Hakwea
Member
- Oct 25, 2018
- 16
- 19
*SIMULIZI YA MAISHA: ZAWADI YA ADHABU*
*MTUNZI: TIMOTHY PETER MSUYA “KIRAKA”*
*Mawasiliano +255 763 305 605*
*Utangulizi*
[Kisha nikarudi tena, na kuona ubatili chini ya jua.
Kuna mtu aliye peke yake, wala hana wa pili wake; naam, hana mwana wala ndugu; hata hivyo amali yake haina mwisho, wala macho yake hayashibi utajiri. Basi asema, Ni kwa ajili ya nani nafanya kazi, na kujinyima nafsi yangu mema?
Hayo nayo ni ubatili, naam, ni taabu kubwa!!
Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao. Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua! Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto?
[Mhubiri 4: 7-11]
******
*Nimefundishwa kuwa…*
_“Kuwaza jambo jema ni jambo la kwanza halafu kutenda jema ni jambo la pili tofauti kabisa!! Kuna wakati unawaza jambo jema ukiwa katikati ya kutenda uovu, au ukawa uko katikati ya kutenda mema huku akili yako ikijiwazia uovu mtupu!! Ingawa mara kadhaa nafsi inaweza kukusuta, si mara zote unaweza kuwa imara kiasi cha kuamua kutenda kile chema unachokiwaza. Lakini daima, uamuzi juu ya kutenda jema, uwe umeliwaza ama la, unao mwenyewe.. Ukiamua kutenda jema, hakuna cha kukuzuia!_
*Una hiyari ya kukubali au kukataa….*
*NINAWAANDIKIA HAYA KATIKA SEHEMU YA KWANZA*
_Alikuwa ndani ya bajaji…_
Jua kali lililoambatana na upepo mkali uliobeba vumbi la kutosha vilishindana kuonyesha umwamba wake! Jua lilimulika kana kwamba lilikuwa likitafuta kitu fulani kilichopotelea ardhini bila mafanikio. Upepo ukashirikiana na vumbi kuichafua hewa kwa makusudi bila kujali kuwa kuna viumbe waliihitaji hewa ile kwa matumizi yaliyohalalishwa. Ulikuwa ni mwanzoni mwa mwezi wa kumi na moja.
Vumbi lilikuwa likitimka bila sababu yoyote ya msingi!!
Kwa wakazi wengi wa Mji wa Singida, hii ilikuwa ni hali ya kawaida kabisa na walikuwa wameizoea na kuifanya sehemu ya maisha yao ya kila siku. Yeye hakuwa na sifa ya kuitwa mkazi mzoefu wa mji huu wa Singida. Vurumai hii ilimkera! Alijikuta akipiga chafya mfululizo huku kamasi nyepesi zikimkereketa puani, akaufikia mfuko wake wa suruali na kukitoa kitambaa safi cheupe, akapenga pua zake asiambulie chochote cha maana.
Akasonya moyoni huku akikunja uso wake uliojaliwa uzuri wa kiume. Ule upepo mkali uliokuwa ukiipuliza bajaji iliyokuwa ikitimka mbio ulimwingia machoni, machozi yakawa yanamchonyota machoni
Alikereka.
Kwa mbali, mawazo yake yalimpeleka Dar es salaam, jiji ambalo pamoja na kukulia na kupatia elimu yake yote, ya darasani na ya maisha, ndilo aliloanzia kufanya kazi. Alitamani sana kuwa Dar es salaam lakini akalipuuza hilo mara moja. Alishaamua kubadili kabisa maisha yake na mojawapo kati ya mabadiliko ya muhimu aliyoyafanya ilikuwa ni kuhamishia makazi yake mkoani Singida. Yaliyomkuta jijini Dar es salaam hakutaka kuyakumbuka hata kidogo, na muhimu kwa wakati ule ilikuwa ni kuyaanza upya maisha yake ambayo almanusura yapotee alipokuwa jijini Dar es salaam. Kwa mbali, ile kero ya vumbi na upepo vilivyokuwa vimemzunguka akavikubali na kujikuta akitabasamu tabasamu hafifu.
