KABURI LA MSOMI.
Karibuni sana wapenzi wa simulizi, leo naitambulisha kwenu simulizi hii iitwayo KABURI LA MSOMI. Ndani ya simulizi hii utakutana na visa, mikasa na matukio ya maisha kwa ujumla, vimbwenga, mapenzi wivu, usaliti, chuki na mauaji. Mwandishi anakukaribisheni kutoa maoni ushauri na mapendekezo usomapo simulizi hii.
Jina la simulizi: KABURI LA MSOMI.
Na Mtunzi wako.
COOOOOOOOUUUUUUUUTTTT!!!
Ilikuwa ni sauti ya juu iliyosikika vema ndani ya chumba cha mahakama kuashilia kuwa shauri lililokuwa likiendeea mahakamani limefungwa kwa siku ile, hivyo wote waliokuwemo mle ndani walinyanyuka vitini na kusimama wima ikiwa ni ishara ya kutoa heshima kwa mamlaka ya Mahakama na mheshimiwa Hakimu alisimama na kutoka mle ndani akifuatiwa na wasaidizi wake.
Kilipita Kimya kidogo kabla ya sauti na minong'ono kuanza kusikika tena. Hazikuwa sauti za kueleweka kwani kila mmoja alikuwa akiongea la kwake, huyu akiongea kwa kukenua na kucheka, huyu akiongea kwa hasira na kuchukia, hawa walikumbatiana na kupongezana hawa walinuniana na kusonyana yaani kulikuwa na hisia mchanganyiko ndani ya ukumbi wa Mahakama ile. Hata hivyo kwakuwa tayari waheshimiwa walikwishaondoka, hata wale wasikilizaji wengine walianza kuondoka, mmoja mmoja kwa walionuna pasipo kuongeleshana, huku kwa wenye furaha wakishikana mikoni na kuongozana kwa madaha na mbwembwe mithili ya maharusi watokapo kanisani kufunga pingu za maisha.
Nje ya Mahakama wanaonekana mamia ya watu, waliojikusanya mafungu mafungu, hawa wameketi na wengine wamesimama ilimradi kila mmojawao alikuwa yupo uelekeo wa Mahakama ile. Katikati ya mamia wale wanaonekana wachache waliokuwa ndani ya sale safi huku wakiwa makini kufatila kila kilichokuwa kikifanywa na umati ule. Bila shaka, hawa walikuwa Askari Polisi waliokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kawaida kuhakikisha usalama wa raia wale. Haikueleweka ni nini hasa kimewakusanya raia wengi kiasi kile nje ya Mahakama ile maana haukuwa utaratibu wala mazoea ya raia wa mji ule kujazana nje ya mahakama eti kwa sababu wanafuatilia kesi.
Hali kama ile ingetokea katika baadhi ya kesi za watu maarufu, hasa wale wanasiasa vipenzi vya wananchi, ndipo ungeweza kushuhudia umati wa watu wengi namna ile, nje na ndani ya viwanja vya Mahakama, lakini leo hii hali ilikuwa tofauti kabisa maana ijapokuwa haikuwa kesi ya kisiasa, umati ulikuwa mkubwa nje ya Mahakama ile ndogo ya wilaya.
Ukubwa na ongezeko la mkusanyiko wa watu ndio uliwafanya askari polisi waliokuwa zamu siku ile kutoa taarifa kwa wakubwa wakiielezea hali hiyo iliyoonekana kutokuwa ya kawaida na kuomba ongezeko la askari wengine ili hata ikitokea sintofahamu yoyote iwe rahisi kuikabili. Haukupita mda mrefu, zilionekana gari mbili zenye nembo ya jeshi la polisi Ubavuni zikiingia kwa kasi sana ndani ya eneo la Mahakama. Kabla hazijasimama kisawasawa, baadhi ya askari waliruka kutoka ndani ya magari yale na kudunda chini kwa ukakamavu wa hali ya juu. Jambo hilo lililopelekea umati kupiga mayowe na kelele za kushangilia. "Jambo Afande" "Jambo" "Jambo Afande" Walipeana salamu na bila kupoteza wakati walipangiana majukumu ya kutekeleza mahali pale.
Kusemakweli hali ya hewa ilikuwa nzuri sana siku hiyo maana licha ya uwepo wa mawingu kiasi lakini bado mvua haikunyesha, hivyo umati ule uliendelea kusubiri pale nje kwa utulivu mkubwa sasa tofauti na mwanzoni ambapo walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali za hamasa. Labda ungesema wamechoka, lakini hapana, maana bado walionekana kuwa na shauku ya kuona madai yao yakitekelezwa, ogezeko la maaskari polisi ndiyo kilikuwa chanzo cha utulivu ule, ni wakati ambapo Mahakama ilikuwa ikiendelea kulitafutia utatuzi lile lililokuwa limevuta hisia za watu wengi kiasi kile.
Hali ilibadirika baada ya wale waliokuwa ndani kujitokeza nje, hapo ilianza minong'ono ya sauti za chinichini kabla ya mwanaume mmoja kuanza kuimbisha wimbo kwa sauti ya juu,
Haki itendeeke, ee
Haki itendeeke, eee
Hatutokaa kimya!!!!
Mpaka mnyonge apewe haki yake!!!!!
Aliimba kwa nguvu na kwa sauti ya juu kabla ya wenzake kudakia ikawa sasa ni kuimba kwa kupokezana na umati wote ulikuwa ukitamka na kuimba maneno yale kwa sauti moja ungezani ni wanakwaya waliopitia mafunzo ya uimbaji. Hali ilibadirika zaidi pale alipojitokeza mwanaume mmoja toka ndani ya Mahakama, alikuwa mwanaume mfupi mfupi aliyevalia tracksuit ya bluu, miwani machoni, raba nyeupe miguuni nywele nyeusi zilizoonekana kutunzwa sana, na mkononi alishikilia kibegi kidogo cha mkononi huku akitafuna kitu mdomoni. Ukimwangalia kwa haraka ungemwona kuwa na uso uliosawajika, hakuwa na furaha japo alijitahidi kuficha hilo.
Watu Walichafukwa zaidi baada ya kumuona mwanaume huyu, nyimbo ziliimbwa zaidi na kwa sauti ya juu, wengine walitoa kauli chafu kumtukana mwanaume yule ambaye hakuonekana kujali sana kuhusu kilichokuwa kikiendea pale nje ya mahakama kwani kile kilichotokea ndani ya Mahakama kilikuwa kimechanganya na kumuumiza zaidi.
Alikuwa Akitatembea kwa hatua za taratibu mithili ya aliyeogopa kujikwaa, hakuwa sawa kabisa mawazo mengi yalikuwa yakipita kichwani mwake hasa kila alipokuwa akijaribu kutafakari yaliyokuwa yanampata sasa. Mwanzoni hakujisumbua na Kelele za watu wale mpaka pale alipopigwa kichwani na chupa ndogo iliyorushwa na kijana mmojawapo wa makutano waliuwepo mahali pale.
Hapo alishtuka akijishaangaa kwa kuwa mjinga kiasi cha kushindwa kuwa makini na hatua zake,hata hivyo aliamua kuwa mpole maana katikati ya umati ule asingeweza kufanya chochote, aliinama na kuiokota ile chupa akataizama kwa kitambo kidogo huku akiiminya kwa hasira kisha akaitia ndani ya kibegi alichokishikilia mkononi.
Wengi walibaki kumshangaa maana hata polisi waliokuwa wakijaribu kumrinda asifikiwe na baadhi ya raia wenye hasira kali walishindwa kuelewa nini hasa kilikuwa kikimpa jeuri namna ile kiasi cha kusimama akionekana kutokuwa na haraka ya kutoweka katikati ya raia walioonyesha chuki za waziwazi juu yake.
Ni kama alizubaa zaidi maana alisimama jambo ambalo lilikuwa ni hatari sana kwake, na kadili alivyozidi kupoteza mda mahali pale ndivyo umati ulivyokuwa ukimkaribia, kama siyo uimala wa askari basi huenda angeishia katika mikono ya raia wale ambao bila shaka wangemuumiza kwa kumjeruhi vibaya au hata kuumuua kabisa maana walimtamani kweli.
Mmoja wa wasaidizi wake alimfata na kumshika mkono alimshinikiza kwa kumvuta na kumlazimisha kuiingia ndani ya gari ambalo liliwashwa haraka na kutoweka kwa kasi mahali pale kiasi cha kuwatimulia vumbi raia wale ambao walikitafsiri kitendo kile kuwa kosa la makusudi alilolifanya mwanaume yule na baadhi yao walijiapiza kutomsamehe kamwe.
Matukio yote hayo yalikuwa yakifatiliwa kwa ukaribu zaidi na jopo la wanaume wanne waliokuwa wameketi kuzunguka meza moja yanye screen iliyokuwa ikionyesha yote yaliyokuwa yakiendelea nje ya Mahakama. "Kazi nzuri sana imefanyika, naamini huu ni mwendelezo mzuri, na kwa kasi hii naona tutafanikiwa hata kabla ya wakati kufika" Aliongea mmoja miongoni kwa watu wale aliyeonekana kuwa kiongozi wao na baada tu ya kauli ile wote walisimama na kutoweka mahali pale pasipo kufanyika maongezi zaidi.
Juu ya jengo moja refu kidogo lililokuwa mkabara na Mahakama ile wanaonekana vijana wawili waliokuwa wakikusanya na kupakia baadhi ya vifaa vyao ndani ya begi kubwa walilokuwa nalo "mpaka hapa kazi yako nimeikamilisha, nafikiri sasa ni mda wa malipo, nikatie asilimia zangu nitembee" Aliongea mmoja ambaye mda huo alikuwa kainama akikusanya baadhi ya vifaa vyake.
Hata hivyo hakupokea majibu toka upande wa pili, aliamua kunyanyuka na kumtazama mwenzake aliyekuwa kimya mda wote akionekana kutafakhari kitu. "sawa bwanamdogo, haina shaka malipo yako utapata kama tulivyokubaliana" Alijibu mwanaume yule kuutoa wasiwasi wa mwenzake. "sasa hela yangu naipataje bosi, maana mda tuliokubaliana ndiyo huu, baada tu ya kumaliza kazi, sasa naona unanitazama tu hufanyi utaratibu wowote mimi nikapata hela yangu" Aliongea tena yule kijana ambaye sasa ameshasimama, kashikilia begi lake mkononi.
"Punguza wasiwasi dogo, hela ipo, okota kwanza hiyo frashi hapo chini tushuke mtaani nikakutolee pesa yako benki". "Haina noma mkubwa, kikubwa mimi nipate changu maana kazi yenyewe ni ngumu sana, kurekodi hii video kwenye eneo kama hili bila kibari maalumu ni jambo hatari sana kaka, ukibainika adhabu yake siyo ya kitoto, na ukizingatia sina mtu serikalini wa kunitete,,,,,, "
Kauli yake ilikatishawa na shambulio la ghafla alilofanyiwa, alijikuta kabanwa shingo na mikono yenye nguvu na kwakua hakuwa amejiandaa kwa tukio hilo aliishia kufurukuta akipambana kujinasua toka kwenye kabari ile. Alifurukuta bila mafanikio kwani adui yake alikuwa mwenyenguvu zaidi, kadili mda ulivyozidi kwenda pumzi zilianza kumwishia, miguu ilikosa nguvu na alijikuta mwenyewe bila kupenda akianguka chini. Kitendo hicho hakikumfanya adui yake kumuachia hivyo alianguka naye akiwa bado kalishikilia kwa nguvu shingo lake.
Ni mpaka pale alipojilidhisha kuwa uhai umeshauacha mwili wa windo lake ndipo aliuachia mwili wa kijana yule, mwanaume muuaji alisimama huku akihema sana kutokana na pulukushani aliyoipata wakati wa kutekeleza mauaji yale, inaonekana hakuwa binadamu wa kawaida, kuua kwake lilikuwa suala dogo ambalo angalifanya mda wowote kwa ustadi wa hali ya juu sana. Aliiwasha simu yake na kuipiga mahali, "Bosi, namba mbili imekamilika sasa" Aliongea maneno hayo mala baada ya simu kupokelewa na mtu wa upande wa pili ambaye hakutoa jibu lolote zaidi ya kuikata simu ile. Baada ya simu kukatwa mwanaume muuaji alilichukua lile begi, aliangaza huku na kule akikikaagua chumba kile kwa awamu ya mwisho kabla ya kufungua mlango na kutokomea nje.
Nje ya Mahakama umati ulikuwa ukizidi kupungua, watu walikuwa wakitoka makundi makundi, baadhi yao waliendelea kuimba nyimbo za kuhanikiza kufanyika kwa yale wayatakayo huku wengine wakipiga kimya ungedhani sio wao waliokuwa wakizomea mda mchache uliopita.
Kulikuwa na misafara mikubwa miwili ya watu, wapo walioelekea upande wa kusini wengine wakishikana kuelekea kaskazini, hata hivyo bado askari polisi waliokuwepo mahali pale wakiendelea kuwadhibiti watu wale kuepusha mtafaruko zaidi. Mda huo simu ilipigwa ikaitikiwa, "Halloo bosi" "Vipi mbona mpaka sasa sijapata mrejesho wowote" Iliuliza sauti ya upande wa pili wa simu, naye mpokeaji akajibu "Bosi, namba moja tayali ilishakamilika dakika tano zilizopita, lakini nilish,,,,, "
Simu ile ilikatwa na aliyekuwa upande wa pili pasipo kumpatia nafasi muongeaji kumalizia kauli yake. "Huyu naye fala kweli, sasa mbona amekata, anashindwa kusubiri nikamwelezea kuwa nilichelewa kumtaarifu kwa sababu sikupata muda wa kufanya hivyo, sasa raia wengi kiasi kile anafikiri ingekuwaje, mda mwingi nilikuwa makini kuwawangalia zaidi ya kufanya jambo lingine. Hata hivyo atajijua mwenyewe kikubwa kazi nimeifanya kama ilivyotakiwa" Alibaki akijiongelesha mwenyewe, akionekana kutofurahishwa na kitendo cha kukatiwa simu na mtu aliyekuwa upande wa pili.
Ni ndani ya nyumba moja ndogo ambayo licha ya kunakshiwa kwa rangi nzuri ya bluu lakini bado inaonekana kuwa ya zamani sana kutokana na muundo wake, aina ya ujenzi na muonekano wake, ilikuwa ni nyumba iliyoezekwa kwa vigae vilivyokwishakuwa vikuukuu sana kiasi cha kuruhusu nyasi kuota juu yake. Kwenye moja ya vyumba vya nyumba hii anaonekana msichana mmoja, amejilaza kwenye sofa kubwa lilokuwa mle ndani, mkononi ameshika grasi ya wine nyekundu akiendelea kukigigida kinywaji hicho taratibu kabisa bila hofu yoyote, mala nyingi jicho lake akiligeuza kwa madaha na mbwembwe kuiangalia simu ndogo iliyokuwa mbele yake juu ya meza ndogo ya kioo.
Kwa kumwangalia tu alikuwa ni aina ya wanawake ambao shida haikuwa sehemu ya maisha yao, mwanamke mrefu kidogo, mweupe, aliyesuka nywele za bei mbaya akiwa ndani ya kijinguo cha kulalia kiliyoiacha wazi sehemu kubwa ya makalio yake.
Kutokana na aina ya uvaaji wake ni wazi kabisa siku hiyo hakuwa na mpango wa kutoka nje ya nyumba ile, pengine labda kulikuwa na kazi maalumu alikuwa akiifanya mahali pale maana hakufanania kuwa mwenyeji wa nyumba ile. Ghafla ile simu ndogo juu ya meza ilitoa mwanga mkali na kuanza kuunguruma kwa nguvu "nshwssss, mda wote ulikuwa wapi, mbona hukupiga!"
Alisonya msichana yule na kutoa maneno hayo huku akijinyanyua kivivu na kukaa. Aliichukua simu ile na kubonyeza kitufe cha kupokea, hakuongea mpaka pale iliposikika sauti ya upande wa pili " Sikiliza Emmy tupo hatua nzuri sasa, mpango namba moja na namba mbili tayali imekamilika, vijana wanajiandaa kukamilisha namba tatu na ndiyo itakuwa kazi ya mwisho kufanyikia mjini kwa siku ya leo, namba nne na namba tano ni juu yako, jitahidi mala kila kitu kitakapokuwa sawa ulikamilishe hili, kumbuka tunakutegemea sana katika hili" Baada ya maelezo hayo, mtu aliyekuwa upande wa pili alikata simu pasipo kungojea jibu lolote.
Baada ya simu ile kukatwa, yule msichana ambaye sasa tunamfahamu kwa jina la Emmy alitoa pumzi ndefu kisha alinyanyuka na kujishikilia kiuononi mithiri ya mchezaji wa mpira wa miguu aliyechoka. Aliinyanyua grasi ile ya wine na kukitazama kinywaji hicho kilichokuwa kikiumwagilia moyo wake kwa wakati huo, alikigigida kinywaji chote mdomoni kwa mkupuo kisha akaiweka grasi mezani na kutoweka mle chumbani.
Pembeni kidogo ya jengo la Mahakama kulikuwepo na kituo cha mafuta ambacho wenyeji wengi wa mji ule hupendelea kukiita "sheli" Ndani ya sheli ile shughuli zilikuwa zikiendelea kama kawaida, siku hiyo biashara ilikuwa nzuri sana kutokana na uwepo wa watu wengi maeneo yale, hivyo biashara hasa ya vinywaji na vitafunwa vilivyokuwa vikipatikana kwenye supermarket ndogo ya sheli hiyo viliuzika sana. Tokea upande wa kuingilia linaonekana gari dogo aina ya "Spacio" likiingia ndani ya sheli ile, na kwenda kupaki uelekeo wa supermarket ile, akashuka kijana mmoja aliyeonekana kuwa na umri kati ya miaka 24 au 25 hivi. Kijana huyu anaonekana kuwa mwenyeji wa maeneo yale, alimchangamkia na kuongea na binti muhudumu wa duka lile kisha akatoweka mahali pale.
Hakwenda mbali na sheli ile bali alizunguka na kuchoma ndani ya jengo moja la ghorofa lililokuwa kwa nyuma, alizipandisha ngazi harakaharaka kuelekea ghorofa ya juu. Alipofika juu ni kamavile alichanganywa na mandhari ya mle ndani "du! Licha ya uenyeji wangu maeneo haya lakini sijawahi kuufaidi utamu wa huu mjengo" Aliwaza wakati ambao alikuwa akijihangaisha kusoma namba zilizoandikwa kwenye milango iliyozunguka korido ile.
Japokuwa hakuwa mgeni wa jengo lile lakini yaelekea alichanganywa na mpangilio wa vyumba, bado hakuwa amekipata kile alichokuwa akikitafuta. Alichukua simu yake ya kupangusa aina ya Tecno Common 20, aliigusa mala mbili haraka haraka ikawaka, akaingiza nywila na kwenda moja kwa moja sehemu yenye kumbukumbu ya jumbe alizokuwa akituma na kutumiwa, hapo alitafuta kidogo mpaka pale alipolipata jina la Morisi wa pili, akaligusa na kuanza kuangalia jumbe walizokuwa wakitumiana yeye na mtu huyo.
Aliweka utuo kwenye ujumbe mmoja ambao sasa aliusoma na kuuelewa "KIWILA HOTEL, room no 23, upper floor, around 8:30am" Baada ya hapo aliirudisha simu yake mfukoni na kuelekea upande wa kulia kwake, alitembea kidogo kuuelekea mlango mmoja, alipoufikia aliunyanyua uso wake na sasa aliweza kuyaona vema maandishi yaliyoandikwa juu ya mlango huo "No 23" ilikuwa imeandikwa kwa namna ya kuchonga na rangi ya manjano ya kukoleza. Mpaka hapo alijua yupo mahali sahihi kabisa, hivyo pasipo kupoteza mda alianza kubisha hodi kwa kugonga mlango taratibu "ngo ngo ngo",,,,
Karibuni sana wapenzi wa simulizi, leo naitambulisha kwenu simulizi hii iitwayo KABURI LA MSOMI. Ndani ya simulizi hii utakutana na visa, mikasa na matukio ya maisha kwa ujumla, vimbwenga, mapenzi wivu, usaliti, chuki na mauaji. Mwandishi anakukaribisheni kutoa maoni ushauri na mapendekezo usomapo simulizi hii.
Jina la simulizi: KABURI LA MSOMI.
Na Mtunzi wako.
COOOOOOOOUUUUUUUUTTTT!!!
Ilikuwa ni sauti ya juu iliyosikika vema ndani ya chumba cha mahakama kuashilia kuwa shauri lililokuwa likiendeea mahakamani limefungwa kwa siku ile, hivyo wote waliokuwemo mle ndani walinyanyuka vitini na kusimama wima ikiwa ni ishara ya kutoa heshima kwa mamlaka ya Mahakama na mheshimiwa Hakimu alisimama na kutoka mle ndani akifuatiwa na wasaidizi wake.
Kilipita Kimya kidogo kabla ya sauti na minong'ono kuanza kusikika tena. Hazikuwa sauti za kueleweka kwani kila mmoja alikuwa akiongea la kwake, huyu akiongea kwa kukenua na kucheka, huyu akiongea kwa hasira na kuchukia, hawa walikumbatiana na kupongezana hawa walinuniana na kusonyana yaani kulikuwa na hisia mchanganyiko ndani ya ukumbi wa Mahakama ile. Hata hivyo kwakuwa tayari waheshimiwa walikwishaondoka, hata wale wasikilizaji wengine walianza kuondoka, mmoja mmoja kwa walionuna pasipo kuongeleshana, huku kwa wenye furaha wakishikana mikoni na kuongozana kwa madaha na mbwembwe mithili ya maharusi watokapo kanisani kufunga pingu za maisha.
Nje ya Mahakama wanaonekana mamia ya watu, waliojikusanya mafungu mafungu, hawa wameketi na wengine wamesimama ilimradi kila mmojawao alikuwa yupo uelekeo wa Mahakama ile. Katikati ya mamia wale wanaonekana wachache waliokuwa ndani ya sale safi huku wakiwa makini kufatila kila kilichokuwa kikifanywa na umati ule. Bila shaka, hawa walikuwa Askari Polisi waliokuwa wakitekeleza majukumu yao ya kawaida kuhakikisha usalama wa raia wale. Haikueleweka ni nini hasa kimewakusanya raia wengi kiasi kile nje ya Mahakama ile maana haukuwa utaratibu wala mazoea ya raia wa mji ule kujazana nje ya mahakama eti kwa sababu wanafuatilia kesi.
Hali kama ile ingetokea katika baadhi ya kesi za watu maarufu, hasa wale wanasiasa vipenzi vya wananchi, ndipo ungeweza kushuhudia umati wa watu wengi namna ile, nje na ndani ya viwanja vya Mahakama, lakini leo hii hali ilikuwa tofauti kabisa maana ijapokuwa haikuwa kesi ya kisiasa, umati ulikuwa mkubwa nje ya Mahakama ile ndogo ya wilaya.
Ukubwa na ongezeko la mkusanyiko wa watu ndio uliwafanya askari polisi waliokuwa zamu siku ile kutoa taarifa kwa wakubwa wakiielezea hali hiyo iliyoonekana kutokuwa ya kawaida na kuomba ongezeko la askari wengine ili hata ikitokea sintofahamu yoyote iwe rahisi kuikabili. Haukupita mda mrefu, zilionekana gari mbili zenye nembo ya jeshi la polisi Ubavuni zikiingia kwa kasi sana ndani ya eneo la Mahakama. Kabla hazijasimama kisawasawa, baadhi ya askari waliruka kutoka ndani ya magari yale na kudunda chini kwa ukakamavu wa hali ya juu. Jambo hilo lililopelekea umati kupiga mayowe na kelele za kushangilia. "Jambo Afande" "Jambo" "Jambo Afande" Walipeana salamu na bila kupoteza wakati walipangiana majukumu ya kutekeleza mahali pale.
Kusemakweli hali ya hewa ilikuwa nzuri sana siku hiyo maana licha ya uwepo wa mawingu kiasi lakini bado mvua haikunyesha, hivyo umati ule uliendelea kusubiri pale nje kwa utulivu mkubwa sasa tofauti na mwanzoni ambapo walikuwa wakiimba nyimbo mbalimbali za hamasa. Labda ungesema wamechoka, lakini hapana, maana bado walionekana kuwa na shauku ya kuona madai yao yakitekelezwa, ogezeko la maaskari polisi ndiyo kilikuwa chanzo cha utulivu ule, ni wakati ambapo Mahakama ilikuwa ikiendelea kulitafutia utatuzi lile lililokuwa limevuta hisia za watu wengi kiasi kile.
Hali ilibadirika baada ya wale waliokuwa ndani kujitokeza nje, hapo ilianza minong'ono ya sauti za chinichini kabla ya mwanaume mmoja kuanza kuimbisha wimbo kwa sauti ya juu,
Haki itendeeke, ee
Haki itendeeke, eee
Hatutokaa kimya!!!!
Mpaka mnyonge apewe haki yake!!!!!
Aliimba kwa nguvu na kwa sauti ya juu kabla ya wenzake kudakia ikawa sasa ni kuimba kwa kupokezana na umati wote ulikuwa ukitamka na kuimba maneno yale kwa sauti moja ungezani ni wanakwaya waliopitia mafunzo ya uimbaji. Hali ilibadirika zaidi pale alipojitokeza mwanaume mmoja toka ndani ya Mahakama, alikuwa mwanaume mfupi mfupi aliyevalia tracksuit ya bluu, miwani machoni, raba nyeupe miguuni nywele nyeusi zilizoonekana kutunzwa sana, na mkononi alishikilia kibegi kidogo cha mkononi huku akitafuna kitu mdomoni. Ukimwangalia kwa haraka ungemwona kuwa na uso uliosawajika, hakuwa na furaha japo alijitahidi kuficha hilo.
Watu Walichafukwa zaidi baada ya kumuona mwanaume huyu, nyimbo ziliimbwa zaidi na kwa sauti ya juu, wengine walitoa kauli chafu kumtukana mwanaume yule ambaye hakuonekana kujali sana kuhusu kilichokuwa kikiendea pale nje ya mahakama kwani kile kilichotokea ndani ya Mahakama kilikuwa kimechanganya na kumuumiza zaidi.
Alikuwa Akitatembea kwa hatua za taratibu mithili ya aliyeogopa kujikwaa, hakuwa sawa kabisa mawazo mengi yalikuwa yakipita kichwani mwake hasa kila alipokuwa akijaribu kutafakari yaliyokuwa yanampata sasa. Mwanzoni hakujisumbua na Kelele za watu wale mpaka pale alipopigwa kichwani na chupa ndogo iliyorushwa na kijana mmojawapo wa makutano waliuwepo mahali pale.
Hapo alishtuka akijishaangaa kwa kuwa mjinga kiasi cha kushindwa kuwa makini na hatua zake,hata hivyo aliamua kuwa mpole maana katikati ya umati ule asingeweza kufanya chochote, aliinama na kuiokota ile chupa akataizama kwa kitambo kidogo huku akiiminya kwa hasira kisha akaitia ndani ya kibegi alichokishikilia mkononi.
Wengi walibaki kumshangaa maana hata polisi waliokuwa wakijaribu kumrinda asifikiwe na baadhi ya raia wenye hasira kali walishindwa kuelewa nini hasa kilikuwa kikimpa jeuri namna ile kiasi cha kusimama akionekana kutokuwa na haraka ya kutoweka katikati ya raia walioonyesha chuki za waziwazi juu yake.
Ni kama alizubaa zaidi maana alisimama jambo ambalo lilikuwa ni hatari sana kwake, na kadili alivyozidi kupoteza mda mahali pale ndivyo umati ulivyokuwa ukimkaribia, kama siyo uimala wa askari basi huenda angeishia katika mikono ya raia wale ambao bila shaka wangemuumiza kwa kumjeruhi vibaya au hata kuumuua kabisa maana walimtamani kweli.
Mmoja wa wasaidizi wake alimfata na kumshika mkono alimshinikiza kwa kumvuta na kumlazimisha kuiingia ndani ya gari ambalo liliwashwa haraka na kutoweka kwa kasi mahali pale kiasi cha kuwatimulia vumbi raia wale ambao walikitafsiri kitendo kile kuwa kosa la makusudi alilolifanya mwanaume yule na baadhi yao walijiapiza kutomsamehe kamwe.
Matukio yote hayo yalikuwa yakifatiliwa kwa ukaribu zaidi na jopo la wanaume wanne waliokuwa wameketi kuzunguka meza moja yanye screen iliyokuwa ikionyesha yote yaliyokuwa yakiendelea nje ya Mahakama. "Kazi nzuri sana imefanyika, naamini huu ni mwendelezo mzuri, na kwa kasi hii naona tutafanikiwa hata kabla ya wakati kufika" Aliongea mmoja miongoni kwa watu wale aliyeonekana kuwa kiongozi wao na baada tu ya kauli ile wote walisimama na kutoweka mahali pale pasipo kufanyika maongezi zaidi.
Juu ya jengo moja refu kidogo lililokuwa mkabara na Mahakama ile wanaonekana vijana wawili waliokuwa wakikusanya na kupakia baadhi ya vifaa vyao ndani ya begi kubwa walilokuwa nalo "mpaka hapa kazi yako nimeikamilisha, nafikiri sasa ni mda wa malipo, nikatie asilimia zangu nitembee" Aliongea mmoja ambaye mda huo alikuwa kainama akikusanya baadhi ya vifaa vyake.
Hata hivyo hakupokea majibu toka upande wa pili, aliamua kunyanyuka na kumtazama mwenzake aliyekuwa kimya mda wote akionekana kutafakhari kitu. "sawa bwanamdogo, haina shaka malipo yako utapata kama tulivyokubaliana" Alijibu mwanaume yule kuutoa wasiwasi wa mwenzake. "sasa hela yangu naipataje bosi, maana mda tuliokubaliana ndiyo huu, baada tu ya kumaliza kazi, sasa naona unanitazama tu hufanyi utaratibu wowote mimi nikapata hela yangu" Aliongea tena yule kijana ambaye sasa ameshasimama, kashikilia begi lake mkononi.
