Simulizi: Utajiri Wa Damu

Simulizi: Utajiri Wa Damu

Sehemu ya 33

Leo, mwanaume yuleyule aliyemsababishia matatizo alimwambia ni lazima atoe siri. Ndani ya gari alihuzunika sana na kitu kimoja kilichokuja kichwani mwake ilikuwa ni lazima amuue, hata kama angetumia kiasi kikubwa, ilikuwa ni lazima amnyamazishe milele.

“Kama nikimlipa dola milioni hamsini, inamaana siku nyingine akihitaji pesa atakuja kwa gia hiihii, kuyaepuka yote ni lazima nimuue,” alisema Maggie huku akiendesha gari lake.

Hakutaka kurudi nyumbani, alichohitaji ni kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha mwanaume huyo anauawa haraka sana. Akaingia Google na kuanza kutafuta makundi ya watekaji yaliyokuwa yakipatikana katika Jiji la Washington DC.

Akafanikiwa kuona makundi mengi lakini kundi pekee lililokuwa hatari lilikuwa Brothers ambalo liliundwa na wanaume wengi weusi.

Hilo ndilo alilotaka kuonana nalo. Hakujua lilipokuwa likipatikana lakini kwa kupitia mwandishi wa habari wa Gazeti la Talk, akafanikiwa kupewa maelekezo mahali ambapo kundi hilo lilipokuwa.

Mwandishi huyo hakujua kilichotakiwa kufanyika, alichukulia poa na kutoa maelekezo ya kina. Maggie akaelekea katika mtaa alipoelekezwa ambapo kundi hilo lilipopatikana.

Baada ya dakika kadhaa akasimama mbele ya ghorofa kubwa, lilionekana kama limetelekezwa, ndani yake kulikuwa na vijana waliyojitolea kuishi maisha ya ajabu, kuvuta bangi, madawa ya kulevya na wasichana waliokuwa wakijiuza kwa kiasi kidogo cha pesa.

Hakutaka kuteremka, kwa jinsi mahali pale kulipoonekana, ilikuwa ni lazima kufuatwa kwa kuhisiwa alikuwa mtu mbaya. Kile alichokifikiria ndicho kilichotokea, mwanaume mmoja aliyekuwa na bunduki akaanza kumsogelea, aliliona gari hilo likiwa limesimama kwa dakika mbili, halikuwa limeondolewa mahali hapo hali iliyomfanya kuhisi inawezekana alikuwa polisi au adui aliyekuja kushambulia.

“Hey bitch! What the *** are you doing here?” (Hey wewe malaya! Unafanya nini hapa?) aliuliza mwanaume huyo huku akimwangalia Maggie ambaye aliteremsha kioo na kumwangalia mwanaume huyo.
“I want to see Joker,” (Ninataka kumuona Joker)

“Who the *** is he?” (Ndiye nani?) aliuliza mwanaume huyo huku akimwangalia Maggie.
 
Sehemu ya 34

Hakulijibu swali hilo, alibaki kimya huku akimwangalia tu kwa mtazamo ulioonyeshwa hakutaka kudanganywa kwani mwanaume huyo alimjua Joker alikuwa nani.

“Okay! Who are you? Are you a fucking cop?” (Sawa! Wewe nani? Polisi?) aliuliza mwanaume huyo.
“Do I look like a fucking cop?” (Naonekana kama polisi?) aliuliza.

Walibaki wakizungumza kwa dakika moja na mwanaume huyo kuridhia kwenda kumuita mtu aliyeitwa kwa jina la Joker. Baada ya dakika chache, mwanaume aliyekuwa na mwili mkubwa ambaye alisindikizwa na wanaume watano waliokuwa na bunduki wakatoka na kuanza kulisogelea gari lile.

Walipolifikia, Maggie akateremsha kioo tena na kumwambia mwanaume huyo aingie kitu ambacho wala hakikuwa tatizo, akaingia na kuanza kuongea naye.

Alijitambulisha, sura yake haikuwa ngeni kwa Joker, alimwambia kile alichokihitaji kwamba kulikuwa na mwanaume alitakiwa kuuawa kwa sababu alionekana kumgeukia kwa kitu kimoja.

Akamwambia malipo, Joker akasema ni lazima walipwe dola elfu arobaini kitu ambacho kwa Maggie hakikuwa tatizo, akakubaliana naye.
“Picha!”

“Ninayo kwenye simu, ngoja nikurushie,” alisema Maggie na kumrushia Joker picha ile na kumuelekeza mahali alipokuwa akiishi.
“Utatuma pesa kwa namba hii!” alisema Joker huku akimuonyeshea namba ya benki kwa simu yake.

“Ngoja nifanye sasa hivi.”
Hapohapo malipo yakafanyika, hilo likamfanya Joker kugundua mwanamke huyo alikuwa siriazi kwa kile alichotaka kifanyike, hivyo ilikuwa ni lazima wafanye kila liwezekanalo kuhakikisha mwanaume huyo anakufa haraka sana.
 
Sehemu ya 35

“Mtatumia muda gani?” aliuliza Maggie.
“Kesho jioni kaa mbele ya televisheni yako,” alisema Joker.

Maggie akaondoka mahali hapo, aliliamini kundi hilo ni lazima kile alichohitaji kifanyike kingefanyika kwa haraka sana.

Alipofika nyumbani aliendelea kuwasiliana na Andrea na kumwambia alitakiwa kupunguza kiasi cha pesa ili amlipe lakini mwanaume huyo alikataa katakata.

Siku iliyofuata, kama kawaida akakaa mbele ya televisheni yake, alitaka kuona kile alichoambiwa kikitokea. Akiwa hapo, huku akiangalia CNN ndipo akakutana na habari ambayo alikuwa akiisubiri kwa hamu kubwa.
Maiti ya mwanaume mmoja, Andrea ilikutwa ufukweni ikiwa imetupwa huku imechomwa visu mara kadhaa tumboni na shingoni mwake.

Maggie alipoiona habari hiyo, haraka sana akampigia simu Joker na kumshukuru, hakuishia hapo, kwa kuwa kazi yake ilifanyika kikamilifu, akamtumia kiasi cha dola elfu kumi kama shukrani kwa kulifanya jambo hilo kwa umakini na kwa haraka kama alivyotaka.

“Usijali! Siku yoyote ukitaka tukufanyie kazi kama hizi, tuambie, hata kama ni nje ya nchi, tutasafiri,” alisikika Joker huku kwa jinsi sauti yake ilivyokuwa ilikuwa ni rahisi kuigundua furaha aliyokuwanayo moyoni mwake.
“Haina shida!” aliitikia Maggie na kukata simu.
.
.

Je, nini kitaendelea?
 
Sehemu ya 35

“Mtatumia muda gani?” aliuliza Maggie.
“Kesho jioni kaa mbele ya televisheni yako,” alisema Joker.

Maggie akaondoka mahali hapo, aliliamini kundi hilo ni lazima kile alichohitaji kifanyike kingefanyika kwa haraka sana.

Alipofika nyumbani aliendelea kuwasiliana na Andrea na kumwambia alitakiwa kupunguza kiasi cha pesa ili amlipe lakini mwanaume huyo alikataa katakata.

Siku iliyofuata, kama kawaida akakaa mbele ya televisheni yake, alitaka kuona kile alichoambiwa kikitokea. Akiwa hapo, huku akiangalia CNN ndipo akakutana na habari ambayo alikuwa akiisubiri kwa hamu kubwa.
Maiti ya mwanaume mmoja, Andrea ilikutwa ufukweni ikiwa imetupwa huku imechomwa visu mara kadhaa tumboni na shingoni mwake.

Maggie alipoiona habari hiyo, haraka sana akampigia simu Joker na kumshukuru, hakuishia hapo, kwa kuwa kazi yake ilifanyika kikamilifu, akamtumia kiasi cha dola elfu kumi kama shukrani kwa kulifanya jambo hilo kwa umakini na kwa haraka kama alivyotaka.

“Usijali! Siku yoyote ukitaka tukufanyie kazi kama hizi, tuambie, hata kama ni nje ya nchi, tutasafiri,” alisikika Joker huku kwa jinsi sauti yake ilivyokuwa ilikuwa ni rahisi kuigundua furaha aliyokuwanayo moyoni mwake.
“Haina shida!” aliitikia Maggie na kukata simu.
.
.

Je, nini kitaendelea?
Hata kama ni nje ya nchi....duh! Cathy wetu take care Maggie sio mtu mzuri
 
Eeishhh! Nilijua Maggie kafanya mkosa mkuubwaaa..khaa!! Kumbe chanzo Ni Andrea na Bado anamuendesha...hatareee.. nasubiri mwendelezo
Santee kipenzi'.
 
SEHEMU YA 36

Siku ziliendelea kwenda mbele, miezi ilikatika na hatimaye mwaka wa tatu uliingia. Kichwa cha Gosling kilichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea muda huo.

Aliishi miaka mitatu na mke wake, Maggie lakini kitu cha kushangaza, katika kipindi chote hicho hakufanikiwa kupata mtoto.
Hakujua tatizo lilikuwa nini, kwake, hakutaka kumuhukumu mke wake, alihisi vibaya kila alipofikiria inawezekana mke wake alikuwa tatizo la kutokupata mimba.

Hakutaka kubaki na suala hilo moyoni, alichokifanya ni kumwambia yeye mwenyewe na hakujua tatizo lilikuwa nini.

Gosling alijua hakuwa na tatizo kwa sababu kule nchini Tanzania, alikuwa na watoto wawili ambao alizaa na Catherine hivyo kuhisi kabisa alikuwa mzima wa afya.

Alichomwambia mke wake ni kwamba waende kupima kwa Dk. Hernandez wa Hospitali ya St. Antony Medical Center iliyokuwa hapo Washington DC kitu ambacho Maggie hakuona kama ni tatizo.

Kutokana na ubize, walichukua siku mbili mpaka kwenda huko. Walipofika, wakaingia kwenye chumba maalumu na kuanza vipimo huku ikiwa ni usiku kwani hawakutaka mtu yeyote zaidi ya wauguzi wajue kwamba walifika mahali hapo.

Dk. Hernandez alikuwa miongoni mwa madaktari waaminifu mno, aliaminika kwa kila mtu na alikuwa mmoja wa watu waliosifika kwa kuwa alikuwa ameokoka na kumpenda Yesu Kristo.

Vipimo vilipomalizika, akawaambia wasubiri ili kuangalia kile kilichokuwa kikiendelea katika tatizo lile walilokuwanalo.

Muda wote Maggie alikuwa na wasiwasi, alijua kabisa inawezekana mwanaume huyo angesema yeye ndiye alikuwa na tatizo.

Hapo alipokuwa na mumewe, kwa jinsi alivyokuwa akiongea naye ilikuwa ni rahisi kugundua alikuwa na hofu moyoni mwake kitu ambacho Gosling alikigundua haraka sana.

“Hutakiwi kuogopa mke wangu,” alisema Gosling huku akimshika mkono mke wake.
“Najua! Ila sijajua kama ikionekana mimi nina tatizo, utafanya nini? Utaniacha?” aliuliza Maggie.

“Siwezi kukuacha kabisa,” alisema Gosling jibu lililoonekana kabisa alikuwa akidanganya.
 
SEHEMU YA 37

“Ninakupenda mume wangu! Kama nitakuwa na tatizo, naomba usiniache, hata ukiwa na tatizo, nakuahidi kutokukuacha,” alisema Maggie huku akimwangalia mume wake.

Moyo wake ulikuwa na hofu kubwa, wakati mwingine alijilaumu sababu iliyompelekea kumuua Andrea na wakati mwisho wa siku ukweli ulikuwa ukienda kujulikana.

Pale alipokuwa, hakujiamini kabisa, alionekana kuwa na hofu muda wote. Baada ya saa moja, mlango wa daktari ukafunguliwa na kuitwa, wakainuka na kuelekea ndani huku Maggie akitokwa na kijasho chembamba.
“Usiogope mke wangu!” alisema Gosling huku akimpoza mke wake.

Wakaingia ndani ya chumba kile huku wakiwaacha walinzi wao nje. Walipofika, wakakaa kwenye viti na Dk. Hernandez kuwaangalia kwa mtazamo uliomaanisha kulikuwa na mmoja wao aliyekuwa na tatizo.
“Mungu nisaidie,” alisema Maggie huku akimwangalia dokta kwa mtazamo uliojaa hofu kubwa.

Dk. Hernandez akachukua karatasi ya majibu na kisha kuanza kuwasomea baadhi ya maneno na kuwaambia alifanikiwa kuwapima na kugundua mmoja wapo alikuwa na tatizo la kiafya.

“Nani?” aliuliza Gosling.
“Wewe,” alijibu Dk. Hernandez.
Gosling akabaki kimya, hakuamini kile alichokisikia kutoka kwa daktari huyo, kitendo cha kuambiwa hakuwa na uwezo wa kumpa mimba mwanamke kulimfanya kuanza kumfikiria Catherine ambaye alimpa mimba na kuzaa watoto wawili.

Alitamani kumwambia daktari mbona kulikuwa na msichana aliyempa mimba lakini akasita kwa kuwa mke wake alikuwa mahali hapo. Alichanganyikiwa, hakujua ni kitu gani kilitokea mpaka asiwe na uwezo wa kumpa mimba mwanamke.

Akamuuliza sababu, daktari huyo akaanza kumpa sababu nyingi za kiafya kwamba mfumo wake wa uzazi haukuwa ukitengeneza homoni zenye nguvu ambazo zingemfanya mwanamke kupata mimba.

Wakati daktari akiyasema hayo, Maggie alikuwa pembeni huku akijifanya kuhuzunika kwa kile alichoambiwa, hakuishia kuhuzunika tu bali wakati mwingine machozi yakaanza kumtoka, alijifanya kuumizwa na kile alichokisema daktari.
 
SEHEMU YA 38

Gosling hakuwa sawa, ni kama alichanganyikiwa, alijijua alikuwa mzima, kwa nini daktari amwambie kuwa hakuwa na uwezo wa kumpa mimba mwanamke na wakati tayari alikuwa na watoto wawili nje ya ndoa yake.
“Impossible,” (Haiwezekani) alisema Gosling huku akimwangalia daktari.

Hakuridhika, akamwambia daktari arudie vipimo, hilo halikuwa tatizo, akarudia vipimo na majibu kuwa yaleyale kwamba hakuwa na uwezo wa kumpa mimba mwanamke.

Moyo wake ulimuuma mno, hakuamini kama leo hii hakuwa akizalisha homoni zilizokuwa na nguvu. Akamuuliza daktari tatizo hilo lilisababishwa na nini, kitu alichomwambia ni kwamba vyakula alivyokuwa akila ndivyo vilivyosababisha hayo yote.

Alibaki akilia, moyo wake ulimuuma mno, maneno ya daktari kwamba hakuwa na uwezo wa kupata mtoto ukamfanya kuhuzunika na kuumia mno. Hakutaka kuishia hapo, akaondoka kurudi nyumbani na kumwambia mkewe walitakiwa kubadilisha hospitali na hivyo kwenda kwenye hospitali nyingine kabisa.

Huko napo, kama alivyoambiwa kule alipopita ndivyo alivyoambiwa hata huko kwamba kwa homoni alizokuwa akizalisha hazikuwa na nguvu, zilifika kwenye mfuko wa uzazi wa mwanamke lakini haukuweza kuzalisha, na ili apate kuelewa zaidi akaonyeshewa mpaka picha iliyopigwa kuonyesha kwamba homoni zake hazikuwa na nguvu.

Alihangaika kwenye hospitali zaidi ya tatu na majibu yalikuwa yaleyale, hakujua ni kipindi gani tatizo hilo lilianza kwani aliwahi kumpa mimba mwanamke kwa siri na wakati huo alikuwa akilea watoto wake hao.

Siku zikakatika, hakujua kama mke wake, Maggie ndiye aliyekuwa akicheza mchezo mzima. Alijua hakuwa na uwezo wa kupata mtoto, hakutaka kuona akimuacha mwanaume huyo kwa kuwa alikuwa na pesa hivyo alichokifanya ni kwenda kwa kila daktari ambaye alitakiwa kuwapima na kumpa pesa ili atakapopima basi aseme mwanaume ndiye aliyekuwa na tatizo.

“Dola elfu kumi ni pesa ya kitoto, na unajua kabisa hiki tunachokwenda kufanya ni hatari,” alisema Dk. Hernandez.

“Wewe unataka kiasi gani?”
“Dola laki tano!”
“Laki tano?” aliuliza Maggie huku akionekana kushtuka.
 
SEHEMU YA 39

“Ndiyo! Hii ni hatari, kama kuna siku Gosling atakuja kugundua, nitakosa kazi, nitadharaulika, sasa ni bora nidharaulike kwa pesa nyingi,” alisema daktari huyo.
Naye Maggie aliiona hiyo hatari, hakuwa na jinsi, kwa sababu mume wake alikuwa na pesa, akamlipa mwanaume huyo kiasi alichokitaka na kuendelea na maisha.

Hivyo ndivyo alivyofanya, kwa kila hospitali aliyokuwa akiisema Gosling walitakiwa kwenda, Maggie alikuwa fasta na alikwenda kuonana na daktari husika na kumlipa kiasi kikubwa cha pesa.

Kwa zaidi ya hospitali tatu ambazo zilimwambia hakuwa na uwezo wa kumpa mimba mwanamke, akakubaliana nazo, naye kichwa chake kikamwambia kweli hakuwa na uwezo huo.

Alikuwa na huzuni, alilia mno, alijifungia chumbani kwake, aliumia lakini hakuweza kubadilisha kile kilichokuwa kikiendelea muda huo.

Hata kubaki nchini Marekani aliona ni tatizo, kila alipomwangalia mke wake aliumia moyoni mwake na kumwambia waachane, wagawiane mali ili akaolewe na mwanaume mwingine na yeye kuishi peke yake lakini Maggie alikataa.

“Haiwezekani! Kama nilisema nitakuwa na wewe mpaka mwisho wa maisha yangu, ni lazima nifanye kile nilichoahidi mbele ya mchungaji,” alisema Maggie maneno yaliyomfanya Gosling kuamini mke wake huyo alikuwa akimpenda.

Ni kweli alitamani kuachana na mwanaume huyo, alitamani kupewa talaka na kugawana mali lakini kwake, kitu alichokihitaji ni mali zote. Ilikuwa ni lazima amuue Gosling, mali zote abaki nazo lakini si kuona akigawana naye.

Wakati moyo wake ukiwa na maumivu makali, miaka minne iliyofuata akasafiri na kuelekea nchini Tanzania kumuona mchepuko wake, Catherine aliyekuwa na watoto wake ambao muda huo walikuwa na miaka saba.
Kwenda huko ilikuwa siri kubwa, alimwambia mke wake kulikuwa na biashara fulani alikuwa akiifuatilia hivyo ilikuwa ni lazima kwenda huko.

Kwa Maggie hakuwa na wasiwasi wowote ule, hakujua kama mwanaume huyo alikuwa akienda kuwaona watoto wake, Ryan na Cassie waliokuwa wamezaliwa na Catherine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom