Simulizi: Utajiri Wa Damu

Simulizi: Utajiri Wa Damu

Asante Shunie love....kastory kashununuje, ndio kwanza nipo episode ya 10 ila nshadata nayo
 
Sehemu ya 22.

Catherine alijua kupiga pesa, aliuweka mwili wake katika mazingira ambayo kila mwanaume aliyemwangalia aliamini alikutana na msichana mrembo ambaye hakuwahi kumuona katika dunia hii.

Kila siku kazi yake hotelini hapo ilikuwa ni kulala na wanaume, alijua kazi kitandani, kila aliyelala naye alidiriki kusema msichana huyo alikuwa miongoni mwa wale waliokuwa wakicheza filamu za kikubwa kwani alifanya kila kitu walichokuwa wakifanya watu hao.

Watu walichanganyikiwa, Wazungu kumlipa dola mia tano halikuwa tatizo lolote lile kwani huduma ambayo walikuwa wakipewa ilikuwa tofauti na wanawake waliokuwa wakijiuza Ulaya au nchini Marekani.

Kila siku aliwatega kwa kuvaa nusu utupu, aliwajua Wazungu, miili yao ilipenda sana ngozi nyeusi hivyo alijua kabisa kama angeuweka mwili wake wazi kwa kiasi fulani basi wanaume wengi wangemkimbilia na ndivyo ilivyokuwa.

Alipanga dili na meneja wa hoteli hiyo, kila siku alikuwa mtu wa kuingia katika gari la watalii na kujifanya naye mtalii. Hakuwa mtu wa kuwahi, alihakikisha watu wote wamekaa na yeye ndiyo anafuata kuhakikisha anachafua hali ya hewa kitu kilichowafanya watu wote kumwangalia kwa matamanio makubwa.

Siku ambayo Gosling na mchumba wake, Maggie waliingia ndani ya gari hilo na yeye kuingia kwa kuchelewa, moyo wa mwanaume huyo ukashtuka na kuanza kudunda kwa nguvu, hakuamini kama angekutana na msichana aliyekuwa mzuri, mwenye umbo la kutamanisha kama Catherine
Kwanza akahisi kuwa msichana huyo alikuwa na mwanaume, akaangalia kule alipotoka ili kuona kama kungekuwa na yeyote ambaye angemfuata, hapakuwa na mtu,

akamwangalia alipoingia mpaka alipokwenda kukaa, alikuwa peke yake huku akijifanya kuwa bize kusikiliza muziki kwenye simu yake.
Akili ya Gosling haikutulia hata kidogo, alitamani muda wote amwangalie msichana huyo lakini alishindwa kwa kuwa Maggie alikuwa pembeni yake, tena alijifanya kujibebisha kupita kawaida.

“Nifanye nini? Mbona yule msichana mzuri hivi?” alijiuliza kwa sauti ya chini kiasi kwamba Maggie alisikia lakini hakuelewa mwanaume huyo alizungumza nini.
“Unasemaje?”
 
Sehemu ya 23.

“Najiuliza kuhusu hii Afrika, mbona imekuwa na mbuga nyingi kuliko zetu? Kwa nini lakini?” alidanganya, kwa jinsi alivyopachikia harakaharaka, ikamfanya Maggie kuhisi kile alichoambiwa na mchumba wake ndicho kile alichosema mara ya kwanza.
Akili yake haikuwa kwenye safari hiyo, alikuwa akimfikiria Catherine tu.

Msichana huyo alikaa kiti cha nyuma kabisa hivyo hata kugeuka alishindwa kwa kuwa Maggie angemshtukia lakini baada ya kukumbuka huko nyuma walikuwepo walinzi wake, akajidai kugeuka kwa lengo la kuzungumza nao.

“Mike!” aliita kwa sauti ya chini, hata Maggie aliposikia mlinzi anaitwa, hakuwa na wasiwasi, kijana huyo akamfuata.

“Ndiyo bosi!”
Gosling hakuongea kitu, akamuonyeshea ishara ya macho mlinzi wake huyo huku akimwangalia Catherine. Mike alijua bosi wake alimaanisha nini, alichokifanya ni kuitikia tu, ‘sawa’.

Mike akaondoka na kurudi nyuma kule, alichokifanya ni kumgusa Catherine begani, msichana huyo alipogeuka tu, akamuita kwa kidole.

“Mimi?” aliuliza huku akimwangalia.
“Ndiyo!”
Catherine akagundua tayari Mzungu alichanganyikiwa, kwa mapozi akainuka na kumfuata Mike pale alipokaa.
“Naomba namba yako! Bosi anaihitaji!” alisema Mike.

“Bosi gani?”
“Hutakiwi kumfahamu! Ila anaihitaji!” alisema Mike, hilo halikuwa tatizo, Catherine akampa.

Ishu ilikuwa ni namba tu, akatoa na Catherine kurudi katika kiti chake. Walipofika sehemu ya kuangalia wanyama, macho ya Gosling na wanaume wengine hayakutulia, muda wote yalikuwa yakimwangalia Catherine.

Na kwa sababu alijua alikuwa akiangaliwa na kila mtu basi ndiyo akazidisha maringo yake, pozi zikawachanganya wanaume kiasi kwamba kila mmoja akatamani kulala naye.
“Haiwezekani! Huyu lazima nilale naye,” alijiapiza Goslin.

Hawakutakiwa kukaa Ngorongoro ila kwa sababu ya Catherine, Gosling akamwambia Maggie ni lazima wachukue chumba mahali hapo kwani alichoka sana.

Msichana huyo akakubali na hivyo kuchukua chumba. Usiku huo wote walichoka lakini Gosling hakutaka kabisa kulala, alijiona kupumzika vya kutosha kila alipomfikiria msichana yule aliyemuona mbugani.
 
Sehemu ya 24.

Haraka sana akasimama na kumwambia Maggie alijisikia kunywa pombe hivyo anakwenda baa na angerudi baada ya dakika kadhaa.

“Sawa bebi,” alisema Maggie, akajigeuza upande mwingine na kuendelea kulala.
Haraka sana Gosling akatoka, kitu cha kwanza kilikuwa ni kuonana na Mike na kumuuliza kuhusu msichana huyo, alichukua namba au alikataa.

“Alinipa!”
“Wasiliana naye, ninataka nionane naye, yule msichana amenivuruga sana, Mike, umeona alivyokuwa mrembo lakini?” aliuliza Gosling.
“Ndiyo bosi. Halafu ana mwili!”

“We’ acha tu! Hebu mpigie simu umuite niende naye sehemu kuzungumza,” alisema Gosling na kumwambia akachukue chumba kingine ambacho yeye angekwenda kulala na Catherine kwa saa moja

“Sawa, haina shida,” alisema Mike, akaenda kuchukua chumba, akampa funguo bosi wake na kisha kumpiga simu Catherine ambapo ilipopokelewa tu, akamwambia kuwa bosi yule aliyehitaji namba yake alihitaji kuonana naye.

“Sawa. Nakuja hapo baa!” alisema Catherine.
“Hapana! Nenda chumba namba 22, utakutana naye,” alisema Mike.
“Sawa. Haina shida,” alisema Catherine na kukata simu.

Kule ndani alipokuwa, Gosling hakuwa akijiamini, alitetemeka huku kijasho chembamba kikimtoka. Hakuamini kama alikuwa akienda kukutana na msichana ambaye alimuona mara moja tu na kumpenda kutoka moyoni mwake.

Alikumbuka jinsi alivyokuwa, alilikumbuka umbo lake, mapaja yake yaliyonona na kiwowowo kilichomchanganya mno, aliona kabisa siku hiyo ingekuwa Vita Kuu ya Tatu ya Dunia.

“Hivi ni mimi kweli ndiyo nakwenda kulala na yule msichana ama? Mbona sijiamini? Gosling hebu tulie, jiamini, una pesa hutakiwi kuogopa...tulia baba...” alijisemea huku akishusha pumzi ndefu.

Mule chumbani hakutulia, wakati mwingine alikuwa akikaa kwenye kiti, mara asimame na kukaa kwenye kitandani, alipoona haitoshi, akaanza kutembea huku na kule, mara aende bafuni, mara chooni, kwa kifupi hakuwa akitulia.

Baada ya dakika chache akasikia mlango ukigongwa, moyo wake ukapiga paaa kwani alijua kabisa mtu aliyekuwa akiugonga alikuwa yule msichana mrembo, Catherine aliyekuwa amemuona mchana wa siku hiyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom