Ijue siri na sababu za malalamiko ya Teuzi kwa hoja za Udini katika Awamu hii ya Sita

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,502
51,098
Tangu Rais Samia aingie madarakani amefanya teuzi nyingi tu na katika teuzi hizo wapo watu wamekaa standby kuangalia majina ya Kizungu (isomeke Kikristo) na Kiarabu (isomeke Kiislamu) ili waone kuwa watu wanaoendana nao kiimani "wameula" zaidi au la!

Nataka nieleze sababu za hivyo:

1. Mosi, kuna sense of entitlement.
Kwa miaka mingi sana nchini tangu Uhuru mpaka leo hii, nafasi za Utumishi wa Umma na Serikali zimekaliwa zaidi na Wakiristo kuliko Waislamu. Teuzi nyingi kuanzia Nyerere hadi leo hii Rais Samia, teuzi nyingi zinakwenda kwa Wakiristo.

Hali hii imelalamikiwa sana na Waislamu kwa miaka mingi, kuwa, hili jambo lina ukakasi. Iweje teuzi ziende kwa watu wa mrengo mmoja tu kila wakati wakati nchi hii ni yetu sote, na watu wenye vigezo wapo pande zote? Majibu ambayo watu hawa wamekuwa wakipata ni kejeli, kuwa nyie hamjasoma, kuwa nyie mnaendekeza elimu ahera, lakini hoja yao hiyo siku hizi imekuwa proven wrong.

Hata ikafikia hatua hadi Sheikh Khalifa kutoa orodha ya Waislamu wasomi mamia kwa mamia ili kufuta propaganda kuwa waislamu wenye vigezo vya kutosha kuhudumu katika teuzi mbalimbali hawapo, lakini licha ya hivyo hoja hiyo imekuwa ikifumbiwa macho. Sasa leo, Samia licha ya bado kuendelea kuteua Wakiristo wengi zaidi kuliko waislamu lakini angalau kidooogo waislamu nao wanaonekanaonekana kwa mbali.

Hili limeshtua wale waliozoea kuona teuzi za mrengo mmoja, wanahaha, wamepandwa na ghadhabu, wanataka waendelee kuteuliwa watu wa imani yao kwa wingi uleule (over representation) kama zamani.

2. Sababu ya pili ni kuwa, Siyo kweli kuwa baadhi ya hawa wanaolalamikia udini katika teuzi hawajui kuwa Samia bado anateua Wakiristo wengi zaidi kuliko Waislamu.

Bali wanataka kumblackmail ili asije akazoea kuteuateua Waislamu. Wanampa meseji kuwa, ukijaribu kubadili status quo katika nchi hii na kuwapa nafasi watu wa imani nyingine katika Utumishi wa Serikali kwa wingi kama sisi basi tutakusagia kunguni kwa watu wa imani yetu ili upate wakati mgumu kisiasa.

Kwa hiyo hizi kelele kimsingi ni fitina ya kumchonganisha Rais na Wakiristo ili Rais aogope kuwapa Waislamu nafasi na kwa hiyo Status quo ya Wakiristo kuendelea kudominate Utumishi wa Umma na Serikali, uendelee kama ilivyokuwa tangu Serikali ya Awamu ya Kwanza hadi leo.

3. Sababu ya tatu ni chuki tu, na ufia dini.

Islamophobia is real, kuna watu wanaamini kuwa, kwa kuwabagua watu wa dini nyingine na kuwapendelea watu wa dini yao ni kumfanyia Mungu Ibada!

Wapo watu makazini wakiona kuna wafanyakazi wanavaa hijabu, muda wa swala umefika wanaenda kuswali, au Salamu ya "Assalam Aleikum" imekuwa nyingi katika korido za ofisi wanaanza kuchukia, wanajenga hila mioyoni mwao na kibaya zaidi kuna baadhi wanakwenda mbali hadi ku collude na like minded people ili kuwaletea fitina wenzao n.k.

Enzi hizo wakati nasoma katika chuo kikuu kimoja hapa nchini, wanafunzi Waislamu waliomba chumba kimoja kilicho idle ili wafanye ibada wakazunguushwa mno, wengine wakawa wanapewa vitisho vya siri kuwa wawe makini na ajenda yao hiyo kwamba wachague chuo au dini (yaani ni kitisho cha kupigwa fitina hadi wafukuzwe chuo).

Lakini at the same time, kila siku jioni na siku za Jumamosi na Jumapili madarasa ya chuo hichohicho Wakiristo wameruhusiwa kuyatumia kusali na kuabudu. Umeona aina hii ya chuki, choyo na roho mbaya?

Ushauri wangu:
1. Watanzania tuachane na habari za kutaka upendeleo katika ajira na teuzi. Hii nchi ni yetu sote. Si vizuri kunung'unika watu wa imani nyingine pia wakipata fursa za kuhudumu katika nchi.

2. Lakini kama tunaona upendeleo wa dhahiri katika teuzi, hapo kweli tuseme na tupige kelele. Kuna wakati nchi hii Rais mmoja aliunda Baraza la Mawaziri la watu zaidi ya 20 akaweka Waislamu watatu. Sasa katika situation kama hiyo kweli hapo jamii nzima haipaswi kukaa kimya.

Hivyo hivyo leo hii Samia akiunda Baraza la Mawaziri akaweka Wakiristo watatu tu hata mimi sitokaa kimya. Tusiwe na double standard, kwamba teuzi zikifavour watu wetu tunanyuti, ila wengine wakianza kuchomoza basi tunakuja hapa JF kuanzisha nyuzi lukuki za udini. Hiyo siyo fair.

3. Tuzidi kuimarisha, Umoja, Amani na Mshikamano. Nchi hii Wakiristo are here to stay, Waislamu are here to stay. Yesu hakuoni mfuasi wake bora kwa kuwa mbaguzi na wala Mtume Muhammad hakuoni mfuasi wake bora kwa kuvunja amana za watu wote. Tupendeane mazuri.

Nawasilisha.
 
Mleta mada ameleta vizuri. Mbona sisi Jumamosi hatufanyi kazi. Nawapongeza ndugu zetu nao wa Ijumaa. Hii ndio real battle, kwa maana unatakiwa ufanye ibada katika wakati ambao unahitajika kwa kazi za watu au kibinafsi sio kama jumapili imepoa sana yaani huna changamoto.

Ijumaa naivulia kofia maana muda wa ibada ndio unakuta kikao kimekolea.
Missile of a natinn andiko kali
 
Mimi ni mkristu lakini katika suala la uteuzi au hata kuchaguliwa katika nafasi mbalimbali katika Idara zote za Serikali yetu lazima kuwepo UWIANO kwa kuzingatia sifa na uzoefu.

kwa kufanya hivyo itasaidia sana kujenga UMOJA na MSHIKAMANO ktk kuijenga nchi yetu.

nakubaliana na mtoa hoja kuwa ni kweli sisi wakristu tulikuwa tumeshika/kuhodhi nafasi nyingi ktk Idara za Serikali tangu nchi ipate uhuru na hilo linatokana na sababu za kihistoria,

Ila kwa zama hizi ambapo kuna wasomi wengi wa dini zote hakuna sababu tena ya kushindwa kuweka UWIANO, hili sio jambo la kupuuzwa hata kidogo.
Kujaza watu wa aina moja ni hatari kwa umoja na MSHIKAMANO wa Taifa letu.

Ni kweli nchi hii ni yetu sote na itajengwa kwa kushirikiana sisi sote kwa umoja; waislam, wakristu na wasio na dini.
 
Listen, miongoni mwa hoja zako ulizoandika hapo juu ikiwemo ya "chuki tu" wewe ndie unachochea hizo chuki kuwepo. Naona umeandika tu jumla kuna watu wanachukia uislam maofisini wakiona hijabu wanakasirika kama vile umeingia ndani ya mioyo yao, kisha ukaziona hizo chuki zao.

Ungekuja angalau na mifano ya matukio halisi yanayothibitisha hii hoja yako iliyojaa hisia iwe fact, lakini kinyume chake, umekuja na mawazo yako binafsi na kuyageuza ndio fact, kwanini hao watu waichukie "hijab" au salamu ya "Assalam alleykum" ikiwa wamekuwa wakizisikia miaka mingi huko mitaani?

Njoo na mifano halisi ya chuki kama ile tunayoiona Zanzibar wakristu wakichomewa makanisa yao, au padri kumwagiwa tindikali ndio tuamini wakristu wanachukia uislamu kama ulivyoandika, lakini sio kwa maneno matupu pekee.

Ulichofanya hapa, umeenda kuokoteza mifano ya nchi za nje na kuja kuitumia hapa kwetu, this is wrong, kwasababu mazingira ya wale na sisi hayafanani hata kidogo, umetumia comparison badala ya mifano ya ndani kuhukumu hapa kwetu.

Hivyo, hata hiki ulichoandika hapa kwangu ni muendelezo wa fikra duni, ujinga; sioni kama taifa tunaweza vipi kupiga hatua kimaendeleo ikiwa bado tutakuwa tunatazamana kwa jicho la dini, kabila, au rangi.

Wewe umekuja hapa kuwatetea wale wa dini yako, simply umekuja kuongeza tatizo, hukumbuki wapo wasio na dini, wakina Kiranga na wenzake wao wamenyamaza kimya, hawana msemaji wao, na wala hawana hivi viherehere mlivyonavyo wengine.

We need to stop this kind of ignorance, kwasababu kutaka watu wa dini yako wawepo kwenye mamlaka hakutakusaidia chochote kama hutakuwa na mahusiano nao ya moja kwa moja, zaidi, kinachowafanya wengi wazungumzie hii issue ni kama ulevi tu, tena usio na tija kwao, wala kwa taifa.

Huu upuuzi una extend mpaka pale anapokuwepo kiongozi fulani, halafu wale wa dini yake wanakuwa hawaoni baya lolote toka kwake, huu nao ni ujinga mwingine mkubwa zaidi, kusifia/tetea kila linalofanywa na yule wa dini yako upuuzi.
 
Kuna Taasisi inaratibu hizo chuki .
Ndo maana unaona Dr Slaa sasa taratibu anatoka CCM kurudi Chadema kuongeza nguvu.
Hopeless idea, bila shaka hiyo taasisi ndiyo inayokuratibu nawe uwe unasifia kila kinachofanywa na wa dini yako, na upinge kila kinachofanywa na yule asie wa dini yako, hovyo kabisa.

Wewe ni nani hata umzuie Dr. Slaa kwenda popote atakapo ilimradi havunji sheria za nchi, au kule anakokwenda?
 
3. Tuzidi kuimarisha, Umoja, Amani na Mshikamano. Nchi hii Wakiristo are here to stay, Waislamu are here to stay. Yesu hakuoni mfuasi wake bora kwa kuwa mbaguzi na wala Mtume Muhammad hakuoni mfuasi wake bora kwa kuvunja amana za watu wote. Tupendeane mazuri.

Nawasilisha.
Go back and revisit your home work. Go back to your drawing board. Wakristo kuwa wengi kwenye nafasi za uteuzi ndani ya Utumishi wa Umma kuliko Waislamu ni de facto inayoanzia kwenye utoafauti wa idadi hizo ndani ya Utumishi wa Umma wenyewe usiokuwa wa uteuzi. Huko huko kwenye MDAs and LGAs waislamu ni wachache(sababu zinaweza kuwa mada nyingine tofauti).

Kwa hiyo katika scaling up, huwezi kuwapata waislamu wengi kuliko wakristo kutokana na sababu hiyo kuu.

Pili, wapagani wengi Tanzania ni de facto wakristo. Yaani sehemu kubwa, kama wazazi ni wapagani hasa bara, mtoto akisoma kidogo, unamkuta ana jina la kikristo(Roman Empire Names).
 
Listen, hata hiki ulichoandika hapa
Mkuu kwa Dunia. ya sasa jambo hilo japo sio Sheria lkn lazima lizingatiwe, ni kama ilivyo ktk suala la Uongozi wa juu kwamba miaka 10 Rais anatoka Bara miaka kumi mingine lazima atoke znz, hakuna Sheria inayo lazimisha hilo lkn ni jambo muhimu ktk kuimarisha muungano wetu.

Vivohivyo katika teuzi zingine mbalimbali UWIANO wa dini zote ni muhimu katika kujenga umoja wa nchi yetu.

Pongezi kwa Rais Samia anajitahidi sana kubalance.
 
Dawa ni kukavunja haka ka muungano na kila mtu arudi kwao ba...
Wa kulaumiwa ni Nyerere ambaye alileta muungano wa kipuuzi akitarajia Zanzibar na Wazanzibari kwa ujumla watatawaliwa na Mtanganyika miaka yote kwa maana lazima Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania atatoka Tanganyika lakini leo tumepigwa na kitu kizito kichwani tunalalamika.
 
nimependa andiko lako.
lakini kimsingi hii inadhihirisha wazi kuwa jamii yetu bado ina muskeli kwa namna tunavyowaza kuhusiana na uongozi na utawala wa nchi kwa kudhani kuwa udini ndiyo kigezo cha eti rais kumteua mtu.

Na kama marais huteua kwa kuangalia hilo basi we are doomed, maana ni wazi hawaangalii utendaji kazi wa mtu bali dini yake.

mimi binafsi sipendi nadharia ya udini kwa sababu hata hizo dini zina madhehebu kibao huko ndani. Tukiendelea kuendekeza udini, ipo siku waislamu watalalamika kwamba rais anaangalia pengine wasuni tu.

Vivyo hivyo wakristo watamnanga rais kwamba anawaogopa wakatoliki (kwa mfano) na anawapa vyeo huku madhehebu mengine ya kiprotestant na kipentekoste anawapotezea.

Kikwete baada ya kulalamikiwa hivi hivi, kipindi fulani aligawa hata nafasi za uwaziri, rc, kwa kuchagua kila mkoa wawepo mawaziri na wakuu wa mikoa.

Madhara yake tuliyaona, maana tulipata mawaziri na RCS vihiyo haijawahi kutokea. Uongozi kwa kuangalia nasaba fulani hauna tija kabisa.
 
Rubbish, unateuaji Tanga mawaziri 4 na Pwani 5 na huku Arusha, Manyara, Dar n.k hakuna hata Waizri 1? kimsingi maza ni mdini sn hafai
VIONGOZI WA NECTA TANGIA KUANZISHWA KWAKE 21/11/73
1
1973 - 1977
P. MSEKWA
MKRISTO

2
1977 – 1980
I.M KADUMA
MKRISTO

3
1980 - 1988
N. A KUHANGA
MKRISTO

4
1988 - 1992
G. R. N.MMARI (prof)
MKRISTO

5
1992 - 1999
M.L LUHANGA
MKRISTO

6
1999 – 2004
G.R.V MMARI (prof)
MKRISTO

7
2004 - 2007
E. MWAIKONDO (PROF)
MKRISTO

8
2007 - 2018
R.S MKANDALA (PROF)
MKRISTO

9
2018 – to date
W.A.L. ANANGISYE (PROF)
MKRISTO

10
SECONDARY KUTOKA (DED)
EMANUEL BARIDI
MKRISTO

11
PRIMARY KUTOKA (DED)
ESTHER THOMAS
MKRISTO

12
UALIMU NA UTAALAM KUTOKA (DED)
JOSEPH KAMILI
MKRISTO
 
Mkuu kwa Dunia. ya sasa jambo hilo japo sio Sheria lkn lazima lizingatiwe, ni kama ilivyo ktk suala la Uongozi wa juu kwamba miaka 10 Rais anatoka Bara miaka kumi mingine lazima atoke znz, hakuna Sheria inayo lazimisha hilo lkn ni jambo muhimu ktk kuimarisha muungano wetu, vivohivyo katika teuzi zingine mbalimbali UWIANO wa dini zote ni muhimu katika kujenga umoja wa nchi yetu.
Pongezi kwa Rais Samia anajitahidi sana kubalance.
Dunia ya sasa ipi unayoizungumzia? hebu nipe mfano wa yale mataifa yaliyoendelea yanayofikiria kidumavu kwenye teuzi zao kama tunavyofikiria sisi? na raia wao muda mwingi wanapiga kelele za kijinga, kama tunazopiga sisi?

The truth is; sisi tupo kwenye dunia yetu ya kijinga, ndio maana tunafikiria kivyetu vyetu, ajabu huu ujinga wetu kwako unauona ujanja, nami wala sikushangai kwasababu ndio umezungukwa nao.

Hata huyo Samia uliemsifia nae sina hakika kama ana huo uelewa, inawezekana kabisa nae akawa kwenye kundi hili hili la wajinga wanaotupigia kelele kila siku.
 
VIONGOZI WA NECTA TANGIA KUANZISHWA KWAKE 21/11/73
1
1973 - 1977
P. MSEKWA
MKRISTO

2
1977 – 1980
I.M KADUMA
MKRISTO

3
1980 - 1988
N. A KUHANGA
MKRISTO

4
1988 - 1992
G. R. N.MMARI (prof)
MKRISTO

5
1992 - 1999
M.L LUHANGA
MKRISTO

6
1999 – 2004
G.R.V MMARI (prof)
MKRISTO

7
2004 - 2007
E. MWAIKONDO (PROF)
MKRISTO

8
2007 - 2018
R.S MKANDALA (PROF)
MKRISTO

9
2018 – to date
W.A.L. ANANGISYE (PROF)
MKRISTO

10
SECONDARY KUTOKA (DED)
EMANUEL BARIDI
MKRISTO

11
PRIMARY KUTOKA (DED)
ESTHER THOMAS
MKRISTO

12
UALIMU NA UTAALAM KUTOKA (DED)
JOSEPH KAMILI
MKRISTO
Hoja yako nini? NECTA kuna nini hata wakiwekwa waislamu wote? twende kwenye ngazi za maamuzi
 
Back
Top Bottom