ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,529
- 21,530
My people,
Haya ni maoni yangu binafsi na si lazima yafanane na wengi wenu,na kutofautiana na wengi wenu nisionekane napinga harakati za kuikomboa Tanganyika
Kuna msemo mmoja wa kiingereza unasema ukitaka kumuua mbwa basi mpe jina baya,maana yake ni kwamba kwa kawaida au akili ya kawaida huwezi kumuua mbwa bila sababu na hasa kwa jamii ambayo wanapenda wanyama wa kufuga.
Ili umuue na kuepuka maswali mengi basi mapema sana unampa jina baya,na Watawala nao wametumia mfano huo huo kuwapa Gez Z jina baya ili wahalalishe kudili nao bila kuwa na tashuwishu nyingi.
Ndio maana umesikia wameitwa wahuni au wezi wa kuiba mali za watu na kuharibu miundo mbinu kama ambavyo tumeyaona yaliyotokea tarehe 29/10/25
Kwahiyo hawa Gen Z ambao wanapanga tena kuandamana tar 9/12/25 siku ya uhuru hawatakuwa na sifa nyingine yoyote ile isipokuwa ni ile ile ya kuitwa WAHUNI NA VIBAKA
Hapo utatumika msemo ule ule ukitaka kumuua mbwa basi muite jina baya,hapo kuna vijana wengine tena watauwawa,tena safari hii kwa kutaka kuiangusha Mamlaka au Serikalli
Msione hii tume ya Maridhiano imeundwa haraka,watapitia humo humo kwamba Serikali ina nia thabiti ya kuleta suluhu lakini wahuni wachache wanakwamisha hizi juhudi na kuleta machafuko hapa nchini,kwahiyo hawatavumiliwa na watashughulikiwa
Vile vile Serikali imeahidi kwamba ndani ya siku 100 italeta au kuanza mchakato wa kupata katiba yenye kuridhiwa na wananchi,hiyo ni fimbo nyingine ya kuwachapia Gen Z ambao sasa wanajulikana kama wahuni wachache.
Kwahiyo ukiangalia kwa mapana yake ni kwamba Serikali imechukua hatua kadhaa ili kuleta kinachoitwa maridhiano lakini kwa upande wa pili lawama zitakuja kwa GEN Z kwamba ni wahuni wachache ambao wanataka kuharibu amani ya nchi,hapo watashughulikiwa,je watashughulikiwa kwa kutumia nguvu kama ya awali? Hakuna anayejua muda utaongea.
Pili sioni uungwaji mkubwa wa watu katika kufanikisha hayo maandamano,watu wameumizwa na yale yaliyo tokea 29 october,wamepoteza wapendwa wao na sidhani kama watakuwa tayar kupoteza wengine tena.
Tatu ile athari ambayo jamii iliipata kama matokeo ya kuzuiwa majumbani na kuacha shughuli zao ili waathiri watu wengi sana,sioni hamasa ya watu kuingia kwenye mazingira yale tena
Nataka kusema nini hapa,maana yake ni kikundi kidogo tu cha watu wataingia barabarani na kukosa uhalali au sapoti ya watu wengi hivyo kukosa ile nguvu ya maandamano ambayo ingetakiwa itikise watawala na hatimaye nguvu ya umma ipate kuonekana
My take, ni ngumu sana kuuondoa utawala kwa maandamano ambayo hayana kiongozi,kwahiyo wote tunataka mabadiliko lakini sioni kuleta mabadiliko kwa stahili hii,sana sana italeta maafa na vijana wengi kupoteza uhai
Naamini kabisa kilichofanyika tar 29 October kimeiamsha dunia na kujua nini kinaendelea hapa Tanzania,ubaya umeonekana na sauti zimesikika,naamini hili halita pita hivi hivi ila litakuwa na athari chanya siku chache zijazo
Mungu ibariki Afrika na Mungu ibariki Tanzania
Ni hayo tu!
Haya ni maoni yangu binafsi na si lazima yafanane na wengi wenu,na kutofautiana na wengi wenu nisionekane napinga harakati za kuikomboa Tanganyika
Kuna msemo mmoja wa kiingereza unasema ukitaka kumuua mbwa basi mpe jina baya,maana yake ni kwamba kwa kawaida au akili ya kawaida huwezi kumuua mbwa bila sababu na hasa kwa jamii ambayo wanapenda wanyama wa kufuga.
Ili umuue na kuepuka maswali mengi basi mapema sana unampa jina baya,na Watawala nao wametumia mfano huo huo kuwapa Gez Z jina baya ili wahalalishe kudili nao bila kuwa na tashuwishu nyingi.
Ndio maana umesikia wameitwa wahuni au wezi wa kuiba mali za watu na kuharibu miundo mbinu kama ambavyo tumeyaona yaliyotokea tarehe 29/10/25
Kwahiyo hawa Gen Z ambao wanapanga tena kuandamana tar 9/12/25 siku ya uhuru hawatakuwa na sifa nyingine yoyote ile isipokuwa ni ile ile ya kuitwa WAHUNI NA VIBAKA
Hapo utatumika msemo ule ule ukitaka kumuua mbwa basi muite jina baya,hapo kuna vijana wengine tena watauwawa,tena safari hii kwa kutaka kuiangusha Mamlaka au Serikalli
Msione hii tume ya Maridhiano imeundwa haraka,watapitia humo humo kwamba Serikali ina nia thabiti ya kuleta suluhu lakini wahuni wachache wanakwamisha hizi juhudi na kuleta machafuko hapa nchini,kwahiyo hawatavumiliwa na watashughulikiwa
Vile vile Serikali imeahidi kwamba ndani ya siku 100 italeta au kuanza mchakato wa kupata katiba yenye kuridhiwa na wananchi,hiyo ni fimbo nyingine ya kuwachapia Gen Z ambao sasa wanajulikana kama wahuni wachache.
Kwahiyo ukiangalia kwa mapana yake ni kwamba Serikali imechukua hatua kadhaa ili kuleta kinachoitwa maridhiano lakini kwa upande wa pili lawama zitakuja kwa GEN Z kwamba ni wahuni wachache ambao wanataka kuharibu amani ya nchi,hapo watashughulikiwa,je watashughulikiwa kwa kutumia nguvu kama ya awali? Hakuna anayejua muda utaongea.
Pili sioni uungwaji mkubwa wa watu katika kufanikisha hayo maandamano,watu wameumizwa na yale yaliyo tokea 29 october,wamepoteza wapendwa wao na sidhani kama watakuwa tayar kupoteza wengine tena.
Tatu ile athari ambayo jamii iliipata kama matokeo ya kuzuiwa majumbani na kuacha shughuli zao ili waathiri watu wengi sana,sioni hamasa ya watu kuingia kwenye mazingira yale tena
Nataka kusema nini hapa,maana yake ni kikundi kidogo tu cha watu wataingia barabarani na kukosa uhalali au sapoti ya watu wengi hivyo kukosa ile nguvu ya maandamano ambayo ingetakiwa itikise watawala na hatimaye nguvu ya umma ipate kuonekana
My take, ni ngumu sana kuuondoa utawala kwa maandamano ambayo hayana kiongozi,kwahiyo wote tunataka mabadiliko lakini sioni kuleta mabadiliko kwa stahili hii,sana sana italeta maafa na vijana wengi kupoteza uhai
Naamini kabisa kilichofanyika tar 29 October kimeiamsha dunia na kujua nini kinaendelea hapa Tanzania,ubaya umeonekana na sauti zimesikika,naamini hili halita pita hivi hivi ila litakuwa na athari chanya siku chache zijazo
Mungu ibariki Afrika na Mungu ibariki Tanzania
Ni hayo tu!