Siri nzito kwa wanaojenga nyumba/vibanda vya biashara

[
....... ni hawa TBS...Shirika la Viwango...wanafanya nini...? Wavivu..Wazembe........Believe me nenda Tandika/K.KOO au Tandale utakuta Gunia linaitwa Lumbesa...!!

QUOTE]

Mambo haya yameenea sehemu nyingi na sio kwa ajili ya kushindwa kwa taasisi moja tu (....TBS....). Nasikitika kusema ni kajimfumo kabaya kanakojengeka katika jamii ya watanzania.

Mfano kwa wengi wa watumishi wa umma; kwa siku anatumia 1 hr kwa chai, anatumia 1 hr kusoma emails binafsi, anatumia 1 hr kwa kusalimiana na wengine (imegawanywa katika vipindi tofauti), bado muda wa simu na messages kwa cellphone yake, akitoka kwenda lunch anatumia kati ya saa au mawili, Kwa wiki ataomba kwenda dharura mara mbili, etc.

Mtu huyu anazalisha wakati gani, na kwa uwiano gani kulingana na muda wa kazi na pia kulingana na anavyolipwa.

Hili linaonyesha mmomonyoko katika jamii, hakuna uaminifu, hakuna kujithamini,
Maswali ya msingi:THAMANI YA MTANZANIA BINAFSI IKO WAPI? Je mwisho wa mambo haya utakuwaje, inasikitisha sana.
Wengine wamesifia kuwa ndiyo bongo kwa janja ya namna hiyo (including hapa jamvini), wengine wanahamisha wajibu kwa kurushia lawama matendo ya baadhi kama vile wizi, ufisadi,n.k.

Dawa au ufumbuzi lazima utoke kwa mtu binafsi, mtu mmoja. Ninaamini iwapo kila mtu ataamua, patakuwa na badiliko. Natambua kuwa sio kazi rahisi au ya muda mfupi, lakini INAWEZEKANA. Lazima mtu aanze ktk eneo linalomhusu. Ninatoa wito kila moja wetu atende kwa uaminifu kabisa.

kwani nchi za wenzetu ambao kwa sehemu kubwa hakuna michezo hii wamewezaje,
mfano mdogo kuna baadhi ya jamii zingine ughaibuni, ni aibu kwa mtu binafsi kukwepa kulipa kodi au ni aibu kula jasho la mwingine kwa hila, Ni fedheha kuiongezea jamii gharama. Kila mtu anajilinda mwenyewe.

THOU IT WILL TAKE LONG, IT IS POSSIBLE TO CHANGE. Some one has to start. It is Me and You!!!
 
bongo bana!!
hata garage usipokuwa makini wanakwambia tumefanya service kumbe wamesafisha oil filter na fuel filter, zinang'aa utafikiri kweli, na hawajagusa kitu, wanalamba hela zao, baadae unawakuta baa wanakamata mayi wakati wewe unaweza kunywa bia moja tu!!!
 
kuibiwa ni sehemu nyingi mfano mizani za madukani,butcher.
Hata mabar med kwa stail nyingi
TAKE CARE
 
Nimeelimika sana na taarifa hii ingawaje najutia kuwa sikuipata mapema zaidi. Naamini kibanda changu kingekuwa kimekwisha. Najiuliza hawa service providers wetu wa mobile phone services tunaweza vipi kuoanisha muda wa maongezi na tariff waliyotutangazia?

Hatuwezi kuwa tunaibiwa kichwani?
 
Kupunguza wizi na mambo ya kienyeji basi anzeni kutumia contactors. Haya mambo ya kufanya ujenzi kama mnanunua pilipili sokoni yamepitwa na wakati.
 
Watz jamani! Hii janja iko kwenye vitu vingi vyenye kuhitaji ...vipimo ( weights and Measures) huwa ni tatizo.....Huwezi kununua kitu kwa wafanya biashara wa kibongo bila kukagua! THIS IS CRAZY!

tena bora bongo jaribu India uone cha moto
 
tz kila mtu ana uhuru wa kumkandamiza mlaji nawaambieni, hakuna sheria wala mfuatiiaji sheria, imagine nimeenda mahali kubuy dining table imebandikwa bei laki 9.5 nikaongea na mhudumu akadai bro km unataka ntakuuzia kwa laki 4, but untanikabidhi laki yangu mapemaaa!! imagine huu km sio ufisadi, walaji tunabaki kuwa hoi hoi kwa matumizi na gharama ziszo za lazima, je wafanyabiashara wananeemmeka kikweli? kihalali? duh kila raia tz ni mwizi i believe!!

Kama serikali imelala watu wafanyeje?
 
Pdidy,
Kwa suala la mbao,hasa pale buguruni ni kweli hata mie nilikwenda na fundi wangu na tukiwa na futi kamba yetu,kwani nilikuwa tayari na taarifa hizo za kutumia vipimo feki,Mwanangu wale jamaa ni kiboko wakati mie nipo ofisini naongea na mwenye mbao jamaa wakaomba kuoina ile futi kamba yetu wakatoka na fundi wangu kule nje mmoja akawa anamsemesha fundi wangu wawili wakaifungua futi kamba yetu na kuikata 8ft katikati na kuiunga na super-glue ni kitendo cha haraka bila kuchelewa kwa bahati mie nikawaona kupitia dirisha la ofisini,palikuwa hapatoshi kwa kifupi hiyo ndio deal yao wote wafanyabiashara wa mbao pale Buguruni.Nikaamua kwenda depo SAO HILL kununua mbao.

Kweli. Nenda Sao Hill kanunue mbao.

Vile vile pale Buguruni zile mbao sio treated kama wanavyo dai. Wanazipaka rangi kusudi zionekane treated wakati sio. Nenda kanunue mbao treated za kweli kiwandani.
 
Magenge na dukani mizani zinategeshewa, walaji nani mlinzi wetu sasa kwa haya mauzauza?
 
Inasemekana mafundi wetu hawa tunaoenda nao ndio wanatumaliza...
Ukiona fundi anakulazimisha twende hapa sehemu wana mbao nzuri weeeeeeeeeeee fungua macho........kingine jamani kwa wale wanaonunua mbao zao tinted....watch out..zimekuja mbao zingine wanazipaka visamvu...na zingine sijui zinanyunyuziwa nini zinapendeza kama orig tinted.......

Upande wa cement....jamani jamani hii nchi ogopa mi nafikiri mungu alikuwa na makusudi ya kunifumbua macho wiki hii,,,,jamani cement wanapiga bomba sijui huko mliko.....huku kimara mwisho hatari kila duka limepigwa bomba yaani wanafungua sehemu then wanapunguza kiasi ....sasa tukinunua za wapalestina wanalalamika.......kuna sehemu si semi kwa chuki binafsi ,,,,,ukiwa unaenda mbezi mwisho....jamani...loh!!!!mafisadi mpaka madukani......ukipita kidogo tu kwa msuuguli kuna sehemu kushoto kwako kama kuna kapori kwa chini ....ukiangalia kuna liwanja likubwa lile ndugu zanguni gari zinaingiaga mchana kweupe alafu baada ya muda unaona gofu zimekaa barabarani....zikianza kutoka unashangaa wanawafwata mpaka kimara then .inasimamishwa baada ya muda waanamalizana .....wananchi wanakwenda kumalizwa.......
 
Kupunguza wizi na mambo ya kienyeji basi anzeni kutumia contactors. Haya mambo ya kufanya ujenzi kama mnanunua pilipili sokoni yamepitwa na wakati.
__________________

KAKA USIPIME NA MA CONTRACTORS...HAO NI BINADAMU KAMA WALE MADALALI...UTAWAACHIA WANAKWENDA WAO BADO YALE YALE
 
Ndugu zanguni habarini za jioni
ni wasaa mwingine tena nimeona niwashirikishe kwa mambo ya ajabu yaliotaka kunitokea leo hii...hakika tunatakiwa kumwamini MUNGU Mkubwa..
Leo hii nilikuwa nimeenda kununua mbao....pale BUGURUNI...kama kawaida nikajaribu kuwakimbia madalalali kupunguza bei....nikampata ndugu mmoja ofisini kwake kabisa..nikiwa na wadogo zangu wawili...tukashuka kutoka 430 mpaka 390 kwa feet..baadae tukaanza kuhesabu mbao kwa kuanza kupima kwa feet...nikashangaa akaja jamaa mmoja akauliza kichwani mguuni...la hasha sikujua kinachoendelea...tukaweka pembeni kama mbao 80...,nikanza kuangalia vizuri jinsi wanavyopima kwa kuangalia ile futi yao vizuri...uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii nilitaka kuangua kilio nikaja kukumbuka kumbe sijatoa hela...nikaingia ndani kumuulizia yule mwenye ile sehemu tulioelewana naeakaja tulipofika nikashangaa kukuta baadhi ya watu tuliokuwa tunapima nao hawapo..nikamwambia unaweza kuangali hiyo futi yako vizuri...hatimae alipoiangalia akakana kwamba ile si yake ndugu zanguni UHUNI uliotumika ni huu

ILE FUTI IMEUNGANISHWA UNGANISHWA....MWANZONI INASOMA

1................6..KATIKATI INAINGIA 10............16...INAUNGWA NA 20.......24..KWA HIYO NDUGU ZANGUNI HUU MCHEZO NI KILA SEHEMU WANAPOUZA MBAO...UKIANGALIA 6....10 WAMECHOMOA 4FT
16....20 IMECHOMOLEWA 4FT AGAIN...KWA UJUMLA UNAKUTA UKIPIMA KILA MBAO WANA FT KAMA 8 ZIKO MFUKONI...KWA HIYO UNAPONUNUA MBAO ZAIDI KAMA ZA MILLIONI MOJA UJUE WANA KAMA LAKI 4 MFUKONI......NAOMBA WATANZANIA TUANZE KUFUNGUKA KWA HILI NAJUA WENGI TUNAHANGAIKA KUPATA HELA ZA UJENZI...SASA SI VYEMA WATU WACHACHE KUJA KUCHUKUA KIRAHISI HIVI......

LINGINE NI KWENYE MABATI.....
USIDANGANYIKE KUNUNUA MABATI YAMEFUNGWA KWA BANDO...LOHHHHH
NDUGU PALE JUU NA LABDA MANNE NDIO YAMEANDIKWA GAGE 28 ZINAZOFWATA NI 30--32 KWA MBELE

LETS OPEN OUR EYES
Bongo kaazi kweli kweli
 
Dawa yake? Nenda na futi yako utakayonunua kwenye duka la Hardware. Mwambie napima mwenyewe! Shenzy Type!
 
Huu ni wizi kabisa umefanya vizuri mkubwa kuwe hadharani ili tuweze kufunguka macho.
Haujamalizia ulinunua hvyohvyo au ulitema?
 
Pole mkuu kwa yaliyokukuta!hiyo issue ya mbao za Buguruni ipo sana tuu!ila ukiwa mjanja fanya kitu kimoja!unaenda na futi yako na kijana wako mmoja wa kushika futi kule inakoanzia na wewe unakomaa kule inakoishia!manake jamaa kule futi inakoishia anasema futi 22 kumbe ni futi 16 tayari kashakupiga changa!ukishamaliza utamuona muuzaja anakuambia kwa hii bei ya Tshs 350 kwa futi hailipi!ongeza hela futi Tshs 500!

Hahaha
 
Huu ni wizi kabisa umefanya vizuri mkubwa kuwe hadharani ili tuweze kufunguka macho.
Haujamalizia ulinunua hvyohvyo au ulitema?

ndugu sikugeuka tena;maana walirudi kwenye bei ya sh 500 per feet..hilo alikuwa tatizo ila nilipoona vile nikahisi hata mbao zao watakuwa wamenipakia visamvu...
 
Mie sio Mwizi-Alhamdulillah..na sitamuibia mtu...!!

Back to the Mada...Unajua ktk watu ambao wanauzi ni hawa TBS...Shirika la Viwango...wanafanya nini...? Natamani niwatukane...Wavivu..Wazembe....Vichwa Maji....Jamani Hata kama Haya tunahitaji Kikwete....?...Believe me nenda Tandika/K.KOO au Tandale utakuta Gunia linaitwa Lumbesa...!!

Hivi kwanini Hatuna standards...? Hawa TBS walivyokuwa wahuni eti wanasema wameingia Mikataba na baadhi ya Kampuni kuchunguza Mizigo kabla haijaingia.....Huku wanaochek Magari Dubai na UK....Usipokuwa na Cheti chao..Angalia Zali...!!

Ukifika K.KOO uliza Visadolin vya Nyanya...au Viazi..Utakuta Viazi vimesimamishwa kwa chini..ukipewa tu unaviona vidogo...Nafikiri TBS inabidi ifumuliwe...hawa ni Mafisadi numberi one...kwani ndio contact no.1 ya mtanzania wa kawaida...Kwanini tusitumie Kg za Uhakika...ktk kila measuremts....!!!

Bahati mbaya sasa hata hawa wenye kutumia Kg nao wanabambika kichizi.....kwani wanakuwekea SUMAKU....Nenda kwa wauza nyama...Mzani washauweka Sumaku....kama una mzani wako nyumbani ukirudi pima kila ulichonunua kwa mzani...Utakuta sehemu kubwa umepigwa Changa la Macho..!!! Wauza Madhiwa nao.....

...inatia Hasira hadi kwa wauza ASALI.....washakuchanganyia matakataka ya mbao...wengine maji...ndani yake anakuwekea Nyuki wa kubabaisha ujue ni Halisi haijachanganywa...!!!

Mkuu Pdidy Poleni sana.....!!! next time ukienda uwe na measurement yako...kumkoma Nyani Giladi...!!!

hata wanaoiba ukiuliza wanasema wanakuhifadhia mkuu

na huku kwenye kuhifadhi upo??
 
Back
Top Bottom