lameckkawawa
JF-Expert Member
- Sep 13, 2015
- 944
- 665
- Thread starter
- #41
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 29
MTUNZI : PATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Saa tatu za asubuhi tayari tulikwisha funga mizigo yetu kwa ajili ya safari.Nilimuomba rafiki yangu Beka atupeleke uwanja wa ndege wa Kilimajnaro halafu abaki na gari langu.Saa tatu na nusu safari ya kuelekea uwanja wa ndege ikaanza.Nilikuwa na furaha isiyo kifani kwani nilitegemea kwamba sasa karaha zote za Emmy nitaziacha nyuma na mimi kuishi maisha ya furaha na amani nikiwa na malaika wangu Clara.Tuliwasili uwanja wa ndege tukaagana na Beka na sisi kuingia sehemu ya kusubiria ndege .
Hatimaye muda wetu ukafika na tukaombwa tuelekee ndegeni.Taratibu tukiwa tumeshikana mikono tukaungana na abiria wengine kuelekea mahala ilipokuwa ndege tutakayosafiri nayo.Kabla hajaikanyaga ngazi ya ndege Clara akasimama.
“ Wayne naishiwa nguvu ..siwezi tena kunyanyua mguu wa…….” Hayo yalikuwa maneno ya mwisho ya Clara.Akaanguka na kabla hajafika chini nikawahi kumdaka.
ENDELEA………………………….
Emmy alikuwa amesimama mbele ya kioo kikubwa akiwa amefura na hasira na sura yake ameikunja..Kwa muda wa saa moja sasa alikuwa amesimama akitazama kioo kile kikubwa mfano wa luninga ,kilichokuwa kikimuonyesha kila kilichokuwa kinaendelea kati ya Wayne na Clara.Hakuwa ameongea chochote toka alipoanza kutazama luninga ile ikiwaonyesha Wayne na Clara walivyokuwa wanajiandaa kwa safari. Wayne na Clara wakiwa uwanjani walionekana ni wenye furaha kubwa .Walikuwa wamekaa wakisubiri zamu yao ya kupanda ndegeni ifike na baadae wakashikana mikono na kuanza kuelekea ndegeni.Clara akauma meno kwa hasira
“ Damn you Wayne..huwezi kunikimbia..Nitakutafuta usiku na mchana.Na huyo mwanamitindo wako ambaye amekupagawisha na kukufanya unitaliki atakiona cha moto..” akawaza Emmy .Muda wote huu mganga alikuwa amesimama pembeni yake akiwa na usinga wake mkononi akiupunga huku na huko huku akiongea maneno yake ya kiganga.
“ Emmy Wayne na Clara wanaondoka na bado haujafanya maamuzi yoyote.hii ni nafasi yako usiiache ikapita..Ukiacha wakiingia ndegeni na wakaiacha ardhi ya Arusha ,kurudi tena itakuwa vigumu mno.Kama bado unataka kuendelea na ile dhamira yako basi huu ndio wakati wake.Yeyote utakayemfunga siku ya leo hatapona hadi siku utakapokufa wewe.” Akasema mganga huku akimuonyeshea Emmy meza iliyokuwa na wanasesere wawili .Emmy hakusema kitu akageuka na kuiendea meza ile kisha akachagua mwanaserere mwenye umbo la mwanamke.Mganga akampa sindano.Emmy akasimama tena mbele ya kile kioo akawashuhudia Wayne na Clara wakikaribia kufika katika ngazi za kupandia ndege.Kwa hasira akauinua mkono wake wa kulia uliokuwa umeshika sindano ndefu na kuichoma upande wa kulia wa yule ukatoka moshi mweupe na sekunde ile ile Clara ambaye alikuwa anajiandaa kuikanyaga ngazi ya kupandia ndegeni akaanguka na hakuweza kuongea wala kuinuka tena.Emmy akatabasamu
" Leo nimekupata " akasema Emmy huku akitabasamu.
“ Kazi imekwisha” akasema mganga.
“ Kwa sasa huyu mwanamke kazi yake imekwisha.Nakuhakikishia Wayne lazima arudi kwako ndani ya muda mfupi. Atakufuata yeye mwenyewe.” Akajigamba mzee Mtuguru.
“ Nashukuru sana Mganga. Nakuahidi zawadi nzuri mno kama Wayne atafanikiwa kuja kwangu.” Akasema Emmy huku akitabasamu
“ Usiseme kama atarudi kwako.nakuhakikishia lazima arudi kwako na safari hii hataweza kuondoka tena.” Mganga akazidi kumpa moyo Emmy.
*************************
Clara..!! Clara !! ..” Niliita kwa nguvu baada ya kumdaka Clara alipotaka kuanguka lakini hakuweza kusema chochote..Nilichanganyikiwa ghafla.Mtu ambaye sekunde chache zilizopita tumekuwa tukiongea vizuri na kucheka lakini ghafla hawezi kuongea tena.Haya yalikuwa ni mambo ya ajabu sana kunitokea.Sikujua Clara amepatwa na ugonjwa gani uliomtokea ghafla namna ile.
Watu waliokuwa karibu wakanisaidia kumbeba Clara na kumuweka pembeni.Bado kichwa changu kilikuwa kizito kuamini kilichotokea.Nilihisi ni kama mchezo wa kuigiza lakini kadiri dakika zilivyokuwa zikisonga ndivyo nilivyojikuta nikilazimika kuamini kwamba Clara alikuwa amepatwa na ugonjwa wa ghafla ambao sikufahamu ni ugonjwa gani.Pamoja na ujasiri wangu wote niliokuwa nao nilijikuta nikitetemeka kila nilipomuona Clara na hali aliyokuwa nayo.Macho yalikuwa yamefumba,hakuweza hata kufumbua jicho.Mwili wake haukuweza hata kutikisika.Machozi ya uchungu yakanitiririka.Wanaume wawili wa makamo ambao nao walikuwa ni wasafiri wakanivuta pembeni baada ya kuiona hali nilioyokuwa nayo.
“ Jipe moyo ndugu yangu..Mungu atakusaidia..” akasema mmoja wao aliyekuwa amevaa suti nyeusi..
“ Tatizo hasa la mwenzio ni nini? Akauliza mwingine aliyekuwa amekaa kushoto kwangu..Nikajikaza na kusema
“ Sifahamu tatizo ni nini ..imetokea ghafla tu akapatwa na ugonjwa ule..” nikajibu kwa ufupi.Tayari uongozi wa pale uwanjani ukataarifiwa kuhusiana na kilichokuwa kimetokea na kwa haraka likatolewa gari kwa ajili ya kumkimbiza Clara katika hospitali ya Rufaa ya KCMC.Kwa kasi ya aina yake wahudumu wa pale uwanjani wakampakia Clara katika gari na mimi nikaingia ndani ya gari lile kisha tukaondoka uwanjani pale kwa kasi kubwa.
Kila nilipokuwa namuangalia Clara nilishindwa kujizuia kutokwa na machozi.Sipati neno ambalo linaweza kuelezea uchungu niliokuwa nao kwa wakati ule.Rangi ya ngozi ya Clara ikaanza kubadilika na kuwa na weusi weusi..nikazidi kuogopa.Nawashukuru watu niliokuwa nao mle garini walijitahidi kwa kila namna walivyoweza kunipa moyo ingawa hata nao nyuso zao zilionyesha mstuko na uoga wa dhahiri.
“ Ouh Clara..nini kimekupata malaika wangu?.. Nilisema kwa uchungu nilipomtazama Clara akiwa amelala mle ndani ya gari hajitambui.Niliogopa sana kwa hali aliyokuwa nayo. Gari ilikuwa inakwenda kwa mwendo mkali sana lakini niliona kama inachelewa kufika hospitali ili Clara aanze kupatiwa matibabu.
Hatimaye tukawasili katika hospitali ya rufaa ya KCMC mjini Moshi na kwa haraka wauguzi wakampokea mgonjwa na kuanza kumshughulikia mara moja. Sampuli za damu na vipimo vingine vikachukuliwa na kupelekwa maabara kwa uchunguzi.
Nilitoa malezo mafupi kwa madaktari kuhusiana na jinsi ugonjwa ule wa Clara ulivyoanza halafu wakaniomba nikasubiri nje ili waendelee na uchunguzi wao.Niliwaomba madaktari wale wafanye kila linalowezekana ili kuokoa maisha ya Clara kwani hali aliyokuwa nayo ilikuwa inaogopesha mno.Miguu haikuwa na nguvu nikatafuta sehemu nikakaa.Bado kichwa changu kilikuwa na mawazo mengi sana juu ya kilichotokea.Ilikuwa ni kama ndoto ya mchana na ilikuwa vigumu sana kuamini kilichotokea.Nilivuta picha ya kuanzia asubuhi tulipokuwa tunajiandaa kwa safari hii ambayo Clara hakutaka kuniambia tunaelekea wapi ingawa tiketi zetu zilionyesha kwamba tulikuwa tunaelekea Dar es salaam.Nikakumbuka tulivyoliacha jiji la Arusha nikiwa na matumaini kwamba nimeyaacha nyuma matatizo yote yaliyotokea kati yangu na Emmy.Sikutarajia kurejea tena Arusha.Niliamini kwamba ninakwenda kuanza maisha mapya nikiwa na malaika wangu Clara.Nilikumbuka tulivyoagana na rafiki yangu Beka pale uwanja wa ndege naye akarejea Arusha na gari langu.Nilimuahidi kuwa nikifika huko tunakokwenda ningemtaarifu kwa simu.Nikakumbuka pia tulivyokuwa tukipiga hatua kuelekea katika ndege na mara kumbu kumbu ambayo mpaka leo nikiikumbuka huwa inaniliza ikanijia kichwani. Ilikuwa ni kama ninatazama filamu.Clara alikuwa tayari ameinua mguu wake ili akanyage ngazi za ndege lakini hakuweza kufanya hivyo kwani alianguka ghafla na hakuweza kuongea tena.machopzi yakaanza kunitiririka tena.Nikafuta machozi nikachukua simu yangu na kumtaarifu rafiki yangu Beka kilichokuwa kimetokea.Hakuamini hata kidogo na alidhani ninamtania.Nilipomuhakikishia kwamba haukuwa utani aliamini na kunitaarifu kwamba tayari anaanza safari ya kuja Moshi kuungana nami katika wakati ule mgumu.Baada ya kuongea na Beka nikampigia simu baba mkwe na kumtaarifu kilichotokea halikadhalika naye akanitaarifu kwamba yuko njiani anakuna Moshi.Nikamtaarifu pia na Chris ambaye tayari tumekwisha maliza tofauti zetu . Kila mmoja niliyemtaarifu alistuka mno .hakuna aliyeamini moja kwa moja.
Nikiwa bado nimekaa pale nje nikiwasiliana na watu mbali mbali kuhusiana na kilichotokea,nikaitwa katika chumba cha daktari.Haraka haraka nikaingia na kuketi kitini.daktari akanitazama kisha akasema
“ Wayne tumemfanyia uchunguzi mgonjwa wako na tumegundua kwamba mgonjwa wako amepatwa na ugonjwa wa kupooza…”
“ What ? ..Unasema ??......Nikauliza kwa mshangao nikiwa nimesimama na macho kunitoka.Nilianza kusikia joto la ghafla.Hii ilikuwa ni taarifa ya kustusha sana.
“ Dakatari tafadhali naomba unielezee vizuri kwa ufasaha ili nikuelewe.Umesema Clara anaumwa nini? Nikauliza tena nikiwa bado nimesimama.
Kabla hajaendelea kunipa taarifa kuhusiana na ugonjwa wa Clara akaniomba niketi chini..
“ wayne mgonjwa wako amepatwa na ugonjwa wa kupooza upande mmoja wa kulia.”
“ Ouh my God !! ..” Nikasema kwa sauti kubwa mikono yangu ikiwa kichwani.Daktari akanitazama na kusema
“ Tulidhani labda tatizo hili limetokana na shinikizo la damu lakini kwa Clara kila kitu kiko katika hali ya kawaida.Vipimo vyote vinaonyesha hakuna tatizo.Bado tunataka kundelea kufanya uchunguzi zaidi ili tuweze kufahamu nini chanzo cha ugonjwa huu.Hata sisi imetushangaza kidogo” akasema Daktari kisha akanyamaza akanitazama na kuendelea.
“ Ugonjwa huu umekuwa ukiwapata watu wengi kwa siku za karibuni .Lakini kwa upande wa Clara hali ni tofauti kidogo hivyo itatulazimu tufanye uchunguzi wa kina tujue nini chanzo cha tatizo hili Kwa sasa kuna kipimo kimoja ambacho tunahitaji kukifanya lakini kwa bahati mbaya mashine yetu imeharibika kwa hiyo itakulazimu uende jijini arusha kwa ajili ya kipimo cha CT Scan.” Akasema daktari..
“ Daktari naomba uniambie tafadhali..Clara atapona ? Ataweza kutembea tena kama zamani? Nikauliza maswali mfululizo.Daktari akanitazama na kusema
‘ Wayne usiwe na hofu ,mgonjwa atapona ingawa siwezi kukwambia lini anaweza akapata nafuu.Tiba kubwa ya ugonjwa huu ni mazoezi .Baada ya kujiridhisha na vipimo vyote kwamba hakuna tatizo lingine basi tutaanza kumfanyisha mazoezi mara moja ” Akasema daktari..
Pamoja na maneno yale ya kutia moyo ya daktari,niliinama na kuzama katika mawazo mengi sana.Nilijaribu kutafakari lakini nikakosa majibu . Nilihisi kama dunia inaniadhibu..
Niliongozana na daktari kwenda kumuona Clara aliyekuwa amelazwa katika chumba maalum cha peke yake.
Nilidondosha machozi nilipomshuhudia mwanamke ambaye masaa machache yaliyopita alikuwa na uzuri usioelezka lakini kwa sasa hata sura yake ilikuwa imebadilika.Alikuwa amelala kitandani hajitambui,rangi ya ngozi yake ilianza kuwa na weusi na mdomo wake ulikuwa umepinda tofauti na ulivyokuwa awali.
Beka na Chris wakawasili kila mmoja na gari lake na kila mmoja alistuka mno kwa hali aliyokuwa nayo Clara.
“ Wayne nina ushauri mmoja..” akasema Chris .
“ Kwa nini tusimuhamishe Clara na kumpeleka jijini Arusha.Kwa sasa kumefunguliwa hospitali moja kubwa ya kimataifa inayotibu magonjwa kama huu uliompata Clara.Kuna mabingwa wa kutibu ugonjwa huu toka nchini Marekani” akashauri Chris.Kwa pamoja tukashauriana na kuafikiana kwamba tumuhamishe Clara na kumpeleka katika hospitali hiyo mpya aliyoshauri Chris.
***************************
" Mganga nakuahidi kurudi tena nikiwa na zawadi nzuri sana ambayo hutaamini." akasema Emmy akiwa na tabasamu pana sana.
" Emmy nimekuhakikishia kwamba huyu mwaanume lazima atarudi kwako na hataondoka tena.Safari hii atakupenda kupita maelezo.Atafanya kila utakalomuamuru alifanye." akasema mganga
" Sipati neno la kukushukuru mganga..lakini utaona mwenyewe zawadi nitakayokuletea " akasema Emmy.Mganga akatoka kidogo na baada ya muda akarejea akiwa na kibuyu chenye dawa.
" Emmy ninakupa dawa hii.Hii ni dawa yenye nguvu sana na unatakiwa uipake mwilini pale tu unapokwenda kuonana na Wayne.Kwa sasa unatakiwa umtafute kwa udi na uvumba hadi umuone lakini usijaribu kumpigia simu.Unatakiwa umstukize .Wakati unakwenda kuonana naye unatakiwa ujipake dawa hii pekee na usichanganye na mafuta ya aina yoyote ile.Hilo ndilo sharti pekee la dawa hii.Ninakuhakikishia kwamba Wayne akikuona tu atastuka mno na dakika hiyo hiyo atakuomba msamaha na mtarudiana tena..." akasema mzee mtuguru na kisha wakaagana na Emmy akaanza safari ya kurejea Arusha.
" Wayne huwezi kunikimbia hata kidogo..wewe ni wangu pekee na siku zote utakuwa wangu..Hahahahaaa namuonea huruma huyo mwanamitindo wako..kwisha kazi yake.Sasa tuone hayo maringo na mikogo yake kama vitakuwepo tena.Nilimuonya asicheze na mali za watu lakini hakusikia.Hahahaaa..ukiona vimeng'aa ujue vimeng;arishwa." akawaza Emmy akiwa katika gari akirejea jijini Arusha.Alikuwa na furaha isiyo kifani nantabasamu halikukauka usoni mwake.
" Japokuwa bado nina majonzi ya kufiwa na mwanangu Baraka lakini ninafuraha kwa upande mwingine kwa sababu ninakwenda tena kurudiana na Wayne.Mimi ni mwanamke wa shoka nimempigania Wayne na mpaka sasa nimefanikiwa kumrejesha tena mikononi mwangu.Safari hii habanduki na hata hao wanga waliokuwa wananiroga ili nigombane na Wayne kwa sasa hawaniwezi tena.Kwa tiba niliyopewa mimi ni kisiki cha mpingo.Hakuna atakayeniweza kwa sasa.Nimejaa kinga kila mahala." akaendelea kuwaza Emmy.
" Kuna kitu nimekumbuka.Sheila alinidokeza kwamba James anaweza akarejea muda wowote katika wiki ijayo.Sijui itakuwaje akisikia kwamba mwanae Baraka amefariki dunia.Ah ! hilo halinihusu kwa sasa akili yangu yote ni kwa Wayne.Baada ya kumrejesha Wayne kwangu ndiyo nitaanza kushughulika na James.Nitamuweka sawa na atanielewa japokuwa itamuumiza sana kwa sababu hakuwahi kumuona mwanae kwani alipoondoka kwenda masomoni Urusi aliniacha nikiwa na mimba changa kabisa na toka wakati ule hajawahi kurejea tena.Ataumia lakini hakuna namna ya kufanya kumrejesha Baraka.Inauma sana lakini nimefanya haya yote kwa ajili ya kulipigania penzi langu.Safari hii ninataka nipate mtoto na Wayne.Nilifanya makosa makubwa sana kuzaa nje ya ndoa.Laiti kama ningezaa na Wayne haya yote yasingenikuta.Sijielewi ni kwa nini sikuwa naridhika na mume wangu hadi nikawa natoka na kwenda kubadilisha wanaume kama nguo .Wayne alinipa kila nilichokihitaji lakini bado nilitoka nje ya ndoa.Lazima nilikuwa nimerogwa.Safari hii watanikoma.." akawaza Emmy
*********************
Emmy alikuwa akiendesha gari lake kwa kasi kubwa kuwahi jijini Arusha.Uso wake haukukaukiwa na tabasamu .
" Ngoja nimpigie simu Sheila simu nimtaarifu juu ya mambo yanavyokwenda japokuwa alikimbia na kuniacha peke yangu." akawaza Emmy kisha akapunguza mwendo wa gari akachukua simu na kuzitafuta namba za simu za Sheila rafiki yake mkubwa akampigia.
" Halo Emmy, niambie shoga yangu" akasema Sheila baada ya kupokea simu ya Emmy
" Sheila mambo yanakwenda vizuri sana" akajibu Emmy huku akitabasamu
" Kivipi Emmy? akauliza Sheila ambaye sauti yake ilionekana dhahiri hakuwa akiyafurahia maongezi yale na Emmy
" Sheila yule mwanamitindo wa Wayne kwisha habari yake."
" Kwisha habari yake ! Mbona sikuelewi Emmy una maanisha nini ? akauliza Sheila
" Tayari nimekwisha mdondosha.Hatainuka tena" akajibu Emmy huku akicheka kicheko cha chini chini.Kikapita kimya cha sekunde kadhaa
" Hallo Sheila upo ." akaita Emmy baada ya kimya kile cha ghafla.
" Nipo Emmy..Nimestuka sana kwa jambo uliloniambia.Ina maana amekufa yule mwanamitindo? akauliza Sheila
" Hapana sijamuua japokuwa nilikuwa na nafasi hiyo. Nilichokifanya ni kwamba nimempa ulemavu wa kudumu na hatainuka tena katika maisha yake.Hivi ninavyokwambia amepelekwa hospitali na hataweza kuinuka wala kutembea tena.Amepooza mwili.Hili ni fundisho kwake kuvamia mabwana wa watu" akasema Emmy.Sheila akavuta pumzi ndefu
" Sheila niko njiani ninarudi.Tutaongea mengi nikisha fika.Bado kuna kazi ninataka unisaidie "
" Nikusaidie tena?.Kuna kazi unataka nikusaidie? .Sheila akauliza kwa mshangao.
" Ndiyo ..mbona umestuka?
" Lazima nistuke Emmy .Wewe ni rafiki yangu wa muda mrefu na lazima nikueleze ukweli.Kwa sasa unatakiwa utulie Emmy.Vitendo unavyoendelea kuvifanya si vya kiungwana na havitakupeleka popote. Nakwambia hivyo kama rafiki yako na mtu ninayekupenda . Nimekwisha ona mwisho wa watu waliojihusisha na masuala hayo ya ushirikina .Siku zote mwisho wao huwa si mzuri hata kidogo.Angalia shoga yangu ni hivi majuzi tu umempoteza mwanao Baraka.Hata wiki moja haijapita Clara naye anapatwa na matatizo. Mpaka lini Emmy utaendelea kuwatesa watu? Hadi lini utaendelea kumtesa Wayne? Clara unayemtesa kitandani amekukosea kitu gani? Watu wengi wanazidi kuteseka kwa sababu yako Emmy. Tafadhali hebu achana na hayo mambo ya kishirikina.Muache Wayne aendelee na maisha yake.Ulishindwa kumtunza na kwa sasa muache afurahie maisha mengine aliyoyanza.Mtegemee Mungu na kama ikimpendeza kumrudisha Wayne kwako atafanya hivyo lakini si kwa kuwategemea waganga wa kienyeji..Emm................" Kabla Sheila hajaendelea Emmy ambaye uso wake ulikwisha jikunja kwa hasira kutokana na maneno ya shoga yake akainglia kati.
" Sheila unaongea maneno gani hayo? Mbona sikuelewi ? Wewe ndiye wa kuniambia maneno kama hayo leo ..?akafoka Emmy.
" Emmy ngoja nimalizie kile ninachotaka kukwambia...." akasema Sheila.Emmy akapunguza mwendo wa gari na kuliegesha kandoni mwa bara bara.
" Emmy napenda ufahamu kwamba mimi sikukifurahia kabisa kitebdo cha kunishirikisha katika masuala yako ya kishirikina.Wazazi wangu hawakunikuza katika misingi ya kuamini mambo kama hayo.Kitendo cha kunipeleka kwa yule mganga na kusababisha akanifanyia kitendo kama alichonifanyia bado kinaniuma mno.Sijui hata nifanye nini ili niweze kuifuta taswira ya kitendo kile katika akili yangu.Nimeumia sana Emmy na kwa maana hiyo naomba ufahamu kwamba urafiki wetu kwa sasa utakuwa na mipaka.Kama unataka urafiki wetu uendelee nakushauri achana kabisa na hayo mambo ya kishirikina ambayo hayana faida yoyote kwako.Ndoa yako umeivuruga wewe mwenyewe na kwa sasa umeanza kuhangaika kumtafuta mchawi wakati mchawi ni wewe mwenyewe.Nakushaur........................."
" Bastard.....!!!" Emmy akakata simu kwa hasira na kuitupa kitini.
" Stupid girl !!..akasema kwa hasira.
" Sheila leo anathubutu kunitamkia maneno kama haya ? Bado siamini kama hata Sheila naye amenigeuka.Mimi nimekuwa mtu wake wa karibu na nimemsaidia katika mambo yake mengi ikiwa ni pamoja na kumkopesha hata mtaji wa kufungua saluni ile anayoringia kwa sasa halafu leo hii ananitamkia maneno kama haya .!!..Hapana siwezi kukubali kudharauliwa na paka kama Sheila. Anaishi mjini kwa sababu yangu mimi na hakupaswa hata kidogo kunidharau.Kwa kuwa naye ameamua kunidharau basi nitamjumuisha katika orodha ya maadui zangu.Nitamuonyesha kazi.Nitamfundisha adabu.Nadhani bado hajanifahamu vizuri" akawaza Emmy akiwa amefura kwa hasira.
" Ninaapa Sheila lazima alikimbie jiji.Nitayafanya maisha yake magumu sana na lazima aje anipigie magoti..." akasema kwa sauti ya hasira kisha akawasha gari lake na kuendelea na safari ....
*************************
Wazo alilolitoa Chris la kumuhamishia Clara katika hospitali kubwa ya St Patrick inayomilikiwa na wamisionari lilikubaliwa hata na madaktari wa pale hospitali ya rufaa ya KCMC. Bila kupoteza muda taratibu zikaanza kufanyika na baada ya dakika chache kila kitu kikawa tayari Clara akapakiwa katika gari la wagonjwa na safari ya kuelekea Arusha ikaanza.Clara alikuwa amelala kitandani macho ameyafumba.Nilishindwa kujizuia kudondosha machozi niliposhuhudia akipakiwa garini.Chris aljitahidi kunisihi niwe mvumilivu katika wakati ule mgumu.Hata kama ungekuwa ni wewe mpenzi msomaji sina hakika kama ungeweza kuvumilia kumuona mtu unayempenda ambaye muda mfupi uliopita ulikuwa ukiongea naye na kucheka lakini ghafla anabadilika na haongei tena.
" Chris sijui nimemkosea nini Mungu .Ninaona ni kama ninaadhibiwa kila kukicha.Wakati nikiamini kwamba kwa sasa matatizo yote ninayaacha nyuma lakini linaibuka tena tatizo lingine. Sikutegemea kama lngetokea jambo kama hili kwa wakati kama huu.Clara alikuwa mzima wa afya na hakuwa na dalili zozote za ugonjwa .Sielewi ni kwa nini mambo haya yote yananitokea mimi tu..." nikamwambia Chris nikiwa katika gari lake tukielekea jijini Arusha tukimpeleka Clara katika hospitali ya St Patrick.
" Wayne naomba usife moyo ndugu yangu.Mungu wetu ni mwema sana na siku zote amekuwa akitusamehe makosa yetu hata tunapomkosea namna gani.Hii ni mitihani tu ya maisha ambayo hatuna budi kukabiliana nayo na inaweza ikampata mtu yeyote yule.Kitu cha msingi ni kukabiliana na ugonjwa huu wa Clara hadi apone.Nina uhakika katika hospitali ile ya St Patrick watamsaidia Clara na atapona kwa sababu kuna mama wa rafiki yangu naye alipatwa na matatizo kama haya ya Clara na akapelekwa pale lakini alipona na hadi sasa hivi huwezi kuamini kama alikuwa amepooza na hakuweza kuongea kwa muda wa miezi zaidi ya sita.Nina uhakika mkubwa sana hata Clara atapona na ataendelea na maisha yake kama kawaida." akasema Chris.
" Ninafikiria labda nimuhamishie nje ya nchi.." nikasema.
" Hapana Wayne.Bado ni mapema sana kufanya maamuzi hayo ya kumpeleka Clara nje ya nchi.Ugonjwa huu unaweza ukatibika hata hapa nchini.Kama litakuwa ni suala la kumpeleka nje ya nchi basi madaktari watatushauri hivyo lakini sina hakika kama kuna ulazima wa kumpeleka nje ya nchi" akasema Chris.
Sura ya Clara haikuweza kuondoka kichwani kwangu.Bado niliendelea kumuona akiwa katika tabasamu na kicheko chake kidogo
" masikini Clara..!!.." nikasema na kutoa kitambaa nikayafuta machozi ambayo nilishindwa kuyazuia kunitoka
" Its ok Wayne..usihuzunike sana .Clara atapona tu.Tunachopaswa kwa sasa ni kumuomba Mungu ampe uponaji wa haraka" akanipa moyo Chris.
" Chris hakuna ajuaye uchungu ninaousikia moyoni mwangu kwa sasa.Ninahisi ni kama moyo wangu unakatwa vipande vipande na kisu kikali sana.Ninasikia machungu ambayo hayaelezeki kwa maneno.Clara alikuwa ni maisha yangu.Clara alikuwa ni kila kitu kwangu. Clara amenifanya niyafurahie maisha japo kwa muda huu mfupi niliokaa naye. Clara ni mwanamke wa tofauti sana.Ana moyo wa ajabu na wa kipekee kabisa.Ana upendo wa dhati na wa kweli.Upendo wake unatoka ndani kabisa ya moyo wake.Kwangu mimi Clara namchukulia ni kama malaika anayeishi..Sikutegema hata siku moja kama angeweza kupatwa na maradhi kama haya.She doesnt deserve this Ouh Clara.why you..!!!..."
Chris akanitazama kisha akaendelea kuendesha gari.
" pamoja na yote yaliyotokea bado upendo wangu kwa Clara hauwezi kupungua.Hata kama itamchukua maisha yake yote akiwa kitandani..nitampenda Clara hadi siku ninaingia kaburini." nikasema nikiwa nimeinama chini.Kikapita kimya cha sekunde kadhaa Chris akasema
" Wayne kuna kitu nakifikiria"...Nikainua kichwa na kumtazama
" Kitu gani Chris? nikauliza
" I'm sorry to say this but I have bad feelings" akasema Chris
" What feelings? nikauliza.Chris akakaa kimya kidogo halafu akasema
" Inawezakana Emmy akawa anahusika na ugonjwa huu wa Clara" akasema Chris.Maneno yale ya Chris yakaifanya akili yangu ianze kufunguka .Muda huu wote sikuwa nimemuwaza tena Emmy.Akili yangu haikuweza kumkumbuka tena.
" Kwa nini umewaza hivyo Chris.? nikauliza
" Nimewaza hivyo kwa sababu ninamfahamu Emmy ana roho ngumu sana.Kama ameweza kumuua mwanae wa kumzaa mwenyewe hatashindwa kufanya kitu kama hiki kwa Clara.Hayo ni mawazo yangu tu Wayne na sina uhakika kama yanaweza kuwa ya kweli ama la" akasema Chris.Nilikuwa ni kama mtu niliyepigwa na bumbuwazi.Nilizama ghafla katika mawazo mengi.
" Wayne unawaza nini? akauliza Chris
" Chris umenikumbusha jambo ambalo sikuwa nimelitilia maanani kabisa.Maelezo yako yamenifanya nipate picha fulani .Usiku ule alipofariki Baraka dakika chache tu kabla ya kupokea simu ya baba mkwe akinitaarifu kwamba Baraka amefariki dunia ,Clara alikurupuka ndotoni .Alikuwa anaweweseka na jasho jingi kumtoka.Nilimuuliza amepatwa na nini akaniambia kwamba ameota ndoto ya ajabu sana na ya kutisha.Nilimuuliza ni ndoto ya namna gani aliyoota lakini hakuwa tayari kuniambia.Aliniomba tupige magoti tusali na tumtegemee Mungu.Sikuelewa alimaanisha nini kwa maneno yale.Baada ya muda mfupi baba mkwe akanipigia simu na kunitaarifu kwamba Baraka amefariki dunia.Ni usiku ule ambao Emmy alikuwa amekwenda kwa mganga Tanga.Jana asubuhi Emmy hakuonekana tena msibani.Hakuna aliyefahamu alikuwa amekwenda wapi.Nimeanza kupata picha kwamba Emmy anahusika kwa kiasi kikubwa na ugonjwa huu wa Clara.Aliapa kwamba atayafanya maisha yangu magumu na hii ndiyo kazi anayoifanya.Kwa nini amtese Clara kiasi hiki? Amemkosea nini? Kama alikuwa na kisasi na mimi alitakiwa kunitesa mimi na si Clara asiye na kosa lolote lile.Niliyemuacha ni mimi na hakupaswa kabisa kumgusa Clara. Kama ni kweli ni yeye ndiye aliyemfanya Clara hivi I swear this time ameingia katika moto.Mungu atanisamehe kwa nitakachomfanyia hayawani huyu" nikasema huku nikiuma meno kwa hasira.Chris akanitazama na kusema
" Wayne,ninamfahamu Emmy ni mwanamke mwenye roho ngumu sana na siku zote huwa hakubali kushindwa kwa maana hiyo anaweza akafanya jambo lolote lile ili kukipata kile anachokitaka. Kama lengo lake lilikuwa ni kupamaba na wewe basi nina uhakika mkubwa kwamba anaweza akawa amemfanyia Clara vile ili kulipa kisasi kwako..." akasema Chris.
" I swear this time I'm going to kill her " nikasema kwa hasira
" Wayne usiseme hivyo na wala usiweke ahadi yoyote ya kulipiza kisasi.Bado hatuna uhakika kwamba ni yeye ndiye aliyefanya hivi.Hizi ni hisia zetu tu.Kama ni yeye ndiye aliyefanya kitendo hiki basi fahamu kwamba hizi ni kazi za shetani.Shetani si lolote mbele za Mungu.Tunachotakiwa kufanya sisi ni kumtegemea Mungu na atamponya Clara.Mungu ni muweza na hashindwi na lolote. Siku zote tunaambiwa tumtegemeze yeye pekee.Tumuombee Clara apone na tumuombee pia Emmy." akasema Chris.Nilishangaa kidogo baada ya kumsikia Chris akiongea maneno yale.Toka nimemfahamu Chris sikuwahi kumsikia akiongea maneno kama haya .
" Chris ! umeongea maneno ambayo yamenistua sana.Sikuwahi kukusikia hata mara moja ukiongea maneno kama haya uliyoyaongea leo." Chris akatabasamu kidogo kisha akasema
" Wayne sikuwa nimekuambia lakini mimi kwa sasa nimeamua kujiweka karibu zaidi na Mungu na kuachana na haya mambo ya kidunia.Nimamua kupokea wokovu.Baada ya kitendo kile kilichotokea baina yetu niliamua kupokea wokovu na kwa sasa mimi ni mtu mpya kabisa na ndiyo maana nina uhakika mkubwa kwamba Clara atapona kwa nguvu za Mungu" akasema Chris.Ni kweli Chris alikuwa amebadilika sana kuanzia tabia na maisha yake kwa ujumla.Bado niliendelea kumshangaa.
" Usisahangae Wayne.Nimeamua kuyabadili maisha yangu.Kwa sasa moyo wangu una furaha na amani.Ninayafurahia maisha yangu ya sasa.Nitamuomba baba askofu ambaye atakuwa anamfanyia maombi Clara kila siku .Kwa maombi yetu na jitihada za madaktari wetu Clara atakuwa mzima tena." akasema Chris.Maneno yale yakaanza kuniingia.Kwa wakati huu nilikuwa tayari kwa lolote lile ambalo lingeweza kumsaidia Clara aweze kupona.
Mara simu yangu ikaita alikuwa ni baba mkwe.Alitaka kufahamu hali ya mgonjwa ilivyokuwa inandelea.Yeye alikuwa katika maandalizi ya kuja Moshi nikamtaarifu kwamba tunamuhamishia Clara katika hospitali ya St Patrick jijini Arusha kwa hiyo hana haja ya kusafiri kuja Moshi.Baba mkwe akaniambia kwamba anatangulia hapo hospitali na tutamkuta pale.Nilifarijika sana kwa namna watu walivyoonyesha kuguswa na ugonjwa ule wa ghafla wa Clara.Tulikuwa nyuma ya gari la wagonjwa lililokuwa likienda kwa kasi kubwa huku likipiga king'ora kuashiria kwamba lilikuwa na mgonjwa ndani yake.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…
SEHEMU YA 29
MTUNZI : PATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Saa tatu za asubuhi tayari tulikwisha funga mizigo yetu kwa ajili ya safari.Nilimuomba rafiki yangu Beka atupeleke uwanja wa ndege wa Kilimajnaro halafu abaki na gari langu.Saa tatu na nusu safari ya kuelekea uwanja wa ndege ikaanza.Nilikuwa na furaha isiyo kifani kwani nilitegemea kwamba sasa karaha zote za Emmy nitaziacha nyuma na mimi kuishi maisha ya furaha na amani nikiwa na malaika wangu Clara.Tuliwasili uwanja wa ndege tukaagana na Beka na sisi kuingia sehemu ya kusubiria ndege .
Hatimaye muda wetu ukafika na tukaombwa tuelekee ndegeni.Taratibu tukiwa tumeshikana mikono tukaungana na abiria wengine kuelekea mahala ilipokuwa ndege tutakayosafiri nayo.Kabla hajaikanyaga ngazi ya ndege Clara akasimama.
“ Wayne naishiwa nguvu ..siwezi tena kunyanyua mguu wa…….” Hayo yalikuwa maneno ya mwisho ya Clara.Akaanguka na kabla hajafika chini nikawahi kumdaka.
ENDELEA………………………….
Emmy alikuwa amesimama mbele ya kioo kikubwa akiwa amefura na hasira na sura yake ameikunja..Kwa muda wa saa moja sasa alikuwa amesimama akitazama kioo kile kikubwa mfano wa luninga ,kilichokuwa kikimuonyesha kila kilichokuwa kinaendelea kati ya Wayne na Clara.Hakuwa ameongea chochote toka alipoanza kutazama luninga ile ikiwaonyesha Wayne na Clara walivyokuwa wanajiandaa kwa safari. Wayne na Clara wakiwa uwanjani walionekana ni wenye furaha kubwa .Walikuwa wamekaa wakisubiri zamu yao ya kupanda ndegeni ifike na baadae wakashikana mikono na kuanza kuelekea ndegeni.Clara akauma meno kwa hasira
“ Damn you Wayne..huwezi kunikimbia..Nitakutafuta usiku na mchana.Na huyo mwanamitindo wako ambaye amekupagawisha na kukufanya unitaliki atakiona cha moto..” akawaza Emmy .Muda wote huu mganga alikuwa amesimama pembeni yake akiwa na usinga wake mkononi akiupunga huku na huko huku akiongea maneno yake ya kiganga.
“ Emmy Wayne na Clara wanaondoka na bado haujafanya maamuzi yoyote.hii ni nafasi yako usiiache ikapita..Ukiacha wakiingia ndegeni na wakaiacha ardhi ya Arusha ,kurudi tena itakuwa vigumu mno.Kama bado unataka kuendelea na ile dhamira yako basi huu ndio wakati wake.Yeyote utakayemfunga siku ya leo hatapona hadi siku utakapokufa wewe.” Akasema mganga huku akimuonyeshea Emmy meza iliyokuwa na wanasesere wawili .Emmy hakusema kitu akageuka na kuiendea meza ile kisha akachagua mwanaserere mwenye umbo la mwanamke.Mganga akampa sindano.Emmy akasimama tena mbele ya kile kioo akawashuhudia Wayne na Clara wakikaribia kufika katika ngazi za kupandia ndege.Kwa hasira akauinua mkono wake wa kulia uliokuwa umeshika sindano ndefu na kuichoma upande wa kulia wa yule ukatoka moshi mweupe na sekunde ile ile Clara ambaye alikuwa anajiandaa kuikanyaga ngazi ya kupandia ndegeni akaanguka na hakuweza kuongea wala kuinuka tena.Emmy akatabasamu
" Leo nimekupata " akasema Emmy huku akitabasamu.
“ Kazi imekwisha” akasema mganga.
“ Kwa sasa huyu mwanamke kazi yake imekwisha.Nakuhakikishia Wayne lazima arudi kwako ndani ya muda mfupi. Atakufuata yeye mwenyewe.” Akajigamba mzee Mtuguru.
“ Nashukuru sana Mganga. Nakuahidi zawadi nzuri mno kama Wayne atafanikiwa kuja kwangu.” Akasema Emmy huku akitabasamu
“ Usiseme kama atarudi kwako.nakuhakikishia lazima arudi kwako na safari hii hataweza kuondoka tena.” Mganga akazidi kumpa moyo Emmy.
*************************
Clara..!! Clara !! ..” Niliita kwa nguvu baada ya kumdaka Clara alipotaka kuanguka lakini hakuweza kusema chochote..Nilichanganyikiwa ghafla.Mtu ambaye sekunde chache zilizopita tumekuwa tukiongea vizuri na kucheka lakini ghafla hawezi kuongea tena.Haya yalikuwa ni mambo ya ajabu sana kunitokea.Sikujua Clara amepatwa na ugonjwa gani uliomtokea ghafla namna ile.
Watu waliokuwa karibu wakanisaidia kumbeba Clara na kumuweka pembeni.Bado kichwa changu kilikuwa kizito kuamini kilichotokea.Nilihisi ni kama mchezo wa kuigiza lakini kadiri dakika zilivyokuwa zikisonga ndivyo nilivyojikuta nikilazimika kuamini kwamba Clara alikuwa amepatwa na ugonjwa wa ghafla ambao sikufahamu ni ugonjwa gani.Pamoja na ujasiri wangu wote niliokuwa nao nilijikuta nikitetemeka kila nilipomuona Clara na hali aliyokuwa nayo.Macho yalikuwa yamefumba,hakuweza hata kufumbua jicho.Mwili wake haukuweza hata kutikisika.Machozi ya uchungu yakanitiririka.Wanaume wawili wa makamo ambao nao walikuwa ni wasafiri wakanivuta pembeni baada ya kuiona hali nilioyokuwa nayo.
“ Jipe moyo ndugu yangu..Mungu atakusaidia..” akasema mmoja wao aliyekuwa amevaa suti nyeusi..
“ Tatizo hasa la mwenzio ni nini? Akauliza mwingine aliyekuwa amekaa kushoto kwangu..Nikajikaza na kusema
“ Sifahamu tatizo ni nini ..imetokea ghafla tu akapatwa na ugonjwa ule..” nikajibu kwa ufupi.Tayari uongozi wa pale uwanjani ukataarifiwa kuhusiana na kilichokuwa kimetokea na kwa haraka likatolewa gari kwa ajili ya kumkimbiza Clara katika hospitali ya Rufaa ya KCMC.Kwa kasi ya aina yake wahudumu wa pale uwanjani wakampakia Clara katika gari na mimi nikaingia ndani ya gari lile kisha tukaondoka uwanjani pale kwa kasi kubwa.
Kila nilipokuwa namuangalia Clara nilishindwa kujizuia kutokwa na machozi.Sipati neno ambalo linaweza kuelezea uchungu niliokuwa nao kwa wakati ule.Rangi ya ngozi ya Clara ikaanza kubadilika na kuwa na weusi weusi..nikazidi kuogopa.Nawashukuru watu niliokuwa nao mle garini walijitahidi kwa kila namna walivyoweza kunipa moyo ingawa hata nao nyuso zao zilionyesha mstuko na uoga wa dhahiri.
“ Ouh Clara..nini kimekupata malaika wangu?.. Nilisema kwa uchungu nilipomtazama Clara akiwa amelala mle ndani ya gari hajitambui.Niliogopa sana kwa hali aliyokuwa nayo. Gari ilikuwa inakwenda kwa mwendo mkali sana lakini niliona kama inachelewa kufika hospitali ili Clara aanze kupatiwa matibabu.
Hatimaye tukawasili katika hospitali ya rufaa ya KCMC mjini Moshi na kwa haraka wauguzi wakampokea mgonjwa na kuanza kumshughulikia mara moja. Sampuli za damu na vipimo vingine vikachukuliwa na kupelekwa maabara kwa uchunguzi.
Nilitoa malezo mafupi kwa madaktari kuhusiana na jinsi ugonjwa ule wa Clara ulivyoanza halafu wakaniomba nikasubiri nje ili waendelee na uchunguzi wao.Niliwaomba madaktari wale wafanye kila linalowezekana ili kuokoa maisha ya Clara kwani hali aliyokuwa nayo ilikuwa inaogopesha mno.Miguu haikuwa na nguvu nikatafuta sehemu nikakaa.Bado kichwa changu kilikuwa na mawazo mengi sana juu ya kilichotokea.Ilikuwa ni kama ndoto ya mchana na ilikuwa vigumu sana kuamini kilichotokea.Nilivuta picha ya kuanzia asubuhi tulipokuwa tunajiandaa kwa safari hii ambayo Clara hakutaka kuniambia tunaelekea wapi ingawa tiketi zetu zilionyesha kwamba tulikuwa tunaelekea Dar es salaam.Nikakumbuka tulivyoliacha jiji la Arusha nikiwa na matumaini kwamba nimeyaacha nyuma matatizo yote yaliyotokea kati yangu na Emmy.Sikutarajia kurejea tena Arusha.Niliamini kwamba ninakwenda kuanza maisha mapya nikiwa na malaika wangu Clara.Nilikumbuka tulivyoagana na rafiki yangu Beka pale uwanja wa ndege naye akarejea Arusha na gari langu.Nilimuahidi kuwa nikifika huko tunakokwenda ningemtaarifu kwa simu.Nikakumbuka pia tulivyokuwa tukipiga hatua kuelekea katika ndege na mara kumbu kumbu ambayo mpaka leo nikiikumbuka huwa inaniliza ikanijia kichwani. Ilikuwa ni kama ninatazama filamu.Clara alikuwa tayari ameinua mguu wake ili akanyage ngazi za ndege lakini hakuweza kufanya hivyo kwani alianguka ghafla na hakuweza kuongea tena.machopzi yakaanza kunitiririka tena.Nikafuta machozi nikachukua simu yangu na kumtaarifu rafiki yangu Beka kilichokuwa kimetokea.Hakuamini hata kidogo na alidhani ninamtania.Nilipomuhakikishia kwamba haukuwa utani aliamini na kunitaarifu kwamba tayari anaanza safari ya kuja Moshi kuungana nami katika wakati ule mgumu.Baada ya kuongea na Beka nikampigia simu baba mkwe na kumtaarifu kilichotokea halikadhalika naye akanitaarifu kwamba yuko njiani anakuna Moshi.Nikamtaarifu pia na Chris ambaye tayari tumekwisha maliza tofauti zetu . Kila mmoja niliyemtaarifu alistuka mno .hakuna aliyeamini moja kwa moja.
Nikiwa bado nimekaa pale nje nikiwasiliana na watu mbali mbali kuhusiana na kilichotokea,nikaitwa katika chumba cha daktari.Haraka haraka nikaingia na kuketi kitini.daktari akanitazama kisha akasema
“ Wayne tumemfanyia uchunguzi mgonjwa wako na tumegundua kwamba mgonjwa wako amepatwa na ugonjwa wa kupooza…”
“ What ? ..Unasema ??......Nikauliza kwa mshangao nikiwa nimesimama na macho kunitoka.Nilianza kusikia joto la ghafla.Hii ilikuwa ni taarifa ya kustusha sana.
“ Dakatari tafadhali naomba unielezee vizuri kwa ufasaha ili nikuelewe.Umesema Clara anaumwa nini? Nikauliza tena nikiwa bado nimesimama.
Kabla hajaendelea kunipa taarifa kuhusiana na ugonjwa wa Clara akaniomba niketi chini..
“ wayne mgonjwa wako amepatwa na ugonjwa wa kupooza upande mmoja wa kulia.”
“ Ouh my God !! ..” Nikasema kwa sauti kubwa mikono yangu ikiwa kichwani.Daktari akanitazama na kusema
“ Tulidhani labda tatizo hili limetokana na shinikizo la damu lakini kwa Clara kila kitu kiko katika hali ya kawaida.Vipimo vyote vinaonyesha hakuna tatizo.Bado tunataka kundelea kufanya uchunguzi zaidi ili tuweze kufahamu nini chanzo cha ugonjwa huu.Hata sisi imetushangaza kidogo” akasema Daktari kisha akanyamaza akanitazama na kuendelea.
“ Ugonjwa huu umekuwa ukiwapata watu wengi kwa siku za karibuni .Lakini kwa upande wa Clara hali ni tofauti kidogo hivyo itatulazimu tufanye uchunguzi wa kina tujue nini chanzo cha tatizo hili Kwa sasa kuna kipimo kimoja ambacho tunahitaji kukifanya lakini kwa bahati mbaya mashine yetu imeharibika kwa hiyo itakulazimu uende jijini arusha kwa ajili ya kipimo cha CT Scan.” Akasema daktari..
“ Daktari naomba uniambie tafadhali..Clara atapona ? Ataweza kutembea tena kama zamani? Nikauliza maswali mfululizo.Daktari akanitazama na kusema
‘ Wayne usiwe na hofu ,mgonjwa atapona ingawa siwezi kukwambia lini anaweza akapata nafuu.Tiba kubwa ya ugonjwa huu ni mazoezi .Baada ya kujiridhisha na vipimo vyote kwamba hakuna tatizo lingine basi tutaanza kumfanyisha mazoezi mara moja ” Akasema daktari..
Pamoja na maneno yale ya kutia moyo ya daktari,niliinama na kuzama katika mawazo mengi sana.Nilijaribu kutafakari lakini nikakosa majibu . Nilihisi kama dunia inaniadhibu..
Niliongozana na daktari kwenda kumuona Clara aliyekuwa amelazwa katika chumba maalum cha peke yake.
Nilidondosha machozi nilipomshuhudia mwanamke ambaye masaa machache yaliyopita alikuwa na uzuri usioelezka lakini kwa sasa hata sura yake ilikuwa imebadilika.Alikuwa amelala kitandani hajitambui,rangi ya ngozi yake ilianza kuwa na weusi na mdomo wake ulikuwa umepinda tofauti na ulivyokuwa awali.
Beka na Chris wakawasili kila mmoja na gari lake na kila mmoja alistuka mno kwa hali aliyokuwa nayo Clara.
“ Wayne nina ushauri mmoja..” akasema Chris .
“ Kwa nini tusimuhamishe Clara na kumpeleka jijini Arusha.Kwa sasa kumefunguliwa hospitali moja kubwa ya kimataifa inayotibu magonjwa kama huu uliompata Clara.Kuna mabingwa wa kutibu ugonjwa huu toka nchini Marekani” akashauri Chris.Kwa pamoja tukashauriana na kuafikiana kwamba tumuhamishe Clara na kumpeleka katika hospitali hiyo mpya aliyoshauri Chris.
***************************
" Mganga nakuahidi kurudi tena nikiwa na zawadi nzuri sana ambayo hutaamini." akasema Emmy akiwa na tabasamu pana sana.
" Emmy nimekuhakikishia kwamba huyu mwaanume lazima atarudi kwako na hataondoka tena.Safari hii atakupenda kupita maelezo.Atafanya kila utakalomuamuru alifanye." akasema mganga
" Sipati neno la kukushukuru mganga..lakini utaona mwenyewe zawadi nitakayokuletea " akasema Emmy.Mganga akatoka kidogo na baada ya muda akarejea akiwa na kibuyu chenye dawa.
" Emmy ninakupa dawa hii.Hii ni dawa yenye nguvu sana na unatakiwa uipake mwilini pale tu unapokwenda kuonana na Wayne.Kwa sasa unatakiwa umtafute kwa udi na uvumba hadi umuone lakini usijaribu kumpigia simu.Unatakiwa umstukize .Wakati unakwenda kuonana naye unatakiwa ujipake dawa hii pekee na usichanganye na mafuta ya aina yoyote ile.Hilo ndilo sharti pekee la dawa hii.Ninakuhakikishia kwamba Wayne akikuona tu atastuka mno na dakika hiyo hiyo atakuomba msamaha na mtarudiana tena..." akasema mzee mtuguru na kisha wakaagana na Emmy akaanza safari ya kurejea Arusha.
" Wayne huwezi kunikimbia hata kidogo..wewe ni wangu pekee na siku zote utakuwa wangu..Hahahahaaa namuonea huruma huyo mwanamitindo wako..kwisha kazi yake.Sasa tuone hayo maringo na mikogo yake kama vitakuwepo tena.Nilimuonya asicheze na mali za watu lakini hakusikia.Hahahaaa..ukiona vimeng'aa ujue vimeng;arishwa." akawaza Emmy akiwa katika gari akirejea jijini Arusha.Alikuwa na furaha isiyo kifani nantabasamu halikukauka usoni mwake.
" Japokuwa bado nina majonzi ya kufiwa na mwanangu Baraka lakini ninafuraha kwa upande mwingine kwa sababu ninakwenda tena kurudiana na Wayne.Mimi ni mwanamke wa shoka nimempigania Wayne na mpaka sasa nimefanikiwa kumrejesha tena mikononi mwangu.Safari hii habanduki na hata hao wanga waliokuwa wananiroga ili nigombane na Wayne kwa sasa hawaniwezi tena.Kwa tiba niliyopewa mimi ni kisiki cha mpingo.Hakuna atakayeniweza kwa sasa.Nimejaa kinga kila mahala." akaendelea kuwaza Emmy.
" Kuna kitu nimekumbuka.Sheila alinidokeza kwamba James anaweza akarejea muda wowote katika wiki ijayo.Sijui itakuwaje akisikia kwamba mwanae Baraka amefariki dunia.Ah ! hilo halinihusu kwa sasa akili yangu yote ni kwa Wayne.Baada ya kumrejesha Wayne kwangu ndiyo nitaanza kushughulika na James.Nitamuweka sawa na atanielewa japokuwa itamuumiza sana kwa sababu hakuwahi kumuona mwanae kwani alipoondoka kwenda masomoni Urusi aliniacha nikiwa na mimba changa kabisa na toka wakati ule hajawahi kurejea tena.Ataumia lakini hakuna namna ya kufanya kumrejesha Baraka.Inauma sana lakini nimefanya haya yote kwa ajili ya kulipigania penzi langu.Safari hii ninataka nipate mtoto na Wayne.Nilifanya makosa makubwa sana kuzaa nje ya ndoa.Laiti kama ningezaa na Wayne haya yote yasingenikuta.Sijielewi ni kwa nini sikuwa naridhika na mume wangu hadi nikawa natoka na kwenda kubadilisha wanaume kama nguo .Wayne alinipa kila nilichokihitaji lakini bado nilitoka nje ya ndoa.Lazima nilikuwa nimerogwa.Safari hii watanikoma.." akawaza Emmy
*********************
Emmy alikuwa akiendesha gari lake kwa kasi kubwa kuwahi jijini Arusha.Uso wake haukukaukiwa na tabasamu .
" Ngoja nimpigie simu Sheila simu nimtaarifu juu ya mambo yanavyokwenda japokuwa alikimbia na kuniacha peke yangu." akawaza Emmy kisha akapunguza mwendo wa gari akachukua simu na kuzitafuta namba za simu za Sheila rafiki yake mkubwa akampigia.
" Halo Emmy, niambie shoga yangu" akasema Sheila baada ya kupokea simu ya Emmy
" Sheila mambo yanakwenda vizuri sana" akajibu Emmy huku akitabasamu
" Kivipi Emmy? akauliza Sheila ambaye sauti yake ilionekana dhahiri hakuwa akiyafurahia maongezi yale na Emmy
" Sheila yule mwanamitindo wa Wayne kwisha habari yake."
" Kwisha habari yake ! Mbona sikuelewi Emmy una maanisha nini ? akauliza Sheila
" Tayari nimekwisha mdondosha.Hatainuka tena" akajibu Emmy huku akicheka kicheko cha chini chini.Kikapita kimya cha sekunde kadhaa
" Hallo Sheila upo ." akaita Emmy baada ya kimya kile cha ghafla.
" Nipo Emmy..Nimestuka sana kwa jambo uliloniambia.Ina maana amekufa yule mwanamitindo? akauliza Sheila
" Hapana sijamuua japokuwa nilikuwa na nafasi hiyo. Nilichokifanya ni kwamba nimempa ulemavu wa kudumu na hatainuka tena katika maisha yake.Hivi ninavyokwambia amepelekwa hospitali na hataweza kuinuka wala kutembea tena.Amepooza mwili.Hili ni fundisho kwake kuvamia mabwana wa watu" akasema Emmy.Sheila akavuta pumzi ndefu
" Sheila niko njiani ninarudi.Tutaongea mengi nikisha fika.Bado kuna kazi ninataka unisaidie "
" Nikusaidie tena?.Kuna kazi unataka nikusaidie? .Sheila akauliza kwa mshangao.
" Ndiyo ..mbona umestuka?
" Lazima nistuke Emmy .Wewe ni rafiki yangu wa muda mrefu na lazima nikueleze ukweli.Kwa sasa unatakiwa utulie Emmy.Vitendo unavyoendelea kuvifanya si vya kiungwana na havitakupeleka popote. Nakwambia hivyo kama rafiki yako na mtu ninayekupenda . Nimekwisha ona mwisho wa watu waliojihusisha na masuala hayo ya ushirikina .Siku zote mwisho wao huwa si mzuri hata kidogo.Angalia shoga yangu ni hivi majuzi tu umempoteza mwanao Baraka.Hata wiki moja haijapita Clara naye anapatwa na matatizo. Mpaka lini Emmy utaendelea kuwatesa watu? Hadi lini utaendelea kumtesa Wayne? Clara unayemtesa kitandani amekukosea kitu gani? Watu wengi wanazidi kuteseka kwa sababu yako Emmy. Tafadhali hebu achana na hayo mambo ya kishirikina.Muache Wayne aendelee na maisha yake.Ulishindwa kumtunza na kwa sasa muache afurahie maisha mengine aliyoyanza.Mtegemee Mungu na kama ikimpendeza kumrudisha Wayne kwako atafanya hivyo lakini si kwa kuwategemea waganga wa kienyeji..Emm................" Kabla Sheila hajaendelea Emmy ambaye uso wake ulikwisha jikunja kwa hasira kutokana na maneno ya shoga yake akainglia kati.
" Sheila unaongea maneno gani hayo? Mbona sikuelewi ? Wewe ndiye wa kuniambia maneno kama hayo leo ..?akafoka Emmy.
" Emmy ngoja nimalizie kile ninachotaka kukwambia...." akasema Sheila.Emmy akapunguza mwendo wa gari na kuliegesha kandoni mwa bara bara.
" Emmy napenda ufahamu kwamba mimi sikukifurahia kabisa kitebdo cha kunishirikisha katika masuala yako ya kishirikina.Wazazi wangu hawakunikuza katika misingi ya kuamini mambo kama hayo.Kitendo cha kunipeleka kwa yule mganga na kusababisha akanifanyia kitendo kama alichonifanyia bado kinaniuma mno.Sijui hata nifanye nini ili niweze kuifuta taswira ya kitendo kile katika akili yangu.Nimeumia sana Emmy na kwa maana hiyo naomba ufahamu kwamba urafiki wetu kwa sasa utakuwa na mipaka.Kama unataka urafiki wetu uendelee nakushauri achana kabisa na hayo mambo ya kishirikina ambayo hayana faida yoyote kwako.Ndoa yako umeivuruga wewe mwenyewe na kwa sasa umeanza kuhangaika kumtafuta mchawi wakati mchawi ni wewe mwenyewe.Nakushaur........................."
" Bastard.....!!!" Emmy akakata simu kwa hasira na kuitupa kitini.
" Stupid girl !!..akasema kwa hasira.
" Sheila leo anathubutu kunitamkia maneno kama haya ? Bado siamini kama hata Sheila naye amenigeuka.Mimi nimekuwa mtu wake wa karibu na nimemsaidia katika mambo yake mengi ikiwa ni pamoja na kumkopesha hata mtaji wa kufungua saluni ile anayoringia kwa sasa halafu leo hii ananitamkia maneno kama haya .!!..Hapana siwezi kukubali kudharauliwa na paka kama Sheila. Anaishi mjini kwa sababu yangu mimi na hakupaswa hata kidogo kunidharau.Kwa kuwa naye ameamua kunidharau basi nitamjumuisha katika orodha ya maadui zangu.Nitamuonyesha kazi.Nitamfundisha adabu.Nadhani bado hajanifahamu vizuri" akawaza Emmy akiwa amefura kwa hasira.
" Ninaapa Sheila lazima alikimbie jiji.Nitayafanya maisha yake magumu sana na lazima aje anipigie magoti..." akasema kwa sauti ya hasira kisha akawasha gari lake na kuendelea na safari ....
*************************
Wazo alilolitoa Chris la kumuhamishia Clara katika hospitali kubwa ya St Patrick inayomilikiwa na wamisionari lilikubaliwa hata na madaktari wa pale hospitali ya rufaa ya KCMC. Bila kupoteza muda taratibu zikaanza kufanyika na baada ya dakika chache kila kitu kikawa tayari Clara akapakiwa katika gari la wagonjwa na safari ya kuelekea Arusha ikaanza.Clara alikuwa amelala kitandani macho ameyafumba.Nilishindwa kujizuia kudondosha machozi niliposhuhudia akipakiwa garini.Chris aljitahidi kunisihi niwe mvumilivu katika wakati ule mgumu.Hata kama ungekuwa ni wewe mpenzi msomaji sina hakika kama ungeweza kuvumilia kumuona mtu unayempenda ambaye muda mfupi uliopita ulikuwa ukiongea naye na kucheka lakini ghafla anabadilika na haongei tena.
" Chris sijui nimemkosea nini Mungu .Ninaona ni kama ninaadhibiwa kila kukicha.Wakati nikiamini kwamba kwa sasa matatizo yote ninayaacha nyuma lakini linaibuka tena tatizo lingine. Sikutegemea kama lngetokea jambo kama hili kwa wakati kama huu.Clara alikuwa mzima wa afya na hakuwa na dalili zozote za ugonjwa .Sielewi ni kwa nini mambo haya yote yananitokea mimi tu..." nikamwambia Chris nikiwa katika gari lake tukielekea jijini Arusha tukimpeleka Clara katika hospitali ya St Patrick.
" Wayne naomba usife moyo ndugu yangu.Mungu wetu ni mwema sana na siku zote amekuwa akitusamehe makosa yetu hata tunapomkosea namna gani.Hii ni mitihani tu ya maisha ambayo hatuna budi kukabiliana nayo na inaweza ikampata mtu yeyote yule.Kitu cha msingi ni kukabiliana na ugonjwa huu wa Clara hadi apone.Nina uhakika katika hospitali ile ya St Patrick watamsaidia Clara na atapona kwa sababu kuna mama wa rafiki yangu naye alipatwa na matatizo kama haya ya Clara na akapelekwa pale lakini alipona na hadi sasa hivi huwezi kuamini kama alikuwa amepooza na hakuweza kuongea kwa muda wa miezi zaidi ya sita.Nina uhakika mkubwa sana hata Clara atapona na ataendelea na maisha yake kama kawaida." akasema Chris.
" Ninafikiria labda nimuhamishie nje ya nchi.." nikasema.
" Hapana Wayne.Bado ni mapema sana kufanya maamuzi hayo ya kumpeleka Clara nje ya nchi.Ugonjwa huu unaweza ukatibika hata hapa nchini.Kama litakuwa ni suala la kumpeleka nje ya nchi basi madaktari watatushauri hivyo lakini sina hakika kama kuna ulazima wa kumpeleka nje ya nchi" akasema Chris.
Sura ya Clara haikuweza kuondoka kichwani kwangu.Bado niliendelea kumuona akiwa katika tabasamu na kicheko chake kidogo
" masikini Clara..!!.." nikasema na kutoa kitambaa nikayafuta machozi ambayo nilishindwa kuyazuia kunitoka
" Its ok Wayne..usihuzunike sana .Clara atapona tu.Tunachopaswa kwa sasa ni kumuomba Mungu ampe uponaji wa haraka" akanipa moyo Chris.
" Chris hakuna ajuaye uchungu ninaousikia moyoni mwangu kwa sasa.Ninahisi ni kama moyo wangu unakatwa vipande vipande na kisu kikali sana.Ninasikia machungu ambayo hayaelezeki kwa maneno.Clara alikuwa ni maisha yangu.Clara alikuwa ni kila kitu kwangu. Clara amenifanya niyafurahie maisha japo kwa muda huu mfupi niliokaa naye. Clara ni mwanamke wa tofauti sana.Ana moyo wa ajabu na wa kipekee kabisa.Ana upendo wa dhati na wa kweli.Upendo wake unatoka ndani kabisa ya moyo wake.Kwangu mimi Clara namchukulia ni kama malaika anayeishi..Sikutegema hata siku moja kama angeweza kupatwa na maradhi kama haya.She doesnt deserve this Ouh Clara.why you..!!!..."
Chris akanitazama kisha akaendelea kuendesha gari.
" pamoja na yote yaliyotokea bado upendo wangu kwa Clara hauwezi kupungua.Hata kama itamchukua maisha yake yote akiwa kitandani..nitampenda Clara hadi siku ninaingia kaburini." nikasema nikiwa nimeinama chini.Kikapita kimya cha sekunde kadhaa Chris akasema
" Wayne kuna kitu nakifikiria"...Nikainua kichwa na kumtazama
" Kitu gani Chris? nikauliza
" I'm sorry to say this but I have bad feelings" akasema Chris
" What feelings? nikauliza.Chris akakaa kimya kidogo halafu akasema
" Inawezakana Emmy akawa anahusika na ugonjwa huu wa Clara" akasema Chris.Maneno yale ya Chris yakaifanya akili yangu ianze kufunguka .Muda huu wote sikuwa nimemuwaza tena Emmy.Akili yangu haikuweza kumkumbuka tena.
" Kwa nini umewaza hivyo Chris.? nikauliza
" Nimewaza hivyo kwa sababu ninamfahamu Emmy ana roho ngumu sana.Kama ameweza kumuua mwanae wa kumzaa mwenyewe hatashindwa kufanya kitu kama hiki kwa Clara.Hayo ni mawazo yangu tu Wayne na sina uhakika kama yanaweza kuwa ya kweli ama la" akasema Chris.Nilikuwa ni kama mtu niliyepigwa na bumbuwazi.Nilizama ghafla katika mawazo mengi.
" Wayne unawaza nini? akauliza Chris
" Chris umenikumbusha jambo ambalo sikuwa nimelitilia maanani kabisa.Maelezo yako yamenifanya nipate picha fulani .Usiku ule alipofariki Baraka dakika chache tu kabla ya kupokea simu ya baba mkwe akinitaarifu kwamba Baraka amefariki dunia ,Clara alikurupuka ndotoni .Alikuwa anaweweseka na jasho jingi kumtoka.Nilimuuliza amepatwa na nini akaniambia kwamba ameota ndoto ya ajabu sana na ya kutisha.Nilimuuliza ni ndoto ya namna gani aliyoota lakini hakuwa tayari kuniambia.Aliniomba tupige magoti tusali na tumtegemee Mungu.Sikuelewa alimaanisha nini kwa maneno yale.Baada ya muda mfupi baba mkwe akanipigia simu na kunitaarifu kwamba Baraka amefariki dunia.Ni usiku ule ambao Emmy alikuwa amekwenda kwa mganga Tanga.Jana asubuhi Emmy hakuonekana tena msibani.Hakuna aliyefahamu alikuwa amekwenda wapi.Nimeanza kupata picha kwamba Emmy anahusika kwa kiasi kikubwa na ugonjwa huu wa Clara.Aliapa kwamba atayafanya maisha yangu magumu na hii ndiyo kazi anayoifanya.Kwa nini amtese Clara kiasi hiki? Amemkosea nini? Kama alikuwa na kisasi na mimi alitakiwa kunitesa mimi na si Clara asiye na kosa lolote lile.Niliyemuacha ni mimi na hakupaswa kabisa kumgusa Clara. Kama ni kweli ni yeye ndiye aliyemfanya Clara hivi I swear this time ameingia katika moto.Mungu atanisamehe kwa nitakachomfanyia hayawani huyu" nikasema huku nikiuma meno kwa hasira.Chris akanitazama na kusema
" Wayne,ninamfahamu Emmy ni mwanamke mwenye roho ngumu sana na siku zote huwa hakubali kushindwa kwa maana hiyo anaweza akafanya jambo lolote lile ili kukipata kile anachokitaka. Kama lengo lake lilikuwa ni kupamaba na wewe basi nina uhakika mkubwa kwamba anaweza akawa amemfanyia Clara vile ili kulipa kisasi kwako..." akasema Chris.
" I swear this time I'm going to kill her " nikasema kwa hasira
" Wayne usiseme hivyo na wala usiweke ahadi yoyote ya kulipiza kisasi.Bado hatuna uhakika kwamba ni yeye ndiye aliyefanya hivi.Hizi ni hisia zetu tu.Kama ni yeye ndiye aliyefanya kitendo hiki basi fahamu kwamba hizi ni kazi za shetani.Shetani si lolote mbele za Mungu.Tunachotakiwa kufanya sisi ni kumtegemea Mungu na atamponya Clara.Mungu ni muweza na hashindwi na lolote. Siku zote tunaambiwa tumtegemeze yeye pekee.Tumuombee Clara apone na tumuombee pia Emmy." akasema Chris.Nilishangaa kidogo baada ya kumsikia Chris akiongea maneno yale.Toka nimemfahamu Chris sikuwahi kumsikia akiongea maneno kama haya .
" Chris ! umeongea maneno ambayo yamenistua sana.Sikuwahi kukusikia hata mara moja ukiongea maneno kama haya uliyoyaongea leo." Chris akatabasamu kidogo kisha akasema
" Wayne sikuwa nimekuambia lakini mimi kwa sasa nimeamua kujiweka karibu zaidi na Mungu na kuachana na haya mambo ya kidunia.Nimamua kupokea wokovu.Baada ya kitendo kile kilichotokea baina yetu niliamua kupokea wokovu na kwa sasa mimi ni mtu mpya kabisa na ndiyo maana nina uhakika mkubwa kwamba Clara atapona kwa nguvu za Mungu" akasema Chris.Ni kweli Chris alikuwa amebadilika sana kuanzia tabia na maisha yake kwa ujumla.Bado niliendelea kumshangaa.
" Usisahangae Wayne.Nimeamua kuyabadili maisha yangu.Kwa sasa moyo wangu una furaha na amani.Ninayafurahia maisha yangu ya sasa.Nitamuomba baba askofu ambaye atakuwa anamfanyia maombi Clara kila siku .Kwa maombi yetu na jitihada za madaktari wetu Clara atakuwa mzima tena." akasema Chris.Maneno yale yakaanza kuniingia.Kwa wakati huu nilikuwa tayari kwa lolote lile ambalo lingeweza kumsaidia Clara aweze kupona.
Mara simu yangu ikaita alikuwa ni baba mkwe.Alitaka kufahamu hali ya mgonjwa ilivyokuwa inandelea.Yeye alikuwa katika maandalizi ya kuja Moshi nikamtaarifu kwamba tunamuhamishia Clara katika hospitali ya St Patrick jijini Arusha kwa hiyo hana haja ya kusafiri kuja Moshi.Baba mkwe akaniambia kwamba anatangulia hapo hospitali na tutamkuta pale.Nilifarijika sana kwa namna watu walivyoonyesha kuguswa na ugonjwa ule wa ghafla wa Clara.Tulikuwa nyuma ya gari la wagonjwa lililokuwa likienda kwa kasi kubwa huku likipiga king'ora kuashiria kwamba lilikuwa na mgonjwa ndani yake.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO…