Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Siku hizi choko choko za udini zimepamba sana moto mitaani na, hata katika mitandao ya kijamii mfano hapa JF. Hebu tujiulize swali moja dogo. Tukiweka udini mbele na kuacha undugu na ujirani kando tunapata maslahi gani? Tunapata faida gani? Huu ni wakati wa kila mtu kuheshimu imani ya mwenzake bila kuingiliana wala kuhoji kwa nini wewe unaingia kusali katika pango!, baada ya hapo dini zote tuishi kama jamii moja isiyobaguana. Sisi ni ndugu na marafiki na tunaishi pamoja mitaani na tunafanya kazi pamoja maofisini na tunashirikiana kuijenga nchi yetu na palipo na sherehe mbali mbali tunaalikana na wake zetu wanaishi vizuri mtaani na watoto wetu wanakwenda shule pamoja na hata sokoni tunafanya biashara huku tukishirikiana meza zetu. Tuishi kwa amani! Anayetaka kuabudu mbuzi ni hiari yake! Na Anayetaka kuabudu jua sawa tu na anayetaka kuabudu mtu yeye tu na anayetaka kuabudu treni aachwe na imani yake.. Tuishi kwa amani lakini tusilazimishane imani. Tutakalia malumbano ya dini, wakati wenzetu wanasonga mbele...Haya ni maoni tu kwa wale wapenda amani wote.