Simwelewi rafiki yangu anataka nini kwangu

Simwelewi rafiki yangu anataka nini kwangu

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
58,636
Reaction score
220,349
Habari za kutwa waungwana,

Nina rafiki tumefahamiana miaka minne iliyopita, kufahamiana kwetu tulikutana kwenye sherehe na tulikaa viti vya karibu na tuliongea na kucheza mziki pamoja. Wakati sherehe ikiendelea nilianza kufikiria usafiri wa kunirudisha nyumbani, nilianza kumuuliza jinsi nitakavyopata tax, aliniuliza kuelelekea wapi? Hapo ndipo niligundua ni jirani yangu kabisa.

Tulichukua tax moja, na baada ya pale tulibadilishana namba za simu.
Kesho yake alinipigia simu, alinialika niende kanisani kwao, nililipenda lile kanisa, niliendelea kusali pale kwa muda. Nilikuja kufahamu huyu kaka ni mlokole wa kufa mtu, mara nyingi ananipigia simu tunachat, mazungumzo mengi ni current affairs, dini, na mara nyingine ananipa offer za dinner.

Kuna wakati nilimwambia nitakwenda nyumbani kuwaona wazazi, aliniambia nisiondoke bila kumuaga, siku ninaondoka alikuja na bahasha nzito. Niliifungua nikiwa njiani, aliniwekea mpunga wakueleweka. Nilimtumia message ya asante, alinijibu asante na karibu. Nilivyorudi nilimfahamisha nimerudi basi. Hajawahi kunisimulia habari ya girl friend, wala hajanitongoza ni mwaka wa nne huu.

Simuelewi huyu rafiki yangu nisaidieni ndugu zangu.
 
si best friend tu au unahis jamaa domo zege?
Sema wazi unataka mambo mwambie tu kuwa unataka mtekenyo jamaa anakusikilizia weww
Ninaogopa nikimueleza inaweza kuvunja urafiki wetu, jamaa ni mlokole, pili si elewi kama ndiye yeye niliyeletewa jamani mwaka wa nne huu sijui tunaelekea wapi. Pia hua ananipikia chakula nikiwa nimechoka, analeta kwenye hot pot.
 
Habari za kutwa waungwana,
Nina rafiki tumefahamiana miaka minne iliyopita, kufahamiana kwetu tulikutana kwenye shere na tulikaa viti vya karibu na tuliongea na kucheza mziki pamoja. Wakati sherehe ikiendelea nilianza kufikiria usafiri wa kunirudisha nyumbani, nilianza kumuuliza jinsi nitakavyopata tax, aliniuliza kuelelekea wapi? Hapo ndipo niligundua ni jirani yangu kabisa. Tulichukua tax moja, na baada ya pale tulibadilishana namba za simu.
Kesho yake alinipigia simu, alinialika niende kanisani kwao, nililipenda lile kanisa, niliendelea kusali pale kwa muda. Nilikuja kufahamu huyu kaka ni mlokole wa kufa mtu, mara nyingi ananipigia simu tunachat, mazungumzo mengi ni current affairs, dini, na mara nyingine ananipa offer za dinner.
Kuna wakati nilimwambia nitakwenda nyumbani kuwaona wazazi, aliniambia nisiondoke bila kumuaga, siku ninaondoka alikuja na bahasha nzito. Niliifungua nikiwa njiani, aliniwekea mpunga wakueleweka. Nilimtumia message ya asante, alinijibu asante na karibu. Nilivyorudi nilimfahamisha nimerudi basi. Hajawahi kunisimulia habari ya girl friend, wala hajanitongoza ni mwaka wa nne huu.
Simuelewi huyu rafiki yangu nisaidieni ndugu zangu.

Kwa nini mambo yetu ya nje unayaleta huku JF?

Unataka nikuchape wewe eeh?
 
Ndo shida yenu Wanawake, angekutongoza ungekilimbia huku, ohhh huyu jirani ananichukuliaje, kakaa kimya unaona siyo. Si kila mwanaume akikupa kitu au akiwa karibu na wewe anakutaka kimapenzi wengine wanataka kampani tu, mapenzi yako kwa mwingine.
 
Ndo shida yenu Wanawake, angekutongoza ungekilimbia huku, ohhh huyu jirani ananichukuliaje, kakaa kimya unaona siyo. Si kila mwanaume akikupa kitu au akiwa karibu na wewe anakutaka kimapenzi wengine wanataka kampani tu, mapenzi yako kwa mwingine.
Ningeelewa kama ingekuwa company tu, sasa na mambo ya kuniwekea pesa kwenye bahasha nayo ni company?
 
Hao ndi marafiki wema ... Kama umempenda we jishobokeshe na khanga moja tu...
Kama hajakutamkia chochote na anakujali we kua na amani.. Ila kama una yako kichwani amini nakwambia atakugo*** tu
 
Itakua ww hauna mvuto wa kutosha
Inawezekana, lakini anaiomba tutoke kwa chakula kwenye hoteli nzuri, sasa kama sina mvuto mbona haoni haya kwenda na mimi in public places, pia tunakwenda wote kanisani J2.
 
Back
Top Bottom