'Siri' za serikali ni zipi?

'Siri' za serikali ni zipi?

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
26,532
Reaction score
26,268
Mara nyingi tumekuwa tukisikia watu wakilaumiwa au kulaumiana kutoa 'siri' za serikali kwa wananchi. Hivi hizo zinazoitwa siri za serikali ni zipi na kwanini zinakuwa siri?

Ikiwa tunaaminishwa kwamba serikali huwekwa madarakani na wananchi na inatawala kwa manufaa ya wananchi, kwanini serikali iwe na siri ambazo wananchi walioiweka madarakani (watawaliwa) hawatakiwa kuzifahamu? Je, siri hizo zina nia njema kwa watawaliwa? Sisi tutaaminije kama hizo siri zina manufaa kwa wananchi wakati zimefanywa siri?

Kwa kuwa mtenda maovu (mwizi, mchawi, mlozi, mkabaji, jambazi, muuaji, fisadi, mnyonya damu, jangili, etc) ndiye hataki siri zake zijulikane, moja kwa moja inajengeka dhana potofu kwamba 'siri' za serikali ni za 'kiovu' kwa kuwa serikali haitaki wananchi wazijue. Ndio maana wakati mwingine serikali imekuwa ikihusishwa katika matendo maovu dhidi ya wananchi, hasa na baadhi ya watu wasioitakia mema serikali yetu tukufu.

Mara zote jambo la kheri hutangazwa sana kwa wananchi ili kuwajuza namna ambavyo serikali yao inawajali. Mfano halisi ni ununuzi wa bombadia, ujenzi wa SGR, mradi wa Stiglier's Gorge, ubanwaji wa mafisadi, n.k. Haya mafanikio yamekuwa yakitangazwa sana kila kukicha. Yasingefanywa SIRI kwa kuwa ni mambo chanya ambayo wananchi wanatakiwa kujuzwa na serikali yao tukufu. Kitendo cha kuficha baadhi ya mambo kwa kuyaita 'siri' ndicho kinacholeta ukakasi juu ya usiri wake.
 
Siri ni muhimu. Mungu ana siri, mwanadamu ana siri, wananchi ambao ndio serekali wana siri. Labda la kuzingatia kipi kiwe siri na kipi si siri? Ingawa neno Siri kwa mwandamu na wananchi limegeuka kuwa kokolo limezoa vingi.
 
Hakuna sehemu isiyokuwa na siri Dunia yenyewe ina siri ambayo wachache sana wanaijua wengi wao wakitaka kuitoa hiyo siri hupotezwa na kuuawa
 
Siri ni muhimu ktk nchi mfano mambo ya kijasusi hayafai kufahamika na wananchi maana adui akizipata taarifa hizo Basi anabadili mpango!. Na Siri nyengine hufichwa kwa propaganda ama uongo
 
15 secret in United republic of Tz government
1st n jina la serikali
Zingine sio mahala lake hapa ndio maana zikawa siri
 
Siri za serikali ni kama vile ununuzi wa silaha, uwezo wa kijeshi, aina ya silaha, idadi ya silaha, idadi ya military personell, majina ya watumishi wa taasisi ya kijasusi, next president, akiba ya fedha za kigeni, budget ya jeshi na ujasusi, next economic strategy to mention the few important!
 
Mara nyingi tumekuwa tukisikia watu wakilaumiwa au kulaumiana kutoa 'siri' za serikali kwa wananchi. Hivi hizo zinazoitwa siri za serikali ni zipi na kwanini zinakuwa siri?

Ikiwa tunaaminishwa kwamba serikali huwekwa madarakani na wananchi na inatawala kwa manufaa ya wananchi, kwanini serikali iwe na siri ambazo wananchi walioiweka madarakani (watawaliwa) hawatakiwa kuzifahamu? Je, siri hizo zina nia njema kwa watawaliwa? Sisi tutaaminije kama hizo siri zina manufaa kwa wananchi wakati zimefanywa siri?

Kwa kuwa mtenda maovu (mwizi, mchawi, mlozi, mkabaji, jambazi, muuaji, fisadi, mnyonya damu, jangili, etc) ndiye hataki siri zake zijulikane, moja kwa moja inajengeka dhana potofu kwamba 'siri' za serikali ni za 'kiovu' kwa kuwa serikali haitaki wananchi wazijue. Ndio maana wakati mwingine serikali imekuwa ikihusishwa katika matendo maovu dhidi ya wananchi, hasa na baadhi ya watu wasioitakia mema serikali yetu tukufu.

Mara zote jambo la kheri hutangazwa sana kwa wananchi ili kuwajuza namna ambavyo serikali yao inawajali. Mfano halisi ni ununuzi wa bombadia, ujenzi wa SGR, mradi wa Stiglier's Gorge, ubanwaji wa mafisadi, n.k. Haya mafanikio yamekuwa yakitangazwa sana kila kukicha. Yasingefanywa SIRI kwa kuwa ni mambo chanya ambayo wananchi wanatakiwa kujuzwa na serikali yao tukufu. Kitendo cha kuficha baadhi ya mambo kwa kuyaita 'siri' ndicho kinacholeta ukakasi juu ya usiri wake.
Classified information! Mfano serikali inunue mizinga ya jeshini na risasi milioni 10 kwa ajili ya uchaguzi mwakani halafu wewe ukachapishe hiyo habari front page kwenye Tanzania daima au mwanahalisi
 
Kwa kuwa mtenda maovu (mwizi, mchawi, mlozi, mkabaji, jambazi, muuaji, fisadi, mnyonya damu, jangili, etc) ndiye hataki siri zake zijulikane,
Siri haiwezi kulalia kwenye upande wa maovu pekee... Hapo umebugi
 
Back
Top Bottom