TULIPOISHIA.
Jambo alilowaza ni ikiwa hatima ya msomi iko kichwani mwake basi siyo yeye atakayetakiwa kumaliza bali kutakuwa na mtu mwingine atakayeifanya hiyo kazi. "Mtu huyo ni nani na kwa nini siyo mimi" Ndilo swali alikuwa akijiuliza asipate majibu, aliamini yeye ndiye alistahili kufanya hilo wala siyo mtu mwingine.
ENDELEA,,
"Kwamba uwezo wangu hauaminiki" aliendelea kuwaza akionekana kuchukizwa sana na kitu kile mpaka akatamani kumpigia aliyemtumia ujumbe lakini alijionya kufanya vile maana ingekuwa kukiuka miiko ya kazi yake.
"Shiiiiiiiiiiiiiiiiiittt!!!!" alimaka kwa hasira akaachia ngumi nzito iliyoipasuapasua meza ya kioo iliyokuwa mbele yake. Hasira zilimpanda sana baada ya kumkumbuka Kipensi akiamini yeye ndiye atakuwa amepewa jukumu la kummaliza msomi. "Una bahati sana kichaa, wanakubeba sana na wanakudekeza mno. Ipo siku yako." Roho ilimuuma sana baada ya kupata wazo hilo, aliwaza namna Kipensi alivyokuwa akibebwa na kupendelewa na wakubwa licha ya uwezo mdogo alionao. Hakuuona mpango ule kuwa sawa kabisa yaani kazi ya heshima namna ile apewe mpuuzi tu ili aonekane kafanya kazi kubwa hali ya kuwa yeye ndiye huwa anahangaika mala zote kusuka mipango na kuhakikisha kila kitu kinafanyika kama kilivyopangwa. "Haina noma, kikubwa muamala wangu uendelee kusoma" Alihitimisha hivo kisha akaingia chumbani alale maana kesho yake alikuwa na ratiba ngumu.
Mithili ya gari la wagonjwa linalomuwahisha mgonjwa mahututi hosipitali, ndivyo lilivyokuwa likikimbia gari hili kwa mwendokasi sana, bahati nzuri ni kwamba tayali ulikuwa usiku mrefu sana hivyo hakukuwa na magari mengi balabalani. Dereva alikuwa makini sana kuuzungusha usukani akipanga na kupangua gia kadili mwenyewe alivyoona inafaa. Mwendo kasi ule haukuja kwa bahati mbaya tu au kujifurahisha kwa dereva bali kuna sababu maalumu ilipelekea hilo kutokea ndiyo maana hakusita kupunguza mwendo baada ya kulifikia gari jingine la aina ile lililokuwa likitembea kwa mwendo wa kawaida. Alipiga honi mala nne mfululizo kisha akaurejea mwendo wake wa awali ambapo alilikimbia kwa kasi sana akalipita lile la mwanzo ambalo nalo liliongeza kasi na kuanza kumfukuzia. Balabala ilikuwa tupu, hakukuwa na magari mengi usiku ule hivyo gari zile zilikimbia kwa kujidai, zikifukuzana kwa kasi sana. Safari ile ilikuja kuishia mbele ya nyumba moja iliyopo nje ya mji eneo lililojitenga kwa kiasi fulani na makazi ya watu. Toka ndani ya gari la kwanza alishuka mwanaume mmoja akaenda kufungua mlango wa nyuma wa gari lake akatoa furushi kubwa liloonekana kuwa zito. Ndani ya gari la pili walishuka wanaume wawili pamoja na msichana mmoja aliyeonekana kutojiweza kabisa, walimnyanyua na kuingia naye ndani ya nyumba. Walitumia dakika mbili tu kukaa ndani ya nyumba ile kisha wakatoka mala hii wakiwa wanaume tu bila yule mwanamke, wakaingia ndani ya magari yao wakayawasha na kuyaondoka kwa mwendo wa kasi sana.
