SIMULIZI: VIFO VYA WAPELELEZI (By FADDY)
SEHEMU YA PILI
........................................................................
"Eti Da Doris wale wageni waliokuja Asubuhi wameshaondoka?" (ilikuwa ni sauti ya Anusiata, Dada mfanya usafi katika hotel ya DP akimuuliza mfanyakazi mwenzake wa mapokezi (Receptionist) mida ya saa moja usiku.
"Mmh, hapana, hawajaondoka, kwani vipi?" (Doris alijibu huku akiwa na mshangao wa lile swali la Anusiata).
"Si uliwapatia vyumba viwili?, kimoja ni cha wale mabinti pacha na kingine ni cha yule mke na mume? (Anusiata aliendelea kumtupia swali jingine Doris)
"We nawe acha umbea, sasa hayo ndo maswali gani!!!, ulitaka mke na mume walale vyumba tofauti au? (Doris alijibu kwa hasira huku akiendelea na shughuli yake ya kuchapa maneno kwenye tanakilishi iliyopo hapo mapokezi)
"Jamani Da Doris, sina nia mbaya, nilitaka tu kujua, maana nilipoenda kwenye chumba cha wale mabinti kubadilisha mashuka nikakuta chumba kipo wazi na watu hawapo. Ila kile chumba cha mke na mume ndo kimefungwa kwa ndani, nikipiga hodi hawafungui" (Anusiata alijitetea)
"Basi itakuwa wapo bize na wazazi wao wanapiga stori, we kama umeshabadilisha hizo shuka kwenye chumba cha mabinti basi inatosha, fanya mambo yako. Hayo mengine waachie wenyewe" (Doris alijibu kwa mkato huku akionekana kukereka kwa yale maswali ya Anusiata).
Anusiata aliondoka kiunyonge ingawa moyoni alihisi kama kuna kitu kisicho cha kawaida kinachoendelea hapo hotelini. Maana tangu ile Familia iingie pale hotelini mida ya asubuhi hakuwaona tena kutoka kama wateja wengine wanavyotokaga mfano kuelekea nje kupunga upepo au kwenda kwenye mgahawa mdogo uliopo Ground floor hapo hotelini. Ila akaamua kupotezea na kuelekea Chumba cha kufulia (washing room) ili aendelee na majukumu yake. Akiwa yupo bize na shughuli ya kuchambua nguo chafu ili aziingize kwenye mashine ya kufulia ghafla ana tahamaki baada ya kukiona kidole cha binadamu kilichoanguka kutoka kwenye zile shuka alizotoa chumba namba 123 (chumba cha wale mabinti). Akiwa bado anashangaa, ghafla anapigwa roba na kuzibwa mdomo na mtu alie nyuma yake.
"shiiiiiii, ole wako upige kelele nitakipasua hiki kichwa, haya niambie kule mapokezi ulikuwa unaongea nini na yule malaya mwenzako ulipotoka chumba namba 123 kuchukua mashuka?" (sauti nzito ya kukoroma ilisikika kutoka kwa huyu jamaa aliyemkaba roba Anusiata huku akimwachia mdomo Anusiata aongee)
"Ni...ni...ni...nilikuwa namuomba funguo za baadhi ya vyumba nikachukue mashukaaaa, pliiz u...uu...siniue" (Anusiata aliongea kwa kigugumizi huku haja ndogo ikianza kumtoka)
"Na ulipoingia chumba namba 123, ulishuhudia nini?" (yule jambazi akauliza kwa ukali huku akimpa nafasi Anusiata ajieleze)
"Ha...ha...hapaaana si...si..jaona chochote mimi,unaniua bure" (Anusiata aliongea kwa sauti ila kelele za mashine ya kufulia ikawa imefanya asisikike hata nje)
"Kelele zako hapa hazitasaidia kitu alafu nilikwambia utulie. Na hicho kidole umekitoa wapi" (yule jambazi aliendelea kuuliza huku akimtaka Anusiata aache kupiga kelele)
"Nisamehe sitasema chochote mie, nakuahidi, sitaongea mimi.Niache usiniue" (Anusiata alizidi kujitetea huku akiwa hana matumaini tena ya kubaki salama)
"Sasa nisaidie jambo moja, humu ndani nipo na wenzangu, tulikodi chumba namba 129. Tuna mzigo wetu tunataka kutoka nao.Tuelekeze mlango wa siri wa kutoka hapa,na mimi nitakuacha salama.ukijifanya kiburi basi nakuua hapahapa," (yule mtekaji aliongea kwa msisitizo)
"Sawa sitosema chochote, twendeni nikawaonyeshe" (Anusiata aliitikia haraka ili kunusuru maisha yake)
Walitoka wote kwenye chumba kile cha kufulia huku akipewa maelekezo ya kujifanya yupo kawaida. Walitembea kama marafiki ingawa kila mmoja alikuwa na lake moyoni. Walitembea kama hatua 20 ndipo wakakifikia kile chumba walichopanga wale majambazi.
"Haya ingia humu" (yule mtekaji akaongea taratibu huku akimuangalia Anusiata)
"Boss, tushamaliza kazi huku na mzigo upo tayari. Ila tumeamua tubebe vyote vinne." (mmoja kati ya majambazi watatu waliopo ndani alikuwa akiongea na simu muda ambao anusiata na yule mtekaji wake wakiingia)
"Safi sana makamanda. Huyo mpuuzi alinisumbua sana, akadhani hatoingia kwenye kumi na nane zangu, hongereni vijana. Vipi lakini CCTV Camera muliweza kuzi-control?" (upande wa pili wa simu uliuliza)
"Ndio Boss, wale wanaohusika na camera tumewamaliza, na CAMERA RECORDER tumeondoka nayo. (kijana alizidi kueleza)
"Basi poa, tukutane ofisini mkitoka huko" (upande wa pili wa simu uliongea na kukata simu)
Baada ya maongezi yale, wakatoka katika chumba kile wote wanne na huyu binti wa usafi ambaye kwa mda huu sasa ndo muongoza njia jumla watano. Wakapita katika mlango ulioandikwa "EMERGENCY DOOR" ambao uliwafikisha katika lift na kushuka na hiyo lift hadi chini ya lile ghorofa. Walipotua wakapita nyuma ya ile hotel hadi pale walipoukuta mlango mwingine tena ulioandikwa "EMERGENCY DOOR" ambapo Anusiata aliufungua kwa funguo zake na wakatokea nje kabisa ya hotel ile.
"Sasa wadau, huyu binti tumfanye nini?, maana ashatutoa nje ya hotel (Yule jambazi mtekaji aliyemshikilia anusiata akawauliza wenzake)
"Tumuue tu, maana ameshaziona sura zetu" (mmoja akadakia na hapohapo akachukua bunduki yake yenye kiwambo cha kuzuia sauti na kummiminia Anusiata risasi zaidi ya nne kwenye kifua chake upande wa moyo)
"Jamaa, unakosea, hukutakiwa kumuua huyu binti bila kutusikiliza wengine tunasemaje, huyu angetusaidia kwa mapishi na usafi kule kambini" (yule jambazi aliyemteka Anusiata kule washing room akaongea huku akionesha kuchukizwa na kitendo cha mwenzake kumuua huyu dada)
"Acheni kulaumiana, mtu ameshakufa bas, muacheni hapo tusepe.( Mwingine akadakia huku akiusukumizia mwili wa Anusiata mtaroni)
Wakaondoka pale kwa kupita njia za vichochoroni na hatimae wakalifikia gari lao walilolipaki mtaa wa pili na kuondoka eneo lile.
.............................................................................................................................................................
NYUMBANI KWA MWAMBA WA CHUMA.
Ni nyumba kubwa ya kisasa, iliyopendezeshwa kwa bustani nzuri ya maua ya kila aina huku sanamu za wanyama mbalimbali kama simba,tembo na chui zilizochongwa kwa udongo zikizidi kupafanya mahali hapa paonekane kama ikulu ndogo. Ama hakika Mwamba wa chuma alijipanga kimaisha. Mshahara wake aliutendea haki, tofauti na wafanyakazi wengi ambao muda mwingi hufikiria starehe tu na anasa za dunia huku wakisahau kuwa ajira ni za muda mfupi tu, ipo siku utaziacha. Mbali na nyumba hiyo Mwamba wa chuma pia alikuwa na nyumba nyingine mbili zilizopo katika jiji la NAIBAS pamoja na vitega uchumi vingine vingi kama magari ya abiria, nyumba za kulala wageni na mashamba makubwa. Ama hakika, huyu ni Mwamba wa chuma kweli kweli, si tu kwenye fani yake ya upelelezi bali hata kwenye maisha nje ya fani yake.
Abdul Mohammed ni mtoto wa kwanza na wa mwisho wa Mzee Mohammed(Mwamba wa chuma). Ni mtoto pekee kwenye familia hii ya mzee Mohamed na mke wake Bi Nusrat au ukipenda muite Mama Abdul. Ni matatizo ya uzazi yaliyokuwa yakimsumbua Bi nusrat ndio yaliyosababisha wawe na mtoto huyo mmoja tu. Abdul mohammed ni msomi wa shahada ya pili (shahada ya uzamili) aliyoipata katika chuo kikuu cha sheria Bloomsbury London,Uingereza. Ingawa bado alikuwa akiishi na wazazi ila haikumfanya kutokuwa mchapakazi kama baba yake, sifa iliyopelekea na yeye kuingizwa katika kazi ya ushushushu ndani ya idara ya usalama wa Taifa la Beirad (BISA). Akiwa na miaka michache tu ndani ya Idara, aliweza kufatilia matukio mbalimbali ya yanayohatarisha usalama wa nchi na kuzuia majaribio kazaa ya uharifu.
Ni asubuhi na mapema, simu ya Mwamba wa chuma inaita. Anakurupuka kutoka usingizini na kuangalia mpigaji ni nani.
"Habari za asubuhi kamanda" ( sauti ilisikika upande wa pili baada ya Mwamba wa chuma kuipokea ile simu)
"Salama mkuu,vipi kuna tatizo?, naona asubuhi sana" (Mwamba wa chuma aliuliza baada ya kuona mpigaji ni Boss wake, Professor John Kluger)
"Nenda DP hotel kuna tukio la mauaji limetokea. Waliouliwa ni Waziri wa Afya Mh. Charles Jaden na familia yake pamoja na wafanyakazi wengine wa hotel" (Professor aliongea na kukata simu)
Mwamba wa chuma alijiandaa haraka na kumuacha mkewe akiwa bado anamalizia usingizi wa asubuhi. Akatafuta funguo ya gari anapowekaga na kuelekea moja kwa moja parking kutoa gari. Akiwa ndani ya gari lake,anageuka siti za nyuma na kukuta bahasha iliyochanwa upande mmoja.
"Hii bahasha ni ya nani tena, mbona jana nilisafisha gari lote na makorokoro yote nilitoa" (Mwamba wa chuma alijiuliza peke yake huku akiisogelea ile bahasha na kuivuta barua iliopo ndani)
"Habari yako Nguli wa ujasusi, najua una kiherehere cha kutaka kufatilia kila jambo. Naomba kwa hili la DP hotel hebu lipotezee. Kina cha hii bahari ni kirefu hutokiweza. Utapotea bure. AHSANTE" .Mwamba wa chuma alishituka baada ya kuisoma barua ile na huku akitafakari bila kupata majibu ya nani aliyeiweka ile barua na alijuaje kama asubuhi ile atatoka. Akaamua kuipotezea ile barua na kuendelea na safari yake kuelekea DP HOTEL.
NINI KITAENDELEA,
NANI AMEMTUMIA BARUA MWAMBA WA CHUMA?,
USIKOSE SEHEM YA TATU. AHSANTE.
Sent using
Jamii Forums mobile app