Hadithi: Lulu

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,206
12,706
Haditi hii ni tafsiri ya hadithi inayoitwa The Pearl iliyoandikwa na John Steinbeck.

Unaweza kusoma hadithi hii na nyingine nyingi kwenye app yetu. huu uzi una maelezo zaidi.


1637557083211.png

LULU
Sura ya Kwanza


Kino aliamka alfajiri na mapema kabla hata ya giza kuisha. Nyota bado zilikuwa zinaonekana angani na mwanga wa jua ulionekana kwa mbali upande wa mashariki. Jogoo walikuwa wameanza kuwika na nguruwe walikuwa wakitafutiza-tafutiza kwenye mabaki waliyokula jana. Nje ya nyumba yake ya fito kwenye mti wa mituna, kulikuwa na kundi la ndege wadogo waliokuwa wakiruka na kupiga kelele huku na kule.

Kino alifumbua macho, kitu cha kwanza kukiona ulikuwa ni mlango, mwanga ulikuwa umetengeneza umbo la mstatili kufuata umbo la mlango, kisha akaangalia kitanda cha kubembea ambacho Koyotito, mwanawe alikuwa amelala. Akageuza kichwa upande wa pili na kumuangalia mke wake Juana aliyekuwa pembeni yake mkekani. Alikuwa kajifunika mtandio wake wa bluu kuzunguka kichwa, ukifunika pua na kufika hadi kifuani.

Juana alikuwa ameshaamka. Kino hakumbuki ni lini amewahi amka na kukuta mke wake hajaamka. Macho meusi ya Juana yalikuwa yaking'aa. Yalikuwa yakimtazama Kino kama ambavyo humtazama siku zote aamkapo.

Kino akasikia sauti ya mawimbi dhaifu yakipiga ufukweni. Ilikuwa ni sauti nzuri sana masikioni mwake. Akafumba macho kuisikiliza vizuri, ilikuwa kama kusikiliza muziki. Pengine ni yeye pekee hufanya hivi, au pengine watu wote wa jamii yake hufanya hivi. Hapo kale watu wa jamii yake walikuwa ni wanamuziki hodari, hivyo kila walichoona, kufikiri au kusikia walikibadilisha kuwa nyimbo. Lakini sasa nyimbo zote zilikuwa ni za zamani, Kino alizifahamu zote lakini hakuna nyimbo mpya zilioongezwa. Hilo halimaanishi kuwa watu hawakuwa na nyimbo zao binafsi. Ndani ya kichwa cha Kino kulikuwa na wimbo, wimbo laini. Na kama angeweza kuipa jina basi angesema ni Wimbo wa Familia.

Akajifunika blanketi hadi kuziba pua ili kujilinda na hewa yenye unyevunyevu ya asubuhi. Pembeni yake Juana aliamka polepole bila kupiga kelele. Akiwa pekupeku akatembea hadi kwenye kitanda cha bembea alichokuwa amelala Koyotito. Akamuinamia na kunong'ona maneno kadhaa. Koyotito akafumbua macho kumuangalia, kisha akayafumba na kuendelea kulala.

Juana alienda sehemu ya kuwashia moto na kutoa kipande cha mkaa kinachowaka. Kipande hicho alikifukia kwenye majivu jana usiku. Alikipuliza huku akikichochea kwa vipande vidogovidogo vya kuni.

Kino naye akasimama na kujifunika blanketi akiacha macho tu. Akavaa makubazi na kuelekea. Alipofika mlangoni akainama na kukusanya blanketi ili lisiburuzike chini, akatoka kwenda kuangalia mapambazuko.

Alipofika nje mbuzi mmoja akamsogelea, akamnusa na kuanza kumkodolea macho. Nyuma yake moto ulikuwa umeshakolea na kutoa mwanga uliopita huku na kule.

Sasa muziki wa familia ukawa unasikika nyuma ya Kino, na ala yake ilikuwa ni sauti ya jiwe la kusaga; Juana alipokuwa anasaga mahindi ili kuoka keki za asubuhi.

Sasa mapambazuko yakaja haraka na mwanga wa jua ukashuka kwenye ghuba ile kama mlipuko. Kino akainamisha macho chini kujikinga na mwanga mkali. Alikuwa akisikia keki zikikandwa na harufu yake tamu zilipokuwa zikiokwa.

Siafu nao walikuwa na harakati nyingi ardhini, siafu wakubwa weusi na wadogo wa kahawia. Kino alimtazama siafu mdogo aliyekuwa anahangaika kujitoa kwenye mtego wa fukufuku, aliangalia kama vile yeye ni Mungu juu yao. Mbwa mmoja aliyekondeana na muoga akaja karibu yake, maneno laini ya Kino yakamfanya ajikunje na kulala miguuni mwake. Alikuwa ni mbwa mweusi akiwa na mabaka ya njano sehemu aliyotakiwa kuwa na nyusi. Kiujumla ilikuwa ni asubuhi kama asubuhi zingine, asubuhi njema.
Kino akasikia sauti ya kitanda cha kubembea cha Koyotito. Juana alikuwa amemchukua ili kumsafisha na kisha akamfunga na kumbeba kifuani mwake. Kino aliweza kuona yote hayo bila ya kuangalia. Juana akaanza kuimba moja ya nyimbo za kale, sehemu ya wimbo wa familia.

Nje ya nyumba yao kulikuwa na nyumba zingine za miti. Moshi ulionekana ukitoka kwenye nyumba hizo. Hizi zilikuwa na nyimbo zao, mambo yao, na wake tofauti na Juana.

Kino alikuwa ni kijana mwenye nguvu, nywele zake nyeusi zikifunika na kuning'inia kwenye paji lake la uso, macho yake yalikuwa makali sana. Mustachi wake mwembamba ulimkaa vema. Sasa baada ya hewa yenye unyevu kuisha, alikuwa ameshusha blanketi lake kufika usoni. Pembeni aliona jogoo wakijiandaa kupigana na juu aliona njiwa pori wakiruka. Dunia ilikuwa imeshaamka, hapo akasimama na kurudi ndani.

Alipofika ndani, Juana akasimama na kumrudisha Koyotito kwenye kitanda chake kisha akabana nywele zake kwa utepe wa kijani. Kino akachuchumaa karibu na moto, akachukua keki ya mahindi akaichovya kwenye mchuzi na kuanza kula. Ukiacha kile cha siku za sikukuu, hiki ndicho kifungua kinywa pekee alichikijua. Kino alipomaliza kula, Juana naye akapata kifungua kinywa. Walikuwa wamezungumza mara moja tu, hakukuwa na haja ya kuzungumza sababu kila kitu kilizoeleka. Mazungumzo yenyewe ni pale kino alipovuta pumzi kuashiria kuwa ameshiba.

Mwanga wa jua ukaanza kuingia ndani na baadhi ya miale ikatua na kuangaza kitanda cha Koyotito. Ghafla wakatulia kama waliopigwa na bumbuwazi. Kuna kitu kilikuwa kinatembea kwenye kitanda cha Koyotito. Kilikuwa kwenye kamba iliyofungwa kwenye paa kushikilia kitanda, na kilikuwa kikishuka kuelekea kwenye kitanda cha bembea cha Koyotito. Alikuwa ni nge aliyekuwa akishuka polepole huku mkia amesimamisha, akiwa tayari kushambulia muda wowote.

Pumzi ilimtoka Kino kwa kasi hadi akaacha mdomo wazi. Wimbo mpya ukawa umeingia kwenye familia, wimbo wa uovu, muziki wa adui.

Nge aliendelea kushuka polepole kwenye ile kamba. Juana akaanza kusema maneno; sala za kujilinda dhidi ya hatari kama ile kulingana na desturi zao, akaongezea kwa kusali sala ya bikira Maria. Kino yeye akaanza kusogelea kitanda cha Koyotito polepole na bila kufanya kelele. Alikuwa kanyoosha mikono mbele kama mtu anayetaka kupiga makofi au kudaka kitu, macho yote yakiwa kwa yule nge.

Ndani ya kitanda Koyotito alikuwa akicheka na kuinua mkono amshike nge yule. Kino alipozidi kusogea, nge yule akahisi hatari, alisimama na kuinua mkia wake juu mgongoni. Mwiba ulio mwisho wa mkia wake uling'aa.

Kino akasimama kimya, Juana yeye aliendelea kunong'ona sala zake, muziki wa adui ulisikika. Kino akapeleka mikono yake mbele taratibu sana. Mkia wa nge ukasimama wima zaidi, wakati huohuo Koyotito alikuwa akicheka, akatingisha kamba na nge akamuangukia.

Kino akawahi amdake lakini akapita na kuanguka kwenye bega la Koyotito. Akamdunga. Kino akamkamata nge yule na kumsaga katikati ya vidole vyake. Akamtupa chini na kuanza kumponda kwa ngumi yake. Koyotito alilia kwa maumivu makali lakini Kino akaendelea kumponda nge yule mpaka akasagika na kuwa alama ya majimaji sakafuni. Alikuwa kapandwa na hasira huku macho yamemuiva.

Juana akambeba mtoto na kuona alipochomwa, tayari palikuwa pameanza kuweka wekundu. Akaweka mdomo wake hapo, akanyonya na kutema, akanyonya tena na kutema. Koyotito alilia kwa sauti kubwa sana. Kino alizungukazunguka asijue la kufanya.

Kilio cha mtoto kiliwaleta majirani, wakakusanyika nje ya nyumba yao. Juan Tomasi, kaka yake Kino na mke wake mnene; Apolonia na watoto wao wanne walijazana mlangoni hadi kuziba njia. Nyuma yao majirani wengine walikuwa wakijitahidi kuchungulia ndani. Wale waliombele waliwataarifu wale wa nyuma; "Nge, mtoto ameumwa na nge."

Juana akawa ameacha kunyonya sumu, tobo alipochomwa mtoto lilikuwa limetanuka na kuwa jeupe pembeni kwa kunyonywa. Lakini uvimbe mwekundu ukawa umesambaa sehemu kubwa zaidi.

Watu wote walikuwa wanajua kuhusu nge. Mtu mzima anaweza kuwa mgonjwa sana akidungwa, lakini mtoto anaweza kufa kirahisi. Walijua kuwa mwanzo huanza uvimbe, homa na koo kubana, baadaye tumbo huanza kunyonga na mwishowe, kama sumu iliyoingia na nyingi, Koyotito anaweza kufa. Sasa maumivu ya kudungwa yakianza kupungua na kilio cha Koyotito kikawa cha kugugumia tu.

Mara zote Kino alishangazwa na tabia ya mke wake, alikuwa ni mtu mwenye subira na kwa muonekano alionekana ni dhaifu, lakini kwa ndani alikuwa ni mtu jasiri sana. Juana aliyekuwa na subira na, mchangamfu, mwenye heshima na mtii aliyeweza kujikunyata kwa maumivu bila kulia kwa sauti. Aliweza kuvumilia kuchoka na njaa kuliko hata Kino. Walipokuwa ndani ya mtumbwi, Juana alifanya mambo kama mwanaume mwenye nguvu. Na hata sasa alifanya jambo la kushangaza sana.

“Daktari,” alisema Juana. “Nenda kamwite daktari.”

Habari zikasambaa kuwafikia majirani waliokuwa wamebanana nje ya uzio wa nyumba yao. Nao walikuwa wakiongea kati yao.

“Juana anamtaka daktari.”

Lilikuwa jambo la kustaajabisha kumtaka daktari. Daktari hajawahi kuja huku kwenye nyumba za miti. Kwanini aje huku wakati alikuwa anapata pesa za kutosha kuwahudumia matajiri walioishi kwenye nyumba za mawe zilizopigwa chokaa mjini!

“Hawezi kuja,” walisema watu waliokuwa uwanjani.

“Hawezi kuja,” walisema watu waliokuwa mlangoni kumwambia Kino.

“Daktari hawezi kuja,” alisema Kino akimwambia Juana

Juana alimuangalia Kino. Macho yake yalikuwa makali kama simba jike. Koyotito ndiye alikuwa mtoto wa kwanza wa Juana. Alikuwa ndiyo kila kitu kwake. Na kino aliona uso wa mkewe ulioonyesha nia isiyotetereka kwenye lengo lake,na sauti ya muziki wa familia ukalia kichwani mwake.

“Basi tutamfuata,” alisema Juana, na kwa mkono mmoja alijitanda mtandio wake wa bluu kichwani, na upande mwingine akatengeneza bembea ya kumbebea mtoto aliyekuwa akigugumia, kisha akamfunika macho kwa sehemu iliyobakia ili kumkinga na jua. Watu waliokuwa mlangoni waliwasukuma walio nyuma yao ili kumpisha apite. Kino alifuata nyuma, wakatoka hadi nje ya geti, na majirani wakaanza kuwafuata. Suala hilo likawa suala la mtaa mzima sasa. Walitembea haraka haraka kuelekea mjini. Juana alikuwa mbele, alifuatia Kino, na nyuma yao, Juan Tomas na Apolonia. Tumbo kubwa la Apolonia lilichezacheza sababu ya mwendo wa kasi. Kisha walifuatia majirani zao, huku watoto wakikimbia pembeni ya msafara.
 
Wakawa wamefika mwisho wa nyumba za miti na mwanzo wa nyumba za mawe za mjini. Mji uliokuwa na kuta imara nje, na bustani nzuri ndani yake. Walisikia ndege wakiimba kwenye bustani hizo. Umati ukakatisha kwenye uwanja wa mji mbele kanisa. Sasa walikuwa ni watu wengi sana. Watu waliojiunga walikuwa wakiambiwa jinsi mtoto alivyodungwa na nge, na kuwa baba na mama yake wanampeleka kwa daktari.

Kati ya watu waliojiunga, walikuwemo ombaomba ambao hukaa mbele ya kanisa. Ombaomba hao walikuwa ni hodari kutambua uwezo wa mtu wa kiuchumi, waliangalia sketi ya bluu ya Juana iliyochoka, mtandio wake uliochanika na utepe wake. Walikadiria umri wa blanketi la Kino, na nguo zake zilizooshwa mara elfu wakaona kuwa ni watu maskini, lakini wakaongozana nao kuona mambo yatakayotokea . Ombaomba hao wanne ambao hukaa mbele ya kanisa walijua kila kitu mjini pale. Walijua kusoma nyuso za wasichana walioingia kwenda kuungama, na nyuso zao walipotoka; kwa hilo waliweza kutambua aina ya dhambi zao. Walijua kashfa zote ndogondogo na hata uhalifu mkubwa. Hakuna mtu alipita kwenda kuungama bila wao kujua. Na walimjua daktari. Walijua kuwa alikuwa ni mjinga tu, tena katili, na walijua ulafi wake wa mali, ulafi wake wa chakula na dhambi zake. Walijua jinsi alivyokuwa akitoa watu mimba kwa namna isiyo ya kitaalamu, na jinsi alivyokuwa bahili, akitoa senti chache tu kwa maskini. Mara nyingi wameshuhudia maiti za watu aliowatibu zikiingia kanisani. Na sababu misa ya asubuhi ilikuwa imekwisha na biashara ya kuomba kuwa siyo nzuri, wakaamua kuongozana na umati. Watu hawa, ambao siku zote walitaka kujua mambo ya wengine, walitaka kujua yule daktari mvivu na mnene atafanya nini juu ya huyu mtoto aliyeumwa na nge, mtoto asiye na hatia.

Hatimaye umati ule wenye kasi ukafika kwenye geti kubwa la nyumba ya daktari. Waliweza kusikia sauti za ndege waliofugwa ndani mule, sauti ya maji na sauti ya fagio. Waliweza kusikia harufu tamu ya nyama ikikaangwa ikitoka ndani ya nyumba ya daktari.

Kwanza Kino akasita; daktari huyu hakuwa mtu wa jamii yao. Kwa miaka karibu mia nne watu wa jamii moja na daktari huyu wamewapiga, wamewasababishia njaa, wamewapora, na kuwadharau watu wa jamii ya Kino. Kino alijihisi mnyonge, hasira na uoga kwa wakati mmoja vilimjaa. Alihisi kuwa itakuwa rahisi , kwake kumuua daktari kuliko kuongea naye, watu wote wa jamii moja na daktari huongea na watu wa jamii ya Kino kama kwamba ni wanyama wasioelewa kitu. Kino alipokuwa akiinua mkono wa kulia kwenda kwenye chuma cha kugongea geti akajikuta hasira kali ikimpanda, na masikioni mwake alisikia mdundo wa muziki wa adui, akauma midomo lakini akasogea na kugonga. Chuma kikalia na Kino akavua kofia yake na kusimama akisubiri. Koyotito aliyekuwa kwenye mikono ya Juana akagugumia kidogo, Juana akamsemesha kwa kumnong’oneza. Umati ukakusanyika karibu ili kuona na kusikia vizuri.

Punde kidogo geti kubwa likafunguliwa lakini kidogo tu. Kupitia uwazi ule Kino aliweza kuona bustani nzuri ya kijani na maji yakiruka kwenye kidimbwi. Mtu aliyekuja kufungua alikuwa ni wa jamii moja na Kino. Kino aliongea naye kwa lugha ya kwao.

“Mtoto, mtoto wetu wa kwanza amedungwa sumu na nge, hivyo tunahitaji msaada wa tabibu.”

Mtumishi yule alifunga geti kidogo na kujibu, lakini hakumjibu Kino kwa lugha yao.

“Nisubiri kidogo, nitaenda kumtaarifu,” akasema mtumishi yule na kisha akafunga geti na kubana komeo. Jua likaanza kuwa kali.

Daktari alikuwa amekaa kwenye kitanda kikubwa chumbani mwake. Alikuwa amevaa pajama nyekundu ya hariri kutoka Paris. Na sasa lilikuwa linambana kifuani kidogo iwapo akifunga vifungo. Mapajani mwake kulikuwa na sinia la fedha likiwa na bakuli ya chokleti, nayo ya fedha, na kikombe kidogo cha udongo. Kwa udhaifu wa kikombe kile, ilionekana jambo la kushangaza na kuchekesha alipokuwa anakiinua na mikono yake mikubwa. Alikishika kwa uangalifu akitumia kidole kimoja na dole gumba. Macho yake yalikuwa yamezungukwa na nyama nene, na mdomo wake ulikuwa umelegea kizembe kama mtu ambaye haridhishwi na maisha yake. Sauti yake ilikuwa ya kukwaruza sababu ya mafuta ya unene kubana koo lake. Pembeni yake kulikuwa na meza na juu yake bakuli iliyokuwa na sigara kadhaa. Chumbani kulikuwa na picha nyingi za kidini, na kulikuwa na picha kubwa ya marehemu mke.

Kuna kipindi, japo kwa muda mfupi, daktari huyu alikuwa ni sehemu ya watu wa tabaka la juu na maisha yake yote yaliyofuatia yalijaa kumbukumbu ya maisha hayo, akitamani maisha aliyoishi Ufaransa.

“Yale ndiyo yalikuwa maishai” alisikika akisema. Kusema hivyo alimaanisha jinsi kwa kipato chake kidogo alivyomudu kula mgahawani na kuwez kuwa na kimada. Alijaza tena kikombe chake chokleti na kuvunja biskuti iliyokuwa mkononi mwake. Mtumishi kutoka getini alisimama mlangoni akisubiri aanzwe kusemeshwa.

“Kuna nini?” aliuliza daktari

“Kuna muhindi mwekundu amekuja na mtoto, anasema ameumwa na nge.”

Daktari aliweka kikombe chini polepole

“Kwani sina jambo la maana la kufanya hadi nianze kutibu wahindi waliomwa na na wadudu? Mimi ni daktari wa watu siyo wa mifugo.”

“Ndiyo bwana mkubwa,” alisema mtumishi.

“Ana pesa zozote?” aliuliza daktari. “Hapana, mara zote huwa hawana pesa. Nimechoka kuwa mtu pekee anayefanya kazi bure duniani. Nenda kaone kama ana pesa zozote!”

Alipofika getini, mtumishi akafungua geti kidogo na kuwaangalia watu waliokuwa wamekusanyika pale nje. Safari hii aliongea kwa lugha yao.

“Unapesa ya kulipia matibabu?”

Kino akaingiza mkono kwenye mifuko ya siri ndani ya blanketi lake. Humo akatoa karatasi lililokuwa limekunjwa mara nyingi. Alilifungua polepole mpaka likawa wazi na lulu nane ndogo zilizokuwa na maumbo mabovu zikaonekana. Zilikuwa mbaya kuzitazama, zilikuwa bapa na za rangi ya kijivu, zilikuwa kama vidonda vidogo. Zilionekana hazina thamani yoyote. Mtumishi alichukua karatasi ile yenye lulu na kufunga tena geti. Lakini safari hii hakukawia, alifungua geti kumuwezesha tu kurudisha karatasi ile.

“Daktari ametoka,” aliwaambia. “Ameitwa kwenye jambo la muhimu zaidi” baada ya kusema hivyo akafunga geti haraka kwa aibu.

Sasa umati wote ukajawa na aibu. Wakanyong’onyea kabisa. Wale ombaomba wakarudi kwenye ngazi za kanisa, wazururaji wakaendelea na mambo yao, na majirani wakatomea ili wasione aibu kubwa iliyomkumba Kino.

Kwa muda kidogo Kino akasimama getini pale, Juana akiwa pembeni yake. Polepole, akavaa kofia yake kwa huzuni. Kisha ghafla akapiga geti kwa nguvu sana akitumia ngumi. Akabaki akishangaa mkono wake uliochunika huku damu ukichuruzika kati ya vidole vyake.
 
Sura ya Pili

Mji ule ulikuwa kwenye ghuba pana, majengo yake ya zamani ya rangi ya manjano yalikuwa yamejengwa hadi kando ya ufukwe. Mitumbwi ya rangi nyeupe na bluu kutoka Nayarit zilikuwa imewekwa ufukweni. Mitumbi hiyo ni ya vizazi na vizazi, ilikuwa imepakwa plasta, ilikuwa ni plasta ngumu sana na isiyoingia maji. Ufundi wa kutengeneza plasta hiyo ulikuwa ni siri ya wavuvi wenyewe. Mitumbi mingine ilikuwa na ilikuwa na nguzo katikati ya kuweza kufunga tanga.

Mwani wa kahawia ulisongwa huko na kule na mawimbi ya bahari hadi ufukweni. Sakafu ya bahari ilikuwa ina mimea na viumbe wengi wa kila namna, kulikuwa na mwani ambao farasi maji waling’ang’ania mashina yake, samaki mwenye sumu na kaa wenye rangi nyangavu. Ufukweni walikuwepo mbwa na nguruwe wenye njaa kutoka mjini. Walikuwa wakitafutiza mizoga ya samaki, au ya ndege wa baharini iliyosombwa na mawimbi wakati wa kuja kwa bahari.

Nyumba za miti za wavuvi zilikuwa kando ya ufukwe, upande wa kulia wa mji. Kwenye ufukwe huo walikuwa wameweka mitumbwi yao. Polepole , Kino na Juana walielekea ufukweni hadi kwenye mashua ya Kino. Hicho ndicho kilikuwa kitu pekee cha thamani alichomiliki. Ilikuwa ni mashua ya zamani sana. Babu yake na Kino ndiye aliyeileta kutoka Nayarit, na ndiye aliyempatia baba yake na Kino, kisha naye kumpatia Kino.Ilikuwa ni mali na chanzo cha chakula pia, mwananume mwenye mtumbwi anaweza kumhakikishia mwanamke kuwa atapata chochote cha kula. Ilikuwa ndiyo ulinzi wao dhidi ya njaa. Kila mwaka Kino alirekebisha mashua yake kwa ile plasta ngumu. Alijifunza njia ya siri ya kutengeneza plasta hiyo kutoka kwa baba yake. Alipofika kwenye mashua yake akaishika kwa wororo kama ilivyokawaida yake. Aliweka jiwe alilotumia kuzamia, kikapu na kamba mbili ndani ya mashua. Baada hayo, akakunja blanketi lake na kulilaza ndani ya mashua.

Juana alimlaza Koyotito kwenye blanketi na kumfunika kwa mtandio wake ili jua lisimpige. Kwa sasa alikuwa halii lakini uvimbe ulikuwa umeenea kutoka begani kwake hadi shingoni na chini ya sikio, uso wake ulionekana kuvimba na alionekana kama mtu mwenye homa. Juana alienda majini na kukusanya mimea fulani ya baharini ya rangi ya kahawia. Akaikamua na kuifikicha kisha akampaka mtoto kwenye bega lililovimba. Ilikuwa ni dawa nzuri, pengine hata kuzidi ile ya daktari. Tatizo ni kuwa haikuhalalishwa naye, sababu ilikuwa ni rahisi na haikuwa na gharama yoyote. Bahati nzuri Koyotito hakupatwa na kunyongwa na tumbo, pengine Juana aliwahi kunyonya sumu, lakini ilionekana wazi hakuweza kunyonya wasiwasi wake juu ya mtoto wake wa kwanza.

Katika sala zake, Juana alikuwa hajaomba moja kwa moja kupona kwa mtoto. Alikuwa ameomba wapate lulu ili waweze kumlipa daktari wa kumtibu motto.

Kino na Juana wakasukuma mashua yao mpaka kwenye maji, kisha Juana akaanza kujipakia sehemu ya mbele ilipoanza kuelea. Kino akamalizia kusukuma sehemu ya nyuma na kujipakia. Kwa pamoja , Kino na Juana wakaanza kupiga makasia kelekea baharini, mashua ikaongeza mwendo. Watafuta lulu wengine walikuwa wamekwishakwenda baharini muda mrefu uliopita. Kino aliweza kuwaona kwa mbali kati ya ukungu.

Mwanga wa jua uliweza kupenya hadi chini baharini ambako chaza wa lulu walikuwa wamejishikilia sakafuni, sakafu ambayo ilikuwa imejaa makombe ya chaza waliofunguliwa yakiwa yametawanyika huku na huko. Hii ndiyo sakafu iliyomtajirisha Mfalme wa Hispania hadi kumfanya kuwa na nguvu sana huko Ulaya katika miaka iliyopita. Iligharamia vita zake, na aliitumia kupamba makanisa ili apate wokovu. Sakafuni pale kulikuwa na aina mbalimbali ya chaza, wakubwa kwa wadogo.

Utengenezaji wa lulu ulikuwa namna hii. Mara kwa mara chaza hawa walipatwa na ajali, punje ya mchanga iliweza kujibanza katika mikunjo ya miili yao. Punje hiyo ikaanza kukwangua mwili wake. Ili kujilinda mwili unaanza kuizungushia punje hiyo kwa kitu kama saruji laini. Lakini mara baada ya kuanza kufanya hivyo, inaendelea kuzungushia na kutengeneza lulu. Lulu huendelea kukua hadi pale inapong’olewa na tufani au chaza anapouwawa.

Karne na karne watu wamekuwa wakizamia na kuwakamata chaza kutoka sakafuni na kuwafungua, wakitafuta punje za mchanga zilizozungushiwa saruji. Samaki wengi waliishi eneo hilo wakila chaza waliotupwa na wazamiaji. Kwahiyo utengenezwaji wa lulu ulikuwa ni ajali tu, na kuipata ilikuwa ni bahati. Bahati kutoka kwa Mungu, miungu au wote kwa pamoja.

Kino alikuwa na kamba mbili. Moja ikifungwa kwenye jiwe zito la kuzamia na nyingine kwenye kikapu. Alivua shati na suruali na kuweka kofia yake ndani ya mashua. Maji yalikuwa yametulia kabisa. Alichukua jiwe kwa mkono mmoja na kikapu kwa ule mwingine. Alijiachia akitanguliza miguu na jiwe likamchukua hadi kwenye sakafu ya bahari. Mapovu ya hewa yalitokea kumzunguka na baada ya sekunde chache yakatulia na aliweza kuona vizuri kabisa. Juu yake kulikuwa kunang’aa kama kioo na aliweza kuona uvungu wa mashua yake.

Kino alitembea kwa uangalifu ili asije kutibua tope na mchanga na kufanya asione vizuri. Aliweka mguu wake kwenye kitanzi alichokuwa amefunga jiwe na akaanza kufanya kazi haraka akitumia mikono. Akaanza kuwabandua chaza kutoka sakafuni, wengine mmoja mmoja na wengine wakiwa kwenye vikundi. Aliwabandua na kuwaweka katika kikapu chake. Chaza wengine walikuwa wamebanana sana, hivyo alivyowabandua alitoka na kundi la chaza.
 
Watu wa Kino walikuwa wameimba juu ya kila kitu na vitu vyote vilivyopata kutokea. Walitunga nyimbo kuhusu samaki, juu ya bahari iliyochafuka na juu ya bahari shwari. Kuhusu mwanga na kuhusu giza, juu ya jua na juu ya mwezi, nyimbo zote hizo zilikuwa ndani ya Kino na watu wake. Kila nyimbo iliyowahi tungwa, hata zile zilizosahaulika. Alipokuwa anajaza kikapu chake, wimbo wa pekee ulikuwa ndani yake, na ala ilikuwa ni moyo wake uliopiga ulipokuwa ukitumia hewa aliyoibana. Ulikuwa ni wimbo wa siri. Haukusikika kirahisi lakini ulikuwepo siku zote na huu ulikuwa wimbo juu ya Lulu itafutwayo. Kila kombe lililowekwa kwenye kikapu kulikuwa na uwezekano kuwa na lulu ndani yake. Uwezekano ulikuwa mdogo, lakini bahati na miungu waliweza kufanya yao. Na Kino alijua kuwa ndani ya mashua Juana alikuwa akitoa sala. Akiwa amejikaza kabisa ili sala yake isikiwe, kunyang’anya bahati toka mikono ya miungu, alihitaji bahati kwaajili ya bega lililovimba la Koyotito. Na sababu uhitaji ulikuwa ni mkubwa, na nia ilikuwa ni kubwa pia, mapigo ya wimbo wa Lulu itafutwayo yalikuwa na nguvu sana asubuhi hii. Aya zake zote zilikuja aya zake zote zilimjia

Kino alikuwa katika ujana wake, alikuwa na nguvu, aliweza kukaa ndani ya maji kwa muda wa dakika mbili bila tatizo lolote. Alifanya kazi kwa bidii, akichagua chaza wakubwa wakubwa. Sababu walitibuliwa, chaza wakajikusanya karibukaribu zaidi. Pembeni kidogo kulia kwake kulikuwa na mwamba ambao juu yake walikuwepo chaza wadogo ambao hawakukomaa kuwa na lulu. Kino alisogea karibu na pango dogo, kwenye pango hilo alimuona chaza mkubwa sana akiwa ametulia pale, huyu hakuwa na chaza wadogo wakimtambaa. Kombe la chaza huyu lilikuwa liko wazi kidogo sababu lile pango dogo lilimlinda chaza huyu. Ndani ya chaza huyu Kino aliona kitu kinang’aa ajabu lakini ghafla kombe likajifunga. Moyo wake ukadunda kwa nguvu, na ala ya lulu itafutwayo ikapiga kelele katika masikio yake. Alimtoa yule chaza polepole na kumshika kwa nguvu kifuani mwake. Alitoa mguu wake kwenye kitanzi kilichofungwa kwenye jiwe na mwili wake ukaelea mpaka juu. Nywele zake nyeusi ziling’aa katika jua. Alishika kingo za mashua na kumuweka chaza yule ndani yake.

Juana akashikilia mashua vizuri ili kino aweze kupanda ndani. Macho ya Kino yalikuwa yanang’aa kwa shauku. Alivuta jiwe lake la kuzamia na kisha akavuta kikapu cha chaza na kuviweka mashuani. Juana aliona shauku yake yake hivyo akajifanya kuangalia pembeni. Si jambo zuri kutaka kitu kupita kiasi. Kufanya hivyo kunaweza kupeperusha bahati. Unatakiwa kukitaka kwa kiasi tu; unatakiwa kuwa mjanja unaposhughulika na Mungu au miungu. Kino alichukua kisu chake kifupi na kigumu. Aliangalia kikapu chake kwa makini. “Pengine itakuwa vema nikimfungua yule chaza mkubwa mwishoni,” aliwaza. Alimchukua chaza mdogo kutoka kwenye kikapu. Alimkata na kuchunguza katika misuli yake na kisha kumtupa majini. Kisha akawa ni kama amemuona yule chaza mkubwa aliyekuwa kwenye sakafu ya mashua kwa mara ya kwanza. Alichuchumaa, alimuinua na kuanza kumchunguza. Kino akaanza kusita kumfungua. Aliwaza pengine aichokiona ni mwanga tu ulioakisiwa. Kwamba labda ni kipande cha kombe kilichoingia kwa ndani, au aliona kiini macho tu. Kwenye ghuba hii yenye mwanga usioeleweka, kulikuwa na viini macho vingi kuliko uhalisia.

Lakini macho ya Juana yalikuwa yakimtazama, na alionekana mwenye shauku ya kujua kilichomo. Aliweka mkono wake kwenye kichwa kilichofunikwa cha Koyotito na kwa sauti tulivu alisema, “Mfungue.”

Kino kwa makini, aliingiza kisu chake kwenye upenyo pembeni ya kombe. Kupitia kisu aliweza kuhisi misuli ya chaza ikijikaza. Alibinjua kisu na misuli ikaachia na kombe likafunguka. Kino aliinua misuli na tazama! Lulu ya ajabu. Haina kasoro; kama mwezi tu. Ilionekana kama inapokea mwanga, inauboresha na kuuakisi ukiwa wa rangi ya fedha. Ilikuwa ni kubwa kama yai la ndege wa baharini, ilikuwa ni lulu bora kuliko zote duniani.

Juana alipumua kwa nguvu. Lakini ala ya siri ya lulu itafutwayo ikamjia Kino kwa uwazi na uzuri wake. Kwenye uso wa lulu ile aliona ndoto zikijitengeneza. Alitoa lulu ile toka kwa chaza anayekufa na kuiweka kiganjani mwake, akaigeuza na kuona kuwa duara lake halina kasoro yoyote. Juana alisogea karibu na kuishangaa ikiwa mkononi mwake. Mkono aliotumia kupiga ngumi geti la daktari, na misuli iliyochanika ilibadilishwa rangi na maji ya bahari kuwa kijivu.

Juana akaenda sehemu aliyolala Koyotito, alitoa yale majani ya dawa kwenye bega lake na kuita kwa sauti;

“Kino.”

Kino aliangalia na kuona kuwa uvimbe kwenye bega la mtoto ulikuwa unapungua. Sumu ilikuwa inaondoka mwilini. Kwa hisia kali, akakunja ngumi kuifumba lulu. Akainua kichwa juu na na kupiga kelele kama mbwa mwitu vile. Mwili ulijikaza, macho yakiangalia juu huku akipiga kelele. Watu waliokuwa kwenye mashua zingine waliangalia kwa mshangao, kisha walitia kasia majini na kupiga kuelekea mashua ya Kino.
 
Watu wa Kino walikuwa wameimba juu ya kila kitu na vitu vyote vilivyopata kutokea. Walitunga nyimbo kuhusu samaki, juu ya bahari iliyochafuka na juu ya bahari shwari. Kuhusu mwanga na kuhusu giza, juu ya jua na juu ya mwezi, nyimbo zote hizo zilikuwa ndani ya Kino na watu wake. Kila nyimbo iliyowahi tungwa, hata zile zilizosahaulika. Alipokuwa anajaza kikapu chake, wimbo wa pekee ulikuwa ndani yake, na ala ilikuwa ni moyo wake uliopiga ulipokuwa ukitumia hewa aliyoibana. Ulikuwa ni wimbo wa siri. Haukusikika kirahisi lakini ulikuwepo siku zote na huu ulikuwa wimbo juu ya Lulu itafutwayo. Kila kombe lililowekwa kwenye kikapu kulikuwa na uwezekano kuwa na lulu ndani yake. Uwezekano ulikuwa mdogo, lakini bahati na miungu waliweza kufanya yao. Na Kino alijua kuwa ndani ya mashua Juana alikuwa akitoa sala. Akiwa amejikaza kabisa ili sala yake isikiwe, kunyang’anya bahati toka mikono ya miungu, alihitaji bahati kwaajili ya bega lililovimba la Koyotito. Na sababu uhitaji ulikuwa ni mkubwa, na nia ilikuwa ni kubwa pia, mapigo ya wimbo wa Lulu itafutwayo yalikuwa na nguvu sana asubuhi hii. Aya zake zote zilikuja aya zake zote zilimjia

Kino alikuwa katika ujana wake, alikuwa na nguvu, aliweza kukaa ndani ya maji kwa muda wa dakika mbili bila tatizo lolote. Alifanya kazi kwa bidii, akichagua chaza wakubwa wakubwa. Sababu walitibuliwa, chaza wakajikusanya karibukaribu zaidi. Pembeni kidogo kulia kwake kulikuwa na mwamba ambao juu yake walikuwepo chaza wadogo ambao hawakukomaa kuwa na lulu. Kino alisogea karibu na pango dogo, kwenye pango hilo alimuona chaza mkubwa sana akiwa ametulia pale, huyu hakuwa na chaza wadogo wakimtambaa. Kombe la chaza huyu lilikuwa liko wazi kidogo sababu lile pango dogo lilimlinda chaza huyu. Ndani ya chaza huyu Kino aliona kitu kinang’aa ajabu lakini ghafla kombe likajifunga. Moyo wake ukadunda kwa nguvu, na ala ya lulu itafutwayo ikapiga kelele katika masikio yake. Alimtoa yule chaza polepole na kumshika kwa nguvu kifuani mwake. Alitoa mguu wake kwenye kitanzi kilichofungwa kwenye jiwe na mwili wake ukaelea mpaka juu. Nywele zake nyeusi ziling’aa katika jua. Alishika kingo za mashua na kumuweka chaza yule ndani yake.

Juana akashikilia mashua vizuri ili kino aweze kupanda ndani. Macho ya Kino yalikuwa yanang’aa kwa shauku. Alivuta jiwe lake la kuzamia na kisha akavuta kikapu cha chaza na kuviweka mashuani. Juana aliona shauku yake yake hivyo akajifanya kuangalia pembeni. Si jambo zuri kutaka kitu kupita kiasi. Kufanya hivyo kunaweza kupeperusha bahati. Unatakiwa kukitaka kwa kiasi tu; unatakiwa kuwa mjanja unaposhughulika na Mungu au miungu. Kino alichukua kisu chake kifupi na kigumu. Aliangalia kikapu chake kwa makini. “Pengine itakuwa vema nikimfungua yule chaza mkubwa mwishoni,” aliwaza. Alimchukua chaza mdogo kutoka kwenye kikapu. Alimkata na kuchunguza katika misuli yake na kisha kumtupa majini. Kisha akawa ni kama amemuona yule chaza mkubwa aliyekuwa kwenye sakafu ya mashua kwa mara ya kwanza. Alichuchumaa, alimuinua na kuanza kumchunguza. Kino akaanza kusita kumfungua. Aliwaza pengine aichokiona ni mwanga tu ulioakisiwa. Kwamba labda ni kipande cha kombe kilichoingia kwa ndani, au aliona kiini macho tu. Kwenye ghuba hii yenye mwanga usioeleweka, kulikuwa na viini macho vingi kuliko uhalisia.

Lakini macho ya Juana yalikuwa yakimtazama, na alionekana mwenye shauku ya kujua kilichomo. Aliweka mkono wake kwenye kichwa kilichofunikwa cha Koyotito na kwa sauti tulivu alisema, “Mfungue.”

Kino kwa makini, aliingiza kisu chake kwenye upenyo pembeni ya kombe. Kupitia kisu aliweza kuhisi misuli ya chaza ikijikaza. Alibinjua kisu na misuli ikaachia na kombe likafunguka. Kino aliinua misuli na tazama! Lulu ya ajabu. Haina kasoro; kama mwezi tu. Ilionekana kama inapokea mwanga, inauboresha na kuuakisi ukiwa wa rangi ya fedha. Ilikuwa ni kubwa kama yai la ndege wa baharini, ilikuwa ni lulu bora kuliko zote duniani.

Juana alipumua kwa nguvu. Lakini ala ya siri ya lulu itafutwayo ikamjia Kino kwa uwazi na uzuri wake. Kwenye uso wa lulu ile aliona ndoto zikijitengeneza. Alitoa lulu ile toka kwa chaza anayekufa na kuiweka kiganjani mwake, akaigeuza na kuona kuwa duara lake halina kasoro yoyote. Juana alisogea karibu na kuishangaa ikiwa mkononi mwake. Mkono aliotumia kupiga ngumi geti la daktari, na misuli iliyochanika ilibadilishwa rangi na maji ya bahari kuwa kijivu.

Juana akaenda sehemu aliyolala Koyotito, alitoa yale majani ya dawa kwenye bega lake na kuita kwa sauti;

“Kino.”

Kino aliangalia na kuona kuwa uvimbe kwenye bega la mtoto ulikuwa unapungua. Sumu ilikuwa inaondoka mwilini. Kwa hisia kali, akakunja ngumi kuifumba lulu. Akainua kichwa juu na na kupiga kelele kama mbwa mwitu vile. Mwili ulijikaza, macho yakiangalia juu huku akipiga kelele. Watu waliokuwa kwenye mashua zingine waliangalia kwa mshangao, kisha walitia kasia majini na kupiga kuelekea mashua ya Kino.

Endelea mkuu
 
Sura ya 3

Mji ni kama mnyama aliyeumbwa na wanyama wengi waishio kama kitu kimoja. Mji una mfumo wa fahamu na kichwa na mabega na miguu. Mji mmoja ni kitu kinachojitofautisha na miji mingine, hakuna miji miwili inayofanana. Na mji una hisia. Jinsi habari zinavyosambaa katika mji ni fumbo ambalo bado kufumbuliwa. Inaonekana habari zinasafiri haraka kuliko mvulana anvyoweza kukimbia kuzisambaza; haraka kuliko wanawake wanavyoweza kuzitangaza.

Kabla ya Kino, Juana na wavuvi wengine hawajafika nyumbani kwa Kino, tayari mji ulikuwa unapwitapwita kwa habari, habari ya Kino kupata lulu bora zaidi. Kabla watoto waliokimbia huku na kule hawajasimulia, mama zao walikuwa wanafahamu. Habari zilisambaa katika zile nyumba za miti, zikapita mawimbi ya ufukweni hadi mjini kwenye nyumba za mawe na chokaa. Zilifika kwa kasisi aliyekuwa akitembea bustanini mwake, zikamfanya uso umbadilike, uwe kama mtu mwenye fikra nyingi, mawazo ya kuwa kanisa lilihitaji marekebisho fulani yalimjia. Aliwaza thamani ya lulu ile itakuwa ngapi. Na aliwaza iwapo alimbatiza mtoto wa Kino, au alimfungisha ndoa. Taarifa zikafika kwa wafanya biashara, nao wakaanza kuangalia nguo za kiume ambazo hazikuwa na mauzo mazuri.

Habari zikamfikia daktari alipokuwa amekaa na mwanamke mmoja ambaye ilionekana ugonjwa wake ni uzee; japo si yeye wala daktari aliyeonekana kukubaliana na ukweli huo. Na ilipojulikana kuwa Kino ni nani, daktari alisema “Ni mteja wangu, ninamtibu mtoto wake aliyedungwa na nge.” Kisha macho ya daktari yakamzunguka, akawaza kuhusu Paris. Alikumbuka chumba alichoishi alipokuwa huko, sehemu ya anasa na starehe. Alikumbuka mwanamke aliyeishi naye kama mwanamke mzuri na mtaratibu, japo kikweli hakuwa na sifa zozote katika hizo. Mawazo ya daktari yalikuwa mbali na mgonjwa wake mzee, alijiona amekaa katika mgahawa huko Paris na mhudumu alikuwa akifungua chupa ya divai.

Habari ziliwafikia ombaomba waliokuwa mbele ya kanisa mapema kabisa. Habari hizo ziliwafanya wacheke kwa furaha. Walijua kuwa hakuna mtoaji mzuri duniani kama mtu maskini aliyebahatika utajiri wa ghafla.

Kino alikuwa amepata lulu ya pekee kabisa. Mjini, kwenye ofisi ndogo ndogo walikuwepo watu walionunua lulu kutoka kwa wavuvi. Walikuwa wakikaa kwenye viti vyao wakisubiri lulu ziletwe. Zilipoletwa; walipambana, walipaza sauti na kutoa vitisho mpaka walipofikia bei ya chini kabisa mvuvi aliyoweza kukubali. Lakini kuna bei ambayo hawakuthubutu kushuka zaidi ya hapo, imewahi tokea mvuvi mmoja alionelea ni bora kutoa lulu zake sadaka kanisani kuliko kuuza kwa bei ya kinyonyaji. Baada ya ununuzi watu hawa walikuwa wakikaa pekee yao wakichezea lulu mikononi mwao, wakitamani lulu zile zingekuwa zao. kiukweli kulikuwa hakuna wanunuzi wengi, alikuwepo mmoja tu. Aliwaweka mawakala wake kwenye ofisi tofautitofauti ili kuonyesha kuna ushindani. Habari zilikuwa zimewafikia watu hawa. Macho yaliwatoka na vidole vikawawasha, kila mmoja ajua kuwa bwana mkubwa wao hataishi milele, na kuwa atahitajika mtu wa kuchukua mahala pake. Kila mmoja aliwaza kuwa endapo angepata mtaji angeanzisha biashara yake.

Watu wa kila aina wakaanza kuvutiwa na Kino. Wauzaji wa vitu, na watu wa kuomba msaada fulani. Kino alikuwa amepata Lulu ya Ulimwengu. Upako wa lulu na upako wa binadamu vilichanganyikana, kisha mchanganyiko tata wa giza ukapatikana. Ndani ya muda mfupi kila mtu akawa anahusika na lulu ya Kino, na lulu ya Kino ikaingia katika ndoto, matarajio, mipango, maisha ya baadaye, matamanio, mahitaji, na njaa ya kila mtu. Na ni mtu mmoja aliyesimama kati yao na lulu hiyo; Kino. Kwa namna ya kushangaza Kino akawa adui wa kila mtu. Habari za lulu zilikuwa zimeamsha kitu fulani kiovu na cheusi kabisa mjini pale. Kitu hicho cheusi kilikuwa kama nge, au njaa inaposikia harufu ya chakula, au upweke unaponyimwa upendo. Tezi za sumu za mji zilikuwa zimeanza kutengeneza sumu, na mji ulituna na kupumua kwa kufoka sababu ya kujaa sumu.

Lakini Kino na Juana hawakujua kuhusu mambo haya. Sababu walikuwa na furaha walifikiri kila mtu alishiriki furaha hiyo. Juan Tomas na Apolonia walishiriki furaha hiyo, na hawa walikuwa ni kila kitu kwao. Jioni wakati jua lilipokuwa limezama milimani, Kino alikuwa amechuchumaa ndani mwake, Juana akiwa pembeni yake. Nyumba ya ilikuwa imejaa majirani zao. Kino aliishika lulu ile mikononi mwake, ilikuwa ya moto na hai mikononi mwake. Muziki wa lulu ulikuwa umeungana na muziki wa familia, kila mmoja ukizidisha uzuri wa mwingine. Majirani waliangalia lulu iliyokuwa mikononi mwa Kino na kustaajabu imekuwaje bahati kama hiyo kumuangukia mtu.

Kisha Juan Tomas , ambaye alikuwa amechuchumaa kulia kwake; sababu ni kaka yake, akauliza: “Utafanya nini sasa baada kuwa tajiri?”

Kino akaangalia lulu yake, na Juana akaangalia chini na kutengeneza ushungi wake kufunika uso ili mshawasha wake usionekane. Katika mwanga ulioakisiwa na lulu picha za ambavyo Kino alivifikiria huko nyuma zikamjia. Vitu alivyofikiri haviwezekani na akavikatia tama. Kwenye lulu alimuona Juana na Koyotito na yeye mwenyewe wakiwa wamesimama, wakipiga magoti mbele ya madhabahu kuu, na sababu sasa waliwea kulipia, walikuwa wakifungishwa ndoa. Kwa upole akasema:

“Tutafunga ndoa kanisani.”

Ndani ya lulu aliona jinsi walivyokuwa wamevaa. Juana ndani ya mtandio mpya kabisa na sketi mpya. Na chini ya sketi hiyio ndefu Kino alimuona kuwa amevaa viatu. Picha hiyo ilikuwa ndani ya lulu. Yeye mwenyewe alijiona akiwa amevaa nguo mpya nyeupe akiwa na kofia mpya, na si kofia ya majani bali ya ngozi bora. Alikuwa pia amevaa viatu, si makubazi bali viatu vyenye kamba kabisa. Lakini zaidi ya wote alikuwa ni Koyotito. Alivaa suti ya kibaharia ya bluu kutoka Marekani, na kofia ndogo ya kinahodha ambayo Kino amewahi iona siku moja meli ya watalii ilipotembelea ghuba yao. Vitu vyote hivi Kino aliviona ndani ya ile lulu inayong’aa, kisha akasema:

“Tutapata nguo mpya.”

Na muziki wa lulu ukaingia masikioni mwake kama sauti ya tarumbeta.

Baada ya hayo, kwenye uso wa kupendeza wa lulu ikatokea picha ya mkuki wa kuvulia, aliokuwa nao aliupoteza mwaka uliopita. Mkuki mpya wa chuma wenye ringi mwishoni mwa mshikio. Kwa taabu akili yake ikaenda mbali zaidi; bunduki. Kwanini isiwe bunduki wakati tayari ni tajiri mkubwa? Hapo Kino alimuona Kino ndani ya lulu, alikuwa ameshika bunduki aina ya Winchester. Ilikuwa ni ndoto ya ajabu ya mchana lakini yenye kuburudisha sana. Jambo hili alilitamka kwa kubabaika-“Bunduki, labda na bunduki pia.”

Wazo la bunduki ndilo lililofungua kila kitu. Kwa yeye kumiliki bunduki ni suala lililoonekana kama haliwezekani, lakini kama sasa anafikiria kumiliki bunduki, basi kila kitu kinawezekana. Inasemwa kuwa binadamu hawaridhiki. Ukiwapatia kitu kimoja watataka na kingine na kingine. Na hili huzungumzwa kama ni jambo baya, lakini hii ni moja ya sifa bora kabisa ya binadamu. Ndiyo inamfanya awe bora kuliko wanyama ambao wanaridhika na walichonacho.

Majirani walizidi kubanana huku wakiwa kimya ndani mule. Walitikisa vichwa vyao kukubaliana na ndoto zake za ajabu. Mmoja wao aliyekuwa nyuma aliwaambia waliokuwa nje:

“Atanunua bunduki.”

Muziki wa lulu ulipokuwa unapiga ndani ya Kino. Juana alimuangalia, macho yake yakistaajabia ujasiri wa Kino na ndoto zake. Mara baada ya kuona kila kitu kinawezekana Kino akawa amepata nguvu za ajabu. Ndani ya lulu alimuona Koyotito akiwa amekaa kwenye dawati dogo shuleni. Alikuwa amevaa koti la suti, shati jeupe na tai ya hariri. Zaidi ni kuwa Koyotito alikuwa akiandika kwenye karatasi kubwa. Kino aliwaangalia jirani kwa uso uliokaza; “Kijana wangu atakwenda shule,” alisema. Majirani zake wakapigwa na butwaa. Juana akavuta pumzi ndefu, macho yake yaling’aa. Haraka akageuka kumtazama Koyotito aliyekuwa mikononi mwake kuhakikisha iwapo jambo hilo linawezekana.

Lakini uso wa Kino uling’aa kwa unabii. “Kijana wangu atasoma na kufungua vitabu, naye atajua kuandika, na mambo haya yatatufanya kuwa huru sababu atakuwa anauelewa-atajua mambo, na kupitia yeye nasi tutajua mambo.” Na ndani ya lulu, Kino alijiona yeye akiwa na Juana wamechuchumaa ndani ya nyumba yao ya miti pembeni ya moto huku Koyotito akisoma kitabu kikubwa.

“Hivi ndivyo lulu itafanya,” aisema Kino. Kino hajawahi maishani mwake kusema maneno mengi kama siku hiyo. Ghafla akaanza kuogopa kwa jinsi alivyoongea sana. Alifumba mkono wake kuifumba lulu mkononi mwake na kuinyima mwanga. Kino alijawa na wasiwasi. Wasiwasi wa mtu anayesema, “Nitafanya” bila kuwa na uhakika.
 
Kufika sasa majirani walikuwa wanajua wameshuhudia jambo la ajabu sana. Walijua kuwa kuanzia sasa watahesabu tarehe wakirejelea lulu ya Kino, na kuwa watazungumzia jambo hili kwa miaka mingi ijayo. Baada ya mambo haya kupita walitarajiwa kuongelea jinsi Kino alivyoonekana siku hiyo, mambo aliyoongea na jinsi macho yake yalivyong’aa, watasema. “Hakuwa mtu wa kawaida. Kulikuwa na nguvu ya ziada ndani yake na ndiyo ulikuwa mwanzo ya yote hadi kuwa mtu mkuu namna hii. Nilishuhudia yote kwa macho yangu.”

Na kama mipangoya Kino haitazaa kitu, majirani hao hao watasema. “Palepale kichaa cha ujinga kilimpanda na akaanza kuonge upumbavu. Mungu atuepushe na mambo hayo. Mungu ndiye alimuadhibu Kino sababu aliasi na kwenda kinyume na utaratibu wa mambo.Si mnaona yaliyompata. Mimi mwenyewe nilishuhudia akili ilipomruka.”

Kino aliangalia kwa makini mkono aliokuwa amefumba lulu, alama za alimojikwaruza wakati amepiga geti zilionekana.

Sasa giza lilianza kuingia. Juana alimzungushia mtoto mtandio na kisha akaenda kwenye sehemu ya kuwashia moto na kutoa kaa la moto kutoka kwenye majivu. Aliweka vijiti vichache juu yake na kuupuliza hadi ulipowaka. Mwanga wa moto ulichezacheza kwenye sura za majirani, walijua kuwa sasa wanapaswa kwenda makwao kuandaa chakula lakini mioyo yao ilikuwa mizito.

Giza lilikuwa limeshaingia minong’ono ilipoingia ndani ikipita toka kwa mtu hadi mtu.

“Padri anakuja-kasisi anakuja.”wanaume walivua kofia zao na kupisha njia mlangoni, wanawake nao walijitanda ushungi vichwani na kuinamisha macho yao chini. Kino na kaka yake Juan Tomas walisimama. Kasisi aliingia, alikuwa ni mzee mwenye mvi lakini mwenye macho makali ya ujana. Aliwachukulia watu hawa kama watoto na alishughulika nao kama anashughulika na watoto.

Kwa sauti ya upole padri akasema, “Kino, jina lako ni la mtu mkuu sasa, baba wa kanisa.”

Aliongea kama vile anatoa baraka.

“Mtu wa jina lako alilishinda jangwa na alinyenyekeza mioyo ya watu wako, hujui kuhusu hilo? Limeandikwa vitabuni.”

Kino alitupa jicho mara moja kumuangalia Koyotito aliyekuwa amepakatwa na Juana. “Siku moja,” alisema kichwani mwake, “Kijana wangu atafahamu yaliyoandikwa vitabuni na ambayo hayakuandikwa.” Wakati huu muziki ulikuwa umetoka kichwani mwa Kino, lakini kwa mbali ala ya muziki wa adui ilianza kusikika. Kino akawatazama majirani zake kuona ni nani ameleta wimbo huo.

Kasisi akaanza kuongea tena. “Nimepata habari kuwa umepatwa na bahati kubwa sana, lulu bora kabisa.”

Kino akafungua mkono wake na kuonyesha lulu yake, kasisi alichunguza kidogo ukubwa na uzuri wa lulu ile kisha akasema, “Natumaini utakumbuka kutoa shukrani mwanangu. Kwa yule aliyekupatia hazina hii, na kuomba upate muongozo wa maisha yako.”

Kino alitikisa kichwa kuitikia kama mtu asiyeelewa kitu, Juana akaongezea kwa kusema. “Tutafanya hivyo Padri. Na sasa tutafunga ndoa, Kino kasema hivyo.” Hapo aliwageukia majirani ambao walitikisa vichwa kuunga mkono maneno yake.

Padri akasema, “Inapendeza kuona kuwa mawazo yenu ya kwanza ni mawazo mazuri. Mungu awabariki wanangu.” Hapo aligeuka na kuondoka zake, watu walimpisha njia apite.

Sasa Kino akawa ameifumba tena lulu yake mkononi. Na alikuwa akitazama huku na huko kwa mashaka, akijaribu kusikia wimbo wa adui ulioimbwa kwa sauti kali dhidi ya muziki wa lulu.

Majirani waliondoka kwenda majumbani mwao, na Juana akachuchumaa mbele ya moto na kutenga chungu chake cha maharage ya kuchemsha motoni. Kino alienda kusimama mlangoni na kuanza kutazama nje. Kama siku zote, alisikia harufu ya moshi kutoka nyumba mbalimbali, na aliweza kuona nyota zikimetameta, na akahisi unyevunyevu wa hewa ya usiku hivyo akajitanda puani kujikinga. Yule mbwa mkondefu akamfuata kumsalimu, Kino alimtazama lakini hakumuona. Mawazo yake yalikuwa mbali kabisa, mbali ya upeo, sehemu yenye baridi na pweke. Alijihisi mpweke asiye na ulinzi wowote. Sauti za nyenze, na vyura zilionekana kama ni ala ya uovu. Kino alianza kutetemeka hivyo alikumbatia zaidi blanketi lake. Bado alikuwa ameibana lulu yake mkononi, ilikuwa ya moto na nyororo.

Nyuma yake alimsikia Juana akitengeneza keki na kuziweka kwenye chombo cha kuokea. Kino alihisi joto na usalama kwa familia yake uko nyuma yake, wimbo wa familia ulisikika nyuma yake kama mungurumo atao paka mwenye furaha.

Kwa kino kusema mipango yake tayari akawa ameunda kitu. Mpango ukishapangwa unakuwa kitu halisi, kama tu vitu vingine halisi. Kamwe hauwezi kuharibiwa, lakini unaweza kushambuliwa kirahisi. Mipango ya baadaye ya Kino ilikuwa kitu halisi, lakini baada ya kuanza kuitekeleza, kuna nguvu zilikuwa zimejipanga kuiharibu, naye alifahamu hilo. Na alikuwa amejiandaa na shambulizi lolote. Na pia Kino alitambua kuwa miungu haipendi mipango ya wanadamu. Pia alifahamu kuwa miungu haipendi mafanikio ya wanadamu isipokuwa yatokee kwa bahati tu. Alifahamu kuwa miungu hulipa kisasi kwa mwanadamu anayefanikiwa kwa jitihada zake mwenyewe. Kwa hiyo Kino alikuwa anaogopa kupanga mipango, lakini kwa vile amekwishaipanga, hangeweza kuiharibu. Na ili kukabiliana na mashambulizi ya dunia, alianza kujipanga dhidi yake. Akili yake na macho yake yalikaa chonjo dhidi ya hatari kabla haijatokea.

Alipokuwa amesimama mlangoni pale, aliona watu wawili wakija; mmoja wao alikuwa amebeba taa ya chemli ambayo ilikuwa ikimulika njia. Waliingia ndani ya fensi ya nyumba yake na kufika mlangoni. Kino aliwatambua kuwa mmoja ni daktari, na mwingine ni kijakazi wake aliyemfungulia mlango asubuhi ile.

Daktari alianza kwa kusema, “Sikuwepo ulipokuja asubuhi ya leo. Lakini punde tu nilipopata nafasi nimeharakisha kuja kumuona mtoto.”

Kino alisimama pale mlangoni, ameuziba wote. Chuki na hasira viliwaka machoni mwake, na uoga pia. Mamia ya miaka ya kukandamizwa yalikuwa ndani yake.

“Kwa sasa mtoto yupo vizuri,” alisema Kino kwa mkato.

Daktari alitabasamu lakini macho yake yaliyozibwa na nyama za unene hayakutabasamu.

Akasema, “Rafiki yangu, nyakati nyingine sumu ya nge huonyesha hali ya kushangaza sana. Unaweza kuona kama mgonjwa anapata nafuu, lakini bila kutarajia-pufu!” Daktari akaweka begi lake karibu na mwanga wa taa. Alijua watu wa jamii ya Kino huamini vifaa hivyo. “Nyakati nyingine,” aliendelea kusema Dktari. ”Nyakati nyingine mguu unaweza kulemaa au jicho kupofuka au mgongo kudhurika. Rafiki nafahamu habari ya kudungwa na nge, nami naweza kutibu.”

Kino alihisi hasira na chuki vikiyeyuka kuwa uoga. Hakuwa na uelewa wowote, pengine daktari huyu anajua zaidi. Hakutaka kuhatarisha maisha ya mtoto na akijua kabisa yeye haelewi chochote juu ya mambo ya tiba, daktari anaweza kuwa anelewa kitu. Alikuwa kwenye mtego ambao watu wake siku zote hujikuta ndani yake. Na atakuwa kwenye mtego huo(kama alivyosema mwenyewe) hadi hapo atakapokuwa na uhakika na mambo yaliyomo kwenye vitabu. Mpaka wakati huo, hakutaka kuhatarisha maisha ya mtoto wake sasa. Alisimama pembeni na daktari na kijakazi wake wakaingia ndani kwake.

Juana akasimama na kurudi nyuma alipomuona daktari akiingia, kisha akamfunika mtoto wake kwa mtandio hadi usoni. Daktari alipomfuata akiwa tayari kumhudumia mtoto, yeye alimkumbatia mtoto hata zaidi huku akimuangalia Kino ambaye alikuwa amesimama huku vivuli vya miale ya moto vikimchezacheza usoni.

Kino alimpa ishara kwa kutingisha kichwa, na hapo Juana alimruhusu daktari amchukue mtoto.

“Inua taa,” daktari alimwambia kijakazi wake na kijakazi akaiinua juu. Daktari akaangalia kidonda cha mtoto. Akatulia kidogo akitafakari kisha akafungua macho ya koyotito na kuyachunguza huku Koyotito akifurukuta mikononi mwake. Akatingisha kichwa na kusema:

“Kama nilichofikiria, sumu imeingia sana ndani na itamdhuru hivi punde. Njoo ujionee,” alisema huku akifungua macho ya Koyotito. “Unaona, ni ya bluu.” Kino alitizama kwa wasiwasi na aliona kuwa kulikuwa na ubluu kidogo, hakufahamu kama ubluu huo ni wa siku zote au la. Vyovyote vile, mtego ukawa umeshategwa. Hakuweza kufanya maamuzi kwa kukisiakisia.

Macho ya daktari yaling’aa kwa furaha. “Nitampatia dawa ya kupambana na sumu.” Alisema huku akimpa Kino mtoto.

Hapo akatoa chupa ndogo iliyokuwa na unga mweupe kutoka katika mkoba wake na tembe moja. Alijaza tembe ile kwa unga ule kisha akaifunga. Akafanya hivyo kwa tembe ya pili pia, alifanya kazi yake kitaalamu sana. Alimchukua mtoto na kumminya mashavu mpaka alipoachama mdomo. Kwa mikono yake minene aliweka tembe ile mdomoni mwa Koyotito ndani kabisa kadri alivyoweza. Kisha akachukua maji na kumywesha, Koyotito alikunywa na kazi ikawa imekwisha. Alitazama tena macho ya mtoto kisha akatulia kama mtu mwenye fikra nyingi.

Mwishowe alimkabidhi Juana mtoto, na kumgeukia Kino. “Nafikiri sumu itafanya kazi yake baada ya saa moja,” akasema. “Dawa itamsaidia mtoto dhidi ya madhara yake, lakini baada ya saa nitafika. Pengine nimeiwahi.” Alivuta pumzi ndefu na kutoka nje ya nyumba, kijakazi wake alimfuata huku ameshika taa.

Hapo juana akawa amepewa mtoto na akawa amembeba kwenye mtandio wake, alikuwa akimuangalia kwa wasiwasi sana. Kino akamsogelea, alifunua mtandio na kumuangalia mtoto. Alitaka kumfungua mtoto macho, hapo ndipo akakumbuka lulu iliyokuwa mkononi mwake.

Hapo Kino alienda kwenye sanduku lililokuwa pembeni na kuchukua kipande cha kitambaa. Aliiviringisha lulu ndani ya kitambaa hicho. Akaenda kwenye pembe moja ya nyumba yake na akachimba shimo dogo kwa vidole, aliweka lulu yake humo na kufukia. Akasawazisha pale juu ili alama isionekane kisha akaenda motoni ambapo Juana alikuwa amechuchumaa akimtazama mtoto usoni.
 
Hapo Kino alienda kwenye sanduku lililokuwa pembeni na kuchukua kipande cha kitambaa. Aliiviringisha lulu ndani ya kitambaa hicho. Akaenda kwenye pembe moja ya nyumba yake na akachimba shimo dogo kwa vidole, aliweka lulu yake humo na kufukia. Akasawazisha pale juu ili alama isionekane kisha akaenda motoni ambapo Juana alikuwa amechuchumaa akimtazama mtoto usoni.

Daktari alikuwa amefika nyumbani kwake, alikuwa ameketi kitini akitazama saa yake. Vijakazi wake walimletea chakula, chokleti, keki za sukari na matunda, alikuwa akikitizama chakula kile kama mtu asiyeridhika na maisha yake.

Kwenye nyumba za majirani wa Kino, maongezi ambayo yangezungumzwa kwa siku nyingi zijazo yalikuwa yameanza. Majirani walitumia vidole vyao kuelezea ukubwa wa lulu, na walionyesha ishara kwa mikono kuonyesha jinsi ilivyokuwa nzuri. Kutoka sasa watakuwa makini kuwatazama Kino na Juana kuona kama utajiri utawabadilisha, maana utajiri hubadilisha watu wote. Kila mtu alijua kwanini daktari alifika kwa Kino. Hakuweza kuficha azma yake vizuri, na ilieleweka vema.

Kwenye ghuba, kundi la samaki wadogo walikuwa wakikimbia, na kuruka juu kuepuka kundi la samaki wakubwa waliotaka kuwala. Na wakazi wa pale waliweza kusikia sauti za samaki wadogo wakijipiga majini, na vishindo vya samaki wakubwa wakijipiga majini kadri karamu ya samaki wakubwa ilivyoendelea. Hewa yenye unyevunyevu ilitoka kwenye ghuba na kutua kwenye vichaka na miti midogo, ikiwa kama matone mdogo ya maji ya chumvi. Panya wa usiku nao walijipenyeza ardhini huku mwewe wa usiku wakiwawinda kimya-kimya.

Yule mbwa mweusi aliyekonda alifika kwenye mlango wa nyumba ya Kino na kuanza kumtazama Kino hakuingia ndani, bali alikuwa akimuangalia Kino kwa makini alipokuwa akila maharage, akiyakombeleza kabisa na kusafisha sahani kwa mkate, na kisha kula mkate na kushushia vyote kwa kinywaji cha kienyeji cha wamexico kiitwacho pulque

Kino alikuwa amemaliza kula na sasa alikuwa akinyonga sigara yake pale Juana alipomwita. “Kino.” Kino, aligeuka, kisha akainuka na kumfuata haraka maana alimuona kama mtu mwenye mashaka. Alisimama kumuangalia lakini mwanga ulikuwa hautoshi, alisogeza vijiti kadhaa motoni, na moto ulipowaka aliweza kuona sura ya Koyotito. Sura yake ilikuwa imevimba na alikuwa anatoa kelele kooni huku udenda ukimtoka. Misuli ya tumbo ilimkaza na alikuwa hoi kabisa.

Kino alipiga magoti pembeni ya mke wake. “Kumbe daktari alifahamu hili,” alisema. Kino alisema hilo lakini bado alikuwa na mashaka kichwani, alikuwa akikumbuka ule unga mweupe kwenye chupa. Juana alikuwa akitikisika huku na huko huku akisema maneno kadha wa kadha ya wimbo wa familia, akitumaini yataondoa hatari. Mtoto akatapika na kujinyonganyonga mikononi mwake. Sintofahamu ikamuingia Kino, na muziki wa uovu ulipiga kichwani mwake, na karibu ufukuzie mbali wimbo wa Juana.

Daktari alimaliza kula chokleti yake na kula vipande vya keki vilivyobakia. Alifuta mikono kwa kitambaa, akaangalia saa yake, na kuchukua mkoba wake.

Taarifa ya ugonjwa wa mtoto ilisambaa haraka kwa majirani, maana kwa watu maskini, ugonjwa ni adui namba mbili baada ya njaa. Wengine kwa sauti ya chini walikuwa wakisema, “Bahati huleta rafiki wabaya.” Kisha walitikisa vichwa vyao na kuamka kuelekea nyumbani kwa Kino.

Walisimama wakishangaa, na wengine wakisema kuwa jambo hili halikutakiwa kutokea wakati huo wa furaha. Na wengine walisema, “Yote mipango ya Mungu.” Wanawake wazee walichuchumaa pembeni ya Juana wakijaribu kumpa msaada wakiweza, au kumfariji wakishindwa.

Ghafla daktari akaingia akifuatiwa na kijakazi wake. Aliwatawanya wanawake wale wazee kama anatawanya kuku. Alimchukua mtoto na kuanza kumchunguza. “Sumu imefanya kazi yake,” alisema. “Nafikiri naweza kuizuia. Nitajitahidi kadiri ya uwezo wangu.” Aliagiza aletewe maji, na ndani ya kikombe aliweka matone matatu ya ammonia, hapo alifungua mdomo wa Koyotito na kumnywesha. Mtoto alifurukuta alipokuwa anakunywa, na Juana alimuangalia kwa macho yaliyojaa mashaka. Daktari alikuwa akimywesha mtoto dawa huku akiongea. “Ni bahati kuwa nafahamu mambo ya sumu ya nge, vinginevyo-“ akatikisa mabega kuonyesha ambacho kingetokea.

Lakini Kino bado alikuwa anashuku kitu, na hakuacha kuangalia mkoba wa daktari uliokuwa wazi, na ile chupa yenye unga mweupe. Polepole kukakamaa kwa Koyotito kulipungua na akawa ametulia mikononi mwa daktari, kisha akashusha pumzi ndefu na kulala, maana alikuwa kachoka sana sababu ya kutapika.

Daktari alimpa Juana mtoto na kusema. “Sasa atapona, nimeshinda.” Juana alimuangalia kwa kumstaajabia.

Sasa daktari akaanza kufunga mkoba wake. “Mnafikiri ni lini mtaweza kunilipa?” alisema kwa sauti ya upole.

“Mara tu nitakapo uza lulu yangu nitakulipa,” alisema Kino.

“Una lulu? Lulu nzuri?” aliuliza daktari kwa shauku.

Hapo majirani wakajibu kama vile wanaimba kiitikio cha wimbo. “Amepata lulu bora kuliko zote duniani,”walitengeneza duara kwa kidole gumba na kidole cha kwanza kuonyesha ni jinsi gani lulu hiyo ilivyokuwa kubwa.

“Kino atakuwa tajiri,” walisema kwa sauti kubwa. “Ni lulu ambayo hakuna mtu amewahi kuiona.”

Daktari alionekana kama ameshangazwa. “Sijasikia kuhusu hilo. Je, unaitunza kwenye eneo salama? Labda ungependa nikutunzie kwenye kasiki langu?”

Hapo macho ya Kino yakawa makali, na mashavu yakamkaza. “Nimeitunza sehemu salama,” akasema. “Kesho nitaiuza na kukulipa deni lako.”

Daktari alitingisha mabega, na hakuacha kumuangalia Kino machoni. Alijua kuwa lulu itakuwa imefukiwa mle ndani, hivyo alijua kuwa Kino ataangalia sehemu alipoifukia. “Itakuwa hasara iwapo itaibiwa kabla hujaiuza,” alisema daktari, na hapo aliona macho ya Kino yakicheza bila kutaka, yakielekea sakafuni, karibu na mlingoni wa kwenye kona ya nyumba.

Baada ya daktari kuondoka, na majirani kujivutavuta kuelekea majumbani mwao, Kino alichuchumaa pembeni ya moto na kusikiliza sauti ya usiku. Sauti nyororo ya mawimbi yakipiga ufukweni, sauti ya upepo ukipiga paa la nyumba yake na sauti nyororo za majirani zake wakiwa majumbani mwao. Watu hawa walikuwa hawalali kimya usiku wote; mara kadhaa walikuwa wakiamka na kuzungumza kidogo na kisha kulala tena. Baada ya kitambo kidogo Kino aliamka na kwenda mlangoni mwa nyumba yake.

Alinusa harufu ya upepo wa baharini, na kutega sikio kusikiliza sauti yoyote ngeni,sauti ya siri inayo nyatia, na macho yake yakachunguza gizani, muziki wa uovu ulikuwa unasikika kichwani mwake, alikuwa anaogopa na wakati huohuo yuko tayari kwa lolote. Baada ya kuchunguza gizani, akaenda kwenye ile nguzo; sehemu alipoifukia lulu yake. Aliichimbua na kwenda nayo kwenye mkeka wake wa kulalia. Chini ya mkeka alichimba shimo lingine dogo na kuifukia.

Juana, aliyekuwa amekaa karibu na moto, alimuangalia kwa macho ya kuhoji, na mara alipomaliza kuifukia, alimuuliza, “Unamuogopa nani?”

Kino alifikiria cha kujibu kwa muda kidogo, na mwishowe akasema, “Kila mtu.”

Baada ya kitambo kidogo wakalala kwenye mkeka wao. Usiku huo Juana hakumuweka mtoto kwenye kitanda chake cha bembea bali alimkumbatia pembeni yake na kumfunika kwa mtandio wake. Mwishowe na moto ukazima na kukawa giza.

Lakini akili ya kino ilikuwa ikifanya kazi hata katika usingizi. Aliota akimuona Koyotito akiweza kusoma, kwamba mmoja wa watu wake anaweza kumueleza ukweli wa mambo. Katika ndoto yake, Koyotito alikuwa akisoma kutoka katika kitabu kilichokuwa kikubwa kama nyumba, herufi zilikuwa kubwa kama mbwa, na maneno yalikuwa yakikimbia kama farasi alipokuwa akiyasoma. Mwishowe aliona giza likitanda juu ya ukurasa ule, pamoja na giza hilo, muziki wa uovu ukaja tena, huo ulimfanya Kino kujitingisha; kujitingisha huko kulimuamsha Juana ambaye alifungua macho yake. Punde kidogo Kino naye akamka, huku muziki wa uovu ukipiga ndani yake, alilala kimya huku akiwa katega masikio kwa makini.

Akiwa katulia hivyo akasikia sauti ndogo kutoka kwenye pembe ya nyumba. Sauti ndogo kiasi kwamba labda ilikuwa ni mawenge yake tu. Alisikia sauti ndogo ya hatua, na sauti ya mtu akipumua kwa mbali. Kino alibana pumzi na alitulia kimya kusikiliza. Kwa muda, hakusikia sauti yoyote. Hapo Kino akakata shauri kuwa pengine hakuna sauti yoyote bali mawazo yake tu. Lakini ghafla akaona mkono wa Juana ukimgusa kumuonya, kisha sauti ikasikika tena, sauti ya hatua za kunyata, na ya vidole ikichakua ardhini.

Sasa uoga wa ajabu ukamjaa Kino, na kama kawaida yake, uoga huo ulikuja na hasira kali. Kino akapeleka mkono kifuani mwake ambako kisu chake kilikuwa kimefungwa kwa kamba shingoni. Ghafla aliruka kama paka mwenye hasira huku huku akichoma kwa kisu chake kitu cheusi ambacho alihisi kipo kwenye pembe ya nyumba yake. Katika kuchoma kwake akahisi amegusa nguo, akachoma pale aliposhika lakini akakosa, akachoma kwa mara ya pili na akahisi kisu kikipenya kwenye nguo. Lakini ghafla akaona nyotanyota na kichwa chake kikipata maumivu makali. Zilisikika vurugu mlangoni pake, vishindo vya kukimbia na baadaye kimya kabisa.

Kino aliweza kuhisi damu ya moto ikitiririka katika paji lake la uso, na akamsikia Juana akimwita. “Kino! Kino!” Sauti yake ilikuwa imejaa uoga.

Akajibu, “Nipo salama, mvamizi amekimbia.”

Akapapasapapasa kurudi mkekani. Juana alikuwa ameanza kuwasha moto. Alitoa kibonge cha moto majivuni na kudondoshea vipande vya gunzi la mahindi juu yake na kupuliza na moto ukawaka na kuangaza nyumba yao. Baada ya hapo akaenda eneo anapoficha vitu na kuchukua mshumaa wa sala na kuuwasha. Alifanya hayo yote kwa haraka sana huku akijiongelesha chinichini. Alitumbukiza mtandio wake kwenye maji na kumfuta Kino damu kutoka kwenye mikwaruzo aliyoipata kwenye paji la uso.

“Sijaumia sana,” alisema Kino lakini sauti yake na macho yake yalikuwa makali, hasira kali ilikuwa inawaka ndani yake.

Sasa dukuduku lililokuwepo ndani ya Juana likatoka. “Hiki kitu ni mkosi,” alisema kwa jazba. “Kitu hiki ni kama dhambi! Kitatuangamiza,” hapo sauti yake ikageuka kuwa kali. “Kitupilie mbali. Tukiponde na mawe. Tukifukie sehemu ya mbali. Tukitupe baharini. Kimeleta mkosi. Kino mume wangu, kitatuangamiza.” Katika mwanga, sura yake ilionekana jinsi ilivyojaa wasiwasi.

Lakini uso wa Kino ulionyesha utulivu mkubwa. “Hii ndiyo nafasi yetu pekee. Mtoto wetu ni lazima aende shule. Anatakiwa kutoka kwenye kifungo tulichomo.”

“Kitatuangamiza sote, hata na mtoto wetu pia.” Alipiga kelele Juana.

“Nyamaza,” alifoka Kino. “Asubuhi tutaiuza, na mkosi utaondoka na kubaki baraka tu. Kwa sasa nyamaza kimya,” macho yake yalionyesha hasira aliyokua nayo. Hapo akakumbuka kuwa bado ana kisu chake mkononi. Alikiinua na kukitazama, akaona kuna alama ya damu kwenye kisu. Alitaka kukipangusa kwenye suruali yake lakini akasita, akakichomeka chini na kukipangusa kwenye mchanga.

Kwa mbali jogoo walisikika wakiwika, hali ya hewa ilibadilika na kukakucha. Upepo wa asubuhi ulichafua maji ya ghuba ile, na kelele za mikoko ikipigwa na upepo ilisikika. Kino aliinua mkeka wa kulalia na kuchimbua lulu yake, aliiweka mbele yake na kuanza kuistaajabia.

Uzuri wa lulu kwenye mwanga wa mshumaa uliuburudisha ubongo wake. Ilikuwa yenye kupendeza na nyororo sana na ilitoa muziki wake-muziki wa ahadi na shangwe. Ilikuwa ni msingi wa maisha mazuri ya baadaye, maisha ya usalama. Mng’ao wake ulikuwa ni ahadi ya dawa dhidi ya magonjwa, ukuta dhidi ya dharau na ulifunga milango dhidi ya njaa. Kadiri Kino alivyoitazama ndivyo alivyopata utulivu zaidi. Ndani ya lulu aliweza kuona taswira ya mshumaa wa ibada uliokuwa ukiwaka, na masikioni mwake alisikia muziki mzuri wa chini ya bahari. Juana, aliyekuwa akimtizama kwa kuibia; alimuona akitabasamu. Na sababu kwa namna fulani walikuwa ni kitu kimoja, wenye lengo moja, akatabasamu pamoja naye.

Walianza siku hiyo kwa matumaini makubwa.
 
SURA YA 4

Ni jambo la kushangaza sana jinsi mji mdogo unavyoendesha mambo yake na vitu vyote ndani yake. Kama kila mtu, mwanaume, mwanamke, mtoto na mtoto mchanga anafanya mambo kulingana na utaratibu, hafanyi lolote tofauti, haumwi, hafanyi chochote kufanya akili za watu zitilie maanani, wala hafanyi chochote kuathiri mtiririko wa mambo mjini hapo, basi mtu huyo anaweza kutokomea na asijulikane kabisa. Lakini mtu mmoja tu akienda kinyume na taratibu za kawaida, akili ya watu wa mji huamka kwa taharuki na habari husambaa kwenye njia zake mjini. Mwishowe mji wote huwasiliana kama kitu kimoja.

Hilo ndilo lililotokea La Paz; asubuhi na mapema ilikwisha julikana mjini kote kuwa Kino alikuwa akienda kuuza lulu yake siku hiyo. Ilijulikana kwa majirani kwenye nyumba za miti, ilijulikana miongoni mwa wavuvi wa lulu, miongoni mwa wachina wanaouza maduka, ilijulikana kanisani; maana wavulana wa altareni walinong’ona kuhusu jambo hilo miongoni mwao. Habari ilipenya kwa watawa; maana ombaomba wa mbele ya kanisa waliizungumza, walitumaini watapata sehemu yao ya bahati ile. Karibu wanunuzi wote wa lulu waliijua habari ile. Siku hiyo ilipofika, kila mnunuzi alikaa peke yake ofisini mwake, kila mmoja akizungusha zungusha lulu mkononi mwake, akiwaza sehemu yake kwenye jambo hilo.

Ilikuwa inadhaniwa kuwa wanunuzi wa lulu walikuwa ni watu binafsi wasio na mahusiano yoyote. Ilidhaniwa kuwa walikuwa wakishindana kila mmoja akitaka kununua lulu. Hapo zamani ilikuwa hivyo. Lakini ilikuwa ni njia yenye hasara, mara nyingi katika kushindana kwao walijikuta wakilipa bei kubwa kuliko bei halisi. Huu ulikuwa ni ufujaji na haukupaswa kuendelea. Sasa kulikuwa na mnunuzi mmoja tu wa lulu, lakini mwenye mikono mingi. Na wanunuzi wote waliokuwa wakimsubiria Kino walikuwa wanajua bei ya kununulia. Walijua kikomo cha mwisho cha bei wanayoruhusiwa kutaja, na kila mmoja alijua njia anayopaswa kutumia.

Japo wananunzi hawa, kwa kununua lulu ya Kino hawatapata faida yoyote zaidi ya mishahara yao, lakini walikuwa na shauku kubwa. Kulikuwa na shauku katika kuwinda, kama kazi ya mtu ni kushusha bei, basi anatakiwa kuburudika awezapo kushusha bei chini kadiri inavyowezekana. Kila mtu duniani hufanya kazi zake kadri ya uwezo wake, hakuna anayefanya chini ya kadri ya uwezo wake, haijalishi yeye mwenyewe ana maoni gani kuhusu hili. Mbali na zawadi anazoweza kupata, mbali na maneno ya sifa, mbali na kupandishwa cheo, mnunuzi wa lulu alikuwa ni mnunuzi wa lulu tu, na mnunua lulu hodari na mwenye furaha ni yule anayenunua kwa bei ya chini zaidi.

Asubuhi hiyo jua lilikuwa la manjano na kali, lilivuta unyevu kutoka kwenye ghuba na kuuning’iniza hewani kama kitambaa, hapo ulichezacheza na kuathiri uoni. Kaskazini ya mjini ulionekana mlima, umbali wa maili zaidi ya miambili, na miteremko ya mlima huo ulifunikwa na misonobari, juu ya miti. Juu ya ukanda wa miti, kilele kirefu cha mwamba kilisimama.

Asubuhi hiyo mashua zilikuwa zimewekwa ufukweni; wavuvi hawakwenda kutafuta lulu, maana mambo mengi yalitarajiwa kutokea, na mambo mengi ya kuona Kino atakapokuwa anakwenda kuuza lulu yake.

Asubuhi hiyo majirani wa Kino walikaa wakipata kifungua kinywa kwa muda mrefu, walikuwa wakiongelea yale ambayo wangefanya iwapo wao ndiyo wangepata lulu ile. Mtu mmoja alisema kuwa angetoa kumpa Baba Mtakatifu wa Roma kama zawadi. Mwingine alisema kuwa angenunua wokovu kwaajili watu wafamilia yake. Mwingine aliwaza kuwa atachukua pesa na kuzigawa kwa watu maskini wa La Paz; wanne yeye aliwaza juu ya mambo yote mazuri anavyoweza kufanya mtu iwapo angekuwa na pesa kwa kuuza lulu ile. Misaada ambayo angeweza kutoa, zawadi na matendo mengine ya rehema ambayo mtu angeweza kufanya iwapo akiwa na pesa. Majirani wote walikuwa wakiomba utajiri wa ghafla wa Kino usimgeuze, usimfanye kuwa kama matajiri walivyo, usimfanye kuwa mlafi, mwenye chuki na kauzu. Kino alikuwa ni mtu aliyependwa na watu, itakuwa jambo la fedheha kama lulu ikimbadilisha. “Itakuwa hasara iwapo mke wake mwema na mtoto wao mzuri wakibadilishwa na utajiri.” Walisema.

Kwa Kino na Juana, asubuhi hiyo ilikuwa ni asubuhi muhimu kuliko zote katika maisha yao, ilifanana kwa umuhimu na siku ile ambayo mtoto wao alizaliwa tu. Siku hii ndiyo itaamua siku zingine zote zitakavyokuwa. Watakuwa wakisema, “Ilikuwa ni miaka miwili kabla hatujauza lulu,” au, “Ilikuwa ni majuma sita baada ya kuuza lulu.” Juana alimvalisha Koyotito nguo bora ambazo aliandaa kwaajili ya siku ya ubatizo; siku akipata pesa kwaajili ya ubatizo. Yeye mwenyewe alichana nywele zake, akazisuka na kuzibana nyuma kwa tepe nyekundu. Kisha akavaa sketi yake ya harusi. Walipomaliza kujiandaa jua tayari lilikuwa limekuwa kali. Japo nguo za Kino zilikuwa zimechakaa, lakini zilikuwa safi, na hii ndiyo ilikuwa siku yake ya mwisho kuvaa midabwaba. Kesho, au hata mchana wa leo atakuwa na nguo mpya.

Majirani zake walikuwa wakichungulia mlango wa Kino kupitia upenyo kwenye nyumba zao, nao pia walijiandaa na walikuwa tayari. Hakuna aliyejiuliza mara mbilimbili juu ya kuungana na Kino na Juana kwenda kuuza lulu. Walitegemewa kufanya hivyo, hilo lilikuwa ni tukio la kihistoria, watakuwa wendawazimu kama hawatakwenda na ingechukuliwa kama ishara ya kukosa urafiki.

Juana alijitanda mtandio wake kichwani vizuri na sehemu iliyobaki akamfunika Koyotito aliyembeba mikononi mwake. Kino alivaa kofia kubwa ya ukindu na kuitengeneza vyema kichwani mwake. Hakutaka kuivaa kizembe kama wavaavyo watu wasiooa au wasio na majukumu, wala si kuivaa kama wavaavyo wazee, bali aliinamisha kidogo mbele kuonyesha kuwa ni mtu makini, shupavu na anayejiamini. Kuna mambo mengi yanaweza kujulikana kuhusu mtu kutokana tu na jinsi alivyovaa kofia. Akavaa makubazi yake ya mtindo wa ndala. Lulu yake aliiviringisha kwenye kipande laini cha ngozi ya swala ambacho alikiweka ndani ya pochi ndogo ya ngozi, na pochi hiyo akaitia katika mfuko wa shati. Alikunja blanketi lake vizuri na kuliweka begani mwake. Sasa wote walikuwa tayari.

Kino alitoka ndani mwake kwa kujiamini, Juana alimfuata nyuma akiwa kambeba Koyotito. Walipokuwa wakitembea kupita njia safi kuelekea mjini, majirani zao walijiunga nao. Nyumba zilitapika watu na milango ilicheua watoto. Lakini sababu ya upekee wa tukio lenyewe, ni mtu mmoja tu ndiye alitembea pamoja na Kino; Kaka yake, Juan Tomas.

Juan Tomasa alimtahadharisha ndugu yake. “Unatakiwa kuwa makini wasije kukutapeli,” alimwambia.

“Nitakuwa makini sana,” alijibu Kino

“Hatujui maeneo mengine bei ya kununulia ni kiasi gani,” alisema Juan Tomas. “Tutajuaje bei halali kama hatujui hawa wanunuzi wanaenda kuuza kwa bei gani?”

“Hilo ni kweli,” alijibu Kino. “lakini tutajuaje? Sisi tupo hapa, hatuko huko kwa wanunuzi wengine.”

Walipokuwa wanatembea kuelekea mjini umati nyuma yao ukazidi kukua. Juan Tomas alikuwa na wasiwasi mwingi, akaendelea kusema.

“Kabla hujazaliwa mababu zetu walibuni mbinu ya kupata bei nzuri ya lulu zao. Waliona ni vema wakawa na wakala wao ambaye atachukua lulu zote na kwenda kuziuza kwenye mji mkuu na yeye kubaki na gawio lake dogo kama faida.”

Kino alitingisha kichwa na kusema, “Nafahamu, ilikuwa ni mbinu nzuri.”

Juan Tomas akaendelea, “Na walimpata wakala. Walikusanya lulu zao zote, na kumpatia akaziuze. Lakini tokea hapo hawakumsikia wala kumuona tena, na lulu zao zikawa zimepotea. Wakatafuta mtu mwingine na kumpatia lulu akauze, naye pia hakuonekana tena. Kuona hivyo, wakaachana na mpango huo na kurudi kama zamani.”

“Nafahamu,” alijibu Kino. “Nimewahi msikia baba yetu akisimulia . Lilikuwa ni wazo zuri, lakini lilikuwa ni kinyume na dini, na Padri aliweka hilo wazi kabisa. Kupotea kwa lulu ilikuwa ni adhabu kwa wale waliotaka kutekeleza majukumu yasiyo yao. Padri ameeleza waziwazi kuwa kila mtu; mke kwa mume ni kama mwanajeshi aliyetumwa na Mungu kulinda sehemu fulani ya ngome ya ulimwengu. Ngome zingine zipo kwenye mahandaki, na zingine chini kabisa ya ukuta kwenye giza. Lakini kila mmoja anatakiwa kubaki katika eneo lake la ulinzi na hatakiwi kutangatanga, kinyume na hivyo ngome inakuwa kwenye hatari ya uvamizi kutoka kuzimu.”

“Nimewahi msikia akihubiri hivyo,” alisema Juana Tomas. “Hutoa mahubiri hayo kila mwaka.”
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom