Simulizi: Utajiri Wa Damu

Simulizi: Utajiri Wa Damu

Sehemu ya 25.

Akamkaribisha, akajiweka kitandani na kunyoosha miguu kama mtu aliyetaka kulala lakini hakupenda kuona shuka likijikunja. Mlango ukafunguliwa na Catherine kuingia.

Mapigo ya moyo wa Gosling yakazidi kudunda kwa nguvu, kila alipomwangalia msichana huyo, alionyesha jinsi alivyokuwa mzuri, alimchanganya na kwa jinsi alivyovaa, ilimuonyesha kabisa hakuwa wa mchezomchezo.

Catherine, changudoa aliyejua kucheza na wanaume alijua kumvutia Gosling, alitembea huku akijifanya kuwa muoga mithili ya mwanamke bikira aliyetembelea chumba cha mwanaume.

Alikuwa akiangalia huku na kule, alijifanya kutokujiamini kabisa kiasi kwamba Gosling akapata moyo wa kujiamini, akainuka na kumsogelea Catherine, alipomfikia tu, akamkumbatia kana kwamba aliwahi kumuona kipindi kirefu nyuma.

“I miss you cute,” (Nimekukumbuka mrembo) alisema Gosling huku akimkumbatia msichana huyo, ili kumfanya Mzungu huyo aone aliokota embe dodo chini ya mpera, Catherine akajifanya kutetemeka mno.
“Than..k you,” (Nash..ukuru) alisema kwa kisauti chake cha kutetemeka.

Wakakaa kitandani na kuanza kuzungumza, muda wote Gosling alipomwangalia Catherine alikiri kukutana na msichana mrembo ambaye hakuwahi kukutana naye maisha yake yote.
Alimwangalia, alipendeza, alinona na pale kitandani alipokaa, mapaja yake yalionekana vizuri kabisa kwa sababu alivalia sketi nyingine fupi iliyoyaacha mapaja kuwa wazi.

“Nakupenda sana,” alitamka neno hilo Gosling kwa mara yasita chumbani humo huku akimwangalia Catherine ambaye bado alijifanya kuogopa kana kwamba alikuwa bikira.

“Nashukuru!” alisema Catherine.
Hawakuingia humo kupiga stori wala kuangaliana, waliingia humo kwa ajili ya kukiliza kitanda tu. Gosling hakutaka kuuliza, hapohapo akamsogelea msichana huyo, akaupeleka mkono wake kwenye paja la Catherine na kuanza kubadilishana mate.

Kama kawaida yake Catherine akajifanya kutokuweza kitu chochote kile, alijifanya kutetemeka kwa woga uliomfanya Gosling kujiamini kuwa yeye ndiye alikuwa masta na ilikuwa ni lazima kumfundisha Catherine namna ya kufanya mapenzi.
 
Sehemu ya 26.

Kichwa cha msichana huyo kilifikiria pesa lakini kwa jinsi alivyomuona Gosling, mwanaume huyo alionekana kumpenda kwa moyo wa dhati hivyo kama angetanguliza pesa mbele basi asingeweza kupata kile ambacho angepewa kwa mwanaume aliyeonekana kuwa na mapenzi ya dhati.

Akalazwa kitandani, Gosling akaja juu. Alikuwa mtu wa pupa, hakujua vizuri namna ya kumuandaa mwanamke na kumuweka tayari kwa ajili ya faragha.

Kwa Catherine aliona kama anazinguliwa, alimuacha Gosling apige pushapu zake, alipomaliza, akamlaza chini yeye na kumuacha aanze kutawala jukwaa.

Gosling alibaki kama mtoto, alifanyiwa mambo ambayo hakuwahi kufanyiwa tangu azaliwe, alipelekwa huku na kule, alifanyiwa hili na lile kiasi kwamba ndani ya dakika ishirini tu akahisi viungo vyake kama vimekatika.

“Una pumzi?” aliuliza Catherine huku akimwangalia Gosling.
“Kwani si tumemaliza?”
“Hapana! Kitabu chenye kurasa mia moja, ndiyo kwanza tumefika kurasa ya tano, una pumzi?” aliuliza Catherine.

Maneno hayo yakamfanya Gosling kushangaa, hakuamini kama mbwembwe zote zile alizofanyiwa ambazo zilimfanya kuwa hoi ndiyo kwanza ulikuwa mwanzo.

Alichoka lakini kwa sababu alikuwa na Catherine, alijua kumrudisha mwanaume mchezoni. Akashikwa huku na kule, mbavu zikashtuliwa, misuli ikachangamshwa na kujikuta akianza kupata nguvu mpya, Catherine akaja juu yake.

Ilikuwa ni kama vita kuu ya tatu, Catherine akatawala mchezo na kazi kubwa ya kulalamika ilikuwa kwa Gosling tu. Alichoka lakini kila wakati misuli yake ilikuwa ikishtuliwa na kujiona akipata nguvu mpya.

Mpaka wanamaliza baada ya saa mbili, kila mmoja alikuwa hoi, kwa shughuli aliyopewa Gosling, akawaona wanawake wote kuwa si ishu, yeye na Catherine mpaka kifo chake.
“Unaitwa nani?” aliuliza Gosling huku akimwangalia catherine.

“Catherine!”
“Ushawahi kuendesha Bughati au Ferrari?”
“Hapana!”

“Utatakiwa kuendesha sasa!”
“Nashukuru sana kipenzi!”
“Unaishi wapi?”
“Hapa hapa Arusha!”
“Kwako?”
“Hapana nimepanga!”
 
Sehemu ya 27.

“Unatakiwa kuwa na nyumba yako, tena ambayo hakuna sehemu nyingine inapopatikana! Umenifanya nijione mwanaume mpya, ninaahidi kutokukuacha hata kama nitaona mwanamke mwingine,” alisema Gosling huku akimwangalia Catherine kwa macho yaliyoonyesha ni kwa jinsi gani alikuwa akimpenda.

Ili kumuonyeshea alimaanisha, akamwachia kiasi cha dola elfu ishirini ambazo zilikuwa ni zaidi ya milioni arobaini na kuchukua business card, akampa kwa ajili ya mawasiliano na kuondoka.

Alipofika ndani, akaenda kulala huku kichwa chake kikimfikiria Catherine tu. Siku hiyo msichana huyo alibadilisha maisha yake kiasi cha kumuona Maggie aliyekuwa pembeni kama gogo fulani alilopelekewa kuwa nalo.
Alichanganyikiwa na Catherine, alimwahidi kumpa gari, kumjengea nyumba lakini hayo yote yalionekana si kitu kwa kile alichofanyiwa usiku huo.

Mule chumbani alipokuwa Catherine, hakuamini kama alipewa kiasi kikubwa ambacho hakufikiria hata siku moja kama angeweza kupewa.

Alimshukuru Mungu, alikumbuka aliahidiwa gari, akaingia Google na kuanza kuyaangalia magari hayo, hakuamini alichokiona, yalikuwa ni magari ya thamani ambayo ilikuwa ni zaidi ya dola laki tano au milioni moja ambazo zilikuwa ni zaidi ya bilioni moja.
“Mungu wangu! Huyu mwanaume ni tajiri ama?” alijiuliza.

Hapohapo akaichukua ile business card, akaliangalia jina lile na kuliandika katika tovuti ya Google, kilichokuja ndicho kilichomshtua zaidi, hakuamini macho yake baada ya kugundua kuwa Gosling alikuwa miongoni mwa mabilionea wakubwa duniani.
Akajuta, aliona kile alichomfanyia mwanaume yule hakikustahili, kwa pesa alizokuwanazo ilikuwa ni lazima kumfanyia zaidi ya vile alivyomfanyia.

Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa wawili hao kuonana. Hawakuishia kufanya siku hiyo, kila siku usiku walikuwa wakikutana chumbani na kufanya mapenzi kama kawaida yao.

Japokuwa walitakiwa kurudi Serengeti hotelini lakini kwa Gosling ilikuwa vigumu kukubali kwani aliona kama angekwenda huko Catherine angeibiwa na mwanaume mwingine.
Walipanga kukaa Tanzania kwa wiki moja lakini kwa kuwa Catherine alikuwa mtamu, wakakaa mwezi mzima ndipo wakarudi nchini Marekani.
 
Sehemu ya 27.

“Unatakiwa kuwa na nyumba yako, tena ambayo hakuna sehemu nyingine inapopatikana! Umenifanya nijione mwanaume mpya, ninaahidi kutokukuacha hata kama nitaona mwanamke mwingine,” alisema Gosling huku akimwangalia Catherine kwa macho yaliyoonyesha ni kwa jinsi gani alikuwa akimpenda.

Ili kumuonyeshea alimaanisha, akamwachia kiasi cha dola elfu ishirini ambazo zilikuwa ni zaidi ya milioni arobaini na kuchukua business card, akampa kwa ajili ya mawasiliano na kuondoka.

Alipofika ndani, akaenda kulala huku kichwa chake kikimfikiria Catherine tu. Siku hiyo msichana huyo alibadilisha maisha yake kiasi cha kumuona Maggie aliyekuwa pembeni kama gogo fulani alilopelekewa kuwa nalo.
Alichanganyikiwa na Catherine, alimwahidi kumpa gari, kumjengea nyumba lakini hayo yote yalionekana si kitu kwa kile alichofanyiwa usiku huo.

Mule chumbani alipokuwa Catherine, hakuamini kama alipewa kiasi kikubwa ambacho hakufikiria hata siku moja kama angeweza kupewa.

Alimshukuru Mungu, alikumbuka aliahidiwa gari, akaingia Google na kuanza kuyaangalia magari hayo, hakuamini alichokiona, yalikuwa ni magari ya thamani ambayo ilikuwa ni zaidi ya dola laki tano au milioni moja ambazo zilikuwa ni zaidi ya bilioni moja.
“Mungu wangu! Huyu mwanaume ni tajiri ama?” alijiuliza.

Hapohapo akaichukua ile business card, akaliangalia jina lile na kuliandika katika tovuti ya Google, kilichokuja ndicho kilichomshtua zaidi, hakuamini macho yake baada ya kugundua kuwa Gosling alikuwa miongoni mwa mabilionea wakubwa duniani.
Akajuta, aliona kile alichomfanyia mwanaume yule hakikustahili, kwa pesa alizokuwanazo ilikuwa ni lazima kumfanyia zaidi ya vile alivyomfanyia.

Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa wawili hao kuonana. Hawakuishia kufanya siku hiyo, kila siku usiku walikuwa wakikutana chumbani na kufanya mapenzi kama kawaida yao.

Japokuwa walitakiwa kurudi Serengeti hotelini lakini kwa Gosling ilikuwa vigumu kukubali kwani aliona kama angekwenda huko Catherine angeibiwa na mwanaume mwingine.
Walipanga kukaa Tanzania kwa wiki moja lakini kwa kuwa Catherine alikuwa mtamu, wakakaa mwezi mzima ndipo wakarudi nchini Marekani.
🔥🔥
🙏
 
Sehemu ya 28

Kila siku waliwasiliana kwenye simu, kuwasiliana skype kwa kuonana na hata kwenye barua pepe. Kila mmoja alionekana kumtamani mwenzake na kwa sababu Gosling alimuahidi msichana huyo vitu vingi, akamtumia pesa Catherine na kumwambia anunue kiwanja kwa ajili ya kujenga jumba kubwa na la kifahari.

Hilo halikuwa tatizo, kwa kuwa alipata alichokihitaji, akaachana na umalaya na kuanza kufanya mambo yake na mwanaume huyo. Kiwanja kikanunuliwa na kumpa taarifa kila kitu kilikuwa tayari.

“Naiagiza kampuni ya ujenzi ije kujenga nyumba huko, ifanane kama za huku,” alisema Gosling.

Alichokisema ndicho kilichotokea. Kampuni moja ya ujenzi kutoka nchini Marekani ikatumwa mpaka Arusha, ikawasiliana na Catherine na hatimaye ujenzi wa nyumba kubwa na ya kisasa kuanza kujengwa hapo.

Kila mtu aliyekuwa akiona ujenzi ulivyokuwa ukiendelea, hakuamini, alimuona Catherine kuwa na pesa nyingi kwani mpaka kampuni ya ujenzi nchini Marekani kwenda kujenga nyumba huko Arusha, ilionekana kumgharimu sana.

“Imekuwaje tena?” aliuliza Amanda huku akishangaa.
“Mzungu bwana!”
“Kafanyaje?”
“Yaani wewe acha. Jamani kweli umalaya unasaidia!”

“Hebu niambie kivipi shoga’angu, yaani unanihadithia vitu nusunusu sana,” alisema Amanda, alikuwa na kimuemue cha kutaka kufahamu ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.

Kwa kuwa alikuwa shoga yake, akaanza kumuhadithia kila kitu. Amanda hakuamini kile alichokisikia, yaani kwa miaka yote ya umalaya aliyofanya hakufanya jambo la maana kama ilivyokuwa kwa Catherine.
“Mh! Na bado una ile nyumba nyingine unayojenga!”

“Ile nitakupa wewe!”
“Kweli Cath!”
“Wala usijali! Tumuombe Mungu!”
Jumba lilitumia miezi miwili tu, likakamilika, akalipiga picha na kumtumia Gosling ambaye alionekana kufurahi mno.

Hilo kwake halikutosha, alijiona kufanya mambo madogo sana, alichokifanya ni kumfungulia kampuni ya utalii, kampuni ya kusambaza vyakula ili mwanamke huyo ayafurahie maisha ya kuwa na mwanaume mwenye pesa.

“Ila kwenye kusambaza chakula, mmh! Nitaweza kweli bebi?”aliuliza Catherine.
“Utaweza tu! Nataka kwanza uje huku kusomea!”
“Wapi?”
 
Sehemu ya 29

“Marekani! Nadhani ukitoka huku utajua sana,” alisema Gosling, hakutaka kuchelewa, alichomwambia ndicho alichokifanya, haraka sana akamtafutia chuo cha miezi sita na kumlipia kila kitu kisha kumuita huko huku akiwa amegharamia kila kitu.

Siku ambayo Catherine aliingia nchini Marekani hakuamini macho yake, wakati mwingine aliona kama alikuwa akiota na muda mfupi angeamka na kujikuta akiwa kitandani.
Huko, akakutana na Gosling ambaye tayari alimuoa Maggie na hivyo kuendelea kula maisha kama kawaida, na kwenye kila mchezo uliokuwa ukichezwa, Catherine alionekana kuwa hatari hata zaidi ya jana.

Wakawa wakifanya mambo mengi kwa siri huku masomo yakiendelea. Aliishi nchini Marekani kwa miezi sita huku akisoma na baada ya hapo akaondoka kurudi zake nchini Tanzania huku tayari akihisi kila dalili za kuwa mjauzito.
“Nahisi nina mimba mpenzi!” alisema Catherine huku akimwangalia Gosling.
“Kweli?”

“Ndiyo! Naona kila dalili za kuwa na mimba,” alisema Catherine.
Japokuwa mara ya kwanza alihisi mwanaume huyo angekataa kwa kuzaa na msichana mweusi lakini cha kushangaza Gosling akawa na furaha kupita kawaida, hakuamini kama alimpa mimba msichana aliyekuwa akimpenda kupita kawaida.

Akamuahidi mambo mengi, angemtunza kwa miaka yote katika dunia hii, alimuahidi kumpenda mtoto wake kuliko kitu chochote kile.

Moyo wa Catherine ulifurahi mno na kuamini sasa angezaa na mwanaume wa ndoto yake. Akarudi mpaka nchini Tanzania kwa ndege ya Gosling, alipofika huko, akafungua kampuni ya kusambaza chakula huku akiwafundisha wafanyakazi wake na kuanza kuingiza pesa kwani chakula hicho alikuwa akikiuza kwenye hoteli kubwa, kilikuwa kilekile kama ambacho Wazungu walikuwa wakila nchini mwao.

Baada ya miezi mitatu, akaamua kwenda kupima Ultra Sound na kugundua alikuwa na watoto mapacha, mmoja wa kike na mmoja wa kiume.

Haraka sana akampigia simu Gosling na kumwambia kile kilichoendelea, mwanaume huyo akachanganyikiwa zaidi, hakutaka kubaki nchini Marekani, akasafiri na kuelekea Tanzania.
 
Sehemu ya 30

Alikaa huko kwa wiki moja huku wakiyafurahia maisha na baada ya hapo, akarudi na kuendelea na kazi zake kama kawaida.

Catherine akaanza kufanikiwa, akaanza kuingiza pesa nyingi kwa kampuni zake mbili alizozianzisha. Kukutana na Gosling siku moja tu kuliyabadilisha maisha yake kwa ujumla.
Siku ziliendelea, miezi ikakatika huku kwenye kila kitu akiwasiliana na Gosling na kumwambia kuhusu hali yake, miezi tisa ilipotimia, akajifungua watoto wawili, wa kiume akaitwa Ryan na wa kike akaitwa Cassie.
*
*

Mawazo ya Maggie yalikuwa kwa Andrea tu, ilikuwa ni lazima akutane na mwanaume huyo na kumuua kama alivyopanga kabla. Kipindi hicho, baada ya kuolewa na Gosling hakutaka kila siku Andrea alikuwa akimpigia simu huku akimsisitiza ni lazima afanye kile alichokuwa amemwambia.

Alimsihi sana asitoe siri ya kile kilichotokea kwa sababu hakutaka kuona akitengana na Gosling, kitu alichokiangalia zaidi kilikuwa ni mali za mwanaume huyo tu na utajiri mkubwa aliokuwanao.

Kidogo Andrea akamuelewa na kumwambia ili siri iendelee kuwa siri alitakiwa kulipwa kiasi cha dola milioni hamisini ili aufumbe mdomo wake na asimwambie mtu yeyote kile kilichotokea.

“Sawa! Ila nitakupaje?” aliuliza Maggie.
“Utaniingizia kwenye akaunti yangu!” alisema Andrea.

“Sawa. Ila kwanza ni lazima nije kwako tuzungumze,” alisema Maggie, kwa Andrea halikuwa tatizo hivyo akamuelekeza mahali alipokuwa akiishi na kwenda kuonana naye.
Ndani ya gari Maggie alikuwa na mawazo tele, Andrea ndiye alikuwa kipingamizi chake, ndiye mwanaume aliyeshikilia maamuzi ya kuendelea na mume wake au la.

Alihuzunika, kwa kile kilichotokea maisha yake ya nyuma kilimuumiza mno lakini kwa muda huo haukuwa wa kujuta, haukuwa wa kuumizwa na kile kilichotokea bali kilikuwa ni kipindi cha kufuarahia maisha yake kwa kile kilichokuwa kikiendelea kutokea.
 
Sehemu ya 31

Andrea alimwambia alikuwa akiishi katika Mtaa wa Mc Kenzie W5 uliokuwa hapohapo Washington DC. Akamuelekeza na msichana huyo kwenda huko kisiri huku akiwa na gari lake, hakutaka kujulikana kwa kuwa kila mtu alimfahamu kutokana na umaarufu wa mume wake.

Alipofika huko, geti likafunguliwa na kuingia. Andrea akatokea na kumpokea kisha kuelekea naye ndani. Akamkaribisha, akakaa na kuanza kuzungumza naye juu ya kile alichohitaji kufanyiwa ili iwe siri.

“Maggie! Kwanza jua kuwa hii taarifa nikiwaambia waandishi wa habari, itakuwa stori kubwa sana duniani kwa mtu kama wewe,” alisema Andrea huku akimwangalia msichana huyo. “Ninajua, ila pesa uliyoniambia nikulipe ni kubwa mno Andy!” alisema msichana huyo.

“Mume wako ana bilioni za dola, unashindwa kuchota dola milioni hamsini na kunilipa?” aliuliza Andrea.

“Mambo si mepesi kama unavyofikiria, naomba unipunguzie,” alisema msichana huyo huku akionekana kuomba hasa.

Andrea alikataa, kiasi alichokihitaji ni dola milioni hamsini tu. Aliendelea kusisitiza kwa msichana huyo kwamba ni lazima amlipe kiasi hicho cha pesa na kama angekataa basi angetoa siri juu ya kile kilichotokea katika uhusiano wao huko nyuma.

Miaka kadhaa iliyopita wawili hao walikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi, walipanga mambo mengi kwamba wangeoana na kuwa mume na mke. Waliheshimiana vya kutosha lakini wakati mapenzi yakiendelea, Maggie alipata ujauzito wa Andrea.

Alizungumza na mwanaume huyo na kumwambia kuhusu ujauzito huo. Wakati Andrea akiambiwa, alikuwa jijini Zenit nchini Urusi.

Haraka sana akarudi nchini Marekani na kuomba kuonana na msichana huyo, alichomwambia kilikuwa kitu kimoja tu kwamba hakuwahi kufikiria kuzaa na Mmarekani, msichana ambaye alipanga kuzaa naye ilikuwa ni lazima awe Mrusi kama alivyokuwa.
“Kwa hiyo?”
“Toa mimba!”

Hilo lilikuwa jambo gumu kwa Maggie, hakupanga katika maisha yake kutoa mimba kama alivyoambiwa, alimwambia Andrea kitu hicho kisingewezekana lakini alichomwambia kama haitowezekana, basi azae lakini asimuhesabu yeye kuwa baba wa mtoto.
 
Sehemu ya 32

Kwa kuwa Maggie alimpenda sana Andrea na hakutaka kumuacha, akakubaliana na kile alichomwambia na hivyo kwenda kutoa mimba hiyo kisiri kwa daktari mmoja ambaye alisoma naye chuo.

Mimba ilionekana kuwa tofauti na mimba nyingine, wakati akitolewa ndipo kizazi chake kiliharibiwa vibaya, damu zilitoka, mimba ikafanikiwa kutoka lakini kizazi kiliharibika na hivyo kuambiwa asingeweza kuzaa tena.
Kwa kipindi hicho hakuona kama kulikuwa na tatizo, kukaa bila mtoto kwake lilionekana kuwa jambo la kawaida sana.

Akakubaliana na daktari na kwenda kumwambia Andrea ambaye baada ya kuambiwa kuwa Maggie asingezaa tena, moyo wake ukawa na furaha na hivyo kuendelea kufanya mapenzi kwani aliamini msichana huyo asingeweza kudaka mimba.

Miaka ikakatika, Andrea akachoka kuishi na Maggie hivyo kumwambia waachane, kwa kuwa naye Maggie alimchoka Andrea, hakuwa na tatizo, akakubaliana naye na hivyo kuachana.

Wakati watu wakijua Maggie na Gosling walikuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi, ndipo Andrea akaibuka, alichohitaji ni pesa, hakujua ni kwa jinsi gani angeweza kuzipata zaidi ya kumwambia msichana huyo angetoa siri hakuwa na uwezo wa kuzaa kitu ambacho Maggie hakupenda kuona dunia ikijua.

Alikuwa tayari kutoa kiasi chochote cha pesa lakini si kuona siri hiyo ikivuja. Alilia sana, alimuomba mno mwanaume huyo asitoe siri lakini alikataa, alimwambia iwe isiwe ni lazima aitoe kama tu asingepewa kiasi alichokuwa akikihitaji.

“Andrea! Unanitesa, naomba jambo hili liendelee kuwa siri mioyoni mwetu,” alisema Maggie, alimuomba sana mwanaume huyo lakini hakuelewa kabisa.

“Maggie! Nimemaliza, bila pesa kesho, nitakwenda kumwambia mume wako,” alisema Andrea na kumfukuza msichana huyo nyumbani kwake.

Maggie akaondoka huku akiwa na maumivu makali moyoni mwake. Alijutia kilichotokea katika maisha yake ya nyuma, alipanga kuzaa na Andrea lakini mwanaume huyohuyo ndiye ambaye alimshauri akatoe mimba na hatimaye kuharibika kwa kizazi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom