Sioni haja ya CCM kufanya kampeni

Sioni haja ya CCM kufanya kampeni

ndio maana yake, turudi kwenye siasa za chama kimoja kuliko kuzuga kuna vyama vingi kumbe hakuna
Vitajichuja vyenyewe taratibu mpaka vibaki viwili au kimoja

Ulaya na Marekani walianza na vyama vingi sana lakini safarini vilianza kujichuja vingine kwa kufa vingine kujitoa kama Chadema ilivyoanza mwisho wa siku unakuta nchi nyingi zina vyama viwili au vitatu tu

Tunakoelekea vitapungua usiwe na wasiwasi kwenye.Siasa za muda mrefu ni kama mbio ndefu wengine huishiwa pumzi njiani mfano Chadema imeshaanza kukata pumzi na sio chama cha kwanza kukata pumzi

Ilikuwepo NCCR ilikuwa na nguvu hatari ikakata pumzi,ikaja TLP ya mrema ikawa na nguvu sana ikakata pumzi,ikaja CUF ya Maalim Seif Sharrif Hamad ikawa na nguvu hasa ikakata pumzi sasa ni zamu ya Chadema kukata Pumzi
 
Una hoja mkuu. Wanachezea tu kodi na misaada
ikiwa hali itaendelea hivi hivi bila uwepo wa chadema kwenye kampeni, ccm haitakuwa na presha kubwa ya kushindwa itajimwayamwaya kufanya kampeni zake miji mikubwa tu tena kwa kuchagua, hakuna upinzani. Vile vyama vya kipuuzi vitakavyojitokeza kufanya kampeni vyenyewe vitajijititimua tu ili vionekane vipo ila hakuna mwananchi mwenye akili timamu ataenda kupoteza muda wake kuvisikiliza vinasema nini kwenye kampeni zao na kura vitapata za kuchekesha
 
Labda huelewi maana ya kampeni, ht hivyo CCM iko na wananchi muda wote, ni juzi alipita Katibu mkuu kusini mwa nchi, sahivi yuko katibu wa uenezi, itikadi na mafunzo. CCM ipo kiganjani mwa wananchi. Kampeni ni wakati wa kuelezea ilani mpya ya 2025-2030, kwa hiyo ni lazima. CCM ni profesa wa siasa bwanamdogo tulieni mjifunze kwanza
Huko ni kuchezea pesa tuu hizo pesa wangeelekeza kwenye mambo mengine, maana rais anajulikana washajiteua wenyewe hamna haja ya kampeni Wala uchaguzi, wangeairisha tuu mpaka 2030, over.
 
ikiwa hali itaendelea hivi hivi bila uwepo wa chadema kwenye kampeni, ccm haitakuwa na presha kubwa ya kushindwa itajimwayamwaya kufanya kampeni zake miji mikubwa tu tena kwa kuchagua, hakuna upinzani. Vile vyama vya kipuuzi vitakavyojitokeza kufanya kampeni vyenyewe vitajijititimua tu ili vionekane vipo ila hakuna mwananchi mwenye akili timamu ataenda kupoteza muda wake kuvisikiliza vinasema nini kwenye kampeni zao na kura vitapata za kuchekesha
Uhakika. Sio ccm wala chauma wala act siwez sogelea jukwaa la hao wapuuzi. Sema walivyo watu wa hivyo watalazimisha watumishi na wanafunzj wahudhurie kampeni zao na kura wapige kwa lazima. Hawana akili
 
ni kweli, hawapaswi kufanya kampeni kwa mukhtadha huu. Hizo pesa za kampeni wazielekeze kwenye miradi ya wananchi

Wala hakuna hata haja ya kufanya uchaguzi, waielekeze Tume imtangaze Samia ndiye mshindi, baada ya hapo sheria inasema hairuhusiwi kuhoji.
 
Hiyo hamasa utakuwa unafanya nyumbani kwako na mke/mme wako. Ukitaka kuiona dola subiri kuanzia sasa. Nyambaf hamuwezi kuisumbua nchi, mmeshindwa kumtumia vizuri Rais mstaarabu km Samia nani ataweza kuwavumilia wapumbavu km nyie?
Rais mstaarab au mnafki?!.
Zero brain kbs.
 
Acha kampeni zifanyie ili
Ikiwa wanao wagombea na Tume kwann wanahangaika kufanya tena kampeni?
walau baadhi ya sekta kama burudani, usafiri, printing, guest houses watengeneze pesa
 
ikiwa hali itaendelea hivi hivi bila uwepo wa chadema kwenye kampeni, ccm haitakuwa na presha kubwa ya kushindwa itajimwayamwaya kufanya kampeni zake miji mikubwa tu tena kwa kuchagua, hakuna upinzani. Vile vyama vya kipuuzi vitakavyojitokeza kufanya kampeni vyenyewe vitajijititimua tu ili vionekane vipo ila hakuna mwananchi mwenye akili timamu ataenda kupoteza muda wake kuvisikiliza vinasema nini kwenye kampeni zao na kura vitapata za kuchekesha
Alafu baadaye kwa usahalifuwao baada ya Chadema kuzuiwa watakuja na igizo kama la COVID-19

CCM Wasahaulifu!!
 
Labda huelewi maana ya kampeni, ht hivyo CCM iko na wananchi muda wote, ni juzi alipita Katibu mkuu kusini mwa nchi, sahivi yuko katibu wa uenezi, itikadi na mafunzo. CCM ipo kiganjani mwa wananchi. Kampeni ni wakati wa kuelezea ilani mpya ya 2025-2030, kwa hiyo ni lazima. CCM ni profesa wa siasa bwanamdogo tulieni mjifunze kwanza
Huelewi Alichoandika Umeropoka....kwa kifupi amemaanisha MNATUPOTEZEA MUDA WA KUUNGA FOLENI NA KUVICHAFUA VIDOLE KUMBE MAJIBU YA MATOKEO TIARI MNAYO
 
Chaguzi zote za Africa ni matumizi mabaya ya Kodi za wananchi pia ni Dili la kupiga ten percent
 
Back
Top Bottom