Singida: Watu 6 wafariki kwa ajali ya gari

Nasema Uongo Ndugu Zangu

JF-Expert Member
Apr 28, 2020
279
773
Ajali mbaya iliyo husisha gari dogo aina ya Raum imetokea wilayani Mkalama katika mkoa wa Singida.

Chanzo cha ajali ni mwendo kasi.

Mzee Kinana nilikwambia kupitia uzi fulani hapa, kazi iendelee.

========

Watu sita wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria aina ya Toyota Raum, kuacha njia na kupinduka katika eneo la Iguguno Ushamba Wilayani Mkalama Mkoani Singida, huku chanzo kikitajwa kuwa ni mwendokasi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Stella Mutabihirwa, amesema tukio hilo limetokea jana na kusema Dereva wa gari hilo alikuwa anaendesha bila kuchukua tahadhari na ndipo gari hilo lilipohamia upande wa pili wa Barabara na kupinduka mara tatu.

Ajali hiyo imetokea kwenye Barabara Kuu ya Dar es Salaam - Mwanza wakati abiria wa gari hilo wakitokea Arusha kuelekea Mwanza ambapo Watu watano kati yao walipoteza maisha papohapo huku Dereva wa gari hilo akipoteza maisha wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Singida.
 
Ajali mbaya iliyo husisha gari dogo aina ya Raum imetokea wilayani Mkalama katika mkoa wa Singida.

Chanzo cha ajali ni mwendo kasi.

Mzee Kinana nilikwambia kupitia uzi fulani hapa, kazi iendelee.
Wewe acha ligi na wanasiasa wala haitakusaidia kitu ajali zimekuwa zikitokea Mara nyingi hata kabla ya Kauli ya Kinana.Tafuta pesa weka akiba upete life.
 
Ajali mbaya iliyo husisha gari dogo aina ya Raum imetokea wilayani Mkalama katika mkoa wa Singida.

Chanzo cha ajali ni mwendo kasi.

Mzee Kinana nilikwambia kupitia uzi fulani hapa, kazi iendelee.
papohapo huku Dereva wa gari hilo akipoteza maisha wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Singida.
Ni sawa na upepo wa Same, Singida kuna upepo mkali sana, hivyo dereva kama siyo mzoefu, na gari ikiwa kama hizo za jamii ya Noah with high speed ajali ni lazima. Tuchukue tahadhari
 
Tatizo ni la Abiria kushindwa kumkemea dereva aache mwendo kasi hadi anawaua
Watakao nusurika ndoo wanatangaza dereva alikuwa mwendo kasi!
Naomba wahusika wawashughulikie watu wa hivyo bila huruma ili iwe Fundisho...
 
Haya ndio Kinana aliyataka. Watu wasafiri kwa uhuru. Maana yake watu wafe mapema.

Marekani ambako wana high ways za kueleweka, zimenyooka na kila aina ya miundombinu ya barabara bora trafiki hawakosekani halafu Kinana anataka barabara hizi wanazojenga ccm zenye matuta na mashimo barabarani watu waruhusiwe kutembea wanavyotaka.

Kinana anataka nchi ijiendeshe kisela kama enzi za kikwete, unregulated county. Haya ndio wanayataka.

Ni yale yale ya Samia alisema wafanyakazi walikua na nidhamu ya uoga, baadae akakiri kwamba nidhamu imeshuka zaidi.

Kinana anataka nchi iniendeshe kama autopilot kama Somalia(home).
 
Back
Top Bottom