TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA SABINI NA TISA
MTUNZI
Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA SABINI NA NANE: hapo akiwa na bangi yake mkononi akajivuta dirishani na kuchungulia na kuona kundi la wakina mama likitoka nje na dakika chache baadae akawaona wanaingia ndani wakiwa wameongozana na watu watatu, ambao ni wageni, Talib alipowatazama wale wageni alijikuta anapatwa na mshtuko wa ajabu, “yule mzee si ananifahamu yule” alijisema Talib, ambae alishtuka sana baada ya kumuona mzee Frank, ambae kwa maelezo ya Soraya ni kwamba alishaenda polisi, na endapo angemuona kijana alie toa vitisho dukani kwake angeenda kumtolea taarifa polisi ili akamatwe……… ENDELEA……..
Hapo Talib akaona kuwa huu ni msala kwake, hivyo akizubaa atakamatwa kabla hajatekeleza mpango wake, “inabidi nitoke nikazuge kitaa mpaka waondoke ndio nirudi” aliwaza Talib huku anavaa viatu vyake haraka kwaajili ya kuondoka pale nyumbani, hakuwaza kuhusu fedha ya kula wala njaa aliyokuwa nayo muda ule, “Soraya nae yaani ujanja wote ule anakuja kubebwa na mafala kama hawa” aliongea Talib kwa kulalamika na kulaumu, huku akiendelea kuvaa viatu vyake na kuvuta bangi yake.
Wakati huo Mahamud alikuwa sebuleni na watu wawili watatu, mmoja wao akiwa ni mjomba wa Soraya, ambae alishafahamishwa juu ya ugeni ule ,wakiwasubiri wageni ambao waliambiwa kuwa tayari wameshafika pale nyumbani, sasa mahamud akasogeza mdomo wake karibu na sikio la Jamal na kumnong’oneza jambo, “Jamal naamini utakuwa una wafahamu watu hao, naomba uwe makini kuwa soma nakusikiliza majibu yao,mana nitawauliza maswali fulani fulani nawe pia una ruhusiwa kuuli maswali” alisema Mahamud, na wakati huo huo wakasikia sauti tulivu iliyojaa nidhamu ya asili ya mngoni halisi toka upande wa mlangoni, “hodi jamani” huku watu wote wanageuza macho kutazama mlangoni.
Naam Jamal ambae alitazama kwa makini sana, ili kuona kama anaweza kuwa tambua wageni wale walioingia pale sebuleni, aliweza kuwaona watu wawili ambao ni wazi kuwa ni mtu na kijana wake, kwa jinsi walivyo tofautiana kwa umri, na pia ukizingatia tayari alishajuwa kuwa wanao kuja ni baba mama na kijana wao, ukweli kabisa Jamal alitegemea kumuona kijana ambae atakuwa anamfahamu, maana kuwa na Soraya sijambo dogo, lakini ilikuwa tofauti kabisa, alikuwa ni mgeni kabisa machoni mwake.
Hapo Jamal akamtazama mzee Mahamud, ambae pia aliamini kuwa atakuwa anamuona kijana huyu kwa mara ya kwanza, lakini akashangaa kumuona Mahamud akitoa macho kwa mshangao, huku ameachama kwa furaha, “hooooo! kijana umekuja siku nzuri sana, tena wakati muafaka, karibu sana” alisema Mahamud kwa sauti iliyojaa furaha, huku anasimama na wakina jamali wakasimama pia kuwa karibisha wakina Higgno, “asante sana mzee Shikamoo” alisalimia Higgno, huku anapokea mkono wa mzee Mahamud, wakionyesha kufahamiana kwa karibu, “marahaba, karibuni sana” alisema Mahamud huku anamshika mkono mzee Frank, “asante sana” aliitikia mzee Frank, ambae alifurahi kuona kijana wake anafahamiana vizuri na mzee huyu tajiri mkubwa hapa songea na Tanzania nzima pia.
Naam walitumia dakika kadhaa kusalimiana, kisha wakaonyeshwa sehemu za kukaa, nao wakakaa, “karibu kijana, umekuja siku ambayo kiukweli ni nzuri, maana yule binti yangu nilie kueleza jana, anakuja kutuonyesha mchumba wake, kwa hiyo ameshapata mchumba” alisema Mahamud, mwenye kuonekana kuwa na furaha kubwa sana, huku anamtazama Higgno ambae alionyesha kumfahamu na kwamba hakutegemea kumuona mahali hapa, ukweli waliokuwepo mule ndani walishangaa kidogo, maana walidhania kuwa Higgno ndie mchumba mwenyewe wa Soraya aliekuwa anasubiriwa “imekuwa vizuri sana, na pengine tunge kuwa tumeingilia na kuvuruga mipango mingine” alisema Higgno, kwa sauti ya upole, huku anacheka kidogo, hapo Mahamud na mzee Frank wakacheka kidogo, maana walijuwa Higgno alikuwa anamaanisha nini, “ni kweli bwana, tena sijui kama tungeeleweka” alisema mzee Frank, huku anaendelea kucheka.
Naam wakiwa wanaongea kwa furaha, huku wanaendelea kuwasubiri wageni wao pasipo kujuwa kuwa wageni wenyewe ndio hawa waliokuwa nao hapa sebuleni, ambao pia hawakuwa wana jijuwa kuwa wao ndio wageni waliokuwa wanasubiriwa, mara wakaanza kusikia kelele na shwangwe za wakina mama zikihamia ndani, zikifuatiwa na kundi dogo la wanawake kuingia ndani na kukaa kwenye makochi, na kwenye jamvi (carpet) yani zuria la manyoya lililo lala juu ya sakafu ya sebule ya jumba hili la kifahari, ambalo ukiingia lazima utavua viatu kabla ya kuuliza au kuambiwa.
Mke wa Mahamud alienda moja kwa moja, mpaka mume wake na kumnong’oneza jambo, “tunaweza kuanza ili tumalize mapema, watu wale waende makwao” alisema mama Soraya, kisha akaenda kumueleza vivyo hivyo kaka yake ambae ndie msemaji kama ilivyo kawaida, baada ya hapo akaenda kukaa karibu na mama Higgno, ambae kiukweli yeye ndie alikuwa anashangaa kuliko maelezo, maana alikuwa anaona mapicha picha tu!, kwasababu kwa jinsi alivyo pokelewa kule nje na wakina mama na kupewa hongera nyingi nyingi, na kuona dalilizote za kuwa ile sherehe ni kwaajili yao, hivyo akashangazwa sana na jambo lile maana alicho juwa yeye ni kwamba wanafika pale wanapata chakula cha mchana kisha wanaondoka kurudi zao nyumbani, lakini kila alipomtazama mume wake yaani mzee Frank, hakuona dalili yoyote ya kushangaa wala kushikwa na butwaa kama ilivyokuwa kwa Higgno.*******
Naam ndani ya kichaka chini ya mwembe, mita kama ishirini toka barabarani mama Hilda na bwana Njogopa rafiki mkubwa wa mume wake, tayari walisha kunywa makopo kadhaa ya ulanzi, ambao ndio kwanza ulikuwa unatoka mianzini haujatiwa hata maji, tayari pombe ilishapanda kichwani kuharibu akili zao kwa kiasi cha kati, na kubakiwa na akili ya kuanza kupapasana sehemu nyeti huku wakipeana mate.
Naam ni kama walikuwa bichi moja nzuri sana yenye upepo mwanana, maana ilifikia wakati hata wakaacha wazi sehemu zao nyeti ili kila mmoja aweze kuchezea ya mwenzie, wakati mama Hilda akichezea dudu ya Njogopa huku yeye akichezewa kikunde chake na kujisikia raha kweli kweli haikuchukuwa muda akatandika kanga yake chini, “tufanye mara moja halafu tuendelee na pombe”, alishauri mama Hilda huku anapandisha gauni lake mpaka kiunino ukweli hakuvaa chupi, kisha akapiga magoti kubinua kiuno chake kwa juu na kuacha vyombo hewani, hapo Njogopa akakenua meno kwa tabasamu la uchu, na kusogelea nyuma ya mama Hilda, kisha akazamisha dudu ndani na kazi ikaanza, wakapeana dudu kwa raha zote kama wapo chumbani, hawakujuwa kuwa mita chache toka pale walipo kuna mwanamke mmoja aliekuwa anatoka madimbeni (mshamba ya kondeni/mtoni) alikuwa anawatazama, huyu alikuwa ni mschana tu, mschana huyu alikuwa anaitwa alikai kwa jina la utani, jina ambalo alipewa kwasababu ya kwamba hakuwa na utaratibu wa kukaa na jambo moyoni mwake, kwa kifupi alikuwa ni cha umbeya, ambae hakukaa sana akatoka mbio kueleka kijijini akiwa na lengo la kwenda nyumbani kwa Njogopa kumueleza mke wa Njogopa kile kilicho kuwa kinaendelea kule maporini.*******
Mlinzi aliishiwa pose baada ya kuambiwa na boss wake kuwa atapata adhabu yake kwa kile kilicho kifanya, yaani kuwazuia wale wageni, “dah! sijui kwanini nilijifanya mkali wakati watu wenyewe walikuwa wanaongea kwa upole” aliwaza Mlinzi ambae kama ulikuwa humjui kwa jina basi alikuwa anaitwa Ndolite au babu Ndolite, japo wenyewe walipenda kumuita babu, “dah! kumbe nilimzuia mchumba wa Soraya” hakika babu alikuwa ameshushuka kweli kweli, “lakini mbona watu wenyewe ni masikin…” kabla babu haja maliza kujiuliza, mata akamuona Talib anakuja pale getini akitokea kwenye nyumba anayo kaa, akitembea kwa mwendo wa tahadhari kubwa, “babu mtu yoyote akiniulizia mwambie sijarudi kabisa, alisema Talib kisha bila kuchelewa akatoka nje pasipo kujali njaa wala ukapa wa fedha alionao, hakujali wala kuwaza atakula wapi na wala ataenda kukaa wapi mpaka muda ambao shughuri hii itakapo kwisha.********
Mzee komba aliekuwa amelala juu ya kitanda cha Hospital njaa inamuuma kweli kweli, maana toka alipokunywa uji asubuhi kule Hospital ya mjini hakuwa amekula tena hata muda wa kunywa dawa ulishapita, tayari maumivu ya kichwa yalishaanza kumchamanda, “yaani mke wangu na binti yangu wanaweza kunifanyia hivi?” aliwaza kwa machungu mzee Komba, ambae sasa alijutia tabia yake ya kuamua kumchukia Frank, ambae hakuwahi kumtendea ubaya hata siku moja, zaidi ni kwamba Frank na familia yake walikuwa wanamtendea yaliyo mema mara zote, na yeye kuamua kulipiza ubaya, ambao matokeo yake ni hayo ya mganga kutembea na mke wake na binti yake, huku yeye akiambulia mshtuko na kuanguka huku akiishia kupooza mguu.
Wakati Komba akiendelea kijiwazia na kujinung’unisha mara akatokea yule nurse akiwa amebeba sahani ya chakula mkononi, “mzee nashindwa kuielewa familia yako kwanini wanakufanyia hivi” alisema nurse huku anavuta meza akiisogeza karibu na kitanda alicholalia Komba, na kisha akaweka chakula juu yake, “yaani toka asubuhi tuna waeleza kuwa utakuwepo hapa zahanati, nimeenda tena kuwaeleza umeshafika na unahitaji chakula, lakini wapi, hawana hata dalili ya kuleta chakula” alisema nurse kwa sauti ya masikitiko makubwa, “mama kwa kweli nimepatikana, sikutegemea kama watanifanyia hivi” alisema mzee Komba, kwa sauti iliyojaa huzuni na masikitiko, “lakini kwa kuwa tupo hapa kijijini, nadhani hakuna yatakayo haribika” alisema nurse huku anatoka na kwenda kuchukuwa chupa ya uji na kikombe, ambapo hakutumia muda mrefu alirudi akiwa amebaba chupa ya uji na kikombe.
Naam ukiachilia taaluma ya unurse pia ongezea na uwana kijiji walionao, nurse alihakikisha anamsaidia mzee Komba ambae ni mwana kijiji mwenzie, ambae alimuinua kitandani na kumnawisha, halafu mzee Komba akaanza kula taratibu, “ndizi na utumbo” tena aliletewa na uji wa ulezi, siku hizi wanaita uji wa lishe, tena chakula ambacho bila kuumwa pengine asinge pata nafasi ya kukila siku za hivi karibuni.
Naam wakati anaendelea kula mara akaingia mama mmoja mtu mzima, japo hakumfikia mzee Komba kwa umri, lakini aliekuwa amevalia mavazi masafi ya kike gauni la kawaida tu, huku juu yake akiwa amevalia vitenge juu yake, “jamani kaka nini kime kupata, yaani toka juzi unaumwa unashindwa kuwa tuma wakina Hilda kuja kutujulisha” alisema yule mwanamke kwa sauti iliyojaa lawama” ukweli Komba hakuwa na jibu juu ya hilo swali, zaidi alianza kutoa machozi, machoni mwake na kumshangaza huyu mwanamke aliemuita kaka, “samahani wewe ni ndugu yake?” aliuliza Nurse akimtazama yule mwanamke, “ndiyo mimi ni ndugu yake watatu kuzaliwa toka kwake, yaani baba mmoja mama mmoja” alijibu yule mwanamke, ambae kumbe ndie yule dada yake wa makemba, ambae alipelekewa ujumbe na Ngonyani kuwa aje haraka Luhila kaka yake anaumwa.
Naam yule Nurse akamsimulia yule mama, kuanzia usiku wa juzi pale mzee Komba alipo pelekwa pale zahanati akiwa amepoteza fahamu, na kukimbiwa na wenzake lilipokuja swala la kumpeleka mjini, na jinsi mke wa bwana Komba na binti yake walivyo mtelekeza, “wacha niende nikamtafute wifi nijuwe ni kwanini anafanya hivi” alisema dada yake Komba pasipo kujuwa kuwa wifi yake alikuwa katika lindi la burundani ya pombe na mapenzi.*******
Turudi mjini, nyumbani kwa Mahamud, ambako watu wote walikuwa ndani wakisubiri tukio la kutambulishwa kwa mchumba wa Soraya, mama Soraya alikuwa makini sana kumtazama Higgno, ambae alitegemea kumuona akijishauwa shauwa, kwa kufanikiwa lengo lake la kumshawishi na kumlaghai Soraya na kufanikiwa kuwa nae, lakini cha kushangaza hakumuona kuwa na hali yoyote ya kufurahia au kutataikia jambo lile, yaani alikuwa ametulia kama mtazamaji mwingine tu, mara mjomba akasimama, “asalaam alaykum mabibi na mabwana, wacha nimkaribishe bwana Mahamud atueleze sababu ya kutuita hapa siku hii ya leo” alisema mjomba, huku watu wote wakiwa kimya kabisa, hasa mama Higgno ambae alikuwa ametulia anasubiri kusikia kinachoendelea na ondoa maswali ya kichwani mwake na wakati huo akaonekana Soraya.
Alisimama mzee Mahamud ambae kama ilivyo kwa mjomba wa Soraya na wakina Jamal na wakina Higgno na baba yake, kuwa kuna wageni walikuwa wanasubiriwa na pengine wapo nje wanasubiri waingie kwa mpangilio maalumu ambao pengine mama Soraya ameupanga, “asalamu alaykum”alisalimia Mahamud ambae alionyesha tabasamu la hali ya juu, tabasamu ambalo lilimshangaza hata mke wake, ambae alitegemea kumuona mume wake akimtazama Higgno kwa jicho la mshaka, “waalaykum salaam” waliitikia watu wote waliokuwepo mule ndani, “kwanza kabisa kabla sijajuwa kama wageni wetu wataingiaje na utaratibu gani umepangwa, mimi nina jambo moja nahitaji kuliongea” alisema Mahamud, na watu wakamtazama, hasa wale wa upande wa kike, ni kama walikuwa wanashangaana, “ina maana hajamtambua mkwe wake mwenyewe, wakati wamekaa wote humu ndani muda wote huu?”alijiuliza mama Soraya kwa mshangao, na wakati huo huo Soraya akaletwa pale sebuleni, akiwa amevalia gauni lake refu nzuri, amepambwa akapambika, pia kichwani kwake alivalishwa niqab, ambayo iliziba uso wake wote na kubakiza macho pekee, “anaonekana mzuri, lakini mwili wake unafanana na Soraya” aliwaza Higgno, akimtazama mwanamke huyu pasipo kujuwa kuwa ni Soraya wake, ambae alienda kukaa sehemu aliyo andaliwa huku akisindikizwa na macho ya watu wote waliokuwepo hapa, huku mzee Mahamud akiwa amesimamisha maongezi yake.
Naam baada ya Soraya kukaa, ndipo Mahamud akaendelea, “nime sema nina jambo la kuongea kwasababu ni muhimu sana kwangu, japo kwenu linaweza lisiwe muhimu, naliongea hapa kwasababu ya heshima kwa kijana huyu, hakika mpaka sasa sikuwahi kulifahamu jina lake, kijana ambae naweza kusema ni tofauti kidogo na vijana wengine niliowahi kuwaona na pengine kuwasikia katika dunia hii ya sasa hivi” alisema Mahamud akionekana mwenye furaha usoni mwake, huku watu wote wakimsikiliza kwa umakini, wakati huo mama Soraya alikuwa anamtazama mwanae kwa umakini sana, akamuona anaangaza macho kushoto na kulia akigeuzagueza shingo yake mpaka alipo mtazama Higgno, ambae hakuwa na mpango wowote wa kumtazama Soraya hata kwa bahati mbaya, kitendo kile kilimshangaza mama Soraya, kuliko Soraya mwenyewe, ambae aliejisemea moyoni, “atakuwa hajanitambua” alisema Soraya, huku baba yake akiendelea kuongea, “ikiwa ni siku muhimu kwangu na familia yangu ambapo tunaenda kumtambua na kumkaribisha kijana ambae ataelekea kuwa mchumba wa binti yetu wapekee, nimeona pia nimkaribishe kijana ambae mwaka mmoja uliopita niliwahi kusema kuwa endapo ninge mfahamu ninge muoza binti yangu, ikiwa pamoja na kuwaandalia kila kitu kizuri kinachohitajika katika maisha, kama vile nyumba gari fedha na biashara pia” mzee Mahamud alieleza kwa mapana simulizi yake inayo muhusu yeye na kijana mpole na mwenye nidhamu ya hali ya juu, tayari Soraya alishajuwa kuwa anae zungumziwa ni Higgno, kasoro mama yake ambae sasa alikuwa anatazama wanaume waliokuwepo mule ndani kuona kama atamuona huyo kijana ambae mume wake alikuwa anamzungumzia, lakini hakumuona mtu mwinge zaidi ya Higgno na baba yake, zaidi ya hapo ni wale aliokuwa anawafahamu.
Mahamud alisimulia mkasa mzima, kuanzia kusaidiwa siku ile ambayo alivamiwana wale vibaka kule msamala, pia alivyokutana nae jana pale mjini alipodondosha wallet yake na yeye kuiokota akimpelekea kama ilivyo, na rundo la fedha ndani yake, hapo kila mmoja akaanza kutazama kumtafuta kijana mwenyewe kama alivyofanya mama Soraya dakika chache zilizopita, wapo waliomtazama Higgno na wapo ambao walidhania kuwa bado hajaingia pale sebuleni, “kweli sikuweza kuvumilia, niliamini kijana huyu ni zawadi kubwa sana katika maisha ya binti yangu, hivyo nilimuomba amchumbie binti yangu, lakini bahati njema kwake, kuwa tayari alikuwa anamchumba na anapanga kupeleka barua, malengo yake yakitimia, ila la kufurahisha mimi nitakuwa mshenga wa kijana huyu, na nitamfanyia mambo mengi ambayo yatakuwa kama msaada katika maisha yake na mke wake” hapo kila mmoja mule ndani akapiga makofi, huku mama Soraya akitamani kumuona kijana huyo mwenye moyo wa ajabu, na sio Higgno ambae licha ya muonekano wake mzuri na wa upole lakini ni tapeli, “bahati mbaya kijana huyu, sijamjuwa jina lake, atajitamburisha mwenyewe, na kuanzia sasa ninamkaribisha hapa nyumbani, na ninaomba kila aliepo hapa amchukulia kama ndugu kwake” alisema Mahamud na kila mmoja akashangilia huku wakistaajabu kwa moyo wa kijana huyu, “kijana hebu simama ujitambulishe mbele ya wageni waliopo hapa pamoja na mama yako yule pale na dada yako huyu hapa ambae leo atatuonyesha mchumba wake” alisema Mahamud na hapo Higgno akasimama na hapo mama Soraya aliekaa karibu kabisa na mama Hoggno aliekuwa anatokwa na mchozi kwa sifa alizopewa mwanae, mama Soraya akatoa macho ya mshangao, na kujikuta amesha nongo’ona, “mungu wangu, kumbe ni huyu Higgno, hakika mungu huwajalia mema wale walio wema, mwenyezi mungu ni samehe” alisema mama Soraya na kumfanya mama Higgno, amtazame kwa mshangao…… ITAENDELEA MUWE NA USIKU MWEMA