutokujiweka katika mazingira ya kutongozwa kwani mwaname hutongoza anapoona kuna mwanya/dalili za kufanikiwa kama akijaribu. Mwanamke ambaye kila kukicha anamueleza mumewe kuwa fulani kamtongoza basi hajafuzu mafunzo ya unyago, atamfanya mumewe kuwa na wasiwasi wakati wote na kushindwa kufanya kazi, pia atamgombanisha na marafiki, jamaa na ndugu zake. Mwanamke ukijiweka katika mazingira ya kutongozwa, mfano kujichekeshachekesha, kuombaomba ofa, kukubali mialiko isiyo ya kazi wala biashara, kupenda sana kusifiwa kuhusu sura na umbile lake,kupenda sana kuwaelezea watu kuhusu madhaifu ya mumewe, na kugawa ovyo namba yake ya simu ni baadhi tu mazingira yanayotoa mwanya wa kutongozwa.
Wanaume tunajua kuwa kuna mwanamke ambaye hata kama unamtamani kiasi gani lakini kila ukimwangalia usoni huoni uwezekano/nafasi ya kukubaliwa, hivyo hujikuta ukiahirisha kila mara wazo la kumtongoza.
...kuna mwanamke ambaye hata kama unamtamani kiasi gani lakini kila ukimwangalia usoni huoni uwezekano/nafasi ya kukubaliwa, hivyo hujikuta ukiahirisha kila mara wazo la kumtongoza
mkeo anatongozwa tena sana hasa kwa sababu na wewe ulimtongoza na mkafika mahali mkakubaliana kuwa mke na mume. Pia ukumbuke kwamba kuna baadhi ya wanaume ambao kwao ni mwiko kupitwa na kiumbe anayeitwa mwanamke bila kumsumbua kwa kumtongoza.
Hivyo ndugu nikuhakikishie bila kuacha shaka kwamba mkeo anatongozwa tu tena narudia anatongozwa sana na anamalizana na watongozaji wake huko huko bila kukuletea taarifa. Sasa anamalizana nao vipi: hilo linabaki kuwa ni la kwake na Mungu wake.
thats actually a great way to pass time.Ni hivi Mwambie mkeo muweke deal...ukitongoza umwambie na akitongozwa akuambie...ili kila siku muambiane mambo ya kutongozana tuuu msikie raha.
unadhani kweli nakaa miaka yote hii sitongozwi?
itakula kwako mazima maana anaweza hata kujitongozesha..watch out!hapo kwenye red Ukimpotezea au ukamwambia pole inakuwaje?
Wanaume tunajua kuwa kuna mwanamke ambaye hata kama unamtamani kiasi gani lakini kila ukimwangalia usoni huoni uwezekano/nafasi ya kukubaliwa, hivyo hujikuta ukiahirisha kila mara wazo la kumtongoza.