singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,498
- 8,419
- Thread starter
- #2,741
SEHEMU YA 489.
Baada ya kufunguliwa mlango na mhudumu mwenye asili ya kiarabu alievalia suti , Edna alishangazwa kukuta sio mtu anaekutana nae bali ni jopo la watu kama ishirini waliojipanga kwenye meza na ajabu ni kwamba mara baada tu ya kuingia wote walisimama kiheshima , kati ya sura alizozifahamu ni moja tu ambaye ni Nadia Alfonso mwanasheria wake.
Edna na Suzzane walihisi wamekosea chumba walichopaswa kuingia na Edna alitoa ishara ya kuomba msamaha kwa kuingilia kikao.
“Karibu sana Madam Persephone” Waliongea wote kwa pamoja kwa lugha ya kingereza na kisha waliinamisha vichwa kuonyesha ishara ya heshima jambo ambalo lilimpagawisha Edna na moyo wake kupiga kwa nguvu , alijihisi ni kama anaota na akishituka ingekuwa ndoto.
Kwa mara ya kwanza alihisi jina la Madam Persephone ambalo alilikuwa akiitwa mara kwa mara bila ya kujua sababu yake alihisi sio la kwake , ule ujasiri aliokuwa nao kwa muda huo ulimpotea na aliishia kuduwaa.
Suzzane pia alikuwa kwenye mshangao asijue nini kinatokea mbele ya macho yake , walikuja hapo kwa minajili ya kukutana na Tajiri Khalifa kutoka Dubai , mtu ambaye alichangia kiasi kikubwa cha pesa katika taasisi ya Edna Foundation na uwepo wao hapo ni kutii wito wa kuonana na tajiri huyo , lakini mambo yanaonyesha kuwa tofauti.
Licha ya kwamba alihisi yupo ndotoni lakini ulikuwa uhalisia na jinsi watu waliokuwa mbele yake walivyokuwa wakimwangalia alijua kabisa walimlenga yeye na ndio ambaye alikuwa akisubiriwa, lakini bado alijiuliza kwanini yeye na ni maigizo gani yanafanyika.
Kwanza chumba kilionekana kilikuwa cha mikutano ndani ya hoteli hii ya Peacock, pili mpangilio wa hapo ndani ulikuwa ni wa kikao muhimu kutokana na watu waliokuwepo , ilikuwa ni meza ndefu ambayo inajumla ya watu kumi kila upande kukamilisha watu ishirini na ni kiti kimoja tu ambacho kilikuwa wazi , kiti cha katikati ambacho huruhusu mkaliaji kuona nyuso za kila mtu aliekuwa mbele yake , ni rahisi kusema ndio kiti cha mwenyekiti kama ni kikao ambacho kinatarajiwa kufanyika.
Watu waliofahamika ambao wapo ni Shekhe Assad , Tajiri Khalifa , Mellisa Luiz , Pastor Cohen , Nadia Alfonso , Zoe Kovacic , Phill Knight na wengine wengi ambao ilionyesha ni wanachama wa Ant- illuminat.
Mwanadada mmoja aliekuwa wa kifilipino , alievalia suti alimsogelea Edna na kuinamisha kichwa mbele yake kwa namna ya heshima na kisha akavuta kiti kilichokuwa wazi na kumuonyesha ishara ya kukaa.
Edna bado aikuwa kwenye mshangao na alishindwa kujua achukue maamuzi , ya kuondoka au abaki na hata aliponyeshwa kiti cha kukaa bado hakupiga hatua kukisogelea maana alijua kukaa kwenye kile kiti ni kama yeye ndio anakwenda kuongoza kile ambacho kingekwenda kuendelea hapo ndani , kitu ambacho hata hakijui ni nini.
“Madam!!!” Suzzane alimshitua Edna ambaye bado alishindwa kufanya chochote licha ya kuonyeshwa kiti cha kukaa.
Edna aliinua uso wake na kuanza kuangalia kila mmoja ambaye yupo ndani ya hiko chumba, kuna wengine alikuwa akiwafahamu na kuna wengine hakuwahi kuwaona popote.
Lakini ghafla tu Edna alitoa tabasamu hafifu kama vile anavyofanyaga akiwa kwenye kampuni yake akiwa na kikao na wafanyakazi wake na alisogelea kile kiti na kuketi na kuwaangalia watu wote waliokuwa hapo ndani kama vile alikuwa akiwajua.
Ni kintendo ambacho hakikumshangaza Suzzane tu lakini kila mmoja kilimuacha na maswali lakini sio hivyo tu pia kiliwafanya kuwa na tumaini.
**********
Roma baada ya kuambiwa na Afande Kweka kwenda kuonana na Zenzhei , hakutaka kuchelewa sana , alikuwa na shauku ya kujua kwanini Zenzhei anataka kurudi Hongmeng baada ya kuishi Tanzania kwa muda mrefu.
Alitaka pia kujua ni jambo gani ambalo Zenzhei alitaka kumwambia , alikuwa na shauku kubwa kutokana na kwamba alikuwa na mpango wa kuivamia Hongmeng siku moja hususani muda huo ambayo alijua kabisa yeye ni adui na jamii hiyo , hivyo alitaka kukusanya kila taarifa iliokuwa ikihusiana na jamii hizo ili kumsaidia huko mbeleni.
Roma alimuaga sekretari wake kwamba anatoka na anagerudi siku iliokuwa inafuata , Tanya alishangaa kutokana na kwamba kuna baadhi ya maamjuzi yalikuwa yakimpasa kuyashughulikia siku hio hio lakini alikosa ujasiri wa kumzuia Master wake.
Ni zaidi ya miezi sasa tokea Tanya achukue majukumu ya Amina kama Secretari na alionekana ashanza kuipenda kazi yake na kuizoea na alikuwa ni msaada mkubwa kwa Roma kwani mambo mengi aliyafanyia kazi.
Muonekano wake ulikuwa umebadilika kwa asilimia mia moja na ilikuwa ngumu kujua ndio anaehusika kuongoza kundi la Yamata kutoka Japani ambalo linamilikiwa na Roma.
Roma alitumia muda machache sana kufika nyumbani kwa babu yake na baada ya kusalimiana na Afande Mstaafu Camilius Kweka ilisalimiana na Zenzhei pia wote walikuwa wamekaa nje kwenye bwawa la kuogelea na ilionekana walikuwa wakiongea.
“Nitawaacha muongee”.
“Camilius haina haja ya kuondoka , ninachoongea na Mr Roma sio kipya kwako”
“Hapana umesubiria muda mrefu na huu ni muda wako, Wewe mtukutu ukimaliza unione kwanza kabla ya kuondoka”Aliongea Afande Kweka na kisha aliondoka eneo hilo.
“Mr Roma samahani kama nimekuchukulia muda wako , muda huu ulipaswa kua kazini”
“Usijali kuhusu hilo , nilipaswa kuja hata jioni lakini kwasababu sikuwa na kitu cha kufanya kazini nimeona nije mapema”Aliongea Romana kumfanya Zenzhei kutingisha kichwa kumuelewa.
Na muda huo mfanyakazi aliwaletea Juisi ya matunda na kuweka mbele yao na kisha akaondoka.
“Mr Roma muda wangu wa kukaa kwenye ulimwengu wa kawaida umeisha”
“Nilipoambiwa unaondoka nimeshangaa , kwani ulikuwa na ukomo wa kuishi Duiani?”
“Nadhani ushawahi kisikia sheria za miliki za kijini juu ya binadamu au viumbe wanaojifunza mbinu za kuvuna nishati za mbingu na Ardhi?”
“Najua watu wa jamii kutoka miliki za kijini na binadamu ambao wamefikia katika levo ya Nafsi hawapaswi kuishi kwenye ulimwengu wa kawaida”
“Upo sahihi Mr Roma na mimi muda wangu wa kuishi hapa duniani ushafikia ukomo?”
“Lakini uliishi kwa miaka mingi hapa Tanzania na naamini bado ulikuwa kwenye levo ya Nafsi , kwanini unaondoka sasa?”
“Ni stori ndefu Mr Roma ambayo nataka unipe muda wako nikuelezee ili upate kujua nia ya mimi kutaka haya maongezi na wewe”
“Nipo tayari kukusikiliza”Alijibu Roma kwa msisimko na Zenzhei alianza kumuhadhithia Roma kila kitu kuanzia namna ambavyo Zenzhei na familia yake walivyokimbia katika miliki za kijini na kuja katika ulimwengu wa kawaida , alielezea namna ambavyo baba yake mzazi na mama yake mzazi walivyopambana na wajumbe kutoka Hongmeng mpaka kuwaua , aliendelea kuelezea namna ambavyo baba yake alipambana na mtu asieonekana ambaye ndio aliyakatisha maisha ya wazazi wake mbele yake , namna ambavyo alipona , namna ambavyo alijiunga na kundi la kininja la Yamaguchi kwa ajili ya kulipiza kisasi kwa The Doni.(Rejea episode ya 317).
Roma alishangazwa na stori nzima ya Zenzhei na sasa alielewa uwepo wa Zenzhei kwenye maisha ya Afande Kweka ni kutokana na misheni aliopewa na kundi la Yamaguchi kukaa nae karibu.
Roma alikuwa akielewa kuhusu Yamaguchi lakini kwenye maisha yake hakuwahi kulipa umuhimu kundi hilo na yote hayo ni kwasababu aliyachukulia kama makundi mengine tu ya kininja ambayo yalikuwa yakiua kwa ajili ya pesa ,lakini hakufahamu kuna zaidi ya hayo.
“Kwahio kundi la Yamaguchi hawakuweza kukufahamu kama unatokea Hongmeng?”
“Hawakuweza kunifahamu mpaka baadae sana nilipowakatalia misheni ya kumuua Cammilius”
“Ushawahi pewa mishenni ya kumuua Afande Kweka?”
“Ndio lakini sikutekeleza agizo, Camillius nilifahamiana nae kwa muda mrefu tokea mke wake akiwa hai na amenisaidia kwenye mambo mengi ambayo yalinigusa moja kwa moja na kwangu nilimchukulia kama ndugu,nilipomuelezea ukweli juu ya kwanini nipo kwenye maisha yake hakukasirika na aliniacha nifanye chaguzi mimi mwenyewe kumchagua yeye au kundi na mamuzi nilioyafanya ni kumchangua yeye na ndio nilipokuja kuwa mlinzi wake mpaka leo hii”
“Nikupe pole kwa yaliokukuta , lakini bado sijapata jibu la moja kwa moja umeishi miaka mingi ndani ya Tanzania na Hongmeng hawajakusumbua , kwanini sasa hivi?”Aliuliza Roma , alishangaa kwani ni kweli Zenzhei alikuwa kwenye levo ya Nafsi na kwa sheria za Hongmeng hakutakiwa kuishi kwenye ulimwengu wa kawaida , lakini ajabu ameshaishi miaka mingi sana bila ya kurudishwa.
“Wazee wa Hongmeng hawakufahamu uwepo wangu duniani , walifahamu nimekwisha kufariki miaka mingi iliopita”.
“Lakini mara ya mwisho ulisema ulikuwa na mawasiliano na Hongmeng”
“Ambao wanafahamu uwepo wangu hawakuuweka wazi kwa Wazee wa Hongmeng , ndio maana nikasema Wazee hawakufahamu uwepo wangu duniani”
“Kama ni hivyo naweza kutafsiri ulikuwa na mawasiliano na wajumbe wa Hongmeng pekee na walificha uwepo wako lakini ukawa unaendelea na mawasiliano nao kama ni hivyo naamini kuna sababu wakaamua kuficha uwepo wako”Aliongea Roma.
“Upo sahihi kuna sababu kubwa ya kuficha siri ya uwepo wangu duniani na ni kutokana na ahadi ya faida”
“Ahadi ya faida?”
“Ndio Mr Roma unaweza kusema niliwaahidi kitu chenye faida ili waendelee kunifichia siri ya uwepo wangu hapa Tanzania”
“Kama ni hivyo kwanini sasa hivi wanataka urudi?”
“Kwasababu ahadi sijaitimiza na siwezi kutimiza kutokana na nia yangu ya kulipiza kisasi kwa kile kilichowatokea wazazi wangu, kutokana na kutotimiza ahadi walinitishia mara nyingi kwenda kutoa taarifa kwa Wazee , lakini nilijitahidi kuwa mjanja kwa kuwasubirisha kwa maneno nikisubiria ujio wako”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa ujio wake tena.
“Unamaanisha nini kusubiria ujio wangu?”Aliongea Roma na Zenzhei alitabasamu.
“Kwasababu kuna mtu nilikutana nae miaka iliopita na akaniomba msaada na kisha akaniambia ikiwa ni muda sahihi rudia haya maneno ‘ Damu na Giza ni laana’”Aliongea Zenzei nakumfanya Roma kutoa macho.
“Ulishawahi kukutana na mtangulizi wangu?”Aliuliza Roma akiwa haamini Zenzhei anafahamu hayo maneno kwasababu yalikuwa ni maneno ambayo ni fumbo.
Mara ya mwisho Roma kuongea na Hades wa zamani alimwambia maneno hayo ya fumbo na kumpa maelekezo mtu yoyote ambaye angeyatamka mbele yake anapaswa kumsaidia.
“Mr Roma kukujibu swali , nitasema ndio nilikutana nae mara moja tu na aliniomba msaada wa kumtambua mwalimu”Aliongea na kumfanya Roma kuzidi kujawa na shauku na mshangao kwa wakati mmoja na Zenzhei alijua Roma hakumuelewa hivyo akamwelezea kwa kirefu.
Kwa maelezo ya Zenzhei ni kwamba Hades wa zamani alimuomba msaada wa kumtajia mwalimu ambaye anaweza kufundisha binadamu mbinu za uvunaji wa nishati ya mbingu na ardhi kwa njia ndefu yaani ile ya Maandiko ya urejesho isio na kikomo ambayo ndio hio aliojifunza Roma na mtu ambaye alimtajia ni Tang Chi yaani master wake Roma.
Kwa lugha nyepesi Zenzhei alimpendekeza Tang Chi kwa Hades wa zamanni na Tang Chi akaja kuwa Master wa Roma.
Roma alishangazwa na ufunuo huo wa mambo lakini bado ilimchanganya kwani kwa namna ambavyo alikutana na Tang Chi ilikuwa ni kabla alipokutana na Hades wa zamani , kuna kitu kilimwambia huenda Master Tang Chi aliagizwa na Hades wa zamani kumfundisha yeye mbinu za kuvuna nishati za mbingu na ardhi.
Roma alijikuta akikumbuka namna ambavyo alikutana na Master Tang Chi ilikuwa ngumu sana kuamini alikuwa ameagizwa na mtu.
“Mr Roma najua mtangulizi wako hajakuambia mambo mengi na mimi pia sio jukumu langu kukuambia yale ambayo hajakuambia kwani hata hivyo siyajui , nilimpendekeza Tang Chi kwasababu ndio binadamu pekee ambaye nilimfahamu kwa mara ya kwanza kujifunza tamaduni za jamii zisizoonekana na tokea nilipomsaidia hatukuwahi kuonana tena , lakini aliniambia msaada niliompatia ukizaa matunda basi nitayashuhudia kwa macho yangu na ndio ninapaswa kutamka maneno ya Damu na Giza ni laana”Aliongea Zenzhei na kumfanya Roma kukuna kichwa , ni kweli hakuwa akijua mambo mengi kuhusu Hades wa zamani na ilikuwa sawa kutokumuelewa, kwanza mtu mwenyewe aliishi miaka mingi hivyo huenda alikuwa na mipango mingi, Roma alifikiria na alijikuta akivuta pumzi.
“Kama ni hivyo nadhani unapaswa kuniambia shida yako na mimi nitakusaidia”Aliongea Roma na kumfanya Zenzhei kuvuta pumzi.
“Ninarudi Hongmeng kwasababu nahitajika kurudi , lakini naenda kukusubiria, mpaka sasa Mr Roma umekuwa adui namba moja wa Hongmeng na muda na saa yoyote watatoka huko walipo na kuja kukushambulia kabla ya muda huo kufika unapaswa kuwa wa kwanza kuchukua hatua”
“Unamaanisha niende Hongmeng na kupigana nao?”
“Ndio njia pekeee ya wewe kuwa salama na watu wako unaowapenda , mbinu uliojifunza ni hatari zaidi na hakuna mtu wa hongmeng yoyote ambaye amefanikisha kufikia leo ya Kuzaliwa upya”
“Lakini kama nitakuja kupambana Hongmeng watanizidi kwa uwezo wangu niliokuwa nao huu na isitoshe taarifa zinaonyesha ni wengi ambao wameshavuka levo ya Dhiki”
“Kuhusu uwezo wako sina wasiwasi umeweza kufikia levo ya kuipita Dhiki ndani ya umri mdogo sana hivyo natarajia utaenda juu zaidi ndani ya muda mfupi sana , nimekuambia nimevunja ahadi ndio maana Wazee wakagundua uwepo wangu duniani basi kile nilichoahidi nitakupatia wewe”Aliongea.
“Unamaanisha?”
“Mr Roma haikuwa bahati mbaya familia yangu kushambuliwa ni kwasababu ukoo wetu ulimiliki kitu cha thamani sana ambacho Baba na Mama hawakuwa tayari kukiweka wazi”Aliongea na kisha akampatia Roma karatasi.
“Hio karatasi imejaa taarifa ambayo ndio inanifanya nirudi Hongmeng, ndio urithi wa pekee kutoka kwa familia yangu nilioutunza kwa muda mrefu, nakupatia wewe kwasababu ni mtu sahihi wa kuwa nao”Aliongea na kumfanya Roma aifungue ile karatasi na alijikuta akishangaa baada ya kuona ni kanuni ya utengenezaji wa vidonge vya kusaidia mafunzo ya kuvuna nishati ya mbingu na Ardhi.
“Hii ni kanuni ya kutengenezea vidonge vya Poya?”
“Inaonekana ushalifahamu tayari jina lake , jibu ni ndio kama utaweza kufanikisha kutengeneza hivyo vidonge itakuwa rahisi kwako kupanda levo ya juu zaidi na hakuna kiumbe chochote kutoka Hongmeng kitakuwa tishio kwako”Aliongea na kumfanya Roma macho yake kuchanua kwa furaha na kupitia kwa haraka ile katatasi.
“Kwanini hukutengeneza hivi Vidonge wewe na kukuwezesha kupanda levo za juu zaidi na kulipiza kisasi?”
“Mr Roma nimekupatia kanuni tu , uwezekano wa kukamilisha utengenezwaji wa hivyo vidonge haitokuja kuwa rahisi na haikuwa rahisi wangu pia kutengeneza nikiwa hapa duniani na sitoweza kutengeneza nikiwa Hongmeng wewe pekee ndio naamini unaweza kukamilisha”Katika siku ambayo Roma alipata kitu cha thamani basi ni siku hio, hakuamini Zenzhei alikuwa na material muhimu na hamwambii mpaka wakati anaondoka , huenda angemsaidia hata kutafsiri kanuni hio.
SEHEMU YA 490.
Abu Dhabi- UAE.
Ni baada ya mwezi mmoja tokea waanze uchunguzi wa kile ambacho alifanya Chriss , kitendo cha kutaka kumuua Edna, waliamini kabisa majaribio ya kuuwawa kwa Edna ni nje ya malengo ya jumuia yao hio ya siri na ndio maana walitaka kuufahamu ukweli , kwanini Chriss kafanya maamuzi alioyafanya.
Uchunguzi ulikamilika mara baada ya Nadia Alfonso kumuhoji Roma na kupata majibu ya kile kilichotokea na pia kumuhoji Suzzane kwa kile ambacho kilitokea na baada ya kupata maelezo yao na kuona yanafanana waliendelea na uchunguzi wa kutaka kujua zaidi kuhusu Chriss aliishi wapi mara baada ya kuokolewa na Hades wa zamani gerezani katika mikono ya CIA.
Naam sasa ilikuwa ni siku ya ijumaa mara baada ya swala ya mchana muda wa saa tisa katika moja ya makazi ya Tajiri Khalifa ndani ya Abu Dhabi kulikuwa na kikao cha siri sana ambacho kilikuwa kikiendelea.
Ni kikao ambacho hakikuhusisha watu wengi sana ,waliohudhuria ndio mhimili wa umoja huo wa siri ufahamikao kwa jina la Ant Illuminat.
“Mmefikia katika hitimisho?”Aliuliza mwanaume mmoja alievalia kilemba kichwani na kanzu.
“Ndio Shekhe”Alijibu kijana alievalia suti huku akiwa ameshikilia kishikwambi mkonnoni na jibu lake liliwafanya watu sita walioketi kwenye meza ya pembe nne wamwangalie kwa shauku ya kutaka kumsikiliza.
“Unaweza kuendelea”Aliongea mwanaume mwingine alievalia suti na miwani , alikuwa ni mzee ambaye umri wake ulionyesha kuwa mkubwa kutokana na nywele zake kuwa nyeupe.
“Nadia Alfonso alifanikisha kufanya mahojiano na Roma Ramoni juu ya kile kilichotokea na ameweza kutupatia majibu yaliorahisisha uchunguzi”Aliongea na kisha akafanya ‘casting’ ya kishikwambi chake na Screen ya TV ya nch 85 ya kampuni ya Sumsung na palepale ilionekana picha ya ua.
“Mnachokiona kwenye Screen ni ua adimu linalofahamika kwa jina la Blue Ghost Orchid, kwa maelezo ya Mr Roma Ramoni kutoka Tanzania anasema kabla ya Chirss hajamshambulia CEO Edna na Miss Suzzane alitokea mwanamke na akawaokoa na baada ya Chriss kufariki mwanamke huyo aliacha zawasi ya hilo ua , Maelezo haya yanafanana na ya Bi Suzzane ambaye pia tulichukua maelezo yake”Aliongea na kisha akapozi kidogo na kuangalia kishikwambi chake na kwenda ukurasa wa pili.
“Blue Ghost Orchid ni utambuisho wa taasisi ya siri yenye makao makuu nchini Singapore lakini pia ni utambulisho rasmi wa mwanachama baada ya kupokea ua hilo kama zawadi kutoka kwa The Doni”aliongea na kuwafanya wale wazee kuangaliana.
“Kwa maelezo yako tunapaswa kuamini The Doni ndio aliemuokoa CEO Edna si ndio?”Aliuliza na kumfanya kijana yule kutingisha kichwa na kisha akaendelea.
“ Kwa maelezo ya Bi Suzzane na Mr Roma mwanamke aliemuua Chriss ni Clellia Allisanto ambaye ni katibu mkuu wa umoja wa mataifa”Aliongea na kuwafanya wote kuangaliana.
“Mr Alban unatuambia kwamba aliemuokoa Edna ni Katibu mkuu wa umoja wa mataifa?”Aliuliza mzee mwingine wa kiafrika alievalia suti.
“Tumeshindwa kufikia kwenye hitimisho kutokana na kwamba hakuna namna yoyote ya kuthibitisha kama Clellia Allisanto ni The Doni”Aliongea na kuwafanya waanze kuongeleshana wao kwa wao kwa dakika kadhaa na kisha wakamgeukia.
“Vipi kuhusu Chriss, aliishi wapi mara baada ya kutolewa gerezani na kwanini alitaka kumuua Bi Edna kuna dhamira yoyote mmepata kuifahamu?”.
“Kamati yetu ya uchunguzi iliweza kupokea nyaraka iliotumwa kwetu kwa njia ya barua pepe na mtu ambaye hakujitambulisha jina na imetoa majibu ambayo tumeshindwa kuyahakiki na nitayaweka wazi”Aliongea na kisha alienda kwenye Gmail na kufungua nyaraka iliotumwa na palepale ilionekana kwenye Skrini na kuwafanya wale wazee wenye miwani kuziweka vizuri ili kusoma na wale ambao macho yao yalikuwa imara walikodoa macho.
“Nyaraka hii inaonyesha Chriss aliishi ndani ya Vatican mara baada ya kutolewa gerezani nchini Marekani na alikuwa ni mkutubi wa maktaba Chemba namba 4”Alielezea ile nyaraka na kuwafanya wale wazee kuendelea kushangaa.
“Kuna taarifa yoyote inaonyesha alikuwa na dhamira ya kutaka kumuua Bi Edna?”Aliuliza na Alban alitingisha kichwa kuashiria jibu ni ndio na kisha akapangusha kishikwambi chake na akatoa nyaraka nyingine iliotumwa kwao kama barua mfumo wa portable file(PDF).
“Hii ni barua ambayo tunaamini imeandikwa na Chriss mwenyewe kabla ya kutekeleza misheni ya kutaka kumuua Bi Edna nchini Tanzania na inaonyesha sababu kwanini alifanya maamuzi tofauti na misheni aliopatiwa.”Aliongea na palepale alianza kuisoma.
Kwa maelezo ya barua inaonyesha ni kweli Chriss alikuwa akiishi ndani ya Vatican kwa kipindi chote tokea atoroshwe kwenye gereza chini ya serikali ya kimarekani , anasema kwamba aliishi kwa Dilema ni upande upi anapaswa kuegamia kutokana na mfanano wa malengo ya dunia ijayo kati ya taasisi mbili tofauti yaani hio ya Ant-Illuminat na nyingine ambayo hakuitaja.
Anaendelea kusema maamuzi alioyafanya ni chaguzi alioifanya yeye mwenyewe na barua hio kama wataisoma basi atakuwa tayari amekwisha kufariki na misheni yake imefeli.
Mwisho kabisa anawafunulia kwamba misheni aliopewa kwa ajili ya Ant -illuminat ni kuwajuza kwamba kiongozi wanaemgojea sio yule ambaye wanamfikiria bali ni yule ambaye anapewa ulinzi na yule wanaemfikiria na ushahidi wa maneno yake upo kwenye mchoro wa unabii.
Mwisho kabisa wa barua anasema kama watakuwa wamefanikisha kupata barua yake basi misheni aliopewa na aliemuokoa imekamilika na atapumzika kwa amani akimlenga Hades wa zamani aliempatia misheni.
“Mchoro wa unabii!!??”Walijikuta wakiongea wote kwa wakati mmoja kwani hawajaelewa.
“Barua hii ni ya kweli inetokea kwake kutokana na sahihi na nadhani kabla ya kufikiria mchoto wa unabii tunapaswa kujua kauli yake: ‘yule tunaemfikiria sio mwenyewe bali yule anaelindwa na tunaemfikiria’ tuanzeni na kufumbua kauli yake”Aliongea mwanaume alievalia suti na Collar ya kiuchungaji.
“Albani kuna taarifa nyingine ambayo bado haujatupatia?”
“Hakuna Shekhe”
“Kwasasa uchunguzi wenu uhamie upande wa Clellia Allisanto ili kufahamu kama ndio The Doni, kuhusu kuthibitisha uwepo wa Chriss ndani ya Vatican tutatumia koneksheni tulizokuwa nazo”Aliongea Shekh na Albani alitingisha kichwa kukubali.
“Unaweza kwenda kwasasa , tunapaswa akujadili”Aliongea na kisha Albani aliondoka , haikueleweka alikuwa akitokea kitengo gani ndani ya taasisi hio ya Ant-illuminat lakini ni dhahiri ni sehemu ya kamati ya uchunguzi ilioutwa kutafiti kifo cha Chriss.
“Pastor Cohen nini maoni yako?”Aliuliza Shekhe na kumfanya mzee alievalia suti na kuwa na kipara cha nywele nyeupe kuvuta pumzi na kuzishusha.
“Mpaka kufikia leo hii ni mengi ambayo yamefanyika na tumejipanua sana ndani ya mabara karibia yote na tuna washirika wengi wa kutuunga mkono kupambana na uovu , lakini licha ya mapambano yetu hatukuwa na kiongozi na wote tunajua tarehe 24 ya mwezi wa nne kwa mujibu wa Kalenda ndio siku ya kumtambua kiongozi wetu , nadhani alichoongea Chriss tunapaswa kukifiria mara mbili ili kupata majawabu lakini pia kuihakikisha kauli yake”Aliongea Paster Cohen kwa lugha ya kingereza.
“Naungana na Pastor Cohen ,nadhani ni wakati sahihi kwanza kuchambua kile alichoandika kwenye barua yake ili tufanye reasoning”Aliongea mwingine.
“Tunaefikiria siku zote kama kiongozi wetu ajae ni mrithi wa Hades ambaye ni Mr Roma Ramoni lakini kama sio yeye kwa kauli ya Chriss je anaemlinda ni nani?”
“Nadhani kujibu swali hilo kwa wepesi ni sisi kujiuliza ni nani wa muhimu kwenye maisha ya Hades mpya?”
“Mke wake ndio muhimu zaidi”
“Upo sahihi Shekhe Assad, nadhani hili pia linatoa majawabu ya kauli ya Chriss kuwa katika Dilema”Aliongea mwingine .
“Kwa haraka haraka inaonyesha Chriss hakuwa akifanya kazi tu kama mkutubi ndani ya Vatican , huenda kuna watu aliokutana nao na kujenga nao mahusiano ambayo yamempelekea kwenye dilema na huenda dilema aliokuwa nayo ni katika kuchagua upande aidha wa kwetu au wa kwao na ni sahihi pia kuamini huenda ndio wamemuonyesha kitu alichokiita mchoro wa unabii”
“Unafikiri huo mchoro wa unabii unahusiana na Edna?”
“Kama Bi Edna anapaswa kuwa kiongozi wa umoja wetu ambaye amechaguliwa na Hades wa zamani nadhani kuna uwezekano mchoro huo wa unabii unamzungumzia na ndio maana Chriss akachagua kutaka kumuua kwa kuagizwa na upande mwingine”
“Lakini kama mchoto unamzungumzia Edna kuwa kiongozi wetu kwanini na The Doni akamuokoa?”.
“Hili ni fumbo gumu , lakini naamini majibu yake tunayo wenyewe”
“Unamaanisha nini Paster Cohen?”
“Wote tunajua namna ambavyo Hades wa zamani alivyomuhusisha Seventeen kwenye mpango LADO, mnafikiri ilikuwa bahati mbaya , Seventeen na Edna ni mapacha tena wa kufanana kabisa na mpaka sasa hatujui Seventeen yuko wapi na tukumbuke yeye ni mwanachama wa ant-illuminat na ndio ambaye alimwingiza Zoe Kovac kwenye uanachama na haikuwa hivyo tu, Seventeen alikuwa na madaraka ya kuchagua mwanachama mpya wa ‘first echelon’ cheo ambacho ni kikubwa katika jumuia yetu na ni madaraka makubwa”
“Lakini wote tunaamini kiongozi wetu amekabidhiwa muhuli na Hades wa zamani , si ndio ulivyosema Shekh Assad namna ya kumtambua?”
“Uko sahihi kwa maelezo ya Hades wa zamani tutamtambua kiongozi kwa kutuonyesha pete ya muhuri(signet ring)?”
“Basi nadhaini hilo ni jibu la hiki tunachojadiliana hapa, kama maneno ya Chriss yapo sahihi na Hades mpya sio mwenye umiliki wa pete yenye muhuri basi mke wake Edna atakuwa nao”
“Upo sahihi ndugu Khalifa , lakini kalenda yetu inatupa muda mchache sana wa kutambua nani mmiliki wa pete hio ya muhuri wa uongozi , kalenda yetu inaonyesha tarehe 24 mwezi wa nne ndio siku ambayo tunapaswa kumtambua kiongozi”Aliongea na kuwafanya watu wote kuingia kwenye mawazo na waliona ana point.
“Nadhani kuna namna moja tu ya kuthibitisha maneno ya Chriss ni ya kweli au ya uongo?”Aliongea Shekhe Assad.
“Unataka kusema nini?”
“Tarehe ishirini na nne ndio siku katika kalenda yetu ya kumtambua kiongozi wetu na Chriss katuachia tayari fumbo na wote tunafahamu mtu muhimu katika maisha ya Hades mpya ni Edna mke wake , nadhani hili ni jibu tosha kwetu, Kama Edna kweli ni kiongozi wetu basi lazima atakuwa na pete ya muhuri wa uongozi na siku hio anapaswa kutuonyesha”Aliongea na kufanya chumba kukaa kimya.
“Wajumbe mnasemaje juu ya wazo la Shekhe Assad?”
“Kama kweli fumbo la Chriss linamuonyesha Edna ndio kiongozi wetu basi lazima atakuwa na muhuri wa uongozi”Alirudia mwingine kauli ileile ya Shekhe Assad.
“Na kama hatokuwa na pete ya muhuri basi tutatambua moja kwa moja yeye sio mlengwa na sio kiongozi wetu na fumbo la Chriss sio sahihi”Aliongea na wote walikubaliana na wazo lake.
“Kama ni hivyo tunafanikishaje kumfanya atuonyeshe pete hio?”Aliuliza Tajiri Khalifa.
“Tunatakiwa kumfanya atuonyeshe na ili hilo lifanikiwe lazima tuwe na mpango, Miss Edna anaweza kuwa na muhuri lakini hana ufahamu wowote kuhusu jumuiya yetu”
“Naunga mkono hoja na matukio mengi yanaonyesha ndio kiongozi wetu na wote hatujui hapa huenda Hades mpya amemkabidhi Edna pete hio kwa maelekezo ya Hades wa zamani”
“Ni kweli kabisa hakuna ambaye anajua nini Hades wa Zamani na Hades mpya waliongea wakati wakukabidhiana urithi , huenda alimwagiza Edna apatiwe muhuli na yeye ndio anaepaswa kumlinda”
“Mimi nina mawazo tofauti , kwa maelezo ya Hades wa Zamani hajamwambia Hades mpya kitu chochote kuhusu Ant illuminat na ameseme yeye mwenyewe angefahamu kitu kimoja kimoja kadri ya muda unavyosonga,tutaomba CEO Edna atuonyeshe muhuri wa uongozi kama kweli anao lakini tusiende na wazo la kuamini kwamba Hades mpya kampatia pete hio ya muhuri wa uongozi, nadhani mpaka sasa tunaelewa kwamba Hades hajamwambia mkewe chochote kuhusu Seventeen kuwa ni pacha wake , unafikiri ingekuwa rahisi kwake kumpatia Muhuri”Aliongea Shekhe na maneno yake yalionekana kuwa na mantiki.
Makubaliano ni tarehe ishirini na nne mwezi wa nne kuonana na Edna ili aonyeshe pete ya muhuri wa uongozi wa jumuia hio ya ant-illuminat.
Naam Edna kukutana na jopo la watu hao kwa kisingizio cha kuonana na Tajiri Khalifa ilikuwa ni mbinu tu, lakini vipi kuhusu hio pete.
SEHEMU YA 491.
ROME – ITALY- Miezi miwili iliopita.
Ni miezi miwili iliopita mashariki mwa jiji la Rome katika moja ya jengo la makumbusho ya kitaifa usiku wa saa mbili na nusu kwenda tatu kulikuwa na kikao cha watu wazito.
Ni watu wazito haswa kutokana na itifaki za ki usalama ambazo zilikuwa zimekwisha kuchukuliwa , jengo hilo lilikuwa kikitumika kama la makumbusho na mara nyingi muda wote linakuwa wazi mpaka saa nne za usiku kuruhusu watu , lakini siku hio jengo hilo lenye muundo wa kikale lilifungwa kwanzia muda wa saa kumi za jioni.
Ilikuwa ni sehemu sahihi sana kwa kufanyia mikutano ya siri kutokana na muundo wa jengo lenyewe lakini kitu kingine barabara ya kuingia ndani ya hili jengo haikuwa na pilikapilika nyingi kama barabara za katikati ya jiji.
Sasa usiku ndani ya vyumba vya Ardhi ndani ya jengo hili kulikuwa na kikao ambacho hakikujumuisha watu wengi sana , jumla ya watu waliokuwa wakifanya kikao walikuwa ni wanne tu, watatu wote walikuwa wamevalia suruali nyeusi na mashati ya rangi ya bluu iliokolea na kuvaa na Collar ambazo kwa harakaraka ziliwatambulisha kama wachungaji.
Mtu mmoja pekee ndio ambaye alivalia suti pamoja na tai , mwanga wa hapo ndani haukuwa mkali sana kutokana na taa zake za rangi ya njano zilizokuwa zikiendana na muundoo wa chumba.
“Barrack nadhani unaelewa sipendezwi na vikao vya dharula”Aliongea mzungu mmoja ambaye umri wake kwa haraka haraka ni kama miaka sabini hivi.
“Andre siwezi kusahau jambo muhimu kama hilo , lakini leo tulipaswa kuonana kwa dharula na nimefarijika mmeweza kutii wito kwa haraka”Aliongea yule mwanaume ambaye amevalia suti na tai akiwaangalia wale wenzake ambao walionyesha kuwa ni wachungaji au mapadri..
“Nini kimetokea?”
“Ni kuhusu Chriss mkutubi wetu ambae alienda Tanzania kwa maagizo yetu”Aliongea na kuwafanya wale wachungaji kuangaliana lakini mwanaume alieitwa kwa jina la Andre alionyesha utofauti.
“Nini kimetokea kuhusu Chriss , makubaliano yetu ajiingize ndani ya jumuia ya Ant Illuminat ili kupata kujua kila kitu kinachoendelea”
“Pastor Michal hiko ndio ambacho kimenifanya kuitisha hiki kikao cha dharula , taarifa zilizonifikia mpaka sasa Chriss amefaiki”Aiongea mwanaume aliefahamika kwa jina la Barrack na kimya kilitawala.
“Nini kimetokea? Je amegundulika ni shushu wetu?”
“Hilo haliwezekani ndio maana nahitaji kusikia kutoka kwenu wote,sisi wanne ndio tunajua kuhusu Chriss na Pastor Andre ulihusika kumbadilisha Chriss na kuwa double agent kazi ambayo ilichukuwa muda mrefu na hata aliporudi kuwa chini yangu ulinihakikishia ni Asset ya faida kwetu na ndio maana nilimsamehe na kumpa nafasi nyingine”
“Mr Barrack tunataka kusikia nini kimepelekea kifo cha Chriss?”Aliongea mchungaji michael.
“Taarifa nilizopata inaonyesha alienda kinyume na misheni aliopewa na Hades wa zamanni ndani ya Ant illuminat na akamshambulia Edna Adebayo mke wa Hades”Aliongea na kufanya wote kumaka lakini Andre muonekano wake haukutafsirika na Barrack aligundua hilo.
“Andre mbona unaonekana kutoshangaa?”
“Chriss alipaswa kunitafuta mara baada ya misheni”Aliongea Andr.
“Unamaanisha nini Andre”
“Ni mimi niliewasiliana nae dakika za mwisho kabisa na kumwambia misheni imebadilika”
“Kwanini?”
“Wameniambia kama hatuwezi kubadili unabii tunaweza kubadili matokeo”Aliongea na kuwafanya wenzake wote kushindwa kumuelewa.
“Nilipokea ujumbe kutoka kwa baraza la 33rd degree ya kumbadilishia Chriss misheni yake na wakati nawasiliana nae aliniambia ashafika eneo la tukio na muda si mrefu angekutana na Edna Adebayo”
“Mbona mimi ndio niliwasiliana nae na kumbadilishia misheni siku moja kabla nini kinaendelea?”Aliwaza ndugu Barrack.
“Andre ni watu gani hao?”
“Prior of sion, wanajua kila kitu ambacho tunakifanya na mipango yetu na hata kifo cha Chriss waliniambia wao wenyewe muhusika mkuu ni Minerva”
“Athena ndio aliemuua Chriss?”Aliuliza Barrack huku akionyesha wasiwasi.
“Hivyo ndio walivyoniambia”
“Papa Andre , ulishawahi kunihadithia umekutana na Athena ana kwa ana nadhani huu ndio muda wa kutuambia anafanana vipi? Je ni kweli Clelia Allisanto ndio yeye?”Aliuliza kwa kutanguliza jina la Pope Mwanzoni.
“Clellia Alisanto katibu wa umoja wa mataifa sio Minerva bali Athena anatumia Clone nina uhakika na hilo”
“I knew it”Aliongea akimaanisha kwamba alijua tu.
Naam mwanaume anaefahamika kwa jina la Barrack ni raisi mstaafu waMarekani na Andre ni Pope , wawili ni Michale ambaye cheo chake haikuwa wazi na pia John cheo chake haikuwa waz.
*********
MASAA KADHAA NYUMA
Ni muda wa saa sita usiku mara baada ya Roma kuondoka nyumbanni na kwenda kuzamia nyumbani kwa Nasra kwa kupitia balkoni, muda huo huo katika chumba chake alionekana mtu mwingine akiibukia na kuanza kuangalia mazingira ya hapo ndani na mara baada ya kuridhika aliingia kwenye chumba anacholala Roma na kuwasha taa na baada ya kuona kitanda hakina mtu alitabasamu kwa kebehi.
“Kulikuwa na haja gani ya kufanya sherehe kubwa na kutuharibia maua kama unakuja kulala mwenyewe”Aliongea kwa lugha ya chini huku akigeuka nyuma.
Alikuwa ni Hermes au Prince Raphaeli ambaye mwezi mmoja nyuma alimuokoa Denisi kwa kumdhibiti Roma kupitia ndoto.
Baada ya kukagua chumba cha Roma kwa dakika kadhaa alitoka kwenye chumba hiko na kuingia kwenye korido na ndani ya dakika chache tu aliibukia kwenye chumba cha Edna.
Baada ya kuingia ndani ya chumba hicho hakuacha kuangalia mandhari ya chumba kizima na kisha akahamia kwenye kitanda na kumwangalia Edna na Lanlan ambao wamelala fofo,
“Hades unaishi na mtoto wako lakini mpaka muda huu umeshindwa kumfahamu, aliesema huna akili kweli kapatia”Alijiwazia huku akimwangalia Lanlan aliemuwekea Edna mguu kwenye shingo.
“Athena sijui ananitakia nini , Hades akiniona namwangalia mke wake namna hii lazima ataniua, inabidi nifanye haraka kilichonileta na kuondoka”Alijiwazia mwenyewe na kisha akanyanyuma mkono wake na kumnyooshea Edna kama vile anamwombea na muda uleule Edna alianza kutingisha kichwa kama vile mtu ambaye yupo ndotoni na Hermes alidumu vilevile kwa dakika kama tano na kisha akaonyesha kuridhika na akageuza macho kwa Lanlan na kumnyooshea mkono kama alivyofanya kwa Edna na Lanlan alianza kutafuna tafuna kwa kasi kama vile kuna kitu analishwa na Hermes alitabasamu na kisha akaondoa mkonno wake.
“Persephone , kwanzia kesho utafanya mambo yako yote bila kujielewa chini ya udhibiti wangu ukiwa ndotoni”Aliongea huku akimwangalia Edna kwa dakika na kisha akafungua mlango wa kutokezea kwenye balkoni na palepale alipotea kufumba na kufumbua.
*********
“Madam Persephone tusamehe kwa kukufanyia hii surprise , yote yamefanyika kwa kuzingatia itifaki za kiusalama wa kuficha kile ambacho kinakwenda kuzungumziwa hapa ndani, nadhani upo kwenye mshituko lakini kabla ya kuendelea na hatua ya pili tutaomba utoe wasiwasi kabisa na kama kila kitu kikienda sawa huenda sisi wote tukawa chini yako”Aliongea Shekh Assad na Edna alishindwa kujibu chochote na alishangaa pia uwepo wa Nadia Alfonso.
“Kwa majina yangu naitwa Ally Assad na ndio msemaji mkuu wa hili jopo lote la watu waliopo mbele yako na Kabla ya kujitambulisha kwako mmoja mmoja na kukuelezea dhumuni la uwepo wetu hapa ndani tunataka ututhibitishie kwa kutuonyesha pete ya muhuri unaokutambulisha kama kiongozi wetu”Aliongea.
“Shekhe Ally Assad unaweza kuketi”Aliongea Edna bila wasiwasi na Shekh Assad alikaa chini na watu wote walimwangalia Edna kwa shauku ya kile ambacho anakwenda kufanya.
Edna hakuonekana kuongea chochote zaidi ya kuchukua mkoba wake na kutoa kijiboksi kidogo cha rangi nyeusi , ni viboksi flani kama vile vya kuwekea pete au mkufu.
Kitendo kile cha kushikiria kile kiboksi kabla hata ya kukifungua kiliwafanya watu wote hapo ndani kuwa na mchecheto wa aina yake.
“Kwasababu wote mmekuja kukutana na mimi leo hii , basi sina budi kuwadhirihirishia kwenu muhuri ambao unanitambulisha kama kiongozi wenu”Aiongea Edna akiwa kama sio yeye vile na kisha akafungua kile kiboksi na ndani yake ilionekana pete ambayo kwa kuiangalia tu haikuwa ya kawaida, ilikuwa na mchoro juu yake ulionakshiwa kwa madini ya shaba , mchoro ulikuwa kama vile ni tunda ambalo limekatwa kwa mshazari katikati sasa ule muonnekano wake wa ndani ndio ulifanana na hio pete.
Edna aliitoa na kuishikilia mkononi na kisha kwa mbwembwe zote aliingiza kidoleni katika mkono wake wa kulia na akaunyoosha juu ule mkono kuelekezea ule upande wa pete kuonekana kwa watu waliokaribu.
“Shekh Ally Assad hii ni Signet ring inatumika kama muhuri na ni kwa muda mrefu haijatumika , unaweza kuiangalia kwa ukaribu kuona kama mchoro wake unafanana na muhuri unaonitambulisha kama kiongozi wenu”Aliongea Edna na Shekhe Ally Assad aliangalia kwa umakini ile pete na alijikuta akipatwa na mshangao usiokuwa wa kawaida na palepale aliwageukia wenzake wote na kuwapa ishara ya kuashiria ndio muhuri wenyewe na wote kwa pamoja walisimamaa na kuinamisha vichwa chini kwa mara nyingine.
“Karibu sana Malkia wetu Persephone”Waliongea kwa mara nyingine baada ya kusimama na Edna alinyoosha mkono juu kuwazuia na akawaambia waketi chini na walitiii.
Suzzane na Nadia walikuwa na mshangao kwani hawakutegemea kutokutana na upinzani kutoka kwa Edna , lakini alionyesha kana kwamba watu waliopo mbele yake anawafahamu mbaya zaidi aliongea kimadaraka.
“Leo nimejitambulisha kwenu kikalenda , lakini muda wangu wa kuwaongoza bado , mpaka muda utakapokuwa sahihi nitawatafuta, kwasasa Shekh Assad ataendelea kuongoza jumuia yetu kwa niaba yangu na malengo yote yanapaswa kutimia kabla ya siku ya kurudi kwangu”Aliongea na kuwafanya kuonyesha sura za kutoelewa maana ya maneno.
*********
Blandna alijikuta akishangaa mara baada ya kuambiwa na raisi Senga kuhusu Roma kile alichomfanyia Desmond mtoto wa raisi Jeremy, hakujua jambo hilo kama limetokea kwani Roma na Edna hawakumwambia.
Usiku wa juzi walivyorudi alijua kabisa kuna jambo ambalo limetokea lakini hakuhoji sana kwani Roma alimwambia hakukuwa na tatizo na ni sherehe tu ambayo haikuwa nzuri.
Na yeye alipotezea baada ya kuwaona Edna na Roma asubuhi walikuwa wamepatana na ile hali ya kununiana ilikuwa imeisha na ndio maana hakuhoji sana.
“Kwahio hiki ndio ambacho ulitaka kuongea na mimi?”Aliuliza Blandina
“Kuna lingine ambalo ulitarajia kusikia kutoka kwangu , nimekuita hapa kukuambia kile alichokifanya mtoto wako ili umuonye kwani akiendelea kuchafua amani ya nchi yangu nitamchukulia hatua”Aliongea na kumfanya Blandina kumwangalia Senga kwa huzuni.
“Kwanini unamwita mtoto wangu peke yangu Senga , Wewe sio mtoto wako? Au ni kwasababu amebadilisha jina na kuitwa Roma ndio kinachokupa shida ya kumtambua, Senga najua huwezi kunisamehe lakini Roma bado ataendelea kuwa mtoto wako”
“Kimya!!!, wewe na Roma kwangu mlishakufa na ndege na sitaki kuhusika na maisha yenu , ninachotaka kutoka kwako ni kumuonya Roma aache kuharibu diplomasia ya nchi”
“Senga tangu lini ukawa mnafiki wa hisia zako mwenyewe?”
“Unamaanisha nini?”Aliongea Raisi Senga huku awamu hii akionyesha kakarisika maradufu.
“Maneno yako yapo tofauti na hisia zako Senga, unafikiria sijui kinachoendelea kwenye moyo wako , ulifikiri nitashindwa kujua kile unachojisikia , sijakusahau Senga”
“Kimyya , Blandina naomba usinikasirishe zaidi kukaa na mimi chumba kimoja usijipe ujasiri wa kuongea unavyojisikia , wakati ule ulishapita na sasa nimekuwa raisi kwa juhudu zangu wakati wewe ukijificha”
“Kinachokusumbua Senga ni kwasababu Roma ana nguvu zaidi kuliko wewe , uwezo wake na nguvu zake zinakufanya ujihisi huwezi kuwa baba mbele yake, Senga acha kuishi kwa mateso unapaswa kuachilia baadhi ya mambo megine yasahaulike kwenye moyo wako”
“Kuna vitu naweza kusahau , lakini siwezi kumsahau mwanamke alienisaliti”Aliongea na kumfanhya Blandina kuanza kutokwa na machozi.
Muda huo maongezi yao walikuwa wakiyafanyia ndani ya chumba cha hoteli hivyo ilikuwa ngumu kwa mtu wa nje kujua kile ambacho kinaongelewa na ilikuwa mara ya kwanza kwa Senga na Blandina kukutana wakiwa peke yao tokea arudi Tanzania na huenda ni mwanzo mzuri wa mapatano.
“Najua Senga huwezi kusahau na huwezi kunisamehe lakini upendo wangu kwako hakuwahi kupotea kwa miaka yote ambayo hukuweza kufahamu nipo hai”
“Blandina acha kuwa mnafiki mbele yangu utanikasirisha , nimekuja hapa kukuonya kuhusu Roma kuingilia amani ya taifa”
“Una uhakika ndio kitu pekee ambacho ulitaka kuniambia mpaka kutaka kuongea na mimi kwa kujificha ficha?”Aliuliza na kumfanya Senga amwangalie Blandina huku akikosa neno la kuongea.
Alichoongea Blandina ni ukweli mtupu, kama kweli alitaka kumuonya tu kuhusu Roma haikuwa na haja ya kumuita hotelini kwenye chumba cha Presidontial Suite tena kwa siri.
Blandina alimwangalia kwa muda namna ambavyo amekosa neno la kuongea na kisha akaangalia mkoba wake na akauchukua.
“Kwa mra ya kwanza nimefurahi kukuona kwa ukaribu Senga, nitamwonya Roma kutokuingilia uongozi wako”Aliongea na kisha alisogelea mlango akitaka kutoka.
“Subiri..!!!”Aliongea na kumfanya Blandina kusimama na kugeuka na Senga aliingiza mkono kwenye mfuko wa koti na ilionekana kuna kitu anatoa.
SEHEMU YA 492
Roma hakujua kinachoendelea kabisa na baada ya kutoka kwa Afande Kweka hakupitia nyumbani kabisa , akili yake ilimwambia aende kuonana na Rufi kwanza kuongea nae kuhusu kanuni aliopewa na Zenzhei ya kutengeneza vidonge vya nguvu za kijini , alikuwa na muwashawasha wa kufahamu kama Rufi angeweza kuelewa kanuni zote.
Dakika chache mbele mara baada ya kuendesha gari aliweza kufunga breki chini ya jengo la apartment anapoishi Rufi na alitoka kwenye gari na kuzisogelea lift.
Baadaya kuingia kwenye lift na kubonyeza kitufe cha floor husika simu yake ilitoa mtetemo wa ujumbe wa meseji ulioingia ,alifungua na kuona ni ujumbe ulitoka kwa Xiao Xiao na aliupotezea palepal.
Ilikuwa ni siku zaidi ya mbili msichana huyo wa kichina hakukata tamaa kutuma jumbe za kumsalimia Roma na nyingine za kuchombeza lakini Roma hakujibu hata moja , hakutaka matatizo na mke wake lakini pia alijua akiwa na ukaribu na msichana huyo itakuwa rahisi kwa Rufi uwepo wake hapa Tanzania kufahamika kwa wepesi , hivyo alijiambia anapaswa kumuepuka kwa nguvu zote.
Baada ya kutoka kwenye lift alibonyeza kengere na mlango kwa ndani ulifunguliwa na Rufi ambaye amevalia tisheti ya jezi ya Man U huku mkononi akiwa ameshikilia juisi ya matunda.Alitabasamu na kumpa ishara ya kuingia na Roma alifanya hivyo.
“Inaonekana unapenda sana mambo ya kompyuta , kwa mwonekano wako ulipaswa kujifunza vitu vilaini vilaini visivyotumia akili nyingi”Aliongea Roma mara baada ya kuona tarakishi ikionyesha namba namba ambazo hata hakuelewa.
“Kompyuta naipenda kwasababu nahisi kama dunia yote naiona , nimejifunza mambo mengi sana na kwasasa najaribu kutafuta Proffesional Hacjer anielekeze baadhi ya mambo madogo madogo”
“Kwahio unataka kuwa mdukuzi , haupendezi kabisa kwa fani hio?””
“Kipi kinanipendeza? Au kutapeli watu ndio kazi nzuri inayonifaaa?”Aliongea na Roma hakumjibu na aliishia kumwangalia tu kuona kama ana shida yoyote kwani tokea amuache mara ya mwisho hakuwasiliana nae kabisa na kumpa habari za Xiao Xiao msichana wa kichina aliemkimbia.
“Unaendelejeaje, ulitoka kweli humu na kwenda kutembea?”
“Naogopa hata kwenda Supermarket na hofia naweza kukutana nae tena” Aliongea huku akijibwaga kwenye sofa kivivu na kumfanya Roma amuonee huruma.
“Unapaswa kutoka bila ya kuhofia chochote hakuna mtu yoyote wa kuja Tanzania na kukufosi urudi ilihali mimi nipo”.
“Ah .. najua unaweza kunilinda lakini hawatoacha kuja mara kwa mara lazima watalazimisha nirudi sitaki kukuongezea zaidi matatizo”
“Nishakuambia usiwe na wasiwasi juu ya hilo nimefuatilia taarifa za msichana uliekuwa unamkimbia yupo Tanzania kikazi”
“Kweli?”
“Unafikiri nakudanganya? , umeacha lini kutokuniamini?”Aliongea Roma na kumfanya Rufi kutabasamu na kushindwa kuongea chochote na Roma aliona apotezee mada hio na kwenda moja kwa moja kwa kile kilichomleta.
“Nimekuja kukuuliza namna ya kutengeneza vidonge”
“Unataka kutengeneza vidonge!?”
“Kwanini unaonyesha kushangaa ,ushasema mwenyewe vidonge ni muhimu katika kusaidia kupanda levo naweza nisihitaji mimi lakini warembo wangu nataka niwapatie ili viwasaidie”
“Ndio vidonge ni muhimu sana kwa wanaoanza mafunzo , lakini kuna mahitaji yake na kanuni za kutengeneza”
“Ndio maana nimekuja kwako nataka kujua hayo mahitaji”Aliongea Roma na kumfanya Rufi kufikiria kidogo.
“Kama kweli una nia ya kutengeneza vidonge. kuna changamoto tatu ambazo unapaswa kuzivuka , Changamoto ya kwanza lazima upate mimea ambayo hutumika kutengenezea, hii sio rahisi kwasababu mimea hio ni adimu sana kupatikana na hata ile ambayo inatengeneza vidonge vya thamani kubwa imepotea kabisa, katika miliki za kijini kwenyewe huwezi kuipata hio mimea na ndio maana licha ya uwepo wa wenye ujuzi mkubwa wa kutengeneza wameishia kutengeneza vidonge vya kawaida tu”
“Lakini umesema kuna wanaokuja huku duniani kutafuta hio mimea ?”
“Ndio kuna wanaosafiri mpaka duniani kwa ajili ya kutafuta mimea ya kutengenezea vidonge lakini mara nyingi huishia maeneo ya karibu na bara la Asia , kwani wengi wao wanasema wanaogopa kuvunja sheria za the gods treaty”
“Kama ni hivyo basi uwezekano wa kupata hio mimea upo ,ninachotakiwa kufanya ni kutuma watu wangu wajaribu kufatilia, je ni wapi ambapo unaamini mimea hio inawezekana kupatikana?”
“Sina uhakika ila marra nyingi ni sehemu ambazo ustaarabu wa kale ulianzia kama vile Misri na maeneo mengine kama hayo”Aliongea na kumfanya Roma kutingisha kichwa kumuelewa.
“Vipi kuhusu changamoto inayofuatia?”
“That is even harder , You would need a high Quality Cauldron”Aliongea akimaanisha kwamba changamoto ya pili ni ngumu zaidi kwasababu atahitajika kuwa na Cauldron.
“Cauldron?”Roma aliuliza.
“Ndio Cauldron ni Dhana ambayo ipo mfano wa chungu kikubwa ambacho kimetengenezwa kwa madini maalumu ambayo yalipatikana enzi za kale,ni madini ambayo yana uwezo wa kuhimili kiwango kikubwa cha joto , kwa uelewa wangu katika miliki za kijini vipo vitano tu hivyo vyungu , Kekexil wanavyo vitatu ,ukoo wa wakwe zangu wanacho kimoja na Hongmeng wenyewe wanacho kimoja , kama kuna jamii nyingine ambazo wana aina hio ya chungu kinaweza kuwa nje ya matumizi hivyo haitokuwa rahisi”
“Changamoto ya tatu ni kuweza kudhibiti moto wa njano na mweupe ambao ndio hutumika kutengenezea hivyo vidonge kwa joto kubwa sana zaidi ya joto la kuyeyushia chuma na kubalansi na Chungu hiko”Chungu kinachozungumziwa hapo ni cha kijini ambacho ni kama Cauldron
“Changamoto ya tatu ya kudhibiti moto wa rangi ya njano na mweupe sio tatizo”
“Unamaanisha unao uwezo huo?”aliuliza huku akionyesha mshangao na Roma alitingisha kichwa.
“Kwanini hujazungumzia kuhusu andiko la kanuni za kutengenezea hizo dwa?”Aliuliza Roma akimaanisha andiko la kanuni alilopatiwa na Zenzhei.
“Kila koo ina kanuni zake , lakini ilisemekana mwanzoni Hongmeng walikuwa na andiko la kanuni ambayo hutengeneza vidonge vyenye uwezo mkubwa sana ,lakini bahati mbaya andiko hilo lilipotea, ndio ninachojua japo sina uhakika,lakini hilo lisikupe shida haina haja ya kuwa na hizo kanuni kikubwa ni namna ya kudhibiti joto la moto wa kichawi mweupe na wa njano ukishafanikisha kupata hiko Chungu”Aliongea
“Nitakuwa naendelea kuvuna nishati huku nikisubiria watu wangu waweze kutafuta hayo maeneo uliozungumzia , unaonaje kama wakifanikisha unisindikize”
“Mimi? , unamaanisha twende pamoja?”
“Ndio ,najua itakuwa usumbufu lakini siwezi kujua mimea inayohitajika nikienda mwenyewe”
“Lakini inawezekana ikawa ni mbali na Tanzani misituni huko”
“Usiwe na wasiwasi nishaishi sana msituni hivyo nina uzoefu wa kutosha”Aliongea Roma.
“Mimi sina tatizo lakini vipi mkeo anaweza akakasirika?”Aliongea kwa sauti ndogo huku akiona aibu.
Na kabla Roma hajajibu simu yake ilianza kuita na aliitoa na kuangalia mtu anaempigia na alishangaa ni Bi Wema , alipokea harakaharaka na kuweka sikioni.
“Mr Roma nadhani Miss Edna kapatwa na tatizo”
“Unamaanisha nini kapatwa na tatizo Bi Wema , nini kimetokea?”
“Amerudi kutoka kazini saa kumi kamili za jioni na akasema ana usingizi , amelala mpaka muda huu na nimejaribu kumuamsha haamki , Lanlan na yeye amejaribu kumuamsha kwa nguvu lakini hajashituka”Aliongea Bi Wema huku sauti yake ikionyesha wasiwasi na kumfanya Roma kuguna.
“Ana pumua?”
“Ndio kifua kinapanda na kushuka ndio hivyo haamki , nadhani ni vyema ukarudi umuangalie nina wasiwasi kwani sio kawaida mtu kulala na kushindwa kuamka”Aliongea Bi Wema na kumfanya Roma apumue kidogo kwa ahueni.
“Nakuja sasa hivi Bi Wema”Aliongea Roma na kisha akata simu.
“Nadhani mke wangu kapatwa na tatizo , ngoja niwahi”Aliongea Roma na Rufi alitingisha kichwa .
******
Afande CammiliusKweka alionekana kuathirika sana na taarifa ya Zenzhei kutaka kurudi Hongmeng , alijitahidi kuonyesha kuwa sawa lakini ukweli alikuwa akiumia kiume lakini hakuwa na uwezo wowote wa kumzuia kutoondoka kwani asingeweza kumlinda zidi ya Hongmeng.
“Zenzhei niseme asante sana’Aliongea Afande Kweka kwa sauti hafifu na muda huo ni kama masaa mawili mara baada ya Roma kuondoka.
“Camillius kwanini unanishukuru?”
“Asante sana kwa kwa kujjifanya kuwa mzee mbele ya macho ya watu ili mradi unilinde bila watu kukushitukia , asante kwa kufanya kazi za hapa kama vile ni mfanyakazi wa ndani , asante sana kwa kumfanya mke wangu kipindi kile kufa kifo cha amani”Aliongea Afande Kweka huku macho yakiwa makundu na hata Zenzhei mwenyewe alishindwa kujizuia na kudondosha chozi.
“Hupaswi kusema hivyo Cammilius ulikuwa ni wajibu wangu”
“Hapana, nimekukatili sana kwa kipindi chote ulichokuwa na mimi lakini bado nikakosa aibu na kuwa mbinafsi na kukufanya uendelee kuwa karibu yangu”
“Camillius usiongee hivyo nilikuwa na furaha kuishi na wewe”
“Zenzhei matumaini yangu ni kwamba hutonichukia , najua kwanini ulikaa na mimi kwa miaka mingi sana lakini nilishindwa kufanya chochote juu ya hisia zako kutokana na kukosa ujasiri , nilishindwa kuzipokea na mpaka sasa nashindwa kuzipokea licha ya uzee huu”Aliongea afande Kweka na kumfanya Zenzhei kufumba macho yake huku machozi yakimtoka.
Ni kweli alikuwa akimpenda Afande Camillius Kweka tokea mara ya kwanza walipokutana , lakini licha ya kuonyesha hisia zake kwa mzee huyo hakuchukua hatua yoyote na yeye kukosa ujasiri wa kuchukua hatua zaidi.
“Camilius kabla sijaondoka nitarudi kwenye mwonekano wangu wa mwanzo wakati tunakutana nadhani itakufanya usijione mwenye hatia” Aliongea Zenzhei na palepale mwili wake ulibadilika taratibu ,ilikuwa ikishangaza mno kwani ndani ya nusu dakika alibadilila na kuwa msichana kama wa miaka ishirini na nne mwanamwali , ilikuwa ni sahihi kusema alikuwa akifanana kabisa na Xiao Xiao japo yeye kidogo alikuwa na umbo la kuvutia na huenda angekutana na Roma angefanya jambo la kueleweka.
Ilionekana ili kuishi na Afande Kweka ilibidi ajizeeshe ili kuficha ujini wake , kwani kama asingefanya hivyo angebakia kuwa msichana mdogo ilihali Afande Kweka alikuwa anazeeka.
“Nakumbuka mara ya kwanza tulipokutana Sudani ulikuwa na miaka hamsini Camilius”Aliongea Zenzhei na sio sura tu iliobadilika hata sauti yake pia ilikuwa imebadilika.
“Haha.. bado urembo wako uko vilevile hakujabadilika chochote”Aliongea huku akitoa kicheko chenye machungu na kumfanya Zenzhei kutabasamu akikosa neno.
“Nadhani hii ni kwaheri ya moja kwa moja, naamini siku ukirudi nitakuwa tayari nimeshakufa”aliendelea kuongea na kumfanya Zenzhei kuingiwa na huzuni.
“Kwaheri ya kuonana Camilius” Aliongea Zenzhei.
“Kwaheri ya kuonana Zenzhei hakikisha unakuwa na maisha ya furaha na kutafuta mtu anaekupenda”
“Asante sana Camilius”Aliongea na kisha wakaangaliana usoni kwa madaki kakadhaa na Zenzhei alikosa ujasiri wa kuendelea kusimama mbele ya Camilius na palepale alipotea kwenye macho yake.Na hio ndio safari ya Zenzhei kurudi ujinini ikaanza rasmi.
