Single mums and dads come this way

Single mums and dads come this way

Mkoroshokigoli

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
14,593
Reaction score
5,582
Kama wewe ni single mum/dad, aidha ulitendwa ulibebeshwa ujauzito usioutarajia ukaachwa au ulipenda kujizalia au uliletewa mtoto ukatupiwa hapo na mamaake kuenda kusikojulikana.

Uliolewa/ulioa ukaachika au kuachwa na kubebeshwa jukumu la ulezi au ni mjane/mgane umefiliwa na mumeo/mkeo.

Karibu hapa tujadiliane kuhusu changamoto za kuwa mzazi wa pekee kwako wewe kama mlezi na kwa mtoto.


  1. Kwanza Maswahibu yepi yalikukuta mpaka ukawa single mum/dad
  2. Una plan gani za maisha ya baadae?
  3. Mtoto wako analichukuliaje suala la kukosa father figure/mother figure katika makuzi yake?na unafanya jitihada gani kulisawazisha hilo?
  4. Usingle mum/dad umeaffect vipi maisha yako?
  5. Ungepewa nafasi ya kuchagua upya mkondo wa maisha yako ungechagua mkondo upi?

Karibuni
 
Mm nakaa pemben kwanza ngoja nione kama watajitokeza...
Haya sasa single mom kujen huku.
 
Hii mada ni nzuri sana sana sana....na ni ya kujenga haswaaa. Lakini humu MMU kuna pepo la kudharau na kukashifu single mums,walioachika na wale waliozaa kabla ya ndoa. Mtu anaweza akaelezea challengez na masahibu yanayompata litakuja jitu linamwambia 'ndo mkome kuvuavua ovyo'. Imagine mtu umepitia mateso na challenge kibao katika kuzaa hadi kulea mtoto na pengine hiyo mimba ulipata kwa mtu ambaye wewe ulimheshimu,ulimpenda, ukajiachia kwake ukidhani ndiye baba watoto wako af mtu anakuja na kauli kama hiyo utajisikiaje? Na huenda hata ulilazimishwa sex na mtu uliyekuwa unamwamini au ulibakwa na bahati mbaya ukashika mimba....kauli za kijinga kama hizi utazivumilia? Huwa naumia sana ninapoona mwanamke mwenzangu anadharaulika kwa kosa ambalo mwanaume pia amechangia.....naumia kwa sababu najua challenge za mahusiano, najua situations ambazo wadada wanakutana nazo katika mahusiano yao, na mbaya zaidi wanaotoa lugha za kashfa kama hizo utaona ndo mabingwa huko mtaani kwa kulazimisha ngono zisizo salama kwa wapenzi wao.
 
Hii mada ni nzuri sana sana sana....na ni ya kujenga haswaaa. Lakini humu MMU kuna pepo la kudharau na kukashifu single mums,walioachika na wale waliozaa kabla ya ndoa. Mtu anaweza akaelezea challengez na masahibu yanayompata litakuja jitu linamwambia 'ndo mkome kuvuavua ovyo'. Imagine mtu umepitia mateso na challenge kibao katika kuzaa hadi kulea mtoto na pengine hiyo mimba ulipata kwa mtu ambaye wewe ulimheshimu,ulimpenda, ukajiachia kwake ukidhani ndiye baba watoto wako af mtu anakuja na kauli kama hiyo utajisikiaje? Na huenda hata ulilazimishwa sex na mtu uliyekuwa unamwamini au ulibakwa na bahati mbaya ukashika mimba....kauli za kijinga kama hizi utazivumilia? Huwa naumia sana ninapoona mwanamke mwenzangu anadharaulika kwa kosa ambalo mwanaume pia amechangia.....naumia kwa sababu najua challenge za mahusiano, najua situations ambazo wadada wanakutana nazo katika mahusiano yao, na mbaya zaidi wanaotoa lugha za kashfa kama hizo utaona ndo mabingwa huko mtaani kwa kulazimisha ngono zisizo salama kwa wapenzi wao.
Ni kweli kabisa unayoyasema mkuu si vyema kumhukumu mtu ambae hujui amepitia maswahibu gani mpaka kufikia hapo alipo na umetaja mifano mingi tu mizuri!Kundi kubwa linalonyanyapaliwa ni la jinsia ya kike na sielewi kwanini wawe wanawake tu ambao ni wakosaji mbona wanaume wengi wanazaa tu hovyo na hawatekelezi majukumu yao na wengine ndo wanasimamia dede wanawake zao wauwe viumbe visivyo na hatia nani atawahukumu wao?
Kwa uelewa wangu mimi:mtu single na mwenye mtoto awe wa jinsia yoyote si lazima awe amezaa nje ya ndoa,!anaweza kuwa amezaa ndani ya ndoa akatengana na mwenzi wake bado ana wadhifa uleule wa kuitwa single mum/dad!
 
Ni kweli kabisa unayoyasema mkuu si vyema kumhukumu mtu ambae hujui amepitia maswahibu gani mpaka kufikia hapo alipo na umetaja mifano mingi tu mizuri!Kundi kubwa linalonyanyapaliwa ni la jinsia ya kike na sielewi kwanini wawe wanawake tu ambao ni wakosaji mbona wanaume wengu wanazaa tu hovyo na hawatekelezi majukumu yao na wengine ndo wanasimamia dede wanawake zao wauwe viumbe visivyo na hatia nani atawahukumu wao?
Kwa uelewa wangu mimi:mtu single na mwenye mtoto awe wa jinsia yoyote si lazima awe amezaa nje ya ndoa,!anaweza kuwa amezaa ndani ya ndoa akatengana na mwenzi wake bado ana wadhifa uleule wa kuitwa single mum/dad!

Wao si wanajiita vidume kwa sababu hawabebi mimba...???? Ukatili wa wanaume huu sijui mwisho wake lini
 
Kwangu Mimi ilikuwa bahati mbaya na nilipomtaarifu mhusika alikana. Baadaye alikubali lakini kila nilipotaka kujua jinsi tutakavyojipanga kumlea mwanetu mtarajiwa akawa anakwepa. It really broke my heart since sikuwa nafahamu chochote kuhusu yeye na hata home walikuja kujua nikiwa nimetimiza miez 6. Aisee I went through a lot mpaka najifungua. Hakuwa mtu wa kupiga simu kujua tunaendeleaje na hela ya matumizi mpaka atakapojisikia yeye. Mtoto alikuja kumuona akiwa na mwaka na miezi 6 tena baada ya kusogea karibu....changamoto ni nyingi lakini kubwa kwangu ni pale napoulizwa " mama baba yuko wapi? " au anapochukua simu na kujifanya kama vile anaongea na baba yake akiomba aletewe soseji, pipi, matunda n.k. Huwa naumia sana natamani he was there for her. Sijui kama niko sahihi but nimepanga kwenda nyumbani kwao (baba) at least mtoto awatambue ndugu zake pia kufight 4 the last time mwanangu apate mapenzi ya baba na mama, na kama itashindikana will move on with my life
 
Kwangu Mimi ilikuwa bahati mbaya na nilipomtaarifu mhusika alikana. Baadaye alikubali lakini kila nilipotaka kujua jinsi tutakavyojipanga kumlea mwanetu mtarajiwa akawa anakwepa. It really broke my heart since sikuwa nafahamu chochote kuhusu yeye na hata home walikuja kujua nikiwa nimetimiza miez 6. Aisee I went through a lot mpaka najifungua. Hakuwa mtu wa kupiga simu kujua tunaendeleaje na hela ya matumizi mpaka atakapojisikia yeye. Mtoto alikuja kumuona akiwa na mwaka na miezi 6 tena baada ya kusogea karibu....changamoto ni nyingi lakini kubwa kwangu ni pale napoulizwa " mama baba yuko wapi? " au anapochukua simu na kujifanya kama vile anaongea na baba yake akiomba aletewe soseji, pipi, matunda n.k. Huwa naumia sana natamani he was there for her. Sijui kama niko sahihi but nimepanga kwenda nyumbani kwao (baba) at least mtoto awatambue ndugu zake pia kufight 4 the last time mwanangu apate mapenzi ya baba na mama, na kama itashindikana will move on with my life

very interesting, sorry devota vijance
 
Last edited by a moderator:
Devota-too sad.inaumiza kwa kweli mtoto anavyofanya. watoto wanahitaji mapenzi ya baba na mama---endelea na mpango wako huo, na Mungu akutangulie
 
Ile mada ya Blue G inayohusu watoto nilichangia kwa moyo mweupe lakini sijui kwa nini mikono yangu kwa hii inakuwa mizito kutaipuuu... labda ni haya makande niliyokula. Nitarudi jioni baada ya kuhojiana na nafsi maana kama single parented na single mom nina mengi ya kusema, ila nampa pole devotha vijance na kumshauri akubali hali aendelee na maisha badala ya kuota kuoana na mwanaume irresponsible na asiyempenda ili tu mwanae aite baba. Ni vyema kujitoa mhanga kwa ajili ya watoto lakini tuwe na kiasi.
 
I wish watu wangeacha kuwa kutoa hukumu, tuwape nafasi single parents watoe changamoto za maisha bila wenzi/wazazi wenzao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom