Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 58,636
- 220,349
Habari za kutwa waungwana,
Nina rafiki tumefahamiana miaka minne iliyopita, kufahamiana kwetu tulikutana kwenye sherehe na tulikaa viti vya karibu na tuliongea na kucheza mziki pamoja. Wakati sherehe ikiendelea nilianza kufikiria usafiri wa kunirudisha nyumbani, nilianza kumuuliza jinsi nitakavyopata tax, aliniuliza kuelelekea wapi? Hapo ndipo niligundua ni jirani yangu kabisa.
Tulichukua tax moja, na baada ya pale tulibadilishana namba za simu.
Kesho yake alinipigia simu, alinialika niende kanisani kwao, nililipenda lile kanisa, niliendelea kusali pale kwa muda. Nilikuja kufahamu huyu kaka ni mlokole wa kufa mtu, mara nyingi ananipigia simu tunachat, mazungumzo mengi ni current affairs, dini, na mara nyingine ananipa offer za dinner.
Kuna wakati nilimwambia nitakwenda nyumbani kuwaona wazazi, aliniambia nisiondoke bila kumuaga, siku ninaondoka alikuja na bahasha nzito. Niliifungua nikiwa njiani, aliniwekea mpunga wakueleweka. Nilimtumia message ya asante, alinijibu asante na karibu. Nilivyorudi nilimfahamisha nimerudi basi. Hajawahi kunisimulia habari ya girl friend, wala hajanitongoza ni mwaka wa nne huu.
Simuelewi huyu rafiki yangu nisaidieni ndugu zangu.
Nina rafiki tumefahamiana miaka minne iliyopita, kufahamiana kwetu tulikutana kwenye sherehe na tulikaa viti vya karibu na tuliongea na kucheza mziki pamoja. Wakati sherehe ikiendelea nilianza kufikiria usafiri wa kunirudisha nyumbani, nilianza kumuuliza jinsi nitakavyopata tax, aliniuliza kuelelekea wapi? Hapo ndipo niligundua ni jirani yangu kabisa.
Tulichukua tax moja, na baada ya pale tulibadilishana namba za simu.
Kesho yake alinipigia simu, alinialika niende kanisani kwao, nililipenda lile kanisa, niliendelea kusali pale kwa muda. Nilikuja kufahamu huyu kaka ni mlokole wa kufa mtu, mara nyingi ananipigia simu tunachat, mazungumzo mengi ni current affairs, dini, na mara nyingine ananipa offer za dinner.
Kuna wakati nilimwambia nitakwenda nyumbani kuwaona wazazi, aliniambia nisiondoke bila kumuaga, siku ninaondoka alikuja na bahasha nzito. Niliifungua nikiwa njiani, aliniwekea mpunga wakueleweka. Nilimtumia message ya asante, alinijibu asante na karibu. Nilivyorudi nilimfahamisha nimerudi basi. Hajawahi kunisimulia habari ya girl friend, wala hajanitongoza ni mwaka wa nne huu.
Simuelewi huyu rafiki yangu nisaidieni ndugu zangu.