Simulizi: Utajiri Wa Damu

Simulizi: Utajiri Wa Damu

SEHEMU YA 40

Alipofika, alifurahi kuwaona, walifanana naye kupita kawaida, moyo wake ukawa na furaha mno, kila alipokuwa na Catherine moyo wake uliridhika, alijiona kupata kila kitu tofauti na kuwa na Maggie ambaye hakuwa na mapenzi makubwa kama aliyokuwanayo kwa Catherine.

Alikaa huko na kupanga mambo mengi, aliendelea kumpa pesa za kufungulia biashara kubwa, alimfanya kuwa mtu mwenye thamani ambaye hakutakiwa kuhofia kuhusu maisha yake hata kidogo kwa kuwa pembeni alikuwepo yeye.

Hakutaka kumficha Catherine juu ya kile kilichotokea nchini Marekani, alimwambia hakuwa na uwezo wa kuzalisha tena kwa kuwa mbegu zake hazikuwa na nguvu hata kidogo.
“Kwa hiyo?” aliuliza Catherine.

“Sitokuwa na mtoto mwingine zaidi ya hawa hapa,” alisema Gosling.
“Pole sana mpenzi!”
“Nashukuru! Ila ninafikiria jambo moja,” alisema.

“Lipi hilo?”
“Kuwagawia watoto wangu utajiri wangu wote. Yule Maggie ninaishi naye ilimradi tu, ni mke wangu lakini hakuna anachonipa katika maisha yangu, ni kama rafiki yangu, hizi mali zote ni lazima niwape watoto wangu,” alisema Gosling.

Alikaa na mpenzi wake huyo, japokuwa alizaa lakini Catherine hakuchoka, kila siku alionekana kama mwanamke mpya kabisa. Ujuzi wake kitandani ulikuwa ni zaidi ya ule aliokuwanao kipindi cha nyuma.

Walifanya sana mapenzi na baada ya wiki moja akarudi nchini Marekani. Maisha yaliendelea, biashara alizokuwanazo ziliendelea kuingiza pesa nyingi, alikuwa bilionea ambaye kila siku alikuwa akiongeza kiasi kikubwa cha pesa kiasi kwamba alionekana kuwa bilionea mkubwa sana hapo baadaye.

Baada ya wiki mbili, Catherine akawasiliana na Gosling na kumpa habari zilizomshtua mno, habari ambayo ilimfanya kuhisi kama kulikuwa na kitu kilichotokea nyuma ya pazia.
“Ulisema huna uwezo wa kumpa mimba mwanamke?” aliuliza Catherine kwenye simu.
“Ndiyo!”
“Hapana! Si kweli!”
“Kwa nini?”

“Nina mimba yako! Umenipa mimba, katika kipindi ulichokuja nilikuwa kwenye siku zangu za hatari Gosling, tumefanya mapenzi na umenipa mimba,” alisema Catherine kwenye simu huku akionekana kuwa na furaha tele.
 
SEHEMU YA 41

“Catherine! Hebu subiri kwanza....unasemaje?” aliuliza Gosling huku akionekana kutokuamini.
“Umenipa mimba!”
“Nimekupa mimba mimi?”
“Ndiyo!”

“Hapana! Unanidanganya!” alisema Gosling.
Alichanganyikiwa, hakutaka kubaki nchini Marekani, akamwambia mke wake alitakiwa kusafiri kuelekea nchini Morocco kwani kulikuwa na biashara ya mafuta aliyotaka kuanza kuifuata.

Maggie akamwamini na hivyo mwanaume huyo kuondoka kuelekea nchini Tanzania. Moyo wake ulikuwa na furaha sana, kile alichoambiwa kilikuwa kama ndoto, hakuamini kwa sababu nchini Marekani aliambiwa hakuwa na uwezo wa kumpa mimba mwanamke.

Ndani ya ndege aliona kama akichelewa, alitamani afike haraka na kuonana na mwanamke huyo na kumwambia kwa mara nyingine kile alichomwambia kwenye simu.

Baada ya kufika Arusha, akapokewa na mpenzi wake huyo na kwenda nyumbani. Walipofika, akamuonyeshea picha aliyopita kwa Ultra Sound ambayo ilionyesha alikuwa na mtoto tumboni.

Gosling akachoka, akakaa chini na kuanza kulia, hakujua ni kitu gani kilitokea, hakuwa na homini zilizokuwa na uwezo, sasa ilikuwaje mpaka ampe mimba Catherine.

“Au ulidanganywa?” aliuliza Catherine.
“Hapana! Hospitali tatu zote wanidanganye?” aliuliza Gosling.
“Hebu jaribu kupima na hapa!”
“Afrika?”

“Ndiyo! Tuna hospitali bora. Pima uone watakwambiaje!” alisema Catherine.
Hakutaka kupima nchini Tanzania, katika maisha yake hakuwahi kuamini huduma za barani Afrika lakini baada ya kulazimishwa sana na mpenzi wake huyo, hakuwa na jinsi, akamchukua yeye na walinzi wake na kwenda katika Hospitali ya Melovian ambayo ilikuwa ni ya watu wenye pesa na kwenda kupima huko.

Walisubiri katika chumba maalumu wao wawili tu, Gosling alikuwa kimya, kichwa chake kilikuwa na mawazo tele, aliyafikiria majibu ambayo alitakiwa kupewa ndani ya chumba hicho.

Muda wote Catherine alikuwa akimtia moyo na kumwambia hakutakiwa kuhofu kitu chochote kile kwani kama kweli mbegu zake zilikuwa na nguvu angeambiwa hapo.

Baada ya saa moja, daktari akawaita na kwenda chumbani. Walikwenda wawili tu ambapo kabla ya kuwapa majibu hayo, akatoa tabasamu pana lililokuwa na matumaini makubwa.
“Vipi?” aliuliza Catherine.
 
SEHEMU YA 42

“Hakuna kitu! Majibu yanaonyesha wote mna nguvu, mayai ya mwanamke yapo imara, na tena tayari una mimba na homoni za mwanaume nazo zina nguvu,” alisema daktari.

“Zina nguvu?”
“Ndiyo! Na zinaweza kuzalisha hata watoto elfu moja, wewe tu,” alisema daktari maneno yaliyomfanya Gosling kutokuamini masikio yake.

Gosling hakuamini alichokisikia, moyo wake ulimuuma alipogundua mke wake alichezea mchezo na madaktari ili ionekane kweli alikuwa na tatizo ndani ya mwili wake.

Akapandwa na hasira kali, alikunja mikono yake kwa staili ya ngumi hali iliyoonyesha kama Maggie angekuwepo mbele yake basi kile ambacho kingefuatia kingekuwa ni kumshambulia kwa ngumi mfululizo.

Catherine akamtuliza kwani aliona kabisa jinsi Gosling alivyokuwa na hasira kali. Akampoza kwa maneno mengi kwamba hakutakiwa kufanya jambo lolote lile kwa kuwa tayari alikuwa na watoto ambao wangempa furaha maisha yake yote.

Hiyo kidogo ilisaidia, akapoa na hivyo kuendelea na maisha kama kawaida. Alimpenda mno Catherine kuliko alivyompenda mke wake wa ndoa.

Hata alipokuwa nchini Marekani hakutaka kumuonyeshea tofauti yoyote ile, alimpenda kama kawaida lakini moyo wake ulikuwa umejaza hasira kali.

Maggie hakujua kilichokuwa kikiendelea, kila alipomwangalia mume wake aliona kawaida tu, alikuwa akimpenda kama siku ya kwanza alivyompenda kumbe moyoni mwa mwanaume huyo kulikuwa na hasira kali dhidi yake.

Wakati mwingine Gosling alijiambia amuue mwanamke huyo, wazo hilo lilimjia kichwani mwake lakini baada ya kufikiria jinsi alivyomzoea, hakuona sababu ya kufanya hivyo.

“Nimuue kisa hajanipa mtoto?” alijiuliza.
“Lakini si nina watoto tayari! Sasa kwa nini nimuue! Yaani nimuue kisa hazai?” alijiuliza kila alipokuwa akimwangalia Maggie kwa tabasamu pana.

Wazo hilo halikupata nafasi kichwani mwake, kama mwanaume alitakiwa kupuuzia kilichokuwa kikiendelea, kama mwanamke huyo hakumpa mtoto basi hata urithi wa mali zake ulitakiwa kwenda kwa watoto wake na hivyo ndivyo alivyofanya.

Siku zilizidi kwenda mbele, miezi ikakatika na hatimaye Catherine kujifungua mtoto wa tatu na kumpa jina la Emilia.
 
SEHEMU YA 43

Furaha ya Gosling ikaongezeka, haraka sana akampigia simu mwanasheria wake na kumwambia alitakiwa kumuongeza mtu mwingine kwenye karatasi ya mirathi kwani hakutaka kabisa kuona Catherine akichukua kitu chochote kile wakati atakapofariki dunia.


Hilo likafanyika, mwanasheria huyo, Jackson Phill alishangaa lakini hakuuliza kwani kwa jinsi alivyomwangalia Gosling aligundua hakuwa sawa, hakuwa kama zamani alivyokuwa.

Nchini Tanzania maisha yalikuwa mazuri, Ryan na Cassie walikuwa wakisoma shule nzuri ya St. Theofil iliyokuwa jijini Dar es Salaam ambayo ilikuwa ikifundisha wanafunzi waliokuwa wakitoka katika familia za viongozi wa serikali hasa mawaziri na watoto wa matajiri.

Walisoma vizuri, kila siku walikuwa wakiwasiliana na mama yao ambaye alikuwa Jijini Arusha alipokuwa akiishi huko.
Miaka ikasogea huku upendo wa Catherine kwa watoto wake ukiwa mkubwa.

Baada ya miaka nane, Gosling akazungumza na Catherine na kumwambia alichoka, kitu pekee alichokihitaji ni kuwa karibu na watoto wake ambao walikuwa na miaka kumi na tano huku Emilia akiwa na miaka nane.
“Unataka ufanye nini?”
“Nimpe talaka, hata akitaka tugawane mali, haina shida,” alisema Gosling.

“Unadhani itawezekana?”
“Niachie mimi!”
Gosling akawasiliana na Jackson na kumwambia kila kitu kwamba ilikuwa ni lazima amwandikie talaka Maggie na amuoe Catherine ili awe karibu na familia yake.

Hakutaka kuona ni kwa jinsi gani mwanamke huyo angenufaika na madai makubwa ya mali, hapo alipofikia lilikuwa ni suala la kuwa na furaha, hakutaka kuangalia pesa, alichokiangalia kilikuwa ni kuwa na familia yake tu.
“Basi haina shida.”
 
SEHEMU YA 44

“Ila Jackson. Siku kama kuna lolote litatokea, mwambie Catherine nina akili na ndiyo maana ninafanya hivi,” alisema Gosling.
“Akili? Kivipi?”

“Wewe mwambie hivyo tu!” alisema Gosling.
Ishu ya talaka ilikuwa ni ya siri kubwa, aliwashirikisha marafiki zake wa karibu na wote kumwambia alitakiwa kufanya kile alichokifanya lakini kitu cha ajabu kabisa, Maggie akaambiwa na mmoja wa marafiki hao mpango mkubwa aliokuwanao mume wake.

Alichanganyikiwa, alikasirika kwa kuona kama asingefanya jitihada za kummaliza mwanaume huyo mapema basi asingepata mali zote hizo, hivyo alichokifanya ni kuanza kupanga mipango ya kummaliza.

Kundi ambalo lilitakiwa kufanya kazi hiyo ni lile la Brothers! Walichotakiwa kufanya ni kutengeneza ajali ya gari, baada ya hapo walilipue gari hilo na kuondoka zao.

Jinsi ya kumpata mume wake halikuwa tatizo, alijua ni kwa jinsi gani jambo hilo lingefanyika kwani alihisi kulikuwa na ufundi mkubwa ambao haujawahi kufanyika duniani kote.

Alichokuwa akikihesabu ni siku tu, vijana hao wakajipanga tayari kwa kutekeleza mpango wao wa kumuua Gosling. Baada ya siku tatu wakampigia simu Maggie na kumwambia mipango yote ilikuwa tayari hivyo walichotakiwa ni kumuua haraka iwezekanavyo.

“Nashukuru sana! Ngoja nifanye mipango yangu pia,” alisema mwanamke huyo na kukata simu huku uso wake ukiwa na tabasamu pana, aliamini piga ua ilikuwa ni lazima kummaliza mwanaume huyo kisha kumiliki mali zote za mumewe na utajiri aliokuwanao.
.
.

Je, nini kitaendelea?
 
Endelea
SEHEMU YA 44

“Ila Jackson. Siku kama kuna lolote litatokea, mwambie Catherine nina akili na ndiyo maana ninafanya hivi,” alisema Gosling.
“Akili? Kivipi?”

“Wewe mwambie hivyo tu!” alisema Gosling.
Ishu ya talaka ilikuwa ni ya siri kubwa, aliwashirikisha marafiki zake wa karibu na wote kumwambia alitakiwa kufanya kile alichokifanya lakini kitu cha ajabu kabisa, Maggie akaambiwa na mmoja wa marafiki hao mpango mkubwa aliokuwanao mume wake.

Alichanganyikiwa, alikasirika kwa kuona kama asingefanya jitihada za kummaliza mwanaume huyo mapema basi asingepata mali zote hizo, hivyo alichokifanya ni kuanza kupanga mipango ya kummaliza.

Kundi ambalo lilitakiwa kufanya kazi hiyo ni lile la Brothers! Walichotakiwa kufanya ni kutengeneza ajali ya gari, baada ya hapo walilipue gari hilo na kuondoka zao.

Jinsi ya kumpata mume wake halikuwa tatizo, alijua ni kwa jinsi gani jambo hilo lingefanyika kwani alihisi kulikuwa na ufundi mkubwa ambao haujawahi kufanyika duniani kote.

Alichokuwa akikihesabu ni siku tu, vijana hao wakajipanga tayari kwa kutekeleza mpango wao wa kumuua Gosling. Baada ya siku tatu wakampigia simu Maggie na kumwambia mipango yote ilikuwa tayari hivyo walichotakiwa ni kumuua haraka iwezekanavyo.

“Nashukuru sana! Ngoja nifanye mipango yangu pia,” alisema mwanamke huyo na kukata simu huku uso wake ukiwa na tabasamu pana, aliamini piga ua ilikuwa ni lazima kummaliza mwanaume huyo kisha kumiliki mali zote za mumewe na utajiri aliokuwanao.
.
.

Je, nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom