SIRI YAFICHUKA: Deni la 2 billion/- latua Ikulu!

SIRI YAFICHUKA: Deni la 2 billion/- latua Ikulu!

Walitegemea faida wakati viti kibao vilikuwa tupu.Hawakutunia akili kabisa ni bora wangeweka kiingilio cha kawaida watu wengejaa na wengeweza kupata zaidi ya hizo.
 
nani kathibitisha ni kiasi hicho? watu ni wasanii sana inawezekana walipitiliza hata malengo lakini unajua watanzania tulivyo, ni ngumu sana kutoa hesabu sahihi
 
I mean nimeipenda taarifa ya kuhus TFF kupata hasara................Wamejitakia........again,nimeipenda sana hii

sawasawa mkuu....naamini kabisa unajua nani mzigo huu unamwangukia....
 
Next time watatia akili, kiingilio kilikuwa kikubwa sana in comparison na hali halisi ya raia wa nchii hii, walitakiwa kufanya mobilisation kwa mashirika na makampuni wasaidie fedha na in return wapewe tickets kwa ajili ya wafanyakazi wao.
 
katika hizo walizopata wameiba ngapi?anyway hasara tuliitegemea kwani dhumuni la kuleta hiyo timu na kuilipa ilikua mutengeneze njia ya kuiba basi,sasa wametimiza lengo,na kama ndio mkopo walichukua nmb kama ilivyosemekana ndio imekula kwao,deni litahamishiwa kwa mdhamini ikulu,baada ya muda litafutwa,haya bwana endelee na michezo yenu tu huko maana mnatuona wananchi wenu ni vichwa vya panzi kiasi hatuelewi kinachoendelea,naichukia TFF,na vichwa vyote vilivyotoa hiyo idea.
 
Mgomo wa JF na kiingilio ghali vilisaidia nini? Mana ukiangalia chati ya makadirio+mapato kule michuzi inaonyesha ticket kibao zilidoda!..
Naomba TFF iwaalike Argentina wakimaliza WC!..ha ha ha
 
Guys nimesoma kwa Mr Michuzi kuwa tff wamekula hasara kwenye mechi kati ya TZ na Brazil.
Tff wamepata tsh 1.6bn wakati walitegemea kupata tsh4bn,katibu mkuu wa tff ndg Mwakalebela kasema haya hivi punde tu.
Nadhani hii blog ya Michuzi siyo ya kutegemewa sana bora tusubiri source ya maana!
 
nadhani hii blog ya michuzi siyo ya kutegemewa sana bora tusubiri source ya maana!

ni blog ya kutegemewa sana mkuu........walikuwepo kwenye mkutano na hao tff.....
 
Tatizo la viongozi wa nchi hii hawataki kuwajumuisha wasomi kwenye maamuzi mazito.Hasara imepatikana kwa sababu ya mipango mibovu iliofanyika.

1.inama wao na akili zao zote walikuwa wanategemea kurudisha hela yote hio kupitia viingilio vya mlangoni tu? na siku mbili kabla baada kuona wana ticket nyingi hazijauzwa kwanini walikubali kuchukua hasara moja kwa moja badala ya kujaribu kupunguza bei za ticket hili wapunguze hasara.

2.waliwalipa Brazil,hio inamaanisha rights zote walikuwa nazo wao za mechi.Je makampuni walioweka matangazo yao uwanjani (ambayo yote yalikuwa makampuni ya nje) waliwalipa TFF pesa ngapi ? watupe hesabu za hela walizopata kutoka yale matangazo ya uwanjani kwani wale ndio waliofaa kubanwa hili TFF hipate faida badala ya kwenda kuwabana walalahoi.

Ukiacha matangazo ya uwanjani je TFF walilipwa pesa ngapi kutoka kwenye mauzo ya TV rights? kampuni iliokuwa na rights ya kulusha mechi live duniani ( nafikiri ESPN) waliwalipa TFF shillingi ngapi? tunataka TFF wajibu hilo pia au waliwaachia waoneshe bure kwa srea yao ya "KUTANGAZIWA UTALII"? ndio maana nasema viongozi wetu ni wazuri sana kwa kurupuka kufanya mambo bila kupiga hesabu kabla matokeo yake ndio haya.
 
Na hasara yenyewe haitakuwa rahisi kujulikana ni ya kiasi gani maana mpaka sasa hivi kiasi waliyolipwa Brazil bado ni siri kali. Inadaiwa walilipwa $6 millioni, mara $2.5 million, mara $3 million. Mpaka hapo TFF au Serikali itakapoamua kusema ukweli ni kiasi gani ambacho Brazil walilipwa hasara halisi ya maamuzi haya ya kipumbavu itaendelea kuwa ni siri kali.
 
Aisee , watu wanakula hela afu wanakuwambieni wamekula hasala !!! Na nyie mnaona kweli kabisa maana viti vilikuwa vitupu ,kama haitoshi wengne wanafulaia kupatika kwa hasala hio ,kumbe watu wameisha tia hela mfukoni.
 
mechi.JPG


Katibu Mkuu wa TFF Frederick Mwakalebela kasema sasa hivi jijini Dar kwamba Shirikisho hilo linajiandaa na mikakati ya kufunika hasara hiyo pamoja na kuweka mambo sawa.


Hakutaka kwenda kwa undani ni shilingi ngapi walikopa na toka wapi lakini kasema Brazil walilipwa pesa yao kwa muda uafaka na kwamba watoa huduma wote walishalipwa na hakuna mwenye kuidai TFF.



Kasema, hata hivyo, mechi hiyo na Brazil ilikuwa na faida kubwa ya muda mrefu, ikiwa ni pamoja ya wachezaji takriban 6 kufuatwa na mawakala wa timu za ulaya kuwataka. Pia amesema utalii utakuwa sana kwani wengi wanaulizia Tanzania.
Hawaeleweki hawa batu. Hii gemu kumbe ilikuwa kibiashara zaidi??. Sasa ni biashara gani inayofanywa bila mpango na upembuzi wa kitaalamu ??.
kwa nini waelezee hasara baada ya kula hiyo shoti wakati hawakutuambia mapema wadau wao kuhusu hii biashara iligharimi mtaji kiasi gani na ulitoka wapi kwa shirikisho hili ambalo halitengenezi faida (a non profit organisation)??,

Hapa si rahisi kuona hiyo hasara kwani ni matarajio tu ya faida (projected profit) na hiyo hasara wanayodai ndio vimeonyeshwa. Haieleweki ni vipi walitegemea kupata faida pasipo kuonyesha mchakato mzima wa kufikia hiyo faida kwa kuzingatia vigezo vya kiasi cha uwekezaji
Kanuni iliyotumika hapa ni kama: Matarajio vs Makusanyo = faida/ hasara) na hakuna chochote cha maana (wizi mtupu!!).

Wamepiga mahesabu ya kitoto kabisa, na matarajio yao hayaonyeshi kama walitegemea faida kutokana na huo mchezo. Iweje walenge kwenye idadi washangiliaji kwa mujibu wa uwezo wa uwanja (majukwaa) na sio kwa idadi ya tiketi walizotengeneza kwa lengo ya kuziuza kwa ajili ya kuuza??, Kama walitengeneza tiketi kiduchu au zaidi ya hapo, mdau wa kawaida atajuaje kuwa viti vyote vingejaaa?. Achilia mbali wale ambapo wanaingia na kusimama na wale wanaoiba tiketi na kuziuza kwa mwendo wa kurusha (hapa si rahisi kuzitanyia mahesabu kwa uwezo wa uwanja.


Hapa huwezi kuona hata kiasi kilitarajiwa kutumika kugharimia maandalizi ya mechi hiyo vs gharama halisi (actual expenditure).
 
sawasawa mkuu....naamini kabisa unajua nani mzigo huu unamwangukia....

Kweli ni mzigo wetu, lakini hii itawafundisha kitu TFF. Mpira haupandi kwa kucheza mechi moja na brazil bana, halafu hiyo hasara ya Tshs 1.3bil kama wangewekeza katika timu si ingekuwa bora zaidi?
 
Kweli ni mzigo wetu, lakini hii itawafundisha kitu TFF. Mpira haupandi kwa kucheza mechi moja na brazil bana, halafu hiyo hasara ya Tshs 1.3bil kama wangewekeza katika timu si ingekuwa bora zaidi?

sidhani kama itawafundisha chochote kwani lengo lao lilikuwa ni kutengeneza mazingira ya kuiba hela na wamefanikiwa.
 
Naona wametangaza hela za kiingilio tu! Hela za matangazo na TV right wamegawana wenyewe, tehe tehe nchi safi sana hii!! Na sitashangaa kama hakuna mwandishi wa habari aliyeulizia.
 
Asalaam Aleykum,

It seemed like a good idea at that time. Ujio wa Brazil unge raise profile ya soka la Tanzania, ungeutangaza Uwanja wa Taifa duniani, ungevutia watalii na wawekezaji Tanzania na ungemjengea sifa JK kwa umma wa Watanzania kama "Mpenzi mahiri wa michezo" kama mabango makubwa yenye picha ya Rais akibusu Kombe la Dunia yalivyopambwa uwanjani siku ya mechi. Ninaambiwa kuwa Rais Kikwete alifurahia sana mpango wa kuileta Brazil nchini na kuamuru serikali itoe kila ushirikiano kwa TFF kufanikisha jambo hili.
Matokeo yake ni kuwa kulikuwa na maelfu ya viti vitupu uwanjani baada ya wananchi kushindwa kulipa kiingilio.

Hii ni ishara tosha ya kuwa serikali hii iliyo ahidi kuleta Maisha Bora kwa kila Mtanzania kumbe wala haijui umasikini halisi wa wananchi wake yenyewe! Hicho kiingilio cha chini cha elfu 30 ni mapato ya mwezi mzima ya Watanzania walio wengi ingawa its just pocket change kwa viongozi wetu.

HII NDIYO NCHI YETU NA HAWA NDIYO VIONGOZI WAKE.

Wakuu kwanza inabidi tukubaliane kuwa Benki zetu zinafanya kazi kwa makini. Kwa maana nyingine ni kuwa professional bankers tuliona nao tunatakiwa kuwaamini na kuheshimu judgements zao.

Politicians as usual wamemess....kama ni kweli ningependa kusikia hatua zikichukuliwa kwa walihusika. Huu utakuwa ni ufisadi na uzembe, they have to be dealt with. Kama wakiachiwa itakuwa kichekesho.
 
MECHI ya kirafiki ya kimataifa kati ya Brazil na Tanzania ‘Taifa Stars' iliyopigwa Juni 7, mwaka huu, kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, imeingiza kiasi cha shilingi bil. 1.67.

Watazamaji 27,550 waliingia kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watu 60,000.
Mafanikio:
Mwakalebela alisema, mechi hiyo imeitangaza kwa kiasi kikubwa kimataifa kutokana na mechi ile ya kirafiki, kurushwa zaidi ya nchi 160.

Alisema kwa vile dhamira haswa ya mechi ile haikuwa nyingine zaidi ya kuitangaza Tanzania kimataifa,

Mbali ya manufaa hayo, Mwakalebela alisema mechi ya Brazil imewapa nafasi kubwa wachezaji wa Stars kuonekana kiasi cha nyota sita wa Stars, wamezivutia klabu mbalimbali duniani.

Alisema licha ya Stars kufungwa mabao 5-1, mechi hiyo imeiweka Tanzania katika historia bora kwa shirikisho

Alisema kitendo cha Brazil kucheza mechi za kirafiki na Zimbabwe na Tanzania, Juni 30 Rais wa Fifa, Sepp Blatter, atakwenda nchini Zimbabwe.
 
serves them right for not heeding to genuine advise and trying to be confidential

Since the governement is the guarantor then it means we are going to pay at the end of the day. Je hii haiwezi kuwa sababu ya kuwaondoa viongozi wa TFF madarakani kwa kuiingiza hasara TFF na serikali?
 
Back
Top Bottom