GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,646
- 109,031
- Thread starter
-
- #101
Mkuu wewe ni mdogo sana ktk nchi hii na akili yako ni ndogo sana kama punje ya mchanga ukilinganisha na akili JPM endapo kama tungeweza kuwalinganisha. Kwahiyo, kusikitika kwako haina madhara yoyote kwetu, kwa taifa na kwa muhusika JPM.
Sent using Jamii Forums mobile app
Vitu havitumiki na havizalishi..... Vibaki vya nini??Inasikitisha sana...
Vitu vya serikali na viheshimiwe jamani... hizo ndege zilikuwepo kwa ajili ya waliyopita na zinatakiwa ziendelee kuwepo kwa ajili ya atakayokuja...
Tusipoangalia tutaanza kupangisha mpaka jumba jeupe...
Cc: mahondaw
Ndege imetengenezwa kwa ajili ya kupaa angani..kama haipai angani basi vifaa vitaanza kuchoka na kutofunction vizur..kwakuwa mzee hasafir sana basi ni wazo zuri sana zitumike kwa shughuli zingine
Sent using Jamii Forums mobile app
Uhai wa ndege ni kuwa hewani ikiwa imepaki inakufa mapema ni sawa na gari, ukiipaki mwaka 1 hadi 2 inapata dents na kisha inakatika na kuwa screper. Raisi yuko sahihi 100%.
Sent using Jamii Forums mobile app
Zama zinabadilika mkuu..enzi za JK kaisafiria sana JPM yeye ni mzee wa road to roadWalipozinunua walikuwa hawayajui hayo?
Nakubaliana na Mheshimiwa Raisi kwa asilimia kubwa, serikali ina ndege tatu za raisi, yeye katoa ndege mbili zitumike commercially badala ya kupaki tu bila kufanya kazi. Lakini pia, hata zikiwa branded 'ATCL' bado viongozi wa serikali wanaweza kuzitumia kwa safari zao.
Mleta mada hujaweka hasara za kiuchumi ambazo serikali itapata zaidi ya kuweka "social prestige" kwa taifa. Hatuangalii fahari kuwa raisi anatembea na ndege yake, tunapigana kutoka kiuchumi.
Nimesikia akisema Fokker-28 na Fokker-50 zipakwe rangi za ATCL zianze kubeba abiria, wewe ulisikia vipi mkuu?Acha Kudanganya na rudi tena ukamsikilize alichokisema tafadhali. Hakusema kuwa Ndege moja itabaki na zile mbili ndiyo zibebe Abiria bali alisema ni Ndege zote. Siku zingine kama huna uhakika na Kitu au labda hujasikia vizuri Mtu kasema nini jiridhishe Kwanza kuliko kuwahi kuja ' Kupopomika ' hapa Jamvini sawa?
Leo umeandika upumbavu wa hali ya juu.
Bila shaka siku mwenge ukipigwa ban mtakuja kulialia hapa japo mnapiga kelele kwamba hauna umuhimu.
Narudia tena umeandika UPUMBAVU MKUBWA.
Ni bwege sana huyu Genta, nilidhani ana hoja kubwa na mbadala kumbe eti moja iuzwe. Hopeless kabisa!
Kwani ukikata ticket unaona na aina ya ndege utakayo panda. Halafu hiyo fokker inatatizo gani mbona maraisi na matajiri wengi wanazimiliki na kuzitumia nakumbaka ata bombadier zilitoka kauli kama hizi. Raisi wetu anaweza kuwa na mapungufu ila siyo kila atalolifanya tuliseme vibaya.
Nimesikia akisema Fokker-28 na Fokker-50 zipakwe rangi za ATCL zianze kubeba abiria, wewe ulisikia vipi mkuu?
Nilikuwa nakuona Kama mtu ambae unafanya research kabla ya kuongea lakini Leo umenisikitisha Sana,unajua raisi wa China na viongozi wa juu wanatumia ndege gani?jibu ni kuwa raisi and Co wanatumia Air China ni ndege mbili zimeteuliwa kutoka air china,raisi wa china anapotaka kusafiri ndege anaitumia Kama hasafiri basi ndege zinabeba abiria,ni BOEING 747,sasa wewe Fokker tu hizi unapiga mayowe du? Mimi kwa maamuzi haya Nampa magufuli heko 100% na ikiwezekana zote tatu za raisi ziwe za biashara,siku wakiwa na safari yy na makamu wake basi wazitumie na Kama hawasafiri basi biashara as usual,amenikosha Sana Leo mh raisi japo ni mpinzani wa ccm na watu wake,viva Mr.prezdaa.Hii ni ' dharau ' kubwa kwa Marais waliopita kuanzia Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere, Mzee Mwinyi, Mzee Mkapa na Mzee Kikwete kwa Mtu mmoja leo kuamua kwa ' Kukurupuka ' tu kuwa Ndege za Rais Forker 50 na Forker 28 ziwe ' Branded ' kama ' Commercial Planes ' za ATCL.
Hili halipo na halijawahi kutokea nchi yoyote ile duniani na naamini hata tungekuwa Mbinguni Kwake Mwenyezi Mungu hata Yeye pia asingefanya hiki ' Kituko ' ambacho GENTAMYCINE nakiita ni cha Kufungulia mwaka huu ambao bado ni mbichi kabisa wa 2019.
Hoja kwamba zipakwe rangi kisha zichuke Abiria kwakuwa huwa zinakuwa ' grounded ' tu na kwamba hata mwenye Kuhusika nazo huwa hazitumii kwakuwa hasafiri mara kwa mara kutolewa na ' PhD Holder ' kidogo ni kutaka Kuwadhalilisha ' Intellectuals ' wote nchini Tanzania.
Wasaidizi wa Rais hebu fanyeni Kazi zenu vyema Kwake kwa Kumshauri mnaogopa nini? Hivi Sekta ya Anga ya leo au ATCL ya leo inahitaji kweli hadi hata Ndege za Marais nazo ziwe ' branded ' na zijumuishwe kama Ndege za Biashara na Kubeba Abiria? Je kuna hilo hitaji kweli?
Ningeambiwa au ningesikia Hoja kwamba labda Ndege hizo ziuzwe na ibaki moja kisha hizo Hela zitumike Kuimarisha Sekta ya Kilimo ambayo inahitaji msaada na ungalizi mkubwa ningemwelewa Mheshimiwa Rais na ningekubaliana nae kwa 100% ila kwa hii Hoja yake ya leo nampinga na naona ni kama vile ' Tusi ' kwa Watangulizi wake.
Wengine tumeumbwa kuwa wakweli na wawazi hivi hivyo mtusamehe tu na tuvumiliane. Tuache Kukurupuka na kuwa na ' Mihemko ' isiyo na Tija wala Mantiki. Halafu akina Donald Trump ' wakitutukana ' Waafrika huwa tunalalamika na kuona labda anatuonea wakati kumbe huwa yuko sahihi tena kwa 100% zote kutokana na ' Madhaifu ' yetu ya asili.
Nimesikitika!
Nawasilisha.
Kwani zitto aliposema chadema inahitaji mabadiliko mbona mlimfukulizia mbali!Zitto alishatuambia kuwa jamaa Ni washamba.
Mi naomba tuwazoee maana katiba inawalinda na hatuwezi kuwafanya chochote
Uingereza, wote wanasafiri na british airways, na ni developed nationKimsingi mheahimiwa rais kakosea Sana kutoa hiyo kauli. Kwa mfano makamu wake rais je atasafiria Nini?
Kesho akiachia madaraka hizo ndege zinarudi Tena kwa rais Kama second hand?
Sababu ya yeye kutokutumia ndge isimfanye akaonekana Kama joka la mdimu. Ndimu halili na hata mwenzie naye asikule.
Halafu nafikir mheshimiwa Ben MKapa aliposema rais aache kauli za kusema "Mimi, Mimi au serikali yangu, serikal yangu" bado hakumuelewesha vzr mheshimiwa rais.
Kama serikal ninya CCM Basi lazima serikal hii ijue Mali za rais siyo Mali za mtu bali ni za taifa. Any change of use lazima ifwate process na siyo kauli tuu ya mtu mmoja
Nimemaliza kumsikiliza vizuri tena, amesema ndege 2 ndiyo ameishatoa maelekezo zipakwe rangi na zitumike kubeba abiria endapo kutakuwa na upungufu....nadhani ninemuelewa vizuri. Ki ufupi, ndege moja itabaki kwa matumizi ya raisi na serikali.Nimesikia akisema Fokker-28 na Fokker-50 zipakwe rangi za ATCL zianze kubeba abiria, wewe ulisikia vipi mkuu?