Sintofahamu ya utoaji zawadi mtumishi bora ikileta picha ya ubaguzi

Sintofahamu ya utoaji zawadi mtumishi bora ikileta picha ya ubaguzi

sindano butu

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2012
Posts
519
Reaction score
182
Hii haijakaa sawa watumishi walioajiriwa taasisi/idara mbalimbali mwingine kupewa zawadi kubwa sana tofauti na mwenzake ilihali wote watanzania na pia wanahudumia Taifa.

Na mzizi wa haya yote ni utofauti wa mishahara. Anayefanya kazi halmashauri au mikoani kulipwa kidogo tofauti na anayefanya kazi kwenye taasisi.

Hii haiko sawa inaleta ubaguzi na mwishowe mtoto wa mkulima ndo wengi wanaumia.

Hii inafanya watumishi walioajiriwa tamisemi , mikoani kujiona sio kitu ilihali mtumishi bora anapewa laki 5 tofauti na wataasisi kupewa milioni kadhaa.
Kuwe na usawa wa maslahi kwa watumishi wote.

Hii nchi ni yetu tunahudumiwa watanzania kwanini wengine walipwe sana tofauti na wengine. Sawa mnasema watu walipwe kulingana na uwezo sehemu halipo kiuhalisia aliyepo kijijini ana mazingira magumu tofauti na wa mjini .

Serikali iliangalie kwa jicho la pili lione jinsi kuweka mambo sawa inawaumiza watumishi moyo wa kazi.
USHAURI KWA SERIKALI- iandae programme maalumu kutoa zawadi kwa kila sehemu bila kutegemea mtu alipo hii itaongeza hamsa ya watumishi kufanya kazi na kujituma kokote walipo
 
Kwa mara nyingine nimekopa hela kwa jamaa na kumdanganya nafika mjini mara moja kumbe nilisafiri mpaka singida ,nikiamini nitakuwa mtumishi bora kwa bidii zote nilizofanya ,changanya mpaka mkuu wa mkoa kumweleza adhma yangu lakini bado nimemwagwa chini .

Hakika nchi ina wenyewe na wenyewe ndiyo wameshinda ,hii ni mara ya kwanza na ya mwisho kujipendekeza na kujituma kuliko akili na nguvu zangu kazini

Kaka Intelligent businessman nimeikosa tena unhhh 😭😭 ,fanyeni mchango wa nauli nirudi Mbeya hela niliinywa yote jana nikiamini leo nitakuwa na kibunda ila wapi😀😀
 
Kwa mara nyingine nimekopa hela kwa jamaa na kumdanganya nafika mjini mara moja kumbe nilisafiri mpaka singida ,nikiamini nitakuwa mtumishi bora kwa bidii zote nilizofanya ,changanya mpaka mkuu wa mkoa kumweleza adhma yangu lakini bado nimemwagwa chini .

Hakika nchi ina wenyewe na wenyewe ndiyo wameshinda ,hii ni mara ya kwanza na ya mwisho kujipendekeza na kujituma kuliko akili na nguvu zangu kazini

Kaka Intelligent businessman nimeikosa tena unhhh 😭😭 ,fanyeni mchango wa nauli nirudi Mbeya hela niliinywa yote jana nikiamini leo nitakuwa na kibunda ila wapi😀😀
mpigie simu mzee wao ni wao, ata kupa suluhisho 😁😂
 
Nimepewa bahasha Ina kimemo tu Cha jina langu na pongezi, natafakari sijui niwafanye nn hawa watu
 
Wacha kulialia Lilia wewe pambana gombea ubunge , gombea urais , anzisha biashara Yako uwe CEO, kopa anzisha biashara hacha kz....Dunia I hakuna haki sawa oky
 
Back
Top Bottom