"Punguza wasiwasi dogo, hela ipo, okota kwanza hiyo frashi hapo chini tushuke mtaani nikakutolee pesa yako benki". "Haina noma mkubwa, kikubwa mimi nipate changu maana kazi yenyewe ni ngumu sana, kurekodi hii video kwenye eneo kama hili bila kibari maalumu ni jambo hatari sana kaka, ukibainika adhabu yake siyo ya kitoto, na ukizingatia sina mtu serikalini wa kunitete,,,,,, "
Kauli yake ilikatishawa na shambulio la ghafla alilofanyiwa, alijikuta kabanwa shingo na mikono yenye nguvu na kwakua hakuwa amejiandaa kwa tukio hilo aliishia kufurukuta akipambana kujinasua toka kwenye kabari ile. Alifurukuta bila mafanikio kwani adui yake alikuwa mwenyenguvu zaidi, kadili mda ulivyozidi kwenda pumzi zilianza kumwishia, miguu ilikosa nguvu na alijikuta mwenyewe bila kupenda akianguka chini. Kitendo hicho hakikumfanya adui yake kumuachia hivyo alianguka naye akiwa bado kalishikilia kwa nguvu shingo lake.
Ni mpaka pale alipojilidhisha kuwa uhai umeshauacha mwili wa windo lake ndipo aliuachia mwili wa kijana yule, mwanaume muuaji alisimama huku akihema sana kutokana na pulukushani aliyoipata wakati wa kutekeleza mauaji yale, inaonekana hakuwa binadamu wa kawaida, kuua kwake lilikuwa suala dogo ambalo angalifanya mda wowote kwa ustadi wa hali ya juu sana. Aliiwasha simu yake na kuipiga mahali, "Bosi, namba mbili imekamilika sasa" Aliongea maneno hayo mala baada ya simu kupokelewa na mtu wa upande wa pili ambaye hakutoa jibu lolote zaidi ya kuikata simu ile. Baada ya simu kukatwa mwanaume muuaji alilichukua lile begi, aliangaza huku na kule akikikaagua chumba kile kwa awamu ya mwisho kabla ya kufungua mlango na kutokomea nje.
Nje ya Mahakama umati ulikuwa ukizidi kupungua, watu walikuwa wakitoka makundi makundi, baadhi yao waliendelea kuimba nyimbo za kuhanikiza kufanyika kwa yale wayatakayo huku wengine wakipiga kimya ungedhani sio wao waliokuwa wakizomea mda mchache uliopita.
Kulikuwa na misafara mikubwa miwili ya watu, wapo walioelekea upande wa kusini wengine wakishikana kuelekea kaskazini, hata hivyo bado askari polisi waliokuwepo mahali pale wakiendelea kuwadhibiti watu wale kuepusha mtafaruko zaidi. Mda huo simu ilipigwa ikaitikiwa, "Halloo bosi" "Vipi mbona mpaka sasa sijapata mrejesho wowote" Iliuliza sauti ya upande wa pili wa simu, naye mpokeaji akajibu "Bosi, namba moja tayali ilishakamilika dakika tano zilizopita, lakini nilish,,,,, "
Simu ile ilikatwa na aliyekuwa upande wa pili pasipo kumpatia nafasi muongeaji kumalizia kauli yake. "Huyu naye fala kweli, sasa mbona amekata, anashindwa kusubiri nikamwelezea kuwa nilichelewa kumtaarifu kwa sababu sikupata muda wa kufanya hivyo, sasa raia wengi kiasi kile anafikiri ingekuwaje, mda mwingi nilikuwa makini kuwawangalia zaidi ya kufanya jambo lingine. Hata hivyo atajijua mwenyewe kikubwa kazi nimeifanya kama ilivyotakiwa" Alibaki akijiongelesha mwenyewe, akionekana kutofurahishwa na kitendo cha kukatiwa simu na mtu aliyekuwa upande wa pili.
Ni ndani ya nyumba moja ndogo ambayo licha ya kunakshiwa kwa rangi nzuri ya bluu lakini bado inaonekana kuwa ya zamani sana kutokana na muundo wake, aina ya ujenzi na muonekano wake, ilikuwa ni nyumba iliyoezekwa kwa vigae vilivyokwishakuwa vikuukuu sana kiasi cha kuruhusu nyasi kuota juu yake. Kwenye moja ya vyumba vya nyumba hii anaonekana msichana mmoja, amejilaza kwenye sofa kubwa lilokuwa mle ndani, mkononi ameshika grasi ya wine nyekundu akiendelea kukigigida kinywaji hicho taratibu kabisa bila hofu yoyote, mala nyingi jicho lake akiligeuza kwa madaha na mbwembwe kuiangalia simu ndogo iliyokuwa mbele yake juu ya meza ndogo ya kioo.
Kwa kumwangalia tu alikuwa ni aina ya wanawake ambao shida haikuwa sehemu ya maisha yao, mwanamke mrefu kidogo, mweupe, aliyesuka nywele za bei mbaya akiwa ndani ya kijinguo cha kulalia kiliyoiacha wazi sehemu kubwa ya makalio yake.
Kutokana na aina ya uvaaji wake ni wazi kabisa siku hiyo hakuwa na mpango wa kutoka nje ya nyumba ile, pengine labda kulikuwa na kazi maalumu alikuwa akiifanya mahali pale maana hakufanania kuwa mwenyeji wa nyumba ile. Ghafla ile simu ndogo juu ya meza ilitoa mwanga mkali na kuanza kuunguruma kwa nguvu "nshwssss, mda wote ulikuwa wapi, mbona hukupiga!"
Alisonya msichana yule na kutoa maneno hayo huku akijinyanyua kivivu na kukaa. Aliichukua simu ile na kubonyeza kitufe cha kupokea, hakuongea mpaka pale iliposikika sauti ya upande wa pili " Sikiliza Emmy tupo hatua nzuri sasa, mpango namba moja na namba mbili tayali imekamilika, vijana wanajiandaa kukamilisha namba tatu na ndiyo itakuwa kazi ya mwisho kufanyikia mjini kwa siku ya leo, namba nne na namba tano ni juu yako, jitahidi mala kila kitu kitakapokuwa sawa ulikamilishe hili, kumbuka tunakutegemea sana katika hili" Baada ya maelezo hayo, mtu aliyekuwa upande wa pili alikata simu pasipo kungojea jibu lolote.
Baada ya simu ile kukatwa, yule msichana ambaye sasa tunamfahamu kwa jina la Emmy alitoa pumzi ndefu kisha alinyanyuka na kujishikilia kiuononi mithiri ya mchezaji wa mpira wa miguu aliyechoka. Aliinyanyua grasi ile ya wine na kukitazama kinywaji hicho kilichokuwa kikiumwagilia moyo wake kwa wakati huo, alikigigida kinywaji chote mdomoni kwa mkupuo kisha akaiweka grasi mezani na kutoweka mle chumbani.
Pembeni kidogo ya jengo la Mahakama kulikuwepo na kituo cha mafuta ambacho wenyeji wengi wa mji ule hupendelea kukiita "sheli" Ndani ya sheli ile shughuli zilikuwa zikiendelea kama kawaida, siku hiyo biashara ilikuwa nzuri sana kutokana na uwepo wa watu wengi maeneo yale, hivyo biashara hasa ya vinywaji na vitafunwa vilivyokuwa vikipatikana kwenye supermarket ndogo ya sheli hiyo viliuzika sana. Tokea upande wa kuingilia linaonekana gari dogo aina ya "Spacio" likiingia ndani ya sheli ile, na kwenda kupaki uelekeo wa supermarket ile, akashuka kijana mmoja aliyeonekana kuwa na umri kati ya miaka 24 au 25 hivi. Kijana huyu anaonekana kuwa mwenyeji wa maeneo yale, alimchangamkia na kuongea na binti muhudumu wa duka lile kisha akatoweka mahali pale.
Hakwenda mbali na sheli ile bali alizunguka na kuchoma ndani ya jengo moja la ghorofa lililokuwa kwa nyuma, alizipandisha ngazi harakaharaka kuelekea ghorofa ya juu. Alipofika juu ni kamavile alichanganywa na mandhari ya mle ndani "du! Licha ya uenyeji wangu maeneo haya lakini sijawahi kuufaidi utamu wa huu mjengo" Aliwaza wakati ambao alikuwa akijihangaisha kusoma namba zilizoandikwa kwenye milango iliyozunguka korido ile.
Japokuwa hakuwa mgeni wa jengo lile lakini yaelekea alichanganywa na mpangilio wa vyumba, bado hakuwa amekipata kile alichokuwa akikitafuta. Alichukua simu yake ya kupangusa aina ya Tecno Common 20, aliigusa mala mbili haraka haraka ikawaka, akaingiza nywila na kwenda moja kwa moja sehemu yenye kumbukumbu ya jumbe alizokuwa akituma na kutumiwa, hapo alitafuta kidogo mpaka pale alipolipata jina la Morisi wa pili, akaligusa na kuanza kuangalia jumbe walizokuwa wakitumiana yeye na mtu huyo.
Aliweka utuo kwenye ujumbe mmoja ambao sasa aliusoma na kuuelewa "KIWILA HOTEL, room no 23, upper floor, around 8:30am" Baada ya hapo aliirudisha simu yake mfukoni na kuelekea upande wa kulia kwake, alitembea kidogo kuuelekea mlango mmoja, alipoufikia aliunyanyua uso wake na sasa aliweza kuyaona vema maandishi yaliyoandikwa juu ya mlango huo "No 23" ilikuwa imeandikwa kwa namna ya kuchonga na rangi ya manjano ya kukoleza. Mpaka hapo alijua yupo mahali sahihi kabisa, hivyo pasipo kupoteza mda alianza kubisha hodi kwa kugonga mlango taratibu "ngo ngo ngo",,,,