Alishaanza kupazoea na kupapenda Singida.
“Tumefika bro” Sauti ilimzindua kutoka mawazoni na akajikuta akishtuka kidogo.
“OK”. Aliitikia huku akishuka kutoka kwenye bajaji ile. Akalipia na kuvuka barabara huku akiiweka sawa tai iliyokuwa imemkaba kooni. Hapo tena, lile timbwili la upepo mkali uliochanganyika na mchanga pamoja na vumbi vikaubusu uso wake na kumuingia kidogo kwenye macho yaliyokuwa nyuma ya miwani aliyokuwa amevaa. Kwa hatua za haraka haraka akalifikia geti la Tanzania Institute of Accountancy ambacho wakazi wengi wa mji ule walipendelea kukiita “uhasibu”.
Bado upepo na vumbi havikumuhurumia msomi huyu, viliendelea kumzomea vikimsindikiza mpaka alipozifikia ngazi za kuingilia ofisini kwake. Hapo vikambusu kwa mara ya mwisho na kumwacha huru.
Naam.. Hapo akawa amefika ofisini kwake. Kule kutembea kwa haraka na kurukaruka kukwepa vumbi na mchanga sasa vikakoma na mwendo wake wa maringo na mikogo ya kisomi vikarejea.
Clifford Chiziza ndilo jina lililokuwapo kwenye vyeti vyake vyote vya shule na vitambulisho vingine vyote. Msomi wa shahada ya uhasibu aliyesajiliwa na bodi ya taifa ya uhasibu na mmiliki mwenza wa kampuni ya Elites Financial Consultants, Clifford aliyependa zaidi kuitwa Cliff alikuwa mkufunzi katika chuo cha TIA tawi la Singida akijikita zaidi katika masomo ya ukaguzi wa hesabu pamoja na uhasibu. Akiwa na miaka 30 tu, alikuwa na sura ya kuvutia iliyotumika pia kuhifadhi tabasamu tamu lililochanua mara kwa mara alipokuwa na watu.
Clifford alitosha kabisa kutumika kumwelezea mwanaume mtanashati. Mavazi yake alijua kuyapangilia vema, mwendo wake wa kiume kabisa, namna alivyozungumza na kupangilia maneno yake pamoja na elimu ya kutosha katika fani yake vilitosha kabisa kumfanya mwanamke yeyote, hata wale walioolewa kumtazama kwa jicho la husuda.
Clifford alikuwa mwanaume hasa!
Haraka aliifikia ofisi aliyokuwa akiitumia kwa kushirikiana na mkufunzi mwingine wa kike aliyeitwa Zulfa Moses. Kwa bahati, alimkuta akiwa amezama katika jitabu kubwa akipekua pekua hapa na pale.
“Hallo Malkia… A very good afternoon to you” Alisabahi huku akimfikia Zulfa na kumpa mkono, kisha akaupokea ule wa Zulfa na kuubusu.
“Afternoon Chiziza.. Za uzima wako?” Aliitikia Zulfa huku kiaibu kikikatiza katika mitaa ya macho yake kwa kule kupokea busu laini kutoka katika papi za midomo ya Clifford..
“There we go again.. Chiziza is that old fella bana.. Mi ukiniita Chiziza nahisi nimezeeka wakati ndio kwanza damu inachemka. Clifford is a name and a half to me” Alisema Clifford huku akiijongea meza yake na kukaa juu yake huku akilegeza tai yake na kutupia kibegi maalumu cha kubebea kompyuta alichokuwa nacho.
“C’moon Cliff.. Umri nao unakwenda bana, na kutumia jina lako naona kama vile nakupa sifa za utoto ambazo zimekupita siku nyingi. Mbona mimi kuna watu wananiita Madam Mosses and I’m jus’ cool with’it?” Alijitetea Zulfa
“You see.. You see… Haya sasa, umeniita Cliff, just the way I like it to be and it sounds really really cool.. Cliff umefupisha Clifford. Hiyo Chiziza ukiifupisha si tunakuwa tunatukanana?” Clifford alilalamika huku uso wake ukichomoza lile tabasamu ambalo alikuwa akilitumia nyakati muhimu hasa awapo na mwanamke mzuri.
Alichokuwa anakitaka akakipata. Kicheko cha kilegevu kikamtoka Zulfa huku akilazimika kukifunika kile kitabu kilichokuwa mikononi mwake. Alicheka kwa sekunde kadhaa huku macho yake yaliyolegea yakimwelekea Clifford.
“Mh.. So you mean Chizi? We mwanaume una vituko kweli” Alisema katikati ya kicheko kile.
Walijadili hili na lile, huku Clifford akitumia muda mwingi kulalamika juu ya hali ya hewa ya mji ule, namna upepo na vumbi vilivyokuwa vikimchachafya na namna usiku alivyokuwa akikosa usingizi kwa kelele za paa la nyumba ambalo lilikuwa likiadabishwa ipaswavyo na upepo ule. Alilalamika pia kuhusu mwenye nyumba kuonekana kutokujali adha ile aliyokuwa akiipata ya kulazimika kukesha akiwa analisikiliza paa lililokuwa likilalamika pasi na msaada wowote. Kwa kusulubiwa na upepo.
“We nawe unadeka sana.. Nyumba uliyopata ni mpya kabisa, na huenda ni changamoto tu za upepo mkali au kuna pahala mafundi hawakuwa makini. Badae nitampigia fundi mmoja mzuri ninaishi naye jirani, we jiandae tu na mwenye nyumba wako aje akusaidie. Umeridhika?” Alimaliza Zulfa.
“Kwakweli hilo limekaa poa, ndio maana nakupendaga mamalake, mmmmmwaaaah” Alichombeza Clifford huku akiachia busu hewani. “Na yule mzee wala sihangaiki kumtaarifu. We nipe namba za huyo jamaa aje anisaidie, mengine tutajua mbele kwa mbele”
“Au kama usumbufu umezidi hamia kwangu basi mpaka atakapotengeneza” Zulfa alisema huku lile jicho lake kubwa lililolegea bila utaratibu akilitumia ipasavyo. Alivaa sura ya utani lakini kwa mwanaume mwerevu kama Clifford alitambua upesi kuwa sehemu fulani ya akili ya mwanamke yule ilimaanisha kile alichokisema.
“Ah.. Wanawake wazuri kama ninyi tena wenye elimu ya kutosha huwa mna wakubwa wanawaweka mjini. Usinitafutie kesi ya mauaji bure mwana wa Chiziza mie.. Hivi una kipindi baadae? Nadhani nitahitaji projector yako, ya kwangu wanaitumia kule procurement” Clifford alibadili mada upesi na aliona waziwazi namna Zulfa alivyokerwa na kitendo kile lakini hakujali.
Hili lilipoisha, wote wakazama katika kujiandaa kwa vipindi vya mchana ule. Mara kwa mara Clifford alikuwa akinua mkono na kutazama saa yake ili kujua muda, na ilipotimu saa nane mchana, akainuka na kompyuya mpakato na kibegi kingine kilichokuwa na projector ya Madam Zulfa na safari ya darasani ikaanza.
Kufundisha masomo ya ukaguzi wa hesabu za fedha na masomo mengine ya uhasibu ilikuwa ni kazi aliyoipenda na aliyoifanya kwa moyo sana huku wanafunzi wake wengi wakimsifia kwa kile kipaji chake kikubwa cha kuweza kufundisha masomo magumu lakini kwa namna iliyowasaidia wengi kumwelewa vema. Pia alikuwa na ukaribu mkubwa na wanafunzi wake, na hakusita kuwasaidia popote walipohitaji msaada wake. Hakika alikuwa kipenzi cha wengi.
Hakuwahi kujua kuwa ufanisi wake katika kazi yake hiyo ungekuja kumgeuka na kumuingiza katika adhabu…
Hakujua kuwa ufanisi huo ungemtunuku zawadi kubwa…
_Zawadi ya adhabu…._
*MTUNZI: TIMOTHY PETER MSUYA “KIRAKA”*
*Mawasiliano +255 763 305 605*
*Utangulizi*
[Kisha nikarudi tena, na kuona ubatili chini ya jua.
Kuna mtu aliye peke yake, wala hana wa pili wake; naam, hana mwana wala ndugu; hata hivyo amali yake haina mwisho, wala macho yake hayashibi utajiri. Basi asema, Ni kwa ajili ya nani nafanya kazi, na kujinyima nafsi yangu mema?
Hayo nayo ni ubatili, naam, ni taabu kubwa!!
Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao. Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua! Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto?
[Mhubiri 4: 7-11]
******
*Nimefundishwa kuwa…*
_“Kuwaza jambo jema ni jambo la kwanza halafu kutenda jema ni jambo la pili tofauti kabisa!! Kuna wakati unawaza jambo jema ukiwa katikati ya kutenda uovu, au ukawa uko katikati ya kutenda mema huku akili yako ikijiwazia uovu mtupu!! Ingawa mara kadhaa nafsi inaweza kukusuta, si mara zote unaweza kuwa imara kiasi cha kuamua kutenda kile chema unachokiwaza. Lakini daima, uamuzi juu ya kutenda jema, uwe umeliwaza ama la, unao mwenyewe.. Ukiamua kutenda jema, hakuna cha kukuzuia!_
*Una hiyari ya kukubali au kukataa….*
*NINAWAANDIKIA HAYA KATIKA SEHEMU YA KWANZA*
_Alikuwa ndani ya bajaji…_
Jua kali lililoambatana na upepo mkali uliobeba vumbi la kutosha vilishindana kuonyesha umwamba wake! Jua lilimulika kana kwamba lilikuwa likitafuta kitu fulani kilichopotelea ardhini bila mafanikio. Upepo ukashirikiana na vumbi kuichafua hewa kwa makusudi bila kujali kuwa kuna viumbe waliihitaji hewa ile kwa matumizi yaliyohalalishwa. Ulikuwa ni mwanzoni mwa mwezi wa kumi na moja.
Vumbi lilikuwa likitimka bila sababu yoyote ya msingi!!
Kwa wakazi wengi wa Mji wa Singida, hii ilikuwa ni hali ya kawaida kabisa na walikuwa wameizoea na kuifanya sehemu ya maisha yao ya kila siku. Yeye hakuwa na sifa ya kuitwa mkazi mzoefu wa mji huu wa Singida. Vurumai hii ilimkera! Alijikuta akipiga chafya mfululizo huku kamasi nyepesi zikimkereketa puani, akaufikia mfuko wake wa suruali na kukitoa kitambaa safi cheupe, akapenga pua zake asiambulie chochote cha maana.
Akasonya moyoni huku akikunja uso wake uliojaliwa uzuri wa kiume. Ule upepo mkali uliokuwa ukiipuliza bajaji iliyokuwa ikitimka mbio ulimwingia machoni, machozi yakawa yanamchonyota machoni
Alikereka.
Kwa mbali, mawazo yake yalimpeleka Dar es salaam, jiji ambalo pamoja na kukulia na kupatia elimu yake yote, ya darasani na ya maisha, ndilo aliloanzia kufanya kazi. Alitamani sana kuwa Dar es salaam lakini akalipuuza hilo mara moja. Alishaamua kubadili kabisa maisha yake na mojawapo kati ya mabadiliko ya muhimu aliyoyafanya ilikuwa ni kuhamishia makazi yake mkoani Singida. Yaliyomkuta jijini Dar es salaam hakutaka kuyakumbuka hata kidogo, na muhimu kwa wakati ule ilikuwa ni kuyaanza upya maisha yake ambayo almanusura yapotee alipokuwa jijini Dar es salaam. Kwa mbali, ile kero ya vumbi na upepo vilivyokuwa vimemzunguka akavikubali na kujikuta akitabasamu tabasamu hafifu.
Alishaanza kupazoea na kupapenda Singida.
“Tumefika bro” Sauti ilimzindua kutoka mawazoni na akajikuta akishtuka kidogo.
“OK”. Aliitikia huku akishuka kutoka kwenye bajaji ile. Akalipia na kuvuka barabara huku akiiweka sawa tai iliyokuwa imemkaba kooni. Hapo tena, lile timbwili la upepo mkali uliochanganyika na mchanga pamoja na vumbi vikaubusu uso wake na kumuingia kidogo kwenye macho yaliyokuwa nyuma ya miwani aliyokuwa amevaa. Kwa hatua za haraka haraka akalifikia geti la Tanzania Institute of Accountancy ambacho wakazi wengi wa mji ule walipendelea kukiita “uhasibu”.
Bado upepo na vumbi havikumuhurumia msomi huyu, viliendelea kumzomea vikimsindikiza mpaka alipozifikia ngazi za kuingilia ofisini kwake. Hapo vikambusu kwa mara ya mwisho na kumwacha huru.
Naam.. Hapo akawa amefika ofisini kwake. Kule kutembea kwa haraka na kurukaruka kukwepa vumbi na mchanga sasa vikakoma na mwendo wake wa maringo na mikogo ya kisomi vikarejea.
Clifford Chiziza ndilo jina lililokuwapo kwenye vyeti vyake vyote vya shule na vitambulisho vingine vyote. Msomi wa shahada ya uhasibu aliyesajiliwa na bodi ya taifa ya uhasibu na mmiliki mwenza wa kampuni ya Elites Financial Consultants, Clifford aliyependa zaidi kuitwa Cliff alikuwa mkufunzi katika chuo cha TIA tawi la Singida akijikita zaidi katika masomo ya ukaguzi wa hesabu pamoja na uhasibu. Akiwa na miaka 30 tu, alikuwa na sura ya kuvutia iliyotumika pia kuhifadhi tabasamu tamu lililochanua mara kwa mara alipokuwa na watu.
Clifford alitosha kabisa kutumika kumwelezea mwanaume mtanashati. Mavazi yake alijua kuyapangilia vema, mwendo wake wa kiume kabisa, namna alivyozungumza na kupangilia maneno yake pamoja na elimu ya kutosha katika fani yake vilitosha kabisa kumfanya mwanamke yeyote, hata wale walioolewa kumtazama kwa jicho la husuda.
Clifford alikuwa mwanaume hasa!
Haraka aliifikia ofisi aliyokuwa akiitumia kwa kushirikiana na mkufunzi mwingine wa kike aliyeitwa Zulfa Moses. Kwa bahati, alimkuta akiwa amezama katika jitabu kubwa akipekua pekua hapa na pale.
“Hallo Malkia… A very good afternoon to you” Alisabahi huku akimfikia Zulfa na kumpa mkono, kisha akaupokea ule wa Zulfa na kuubusu.
“Afternoon Chiziza.. Za uzima wako?” Aliitikia Zulfa huku kiaibu kikikatiza katika mitaa ya macho yake kwa kule kupokea busu laini kutoka katika papi za midomo ya Clifford..
“There we go again.. Chiziza is that old fella bana.. Mi ukiniita Chiziza nahisi nimezeeka wakati ndio kwanza damu inachemka. Clifford is a name and a half to me” Alisema Clifford huku akiijongea meza yake na kukaa juu yake huku akilegeza tai yake na kutupia kibegi maalumu cha kubebea kompyuta alichokuwa nacho.
“C’moon Cliff.. Umri nao unakwenda bana, na kutumia jina lako naona kama vile nakupa sifa za utoto ambazo zimekupita siku nyingi. Mbona mimi kuna watu wananiita Madam Mosses and I’m jus’ cool with’it?” Alijitetea Zulfa
“You see.. You see… Haya sasa, umeniita Cliff, just the way I like it to be and it sounds really really cool.. Cliff umefupisha Clifford. Hiyo Chiziza ukiifupisha si tunakuwa tunatukanana?” Clifford alilalamika huku uso wake ukichomoza lile tabasamu ambalo alikuwa akilitumia nyakati muhimu hasa awapo na mwanamke mzuri.
Alichokuwa anakitaka akakipata. Kicheko cha kilegevu kikamtoka Zulfa huku akilazimika kukifunika kile kitabu kilichokuwa mikononi mwake. Alicheka kwa sekunde kadhaa huku macho yake yaliyolegea yakimwelekea Clifford.
“Mh.. So you mean Chizi? We mwanaume una vituko kweli” Alisema katikati ya kicheko kile.
Walijadili hili na lile, huku Clifford akitumia muda mwingi kulalamika juu ya hali ya hewa ya mji ule, namna upepo na vumbi vilivyokuwa vikimchachafya na namna usiku alivyokuwa akikosa usingizi kwa kelele za paa la nyumba ambalo lilikuwa likiadabishwa ipaswavyo na upepo ule. Alilalamika pia kuhusu mwenye nyumba kuonekana kutokujali adha ile aliyokuwa akiipata ya kulazimika kukesha akiwa analisikiliza paa lililokuwa likilalamika pasi na msaada wowote. Kwa kusulubiwa na upepo.
“We nawe unadeka sana.. Nyumba uliyopata ni mpya kabisa, na huenda ni changamoto tu za upepo mkali au kuna pahala mafundi hawakuwa makini. Badae nitampigia fundi mmoja mzuri ninaishi naye jirani, we jiandae tu na mwenye nyumba wako aje akusaidie. Umeridhika?” Alimaliza Zulfa.
“Kwakweli hilo limekaa poa, ndio maana nakupendaga mamalake, mmmmmwaaaah” Alichombeza Clifford huku akiachia busu hewani. “Na yule mzee wala sihangaiki kumtaarifu. We nipe namba za huyo jamaa aje anisaidie, mengine tutajua mbele kwa mbele”
“Au kama usumbufu umezidi hamia kwangu basi mpaka atakapotengeneza” Zulfa alisema huku lile jicho lake kubwa lililolegea bila utaratibu akilitumia ipasavyo. Alivaa sura ya utani lakini kwa mwanaume mwerevu kama Clifford alitambua upesi kuwa sehemu fulani ya akili ya mwanamke yule ilimaanisha kile alichokisema.
“Ah.. Wanawake wazuri kama ninyi tena wenye elimu ya kutosha huwa mna wakubwa wanawaweka mjini. Usinitafutie kesi ya mauaji bure mwana wa Chiziza mie.. Hivi una kipindi baadae? Nadhani nitahitaji projector yako, ya kwangu wanaitumia kule procurement” Clifford alibadili mada upesi na aliona waziwazi namna Zulfa alivyokerwa na kitendo kile lakini hakujali.
Hili lilipoisha, wote wakazama katika kujiandaa kwa vipindi vya mchana ule. Mara kwa mara Clifford alikuwa akinua mkono na kutazama saa yake ili kujua muda, na ilipotimu saa nane mchana, akainuka na kompyuya mpakato na kibegi kingine kilichokuwa na projector ya Madam Zulfa na safari ya darasani ikaanza.
Kufundisha masomo ya ukaguzi wa hesabu za fedha na masomo mengine ya uhasibu ilikuwa ni kazi aliyoipenda na aliyoifanya kwa moyo sana huku wanafunzi wake wengi wakimsifia kwa kile kipaji chake kikubwa cha kuweza kufundisha masomo magumu lakini kwa namna iliyowasaidia wengi kumwelewa vema. Pia alikuwa na ukaribu mkubwa na wanafunzi wake, na hakusita kuwasaidia popote walipohitaji msaada wake. Hakika alikuwa kipenzi cha wengi.
Hakuwahi kujua kuwa ufanisi wake katika kazi yake hiyo ungekuja kumgeuka na kumuingiza katika adhabu…
Hakujua kuwa ufanisi huo ungemtunuku zawadi kubwa…
_Zawadi ya adhabu…._