LIJUE KUSUDI LA WEWE KUZALIWA HAPA DUNIANI KAMA BINADAMU! KUPITIA NYOTA YAKO
Sehemu ya 2.
Dr
DOGOLI KINYAMKELA 💀☠️
Unapokubali utume au wito (calling) ya kuja huku duniani, ulimwengu wa roho unafanya kila linalowezekana uje huku duniani uzaliwe.
Anakuwa ashachaguliwa mtu maalum wa kukupitisha ili upate mwili wako hapa duniani na huanze maisha ya utumishi wako hapa hapa duniani ukiwakilisha Ancestors kama tulivyokwisha kubaliana.
Hata Mungu wa Wayahudi/ Waebrania ni Ancestor, ndio maana ya "MZEE WA SIKU" na huko alipo amezungukwa na wazee wenzake 24, wakimsikiliza kila sekunde na kutekeleza maelekezo yake.
Wewe unawakilisha Mazee, Miungu, Mabwana; wanaoishi kwenye Ulimwengu usioonekana au Ulimwengu wa kiroho (mbinguni?)
Umekuja for a special task. You have to know, yaani lazima ujue.
Usipojua na ukafa/ ukaondoka bila report ya uhakika ya wito/ utume wako, my friend, una kesi ya kujibu (nitaongelea hili huko mbeleni)
Ndio maana Wazee (Stars), wewe Waite may be malaika, ni sawa tu, kwenye Siku yako ya kuzaliwa wanakuwepo kuhakikisha kila kitu kinakwenda sawa, wakiwa mashuhuda wa wito wako. Wajiridhishe kuwa umeshapata mwili wa damu na nyama wa kuingia ili jukumu lako lianze from that particular day.
Walioangaziwa akili zao (enlightened) huko zamani walihakikisha wanaliishi kusudi lao na waliwasadia watoto wao kuliishi.
Walipolikamilisha waliondoka bila madeni yoyote ya kulipa.
"Kwa maana DAUDI alipokwisha KULITUMIKIA SHAURI LA MUNGU katika kizazi chake, ALILALA, akawekwa pamoja na wazee wake" (Matendo ya Mitume 13:36)
Mimi na wewe tuna SHAURI/ KUSUDI la kutimiza, ambalo tumetumwa KULIKAMILISHA ndipo tufe (kimwili), kiroho turudi home (kwa wazee wetu au kwa Mungu wetu, mbinguni, kwenye Nchi nyingine ya kiroho tulipotoka)
Wewe ulizaliwa uwe mwanamuziki, lakini unafanya biashara; unapoteza muda.
Ulizaliwa uwe mwanasiasa lakini unafundisha, unapoteza muda.
Ulizaliwa uwe Kiongozi wa kisiasa au kijamii lakini hupo jeshini, umejichanganya!
Hata kama unapata hela, hizo hela hazitakupa furaha hata kidogo isipokuwa zinaweza kukuongezea matatizo kwa sababu hazikuja kwa njia sahihi.
Kama unafanya kazi yoyote ambayo inakupa fedha (mshahara) lakini huna raha nayo, hiyo sio kazi yako, umekalia kiti cha mwingine, ondoka utafute kiti chako; la sivyo utaadhibiwa, trust me!
Ulizaliwa makusudi kuanzia March 21 hadi April 20 (kwenye hizo tarehe na huo mwezi) ili ufanye kazi za nguvu!
Wewe ni Punda (Aries) una kichwa kikubwa; umezaliwa kubeba mizigo mizito kama Wanyamwezi🤣
Ukifanya kazi zisizo za nguvu utaugua magonjwa na ufe mapema au hutapata raha. Ndio maana wanajeshi wote waliozaliwa kwenye mwezi March/April (Aries) wana raha na kazi zao, wana kipato na maisha yao ni mazuri sana, tofauti na waliozaliwa miezi mingine.
Ulizaliwa kati ya April 21 na Mei 20?
Wewe ni Ng'ombe (Taurus)
Unatakiwa ujikite kwenye kazi za kilimo. Kodisha au nunua mashamba lima, Fuga utaona raha na fedha za kutosha. Umeitwa kuwa mzalishaji wa chakula, ili wana wa Mungu wale na kushiba. Mtu akifa kwa njaa kwenye mazingira yako, unalo deni nakwambia. Utayakumbuka maneno yangu ukiwa umechelewa, labda unielewe leo na uchukue hatua.
Labda utaniuliza; mbona nafanya kazi fulani na inanipa raha, furaha na amani na napata fedha za kutosha?
Jibu: Fedha hizo ni halali?
Kama ni halali, basi ni sehemu tu ya wito wako, kama kazi yako haihusishi kilimo na mifugo (ardhi), ni ya ziada tu, sio basic!
Taurus nyie ni watu wa ardhi, ingawa pia mmejaaliwa sauti nzuri sana na za kipekee mnaweza kuimba muziki pia mkapata furaha, amani na fedha nyingi.
Wewe
Gemini ; ulizaliwa kati ya Mei 21 na Juni 20.
Kazi zako ni kuongea my friend.
Pambana uwe msemaji wa Yanga🤣
Kama hupendi soka tafuta kuwa msemaji wa Serikali walau ya eneo lako au ingia kwenye siasa uwe Mweneza sera za chama; achana na udaktari. Madaktari ni wale waliozaliwa kati ya August 23 na Sept 22. Akina Virgo. Hawa wamezaliwa kuwa matabibu au kulima na kufuga, sio kuongea ongea.
Wewe Gemini, my friend, kwenye udaktari huwezi nakwambia, utaishia kutoboa Siri za wagonjwa wako!
Nenda kasomee uandishi wa habari au uanzishe ki-web chako au ki-online TV mbona utaEnjoy sana life na hela itakuja!!!
Cancer unaenda Jeshi?!
Maajabu, utaishia kwenye stress nakwambia. Wewe ni mtu wa kukaa home ukishughulikia mali za ukoo/ familia, ukisoma vitabu na kuchimba historia ya vizazi na vizazi na kazi kama hizo. Wewe utakuwa bora maeneo hayo maana u mtulivu sana rafiki yangu; huna makelele na hupendi makelele kabisa; ni Mzee wa kujichimbia. Unafaa kuwa daktari pia uponye watu.
Ukishindwa kote huko anzisha kijitaasisisi chako cha kusaidia wajane, wazee na watu waishio kwenye mazingira magumu, utapenya sana. Utapiga hela halali na pia utakuwa mtu unayeipenda sana kazi yako.
Ukikutana na mtu hapendi kazi yake, mpatie ushauri maana unaweza kuta hakuja duniani kwa ajili hiyo.
Huko wapi ndugu yangu Mr. Leo? Mzee wa misifa na mikogo!!😃
We jamaa mahali pako ni kwenye Creativity industries.
Wewe ni msanii mzuri wa maigizo, mtunzi wa hadithi, mwandishi wa vitabu, mwimba muziki kama Taurus na kina Libra nk. Wekeza nguvu na muda wako huko. You're born a leader; nenda ukaanzishe kitu maana ninyi mmekuja duniani kubuni vitu, mle raha na muwe matajiri wakubwa. Anzisha vitu, coach watu ndo mahali penu huko, ila kilimo, ufugaji, vibanda vya M-PESA nk. hayo hayawahusu!
Ukimtaka kocha mzuri (good mentor) kwenye mambo yako tafuta hawa kina Leo/ Simba, ni Waalimu kwa asili, watahakikisha jambo lako linafanikiwa, ila usisahau hawatawaliki, nenda nao kwa akili sana; kukuzingua ni chap🤣
Wale wazee wa maono, ndoto, mafunuo, unabii na mambo ya kiroho; enyi Samaki (Pisces)
Nyie mmekuja duniani kuwaletea watu maono ya kimbingu. Mnajua sana kutulia kwenye 'uwepo' (wazee wa meditation) huwa hampendagi makelele kabisa.
Nyie ndo mnatakiwa kuwa viongozi wa dini (kiroho) maana mna connection ya haraka kwenye spiritual realm.
Asiyeamini amtafute Samaki/ Pisces, mtu aliyezaliwa kati ya Feb. 20 na Machi 20, aniambie kama hawa watu wanapendaga makelele!!!
Au kama hawaotagi ndoto za kweli!
Hawa nakwambia wanaona sana maono na kwa kweli hawa watu kama ni dhambi, wanazo kidogo mnooo maana huwa hawapendi hata makundi. Hayo mambo ya magrup wapelekee kina Libra na Aquarius na Gemini, hao ndio kutengeneza marafiki kwao ni simple. Kwenye mabasi ya mikoani, kwenye daladala au mwendokasi za Dar, hawa ndio uwa wanateka mijadala yote!
Je, ungependa kupata ushauri maalum (counseling) kuhusu kazi unayotakiwa kufanya?
Kama jibu ni ndiyo basi jiunge kwenye group maalum
*Somo litaendelea....
Kwa msaada wa tiba ya nyota, maisha, uchumi, mahusiano na magonjwa, wasiliana nasi
By
Dr DOGOLI KINYAMKELA 💀☠️ , mtafiti na mkufunzi wa maswala ya kiroho.
MENEMENE TEKERI NA PERESI Tumwesige senior Anastasia21