Singida: Godbless Lema ameachiwa kwa dhamana leo, baada ya kushikiliwa Polisi tangu Jumatatu Machi 2, 2020

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,815
4,565
1583399273989.png

Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA), Godbless Lema ameachiwa kwa dhamana leo, baada ya kushikiliwa Polisi tangu Jumatatu Machi 2, 2020

Lema alienda kuripoti Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Polisi (RCO) Arusha kama alivyotakiwa kufanya baada ya kupigiwa simu na Polisi ambao walienda kwake na kumkosa

Baada ya hapo alisafirishwa kwenda Kituo Kikuu cha Polisi Singida ambapo alihojiwa akituhumiwa kutoa taarifa za upotoshaji zenye lengo la kuchonganisha Jeshi hilo na Wananchi

Aidha, Katibu wa CHADEMA Wilaya Singida Mjini, alisema Lema alimwambia kuwa kosa analodaiwa kutenda ni kutaja orodha ya watu 14 waliouawa Manyoni kwa kuchinjwa na kuchomwa moto.

PIA SOMA:
Godbless Lema aitwa na Ofisi ya RCO Arusha, asafirishwa na Polisi usiku kwenda Singida
 

Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA), Godbless Lema ameachiwa kwa dhamana leo, baada ya kushikiliwa Polisi tangu Jumatatu Machi 2, 2020

Lema alienda kuripoti Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa Polisi (RCO) Arusha kama alivyotakiwa kufanya baada ya kupigiwa simu na Polisi ambao walienda kwake na kumkosa

Baada ya hapo alisafirishwa kwenda Kituo Kikuu cha Polisi Singida ambapo alihojiwa akituhumiwa kutoa taarifa za upotoshaji zenye lengo la kuchonganisha Jeshi hilo na Wananchi

Aidha, Katibu wa CHADEMA Wilaya Singida Mjini, alisema Lema alimwambia kuwa kosa analodaiwa kutenda ni kutaja orodha ya watu 14 waliouawa Manyoni kwa kuchinjwa na kuchomwa moto.

PIA SOMA:
Godbless Lema aitwa na Ofisi ya RCO Arusha, asafirishwa na Polisi usiku kwenda Singida
Shetani hajawahi kumshinda Mungu
 
Hivi polisi huwa hawaoni aibu kila kitu huwa mpaka washinikizwe ni kama huwa hawajui kazi yao,au wamezoea kuamrishwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Wnaijua kazi yao vizuri, nasi tujue pa kuropokea na pasipo stahili. Mtu unayo majina ya Marehemu waliouwawa, na unaficha ya watuhumiwa au yale majambazi waliofanya unyama huo, kwa sababu ya kuyatumia majina ya hao wauwaji, kwa manufa ya kujijenga kisiasa.

Lema faida aliyoitaka ni kuufanya uhasama huo kama mtaji wa kisiasa, ni lazima upingwe.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wnaijua kazi yao vizuri, nasi tujue pa kuropokea na pasipo stahili. Mtu unayo majina ya Marehemu waliouwawa, na unaficha ya watuhumiwa au yale majambazi waliofanya unyama huo, kwa sababu ya kuyatumia majina ya hao wauwaji, kwa manufa ya kujijenga kisiasa.

Lema faida aliyoitaka ni kuufanya uhasama huo kama mtaji wa kisiasa, ni lazima upingwe.



Sent using Jamii Forums mobile app
Anayeweza kuficha majina ya majambazi ni yule mwenye mandate ya kuwatafuta kwa wengine tukiwajua mguvu ya umma inawahusu!!!!!!
 
Back
Top Bottom