Sioi Solomon Sumari kugombea Arumeru

Sioi Solomon Sumari kugombea Arumeru

Hii inaweza kuwafanya watu wengine waendeshwe na hisia za huruma kwa kufiwa na baba yake hivyo kumpa kura za huruma.Inawezekana kijana anataka kutumia ''APILI TU PITI''.
 
Kama Marehemu Jeremia Sumari alikuwa ni kipenzi cha wana Arumeru, then, mtoto wake ndie atasimamishwa na CCM na ndiye atakayechaguliwa!. Huu ni ukweli mchungu, ila ndio ukweli halisi!.

Hizi siasa za kurithishana hazikuanza leo. Kwani Abedi Karume anajua siasa gani?. Kisiasa Abedi Karume, si lolote sii chochote zaidi ya jina la Baba yake (wa kufikia?). Dr. Husein Mwinyi ana siasa gani?, ni jina la baba!. Vita Kawawa ana siasa gani?, ni jina la baba na jimbo la baba!. Adam Malima ana siasa gani?, ni jina la baba na jimbo la baba! and the list goes on!.

2015, Ndesamburo hatagombea tena Moshi mjini, wala Mrema hatagombea Vunjo. Hawa wote ni vipenzi vya watu wa majimbo yao, hivyo yoyote watakayemshika kumnyanyua mkono, ndiye atakaye chaguliwa!.

CCM italazimika kumpitisha Sioi sio kwasababu ndio inampenda sana, no!, itampitisha ili kujiokoa vinginevyo jimbo linakwenda Chadema!.

na ndivyo itakavokuwa . Asante sana.
 
Lowassa(CCM)+Lubuva(NEC) = Sioi(MP ARUMERU).

Kwa kombineisheni hii tujiandae kupokea habari mbaya ifikapo hiyo April.
 
Mtaji wake utakuwa huruma ya wameru kwa ajili ya babake
 
Sioi sio kwamba ni mzuri.sio tishio katu na ni mweupe sana kwa nassary tatizo hatutaki utawala wa koo kama kule kismayu
 
nimemuona jana katika taarifa ya habari ya channel ten akiongea baada ya kuchukua fomu ya kugombea kupitia CCM,hakuonyesha kama mwanasiasa mzuri,hakuonyesha kujiamini,nadhani kumekuwepo msukumo toka nje kumtaka agombee.
 
huku nje NYC anaendelea kupiga jeramba kujiandaa na mtanange wa 2015 utakaofanyika mtera stadium. we rizi1 uko wapi huwaoni wenzako au unasubiri 2014 ukajitambulishe chalinzi au bagayoko?
 
Watanzania wenzangu tuwe na mawazo chanya, sioni kama kuna tatizo huyu kijana kugombea, kama anao uwezo anastaili kugombea, katiba yetu iko wazi. Aachwe agombee tu.mbona mtoto wa bushi aligombea na akashinda tena kwa taifa kubwa kama lile.ni haki yake ya msingi kama ilvyo kwako
 
Mtoto wa marehemu jeremiah solomon sumary amechukua fomu ya ugombea ubunge kwa tiketi ya ccm . Kuna uwezakano mkubwa akapitishwa kuwa mgombea wa ccm kupambana na upinzani .
Ni mkwe wa Lowassa huyu, na sidhani kama ccm watampa nafasi maana watakuwa wanazidi kumpa nguvu Lowassa na atakuwa mtandao wake tu kwa vyovyote. wakimpitisha basi watakuwa wamejimaliza pia! Lowassa mjanja sana nadhani angekuwa na binti wengi basi angejiweka mahali pazuri sana kuliko sasa maana huwezi mpinga mkwe
😛oa Ila pamoja na yote Chadema wakimpitisha Kijana Joshua Nassary ni wazi kuwa huyo mkwe wa Lowassa na mwingine yeyote ataambulia tu kura za ndg zake wa hapo mtaani
 
Wewe kuona mtu kachukua fomu na kusema ni urithi waona kuna hoja hapo?
mgombea wa ubunge kwa taratibu za chama chetu ni kupitia kura za maoni zilizowazi.
OTIS

Wewe vipi bwana, eti chama chenu............ Kwni wewe ni RizOne??

Kama kingekuwa ni chama chenu (sijui ni wewe na nani) kweli basi ungejua utaratibu unaotubika kwenye chaguzi ndogo. Kwa taarifa yako Nape alishatoa ratiba na hatukouna hizo kura za maoni kwenye hiyo ratiba.
 
ushauri wa bure! sisiemu wangeliacha tu hilo jimbo! kwa sababu ilishaonekana tangu wakati wa msiba wa huyo baba kuwa sasa jimbo linahamia wapi. Maana alipoingia kamanda Lema Godbless Msibani kila mtu alijua kuwa sasa jimbo hatuna. Kwa mtazamo huo tu sisiemu liacheni hilo jimbo. Mtawasumbua polisi bure waanze kuwakamata watu wakati kila kitu kinajulikana.
 
Sasa ataoa lini huyu?

Ndo anataka sasa kuwaoa wameru
A%20S%20embarassed.gif
:yawn:
 
hawa watoto wa mawaziri wa ccm, watoto na familia ya Kikwete , hanana kazi ya kufanya ila siasa, hata mtu akisoma taaluma kama udaktari bado tu anadhani kuishi bila siasa haiwezekani.

sasa mibaba zao iwe inarecord maridadi, tumemuona hapa juzi mtoto wa MALECELA, KATOKA KUBEBA box huko Marekani kaja kuona umaskini wa wana Mtera , umaskini ambao babake pia ni chanzo,

wanakera sana, wanatufanya waTz ni wajinga, walaaniwe hawa watoto, hadi waanzi kujutia umaskini ambao baba zao wametutia katika taifa hili.
 
Wakuu heshima kwenu, Nimesoma comments za wengi humu, nimegundua wengi wetu tunatoa comments kiushabiki zaidi ya hali halisi ilivyo. Wengi wetu tunadhani CDM wanachukua jimbo kirahisi safari hii na hii si kweli hata kidogo. kuna thread moja nilichangia kuhusu Jimbo hili mara baada ya kifo cha Mzee Sumari. nitarudia tena hapa. Yeyote kati ya CDM na CCM anaweza ibuka mshindi ktk jimbo hili kwa sababu zifuatazo: Wakazi wa jimbo hili wamegawanyika katika makundi mawili yaani Wenyeji na wahamiaji. kundi la wenyeji kama wengi tukikumbuka huko nyuma lina misuguano ya muda mrefu kwenye koo zao (rejea ugomvi wa KKKT 1989/1990), na kwa kawaida ya hawa ndugu zetu ni wagumu kusamehe haraka. kwa hiyo mshindi wa ubunge inategemea sana anaungwa mkono na koo zipi. kundi la pili ni la wahamiaji na kwa kawaida wengi wao (80%) wataunga mkono CDM na hawa utawapata sana maeneo ya pembezoni mwa barabara kuu. Technically CDM wakicheza vizuri kete zao wanaweza shinda kwa sababu ukoo wa Nassari (iwapo CDM watamteua) ni moja ya koo zisizofungamana na upande wowote kama ilivyokuwa kwa Sumari. Lakini pia kama CCM nao watazingatia uzaifu wa koo hizi wakaja na jina kutoka kwa wasiofungamana na upande wowote then kazi ipo na ni pevu. kumbuka Mzee Sumari hakutaka kugombea 2010 kwa sababu za kiafya lakini wazee wa pale walilazimisha na hata kampeni hakushiriki kwa kiwango kikubwa. CDM wanatakiwa kusahihisha makosa yaliyofanyika 2010, CDM mkoa walijikita sana Mjini na nguvu kidogo walizipeleka kwa Nassari, na hata kuna maeneo mengine nadhani ilishindikana kuweka mawakala, na hapo ndipo CCM ilipiga bao ingawa hata kwa kutokuchakuchua bado nina imani CCM wangeshinda kwa kura chache. Wapiga kura wa Arumeru mashariki (wenyeji) wengi wao ni wazee hasa kina mama, na kama CCM wataleta jina neutral CDM msitarajie kupigiwa kura na kundi hili. ni wagumu sana kubadilika na kuelimika haraka. Ni matumaini yangu kwamba CCM watakuja na the Kaayas, the Palangyos, the Ayos and the likes, na hapo for sure CDM watapiga bao kama kumsukuma mlevi.
 
hawa watoto wa mawaziri wa ccm, watoto na familia ya Kikwete , hanana kazi ya kufanya ila siasa, hata mtu akisoma taaluma kama udaktari bado tu anadhani kuishi bila siasa haiwezekani.sasa mibaba zao iwe inarecord maridadi, tumemuona hapa juzi mtoto wa MALECELA, KATOKA KUBEBA box huko Marekani kaja kuona umaskini wa wana Mtera , umaskini ambao babake pia ni chanzo,wanakera sana, wanatufanya waTz ni wajinga, walaaniwe hawa watoto, hadi waanzi kujutia umaskini ambao baba zao wametutia katika taifa hili.
Nguvumali.......Kansa ya kurithishana na kutumia kigezo cha undugu kupeana vyeo/nafasi za kugombea uongozi haipo CCM peke yake....Ipo karibu katika kila chama na ndio kiini cha kudumaa kwa demokrasia na maendeleo ya Tanzania...Japo CCM ndio wanaongoza kwa hili,CHADEMA wanafuatia(hasa kwenye ubunge) watu wamegawana ubunge wa viti maalum kama njugu kisa tu ni ndugu ama wana uhusiano wa karibu...........Inakera na kusikitisha sana
 
So ccm by not having preferential votes to get their candidate is trying to avoid unnecessary costs? CCM is the GRAND OLD PARTY it should know that democracy is never cheap!! Anaefanya vurugu ni nani ; si hao ccm wenyewe na wanashindwa kuthibitiana kwavile hawana nidhamu!

Kwa mtazamo wako, kwanini Igunga hapakuwa na kura za maoni katika uchaguzi mdogo?
 
Back
Top Bottom