Mto Songwe
JF-Expert Member
- Jul 17, 2023
- 6,023
- 12,315
Siri muhimu kwa taifa masikini kuinuka kutoka katika dimbwi la umasikini.
Hii siri ambayo viongozi na wananchi wengi wa mataifa masikini hatupo tayari kuipokea na kuikubali.
Kama taifa tunataka tutoke haraka hapa tulipo kuna siri moja ya muhimu sana ambayo tunapaswa kuifahamu na kuikubali hata kama itapingana na mawazo na fikra zetu kwa kiasi kikubwa.
Maendeleo ya taifa ya haraka ni safari ya maumivu na machungu mengi sana ni safari iliyo jawa na miba mingi sana.
Hakuna maendeleo ya taifa yayoletwa kwa sisi kupiga domo tu bila kusacrifice miili yetu na roho zetu kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu.
Tunahitaji kufanya kazi kwa bidii na kwa dhati kwa mapenzi ya taifa letu liwe strong kuliko lolote ili tusirudi utumwani tena.
Mapambano haya sio kwamba yana hitaji mioyo ya dhati ya viongozi pekee la hasha hata wananchi wote kwa pamoja wakubwa kwa wadogo lazima tupambane bila kukata tamaa.
Tufanye kazi kwa bidii kwa maendeleo ya taifa kama vile kesho haipo.
Napenda kuwapa mifano ya hii jamii ya wakorea, wajapan, wachina hawa watu wanafanya kazi kuliko kawaida kama umewahi kufanya kazi na hii jamii utaelewa nini maana ya kufanya kazi kama vile kesho haipo ikiwezekana mtafute moja wapo kati ya mkorea, mjapan, mchina na uchunguze spirit yake ya kazi.
Hawa watu wanajenga nchi zao kwa dhati ya mioyo yao bila mashinikizo ya viongozi wakipanga wapambane wafanye hili au wawe pale watapambana kwa jasho na damu mpaka taifa linafanikiwa.
Kwa msaada wa kihistoria juu ya hawa watu miaka walio sacrifice maisha yao kwa maendeleo ya taifa lao umetawaliwa na maumivu na machungu mengi sana mfano:-
i. Taiwan (miaka ya 1960- 1990 )
ii. Japan (miaka ya 1860- 1990 )
iii. China (miaka ya 1950- 2000)
iv. Korea (miaka ya 1970-1990/2000)
V. Singapore (miaka ya 1960- 1990 )
Hio ni michache tu ya kugusia kwa atakae taka kujifunza.
Mazee hawa watu wanafanya kazi na wana spirit kutaka kuona nchi zao zinafika juu sio viongozi sio wananchi.
Hii jamii inatoa funzo kubwa sana kwetu kama tukiamua kuwa serious na kujifunza spirit yao lakini lazima tuhakikishe kweli tunaipenda nchi yetu na tunataka nchi yetu iwe giant of Africa na dunia.
Jambo la kufurahisha zaidi hawa watu hufikia mpaka hatua ya kulia kwa machozi mengi kwa uchungu juu ya nchi especially hao wachina ni mara nyingi sana nimeshuhudia hili mapenzi yalipo pitiliza kwa nchi hawa ndio wanayo.
Bila kukubali maumivu ya ujenzi ya nchi yatupitie hakika hatuwezi kufanikiwa kamwe maendeleo ya haraka hayaletwi kwa kupiga sogo na kelele za majukwaani.
"Siku zote nchi inapo piga hatua kubwa kimaendeleo wananchi wenye true spirit ulia kwa uchungu pale wimbo wa taifa unapo pigwa ukiwakilisha machungu yao katika ujenzi wa nchi".
R.I.P mashujaa (mabibi na mababu) wote mliopinga utumwa na ukoloni mpaka teno la damu la mwisho🕊️.
Hii siri ambayo viongozi na wananchi wengi wa mataifa masikini hatupo tayari kuipokea na kuikubali.
Kama taifa tunataka tutoke haraka hapa tulipo kuna siri moja ya muhimu sana ambayo tunapaswa kuifahamu na kuikubali hata kama itapingana na mawazo na fikra zetu kwa kiasi kikubwa.
Maendeleo ya taifa ya haraka ni safari ya maumivu na machungu mengi sana ni safari iliyo jawa na miba mingi sana.
Hakuna maendeleo ya taifa yayoletwa kwa sisi kupiga domo tu bila kusacrifice miili yetu na roho zetu kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu.
Tunahitaji kufanya kazi kwa bidii na kwa dhati kwa mapenzi ya taifa letu liwe strong kuliko lolote ili tusirudi utumwani tena.
Mapambano haya sio kwamba yana hitaji mioyo ya dhati ya viongozi pekee la hasha hata wananchi wote kwa pamoja wakubwa kwa wadogo lazima tupambane bila kukata tamaa.
Tufanye kazi kwa bidii kwa maendeleo ya taifa kama vile kesho haipo.
Napenda kuwapa mifano ya hii jamii ya wakorea, wajapan, wachina hawa watu wanafanya kazi kuliko kawaida kama umewahi kufanya kazi na hii jamii utaelewa nini maana ya kufanya kazi kama vile kesho haipo ikiwezekana mtafute moja wapo kati ya mkorea, mjapan, mchina na uchunguze spirit yake ya kazi.
Hawa watu wanajenga nchi zao kwa dhati ya mioyo yao bila mashinikizo ya viongozi wakipanga wapambane wafanye hili au wawe pale watapambana kwa jasho na damu mpaka taifa linafanikiwa.
Kwa msaada wa kihistoria juu ya hawa watu miaka walio sacrifice maisha yao kwa maendeleo ya taifa lao umetawaliwa na maumivu na machungu mengi sana mfano:-
i. Taiwan (miaka ya 1960- 1990 )
ii. Japan (miaka ya 1860- 1990 )
iii. China (miaka ya 1950- 2000)
iv. Korea (miaka ya 1970-1990/2000)
V. Singapore (miaka ya 1960- 1990 )
Hio ni michache tu ya kugusia kwa atakae taka kujifunza.
Mazee hawa watu wanafanya kazi na wana spirit kutaka kuona nchi zao zinafika juu sio viongozi sio wananchi.
Hii jamii inatoa funzo kubwa sana kwetu kama tukiamua kuwa serious na kujifunza spirit yao lakini lazima tuhakikishe kweli tunaipenda nchi yetu na tunataka nchi yetu iwe giant of Africa na dunia.
Jambo la kufurahisha zaidi hawa watu hufikia mpaka hatua ya kulia kwa machozi mengi kwa uchungu juu ya nchi especially hao wachina ni mara nyingi sana nimeshuhudia hili mapenzi yalipo pitiliza kwa nchi hawa ndio wanayo.
Bila kukubali maumivu ya ujenzi ya nchi yatupitie hakika hatuwezi kufanikiwa kamwe maendeleo ya haraka hayaletwi kwa kupiga sogo na kelele za majukwaani.
"Siku zote nchi inapo piga hatua kubwa kimaendeleo wananchi wenye true spirit ulia kwa uchungu pale wimbo wa taifa unapo pigwa ukiwakilisha machungu yao katika ujenzi wa nchi".
R.I.P mashujaa (mabibi na mababu) wote mliopinga utumwa na ukoloni mpaka teno la damu la mwisho🕊️.