Nyumbani kwa tajiri Isaya mambo yalikuwa shwari kabisa asubuhi ile. Nje ya nyumba wanaonekana walinzi waliovalia suti safi nyeusi zilizoichora vema miili yao iliyojaa kwa mazoezi, kila mmoja alikuwa makini kuhakikisha usalama hasa usalama wa watu waliokuwa ndani ya jumba lile. Sebuleni walionekana wanawake watatu waliovalia sare, walikuwa wafanyakazi wa ndani, wawili walikuwa wasichana na mmoja alionekana mwanamke wa umri wa makamo. Ndani ya moja ya vyumba vya jengo lile alionekana tajiri mwenyewe Mr Isaya aliyekaa kitandani peke yake akiwa kajiinamia na kushika tama kama mtu asiyekuwa na tumaini lolote ndani ya siku hii mpya. Mda huo mlango wa chumba ulifunguliwa akaingia yule mwanamke aliyekuwa sebuleni mkononi akiwa kashikilia sahani kubwa lililokuwa na baadhi ya vinywaji ndani yake.
"Umeamkaje"
"Niko salama sijui wewe unaendeleaje"
"Namshukuru Mungu angalau afya yangu inazidi kuimalika sasa ndiyo maana nikaona nije mwenyewe leo nimpumzishe binti yako."
"Ni habari njema kama unaendelea vizuri, na vipi halakati zetu zinaendaje kwa sasa! maana nimekuwa bize sana kiasi cha kushindwa kufatilia chochote."
"Bado kila kitu kipo sawa japo uwepo wako unahitajika sana, kwa sasa hali ya masoko siyo nzuri kabisa, ukijumlisha na hiki kinachozungumzwa sahivi soko limeshuka sana kaka yangu, bidhaa haziendi. Inatakiwa kufanyike jambo haraka kuweka mambo sawa maana tukisema tusubilie zaidi ndivyo tutakuwa tunajichimbia shimo la kujizika wenyewe."
"Sawa Esinati, kwahiyo wewe unawaza kipi kifanyike."
"Itatakiwa tuuze baadhi ya hisa tulizonazo kwenye makampuni ya nje ili angalau tuwe na pesa ya kutosha kuendeleza mapambano ya ndani maana bila kufanya hivo itakuwa ngumu kuwashawishi wabia wetu kuendelea kutuamini, lakini pia hatujui nini mahakama itaamua kwahiyo ni vizuri kuweka tahadhari ili hata likitokea lolote tujue namna ya kulikabiri."
Isaya alinyanyuka na kumkumbatia mwanamke yule tunayemfahamu sasa kwa jina la Esinati, "Najivunia sana kuwa na ndugu kama wewe umekuwa msaada mkubwa sana kwangu, licha ya aina ya maisha unayoishi lakini mala zote umekuwa msaada kwangu. Naahidi kukulinda mpaka dakika ya mwisho ya uhai wangu, si kwa sababu ya ahadi niliyomuahidi baba yetu kipindi kile bali ni kwasababu ya upendo wangu kwako. Nakupenda sana Esinati mdogo wangu, naomba unisamehe sasa kwa nyakati nilizowahi kukuudhi na kukuumiza." Tajiri aliongea kwa sauti ya uchungu akiwa kamkumbatia mdogo wake kwa nguvu sana, machozi yalikuwa yakimlengalenga machoni ishara ya hisia nzito alizokuwa nazo, Esinati hakujibu chochote, alikiwa mkimya akinaribu kumbembeleza kaka yake.
"Mda sio rafiki, unapaswa kuondoka mapema, kafanye kile ulichonieleza na mengine utaamua mwenyewe kwa wakati ambao sitakuwepo, nakuamini sana Esinati, wewe ni mwanamke jasiri sana. Nenda uendelee kuishi kama mwanzo, usije ukabadili mfumo wa maisha hata kama nitahukumiwa kunyongwa maana siku utakapobadilika itakuwa ndiyo mwanzo wa mwisho wako. Nenda usichelewe uwasalimie wanangu, wambie nawapenda sana" Isaya aliongea maneno hayo kisha akamfukuza mwanamke yule ambaye aliondoka akitokwa na machozi. Maneno aliyoambiwa na kaka yake yalikuwa mazito sana alitamani aendelee kuwepo eneo lile ili ahoji vizuri maana yake, lakini asingethubutu kufanya vile. Aliijua hatari ya kuendelea kuwepo eneo lile hivyo alijikaza akafuta machozi kujiweka sawa kisha akaondoka.
Tajiri Isaya alibaki akimwangalia mwanamke yule wakati akiondoka, alikuwa akikukumbuka matukio mengi ya siku za nyuma namna walivyokuwa wakiishi kwa amani wakiwa watoto wawili pekee wa familia ya mzee Akilimali. Maisha yao yalikuwa mazuri mpaka siku shetani la mabalaa lilipokosea njia na kuingia nyumbani kwao. Ni siku ambayo hataisahau, siku iliyoacha kumbukumbu mbaya zisizofutika akilini mwake. Ilikuwa ni siku ya jumapili siku ambayo kwa kawaida familia yao huamka asubuhi na mapema kujiandaa kwa ajili kwenda kanisani maana mama yao alipendelea kuhudhuria misa ya kwanza. Baba yao hakuwa mpenzi sana wa kuhudhuria kanisani, yeye angeenda mala chache sana hasa zile siku za matukio yanayomhusu kama vile siku ya ubatizo wa watoto wake. Asubuhi ile Isaya alidamka mapema sana si kwa sababu alipenda iwe hivo bali ni baada ya kuota ndoto mbaya iliyomshitua na hakufanikiwa tena kupata usingizi. Mda huo alitulia kitandani akawaza namna mama yake atakavyokuaja kumuamsha mala tu itakapofika saa kumi na moja kamili arufajiri. Siku hiyo alipanga kutokwenda kanisani ili aambatane na baba yake kwenda mgodini alikokuwa akifanyia kazi. Aliyakumbuka vema maneno aliyoambiwa na baba yake usiku wa jana yake alipomweleza mpango wake. "Wewe ni mwanaume, unatakiwa kujisimamia na kujitegemea mwenyewe, kama hujisikii kwenda kanisani kesho basi unatakiwa umweleze mama yako kama ulivyonieleza mimi, wala hatokuzuia" Ndivyo alivyojibiwa na baba yake wakati alipojaribu kumshawishi amuombee ruhusa kwa mama yake ili kesho asiende kanisani. Isaya alikuwa amemzoea na kumheshimu sana mama yake kiasi kwamba asingeweza kumbishia kwa chochote, tofauti na baba yake ambaye angeongea naye kawaida au hata kubishana naye maana mzee mwenyewe ndiye alimlea vile. Ilipofika saa kumi na moja kamili, aliweza kuusikia mlango wa chumba chake ukifunguliwa hapo akajua ni mama yake anaingia kumuamsha, aliigiza kupitiwa na usingizi akiwaza namna gani atamshawishi mama yake abaki nyumbani. Aliendelea kutulia akijiandaa kwa kupangilia vema maneno atakayomwambia mama yake mala tu atakapomgusa. Aliisikia vizuri sauti hafifu ya hatua za mtu akisogea kuja pale alipo, alitulia mpaka pale alipohisi kuguswa, "mama, mimi leo sijisikii kwenda kanisani" aliongea kwa kukulupuka huku akiling'ang'ania blanketi alilojifunika hata hivyo hakusikia sauti ya mama yake akijibu kile alichomwambia. Milio wa simu yake ndiyo ulimshitua toka kwenye dimbwi la mawazo yaliyokuwa yameuhamisha ulimwengu wake mda mfupi uliopita.
Haukuwa mwito wa simu bali sauti ya malamoja kuashiria kuingia kwa ujumbe. Iliichukua simu yake na kuufungua ujumbe ule akausoma,,
"Unaendeleaje Isaya wangu, leo nitahitaji tukutane tena kama tulivyokuwa tukikutana siku za nyuma, eneo lile lile saa na sekunde ileile. Nimekukumbuka sana mpendwa wangu, jitahidi ufike unifurahishe nami nitakufurahisha kwa kukuletea wanao, naamini umewakumbuka sana."
Ujumbe huo ulimshtua sana, mapigo yake ya moyo yaligonga kwa kasi kiasi cha kuufanya mwili mzima kuanza kutetemeka. Licha ya namba iliyotumika kuwa ngeni kwake lakini ujumbe ulioandikwa haukuwa mpya kabisa. Ni aina ya jumbe ambazo yeye mwenyewe hupendelea kuziandika. Yaani ujumbe uliokamilika na kujitosheleza unaeleweka kwa msomaji. Tajiri Isaya hakuwa mpenzi wa kuwasiliana kupitia njia ya ujumbe wa maandishi kwani aliona inampotezea mda mwingi kusoma na kujibu hivyo hata mala chache inapomlazimu kutuma ujumbe wa maandishi basi angetuma ujumbe uliokamilika ili mlemgwa atakapousoma aweze kuuelewa vizuri. Tabia hiyo amekuwanayo tokea ujanani na alishawaambukiza marafiki zake wengi hasa wale aliokuwa karibu nao. Aliishikilia vema simu yake kwa mikono miwili akisoma kwa kurudiarudia ujumbe aliotumiwa. Ni kama hakuamini kile alichokuwa akikisoma kama ndicho kilichoandikwa au ni macho yanamdanganya, lakini ulikuwa ndiyo uhalisia. Alipatwa na hisia mchanganyiko kwa wakati mmoja, sura yake haikueleweka kama anahuzunika ama anafurahi. Kila akisoma sentensi inayozungumzia watoto angejihisi furaha iliyochanganyika na shauku ya kutaka kuwaona wanae ama kweli aliyemtumia ujumbe huo alikuwa akimjua vilivyo na alijua kama amewakumbuka sana watoto wake na ana shauku kubwa ya kutaka kuwaona. Ujumbe ulikuwa mzuri wa kutosha kuifurahisha roho yake lakini kila anapomkumbuka mtumaji wa ujumbe moyo ulidunda kwa kasi mno, alipatwa na hofu sana. Alimkumbuka vizuri mtu aliyemtenga yeye na wanae. Licha ya utajiri mkubwa na umaalufu alionao, tajiri Isaya hajawahi kuishi kwa amani, hajawahi kuwa na raha au furaha ya kudumu katika maisha yake ya kifahari. Sio yeye tu bali hata ndugu zake wote waliojulikana walipitia wakati mgumu kama ilivyo kwake. Nyuma ya yote hayo alikuwepo mtu. Mtu aliyepotayari kufanya chochote kwa gharama yoyote kuhakikisha hayo yanatokea. Mtu Huyo ndiye muhusika na muumbaji halisi wa magumu yote anayopitia. Mtu huyo ndiye aliyemtumia ujumbe asubuhi ya leo.
Tajiri Isaya alikosa amani kabisa, licha ya kuwa na shauku ya kuwaona wanae lakini alikuwa na hofu sana, alihofia maisha yake maana alijua hatokuwa salama tena baada ya kukutana na mtu huyo. Aliuona mwisho wa simulizi yake tokea dakika ile atakapomtia machoni mtesi wake.
"Sijui nini kitanipata, lakini lazima niende kwa ajili ya wanangu, nitaenda niwaone hata kama hii ndiyo itakuwa mala ya mwisho. Liwalo na liwe." Alihitisha kwa kutoa kauli ya kiume kujitia moyo. Aliamua kwenda mahali alipoitwa. Aliukubali wito wa adui yake kwa ajili ya wanae. Alikuwa na shauku kubwa, shauku ya kuwaona wanae aliotenganishwa nao kwa miaka mingi. Shauku na hamu vilimzidia mpaka ile hofu aliyokuwanayo ikatoweka, mwili haukumtetemeka tena, mapigo ya moyo yakarudi kudundia kwenye mhimili wake, usoni alichanua tabasamu, tabasamu la ujasiri mkubwa sana. "Nitaenda. Ndiyo. Lazima niende." ,,,,,,,,,
ITAENDELEA.
😇😇😇
Tajiri Isaya ameamua kwenda alikoitwa, je nini itakuwa hatima yake?
Anaenda wapi?
Ana uhusiano gani na mtu aliyemuita?
Je, watoto wake wapo kweli na ni kina nani?
Kujua yote haya, usikose kufuatilia sehemu ijayo.
"KABURI LA MSOMI"
JJ former.
Tukutane Jumanne mda na wasaa kama huu. ✍️✍️✍️