Baada ya kufunguliwa mlango na mhudumu mwenye asili ya kiarabu alievalia suti , Edna alishangazwa kukuta sio mtu anaekutana nae bali ni jopo la watu kama ishirini waliojipanga kwenye meza na ajabu ni kwamba mara baada tu ya kuingia wote walisimama kiheshima , kati ya sura alizozifahamu ni moja tu ambaye ni Nadia Alfonso mwanasheria wake.
Edna na Suzzane walihisi wamekosea chumba walichopaswa kuingia na Edna alitoa ishara ya kuomba msamaha kwa kuingilia kikao.
“Karibu sana Madam Persephone” Waliongea wote kwa pamoja kwa lugha ya kingereza na kisha waliinamisha vichwa kuonyesha ishara ya heshima jambo ambalo lilimpagawisha Edna na moyo wake kupiga kwa nguvu , alijihisi ni kama anaota na akishituka ingekuwa ndoto.
Kwa mara ya kwanza alihisi jina la Madam Persephone ambalo alilikuwa akiitwa mara kwa mara bila ya kujua sababu yake alihisi sio la kwake , ule ujasiri aliokuwa nao kwa muda huo ulimpotea na aliishia kuduwaa.
Suzzane pia alikuwa kwenye mshangao asijue nini kinatokea mbele ya macho yake , walikuja hapo kwa minajili ya kukutana na Tajiri Khalifa kutoka Dubai , mtu ambaye alichangia kiasi kikubwa cha pesa katika taasisi ya Edna Foundation na uwepo wao hapo ni kutii wito wa kuonana na tajiri huyo , lakini mambo yanaonyesha kuwa tofauti.
Licha ya kwamba alihisi yupo ndotoni lakini ulikuwa uhalisia na jinsi watu waliokuwa mbele yake walivyokuwa wakimwangalia alijua kabisa walimlenga yeye na ndio ambaye alikuwa akisubiriwa, lakini bado alijiuliza kwanini yeye na ni maigizo gani yanafanyika.
Kwanza chumba kilionekana kilikuwa cha mikutano ndani ya hoteli hii ya Peacock, pili mpangilio wa hapo ndani ulikuwa ni wa kikao muhimu kutokana na watu waliokuwepo , ilikuwa ni meza ndefu ambayo inajumla ya watu kumi kila upande kukamilisha watu ishirini na ni kiti kimoja tu ambacho kilikuwa wazi , kiti cha katikati ambacho huruhusu mkaliaji kuona nyuso za kila mtu aliekuwa mbele yake , ni rahisi kusema ndio kiti cha mwenyekiti kama ni kikao ambacho kinatarajiwa kufanyika.
Watu waliofahamika ambao wapo ni Shekhe Assad , Tajiri Khalifa , Mellisa Luiz , Pastor Cohen , Nadia Alfonso , Zoe Kovacic , Phill Knight na wengine wengi ambao ilionyesha ni wanachama wa Ant- illuminat.
Mwanadada mmoja aliekuwa wa kifilipino , alievalia suti alimsogelea Edna na kuinamisha kichwa mbele yake kwa namna ya heshima na kisha akavuta kiti kilichokuwa wazi na kumuonyesha ishara ya kukaa.
Edna bado aikuwa kwenye mshangao na alishindwa kujua achukue maamuzi , ya kuondoka au abaki na hata aliponyeshwa kiti cha kukaa bado hakupiga hatua kukisogelea maana alijua kukaa kwenye kile kiti ni kama yeye ndio anakwenda kuongoza kile ambacho kingekwenda kuendelea hapo ndani , kitu ambacho hata hakijui ni nini.
“Madam!!!” Suzzane alimshitua Edna ambaye bado alishindwa kufanya chochote licha ya kuonyeshwa kiti cha kukaa.
Edna aliinua uso wake na kuanza kuangalia kila mmoja ambaye yupo ndani ya hiko chumba, kuna wengine alikuwa akiwafahamu na kuna wengine hakuwahi kuwaona popote.
Lakini ghafla tu Edna alitoa tabasamu hafifu kama vile anavyofanyaga akiwa kwenye kampuni yake akiwa na kikao na wafanyakazi wake na alisogelea kile kiti na kuketi na kuwaangalia watu wote waliokuwa hapo ndani kama vile alikuwa akiwajua.
Ni kintendo ambacho hakikumshangaza Suzzane tu lakini kila mmoja kilimuacha na maswali lakini sio hivyo tu pia kiliwafanya kuwa na tumaini.
**********
Roma baada ya kuambiwa na Afande Kweka kwenda kuonana na Zenzhei , hakutaka kuchelewa sana , alikuwa na shauku ya kujua kwanini Zenzhei anataka kurudi Hongmeng baada ya kuishi Tanzania kwa muda mrefu.
Alitaka pia kujua ni jambo gani ambalo Zenzhei alitaka kumwambia , alikuwa na shauku kubwa kutokana na kwamba alikuwa na mpango wa kuivamia Hongmeng siku moja hususani muda huo ambayo alijua kabisa yeye ni adui na jamii hiyo , hivyo alitaka kukusanya kila taarifa iliokuwa ikihusiana na jamii hizo ili kumsaidia huko mbeleni.
Roma alimuaga sekretari wake kwamba anatoka na anagerudi siku iliokuwa inafuata , Tanya alishangaa kutokana na kwamba kuna baadhi ya maamjuzi yalikuwa yakimpasa kuyashughulikia siku hio hio lakini alikosa ujasiri wa kumzuia Master wake.
Ni zaidi ya miezi sasa tokea Tanya achukue majukumu ya Amina kama Secretari na alionekana ashanza kuipenda kazi yake na kuizoea na alikuwa ni msaada mkubwa kwa Roma kwani mambo mengi aliyafanyia kazi.
Muonekano wake ulikuwa umebadilika kwa asilimia mia moja na ilikuwa ngumu kujua ndio anaehusika kuongoza kundi la Yamata kutoka Japani ambalo linamilikiwa na Roma.
Roma alitumia muda machache sana kufika nyumbani kwa babu yake na baada ya kusalimiana na Afande Mstaafu Camilius Kweka ilisalimiana na Zenzhei pia wote walikuwa wamekaa nje kwenye bwawa la kuogelea na ilionekana walikuwa wakiongea.
“Nitawaacha muongee”.
“Camilius haina haja ya kuondoka , ninachoongea na Mr Roma sio kipya kwako”
“Hapana umesubiria muda mrefu na huu ni muda wako, Wewe mtukutu ukimaliza unione kwanza kabla ya kuondoka”Aliongea Afande Kweka na kisha aliondoka eneo hilo.
“Mr Roma samahani kama nimekuchukulia muda wako , muda huu ulipaswa kua kazini”
“Usijali kuhusu hilo , nilipaswa kuja hata jioni lakini kwasababu sikuwa na kitu cha kufanya kazini nimeona nije mapema”Aliongea Romana kumfanya Zenzhei kutingisha kichwa kumuelewa.
Na muda huo mfanyakazi aliwaletea Juisi ya matunda na kuweka mbele yao na kisha akaondoka.
“Mr Roma muda wangu wa kukaa kwenye ulimwengu wa kawaida umeisha”
“Nilipoambiwa unaondoka nimeshangaa , kwani ulikuwa na ukomo wa kuishi Duiani?”
“Nadhani ushawahi kisikia sheria za miliki za kijini juu ya binadamu au viumbe wanaojifunza mbinu za kuvuna nishati za mbingu na Ardhi?”
“Najua watu wa jamii kutoka miliki za kijini na binadamu ambao wamefikia katika levo ya Nafsi hawapaswi kuishi kwenye ulimwengu wa kawaida”
“Upo sahihi Mr Roma na mimi muda wangu wa kuishi hapa duniani ushafikia ukomo?”
“Lakini uliishi kwa miaka mingi hapa Tanzania na naamini bado ulikuwa kwenye levo ya Nafsi , kwanini unaondoka sasa?”
“Ni stori ndefu Mr Roma ambayo nataka unipe muda wako nikuelezee ili upate kujua nia ya mimi kutaka haya maongezi na wewe”
“Nipo tayari kukusikiliza”Alijibu Roma kwa msisimko na Zenzhei alianza kumuhadhithia Roma kila kitu kuanzia namna ambavyo Zenzhei na familia yake walivyokimbia katika miliki za kijini na kuja katika ulimwengu wa kawaida , alielezea namna ambavyo baba yake mzazi na mama yake mzazi walivyopambana na wajumbe kutoka Hongmeng mpaka kuwaua , aliendelea kuelezea namna ambavyo baba yake alipambana na mtu asieonekana ambaye ndio aliyakatisha maisha ya wazazi wake mbele yake , namna ambavyo alipona , namna ambavyo alijiunga na kundi la kininja la Yamaguchi kwa ajili ya kulipiza kisasi kwa The Doni.(Rejea episode ya 317).
Roma alishangazwa na stori nzima ya Zenzhei na sasa alielewa uwepo wa Zenzhei kwenye maisha ya Afande Kweka ni kutokana na misheni aliopewa na kundi la Yamaguchi kukaa nae karibu.
Roma alikuwa akielewa kuhusu Yamaguchi lakini kwenye maisha yake hakuwahi kulipa umuhimu kundi hilo na yote hayo ni kwasababu aliyachukulia kama makundi mengine tu ya kininja ambayo yalikuwa yakiua kwa ajili ya pesa ,lakini hakufahamu kuna zaidi ya hayo.
“Kwahio kundi la Yamaguchi hawakuweza kukufahamu kama unatokea Hongmeng?”
“Hawakuweza kunifahamu mpaka baadae sana nilipowakatalia misheni ya kumuua Cammilius”
“Ushawahi pewa mishenni ya kumuua Afande Kweka?”
“Ndio lakini sikutekeleza agizo, Camillius nilifahamiana nae kwa muda mrefu tokea mke wake akiwa hai na amenisaidia kwenye mambo mengi ambayo yalinigusa moja kwa moja na kwangu nilimchukulia kama ndugu,nilipomuelezea ukweli juu ya kwanini nipo kwenye maisha yake hakukasirika na aliniacha nifanye chaguzi mimi mwenyewe kumchagua yeye au kundi na mamuzi nilioyafanya ni kumchangua yeye na ndio nilipokuja kuwa mlinzi wake mpaka leo hii”
“Nikupe pole kwa yaliokukuta , lakini bado sijapata jibu la moja kwa moja umeishi miaka mingi ndani ya Tanzania na Hongmeng hawajakusumbua , kwanini sasa hivi?”Aliuliza Roma , alishangaa kwani ni kweli Zenzhei alikuwa kwenye levo ya Nafsi na kwa sheria za Hongmeng hakutakiwa kuishi kwenye ulimwengu wa kawaida , lakini ajabu ameshaishi miaka mingi sana bila ya kurudishwa.
“Wazee wa Hongmeng hawakufahamu uwepo wangu duniani , walifahamu nimekwisha kufariki miaka mingi iliopita”.
“Lakini mara ya mwisho ulisema ulikuwa na mawasiliano na Hongmeng”
“Ambao wanafahamu uwepo wangu hawakuuweka wazi kwa Wazee wa Hongmeng , ndio maana nikasema Wazee hawakufahamu uwepo wangu duniani”
“Kama ni hivyo naweza kutafsiri ulikuwa na mawasiliano na wajumbe wa Hongmeng pekee na walificha uwepo wako lakini ukawa unaendelea na mawasiliano nao kama ni hivyo naamini kuna sababu wakaamua kuficha uwepo wako”Aliongea Roma.
“Upo sahihi kuna sababu kubwa ya kuficha siri ya uwepo wangu duniani na ni kutokana na ahadi ya faida”
“Ahadi ya faida?”
“Ndio Mr Roma unaweza kusema niliwaahidi kitu chenye faida ili waendelee kunifichia siri ya uwepo wangu hapa Tanzania”
“Kama ni hivyo kwanini sasa hivi wanataka urudi?”
“Kwasababu ahadi sijaitimiza na siwezi kutimiza kutokana na nia yangu ya kulipiza kisasi kwa kile kilichowatokea wazazi wangu, kutokana na kutotimiza ahadi walinitishia mara nyingi kwenda kutoa taarifa kwa Wazee , lakini nilijitahidi kuwa mjanja kwa kuwasubirisha kwa maneno nikisubiria ujio wako”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa ujio wake tena.
“Unamaanisha nini kusubiria ujio wangu?”Aliongea Roma na Zenzhei alitabasamu.
“Kwasababu kuna mtu nilikutana nae miaka iliopita na akaniomba msaada na kisha akaniambia ikiwa ni muda sahihi rudia haya maneno ‘ Damu na Giza ni laana’”Aliongea Zenzei nakumfanya Roma kutoa macho.
“Ulishawahi kukutana na mtangulizi wangu?”Aliuliza Roma akiwa haamini Zenzhei anafahamu hayo maneno kwasababu yalikuwa ni maneno ambayo ni fumbo.
Mara ya mwisho Roma kuongea na Hades wa zamani alimwambia maneno hayo ya fumbo na kumpa maelekezo mtu yoyote ambaye angeyatamka mbele yake anapaswa kumsaidia.
“Mr Roma kukujibu swali , nitasema ndio nilikutana nae mara moja tu na aliniomba msaada wa kumtambua mwalimu”Aliongea na kumfanya Roma kuzidi kujawa na shauku na mshangao kwa wakati mmoja na Zenzhei alijua Roma hakumuelewa hivyo akamwelezea kwa kirefu.
Kwa maelezo ya Zenzhei ni kwamba Hades wa zamani alimuomba msaada wa kumtajia mwalimu ambaye anaweza kufundisha binadamu mbinu za uvunaji wa nishati ya mbingu na ardhi kwa njia ndefu yaani ile ya Maandiko ya urejesho isio na kikomo ambayo ndio hio aliojifunza Roma na mtu ambaye alimtajia ni Tang Chi yaani master wake Roma.
Kwa lugha nyepesi Zenzhei alimpendekeza Tang Chi kwa Hades wa zamanni na Tang Chi akaja kuwa Master wa Roma.
Roma alishangazwa na ufunuo huo wa mambo lakini bado ilimchanganya kwani kwa namna ambavyo alikutana na Tang Chi ilikuwa ni kabla alipokutana na Hades wa zamani , kuna kitu kilimwambia huenda Master Tang Chi aliagizwa na Hades wa zamani kumfundisha yeye mbinu za kuvuna nishati za mbingu na ardhi.
Roma alijikuta akikumbuka namna ambavyo alikutana na Master Tang Chi ilikuwa ngumu sana kuamini alikuwa ameagizwa na mtu.
“Mr Roma najua mtangulizi wako hajakuambia mambo mengi na mimi pia sio jukumu langu kukuambia yale ambayo hajakuambia kwani hata hivyo siyajui , nilimpendekeza Tang Chi kwasababu ndio binadamu pekee ambaye nilimfahamu kwa mara ya kwanza kujifunza tamaduni za jamii zisizoonekana na tokea nilipomsaidia hatukuwahi kuonana tena , lakini aliniambia msaada niliompatia ukizaa matunda basi nitayashuhudia kwa macho yangu na ndio ninapaswa kutamka maneno ya Damu na Giza ni laana”Aliongea Zenzhei na kumfanya Roma kukuna kichwa , ni kweli hakuwa akijua mambo mengi kuhusu Hades wa zamani na ilikuwa sawa kutokumuelewa, kwanza mtu mwenyewe aliishi miaka mingi hivyo huenda alikuwa na mipango mingi, Roma alifikiria na alijikuta akivuta pumzi.
“Kama ni hivyo nadhani unapaswa kuniambia shida yako na mimi nitakusaidia”Aliongea Roma na kumfanya Zenzhei kuvuta pumzi.
“Ninarudi Hongmeng kwasababu nahitajika kurudi , lakini naenda kukusubiria, mpaka sasa Mr Roma umekuwa adui namba moja wa Hongmeng na muda na saa yoyote watatoka huko walipo na kuja kukushambulia kabla ya muda huo kufika unapaswa kuwa wa kwanza kuchukua hatua”
“Unamaanisha niende Hongmeng na kupigana nao?”
“Ndio njia pekeee ya wewe kuwa salama na watu wako unaowapenda , mbinu uliojifunza ni hatari zaidi na hakuna mtu wa hongmeng yoyote ambaye amefanikisha kufikia leo ya Kuzaliwa upya”
“Lakini kama nitakuja kupambana Hongmeng watanizidi kwa uwezo wangu niliokuwa nao huu na isitoshe taarifa zinaonyesha ni wengi ambao wameshavuka levo ya Dhiki”
“Kuhusu uwezo wako sina wasiwasi umeweza kufikia levo ya kuipita Dhiki ndani ya umri mdogo sana hivyo natarajia utaenda juu zaidi ndani ya muda mfupi sana , nimekuambia nimevunja ahadi ndio maana Wazee wakagundua uwepo wangu duniani basi kile nilichoahidi nitakupatia wewe”Aliongea.
“Unamaanisha?”
“Mr Roma haikuwa bahati mbaya familia yangu kushambuliwa ni kwasababu ukoo wetu ulimiliki kitu cha thamani sana ambacho Baba na Mama hawakuwa tayari kukiweka wazi”Aliongea na kisha akampatia Roma karatasi.
“Hio karatasi imejaa taarifa ambayo ndio inanifanya nirudi Hongmeng, ndio urithi wa pekee kutoka kwa familia yangu nilioutunza kwa muda mrefu, nakupatia wewe kwasababu ni mtu sahihi wa kuwa nao”Aliongea na kumfanya Roma aifungue ile karatasi na alijikuta akishangaa baada ya kuona ni kanuni ya utengenezaji wa vidonge vya kusaidia mafunzo ya kuvuna nishati ya mbingu na Ardhi.
“Hii ni kanuni ya kutengenezea vidonge vya Poya?”
“Inaonekana ushalifahamu tayari jina lake , jibu ni ndio kama utaweza kufanikisha kutengeneza hivyo vidonge itakuwa rahisi kwako kupanda levo ya juu zaidi na hakuna kiumbe chochote kutoka Hongmeng kitakuwa tishio kwako”Aliongea na kumfanya Roma macho yake kuchanua kwa furaha na kupitia kwa haraka ile katatasi.
“Kwanini hukutengeneza hivi Vidonge wewe na kukuwezesha kupanda levo za juu zaidi na kulipiza kisasi?”
“Mr Roma nimekupatia kanuni tu , uwezekano wa kukamilisha utengenezwaji wa hivyo vidonge haitokuja kuwa rahisi na haikuwa rahisi wangu pia kutengeneza nikiwa hapa duniani na sitoweza kutengeneza nikiwa Hongmeng wewe pekee ndio naamini unaweza kukamilisha”Katika siku ambayo Roma alipata kitu cha thamani basi ni siku hio, hakuamini Zenzhei alikuwa na material muhimu na hamwambii mpaka wakati anaondoka , huenda angemsaidia hata kutafsiri kanuni hio.
SEHEMU YA 490.
Abu Dhabi- UAE.
Ni baada ya mwezi mmoja tokea waanze uchunguzi wa kile ambacho alifanya Chriss , kitendo cha kutaka kumuua Edna, waliamini kabisa majaribio ya kuuwawa kwa Edna ni nje ya malengo ya jumuia yao hio ya siri na ndio maana walitaka kuufahamu ukweli , kwanini Chriss kafanya maamuzi alioyafanya.
Uchunguzi ulikamilika mara baada ya Nadia Alfonso kumuhoji Roma na kupata majibu ya kile kilichotokea na pia kumuhoji Suzzane kwa kile ambacho kilitokea na baada ya kupata maelezo yao na kuona yanafanana waliendelea na uchunguzi wa kutaka kujua zaidi kuhusu Chriss aliishi wapi mara baada ya kuokolewa na Hades wa zamani gerezani katika mikono ya CIA.
Naam sasa ilikuwa ni siku ya ijumaa mara baada ya swala ya mchana muda wa saa tisa katika moja ya makazi ya Tajiri Khalifa ndani ya Abu Dhabi kulikuwa na kikao cha siri sana ambacho kilikuwa kikiendelea.
Ni kikao ambacho hakikuhusisha watu wengi sana ,waliohudhuria ndio mhimili wa umoja huo wa siri ufahamikao kwa jina la Ant Illuminat.
“Mmefikia katika hitimisho?”Aliuliza mwanaume mmoja alievalia kilemba kichwani na kanzu.
“Ndio Shekhe”Alijibu kijana alievalia suti huku akiwa ameshikilia kishikwambi mkonnoni na jibu lake liliwafanya watu sita walioketi kwenye meza ya pembe nne wamwangalie kwa shauku ya kutaka kumsikiliza.
“Unaweza kuendelea”Aliongea mwanaume mwingine alievalia suti na miwani , alikuwa ni mzee ambaye umri wake ulionyesha kuwa mkubwa kutokana na nywele zake kuwa nyeupe.
“Nadia Alfonso alifanikisha kufanya mahojiano na Roma Ramoni juu ya kile kilichotokea na ameweza kutupatia majibu yaliorahisisha uchunguzi”Aliongea na kisha akafanya ‘casting’ ya kishikwambi chake na Screen ya TV ya nch 85 ya kampuni ya Sumsung na palepale ilionekana picha ya ua.
“Mnachokiona kwenye Screen ni ua adimu linalofahamika kwa jina la Blue Ghost Orchid, kwa maelezo ya Mr Roma Ramoni kutoka Tanzania anasema kabla ya Chirss hajamshambulia CEO Edna na Miss Suzzane alitokea mwanamke na akawaokoa na baada ya Chriss kufariki mwanamke huyo aliacha zawasi ya hilo ua , Maelezo haya yanafanana na ya Bi Suzzane ambaye pia tulichukua maelezo yake”Aliongea na kisha akapozi kidogo na kuangalia kishikwambi chake na kwenda ukurasa wa pili.
“Blue Ghost Orchid ni utambuisho wa taasisi ya siri yenye makao makuu nchini Singapore lakini pia ni utambulisho rasmi wa mwanachama baada ya kupokea ua hilo kama zawadi kutoka kwa The Doni”aliongea na kuwafanya wale wazee kuangaliana.
“Kwa maelezo yako tunapaswa kuamini The Doni ndio aliemuokoa CEO Edna si ndio?”Aliuliza na kumfanya kijana yule kutingisha kichwa na kisha akaendelea.
“ Kwa maelezo ya Bi Suzzane na Mr Roma mwanamke aliemuua Chriss ni Clellia Allisanto ambaye ni katibu mkuu wa umoja wa mataifa”Aliongea na kuwafanya wote kuangaliana.
“Mr Alban unatuambia kwamba aliemuokoa Edna ni Katibu mkuu wa umoja wa mataifa?”Aliuliza mzee mwingine wa kiafrika alievalia suti.
“Tumeshindwa kufikia kwenye hitimisho kutokana na kwamba hakuna namna yoyote ya kuthibitisha kama Clellia Allisanto ni The Doni”Aliongea na kuwafanya waanze kuongeleshana wao kwa wao kwa dakika kadhaa na kisha wakamgeukia.
“Vipi kuhusu Chriss, aliishi wapi mara baada ya kutolewa gerezani na kwanini alitaka kumuua Bi Edna kuna dhamira yoyote mmepata kuifahamu?”.
“Kamati yetu ya uchunguzi iliweza kupokea nyaraka iliotumwa kwetu kwa njia ya barua pepe na mtu ambaye hakujitambulisha jina na imetoa majibu ambayo tumeshindwa kuyahakiki na nitayaweka wazi”Aliongea na kisha alienda kwenye Gmail na kufungua nyaraka iliotumwa na palepale ilionekana kwenye Skrini na kuwafanya wale wazee wenye miwani kuziweka vizuri ili kusoma na wale ambao macho yao yalikuwa imara walikodoa macho.
“Nyaraka hii inaonyesha Chriss aliishi ndani ya Vatican mara baada ya kutolewa gerezani nchini Marekani na alikuwa ni mkutubi wa maktaba Chemba namba 4”Alielezea ile nyaraka na kuwafanya wale wazee kuendelea kushangaa.
“Kuna taarifa yoyote inaonyesha alikuwa na dhamira ya kutaka kumuua Bi Edna?”Aliuliza na Alban alitingisha kichwa kuashiria jibu ni ndio na kisha akapangusha kishikwambi chake na akatoa nyaraka nyingine iliotumwa kwao kama barua mfumo wa portable file(PDF).
“Hii ni barua ambayo tunaamini imeandikwa na Chriss mwenyewe kabla ya kutekeleza misheni ya kutaka kumuua Bi Edna nchini Tanzania na inaonyesha sababu kwanini alifanya maamuzi tofauti na misheni aliopatiwa.”Aliongea na palepale alianza kuisoma.
Kwa maelezo ya barua inaonyesha ni kweli Chriss alikuwa akiishi ndani ya Vatican kwa kipindi chote tokea atoroshwe kwenye gereza chini ya serikali ya kimarekani , anasema kwamba aliishi kwa Dilema ni upande upi anapaswa kuegamia kutokana na mfanano wa malengo ya dunia ijayo kati ya taasisi mbili tofauti yaani hio ya Ant-Illuminat na nyingine ambayo hakuitaja.
Anaendelea kusema maamuzi alioyafanya ni chaguzi alioifanya yeye mwenyewe na barua hio kama wataisoma basi atakuwa tayari amekwisha kufariki na misheni yake imefeli.
Mwisho kabisa anawafunulia kwamba misheni aliopewa kwa ajili ya Ant -illuminat ni kuwajuza kwamba kiongozi wanaemgojea sio yule ambaye wanamfikiria bali ni yule ambaye anapewa ulinzi na yule wanaemfikiria na ushahidi wa maneno yake upo kwenye mchoro wa unabii.
Mwisho kabisa wa barua anasema kama watakuwa wamefanikisha kupata barua yake basi misheni aliopewa na aliemuokoa imekamilika na atapumzika kwa amani akimlenga Hades wa zamani aliempatia misheni.
“Mchoro wa unabii!!??”Walijikuta wakiongea wote kwa wakati mmoja kwani hawajaelewa.
“Barua hii ni ya kweli inetokea kwake kutokana na sahihi na nadhani kabla ya kufikiria mchoto wa unabii tunapaswa kujua kauli yake: ‘yule tunaemfikiria sio mwenyewe bali yule anaelindwa na tunaemfikiria’ tuanzeni na kufumbua kauli yake”Aliongea mwanaume alievalia suti na Collar ya kiuchungaji.
“Albani kuna taarifa nyingine ambayo bado haujatupatia?”
“Hakuna Shekhe”
“Kwasasa uchunguzi wenu uhamie upande wa Clellia Allisanto ili kufahamu kama ndio The Doni, kuhusu kuthibitisha uwepo wa Chriss ndani ya Vatican tutatumia koneksheni tulizokuwa nazo”Aliongea Shekh na Albani alitingisha kichwa kukubali.
“Unaweza kwenda kwasasa , tunapaswa akujadili”Aliongea na kisha Albani aliondoka , haikueleweka alikuwa akitokea kitengo gani ndani ya taasisi hio ya Ant-illuminat lakini ni dhahiri ni sehemu ya kamati ya uchunguzi ilioutwa kutafiti kifo cha Chriss.
“Pastor Cohen nini maoni yako?”Aliuliza Shekhe na kumfanya mzee alievalia suti na kuwa na kipara cha nywele nyeupe kuvuta pumzi na kuzishusha.
“Mpaka kufikia leo hii ni mengi ambayo yamefanyika na tumejipanua sana ndani ya mabara karibia yote na tuna washirika wengi wa kutuunga mkono kupambana na uovu , lakini licha ya mapambano yetu hatukuwa na kiongozi na wote tunajua tarehe 24 ya mwezi wa nne kwa mujibu wa Kalenda ndio siku ya kumtambua kiongozi wetu , nadhani alichoongea Chriss tunapaswa kukifiria mara mbili ili kupata majawabu lakini pia kuihakikisha kauli yake”Aliongea Paster Cohen kwa lugha ya kingereza.
“Naungana na Pastor Cohen ,nadhani ni wakati sahihi kwanza kuchambua kile alichoandika kwenye barua yake ili tufanye reasoning”Aliongea mwingine.
“Tunaefikiria siku zote kama kiongozi wetu ajae ni mrithi wa Hades ambaye ni Mr Roma Ramoni lakini kama sio yeye kwa kauli ya Chriss je anaemlinda ni nani?”
“Nadhani kujibu swali hilo kwa wepesi ni sisi kujiuliza ni nani wa muhimu kwenye maisha ya Hades mpya?”
“Mke wake ndio muhimu zaidi”
“Upo sahihi Shekhe Assad, nadhani hili pia linatoa majawabu ya kauli ya Chriss kuwa katika Dilema”Aliongea mwingine .
“Kwa haraka haraka inaonyesha Chriss hakuwa akifanya kazi tu kama mkutubi ndani ya Vatican , huenda kuna watu aliokutana nao na kujenga nao mahusiano ambayo yamempelekea kwenye dilema na huenda dilema aliokuwa nayo ni katika kuchagua upande aidha wa kwetu au wa kwao na ni sahihi pia kuamini huenda ndio wamemuonyesha kitu alichokiita mchoro wa unabii”
“Unafikiri huo mchoro wa unabii unahusiana na Edna?”
“Kama Bi Edna anapaswa kuwa kiongozi wa umoja wetu ambaye amechaguliwa na Hades wa zamani nadhani kuna uwezekano mchoro huo wa unabii unamzungumzia na ndio maana Chriss akachagua kutaka kumuua kwa kuagizwa na upande mwingine”
“Lakini kama mchoto unamzungumzia Edna kuwa kiongozi wetu kwanini na The Doni akamuokoa?”.
“Hili ni fumbo gumu , lakini naamini majibu yake tunayo wenyewe”
“Unamaanisha nini Paster Cohen?”
“Wote tunajua namna ambavyo Hades wa zamani alivyomuhusisha Seventeen kwenye mpango LADO, mnafikiri ilikuwa bahati mbaya , Seventeen na Edna ni mapacha tena wa kufanana kabisa na mpaka sasa hatujui Seventeen yuko wapi na tukumbuke yeye ni mwanachama wa ant-illuminat na ndio ambaye alimwingiza Zoe Kovac kwenye uanachama na haikuwa hivyo tu, Seventeen alikuwa na madaraka ya kuchagua mwanachama mpya wa ‘first echelon’ cheo ambacho ni kikubwa katika jumuia yetu na ni madaraka makubwa”
“Lakini wote tunaamini kiongozi wetu amekabidhiwa muhuli na Hades wa zamani , si ndio ulivyosema Shekh Assad namna ya kumtambua?”
“Uko sahihi kwa maelezo ya Hades wa zamani tutamtambua kiongozi kwa kutuonyesha pete ya muhuri(signet ring)?”
“Basi nadhaini hilo ni jibu la hiki tunachojadiliana hapa, kama maneno ya Chriss yapo sahihi na Hades mpya sio mwenye umiliki wa pete yenye muhuri basi mke wake Edna atakuwa nao”
“Upo sahihi ndugu Khalifa , lakini kalenda yetu inatupa muda mchache sana wa kutambua nani mmiliki wa pete hio ya muhuri wa uongozi , kalenda yetu inaonyesha tarehe 24 mwezi wa nne ndio siku ambayo tunapaswa kumtambua kiongozi”Aliongea na kuwafanya watu wote kuingia kwenye mawazo na waliona ana point.
“Nadhani kuna namna moja tu ya kuthibitisha maneno ya Chriss ni ya kweli au ya uongo?”Aliongea Shekhe Assad.
“Unataka kusema nini?”
“Tarehe ishirini na nne ndio siku katika kalenda yetu ya kumtambua kiongozi wetu na Chriss katuachia tayari fumbo na wote tunafahamu mtu muhimu katika maisha ya Hades mpya ni Edna mke wake , nadhani hili ni jibu tosha kwetu, Kama Edna kweli ni kiongozi wetu basi lazima atakuwa na pete ya muhuri wa uongozi na siku hio anapaswa kutuonyesha”Aliongea na kufanya chumba kukaa kimya.
“Wajumbe mnasemaje juu ya wazo la Shekhe Assad?”
“Kama kweli fumbo la Chriss linamuonyesha Edna ndio kiongozi wetu basi lazima atakuwa na muhuri wa uongozi”Alirudia mwingine kauli ileile ya Shekhe Assad.
“Na kama hatokuwa na pete ya muhuri basi tutatambua moja kwa moja yeye sio mlengwa na sio kiongozi wetu na fumbo la Chriss sio sahihi”Aliongea na wote walikubaliana na wazo lake.
“Kama ni hivyo tunafanikishaje kumfanya atuonyeshe pete hio?”Aliuliza Tajiri Khalifa.
“Tunatakiwa kumfanya atuonyeshe na ili hilo lifanikiwe lazima tuwe na mpango, Miss Edna anaweza kuwa na muhuri lakini hana ufahamu wowote kuhusu jumuiya yetu”
“Naunga mkono hoja na matukio mengi yanaonyesha ndio kiongozi wetu na wote hatujui hapa huenda Hades mpya amemkabidhi Edna pete hio kwa maelekezo ya Hades wa zamani”
“Ni kweli kabisa hakuna ambaye anajua nini Hades wa Zamani na Hades mpya waliongea wakati wakukabidhiana urithi , huenda alimwagiza Edna apatiwe muhuli na yeye ndio anaepaswa kumlinda”
“Mimi nina mawazo tofauti , kwa maelezo ya Hades wa Zamani hajamwambia Hades mpya kitu chochote kuhusu Ant illuminat na ameseme yeye mwenyewe angefahamu kitu kimoja kimoja kadri ya muda unavyosonga,tutaomba CEO Edna atuonyeshe muhuri wa uongozi kama kweli anao lakini tusiende na wazo la kuamini kwamba Hades mpya kampatia pete hio ya muhuri wa uongozi, nadhani mpaka sasa tunaelewa kwamba Hades hajamwambia mkewe chochote kuhusu Seventeen kuwa ni pacha wake , unafikiri ingekuwa rahisi kwake kumpatia Muhuri”Aliongea Shekhe na maneno yake yalionekana kuwa na mantiki.
Makubaliano ni tarehe ishirini na nne mwezi wa nne kuonana na Edna ili aonyeshe pete ya muhuri wa uongozi wa jumuia hio ya ant-illuminat.
Naam Edna kukutana na jopo la watu hao kwa kisingizio cha kuonana na Tajiri Khalifa ilikuwa ni mbinu tu, lakini vipi kuhusu hio pete.
SEHEMU YA 491.
ROME – ITALY- Miezi miwili iliopita.
Ni miezi miwili iliopita mashariki mwa jiji la Rome katika moja ya jengo la makumbusho ya kitaifa usiku wa saa mbili na nusu kwenda tatu kulikuwa na kikao cha watu wazito.
Ni watu wazito haswa kutokana na itifaki za ki usalama ambazo zilikuwa zimekwisha kuchukuliwa , jengo hilo lilikuwa kikitumika kama la makumbusho na mara nyingi muda wote linakuwa wazi mpaka saa nne za usiku kuruhusu watu , lakini siku hio jengo hilo lenye muundo wa kikale lilifungwa kwanzia muda wa saa kumi za jioni.
Ilikuwa ni sehemu sahihi sana kwa kufanyia mikutano ya siri kutokana na muundo wa jengo lenyewe lakini kitu kingine barabara ya kuingia ndani ya hili jengo haikuwa na pilikapilika nyingi kama barabara za katikati ya jiji.
Sasa usiku ndani ya vyumba vya Ardhi ndani ya jengo hili kulikuwa na kikao ambacho hakikujumuisha watu wengi sana , jumla ya watu waliokuwa wakifanya kikao walikuwa ni wanne tu, watatu wote walikuwa wamevalia suruali nyeusi na mashati ya rangi ya bluu iliokolea na kuvaa na Collar ambazo kwa harakaraka ziliwatambulisha kama wachungaji.
Mtu mmoja pekee ndio ambaye alivalia suti pamoja na tai , mwanga wa hapo ndani haukuwa mkali sana kutokana na taa zake za rangi ya njano zilizokuwa zikiendana na muundoo wa chumba.
“Barrack nadhani unaelewa sipendezwi na vikao vya dharula”Aliongea mzungu mmoja ambaye umri wake kwa haraka haraka ni kama miaka sabini hivi.
“Andre siwezi kusahau jambo muhimu kama hilo , lakini leo tulipaswa kuonana kwa dharula na nimefarijika mmeweza kutii wito kwa haraka”Aliongea yule mwanaume ambaye amevalia suti na tai akiwaangalia wale wenzake ambao walionyesha kuwa ni wachungaji au mapadri..
“Nini kimetokea?”
“Ni kuhusu Chriss mkutubi wetu ambae alienda Tanzania kwa maagizo yetu”Aliongea na kuwafanya wale wachungaji kuangaliana lakini mwanaume alieitwa kwa jina la Andre alionyesha utofauti.
“Nini kimetokea kuhusu Chriss , makubaliano yetu ajiingize ndani ya jumuia ya Ant Illuminat ili kupata kujua kila kitu kinachoendelea”
“Pastor Michal hiko ndio ambacho kimenifanya kuitisha hiki kikao cha dharula , taarifa zilizonifikia mpaka sasa Chriss amefaiki”Aiongea mwanaume aliefahamika kwa jina la Barrack na kimya kilitawala.
“Nini kimetokea? Je amegundulika ni shushu wetu?”
“Hilo haliwezekani ndio maana nahitaji kusikia kutoka kwenu wote,sisi wanne ndio tunajua kuhusu Chriss na Pastor Andre ulihusika kumbadilisha Chriss na kuwa double agent kazi ambayo ilichukuwa muda mrefu na hata aliporudi kuwa chini yangu ulinihakikishia ni Asset ya faida kwetu na ndio maana nilimsamehe na kumpa nafasi nyingine”
“Mr Barrack tunataka kusikia nini kimepelekea kifo cha Chriss?”Aliongea mchungaji michael.
“Taarifa nilizopata inaonyesha alienda kinyume na misheni aliopewa na Hades wa zamanni ndani ya Ant illuminat na akamshambulia Edna Adebayo mke wa Hades”Aliongea na kufanya wote kumaka lakini Andre muonekano wake haukutafsirika na Barrack aligundua hilo.
“Andre mbona unaonekana kutoshangaa?”
“Chriss alipaswa kunitafuta mara baada ya misheni”Aliongea Andr.
“Unamaanisha nini Andre”
“Ni mimi niliewasiliana nae dakika za mwisho kabisa na kumwambia misheni imebadilika”
“Kwanini?”
“Wameniambia kama hatuwezi kubadili unabii tunaweza kubadili matokeo”Aliongea na kuwafanya wenzake wote kushindwa kumuelewa.
“Nilipokea ujumbe kutoka kwa baraza la 33rd degree ya kumbadilishia Chriss misheni yake na wakati nawasiliana nae aliniambia ashafika eneo la tukio na muda si mrefu angekutana na Edna Adebayo”
“Mbona mimi ndio niliwasiliana nae na kumbadilishia misheni siku moja kabla nini kinaendelea?”Aliwaza ndugu Barrack.
“Andre ni watu gani hao?”
“Prior of sion, wanajua kila kitu ambacho tunakifanya na mipango yetu na hata kifo cha Chriss waliniambia wao wenyewe muhusika mkuu ni Minerva”
“Athena ndio aliemuua Chriss?”Aliuliza Barrack huku akionyesha wasiwasi.
“Hivyo ndio walivyoniambia”
“Papa Andre , ulishawahi kunihadithia umekutana na Athena ana kwa ana nadhani huu ndio muda wa kutuambia anafanana vipi? Je ni kweli Clelia Allisanto ndio yeye?”Aliuliza kwa kutanguliza jina la Pope Mwanzoni.
“Clellia Alisanto katibu wa umoja wa mataifa sio Minerva bali Athena anatumia Clone nina uhakika na hilo”
“I knew it”Aliongea akimaanisha kwamba alijua tu.
Naam mwanaume anaefahamika kwa jina la Barrack ni raisi mstaafu waMarekani na Andre ni Pope , wawili ni Michale ambaye cheo chake haikuwa wazi na pia John cheo chake haikuwa waz.
*********
MASAA KADHAA NYUMA
Ni muda wa saa sita usiku mara baada ya Roma kuondoka nyumbanni na kwenda kuzamia nyumbani kwa Nasra kwa kupitia balkoni, muda huo huo katika chumba chake alionekana mtu mwingine akiibukia na kuanza kuangalia mazingira ya hapo ndani na mara baada ya kuridhika aliingia kwenye chumba anacholala Roma na kuwasha taa na baada ya kuona kitanda hakina mtu alitabasamu kwa kebehi.
“Kulikuwa na haja gani ya kufanya sherehe kubwa na kutuharibia maua kama unakuja kulala mwenyewe”Aliongea kwa lugha ya chini huku akigeuka nyuma.
Alikuwa ni Hermes au Prince Raphaeli ambaye mwezi mmoja nyuma alimuokoa Denisi kwa kumdhibiti Roma kupitia ndoto.
Baada ya kukagua chumba cha Roma kwa dakika kadhaa alitoka kwenye chumba hiko na kuingia kwenye korido na ndani ya dakika chache tu aliibukia kwenye chumba cha Edna.
Baada ya kuingia ndani ya chumba hicho hakuacha kuangalia mandhari ya chumba kizima na kisha akahamia kwenye kitanda na kumwangalia Edna na Lanlan ambao wamelala fofo,
“Hades unaishi na mtoto wako lakini mpaka muda huu umeshindwa kumfahamu, aliesema huna akili kweli kapatia”Alijiwazia huku akimwangalia Lanlan aliemuwekea Edna mguu kwenye shingo.
“Athena sijui ananitakia nini , Hades akiniona namwangalia mke wake namna hii lazima ataniua, inabidi nifanye haraka kilichonileta na kuondoka”Alijiwazia mwenyewe na kisha akanyanyuma mkono wake na kumnyooshea Edna kama vile anamwombea na muda uleule Edna alianza kutingisha kichwa kama vile mtu ambaye yupo ndotoni na Hermes alidumu vilevile kwa dakika kama tano na kisha akaonyesha kuridhika na akageuza macho kwa Lanlan na kumnyooshea mkono kama alivyofanya kwa Edna na Lanlan alianza kutafuna tafuna kwa kasi kama vile kuna kitu analishwa na Hermes alitabasamu na kisha akaondoa mkonno wake.
“Persephone , kwanzia kesho utafanya mambo yako yote bila kujielewa chini ya udhibiti wangu ukiwa ndotoni”Aliongea huku akimwangalia Edna kwa dakika na kisha akafungua mlango wa kutokezea kwenye balkoni na palepale alipotea kufumba na kufumbua.
*********
“Madam Persephone tusamehe kwa kukufanyia hii surprise , yote yamefanyika kwa kuzingatia itifaki za kiusalama wa kuficha kile ambacho kinakwenda kuzungumziwa hapa ndani, nadhani upo kwenye mshituko lakini kabla ya kuendelea na hatua ya pili tutaomba utoe wasiwasi kabisa na kama kila kitu kikienda sawa huenda sisi wote tukawa chini yako”Aliongea Shekh Assad na Edna alishindwa kujibu chochote na alishangaa pia uwepo wa Nadia Alfonso.
“Kwa majina yangu naitwa Ally Assad na ndio msemaji mkuu wa hili jopo lote la watu waliopo mbele yako na Kabla ya kujitambulisha kwako mmoja mmoja na kukuelezea dhumuni la uwepo wetu hapa ndani tunataka ututhibitishie kwa kutuonyesha pete ya muhuri unaokutambulisha kama kiongozi wetu”Aliongea.
“Shekhe Ally Assad unaweza kuketi”Aliongea Edna bila wasiwasi na Shekh Assad alikaa chini na watu wote walimwangalia Edna kwa shauku ya kile ambacho anakwenda kufanya.
Edna hakuonekana kuongea chochote zaidi ya kuchukua mkoba wake na kutoa kijiboksi kidogo cha rangi nyeusi , ni viboksi flani kama vile vya kuwekea pete au mkufu.
Kitendo kile cha kushikiria kile kiboksi kabla hata ya kukifungua kiliwafanya watu wote hapo ndani kuwa na mchecheto wa aina yake.
“Kwasababu wote mmekuja kukutana na mimi leo hii , basi sina budi kuwadhirihirishia kwenu muhuri ambao unanitambulisha kama kiongozi wenu”Aiongea Edna akiwa kama sio yeye vile na kisha akafungua kile kiboksi na ndani yake ilionekana pete ambayo kwa kuiangalia tu haikuwa ya kawaida, ilikuwa na mchoro juu yake ulionakshiwa kwa madini ya shaba , mchoro ulikuwa kama vile ni tunda ambalo limekatwa kwa mshazari katikati sasa ule muonnekano wake wa ndani ndio ulifanana na hio pete.
Edna aliitoa na kuishikilia mkononi na kisha kwa mbwembwe zote aliingiza kidoleni katika mkono wake wa kulia na akaunyoosha juu ule mkono kuelekezea ule upande wa pete kuonekana kwa watu waliokaribu.
“Shekh Ally Assad hii ni Signet ring inatumika kama muhuri na ni kwa muda mrefu haijatumika , unaweza kuiangalia kwa ukaribu kuona kama mchoro wake unafanana na muhuri unaonitambulisha kama kiongozi wenu”Aliongea Edna na Shekhe Ally Assad aliangalia kwa umakini ile pete na alijikuta akipatwa na mshangao usiokuwa wa kawaida na palepale aliwageukia wenzake wote na kuwapa ishara ya kuashiria ndio muhuri wenyewe na wote kwa pamoja walisimamaa na kuinamisha vichwa chini kwa mara nyingine.
“Karibu sana Malkia wetu Persephone”Waliongea kwa mara nyingine baada ya kusimama na Edna alinyoosha mkono juu kuwazuia na akawaambia waketi chini na walitiii.
Suzzane na Nadia walikuwa na mshangao kwani hawakutegemea kutokutana na upinzani kutoka kwa Edna , lakini alionyesha kana kwamba watu waliopo mbele yake anawafahamu mbaya zaidi aliongea kimadaraka.
“Leo nimejitambulisha kwenu kikalenda , lakini muda wangu wa kuwaongoza bado , mpaka muda utakapokuwa sahihi nitawatafuta, kwasasa Shekh Assad ataendelea kuongoza jumuia yetu kwa niaba yangu na malengo yote yanapaswa kutimia kabla ya siku ya kurudi kwangu”Aliongea na kuwafanya kuonyesha sura za kutoelewa maana ya maneno.
*********
Blandna alijikuta akishangaa mara baada ya kuambiwa na raisi Senga kuhusu Roma kile alichomfanyia Desmond mtoto wa raisi Jeremy, hakujua jambo hilo kama limetokea kwani Roma na Edna hawakumwambia.
Usiku wa juzi walivyorudi alijua kabisa kuna jambo ambalo limetokea lakini hakuhoji sana kwani Roma alimwambia hakukuwa na tatizo na ni sherehe tu ambayo haikuwa nzuri.
Na yeye alipotezea baada ya kuwaona Edna na Roma asubuhi walikuwa wamepatana na ile hali ya kununiana ilikuwa imeisha na ndio maana hakuhoji sana.
“Kwahio hiki ndio ambacho ulitaka kuongea na mimi?”Aliuliza Blandina
“Kuna lingine ambalo ulitarajia kusikia kutoka kwangu , nimekuita hapa kukuambia kile alichokifanya mtoto wako ili umuonye kwani akiendelea kuchafua amani ya nchi yangu nitamchukulia hatua”Aliongea na kumfanya Blandina kumwangalia Senga kwa huzuni.
“Kwanini unamwita mtoto wangu peke yangu Senga , Wewe sio mtoto wako? Au ni kwasababu amebadilisha jina na kuitwa Roma ndio kinachokupa shida ya kumtambua, Senga najua huwezi kunisamehe lakini Roma bado ataendelea kuwa mtoto wako”
“Kimya!!!, wewe na Roma kwangu mlishakufa na ndege na sitaki kuhusika na maisha yenu , ninachotaka kutoka kwako ni kumuonya Roma aache kuharibu diplomasia ya nchi”
“Senga tangu lini ukawa mnafiki wa hisia zako mwenyewe?”
“Unamaanisha nini?”Aliongea Raisi Senga huku awamu hii akionyesha kakarisika maradufu.
“Maneno yako yapo tofauti na hisia zako Senga, unafikiria sijui kinachoendelea kwenye moyo wako , ulifikiri nitashindwa kujua kile unachojisikia , sijakusahau Senga”
“Kimyya , Blandina naomba usinikasirishe zaidi kukaa na mimi chumba kimoja usijipe ujasiri wa kuongea unavyojisikia , wakati ule ulishapita na sasa nimekuwa raisi kwa juhudu zangu wakati wewe ukijificha”
“Kinachokusumbua Senga ni kwasababu Roma ana nguvu zaidi kuliko wewe , uwezo wake na nguvu zake zinakufanya ujihisi huwezi kuwa baba mbele yake, Senga acha kuishi kwa mateso unapaswa kuachilia baadhi ya mambo megine yasahaulike kwenye moyo wako”
“Kuna vitu naweza kusahau , lakini siwezi kumsahau mwanamke alienisaliti”Aliongea na kumfanhya Blandina kuanza kutokwa na machozi.
Muda huo maongezi yao walikuwa wakiyafanyia ndani ya chumba cha hoteli hivyo ilikuwa ngumu kwa mtu wa nje kujua kile ambacho kinaongelewa na ilikuwa mara ya kwanza kwa Senga na Blandina kukutana wakiwa peke yao tokea arudi Tanzania na huenda ni mwanzo mzuri wa mapatano.
“Najua Senga huwezi kusahau na huwezi kunisamehe lakini upendo wangu kwako hakuwahi kupotea kwa miaka yote ambayo hukuweza kufahamu nipo hai”
“Blandina acha kuwa mnafiki mbele yangu utanikasirisha , nimekuja hapa kukuonya kuhusu Roma kuingilia amani ya taifa”
“Una uhakika ndio kitu pekee ambacho ulitaka kuniambia mpaka kutaka kuongea na mimi kwa kujificha ficha?”Aliuliza na kumfanya Senga amwangalie Blandina huku akikosa neno la kuongea.
Alichoongea Blandina ni ukweli mtupu, kama kweli alitaka kumuonya tu kuhusu Roma haikuwa na haja ya kumuita hotelini kwenye chumba cha Presidontial Suite tena kwa siri.
Blandina alimwangalia kwa muda namna ambavyo amekosa neno la kuongea na kisha akaangalia mkoba wake na akauchukua.
“Kwa mra ya kwanza nimefurahi kukuona kwa ukaribu Senga, nitamwonya Roma kutokuingilia uongozi wako”Aliongea na kisha alisogelea mlango akitaka kutoka.
“Subiri..!!!”Aliongea na kumfanya Blandina kusimama na kugeuka na Senga aliingiza mkono kwenye mfuko wa koti na ilionekana kuna kitu anatoa.
SEHEMU YA 492
Roma hakujua kinachoendelea kabisa na baada ya kutoka kwa Afande Kweka hakupitia nyumbani kabisa , akili yake ilimwambia aende kuonana na Rufi kwanza kuongea nae kuhusu kanuni aliopewa na Zenzhei ya kutengeneza vidonge vya nguvu za kijini , alikuwa na muwashawasha wa kufahamu kama Rufi angeweza kuelewa kanuni zote.
Dakika chache mbele mara baada ya kuendesha gari aliweza kufunga breki chini ya jengo la apartment anapoishi Rufi na alitoka kwenye gari na kuzisogelea lift.
Baadaya kuingia kwenye lift na kubonyeza kitufe cha floor husika simu yake ilitoa mtetemo wa ujumbe wa meseji ulioingia ,alifungua na kuona ni ujumbe ulitoka kwa Xiao Xiao na aliupotezea palepal.
Ilikuwa ni siku zaidi ya mbili msichana huyo wa kichina hakukata tamaa kutuma jumbe za kumsalimia Roma na nyingine za kuchombeza lakini Roma hakujibu hata moja , hakutaka matatizo na mke wake lakini pia alijua akiwa na ukaribu na msichana huyo itakuwa rahisi kwa Rufi uwepo wake hapa Tanzania kufahamika kwa wepesi , hivyo alijiambia anapaswa kumuepuka kwa nguvu zote.
Baada ya kutoka kwenye lift alibonyeza kengere na mlango kwa ndani ulifunguliwa na Rufi ambaye amevalia tisheti ya jezi ya Man U huku mkononi akiwa ameshikilia juisi ya matunda.Alitabasamu na kumpa ishara ya kuingia na Roma alifanya hivyo.
“Inaonekana unapenda sana mambo ya kompyuta , kwa mwonekano wako ulipaswa kujifunza vitu vilaini vilaini visivyotumia akili nyingi”Aliongea Roma mara baada ya kuona tarakishi ikionyesha namba namba ambazo hata hakuelewa.
“Kompyuta naipenda kwasababu nahisi kama dunia yote naiona , nimejifunza mambo mengi sana na kwasasa najaribu kutafuta Proffesional Hacjer anielekeze baadhi ya mambo madogo madogo”
“Kwahio unataka kuwa mdukuzi , haupendezi kabisa kwa fani hio?””
“Kipi kinanipendeza? Au kutapeli watu ndio kazi nzuri inayonifaaa?”Aliongea na Roma hakumjibu na aliishia kumwangalia tu kuona kama ana shida yoyote kwani tokea amuache mara ya mwisho hakuwasiliana nae kabisa na kumpa habari za Xiao Xiao msichana wa kichina aliemkimbia.
“Unaendelejeaje, ulitoka kweli humu na kwenda kutembea?”
“Naogopa hata kwenda Supermarket na hofia naweza kukutana nae tena” Aliongea huku akijibwaga kwenye sofa kivivu na kumfanya Roma amuonee huruma.
“Unapaswa kutoka bila ya kuhofia chochote hakuna mtu yoyote wa kuja Tanzania na kukufosi urudi ilihali mimi nipo”.
“Ah .. najua unaweza kunilinda lakini hawatoacha kuja mara kwa mara lazima watalazimisha nirudi sitaki kukuongezea zaidi matatizo”
“Nishakuambia usiwe na wasiwasi juu ya hilo nimefuatilia taarifa za msichana uliekuwa unamkimbia yupo Tanzania kikazi”
“Kweli?”
“Unafikiri nakudanganya? , umeacha lini kutokuniamini?”Aliongea Roma na kumfanya Rufi kutabasamu na kushindwa kuongea chochote na Roma aliona apotezee mada hio na kwenda moja kwa moja kwa kile kilichomleta.
“Nimekuja kukuuliza namna ya kutengeneza vidonge”
“Unataka kutengeneza vidonge!?”
“Kwanini unaonyesha kushangaa ,ushasema mwenyewe vidonge ni muhimu katika kusaidia kupanda levo naweza nisihitaji mimi lakini warembo wangu nataka niwapatie ili viwasaidie”
“Ndio vidonge ni muhimu sana kwa wanaoanza mafunzo , lakini kuna mahitaji yake na kanuni za kutengeneza”
“Ndio maana nimekuja kwako nataka kujua hayo mahitaji”Aliongea Roma na kumfanya Rufi kufikiria kidogo.
“Kama kweli una nia ya kutengeneza vidonge. kuna changamoto tatu ambazo unapaswa kuzivuka , Changamoto ya kwanza lazima upate mimea ambayo hutumika kutengenezea, hii sio rahisi kwasababu mimea hio ni adimu sana kupatikana na hata ile ambayo inatengeneza vidonge vya thamani kubwa imepotea kabisa, katika miliki za kijini kwenyewe huwezi kuipata hio mimea na ndio maana licha ya uwepo wa wenye ujuzi mkubwa wa kutengeneza wameishia kutengeneza vidonge vya kawaida tu”
“Lakini umesema kuna wanaokuja huku duniani kutafuta hio mimea ?”
“Ndio kuna wanaosafiri mpaka duniani kwa ajili ya kutafuta mimea ya kutengenezea vidonge lakini mara nyingi huishia maeneo ya karibu na bara la Asia , kwani wengi wao wanasema wanaogopa kuvunja sheria za the gods treaty”
“Kama ni hivyo basi uwezekano wa kupata hio mimea upo ,ninachotakiwa kufanya ni kutuma watu wangu wajaribu kufatilia, je ni wapi ambapo unaamini mimea hio inawezekana kupatikana?”
“Sina uhakika ila marra nyingi ni sehemu ambazo ustaarabu wa kale ulianzia kama vile Misri na maeneo mengine kama hayo”Aliongea na kumfanya Roma kutingisha kichwa kumuelewa.
“Vipi kuhusu changamoto inayofuatia?”
“That is even harder , You would need a high Quality Cauldron”Aliongea akimaanisha kwamba changamoto ya pili ni ngumu zaidi kwasababu atahitajika kuwa na Cauldron.
“Cauldron?”Roma aliuliza.
“Ndio Cauldron ni Dhana ambayo ipo mfano wa chungu kikubwa ambacho kimetengenezwa kwa madini maalumu ambayo yalipatikana enzi za kale,ni madini ambayo yana uwezo wa kuhimili kiwango kikubwa cha joto , kwa uelewa wangu katika miliki za kijini vipo vitano tu hivyo vyungu , Kekexil wanavyo vitatu ,ukoo wa wakwe zangu wanacho kimoja na Hongmeng wenyewe wanacho kimoja , kama kuna jamii nyingine ambazo wana aina hio ya chungu kinaweza kuwa nje ya matumizi hivyo haitokuwa rahisi”
“Changamoto ya tatu ni kuweza kudhibiti moto wa njano na mweupe ambao ndio hutumika kutengenezea hivyo vidonge kwa joto kubwa sana zaidi ya joto la kuyeyushia chuma na kubalansi na Chungu hiko”Chungu kinachozungumziwa hapo ni cha kijini ambacho ni kama Cauldron
“Changamoto ya tatu ya kudhibiti moto wa rangi ya njano na mweupe sio tatizo”
“Unamaanisha unao uwezo huo?”aliuliza huku akionyesha mshangao na Roma alitingisha kichwa.
“Kwanini hujazungumzia kuhusu andiko la kanuni za kutengenezea hizo dwa?”Aliuliza Roma akimaanisha andiko la kanuni alilopatiwa na Zenzhei.
“Kila koo ina kanuni zake , lakini ilisemekana mwanzoni Hongmeng walikuwa na andiko la kanuni ambayo hutengeneza vidonge vyenye uwezo mkubwa sana ,lakini bahati mbaya andiko hilo lilipotea, ndio ninachojua japo sina uhakika,lakini hilo lisikupe shida haina haja ya kuwa na hizo kanuni kikubwa ni namna ya kudhibiti joto la moto wa kichawi mweupe na wa njano ukishafanikisha kupata hiko Chungu”Aliongea
“Nitakuwa naendelea kuvuna nishati huku nikisubiria watu wangu waweze kutafuta hayo maeneo uliozungumzia , unaonaje kama wakifanikisha unisindikize”
“Mimi? , unamaanisha twende pamoja?”
“Ndio ,najua itakuwa usumbufu lakini siwezi kujua mimea inayohitajika nikienda mwenyewe”
“Lakini inawezekana ikawa ni mbali na Tanzani misituni huko”
“Usiwe na wasiwasi nishaishi sana msituni hivyo nina uzoefu wa kutosha”Aliongea Roma.
“Mimi sina tatizo lakini vipi mkeo anaweza akakasirika?”Aliongea kwa sauti ndogo huku akiona aibu.
Na kabla Roma hajajibu simu yake ilianza kuita na aliitoa na kuangalia mtu anaempigia na alishangaa ni Bi Wema , alipokea harakaharaka na kuweka sikioni.
“Mr Roma nadhani Miss Edna kapatwa na tatizo”
“Unamaanisha nini kapatwa na tatizo Bi Wema , nini kimetokea?”
“Amerudi kutoka kazini saa kumi kamili za jioni na akasema ana usingizi , amelala mpaka muda huu na nimejaribu kumuamsha haamki , Lanlan na yeye amejaribu kumuamsha kwa nguvu lakini hajashituka”Aliongea Bi Wema huku sauti yake ikionyesha wasiwasi na kumfanya Roma kuguna.
“Ana pumua?”
“Ndio kifua kinapanda na kushuka ndio hivyo haamki , nadhani ni vyema ukarudi umuangalie nina wasiwasi kwani sio kawaida mtu kulala na kushindwa kuamka”Aliongea Bi Wema na kumfanya Roma apumue kidogo kwa ahueni.
“Nakuja sasa hivi Bi Wema”Aliongea Roma na kisha akata simu.
“Nadhani mke wangu kapatwa na tatizo , ngoja niwahi”Aliongea Roma na Rufi alitingisha kichwa .
******
Afande CammiliusKweka alionekana kuathirika sana na taarifa ya Zenzhei kutaka kurudi Hongmeng , alijitahidi kuonyesha kuwa sawa lakini ukweli alikuwa akiumia kiume lakini hakuwa na uwezo wowote wa kumzuia kutoondoka kwani asingeweza kumlinda zidi ya Hongmeng.
“Zenzhei niseme asante sana’Aliongea Afande Kweka kwa sauti hafifu na muda huo ni kama masaa mawili mara baada ya Roma kuondoka.
“Camillius kwanini unanishukuru?”
“Asante sana kwa kwa kujjifanya kuwa mzee mbele ya macho ya watu ili mradi unilinde bila watu kukushitukia , asante kwa kufanya kazi za hapa kama vile ni mfanyakazi wa ndani , asante sana kwa kumfanya mke wangu kipindi kile kufa kifo cha amani”Aliongea Afande Kweka huku macho yakiwa makundu na hata Zenzhei mwenyewe alishindwa kujizuia na kudondosha chozi.
“Hupaswi kusema hivyo Cammilius ulikuwa ni wajibu wangu”
“Hapana, nimekukatili sana kwa kipindi chote ulichokuwa na mimi lakini bado nikakosa aibu na kuwa mbinafsi na kukufanya uendelee kuwa karibu yangu”
“Camillius usiongee hivyo nilikuwa na furaha kuishi na wewe”
“Zenzhei matumaini yangu ni kwamba hutonichukia , najua kwanini ulikaa na mimi kwa miaka mingi sana lakini nilishindwa kufanya chochote juu ya hisia zako kutokana na kukosa ujasiri , nilishindwa kuzipokea na mpaka sasa nashindwa kuzipokea licha ya uzee huu”Aliongea afande Kweka na kumfanya Zenzhei kufumba macho yake huku machozi yakimtoka.
Ni kweli alikuwa akimpenda Afande Camillius Kweka tokea mara ya kwanza walipokutana , lakini licha ya kuonyesha hisia zake kwa mzee huyo hakuchukua hatua yoyote na yeye kukosa ujasiri wa kuchukua hatua zaidi.
“Camilius kabla sijaondoka nitarudi kwenye mwonekano wangu wa mwanzo wakati tunakutana nadhani itakufanya usijione mwenye hatia” Aliongea Zenzhei na palepale mwili wake ulibadilika taratibu ,ilikuwa ikishangaza mno kwani ndani ya nusu dakika alibadilila na kuwa msichana kama wa miaka ishirini na nne mwanamwali , ilikuwa ni sahihi kusema alikuwa akifanana kabisa na Xiao Xiao japo yeye kidogo alikuwa na umbo la kuvutia na huenda angekutana na Roma angefanya jambo la kueleweka.
Ilionekana ili kuishi na Afande Kweka ilibidi ajizeeshe ili kuficha ujini wake , kwani kama asingefanya hivyo angebakia kuwa msichana mdogo ilihali Afande Kweka alikuwa anazeeka.
“Nakumbuka mara ya kwanza tulipokutana Sudani ulikuwa na miaka hamsini Camilius”Aliongea Zenzhei na sio sura tu iliobadilika hata sauti yake pia ilikuwa imebadilika.
“Haha.. bado urembo wako uko vilevile hakujabadilika chochote”Aliongea huku akitoa kicheko chenye machungu na kumfanya Zenzhei kutabasamu akikosa neno.
“Nadhani hii ni kwaheri ya moja kwa moja, naamini siku ukirudi nitakuwa tayari nimeshakufa”aliendelea kuongea na kumfanya Zenzhei kuingiwa na huzuni.
“Kwaheri ya kuonana Camilius” Aliongea Zenzhei.
“Kwaheri ya kuonana Zenzhei hakikisha unakuwa na maisha ya furaha na kutafuta mtu anaekupenda”
“Asante sana Camilius”Aliongea na kisha wakaangaliana usoni kwa madaki kakadhaa na Zenzhei alikosa ujasiri wa kuendelea kusimama mbele ya Camilius na palepale alipotea kwenye macho yake.Na hio ndio safari ya Zenzhei kurudi ujinini ikaanza rasmi.