Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,638
- 697,929
Ukiachana na kile kitengo cha propaganda cha CCM na ile praise team. Wengine wote hatupaswi kuwa na muono kimo cha mbilikimo. Ni lazima tuwaze zaidi ya mwisho wa uono wa macho yetu.
Nimemuona P kwenye mada za CHADEMA. Utabiri wa mabaya. P ulituasa tuepuke prophecy of doom. Tusiwaase wengine huku sisi tunatenda.
Natambua mgongano wa mawazo na hoja. Natambua tofauti za kimtazamo kati yetu lakini haya yasitufanye tukafika mahali tukawa na mitazamo finyu. Tunaihitaji CHADEMA kama taasisi imara ili CCM isijisahau sana. Miaka ile ya 1995-2005. Wakati huo NCCR kikiwa chama chenye nguvu na ushawishi, kuna mengi yaliyotokea lakini pengine hayakumbukwi sana.
Alitokea Augustine Mrema, waziri machachari wa CCM aliyebwaga manyanga na kujiunga na NCCR Mageuzi. Wengi bado tunakumbuka kilichotokea pale, kukawa na vichwa hasa.
Baadae NCCR ikafitinishwa na kumgeuka. Kukawa na NCCR mbili. Huo ndio ukawa mwisho wa kile chama. Kuna mtu pale NCCR mmojawapo wa viongozi mahiri akiitwa Prince Bangeda. Mpaka leo sijui alitofautiana nini na Mrema. Alimuandika vibaya na kumchambua Mrema kwenye safu yake ndani ya gazeti la Rai kila Jumatano kwa makala ndefu ndefu kwa miezi kadhaa. Nadhani hakuna mwanasiasa alichambuliwa na kuandikwa vibaya mpaka leo hii kama alivyofanya Bangeda kwa Mrema.
Leo hii Bangeda yuko wapi na Mrema yuko wapi? Unapotumika angalia unatumikaje. Usipojiongeza, wanaweza kukufanya kama toilet paper.
CHADEMA inapigwa vita sana kwakuwa ni mwiba mchungu kwa CCM. Project za kukiangamiza hiki chama ni nyingi mno. Watu wanaotumika ni wengi mno. Pesa iliyokwisha tumika ni nyingi mno. Hakuna chama cha siasa kimepitia mapigo mengi kama CHADEMA, lakini mpaka leo kipo hai na kinadunda. Kukiombea kife ni:
Kupoteza matumaini ya vijana wasomi wengi
Ni kupoteza viongozi wazuri wa kesho
Ni kupoteza matumaini na furaha wa wapiga kura milioni 7
Ni kupoteza matumaini na furaha ya wapenzi, washabiki na wafurukutwa zaidi ya milioni kumi
Hakuna kosa kubwa tutalifanya kama kuombea CHADEMA ife. Hiyo laana haitakaa ituache, itakula nasi sahani moja. Kama tulikubali NCCR na CUF vinyongwe, tusikubali haya kwa CHADEMA.
Viongozi walioko CHADEMA ni binadamu kama wewe na mimi wana mapungufu yao, lakini kwenye mizania ya haki wana mengi mazuri ya kukumbukwa vizazi na vizazi. Wanahitaji tuwatie moyo, tuwasaidie na kuwapa faraja kwenye kila hatua wanayopitia. Tusiwakatishe tamaa. CCM iliyokuwa na upendo wa kweli kwa Watanzania ni ile ya Mwalimu Nyerere tu. Baada ya hapo ni vurugu mechi kwa kwenda mbele.
Makala nyingi za kuiponda CHADEMA na kukiombea mabaya hata kama sio sehemu ya zile project zina ukakasi na kuacha maswali mengi kuliko majibu.
Je, kuna personal issues nje ya politik?
Jr
Nimemuona P kwenye mada za CHADEMA. Utabiri wa mabaya. P ulituasa tuepuke prophecy of doom. Tusiwaase wengine huku sisi tunatenda.
Natambua mgongano wa mawazo na hoja. Natambua tofauti za kimtazamo kati yetu lakini haya yasitufanye tukafika mahali tukawa na mitazamo finyu. Tunaihitaji CHADEMA kama taasisi imara ili CCM isijisahau sana. Miaka ile ya 1995-2005. Wakati huo NCCR kikiwa chama chenye nguvu na ushawishi, kuna mengi yaliyotokea lakini pengine hayakumbukwi sana.
Alitokea Augustine Mrema, waziri machachari wa CCM aliyebwaga manyanga na kujiunga na NCCR Mageuzi. Wengi bado tunakumbuka kilichotokea pale, kukawa na vichwa hasa.
Baadae NCCR ikafitinishwa na kumgeuka. Kukawa na NCCR mbili. Huo ndio ukawa mwisho wa kile chama. Kuna mtu pale NCCR mmojawapo wa viongozi mahiri akiitwa Prince Bangeda. Mpaka leo sijui alitofautiana nini na Mrema. Alimuandika vibaya na kumchambua Mrema kwenye safu yake ndani ya gazeti la Rai kila Jumatano kwa makala ndefu ndefu kwa miezi kadhaa. Nadhani hakuna mwanasiasa alichambuliwa na kuandikwa vibaya mpaka leo hii kama alivyofanya Bangeda kwa Mrema.
Leo hii Bangeda yuko wapi na Mrema yuko wapi? Unapotumika angalia unatumikaje. Usipojiongeza, wanaweza kukufanya kama toilet paper.
CHADEMA inapigwa vita sana kwakuwa ni mwiba mchungu kwa CCM. Project za kukiangamiza hiki chama ni nyingi mno. Watu wanaotumika ni wengi mno. Pesa iliyokwisha tumika ni nyingi mno. Hakuna chama cha siasa kimepitia mapigo mengi kama CHADEMA, lakini mpaka leo kipo hai na kinadunda. Kukiombea kife ni:
Kupoteza matumaini ya vijana wasomi wengi
Ni kupoteza viongozi wazuri wa kesho
Ni kupoteza matumaini na furaha wa wapiga kura milioni 7
Ni kupoteza matumaini na furaha ya wapenzi, washabiki na wafurukutwa zaidi ya milioni kumi
Hakuna kosa kubwa tutalifanya kama kuombea CHADEMA ife. Hiyo laana haitakaa ituache, itakula nasi sahani moja. Kama tulikubali NCCR na CUF vinyongwe, tusikubali haya kwa CHADEMA.
Viongozi walioko CHADEMA ni binadamu kama wewe na mimi wana mapungufu yao, lakini kwenye mizania ya haki wana mengi mazuri ya kukumbukwa vizazi na vizazi. Wanahitaji tuwatie moyo, tuwasaidie na kuwapa faraja kwenye kila hatua wanayopitia. Tusiwakatishe tamaa. CCM iliyokuwa na upendo wa kweli kwa Watanzania ni ile ya Mwalimu Nyerere tu. Baada ya hapo ni vurugu mechi kwa kwenda mbele.
Makala nyingi za kuiponda CHADEMA na kukiombea mabaya hata kama sio sehemu ya zile project zina ukakasi na kuacha maswali mengi kuliko majibu.
Je, kuna personal issues nje ya politik?
Jr