SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA AROBAINI NA NANE
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA SABA: moja kwa moja mpaka kwenye kile kibanda kidogo cha udongo ambacho nje yake kulikuwa na mtu amekaa karibu na moto, huku zikionekana nyama na samaki wengi wakibanikwa juu yake, “ndio yeye” alisema nong’ona Soraya huku yeye na Layla wana mtazama kijana pole ambae sasa alisha mjua jina kuwa ni Higno, ambae alikuwa analishangaa gari lile lililopandishwa vioo, lililokuwa linamulika kwa taa zake, “ndiyo ni yeye” alisema Laylah kwa sauti ya kunong’ona pia, “mwenzio naona aibu, tushuke kwanza wote halafu utaondoka” alisema Soraya kwa sauti ya kunong’ona huku anajichekesha kicheko cha chini chini kilichojaa aibu ……… ENDELEA….
Huku wakimtazama Higgno aliekuwa amevalia bukta na kandambili bila tishet wala shati na kuacha wazi kifua chake kipana kilicho jengeka kimazoezi na kufanya kionekane mbele ya waschana hawa wawili, ambae alikuwa anasimama pale pembeni ya moto akilitazama gari huku uso wake ukionyesha wazi kulishangaa, “halafu nikishuka mimi nitafanyaje?” aliuliza Laylah kwa sauti ya chini huku wakiendelea kumtazama kijana mpole, ambae sasa alianza kutembea taratibu kulisogelea lile gari ambalo lilikuwa limesimama mita kama kumi au kumi na tano toka kilipo kibanda, “huyooo anakuja twende bwana” alisema Soraya aliekaa nyuma ya seat ya Laylah, huku anaendelea kutazama kifua na Suraya ya kijana mpole aliekuwa analisogelea bila wasi wasi wowote gari lao, japo bado alionekana kujiuliza maswali juu yao, “haya tushuke sasa” alisema Laylah kwa sauti ya kunong’ona yenye wasi wasi, ambae kiukweli aliogopa kwa kile alichomfanyia Higgno kule ofisini, akichelea kuwa atamuona mtu mbaya kwake, “anza kushuka wewe bwana” alisema Soraya kwa sauti ya chini, iliyojaa wasi wasi na kijiuoga cha kupendeza, huku akimgusa gusa Laylah begani ambae alipata wazo la haraka, nalo ni kushusha kioo ili aongee nae kupitia hapo.
Naam Higgno akiwa mwenye kujiuliza kuhusu ujio wa gari la mschana wa kiarabu aliemsaidia jana mida hii ya usiku, alilisogelea gari lile mpaka usawa wa mlango wa upande wa dereva wa gari lile lililokuwa bado lina unguruma na taa zipo wazi zinamulika kwenye kibanda, ambako samaki na nyama za porini zilikuwa zina endelea kubanikwa juu ya moto wa wastani na kutoa harufu nzuri ya kuleta hamu ya kula ambayo iliingiia ndani ya gari kupitia kioo ambacho kilikuwa wazi na kupenya kwenye pua za waschana hawa wawili waliozoea vyakula vya kuungwa na vikorombwezo vingi.
Higgno alipeleka macho yake moja kwa moja kwa Dereva akitarajia kumuona yule mschana aliemsaidia jana mchana, lakini akakutana na sura ya yule mschana dereva aliemuekea ngumu kule kwenye maombi ya kazi, hapo Laylah akatarajia kuona sura ya kijana huyu ikibadilika kwa hasira huku Soraya akiinamisha kichwa chake na kukificha nyuma ya seat ya dereva.
Lakini ilikuwa tofauti na mawazo ya Laylah, ndio kwanza akaiona ile sura ya upole ya yule kijana mpole Higgno ikiunda tabasamu na kumfanya azidi kufichua uzuri wake wa kiume uliobebwa na muonekano wa upole, “karibu dada, naona umekuja usiku, unaulizia shambani kwa boss wako?….yaani namanisha kwa yule mschana mzuri?” aliuliza Higgno kwa sauti ya upole, akionekana kubabaika kidogo, nadhani ni kwasababu ya kumuona Laylah usiku kama ule kule porini.
Hakika lile neno mzuri lilimsisimua Soraya aliekuwa kiti cha nyuma amejibanza na kujikuta akicheka kidogo chini chini kicheko cha raha japo kilijaa aibu, kicheko ambacho kilimfikia Higgno na kumfanya ashangae kidogo, maana alisikia cheko bila kujuwa nani kacheka kwasababu Laylah hakuonekana kucheka zaidi ya kutabasamu baada ya kicheko kusikika, “hapana kaka Higgno, nimemleta Da’Soraya, ana maongezi na wewe” alisema Laylah, na kumfanya Soraya atabasamu huku mapigo yake ya moyo yakianza kwenda mbio kwa hofu ya kukataliwa maongezi na kijana mpole ambae ni kama alionekana kushangaa kidogo, “mhh! sasa mbona usiku sana, kwanini… kwanini asi..” kabla Higgno haja malizia Laylah akamdaka juu kwa juu huku akionekana kushtuka kama vile ametekenywa mbavu, “ndio ni usiku amekuja kusema asante kwa vile unavyo msaidiaga” alisema Laylah, ni baada ya kutekenywa na Soraya ambae alimtaka aongee neno ili asikataliwe, “hoooo! yupo humu ndani ya gari?” aliuliza Higgno kwa sauti ya upole lakini iliyochangamka kidogo akionyesha kutokuamini, “mhmh!” safari hii ilikuwa ni sauti nyororo nyembamba na tamu kwenye masikio toka seat ya nyuma, “asante na wewe dada yangu, lakini hukupaswa kusumbuka hivyo, pengine tungeonana siku nyingine” alisema Higgno kwa sauti ya upole ile ile ya kuchangamka.
Kusikia hivyo Soraya akamgusa tena Laylah kwenye mbavu nae akashtuka kidogo huku hajui aongee nini, “eti amekuja anataka akae kidogo hapa muongee kidogo” alisema Laylah, huku anapeleka mkono kwenye seat ya pembeni yake na kuchukua begi dogo la Soraya na kumkabidhi Higgno kupitia dirishani, na Higgno akalipokea huku akiachama mdomo kwa mshangao, na wakati huo huo simu ya Soraya ikasikika ikiita, hapo Soraya akapokea ile simu na akiwa bado ndani ya gari, “Hallow baba assalamu alaykum” alisalimia Soraya kwa sauti ya kawaida akijiaribu kijiweka sawa aonekane yupo kawaida, “waalaykum salaam, vipi mushafika kwa kina Laylah” aliuliza mzee Mahamud kwa sauti fulani iliyo onyesha kupungua hofu na mashaka, “ndio tunaingia hata bado hatuja shuka toka kwenye gari” alisema Soraya kwa sauti ya uchangamfu, na kumfanya Higgno ashangae zaidi kwa kudhania kuwa baba wa mwanamke huyu anafahamu kuwa yeye amekuja huku kwake, “ok! basi nakutakia usiku mwema, mama yako ameshaanza kukukumbuka” alisema mzee Mahamud na Soraya akacheka kidogo, “ nae sasa nikiolewa atafanyaje, na nyie pia nawatakia usiku mwema baba” alisema Soraya na kukata simu, kisha akamuuliza Laylah, nishuke?” ilikuwa ni sauti ya chini ya kuning’ona, “ndio begi lako nimeshampa” alisema Laylah, na hapo Higgno aliekuwa amesimama mita moja nje ya gari akaona mlango wa nyuma wa gari unafunguliwa na akatoka mschana mwenye urefu wa wastani na umbo la kupendeza lililo umbwa likaumbika akiwa amevalia nguo ndefu nyeusi na niqab usoni, hapo ndipo alipo mkumbuka yule mwanamke alieleweshwa na kuomba msaada wake, “hooo! kumbe ulikuwa wewe” alijisemea Higgno kimoyo moyo huku anamtazama yule mwanamke ambae alikuwa amesha shuka na kusimama karibu yake, “assaalam alaykum” alisalimia Soraya huku anatazamisha kichwa chini kwa aibu, japo Higgno hakuwahi kusalimiwa salamu kama ile lakini aliweza kuitikia kwasababu alikuwa anaifahamu, “alaykum salam” japo aliitikia kama msukuma kwa ukavu wa matamshi yake, baada ya hapo wote wakasimama kimya kama vile hakuna aliejua kifuatacho huku Layla akianza kugeuza gari na kupata uelekeo wa barabarani, Higgno akidhania kuwa mschana yule anageuza gari kisha analipaki na kushuka, lakini akashangaa kusikia Laylah akisema, “kesho nitakuja saa kumi na mbili” neno la Laylah, lilimshtua Higgno saa kumi na mbili ipi wakati sasa ni saa mbili inaeleka saa tatu, kabla hajauliza akamsikia Soraya akijibu, “njoo saa moja nitakuwa nimesha jiandaa” hapo Higgno akaona kuwa ule haukuwa mchezo ila ni kitu serious, na aligundua hilo mara baada ya kuona Laylah akiondoa gari taratibu kuifuata barabara kuu, wote wakabakia kama milingoti huku wakilisindikiza kwa macho Land Rover Discovery, ambalo lilitiririka taratibu na kushika barabara kisha likaongezwa mwendo na kutokomea upande wa mjini.
Naam sasa walikuwa wamebakia wawili pale shambani bado wamesimama, Higgno kama ameshikwa na mshangao hakujuwa huyu mgeni amekuja hapa kwa maongezi gani na atakaa kaaje, “karibu” alisema Higgno kwa sauti ya upole akiongoza kwenye kibanda huku Soraya akija taratibu nyuma yake.
Higgno haraka sana akaanza kukifuta futa kiti kidogo cha chini, (kigoda) kile alichokalia yeye mwanzo na kukisogeaza pembeni kidogo ya moto, “karibu ukae samahani sana maana viti vyenyewe ..” alisema Higgno kwa sauti yake ya upole ambayo kwa sasa ilionyesha kufadhaika kidogo kutokana na mazingira yaliyopo pale kwake, “bila samahani, mbona hata kwetu vipo” alijibu Soraya kwa sauti ile ile ya chini nyororo, yenye kunoga masikioni huku anakusanya gauni lake na kulibana mapajani na kukaa kwenye kile kigoda, “mh! hata kwao vipo?” aliuliza Higgno, huku anamtazama yule mschana aliejiziba uso kwa niqab na kubakiza macho pekee, ambayo kwa wakati huo yalikuwa yana mtazama Higgno na kusababisha ya kutane, hapo wote wakajikuta wanatazama pembeni wakikwepesha macho yao yasitazamane, “huo mkoba niwekee ndani” alisema Soraya na hapo kama aliekimbizwa Higgno aliingia ndani kwa haraka, nadhani ni msaada wa moto uliokuwa unawaka pale nje, aliweza kuuweka mkoba juu ya meza na kutoka na ndoo moja tupu ambayo aliitumia kama kiti na wote wakawa kimya kama vile wanasikiliza mafundisho fulani au mawaidha ya dini, huku masikio yao yakisikia sauti za ndege wa usiku na vijidudu vya porini, mara kwa mara Higgno akiendelea kutupia kuni kwenye moto pasipo kujua kuwa anauzidisha na anaweza kuleta madhara hapo baadae.*****
Naam tutembelee nyumbani kwa bwana Mahadhi, kule mfaranyaki, ilikuwa imeshapita siku moja toka waumbuliwe kule nyumbani kwa mzee Mahamud, Idd alikuwa akishinda kutwa nzima akinywa pombe huku baba yake akijaribu kumpooza kwa maneno ya kumfariji, “lakini baba, tume kosea wapi, mbona ilikuwa ni kitendo cha baba yake kutoa amri kuwa barua imeshapokelewa” alisema Idd kilevi, “tatizo Idd una haraka sana we si umemsikia mwenyewe yule binti amesema kuwa huyo kijana hamjui hata jina, we unadhani kuna nini hapo” alisema mzee Mahadhi kwa kujiamini, “lakini baba, huyo mtu si yupo?” aliuliza Idd alieonyesha kukata tamaa, “akiwepo ndio nini sasa, cha msingi tuna takiwa kufanya mambo mawili, kwanza ni kutengeneza maneno ambayo yataharibu jina la Mahamud, na ili kujisafisha basi atalazimika kukubali wewe umuoe Soraya” alisema Mahadhi kwa sauti iliyo tawaliwa na furaha ya mafanikio, “hapo kama una kuja kuja baba, sasa ni maneno gani hayo ambayo yatamfanya Mahamud alazimike kumuamrisha mwanae akubali nimuoe” aliuliza Idd, akionyesha mwenye shauku na tumaini jipya la kumpata Soraya na mali za baba yake, maana licha ya utajiri wa mzee Mahamud, pia tayari Idd alishasikia habari za magari mapya ya Soraya EXPRESS yatakayo unda kampuni ambayo itakuwa pacha na ile ya Mahamud Trans, “we! niachie mimi, utaona jinsi fitina zinavyo faanywa, halafu kwa taarifa yako pia nataka ionekane kuwa wewe walikusingizia kuwa ulimfanyia ujanja Soraya ili ukose kumchumbia, hivyo itakusaidia kukusafishia jina lako na wao kukupa mke ikiwa ni njia ya kufuta hiyo kashfa” alisema Mahadhi, na hapo Idd akapiga makofi kilevi levi, “mbona nakuaminia professor wangu” alisema Idd kilevi levi.*****
Giza lilikuwa limetanda kiasi, bado ungeweza kuona mtu mmoja mmoja akitembea kwenye barabara tulivu za mitaa ya Luhila, ama alikuwa anaelekea dukani au anaelekea nyumbani akitoka kwenye mihangaiko ya kila siku, maana mida ya walevi ilikuwa bado kama ilivyozoeleka kwa mitaa hii ya Luhuila.
Tofauti na kule ndani ya mitaa kwa kina mzee Frank, huku barabara kuu iendayo mikoa ya kusini mambo yalikuwa tofauti, maana palionekana kuchangaka sana tena sana, ungedhania sio saa tatu za usiku kwa uchangamkaji wake, music ulisikika kwa fujo, maana kila kilabu cha pombe za kienyeji na zile bar za pombe za kizungu ambazo zilikuwa zime karibiana sana na kusheheni watu kila moja ilikuwa na music wake, tena tofauti tofauti, hapa ungesikia inapigwa salome ya Dully Seyks, hapa ungesikia caupe bibamba ya Awilo Longomba, nyingine ungesikia wimbo wa manung’a embe wa ngoni tribe, huku ungemsikia, Luck dube na wimbo wake wa remember me, na kila mmiliki wa kilabu angeongeza sauti mpaka juu ili amzidi mwenzie.
Hilda leo kidogo mambo yake yalikuwa yamekaa vibaya, maana toka alipofika eneo lile kwaajili ya kuopoa mwanaume atakae hitaji kufanya mazoezi kwake kwa malipo ya ulanzi, lakini hakufanikiwa na baada ya kukaa kwa dakika kadhaa, ndipo alipoona kuwa mahali pale hapakumfaa kabisa, hivyo bora aondoke zake.
Lakini wakati anaondoka mara akamuona kijana Talib, akikatiza mitaa ya barabara kuu kwa mwendo wa haraka na kueleka kwenye kilabu cha mwisho kabisa upande wa mashariki akiwa na dumu la lita tano mkononi mwake, ni kama lilikuwa na maji au mafuta ndani yake, “mh! yule amefuata nini huku Luhila usiku kama huu?” alijiuliza Hilda huku anamtazama Talib kwa macho ya mshangao kama vile hakuamini macho yake kwa kile alichokiona, “au ameharibikiwa na gari?” alijuliza Hilda binti komba huku anaanza kutembea kumfuata Talib ambae aliongoza moja kwa moja kwenye mlango wa ile bar ya mwisho, na kuingia ndani, “mbona anaingia mule, wacha nimuwahi” alisema Hilda akitembea kwa haraka, mwendo wa nusu kikimbia ili kumuwahi Talib, akili yake ikiwa ni kwenda kupewa offer ya ulanzi, huku akisahau yaliyomtokea week chache zilizopita juu ya kijana huyubambae ni baba wa mtoto wake.******
Mahilo, nje ya kibanda cha Higgno moto ulionekana ukiwaka kwa nguvu sana kiasi cha kusababisha hata nyama na samaki zilizo tandazwa kwenye waya juu ya moto ule kuanza kutoa harufu ya kuungua, na moto ule uliosababishwa na kuni nyingi zilizowekwa na Higgno, ambae alijikuta akifanya hivyo kwa kukosa la kufanya au kuongea mbele ya Soraya, ambae mara kwa mara alikuwa anamtazama kwa macho ya wizi, akitazama sana sehemu za kifua na usoni huku muda wote wakiwa kimya, hakuna aliemsemesha mwenzie kwa dakika kumi nzima, “mbona kama unaunguza” alisema Soraya huku anajaribu kupeleka mkono kugeuza samaki mmoja aliekuwa karibu yake, lakini kabla hajagusa tayari Higgno alishamdaka mkono, “hapa utaungua” alisema Higgno akimzuia mschana huyu na kisha yeye akaanza tena kuondoa moto jikoni kwa maana ya kuupunguza, ilimradi alikuwa busy.
Ni kama Soraya aligundua kuwa Higgno yupo busy kwasababu yake, akamtazama kwa sekunde kadhaa, “Higgno huogopi kukaa peke yako” aliuliza Soraya kwa sauti yake nyororo iliyoambatana na kijicheko fulani huku akimtazama Higgno “mbona hakutishi, kwani wewe unaogopa?” aliuliza Higgno huku akiwa busy na kugeuza samaki, “wala siogopi si nipo na wewe” alijibu Soraya na wote wakacheka kidogo, hapo kikapita kimya kingine cha sekunde kadhaa, ni kama Soraya alikuwa anatafuta swali jingine, “Higgno kwani hiyo nyama ya nini?” aliuliza Soraya huku akimtazama Higgno, “ngolombwe vipi unakulaga?” aliuliza Higgno huku akiendelea kugeuza samaki na pande ya nyama, “nilikula zamani sana aliletaga baba” alijibu Soraya ambae ni kama alianza kumzoea Higgno taratibu.
Kikapita kimya kingine Soraya akitafuta swali, maana alishaona akikaa kimya ingekula kwake, kwasababu Higgno sio mwongeaji, “kwani hawa samaki unawauzaga?” aliulizia Soraya huku akimtazama Higgno bila wasi wasi wowote, maana alishagundua kuwa kijana huyu asinge weza kumtazama usoni, “hapana hawa nawavua kwaajili ya kula unaweza kuonja mmoja ni watamu sana” alisema Higgno huku tayari mkononi mwake akiwa na samaki mmoja mkubwa sana aliekuwa anachuruzika mafuta kutokana na ule moto mkali, “ndiyo nitakula” alisema Soraya kwa sauti yake nyororo huku anasimama, “ngoja ni chukue sahani maana anamoto, “alisema Higgno akimrudisha samaki juu ya waya lakini pembeni kidogo na kuinuka akitaka kuingia ndani, “subiri kidogo” alisema Soraya na hapo Higgno akasimama kumtazama Soraya ambae alikuwa anafungua ile niqab na kuiondoa usoni mwake, akiacha sura wazi na kumpa Higgno wasaa mwingine wa kuitazama sura yenye kila sifa ya kuitwa nzuri, hapo Higgno aliduwaa mpaka alipokabidhiwa ile niqab mkononi, na kabla hajaondoka akamuona anatoa kitambaa cha kichwani yaani ushungi na kumpatia Higgno, ambae baada ya kupokea akataka kuondoka maana alihisi anaweza kugundulika kuwa alizishangaa nywele ndefu za mschana yule zilizo vuka mabega na kumwagika mgongoni, “subiri na hili baibui maana nasikia joto” alisema Soraya huku anashika baibui lake jeusi na kuanza kulipandisha juu kwa lengo la kulivuwa, hapo Higgno akajihisi mwili unamsisimka maana hakujuwa mschana huyu akivua baibui atabakia na nguo gani ndani…… ITAENDELEA MUWE NA USIKU MWEMA
 
Andaeni popcorn andaeni popcorn
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA AROBAINI NA NANE
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA SABA: moja kwa moja mpaka kwenye kile kibanda kidogo cha udongo ambacho nje yake kulikuwa na mtu amekaa karibu na moto, huku zikionekana nyama na samaki wengi wakibanikwa juu yake, “ndio yeye” alisema nong’ona Soraya huku yeye na Layla wana mtazama kijana pole ambae sasa alisha mjua jina kuwa ni Higno, ambae alikuwa analishangaa gari lile lililopandishwa vioo, lililokuwa linamulika kwa taa zake, “ndiyo ni yeye” alisema Laylah kwa sauti ya kunong’ona pia, “mwenzio naona aibu, tushuke kwanza wote halafu utaondoka” alisema Soraya kwa sauti ya kunong’ona huku anajichekesha kicheko cha chini chini kilichojaa aibu ……… ENDELEA….
Huku wakimtazama Higgno aliekuwa amevalia bukta na kandambili bila tishet wala shati na kuacha wazi kifua chake kipana kilicho jengeka kimazoezi na kufanya kionekane mbele ya waschana hawa wawili, ambae alikuwa anasimama pale pembeni ya moto akilitazama gari huku uso wake ukionyesha wazi kulishangaa, “halafu nikishuka mimi nitafanyaje?” aliuliza Laylah kwa sauti ya chini huku wakiendelea kumtazama kijana mpole, ambae sasa alianza kutembea taratibu kulisogelea lile gari ambalo lilikuwa limesimama mita kama kumi au kumi na tano toka kilipo kibanda, “huyooo anakuja twende bwana” alisema Soraya aliekaa nyuma ya seat ya Laylah, huku anaendelea kutazama kifua na Suraya ya kijana mpole aliekuwa analisogelea bila wasi wasi wowote gari lao, japo bado alionekana kujiuliza maswali juu yao, “haya tushuke sasa” alisema Laylah kwa sauti ya kunong’ona yenye wasi wasi, ambae kiukweli aliogopa kwa kile alichomfanyia Higgno kule ofisini, akichelea kuwa atamuona mtu mbaya kwake, “anza kushuka wewe bwana” alisema Soraya kwa sauti ya chini, iliyojaa wasi wasi na kijiuoga cha kupendeza, huku akimgusa gusa Laylah begani ambae alipata wazo la haraka, nalo ni kushusha kioo ili aongee nae kupitia hapo.
Naam Higgno akiwa mwenye kujiuliza kuhusu ujio wa gari la mschana wa kiarabu aliemsaidia jana mida hii ya usiku, alilisogelea gari lile mpaka usawa wa mlango wa upande wa dereva wa gari lile lililokuwa bado lina unguruma na taa zipo wazi zinamulika kwenye kibanda, ambako samaki na nyama za porini zilikuwa zina endelea kubanikwa juu ya moto wa wastani na kutoa harufu nzuri ya kuleta hamu ya kula ambayo iliingiia ndani ya gari kupitia kioo ambacho kilikuwa wazi na kupenya kwenye pua za waschana hawa wawili waliozoea vyakula vya kuungwa na vikorombwezo vingi.
Higgno alipeleka macho yake moja kwa moja kwa Dereva akitarajia kumuona yule mschana aliemsaidia jana mchana, lakini akakutana na sura ya yule mschana dereva aliemuekea ngumu kule kwenye maombi ya kazi, hapo Laylah akatarajia kuona sura ya kijana huyu ikibadilika kwa hasira huku Soraya akiinamisha kichwa chake na kukificha nyuma ya seat ya dereva.
Lakini ilikuwa tofauti na mawazo ya Laylah, ndio kwanza akaiona ile sura ya upole ya yule kijana mpole Higgno ikiunda tabasamu na kumfanya azidi kufichua uzuri wake wa kiume uliobebwa na muonekano wa upole, “karibu dada, naona umekuja usiku, unaulizia shambani kwa boss wako?….yaani namanisha kwa yule mschana mzuri?” aliuliza Higgno kwa sauti ya upole, akionekana kubabaika kidogo, nadhani ni kwasababu ya kumuona Laylah usiku kama ule kule porini.
Hakika lile neno mzuri lilimsisimua Soraya aliekuwa kiti cha nyuma amejibanza na kujikuta akicheka kidogo chini chini kicheko cha raha japo kilijaa aibu, kicheko ambacho kilimfikia Higgno na kumfanya ashangae kidogo, maana alisikia cheko bila kujuwa nani kacheka kwasababu Laylah hakuonekana kucheka zaidi ya kutabasamu baada ya kicheko kusikika, “hapana kaka Higgno, nimemleta Da’Soraya, ana maongezi na wewe” alisema Laylah, na kumfanya Soraya atabasamu huku mapigo yake ya moyo yakianza kwenda mbio kwa hofu ya kukataliwa maongezi na kijana mpole ambae ni kama alionekana kushangaa kidogo, “mhh! sasa mbona usiku sana, kwanini… kwanini asi..” kabla Higgno haja malizia Laylah akamdaka juu kwa juu huku akionekana kushtuka kama vile ametekenywa mbavu, “ndio ni usiku amekuja kusema asante kwa vile unavyo msaidiaga” alisema Laylah, ni baada ya kutekenywa na Soraya ambae alimtaka aongee neno ili asikataliwe, “hoooo! yupo humu ndani ya gari?” aliuliza Higgno kwa sauti ya upole lakini iliyochangamka kidogo akionyesha kutokuamini, “mhmh!” safari hii ilikuwa ni sauti nyororo nyembamba na tamu kwenye masikio toka seat ya nyuma, “asante na wewe dada yangu, lakini hukupaswa kusumbuka hivyo, pengine tungeonana siku nyingine” alisema Higgno kwa sauti ya upole ile ile ya kuchangamka.
Kusikia hivyo Soraya akamgusa tena Laylah kwenye mbavu nae akashtuka kidogo huku hajui aongee nini, “eti amekuja anataka akae kidogo hapa muongee kidogo” alisema Laylah, huku anapeleka mkono kwenye seat ya pembeni yake na kuchukua begi dogo la Soraya na kumkabidhi Higgno kupitia dirishani, na Higgno akalipokea huku akiachama mdomo kwa mshangao, na wakati huo huo simu ya Soraya ikasikika ikiita, hapo Soraya akapokea ile simu na akiwa bado ndani ya gari, “Hallow baba assalamu alaykum” alisalimia Soraya kwa sauti ya kawaida akijiaribu kijiweka sawa aonekane yupo kawaida, “waalaykum salaam, vipi mushafika kwa kina Laylah” aliuliza mzee Mahamud kwa sauti fulani iliyo onyesha kupungua hofu na mashaka, “ndio tunaingia hata bado hatuja shuka toka kwenye gari” alisema Soraya kwa sauti ya uchangamfu, na kumfanya Higgno ashangae zaidi kwa kudhania kuwa baba wa mwanamke huyu anafahamu kuwa yeye amekuja huku kwake, “ok! basi nakutakia usiku mwema, mama yako ameshaanza kukukumbuka” alisema mzee Mahamud na Soraya akacheka kidogo, “ nae sasa nikiolewa atafanyaje, na nyie pia nawatakia usiku mwema baba” alisema Soraya na kukata simu, kisha akamuuliza Laylah, nishuke?” ilikuwa ni sauti ya chini ya kuning’ona, “ndio begi lako nimeshampa” alisema Laylah, na hapo Higgno aliekuwa amesimama mita moja nje ya gari akaona mlango wa nyuma wa gari unafunguliwa na akatoka mschana mwenye urefu wa wastani na umbo la kupendeza lililo umbwa likaumbika akiwa amevalia nguo ndefu nyeusi na niqab usoni, hapo ndipo alipo mkumbuka yule mwanamke alieleweshwa na kuomba msaada wake, “hooo! kumbe ulikuwa wewe” alijisemea Higgno kimoyo moyo huku anamtazama yule mwanamke ambae alikuwa amesha shuka na kusimama karibu yake, “assaalam alaykum” alisalimia Soraya huku anatazamisha kichwa chini kwa aibu, japo Higgno hakuwahi kusalimiwa salamu kama ile lakini aliweza kuitikia kwasababu alikuwa anaifahamu, “alaykum salam” japo aliitikia kama msukuma kwa ukavu wa matamshi yake, baada ya hapo wote wakasimama kimya kama vile hakuna aliejua kifuatacho huku Layla akianza kugeuza gari na kupata uelekeo wa barabarani, Higgno akidhania kuwa mschana yule anageuza gari kisha analipaki na kushuka, lakini akashangaa kusikia Laylah akisema, “kesho nitakuja saa kumi na mbili” neno la Laylah, lilimshtua Higgno saa kumi na mbili ipi wakati sasa ni saa mbili inaeleka saa tatu, kabla hajauliza akamsikia Soraya akijibu, “njoo saa moja nitakuwa nimesha jiandaa” hapo Higgno akaona kuwa ule haukuwa mchezo ila ni kitu serious, na aligundua hilo mara baada ya kuona Laylah akiondoa gari taratibu kuifuata barabara kuu, wote wakabakia kama milingoti huku wakilisindikiza kwa macho Land Rover Discovery, ambalo lilitiririka taratibu na kushika barabara kisha likaongezwa mwendo na kutokomea upande wa mjini.
Naam sasa walikuwa wamebakia wawili pale shambani bado wamesimama, Higgno kama ameshikwa na mshangao hakujuwa huyu mgeni amekuja hapa kwa maongezi gani na atakaa kaaje, “karibu” alisema Higgno kwa sauti ya upole akiongoza kwenye kibanda huku Soraya akija taratibu nyuma yake.
Higgno haraka sana akaanza kukifuta futa kiti kidogo cha chini, (kigoda) kile alichokalia yeye mwanzo na kukisogeaza pembeni kidogo ya moto, “karibu ukae samahani sana maana viti vyenyewe ..” alisema Higgno kwa sauti yake ya upole ambayo kwa sasa ilionyesha kufadhaika kidogo kutokana na mazingira yaliyopo pale kwake, “bila samahani, mbona hata kwetu vipo” alijibu Soraya kwa sauti ile ile ya chini nyororo, yenye kunoga masikioni huku anakusanya gauni lake na kulibana mapajani na kukaa kwenye kile kigoda, “mh! hata kwao vipo?” aliuliza Higgno, huku anamtazama yule mschana aliejiziba uso kwa niqab na kubakiza macho pekee, ambayo kwa wakati huo yalikuwa yana mtazama Higgno na kusababisha ya kutane, hapo wote wakajikuta wanatazama pembeni wakikwepesha macho yao yasitazamane, “huo mkoba niwekee ndani” alisema Soraya na hapo kama aliekimbizwa Higgno aliingia ndani kwa haraka, nadhani ni msaada wa moto uliokuwa unawaka pale nje, aliweza kuuweka mkoba juu ya meza na kutoka na ndoo moja tupu ambayo aliitumia kama kiti na wote wakawa kimya kama vile wanasikiliza mafundisho fulani au mawaidha ya dini, huku masikio yao yakisikia sauti za ndege wa usiku na vijidudu vya porini, mara kwa mara Higgno akiendelea kutupia kuni kwenye moto pasipo kujua kuwa anauzidisha na anaweza kuleta madhara hapo baadae.*****
Naam tutembelee nyumbani kwa bwana Mahadhi, kule mfaranyaki, ilikuwa imeshapita siku moja toka waumbuliwe kule nyumbani kwa mzee Mahamud, Idd alikuwa akishinda kutwa nzima akinywa pombe huku baba yake akijaribu kumpooza kwa maneno ya kumfariji, “lakini baba, tume kosea wapi, mbona ilikuwa ni kitendo cha baba yake kutoa amri kuwa barua imeshapokelewa” alisema Idd kilevi, “tatizo Idd una haraka sana we si umemsikia mwenyewe yule binti amesema kuwa huyo kijana hamjui hata jina, we unadhani kuna nini hapo” alisema mzee Mahadhi kwa kujiamini, “lakini baba, huyo mtu si yupo?” aliuliza Idd alieonyesha kukata tamaa, “akiwepo ndio nini sasa, cha msingi tuna takiwa kufanya mambo mawili, kwanza ni kutengeneza maneno ambayo yataharibu jina la Mahamud, na ili kujisafisha basi atalazimika kukubali wewe umuoe Soraya” alisema Mahadhi kwa sauti iliyo tawaliwa na furaha ya mafanikio, “hapo kama una kuja kuja baba, sasa ni maneno gani hayo ambayo yatamfanya Mahamud alazimike kumuamrisha mwanae akubali nimuoe” aliuliza Idd, akionyesha mwenye shauku na tumaini jipya la kumpata Soraya na mali za baba yake, maana licha ya utajiri wa mzee Mahamud, pia tayari Idd alishasikia habari za magari mapya ya Soraya EXPRESS yatakayo unda kampuni ambayo itakuwa pacha na ile ya Mahamud Trans, “we! niachie mimi, utaona jinsi fitina zinavyo faanywa, halafu kwa taarifa yako pia nataka ionekane kuwa wewe walikusingizia kuwa ulimfanyia ujanja Soraya ili ukose kumchumbia, hivyo itakusaidia kukusafishia jina lako na wao kukupa mke ikiwa ni njia ya kufuta hiyo kashfa” alisema Mahadhi, na hapo Idd akapiga makofi kilevi levi, “mbona nakuaminia professor wangu” alisema Idd kilevi levi.*****
Giza lilikuwa limetanda kiasi, bado ungeweza kuona mtu mmoja mmoja akitembea kwenye barabara tulivu za mitaa ya Luhila, ama alikuwa anaelekea dukani au anaelekea nyumbani akitoka kwenye mihangaiko ya kila siku, maana mida ya walevi ilikuwa bado kama ilivyozoeleka kwa mitaa hii ya Luhuila.
Tofauti na kule ndani ya mitaa kwa kina mzee Frank, huku barabara kuu iendayo mikoa ya kusini mambo yalikuwa tofauti, maana palionekana kuchangaka sana tena sana, ungedhania sio saa tatu za usiku kwa uchangamkaji wake, music ulisikika kwa fujo, maana kila kilabu cha pombe za kienyeji na zile bar za pombe za kizungu ambazo zilikuwa zime karibiana sana na kusheheni watu kila moja ilikuwa na music wake, tena tofauti tofauti, hapa ungesikia inapigwa salome ya Dully Seyks, hapa ungesikia caupe bibamba ya Awilo Longomba, nyingine ungesikia wimbo wa manung’a embe wa ngoni tribe, huku ungemsikia, Luck dube na wimbo wake wa remember me, na kila mmiliki wa kilabu angeongeza sauti mpaka juu ili amzidi mwenzie.
Hilda leo kidogo mambo yake yalikuwa yamekaa vibaya, maana toka alipofika eneo lile kwaajili ya kuopoa mwanaume atakae hitaji kufanya mazoezi kwake kwa malipo ya ulanzi, lakini hakufanikiwa na baada ya kukaa kwa dakika kadhaa, ndipo alipoona kuwa mahali pale hapakumfaa kabisa, hivyo bora aondoke zake.
Lakini wakati anaondoka mara akamuona kijana Talib, akikatiza mitaa ya barabara kuu kwa mwendo wa haraka na kueleka kwenye kilabu cha mwisho kabisa upande wa mashariki akiwa na dumu la lita tano mkononi mwake, ni kama lilikuwa na maji au mafuta ndani yake, “mh! yule amefuata nini huku Luhila usiku kama huu?” alijiuliza Hilda huku anamtazama Talib kwa macho ya mshangao kama vile hakuamini macho yake kwa kile alichokiona, “au ameharibikiwa na gari?” alijuliza Hilda binti komba huku anaanza kutembea kumfuata Talib ambae aliongoza moja kwa moja kwenye mlango wa ile bar ya mwisho, na kuingia ndani, “mbona anaingia mule, wacha nimuwahi” alisema Hilda akitembea kwa haraka, mwendo wa nusu kikimbia ili kumuwahi Talib, akili yake ikiwa ni kwenda kupewa offer ya ulanzi, huku akisahau yaliyomtokea week chache zilizopita juu ya kijana huyubambae ni baba wa mtoto wake.******
Mahilo, nje ya kibanda cha Higgno moto ulionekana ukiwaka kwa nguvu sana kiasi cha kusababisha hata nyama na samaki zilizo tandazwa kwenye waya juu ya moto ule kuanza kutoa harufu ya kuungua, na moto ule uliosababishwa na kuni nyingi zilizowekwa na Higgno, ambae alijikuta akifanya hivyo kwa kukosa la kufanya au kuongea mbele ya Soraya, ambae mara kwa mara alikuwa anamtazama kwa macho ya wizi, akitazama sana sehemu za kifua na usoni huku muda wote wakiwa kimya, hakuna aliemsemesha mwenzie kwa dakika kumi nzima, “mbona kama unaunguza” alisema Soraya huku anajaribu kupeleka mkono kugeuza samaki mmoja aliekuwa karibu yake, lakini kabla hajagusa tayari Higgno alishamdaka mkono, “hapa utaungua” alisema Higgno akimzuia mschana huyu na kisha yeye akaanza tena kuondoa moto jikoni kwa maana ya kuupunguza, ilimradi alikuwa busy.
Ni kama Soraya aligundua kuwa Higgno yupo busy kwasababu yake, akamtazama kwa sekunde kadhaa, “Higgno huogopi kukaa peke yako” aliuliza Soraya kwa sauti yake nyororo iliyoambatana na kijicheko fulani huku akimtazama Higgno “mbona hakutishi, kwani wewe unaogopa?” aliuliza Higgno huku akiwa busy na kugeuza samaki, “wala siogopi si nipo na wewe” alijibu Soraya na wote wakacheka kidogo, hapo kikapita kimya kingine cha sekunde kadhaa, ni kama Soraya alikuwa anatafuta swali jingine, “Higgno kwani hiyo nyama ya nini?” aliuliza Soraya huku akimtazama Higgno, “ngolombwe vipi unakulaga?” aliuliza Higgno huku akiendelea kugeuza samaki na pande ya nyama, “nilikula zamani sana aliletaga baba” alijibu Soraya ambae ni kama alianza kumzoea Higgno taratibu.
Kikapita kimya kingine Soraya akitafuta swali, maana alishaona akikaa kimya ingekula kwake, kwasababu Higgno sio mwongeaji, “kwani hawa samaki unawauzaga?” aliulizia Soraya huku akimtazama Higgno bila wasi wasi wowote, maana alishagundua kuwa kijana huyu asinge weza kumtazama usoni, “hapana hawa nawavua kwaajili ya kula unaweza kuonja mmoja ni watamu sana” alisema Higgno huku tayari mkononi mwake akiwa na samaki mmoja mkubwa sana aliekuwa anachuruzika mafuta kutokana na ule moto mkali, “ndiyo nitakula” alisema Soraya kwa sauti yake nyororo huku anasimama, “ngoja ni chukue sahani maana anamoto, “alisema Higgno akimrudisha samaki juu ya waya lakini pembeni kidogo na kuinuka akitaka kuingia ndani, “subiri kidogo” alisema Soraya na hapo Higgno akasimama kumtazama Soraya ambae alikuwa anafungua ile niqab na kuiondoa usoni mwake, akiacha sura wazi na kumpa Higgno wasaa mwingine wa kuitazama sura yenye kila sifa ya kuitwa nzuri, hapo Higgno aliduwaa mpaka alipokabidhiwa ile niqab mkononi, na kabla hajaondoka akamuona anatoa kitambaa cha kichwani yaani ushungi na kumpatia Higgno, ambae baada ya kupokea akataka kuondoka maana alihisi anaweza kugundulika kuwa alizishangaa nywele ndefu za mschana yule zilizo vuka mabega na kumwagika mgongoni, “subiri na hili baibui maana nasikia joto” alisema Soraya huku anashika baibui lake jeusi na kuanza kulipandisha juu kwa lengo la kulivuwa, hapo Higgno akajihisi mwili unamsisimka maana hakujuwa mschana huyu akivua baibui atabakia na nguo gani ndani…… ITAENDELEA MUWE NA USIKU MWEMA
Hapa bila huyu mlimbwende kujiongeza, jamaa yangu alikua anaunguza mpaka kibanda maana sio kwa kuchochea huko. 🔥🔥🔥🔥😂🤣😂
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA AROBAINI NA TISA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA NANE: hapo Higgno aliduwaa mpaka alipo kabidhiwa ile niqab mkononi na kabla hajaondoka akamuona anatoa kitambaa cha kichwani yaani ushungi na kumpatia Higgno, ambae baada ya kupokea akataka kuondoka, maana alihisi anaweza kugundulika kuwa alizishangaa nywele ndefu za mschana yule alizo vuka mabega na kumwagika mgongoni, “subiri na hili baibui maana nasikia joto” alisema Soraya huku anashika baibui lake jeusi na kuanza kulipandisha juu kwa lengo la kulivuwa hapo Higgno akajihisi mwili una msisimka maana hakujuwa mschana huyu akivua baibui atabakia na nguo gani ndani ..…ENDELEA….
Higgno akajikuta akitazama pembeni mwenyewe bila kuambiwa, akikwepa kuona vitu ambavyo alihisi kuwa havimuhusu, huku ana sikiliza harufu nzuri ya marashi, “hii hapa” alisema Soraya na hapo Higgno akainua uso wake kumtazama Soraya akianzia miguuni na kupandisha juu, na macho yake yakapata nafasi ya kuona umbo zuri la mschana huyu ambae ni wazi kabisa kuwa ametokea kwenye familia ya kitajiri, uliokuwa ndani ya gauni jepesi sana, ambalo liliweza kuonyesha umbo mwanana la mschana huyu, “gauni langu la kulalia” alisema Soraya na hapo Higgno akashtuka kuwa Soraya amegunduwa kuwa alikuwa anamtazama, “nzur….. ni zuri sana” alisema Higgno huku anapokea lile baibui na kuingia nalo ndani, ambako alilitundika kwenye msumari mmoja kati ya minne ambayo hutumia kutundikia nguo na kufanya mule ndani mutawaliwe na harufu ya marashi na vile vitu vingne aliviweka mezani karibu na ule mkoba wa Soraya, akachukua sahani na kuanza kutoka nje pasipo kujua kuwa tayari sehemu zake za siri yaani dudu ilisha ingia kwenye matamanio na tayari ilisha jitutumua na kuanza kusimama kuiinua bukta yake ambayo sasa ilituna kwa mbele, maana Soraya hakuwa wa kawaida.******
Mzee Mahamud na mke wake ni kama walikosa amani juu safari ya ghafla ya Soraya kwenda kulala kwa Laylah, “lakini Soraya amesha kuwa mkubwa tena bahati nzuri anajitambua, tuache kumchukulia kama mtoto mdogo, akiolewa tutapata shida sana” alisema mama Soraya na hapo mume wake akavuta pumzi ndefu na kuishusha kama alivyo ivuta, “ni kweli mke wangu, tumezoea kuwalea hawa watoto utadhani ni wachanga, wakati wameshakuwa wakubwa kabisa na wao wana mambo yao ya kufanya na kujifunza katika maisha” alisema Mahamud akiwa na mke wake wamejilaza kitandani, “unamzungumzia mtoto gani mwingine?” aliuliza mama Soraya ambae alikuwa amejilaz kifuani kwa mume wake, akipitisha pitisha mkono wake kwenye kifua cha mume wake kilicho jaa vinyoleo, “si Talib, huyu ni sawa na kijana wetu tumemlea toka akiwa mdogo na sasa amekuwa mkubwa” alisema mzee Mahamud, huku akipitisha kiganja cha mkono wake kwenye nywele za mke wake eneo la kisogoni karibu na shingo, “mh! Talib usimzungumzie kabisa, yeye alisha jikomalia kabisa hana chochote cha kujifunza, si unakumbuka aliletewa mtoto” alisema mama Soraya, huku sauti yake ikianza kulegea na kuwa ya kivivu huku anapeleka mkono wake kwenye usawa wa dudu ya mume wake ambayo ilishaanza kuchachamaa ikihitaji ile kitu ya kuingiza, “lakini amesha jirekebisha, si umeona ameweza kusimaia biashara yake kwa mwaka mzima, hapa nafikiria kumuingiza rasmi kwenye kampuni anisaidie majukumu, maana Soraya atakuwa busy na kampuni yake” alisema Mahamud kwa sauti ambayo sasa ilianza kuwa nzito huku anaamisha mkonobwake toka kichwani kwenda kifuani kwa mke wake na kulikamata nyonyo akianza kuchezea chuchu, huku mke wake akianza kuichezea dudu.******
Talib akiwa na uhakika kuwa yupo makini, kichwa kimejaa kilevi cha bangi aliyoivuta kwa lengo la kumpa nguvu na kusimamia mpango wake wa kwenda kumkomesha Higgno kwa kumchoma ndani ya nyumba aliyokuwa anaishi kwa kutumia mafuta ya petrol aliyo ya beba kwenye dumu la lita tano, aliingia ndani ya ile bar wanayouza pombe za kienyeji, kwa lengo la kwenda kupata ulanzi , aliingia ndani ya ile bar wanayouza pombe za kienyeji, kwa lengo la kwenda kupata ulanzi, pombe ambayo ilikuwa inapatikana kwa wingi eneo lile la Luhila seko.
Talib akiwa anaamini kuwa hakuna mtu aliemuona na kumfahamu, aliingia ndani ya kile kilabu ambacho hutegemea mwanga wa taa ya kandiri huku wakitumia betri la gari kuliza music kwa sauti kubwa toka kwenye redio casset ya duble deck, akaenda kukaa kwenye bench moja la pembeni kabisa ambapo palikuwa na giza giza fulani ambalo ndilo alilolifuata akakaa na kuagiza kopo kubwa la ulanzi, wenyewe wanaita dumla, yani lile kopo la sadolin lenye ujazo wa lita tano akilipia shilingi mia tano, na wakati anasubiri akatoa simu yake na kutazama muda, ilikuwa ni saa tatu na robo, “mpaka namaliza itakuwa ni saa nne” alijisemea Talib, huku akiiweka simu yake mfukoni na kulikamata dumu lake la lita tano lililojaa petrol akalisokomeza chini ya benchi alilo kalia, “niambie mwenzangu ndo nini kunifanyia vile mwenzio” Talib alishtushwa na sauti ya kike ambayo aliitambua mara moja kuwa ni sauti ya Hilda, ambae alikuwa anakaa pembeni ya mpenzi wake huyu ambae haishi kumfanyia vituko kila kukicha, haraka sana Talib akachekecha akili, kwanza alifikiri kuwa endapo angekaa na Hilda mpaka mwisho mpango wake ungevulugika, lakini hapo hapo Talib akapata wazo jingine ni wazo la kumtumia Hilda kufanikisha mpango wake, maana alisha ujuwa udhaifu wa Hilda juu yake, ni kuhitaji ndoa kwa kutegemea kuwa atapata maisha mazuri, “tulia kwanza ndugu yangu, unajuwa damu zetu zinaendana kinoma” alisema Talib, huku akimtazama Hilda kwa macho legevu na tabasamu la kivivu kama ilivyo sauti yake ya kilevi, “nitulie nini bwana, mwenzio ukaniacha hata bila nauli” alisema Hilda kwa sauti ya kujidekeza huku akimtazama mwanamke aliekuwa anakuja na lile dumla lillilo jaa ulanzi, “kikapita kimya kidogo wakati yule dada mhudumu akiweka Ulanzi mezani, “tatizo lako una haraka sana Hilda, we nisikilize kilicho tokea siku ile” alisema Talib,mara baada ya yule mdada kuondoka, kisha akainua dumla na kulisogeza mdomoni akalipiga mafunda mawili ya mkupuo, kisha akampatia Hilda, “haya nidanganye sasa” alisema Hilda huku anapokea dumla na kufanya kama alivyo fanya Talib na kuliweka mezani, “siku ile nilipigiwa simu naitwa na anko, yaani muda ule umefika pale nyumbani sisi tulikuwa ofisini tuna panga mipango ya kiofisi ndio maana mlinzi alikuzuia” alisema Talib na kuchukuwa tena dumla na kugida ulanzi na kumpatia Hilda, kisha akaendelea kuongea, “sasa baada ya hapo nikasema nifanye mpango mmoja wa ukweli, ili nikifanikiwa ninunue nyumba kubwa na gari jipya ili tukaishi na mtoto wetu, sasa huyu mwanaume wako ndiyo akatibua mpango mzima, yaani ilikuwa nipige hela ndefu kishenzi” alisema Talib, na Hilda ambae alisha maliza kunywa Ulanzi na kuweka dumla mezani, “huyu huyu Higgno, mbona mshenzi sana huyu nuksi” alisema Hilda kwa sauti iliyojaa chuki, “yaani Hilda nasemaje, hapa nikuwa nakunywa kidogo ili nije nikutafute ili tukamkomeshe, maana bila hivyo anaweza kuniharibia mpango wangu mwingine” alisema Talib kwa sauti ya chini, “mpango gani huo?” aliuliza Hilda kwa sauti ya chini pia.
Hapo ndipo Talib alipokuwa anapataka, kwanza aliinua dumla la ulanzi na kulisogeza mdomoni mwake, kisha akagugumia ulanzi na kumpatia Hilda ambae pia alimsubiri aunywe kwanza kisha akaanza kueleza mpango wake kwa sauti ya chini, “sasa hapo umemkosa, kwasababu Higgy sasa hivi hakai huku Luhuila” alisema Hilda kwa sauti ya chini na kumshtua kidogo Talib, ambae pia alikumbuka maneno ya baba yake Higgno, kwamba Higgno hayupo pale nyumbani, “dah! sasa tutafayaje?, maana nilitaka nikamtie moto mshenzi yule” alisema Talib kwa sauti ya kuchoka, “yaani ingekuwa vizuri sana, mwenzio simpendi” alisema Hilda huku wakiendelea kunywa pombe yao.
Naam baada ya kujadili cha kufanya Hilda akatoa wazo, “twende tukachome duka lao, maana wanajidai na lile duka, eti wanajifanya ndio matajiri” alisema Hilda kwa sauti ya kunong’ona, “hapo umesema, nadhani yule fala akiona hivyo hatorudia tena” alisema Talib, “tena wanakijiji watafurahi sana, pengine yule mzee ataruka kichaa” alisema Hilda kwa furaha na hapo wakaendelea kupanga mipango yao huku wakinywa ulanzi wao wakisubiri muda waende kwenye tukio.******
Huko nje Soraya nae alipomuona Higgno ameingia ndani, akamsindikiza kwa macho huku anajitabasamulia, “na yeye atakuwa ananipenda, si alimuambia Laylah, kuwa mimi ni mzuri, halafu ana nitazama sana” alijiwazia Soraya huku anatazama ndani ya kibanda ambako kulikuwa na giza, hivyo hakuweza kuona chochote, “mwenyewe anajikalia peke yake halafu pametulia mpaka raha” aliwaza Soraya, hakika ungeshangaa kwanini anawaza kitu kama hiki, kwasababu yeye anakaa sehemu nzuri sana ambayo kila mtu hutamani kuishi sehemu kama hiyo, leo anasema anapoishi Higgno ndiyo pazuri, “mh! leo nimemuona Kijana mpole” aliwaza Soraya bila kuwa na wasi wasi wowote, kifupi alijiona yupo salama, sijui wakati wa kulala atataka kunifanya?” aliwaza Soraya huku anatabasamu na kupeleka macho yake mlangoni, baada ya kusikia vishindo vyepesi vya miguu ya Higgno vikija nje, macho yake yakatua moja kwa moja kwenye usawa wa kaptulah ya Higgno, ambayo ilikuwa imeinuliwa na dudu ungesema ameficha kitu fulani.
Naam Soraya alijikuta anasisimkwa na mwili, huku vitu kama shoti za umeme zikitambaa mwilini kushuka chini na kuishia mapajani zikisambaa mpaka kwenye kitumbua chake, kitu ambacho akikuwahi kumtokea mwanzo, hapo akajikuta anakwepesha macho kwa kuyapandisha kwenye sahani ya plastic aliyoibeba Higgno, “samahani vyombo vye nyewe sio vizuri kama vya huko kwenu” alisema Higgno, kwa sauti yake ya upole, huku anasogea pale kwenye jiko na kutoa yule samaki aliekuwa amewekwa pembeni anavuja mafuta nakumuweka kwenye sahani, “mbona hata sisi tunatumia sahani kama hizi” alisema Soraya huku anapokea sahani yenye samaki toka kwa Higgno. ambae alijua fika kuwa yule mschana alieitwa Soraya anamdanganya na hakujua kwanini ana mdanganya.
Kikapita kimya kifupi huku Soraya akiendelea kula samaki kwa utulivu na umakini wakuhofia miba, huku wote wawili wakijaribu kutazamana kwa kuibia, wakati Higgno akiitazama sura nzuri ya mschana huyu huku Soraya alikuwa akizama Kifua na sura ya kijana huyu, maana wakati mwingine walijikuta wakigonganisha macho yao, na kuishaia kuchekeana na kukwepesha macho kwa aibu, na baada ya kimya kirefu hata Soraya alipomaliza samaki japo hakummaliza wote kisha akasimama na ile sahani mkononi, “asante sana Higgno, samaki ni mtamu sana, nitakuwa nakuja kila siku nile samaki mmoja” alisema Soraya kwa sauti nzuri kama illvyo kawaida yake, lakini Higgno alishindwa kujibu, “nikaiweke wapi?” aliuliza Soraya, “hapana Soraya wacha tu! nitaipeleka mimi” alisema Higgno huku anainuka nakuichukua ile sahani mkono mwa Soraya, “lakini kwetu wanawake ndio wanafanya kazi kwa waume” alisema Soraya ambae alibakia amesimama akimtazama Higgno aliesogea pembeni ya kile kibanda chake akiwa na ile sahani, ambapo palikuwa na ndoo moja kubwa ya maji na kikombe ndani yake, “lakini wewe ni mgeni hupaswi kufanya kazi katika siku yako ya kwanza, labda ukishazoea na kuwa mwenyeji” alisema Higgno kwa sauti yake ya upole huku akianza kuiosha ile sahani, kusikia hivyo Soraya akatabasamu, “kwani Higgno unapenda niwe nakujaga” aliuliza Soraya, akiwa bado amesimama, “mh… mhh! siwezi kukuzuia kuja kunitembelea, lakini usiku ni hatari kwako” alijibu Higgno, huku anamaliza kuosha ile sahani na kuchota maji kwenye kikombe na kurudi pale aliposimama Soraya na kuanza kumnawisha mkono kwa kumnyunyizia maji mikononi, huku wote wakiwa kimya, Soraya kichwani mwake akiwa anatafakari jibu la Higgno ambalo lilikuwa na muelekeo wa kuwa kijana huyu hakutammbua nia yake, “kwanini unasema hivyo Higgno?” aliuliza Soraya mara baada ya kumaliza kunawa na kukaa tena kwenye kile kigoda, “kwasababu yule dereva wako akiharibikiwa na gari na kushindwa kukufuata unadhani utarudije nyumbani usiku huu, sina baiskeri huku porini?” aliuliza Higgno kwa sauti ya upole akionyesha wazi anamuonea huruma Soraya, “asipofika kunichukuwa si nitalala hapa hapa kwako” alijibu Soraya huku anacheka cheka, “hapana huwezi kulala huku” alisema Higgno, huku akiingia ndani kuweka kikombe na ile sahani.
Hapo Soraya akajuwa kuwa ni kweli kijana mpole hakujuwa yeye anawaza nini kichwani mwake, hivyo akamsubiri atoke tu! na alipotoka Soraya akamdaka, “eti! Higgno, nikuulize kitu?” aliuliza Soraya kwa sauti nyororo ya upole safari hii ikiwa imenyongea kidogo, “niulize nakujibu” alijibu Higgno kwa sauti yake ya upole huku anakaa juu ya ndoo pale alipokaa mwanzo, “kwani wewe una mwanamke mwingine?” aliuliza Soraya safari hii kwa sauti ya upole hapo Higgno akacheka kidogo, “mbona umeuliza kuwa na mwanamke mwingine, na kwanini huku niuliza kama nina mwanamke?, maana sina hata huyo mwanamke mmoja na sijawahi kuwa nae” aljibu Higgno na kucheka kidogo huku Soraya akicheka kidogo, “sasa kwanini unanizuia nilale hapa kwako au hunipendi” aliuliza Soraya, kwa sauti ya kulalamika, lalamiko lenyewe ni lile la kudeka, “lakini nina kitanda kimoja kidogo, tena sio kizuri…”kabla hajamalizia Soraya akadakia, “mbona hata sisi vitanda vyetu vidogo” alisema Soraya kwa sauti ile ile ya kulalamika na kuwa kama anaedeka fulani hivi na kumfanya Higgno ashangae kidogo, “sawa hakuna tatizo, siku ikitokea ukashindwa kurudi nitakuandalia vizuri sehemu ya kulala mimi nitajuwa nalalaje” alisema Higgno wa sauti fulani ya kumlaghai Soraya akiwa na mawazo kuwa Laylah anarudi kuja kumchukua na kwamba yale yalikuwa ni maongezi tu, maana ukiachilia hadhi ya mschana yule asinge weza kuacha nyumba kubwa huko kwao nakuja kulala sehemu kama ile, pia ingekuwa vigumu mschana mrembo ambae sio mpenzi wake kuamua kuja kulala kule usiku kama ule, “wewe si umesema hauna mwanake mwingine?” aliuliza Soraya, “ndio sina mwanamke”alijibu Higgno, ambae alikuwa anaendelea kushangaa aina ya maongezi ya Soraya, “sasa mbona unakataa kulala na mimi au unaogopa utani fanya nini?” aliuliza Soraya, ambae kiukweli kichwani mwake alikuwa anamchukulia Higgno kama vile tayari ni mpenzi wake kwa jinsi alivyo onyesha moyo wa upendo wa dhati toka miaka mingi iliyopita…….. ITAENDELEA


TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA HAMSINI
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA TISA: akiwa na mwazo kuwa Laylah anarudi kuja kumchukua na kwamba yale yalikuwa ni maongezi tu, maana ukiachilia hadhi ya mschana yule asingeweza kuacha nyumba kubwa huko kwao nakuja kulala sehemu kama ile, pia ingekuwa vigumu mschana mrembo ambae sio mpenzi wake kuamua kuja kulala kule usiku kama ule, “wewe si umesema hauna mwaname mwingine?” aliuliza Soraya, “ndio sina mwanamke”alijibu Higgno, ambae alikuwa anaendelea kushangaa aina ya maongezi ya Soraya, “sasa mbona unakataa kulala na mimi au unaogopa utanifanya nini?” aliuliza Soraya ambae kiukweli kichwani mwake alikuwa anamchukulia Higgno kama vile tayari ni mpenzi wake kwa jinsi alivyo onyesha moyo wa upendo wa dhati toka miaka mingi iliyopita ….. ENDELEA….
Sasa Higgno aliona wazi kuwa Soraya anamtania, kwa maana ya kuwa alikuwa anaongea ili kuvuta muda wa mwenzie kumfuata, baada ya kuja kumuona na kumuambia asante kwa yale aliyomfanyia, “kwani wanafanyaga bila kukubaliana kuwa wapenzi?” aliuliza Higgno kwa sauti yake ya upole huku akicheka cheka na Soraya nae akacheka kikike, kisha kikapita kimya kifupi, ni kama walikuwa wanatafakari waliyo yaongea mwanzo, kabla Soraya hajavunja ukimya huo, “kwahiyo huwa unalalaga hapa na mpenzi wako?” aliuliza Soraya kwa sauti tulivu huku anamtazama Higgno kwa macho ya tahadhari, ikionekana alikuwa analihofia jibu fulani akichelea kuumiza moyo wake endapo angelisikia toka kwa Higgno, japo swali lile aliliuliza yeye mwenyewe.
Kwanza akamuona Higgno akianza kwa kucheka kidogo, kicheko ni kile kile cha taratibu, “sijawahi kuwa na mwanamke, na nimekaa muda mrefu bila kuhitaji mwanamke” alisema Higgno na kumfanya Soraya atabasamu kidogo, “mmh! we muongo, bora hata useme kuwa ulikuwa nae lakini umesha achana nae” alisema Soraya kwa sauti ya uchangamfu, huku anamtazama Higgno, ambae licha ya kujisikia raha fulani kuongea na aina ya mwanamke ambae alikuwa anamuotea siku zote, “siwezi kusema nilikuwa nae ila alinifanya nishindwe kuwapenda ninao wapenda” alisema Higgno kwa sauti ya upole iliyoambatana na kijihuzuni fulani hivi, “sijakuelewa Higgno, huwezi kusema kama ulikuwa nae lakini alikufanya usiwapende uliowapenda kivipi, na wakina nani uliowapenda?” aliuliza Soraya kwa sauti fulani hivi ambayo ukiisikiliza vizuri unaweza kusema ilikuwa inaashiria kijiwivu fulani.
Hapo hata mimi sijui ni kwanini Higgno alivuta pumzi ndefu na kuishusha kwa ujumla wake, kisha akamtazama Soraya kwa macho yenye dalili ya huzuni, “Sijawahi kukaa na kumsimulia mtu yoyote zaidi ya wale wanaofahamu yaliyonikuta kama vile mama yangu baba yangu, majirani, marafiki, hata watu waliohusika kunifanya niwe hivyo” alisema Higgno kwa sauti yake ya upole, ambayo kiukweli sasa ilikuwa imezidi utulivu ikionyesha kuwa Higgno hakupenda kukumbuka habari zile zilizopita, sauti ambayo ilimvuta Soraya na kutamani kusikia simulizi ile ya Higgno ambayo ingeeleza kitu ambacho kingemfanya kijana huyu asiweze kuwa na mwanamke, “Higgno unaweza kunisimulia ilikuwaje” alisema Soraya kwa sauti tulivu na hapo Higgno akaanza kumsimulia Soraya juu ya urafiki wake na Hilda, toka kipindi kile wapo shule ya msingi hata walipoingia sekondari na kukubaliana kuwa wapenzi kwa makubaliano kuwa wakifika kidato cha pili waanze kwa kufanya mapenzi, “lakini akatokea mtu mmoja ambae tulikuwa tuna soma nae, ni mtoto wa tajiri, akamchukua yule mschana, niliwahi wakuta wakiwana fanya mapenzi kabisa” alieleza Higgno na kuendelea kusimulia kila kitu bila kutaja majina ya watu aliokuwa anawasimulia katika mkasa wake.********
Naam saa nne kamili, ndiyo muda ambao mzee Frank yaani baba yake Higgno, alifunga duka na kuingia ndani huku akiwa ametawaliwa na mawazo pungufu kuhusu mafanikio ya mwanae Higgno kule alikoenda kuomba kazi, “pengine amepata kazi na kuanza leo leo” alisema mama Higgno baada ya mume wake kuingia ndani na kumuona amejawa na mawazo, “lakini inawezekanaje apate kazi leo leo na kuanza hapo hapo?” aliuliza mzee Frank, kwa namna yakuto kuyaamini maneno ya mke wake, sasa unadhani ni kwanini hajapitia kutupa majibu ya huko?” aliuliza mke wake katika kuondoa shaka juu ya maneno aliyo yaongea, “hilo swali nimeshajiuliza toka saa kumi za jioni, lakini mpaka sasa sijapata jibu” alisema mzee Frank huku anavua nguo tayari kulala, “cha msingi tusubiri pakuche tuone kama atakuja au laa” alisema mama Higgno, huku pua zake zikianza kunusa harufu fulani ya vitu kuungua, “tatizo mama Higgno kuna jambo sijakueleza, ujue kuna kijana mmoja alikuja na kuapia vibaya sana juu ya Higgno, isije kuwa amemzuru huko mitaani wakati anarudi” alisema mzee Frank kwa sauti yenye mashaka, huku na yeye anainua pua yake kuvuta harufu ya kitu kilichokuwa kina ungua, “hivi kuna kitu ulisahau jikoni?” aliuliza mzee Frank, yaani baba yake Higgno, “moto nilishauzimisha, tena nilipikia jiko la nje” alisema mama Higgno yaani mke wa mzee Frank, “mh! sasa wewe husikii hiyoo harufu” alisema mzee Frank ambae alimaalizia kuvua nguo zake kisha akapanda kitandani, “mh! baba Higgy, hebu tazama dirishani” alisema mama Higgno kwa sauti ya juu ya kugofya huku ana tazama dirishani, na baba Higgno nae akatazama dirishani na kuona mwanga mkali ambao ulionyesha wazi kuwa ni mwanga uliosababishwa na miali yamoto, tena ni moto mkubwa, mh! lazima kutakuwa na mto huko…” baba Higgno hakuweza kumalizia kuongea, kabla hajasikia kelele toka nje, “motoooo! jamani motoooo! duka linawaka motoooo hukuuuuu!” kelele hizo ambazo zilitoka kwa watu wengi, ambazo kwa wenyeji wa mkoa huuu wanaita mlete, kama wengine wanavyoita nduru, au yowe la kuomba msaada.
Kama sio mama Higgno kumzuia mume wake kwa kumkamataka mkono pale mlangoni basi mzee frank ange toka nje na nguo ya ndani pekee, “vaa kwanza nguo mume wangu” alisema mama Higgno akiwa amemdaka mkono mume wake huku wakiendelea kusikia sauti na kelele za watu waliokuwa wana jaribu kuzima moto huko nje.*****
“Ndio nikaamua nije nikae huku shambani, sikuhitaji tena kukaa karibu na watu ambao siku zote wanafanya mambo yanayo nikomoa na kuniharibia mipango ya maisha yangu” alimaliza kusimulia Higgno, na hapo Soraya alishusha pumzi ndefu, “kwahiyo ulilala nae kitanda kimoja mwaka mzima bila kufanya nae kitu chochote?” aliuliza Soraya, akimtazama Higgno ambae alikuwa anaendelea kugeuza samaki juu ya jiko, “sikulala nae kitanda kimoja, nilikuwa na lala chini, kumpisha yeye na mtoto aliezaa na huyo mwanaume wake” alisema Higgno kwa sauti yake ya upole, “ok! lakini Higgno bado hujanitajia jina la huyo mtoto wa tajiri na huyo mschana” alisema Soraya, “huyo mschana anaitwa Hilda, na yule jamaa anaitwa Talib ni mtoto wa Tajiri mwarabu anaeitwa Mahamud yule mwenye mabus” alisema Higgno aliekuwa anaendelea kugeuza nyama na samaki, na hapo Soraya akashtuka kidogo na kumtazama Higgno aliekuwa busy na vitu vyake jikoni, “Talib, alisoma Luhuwiko, mtoto wa Mahamud?” aliuliza Soraya kwa sauti ya mshangao, “ndiyo ni mtoto wa Mahamud, nadhani anafahamiana na huyu rafiki yako aliekuleta” alisema Higgno, na hapo Soraya akagundua kuwa Higgno hakuwa anajuwa kuwa yeye ni mtoto wa Mahamud, “kwanini unasema hivyo?” aliuliza Soraya, huku wakati wote akimtazama Higgno aliekuwa tumbo wazi, “unajuwa kuna siku moja wakati natoka chuo cha ufundi pale mission nikamkuta mzee Mahamud anavamiwa na wezi, nikamsaidia halafu akataka kunipa hela, sikuona vyema kupokea hela kwaajili ya msaada nilioutoa, nikakataa na kumuomba aniajiri wakati nitakapo maliza chuo, sasa leo nimeenda kuomba kazi nikamuona huyu rafiki yako, nadhani alishaambiwa na Talib aninyime nafasi ya kuingia kwenye mahojiano na kusababisha nikose kazi” alisema Higgno, “pole sana, lakini nadhani utapata kazi tena nzuri kuliko ulivyotegemea” alisema Soraya, kisha kikapita kimya kifupi, ni Soraya ndie alievunja ukimya ule, “ulisema kuwa Hilda alikufanya ushindwe kuwa na uliowapenda, sasa mbona hujanitajia mschana ulie mpenda?” aliuliza Soraya huku akicheka cheka, na Soraya nae akacheka kidogo, “haaa! …… unataka kumjua?” aliuliza Higgno akiendelea kucheka cheka, “ndiyo niambie” alisema Soraya kwa sauti fulani ambayo ungeisikia ungesema watu hawa urafiki wao ulianzia siku nyingi, “zilikuwa ni ndoto za mchana, mara nilipo kuona kwa mara ya kwanza nilianza kukupenda lakini nilijua siwezi kuwa na wewe, ila nilitamani kuwa na mwanamke mzuri kama wewe” alisema Higgno kwa sauti fulani iliyoambatana na kicheko cha utani na Soraya nae akacheka kicheko cha raha, “kwanini ulidhania huwezi kuwa na mimi?” aliuliza Soraya huku akijichekea kimya kimya kwa kujua kuwa Higgno hakuwa anamtazama, Higgno alicheka kidogo, “mh! sikujua ningeanzaje kukueleza sikuwa na chochote cha kukupa, kama nilishindwa kumridhisha Hilda kwa kile anachohitaji ningewezaje kwako?” alisema Higgno huku akijichekesha kibwege.*****
Ndani ya nusu saa, tayari duka la mzee Frank, lilikuwa limesha ungua karibu lote na bado moto ulikuwa unaendelea kuwaka, huku watu wakijaribu kuuzima moto bila mafanikio na duka kuzudi kuteketea kwa kasi ya ajabu, mzee Frank, ambae alikuwa amesimama pembeni akilitazama duka lake likiteketea nikama alikuwa amechanganyikiwa, maana alisimama kama zezeta akijiuliza ni kitu gani kimesababisha moto, maana wakati anafunga duka muda mfupi kabla ya moto kuanza kuwaka lakini licha ya kujaribu kukumbuka sana hakuweza kukumbuka chochote ambacho amekiacha mule ndani na kingesababisha moto, “au ni yule kijana ambae alisema Higgno atamfanyia kitu kibaya” aliwaza mzee Frank huku mke wake akiwa anaangua kilio cha machungu kwa kuunguliwa na duka lao, na sasa watu waliokuwa upande wa barabarani kwenye vilabu vya pombe wakimiminika kuja upande wa duka lile ambalo sasa watu wengi walikuwa wamelizinguka kwa mbali wakihofia moto mkali ambao ulikuwa unaendelea kuwaka, kati ya watu waliokuwepo eneo lile ni mzee Komba na mke wake ambae hakujari kama bado uvunguni kwake kuna pwita pwita kwa kile alicho fanyiwa na mabudi, walijiunga na wanakijiji wenzao kushuhudia ajari ile ya moto huku vichwani mwao wakiamini kuwa ni kazi ya babu Mabudi, hakika nyoyo zao zilisuuzika, “kesho mtume Hilda kwa Mabudi akamueleze kilicho tokea, alisema mzee Komba pasipo kujuwa kinachoenda kumpata binti yake.
Kumbe basi, wakati moto mkali ukiendelea kuteketeza duka wakati huo huo, umbali wa mita mia mbili toka pale dukani kwenye njia panda ya shuleni, pembeni ya barabara mita kumi au kumi na mbili ndani ya kichaka Talib na Hilda walikuwa wanamalizia kupeana dudu, wakisherehekea ushindi kwa kile walichokifanya, walivaa nguo zao na kutoka kichakani kwa tahadhari na walipofika barabarani wakaanza safari kuelekea upande wa barabara kuu wakipishana na watu wengi waliokuwa wanaelekea kwenye ajali ya moto, na baada ya kupiga hatua kadhaa Talib akamgeukia Hilda, “sasa Hilda we ishia hapa mimi niwahi nikachukuwe usafiri niwahi home, ila usimuambie mtu yoyote kuhusu hii inshu” alisisitiza Talib, nimwambie mtu ili nikamatwe?” alisema Hilda, akimuhakikishia Talib kuwa atomuabia mtu yoyote.
Hivyo ndivyo walivyo agana Hilda na Talib, Hilda akarudi kwenye ajali ya moto na Talib akaongoza upande wa barabara kuu iendayo kusini mwa tanzania, yaani Lindi na Mtwara.*******
Naam muda ulikuwa umeenda sana, sio soraya pekee ambae alikuwa ameshashikwa na usingizi, hata Higgno pia alikuwa ameshikwa na usingizi, lakini alilazimika kubakia pale akisubiria mgeni wake aje achukuliwe, “Higgy mwenzio naona usingizi, nataka kulala” alisema Soraya kwa sauti ya kijidekeza, “hata mimi usingizi umenishika, nashangaa mwenzio anachelewa kukufuata” alisema Higgno na kumshangaza tena Soraya, ambae aliwaza amuambiaje, mara akamsikia akicheka kidogo, “japo sitamani uondoke, maana nimefurahi sana kwa ujio wako” alisema Higgno, na Soraya nae akacheka kidogo, “kwahiyo nikilala hapa utafurahi?” aliuliza Soraya, huku anacheka cheka kikike na kijisauti kilicho ambatana na aibu na Higgno pia akacheka, “nitajua unatania sifikirii mschana mzuri kama wewe kulala hapa” alisema Higgno akicheka cheka, “mbona hata kwetu tuna lala sehemu kama hii” alisema Soraya akidanganya kama ilivyo kawaida yake, Higgno alimtazama Soraya kwa mshangao, “kwa sekunde kadhaa, kabla haja sema, “ndiyo maana nasema kuwa unatania, unawezaje kuwa unalalaga sehemu kama hii” alisema Higgno, huku bado akimtazama Soraya aliekuwa anatabasamu, “wala sitanii, leo na lala hapa hapa” alisema Soraya huku akicheka cheka na kumfanya Higgno nae acheke cheke.*****
Mahamud na mke wake walisha maliza kupeana dudu na kuingia bafuni kuoga, na wakati wanajiandaa kulala ndipo Mahamud aliposikia geti dogo la chuma lililopo kwenye geti kubwa la pale langoni kwake likigongwa kwa mbali, akashangaa na kujiuliza atakuwa nani, hivyo akazima taa ya ndani, yaani chumbani kwake na kufungua panzia kisha akachungulia nje, wakati huo ulisikika mlio wa kwichi! kwichi! yaani komeo linafunguliwa, na alipochungulia vizuri upande wa geti la nyumba yake akamuona mlinzi anafunguwa geti dogo na kisha akaingia Talib, ni kama waliongea kwa sauti za chini chini, kisha Talib akaondoka kuelekea kwenye nyumba anayoishi kwa mwendo wa tahadhari, akaingia ndani na kufunga mlango, “mh! huyu anarudi saa hizi anatoka wapi usiku huu?” alijiuliza Mahamud, huku anasogea kwenye meza yake na kuchukuwa simu na kutazama muda, ilishatimia saa tano na nusu, “huyu mtu ana usalama kweli na safari zake za usiku?” alijiuliza Mahamud huku anavuta kumbu kumbu ya mwendo wa kunyatia aliokuwa anatembea mpwa wake huyu, wakati anaingia ndani.*******
Tayari muda ulikuwa umeshaenda sana, kila mmoja alitamani kulala lakini hakuna alieweza kumueleza mwenzie kuwa anaenda kulala, lakini baada ya kuvizia sana ndipo Soraya uvumulivu ukamshinda, “Higgno, muda umeenda twende tukalale” alisema Soraya kwa sauti fulani ya kijidekeza akimalizia na muhayo mfupi wa usingizi… ITAENDELEA
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA AROBAINI NA TISA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA NANE: hapo Higgno aliduwaa mpaka alipo kabidhiwa ile niqab mkononi na kabla hajaondoka akamuona anatoa kitambaa cha kichwani yaani ushungi na kumpatia Higgno, ambae baada ya kupokea akataka kuondoka, maana alihisi anaweza kugundulika kuwa alizishangaa nywele ndefu za mschana yule alizo vuka mabega na kumwagika mgongoni, “subiri na hili baibui maana nasikia joto” alisema Soraya huku anashika baibui lake jeusi na kuanza kulipandisha juu kwa lengo la kulivuwa hapo Higgno akajihisi mwili una msisimka maana hakujuwa mschana huyu akivua baibui atabakia na nguo gani ndani ..…ENDELEA….
Higgno akajikuta akitazama pembeni mwenyewe bila kuambiwa, akikwepa kuona vitu ambavyo alihisi kuwa havimuhusu, huku ana sikiliza harufu nzuri ya marashi, “hii hapa” alisema Soraya na hapo Higgno akainua uso wake kumtazama Soraya akianzia miguuni na kupandisha juu, na macho yake yakapata nafasi ya kuona umbo zuri la mschana huyu ambae ni wazi kabisa kuwa ametokea kwenye familia ya kitajiri, uliokuwa ndani ya gauni jepesi sana, ambalo liliweza kuonyesha umbo mwanana la mschana huyu, “gauni langu la kulalia” alisema Soraya na hapo Higgno akashtuka kuwa Soraya amegunduwa kuwa alikuwa anamtazama, “nzur….. ni zuri sana” alisema Higgno huku anapokea lile baibui na kuingia nalo ndani, ambako alilitundika kwenye msumari mmoja kati ya minne ambayo hutumia kutundikia nguo na kufanya mule ndani mutawaliwe na harufu ya marashi na vile vitu vingne aliviweka mezani karibu na ule mkoba wa Soraya, akachukua sahani na kuanza kutoka nje pasipo kujua kuwa tayari sehemu zake za siri yaani dudu ilisha ingia kwenye matamanio na tayari ilisha jitutumua na kuanza kusimama kuiinua bukta yake ambayo sasa ilituna kwa mbele, maana Soraya hakuwa wa kawaida.******
Mzee Mahamud na mke wake ni kama walikosa amani juu safari ya ghafla ya Soraya kwenda kulala kwa Laylah, “lakini Soraya amesha kuwa mkubwa tena bahati nzuri anajitambua, tuache kumchukulia kama mtoto mdogo, akiolewa tutapata shida sana” alisema mama Soraya na hapo mume wake akavuta pumzi ndefu na kuishusha kama alivyo ivuta, “ni kweli mke wangu, tumezoea kuwalea hawa watoto utadhani ni wachanga, wakati wameshakuwa wakubwa kabisa na wao wana mambo yao ya kufanya na kujifunza katika maisha” alisema Mahamud akiwa na mke wake wamejilaza kitandani, “unamzungumzia mtoto gani mwingine?” aliuliza mama Soraya ambae alikuwa amejilaz kifuani kwa mume wake, akipitisha pitisha mkono wake kwenye kifua cha mume wake kilicho jaa vinyoleo, “si Talib, huyu ni sawa na kijana wetu tumemlea toka akiwa mdogo na sasa amekuwa mkubwa” alisema mzee Mahamud, huku akipitisha kiganja cha mkono wake kwenye nywele za mke wake eneo la kisogoni karibu na shingo, “mh! Talib usimzungumzie kabisa, yeye alisha jikomalia kabisa hana chochote cha kujifunza, si unakumbuka aliletewa mtoto” alisema mama Soraya, huku sauti yake ikianza kulegea na kuwa ya kivivu huku anapeleka mkono wake kwenye usawa wa dudu ya mume wake ambayo ilishaanza kuchachamaa ikihitaji ile kitu ya kuingiza, “lakini amesha jirekebisha, si umeona ameweza kusimaia biashara yake kwa mwaka mzima, hapa nafikiria kumuingiza rasmi kwenye kampuni anisaidie majukumu, maana Soraya atakuwa busy na kampuni yake” alisema Mahamud kwa sauti ambayo sasa ilianza kuwa nzito huku anaamisha mkonobwake toka kichwani kwenda kifuani kwa mke wake na kulikamata nyonyo akianza kuchezea chuchu, huku mke wake akianza kuichezea dudu.******
Talib akiwa na uhakika kuwa yupo makini, kichwa kimejaa kilevi cha bangi aliyoivuta kwa lengo la kumpa nguvu na kusimamia mpango wake wa kwenda kumkomesha Higgno kwa kumchoma ndani ya nyumba aliyokuwa anaishi kwa kutumia mafuta ya petrol aliyo ya beba kwenye dumu la lita tano, aliingia ndani ya ile bar wanayouza pombe za kienyeji, kwa lengo la kwenda kupata ulanzi , aliingia ndani ya ile bar wanayouza pombe za kienyeji, kwa lengo la kwenda kupata ulanzi, pombe ambayo ilikuwa inapatikana kwa wingi eneo lile la Luhila seko.
Talib akiwa anaamini kuwa hakuna mtu aliemuona na kumfahamu, aliingia ndani ya kile kilabu ambacho hutegemea mwanga wa taa ya kandiri huku wakitumia betri la gari kuliza music kwa sauti kubwa toka kwenye redio casset ya duble deck, akaenda kukaa kwenye bench moja la pembeni kabisa ambapo palikuwa na giza giza fulani ambalo ndilo alilolifuata akakaa na kuagiza kopo kubwa la ulanzi, wenyewe wanaita dumla, yani lile kopo la sadolin lenye ujazo wa lita tano akilipia shilingi mia tano, na wakati anasubiri akatoa simu yake na kutazama muda, ilikuwa ni saa tatu na robo, “mpaka namaliza itakuwa ni saa nne” alijisemea Talib, huku akiiweka simu yake mfukoni na kulikamata dumu lake la lita tano lililojaa petrol akalisokomeza chini ya benchi alilo kalia, “niambie mwenzangu ndo nini kunifanyia vile mwenzio” Talib alishtushwa na sauti ya kike ambayo aliitambua mara moja kuwa ni sauti ya Hilda, ambae alikuwa anakaa pembeni ya mpenzi wake huyu ambae haishi kumfanyia vituko kila kukicha, haraka sana Talib akachekecha akili, kwanza alifikiri kuwa endapo angekaa na Hilda mpaka mwisho mpango wake ungevulugika, lakini hapo hapo Talib akapata wazo jingine ni wazo la kumtumia Hilda kufanikisha mpango wake, maana alisha ujuwa udhaifu wa Hilda juu yake, ni kuhitaji ndoa kwa kutegemea kuwa atapata maisha mazuri, “tulia kwanza ndugu yangu, unajuwa damu zetu zinaendana kinoma” alisema Talib, huku akimtazama Hilda kwa macho legevu na tabasamu la kivivu kama ilivyo sauti yake ya kilevi, “nitulie nini bwana, mwenzio ukaniacha hata bila nauli” alisema Hilda kwa sauti ya kujidekeza huku akimtazama mwanamke aliekuwa anakuja na lile dumla lillilo jaa ulanzi, “kikapita kimya kidogo wakati yule dada mhudumu akiweka Ulanzi mezani, “tatizo lako una haraka sana Hilda, we nisikilize kilicho tokea siku ile” alisema Talib,mara baada ya yule mdada kuondoka, kisha akainua dumla na kulisogeza mdomoni akalipiga mafunda mawili ya mkupuo, kisha akampatia Hilda, “haya nidanganye sasa” alisema Hilda huku anapokea dumla na kufanya kama alivyo fanya Talib na kuliweka mezani, “siku ile nilipigiwa simu naitwa na anko, yaani muda ule umefika pale nyumbani sisi tulikuwa ofisini tuna panga mipango ya kiofisi ndio maana mlinzi alikuzuia” alisema Talib na kuchukuwa tena dumla na kugida ulanzi na kumpatia Hilda, kisha akaendelea kuongea, “sasa baada ya hapo nikasema nifanye mpango mmoja wa ukweli, ili nikifanikiwa ninunue nyumba kubwa na gari jipya ili tukaishi na mtoto wetu, sasa huyu mwanaume wako ndiyo akatibua mpango mzima, yaani ilikuwa nipige hela ndefu kishenzi” alisema Talib, na Hilda ambae alisha maliza kunywa Ulanzi na kuweka dumla mezani, “huyu huyu Higgno, mbona mshenzi sana huyu nuksi” alisema Hilda kwa sauti iliyojaa chuki, “yaani Hilda nasemaje, hapa nikuwa nakunywa kidogo ili nije nikutafute ili tukamkomeshe, maana bila hivyo anaweza kuniharibia mpango wangu mwingine” alisema Talib kwa sauti ya chini, “mpango gani huo?” aliuliza Hilda kwa sauti ya chini pia.
Hapo ndipo Talib alipokuwa anapataka, kwanza aliinua dumla la ulanzi na kulisogeza mdomoni mwake, kisha akagugumia ulanzi na kumpatia Hilda ambae pia alimsubiri aunywe kwanza kisha akaanza kueleza mpango wake kwa sauti ya chini, “sasa hapo umemkosa, kwasababu Higgy sasa hivi hakai huku Luhuila” alisema Hilda kwa sauti ya chini na kumshtua kidogo Talib, ambae pia alikumbuka maneno ya baba yake Higgno, kwamba Higgno hayupo pale nyumbani, “dah! sasa tutafayaje?, maana nilitaka nikamtie moto mshenzi yule” alisema Talib kwa sauti ya kuchoka, “yaani ingekuwa vizuri sana, mwenzio simpendi” alisema Hilda huku wakiendelea kunywa pombe yao.
Naam baada ya kujadili cha kufanya Hilda akatoa wazo, “twende tukachome duka lao, maana wanajidai na lile duka, eti wanajifanya ndio matajiri” alisema Hilda kwa sauti ya kunong’ona, “hapo umesema, nadhani yule fala akiona hivyo hatorudia tena” alisema Talib, “tena wanakijiji watafurahi sana, pengine yule mzee ataruka kichaa” alisema Hilda kwa furaha na hapo wakaendelea kupanga mipango yao huku wakinywa ulanzi wao wakisubiri muda waende kwenye tukio.******
Huko nje Soraya nae alipomuona Higgno ameingia ndani, akamsindikiza kwa macho huku anajitabasamulia, “na yeye atakuwa ananipenda, si alimuambia Laylah, kuwa mimi ni mzuri, halafu ana nitazama sana” alijiwazia Soraya huku anatazama ndani ya kibanda ambako kulikuwa na giza, hivyo hakuweza kuona chochote, “mwenyewe anajikalia peke yake halafu pametulia mpaka raha” aliwaza Soraya, hakika ungeshangaa kwanini anawaza kitu kama hiki, kwasababu yeye anakaa sehemu nzuri sana ambayo kila mtu hutamani kuishi sehemu kama hiyo, leo anasema anapoishi Higgno ndiyo pazuri, “mh! leo nimemuona Kijana mpole” aliwaza Soraya bila kuwa na wasi wasi wowote, kifupi alijiona yupo salama, sijui wakati wa kulala atataka kunifanya?” aliwaza Soraya huku anatabasamu na kupeleka macho yake mlangoni, baada ya kusikia vishindo vyepesi vya miguu ya Higgno vikija nje, macho yake yakatua moja kwa moja kwenye usawa wa kaptulah ya Higgno, ambayo ilikuwa imeinuliwa na dudu ungesema ameficha kitu fulani.
Naam Soraya alijikuta anasisimkwa na mwili, huku vitu kama shoti za umeme zikitambaa mwilini kushuka chini na kuishia mapajani zikisambaa mpaka kwenye kitumbua chake, kitu ambacho akikuwahi kumtokea mwanzo, hapo akajikuta anakwepesha macho kwa kuyapandisha kwenye sahani ya plastic aliyoibeba Higgno, “samahani vyombo vye nyewe sio vizuri kama vya huko kwenu” alisema Higgno, kwa sauti yake ya upole, huku anasogea pale kwenye jiko na kutoa yule samaki aliekuwa amewekwa pembeni anavuja mafuta nakumuweka kwenye sahani, “mbona hata sisi tunatumia sahani kama hizi” alisema Soraya huku anapokea sahani yenye samaki toka kwa Higgno. ambae alijua fika kuwa yule mschana alieitwa Soraya anamdanganya na hakujua kwanini ana mdanganya.
Kikapita kimya kifupi huku Soraya akiendelea kula samaki kwa utulivu na umakini wakuhofia miba, huku wote wawili wakijaribu kutazamana kwa kuibia, wakati Higgno akiitazama sura nzuri ya mschana huyu huku Soraya alikuwa akizama Kifua na sura ya kijana huyu, maana wakati mwingine walijikuta wakigonganisha macho yao, na kuishaia kuchekeana na kukwepesha macho kwa aibu, na baada ya kimya kirefu hata Soraya alipomaliza samaki japo hakummaliza wote kisha akasimama na ile sahani mkononi, “asante sana Higgno, samaki ni mtamu sana, nitakuwa nakuja kila siku nile samaki mmoja” alisema Soraya kwa sauti nzuri kama illvyo kawaida yake, lakini Higgno alishindwa kujibu, “nikaiweke wapi?” aliuliza Soraya, “hapana Soraya wacha tu! nitaipeleka mimi” alisema Higgno huku anainuka nakuichukua ile sahani mkono mwa Soraya, “lakini kwetu wanawake ndio wanafanya kazi kwa waume” alisema Soraya ambae alibakia amesimama akimtazama Higgno aliesogea pembeni ya kile kibanda chake akiwa na ile sahani, ambapo palikuwa na ndoo moja kubwa ya maji na kikombe ndani yake, “lakini wewe ni mgeni hupaswi kufanya kazi katika siku yako ya kwanza, labda ukishazoea na kuwa mwenyeji” alisema Higgno kwa sauti yake ya upole huku akianza kuiosha ile sahani, kusikia hivyo Soraya akatabasamu, “kwani Higgno unapenda niwe nakujaga” aliuliza Soraya, akiwa bado amesimama, “mh… mhh! siwezi kukuzuia kuja kunitembelea, lakini usiku ni hatari kwako” alijibu Higgno, huku anamaliza kuosha ile sahani na kuchota maji kwenye kikombe na kurudi pale aliposimama Soraya na kuanza kumnawisha mkono kwa kumnyunyizia maji mikononi, huku wote wakiwa kimya, Soraya kichwani mwake akiwa anatafakari jibu la Higgno ambalo lilikuwa na muelekeo wa kuwa kijana huyu hakutammbua nia yake, “kwanini unasema hivyo Higgno?” aliuliza Soraya mara baada ya kumaliza kunawa na kukaa tena kwenye kile kigoda, “kwasababu yule dereva wako akiharibikiwa na gari na kushindwa kukufuata unadhani utarudije nyumbani usiku huu, sina baiskeri huku porini?” aliuliza Higgno kwa sauti ya upole akionyesha wazi anamuonea huruma Soraya, “asipofika kunichukuwa si nitalala hapa hapa kwako” alijibu Soraya huku anacheka cheka, “hapana huwezi kulala huku” alisema Higgno, huku akiingia ndani kuweka kikombe na ile sahani.
Hapo Soraya akajuwa kuwa ni kweli kijana mpole hakujuwa yeye anawaza nini kichwani mwake, hivyo akamsubiri atoke tu! na alipotoka Soraya akamdaka, “eti! Higgno, nikuulize kitu?” aliuliza Soraya kwa sauti nyororo ya upole safari hii ikiwa imenyongea kidogo, “niulize nakujibu” alijibu Higgno kwa sauti yake ya upole huku anakaa juu ya ndoo pale alipokaa mwanzo, “kwani wewe una mwanamke mwingine?” aliuliza Soraya safari hii kwa sauti ya upole hapo Higgno akacheka kidogo, “mbona umeuliza kuwa na mwanamke mwingine, na kwanini huku niuliza kama nina mwanamke?, maana sina hata huyo mwanamke mmoja na sijawahi kuwa nae” aljibu Higgno na kucheka kidogo huku Soraya akicheka kidogo, “sasa kwanini unanizuia nilale hapa kwako au hunipendi” aliuliza Soraya, kwa sauti ya kulalamika, lalamiko lenyewe ni lile la kudeka, “lakini nina kitanda kimoja kidogo, tena sio kizuri…”kabla hajamalizia Soraya akadakia, “mbona hata sisi vitanda vyetu vidogo” alisema Soraya kwa sauti ile ile ya kulalamika na kuwa kama anaedeka fulani hivi na kumfanya Higgno ashangae kidogo, “sawa hakuna tatizo, siku ikitokea ukashindwa kurudi nitakuandalia vizuri sehemu ya kulala mimi nitajuwa nalalaje” alisema Higgno wa sauti fulani ya kumlaghai Soraya akiwa na mawazo kuwa Laylah anarudi kuja kumchukua na kwamba yale yalikuwa ni maongezi tu, maana ukiachilia hadhi ya mschana yule asinge weza kuacha nyumba kubwa huko kwao nakuja kulala sehemu kama ile, pia ingekuwa vigumu mschana mrembo ambae sio mpenzi wake kuamua kuja kulala kule usiku kama ule, “wewe si umesema hauna mwanake mwingine?” aliuliza Soraya, “ndio sina mwanamke”alijibu Higgno, ambae alikuwa anaendelea kushangaa aina ya maongezi ya Soraya, “sasa mbona unakataa kulala na mimi au unaogopa utani fanya nini?” aliuliza Soraya, ambae kiukweli kichwani mwake alikuwa anamchukulia Higgno kama vile tayari ni mpenzi wake kwa jinsi alivyo onyesha moyo wa upendo wa dhati toka miaka mingi iliyopita…….. ITAENDELEA


TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA HAMSINI
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA TISA: akiwa na mwazo kuwa Laylah anarudi kuja kumchukua na kwamba yale yalikuwa ni maongezi tu, maana ukiachilia hadhi ya mschana yule asingeweza kuacha nyumba kubwa huko kwao nakuja kulala sehemu kama ile, pia ingekuwa vigumu mschana mrembo ambae sio mpenzi wake kuamua kuja kulala kule usiku kama ule, “wewe si umesema hauna mwaname mwingine?” aliuliza Soraya, “ndio sina mwanamke”alijibu Higgno, ambae alikuwa anaendelea kushangaa aina ya maongezi ya Soraya, “sasa mbona unakataa kulala na mimi au unaogopa utanifanya nini?” aliuliza Soraya ambae kiukweli kichwani mwake alikuwa anamchukulia Higgno kama vile tayari ni mpenzi wake kwa jinsi alivyo onyesha moyo wa upendo wa dhati toka miaka mingi iliyopita ….. ENDELEA….
Sasa Higgno aliona wazi kuwa Soraya anamtania, kwa maana ya kuwa alikuwa anaongea ili kuvuta muda wa mwenzie kumfuata, baada ya kuja kumuona na kumuambia asante kwa yale aliyomfanyia, “kwani wanafanyaga bila kukubaliana kuwa wapenzi?” aliuliza Higgno kwa sauti yake ya upole huku akicheka cheka na Soraya nae akacheka kikike, kisha kikapita kimya kifupi, ni kama walikuwa wanatafakari waliyo yaongea mwanzo, kabla Soraya hajavunja ukimya huo, “kwahiyo huwa unalalaga hapa na mpenzi wako?” aliuliza Soraya kwa sauti tulivu huku anamtazama Higgno kwa macho ya tahadhari, ikionekana alikuwa analihofia jibu fulani akichelea kuumiza moyo wake endapo angelisikia toka kwa Higgno, japo swali lile aliliuliza yeye mwenyewe.
Kwanza akamuona Higgno akianza kwa kucheka kidogo, kicheko ni kile kile cha taratibu, “sijawahi kuwa na mwanamke, na nimekaa muda mrefu bila kuhitaji mwanamke” alisema Higgno na kumfanya Soraya atabasamu kidogo, “mmh! we muongo, bora hata useme kuwa ulikuwa nae lakini umesha achana nae” alisema Soraya kwa sauti ya uchangamfu, huku anamtazama Higgno, ambae licha ya kujisikia raha fulani kuongea na aina ya mwanamke ambae alikuwa anamuotea siku zote, “siwezi kusema nilikuwa nae ila alinifanya nishindwe kuwapenda ninao wapenda” alisema Higgno kwa sauti ya upole iliyoambatana na kijihuzuni fulani hivi, “sijakuelewa Higgno, huwezi kusema kama ulikuwa nae lakini alikufanya usiwapende uliowapenda kivipi, na wakina nani uliowapenda?” aliuliza Soraya kwa sauti fulani hivi ambayo ukiisikiliza vizuri unaweza kusema ilikuwa inaashiria kijiwivu fulani.
Hapo hata mimi sijui ni kwanini Higgno alivuta pumzi ndefu na kuishusha kwa ujumla wake, kisha akamtazama Soraya kwa macho yenye dalili ya huzuni, “Sijawahi kukaa na kumsimulia mtu yoyote zaidi ya wale wanaofahamu yaliyonikuta kama vile mama yangu baba yangu, majirani, marafiki, hata watu waliohusika kunifanya niwe hivyo” alisema Higgno kwa sauti yake ya upole, ambayo kiukweli sasa ilikuwa imezidi utulivu ikionyesha kuwa Higgno hakupenda kukumbuka habari zile zilizopita, sauti ambayo ilimvuta Soraya na kutamani kusikia simulizi ile ya Higgno ambayo ingeeleza kitu ambacho kingemfanya kijana huyu asiweze kuwa na mwanamke, “Higgno unaweza kunisimulia ilikuwaje” alisema Soraya kwa sauti tulivu na hapo Higgno akaanza kumsimulia Soraya juu ya urafiki wake na Hilda, toka kipindi kile wapo shule ya msingi hata walipoingia sekondari na kukubaliana kuwa wapenzi kwa makubaliano kuwa wakifika kidato cha pili waanze kwa kufanya mapenzi, “lakini akatokea mtu mmoja ambae tulikuwa tuna soma nae, ni mtoto wa tajiri, akamchukua yule mschana, niliwahi wakuta wakiwana fanya mapenzi kabisa” alieleza Higgno na kuendelea kusimulia kila kitu bila kutaja majina ya watu aliokuwa anawasimulia katika mkasa wake.********
Naam saa nne kamili, ndiyo muda ambao mzee Frank yaani baba yake Higgno, alifunga duka na kuingia ndani huku akiwa ametawaliwa na mawazo pungufu kuhusu mafanikio ya mwanae Higgno kule alikoenda kuomba kazi, “pengine amepata kazi na kuanza leo leo” alisema mama Higgno baada ya mume wake kuingia ndani na kumuona amejawa na mawazo, “lakini inawezekanaje apate kazi leo leo na kuanza hapo hapo?” aliuliza mzee Frank, kwa namna yakuto kuyaamini maneno ya mke wake, sasa unadhani ni kwanini hajapitia kutupa majibu ya huko?” aliuliza mke wake katika kuondoa shaka juu ya maneno aliyo yaongea, “hilo swali nimeshajiuliza toka saa kumi za jioni, lakini mpaka sasa sijapata jibu” alisema mzee Frank huku anavua nguo tayari kulala, “cha msingi tusubiri pakuche tuone kama atakuja au laa” alisema mama Higgno, huku pua zake zikianza kunusa harufu fulani ya vitu kuungua, “tatizo mama Higgno kuna jambo sijakueleza, ujue kuna kijana mmoja alikuja na kuapia vibaya sana juu ya Higgno, isije kuwa amemzuru huko mitaani wakati anarudi” alisema mzee Frank kwa sauti yenye mashaka, huku na yeye anainua pua yake kuvuta harufu ya kitu kilichokuwa kina ungua, “hivi kuna kitu ulisahau jikoni?” aliuliza mzee Frank, yaani baba yake Higgno, “moto nilishauzimisha, tena nilipikia jiko la nje” alisema mama Higgno yaani mke wa mzee Frank, “mh! sasa wewe husikii hiyoo harufu” alisema mzee Frank ambae alimaalizia kuvua nguo zake kisha akapanda kitandani, “mh! baba Higgy, hebu tazama dirishani” alisema mama Higgno kwa sauti ya juu ya kugofya huku ana tazama dirishani, na baba Higgno nae akatazama dirishani na kuona mwanga mkali ambao ulionyesha wazi kuwa ni mwanga uliosababishwa na miali yamoto, tena ni moto mkubwa, mh! lazima kutakuwa na mto huko…” baba Higgno hakuweza kumalizia kuongea, kabla hajasikia kelele toka nje, “motoooo! jamani motoooo! duka linawaka motoooo hukuuuuu!” kelele hizo ambazo zilitoka kwa watu wengi, ambazo kwa wenyeji wa mkoa huuu wanaita mlete, kama wengine wanavyoita nduru, au yowe la kuomba msaada.
Kama sio mama Higgno kumzuia mume wake kwa kumkamataka mkono pale mlangoni basi mzee frank ange toka nje na nguo ya ndani pekee, “vaa kwanza nguo mume wangu” alisema mama Higgno akiwa amemdaka mkono mume wake huku wakiendelea kusikia sauti na kelele za watu waliokuwa wana jaribu kuzima moto huko nje.*****
“Ndio nikaamua nije nikae huku shambani, sikuhitaji tena kukaa karibu na watu ambao siku zote wanafanya mambo yanayo nikomoa na kuniharibia mipango ya maisha yangu” alimaliza kusimulia Higgno, na hapo Soraya alishusha pumzi ndefu, “kwahiyo ulilala nae kitanda kimoja mwaka mzima bila kufanya nae kitu chochote?” aliuliza Soraya, akimtazama Higgno ambae alikuwa anaendelea kugeuza samaki juu ya jiko, “sikulala nae kitanda kimoja, nilikuwa na lala chini, kumpisha yeye na mtoto aliezaa na huyo mwanaume wake” alisema Higgno kwa sauti yake ya upole, “ok! lakini Higgno bado hujanitajia jina la huyo mtoto wa tajiri na huyo mschana” alisema Soraya, “huyo mschana anaitwa Hilda, na yule jamaa anaitwa Talib ni mtoto wa Tajiri mwarabu anaeitwa Mahamud yule mwenye mabus” alisema Higgno aliekuwa anaendelea kugeuza nyama na samaki, na hapo Soraya akashtuka kidogo na kumtazama Higgno aliekuwa busy na vitu vyake jikoni, “Talib, alisoma Luhuwiko, mtoto wa Mahamud?” aliuliza Soraya kwa sauti ya mshangao, “ndiyo ni mtoto wa Mahamud, nadhani anafahamiana na huyu rafiki yako aliekuleta” alisema Higgno, na hapo Soraya akagundua kuwa Higgno hakuwa anajuwa kuwa yeye ni mtoto wa Mahamud, “kwanini unasema hivyo?” aliuliza Soraya, huku wakati wote akimtazama Higgno aliekuwa tumbo wazi, “unajuwa kuna siku moja wakati natoka chuo cha ufundi pale mission nikamkuta mzee Mahamud anavamiwa na wezi, nikamsaidia halafu akataka kunipa hela, sikuona vyema kupokea hela kwaajili ya msaada nilioutoa, nikakataa na kumuomba aniajiri wakati nitakapo maliza chuo, sasa leo nimeenda kuomba kazi nikamuona huyu rafiki yako, nadhani alishaambiwa na Talib aninyime nafasi ya kuingia kwenye mahojiano na kusababisha nikose kazi” alisema Higgno, “pole sana, lakini nadhani utapata kazi tena nzuri kuliko ulivyotegemea” alisema Soraya, kisha kikapita kimya kifupi, ni Soraya ndie alievunja ukimya ule, “ulisema kuwa Hilda alikufanya ushindwe kuwa na uliowapenda, sasa mbona hujanitajia mschana ulie mpenda?” aliuliza Soraya huku akicheka cheka, na Soraya nae akacheka kidogo, “haaa! …… unataka kumjua?” aliuliza Higgno akiendelea kucheka cheka, “ndiyo niambie” alisema Soraya kwa sauti fulani ambayo ungeisikia ungesema watu hawa urafiki wao ulianzia siku nyingi, “zilikuwa ni ndoto za mchana, mara nilipo kuona kwa mara ya kwanza nilianza kukupenda lakini nilijua siwezi kuwa na wewe, ila nilitamani kuwa na mwanamke mzuri kama wewe” alisema Higgno kwa sauti fulani iliyoambatana na kicheko cha utani na Soraya nae akacheka kicheko cha raha, “kwanini ulidhania huwezi kuwa na mimi?” aliuliza Soraya huku akijichekea kimya kimya kwa kujua kuwa Higgno hakuwa anamtazama, Higgno alicheka kidogo, “mh! sikujua ningeanzaje kukueleza sikuwa na chochote cha kukupa, kama nilishindwa kumridhisha Hilda kwa kile anachohitaji ningewezaje kwako?” alisema Higgno huku akijichekesha kibwege.*****
Ndani ya nusu saa, tayari duka la mzee Frank, lilikuwa limesha ungua karibu lote na bado moto ulikuwa unaendelea kuwaka, huku watu wakijaribu kuuzima moto bila mafanikio na duka kuzudi kuteketea kwa kasi ya ajabu, mzee Frank, ambae alikuwa amesimama pembeni akilitazama duka lake likiteketea nikama alikuwa amechanganyikiwa, maana alisimama kama zezeta akijiuliza ni kitu gani kimesababisha moto, maana wakati anafunga duka muda mfupi kabla ya moto kuanza kuwaka lakini licha ya kujaribu kukumbuka sana hakuweza kukumbuka chochote ambacho amekiacha mule ndani na kingesababisha moto, “au ni yule kijana ambae alisema Higgno atamfanyia kitu kibaya” aliwaza mzee Frank huku mke wake akiwa anaangua kilio cha machungu kwa kuunguliwa na duka lao, na sasa watu waliokuwa upande wa barabarani kwenye vilabu vya pombe wakimiminika kuja upande wa duka lile ambalo sasa watu wengi walikuwa wamelizinguka kwa mbali wakihofia moto mkali ambao ulikuwa unaendelea kuwaka, kati ya watu waliokuwepo eneo lile ni mzee Komba na mke wake ambae hakujari kama bado uvunguni kwake kuna pwita pwita kwa kile alicho fanyiwa na mabudi, walijiunga na wanakijiji wenzao kushuhudia ajari ile ya moto huku vichwani mwao wakiamini kuwa ni kazi ya babu Mabudi, hakika nyoyo zao zilisuuzika, “kesho mtume Hilda kwa Mabudi akamueleze kilicho tokea, alisema mzee Komba pasipo kujuwa kinachoenda kumpata binti yake.
Kumbe basi, wakati moto mkali ukiendelea kuteketeza duka wakati huo huo, umbali wa mita mia mbili toka pale dukani kwenye njia panda ya shuleni, pembeni ya barabara mita kumi au kumi na mbili ndani ya kichaka Talib na Hilda walikuwa wanamalizia kupeana dudu, wakisherehekea ushindi kwa kile walichokifanya, walivaa nguo zao na kutoka kichakani kwa tahadhari na walipofika barabarani wakaanza safari kuelekea upande wa barabara kuu wakipishana na watu wengi waliokuwa wanaelekea kwenye ajali ya moto, na baada ya kupiga hatua kadhaa Talib akamgeukia Hilda, “sasa Hilda we ishia hapa mimi niwahi nikachukuwe usafiri niwahi home, ila usimuambie mtu yoyote kuhusu hii inshu” alisisitiza Talib, nimwambie mtu ili nikamatwe?” alisema Hilda, akimuhakikishia Talib kuwa atomuabia mtu yoyote.
Hivyo ndivyo walivyo agana Hilda na Talib, Hilda akarudi kwenye ajali ya moto na Talib akaongoza upande wa barabara kuu iendayo kusini mwa tanzania, yaani Lindi na Mtwara.*******
Naam muda ulikuwa umeenda sana, sio soraya pekee ambae alikuwa ameshashikwa na usingizi, hata Higgno pia alikuwa ameshikwa na usingizi, lakini alilazimika kubakia pale akisubiria mgeni wake aje achukuliwe, “Higgy mwenzio naona usingizi, nataka kulala” alisema Soraya kwa sauti ya kijidekeza, “hata mimi usingizi umenishika, nashangaa mwenzio anachelewa kukufuata” alisema Higgno na kumshangaza tena Soraya, ambae aliwaza amuambiaje, mara akamsikia akicheka kidogo, “japo sitamani uondoke, maana nimefurahi sana kwa ujio wako” alisema Higgno, na Soraya nae akacheka kidogo, “kwahiyo nikilala hapa utafurahi?” aliuliza Soraya, huku anacheka cheka kikike na kijisauti kilicho ambatana na aibu na Higgno pia akacheka, “nitajua unatania sifikirii mschana mzuri kama wewe kulala hapa” alisema Higgno akicheka cheka, “mbona hata kwetu tuna lala sehemu kama hii” alisema Soraya akidanganya kama ilivyo kawaida yake, Higgno alimtazama Soraya kwa mshangao, “kwa sekunde kadhaa, kabla haja sema, “ndiyo maana nasema kuwa unatania, unawezaje kuwa unalalaga sehemu kama hii” alisema Higgno, huku bado akimtazama Soraya aliekuwa anatabasamu, “wala sitanii, leo na lala hapa hapa” alisema Soraya huku akicheka cheka na kumfanya Higgno nae acheke cheke.*****
Mahamud na mke wake walisha maliza kupeana dudu na kuingia bafuni kuoga, na wakati wanajiandaa kulala ndipo Mahamud aliposikia geti dogo la chuma lililopo kwenye geti kubwa la pale langoni kwake likigongwa kwa mbali, akashangaa na kujiuliza atakuwa nani, hivyo akazima taa ya ndani, yaani chumbani kwake na kufungua panzia kisha akachungulia nje, wakati huo ulisikika mlio wa kwichi! kwichi! yaani komeo linafunguliwa, na alipochungulia vizuri upande wa geti la nyumba yake akamuona mlinzi anafunguwa geti dogo na kisha akaingia Talib, ni kama waliongea kwa sauti za chini chini, kisha Talib akaondoka kuelekea kwenye nyumba anayoishi kwa mwendo wa tahadhari, akaingia ndani na kufunga mlango, “mh! huyu anarudi saa hizi anatoka wapi usiku huu?” alijiuliza Mahamud, huku anasogea kwenye meza yake na kuchukuwa simu na kutazama muda, ilishatimia saa tano na nusu, “huyu mtu ana usalama kweli na safari zake za usiku?” alijiuliza Mahamud huku anavuta kumbu kumbu ya mwendo wa kunyatia aliokuwa anatembea mpwa wake huyu, wakati anaingia ndani.*******
Tayari muda ulikuwa umeshaenda sana, kila mmoja alitamani kulala lakini hakuna alieweza kumueleza mwenzie kuwa anaenda kulala, lakini baada ya kuvizia sana ndipo Soraya uvumulivu ukamshinda, “Higgno, muda umeenda twende tukalale” alisema Soraya kwa sauti fulani ya kijidekeza akimalizia na muhayo mfupi wa usingizi… ITAENDELEA
Litakufa jitu sehemu iliyofikia sio ya kukosa😂
 
Back
Top Bottom