Sio dhambi kuungwa mkono na CCM - Kansa Mbarouk

Sio dhambi kuungwa mkono na CCM - Kansa Mbarouk

Greenwhich

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
1,337
Reaction score
968
Mgombea Uenyekiti CHADEMA Kansa Mbarouk amelalamikia wafuasi wa chama hicho wanaosema hafai kuchaguliwa kwa sababu anashabikiwa na CCM.

Katika mahojiano na gazeti la FAHAMU mgombea huyo amesema haoni dhambi kupendwa na mashabiki wa CCM kwani hiyo ndiyo demokrasia.

Mgombea huyo anayeshutumiwa kuwa kibaraka wa CCM amewataka wajumbe wa mkutano mkuu wa Chadema kumchagua kwa sababu ndiye anayefaa.

Uchaguzi mkuu wa Chadema unafanyika Septemba 14 ambapo Kansa Mbarouk anashindana na Freeman Mbowe Mwenyekiti anayemaliza muda wake na akitarajiwa kutetea nafasi yake kwa ushindi wa kishindo.
 
Huyo Mchepuko tumeshakinai habari zake!
 
Kuna gazeti linaitwa Fahamu,

Mbona halina ufahamu

Na hatulifahamu.

Njaa inamuuma sana
 
Kwa mantiki yake ni poa tu kuungwa mkono na ibilisi wakati wewe ni wa Mungu wa Israel? I don't buy that maana hakuna ushirika kati ya nuru na giza!
 
Mbaruku ataifufua chadema iliyouliwa na mbowe kwa kufisadi pesa za ruzuku.
 
Mbowe anahaha kuhamisha pesa za ruzuku kwenda kwenye account yake,,Ameshajua Mbaruku anashinda uchaguzi
 
Mgombea Uenyekiti CHADEMA Kansa Mbarouk amelalamikia wafuasi wa chama hicho wanaosema hafai kuchaguliwa kwa sababu anashabikiwa na CCM.

Katika mahojiano na gazeti la FAHAMU mgombea huyo amesema haoni dhambi kupendwa na mashabiki wa CCM kwani hiyo ndiyo demokrasia.

Mgombea huyo anayeshutumiwa kuwa kibaraka wa CCM amewataka wajumbe wa mkutano mkuu wa Chadema kumchagua kwa sababu ndiye anayefaa.

Uchaguzi mkuu wa Chadema unafanyika Septemba 14 ambapo Kansa Mbarouk anashindana na Freeman Mbowe Mwenyekiti anayemaliza muda wake na akitarajiwa kutetea nafasi yake kwa ushindi wa kishindo.

Ha ha ha haaaa ! ! !
 
Anazidi kujifunua rangi zake

Yeye na waliomtuma wanafahamu kuwa ni garasha! Ametumwa kuja kuropoka kwa kutumia uchaguzi huu! Wanafahamu pia kwamba hawatafanikiwa ndio maana hawana cha kuzungumza zaidi ya upuuzi!

Binafsi bado nawashangaa CCM! Waliposhtukiwa mpango wao through Zitto, wamekuwa mang'aa kabisa! Watu waliokuwa viongozi ndani ya cdm na wakaona kwenye chaguzi hizi zinazoendelea hawataweza kurudi kwenye nafasi zao wamechungulîa fursa na wanapiga hela kama vile za mjingaa flan hivi. Wanazikomba kweli kweli na hakika hadi uchaguzi wa ndani ya chadema uishe, kuna watu watakuwa wametoka! Tatizo lao ni kutokuwa na kumbukumbu kwamba watakuja kutupwa kama kondomu baada ya kutumika!
 
Kwa mantiki yake ni poa tu kuungwa mkono na ibilisi wakati wewe ni wa Mungu wa Israel? I don't buy that maana hakuna ushirika kati ya nuru na giza!

Mkuu Mtoboasiri

Unadhani Kansa Mabruki angesemaje sasa iwapo Chadema hawamsapoti?

Ni wazi neno hili la Kansa limesadifu yaliyosemwa kabla hata hajachukua fomu kugombea uenyekiti (T) huko Chadema, ama unaonaje?
 
Kuna gazeti linaitwa Fahamu,

Mbona halina ufahamu

Na hatulifahamu.

Njaa inamuuma sana

Kwa hiyo anamaanisha Mbowe atachaguliwa na Wanachadema na Kansa atachaguliwa na wanaCCM

Ok...
 
Kwa mantiki yake ni poa tu kuungwa mkono na ibilisi wakati wewe ni wa Mungu wa Israel? I don't buy that maana hakuna ushirika kati ya nuru na giza!

Ameamua kujiweka wazi ili wanachama waamue wenyewe kuchagua kati ya Nuru na giza.
 
Back
Top Bottom