SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA AROBAINI NA SITA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA TANO: “kwani baba yako unaishi nae huko shambani?” aliuliza Laylah, “hapana kule naishi mwenyewe” alijibu Higgno kwa sauti ya upole, hapo Laylah, akashusha pumzi ndefu huku anatazama chini, kisha akatulia kwa sekunde kadhaa na kuinua uso wake kumtazama Higgno, “sikia kaka yangu, jina lako lilitwa kwa bahati mbaya, lakini kiukweli hauna sifa za kuwa mwajiriwa wa kampuni hii, hivyo unaweza kwenda” alisema Laylah, huku anampatia Higgno bahasha yake, kisha akaingia pamoja na mlinzi na kufunga, huku Higgno akikosa nafasi ya kukumbusha kuwa alikuwa ana ahadi na mwarabu Mahamud ……. ENDELEA….
“huyu mwanamke anadhani na mimi nilikuwa mwanafunzi wa songea boys au?” alijiuliza Higgno kwa mshangao, akishindwa kuelewa alichofanyiwa na huyu mwanamke Dereva wa mschana mwarabu, halafu anafanya nini kwa huyu mzee, ina maana aliachaga kazi kwa yule maschana?” alijiuliza tena Higgno ambae aliendelea kusimama pale nje ya gate kwa dakika kadhaa, huku akiwaza afanye nini, maana hakuamini kama kweli ndoto zake za kupata kazi, zimeishia hewani, alitamani kugonga gate ili aombe kuonana na mzee Mahamud mwenyewe pengine ange mkumbuka au hata kwa kumkumbusha ilimradi apate kazi na kutimiza malengo yake ikiwa ni kupata kazi nzuri ambayo itampatia maisha mazuri, ambayo yange msaidia kupata mwanamke mzuri wa kumfanya mke wake, “sidhani kama mzee Mahamud anaweza kuninyima kazi, ikiwa nitakutana nae uso kwa uso” aliwaza Higgno, huku anaanza kuondoka taratibu eneo lile, nitamtafuta yeye mwenyewe, nitamtafuta kwa muda wangu, nadhani huyu mwanamke ameniwazia vibaya ndio maana amenikosesha kazi” hivyo ndivyo Higgno alivyo waza na kupanga huku analekea kituo cha dala dala na kupanda dala dala kuelekea nyumbani kwao.******
Wakati huo mzee Frank alikuwa dukani kwake anasubiri muda ufike na kijana wake aje kutoka kwenye maomba ya kazi akiwa na habari njema za kuwa amepata kazi, lakini wakati anasubiria wateja wake ambao mida hii sio sana kuonekana dukani, huku anamuombea mwanae mafanikio, mara akamuona kijana mmoja amesimama mbele ya dirisha la duka lake, “karibu kijana” alisema mzee Frank huku anasimama toka kwenye kiti, “naomba sigara” alisema yule kijana bila hata salamu kama ilivyo kwa wateja wengine wanapo fika pale dukani huwa wanasalimia kisha kueleza wanacho hitaji, mzee Frank akatoa sigara aliyo hitaji yule kijana mgeni machoni mwake na kumpatia pamoja na kiberiti, kijana yule akapokea na kuwasha sigara kisha akavuta funda moja kwa mkupuo na kutoa moshi kwa mwingi, “Higgno yupo” aliuliza yule kijana ambae hakika mzee Frank hakuwa anamfahamu, Higgno ametoka hata hivyo siku hizi hakai hapa, anaishi mashambani huko Mahilo….” alisema mzee Frank, na kabla hajamaliza kuongea yule kijana akamdaka juu kwa juu, “weeee! usijaribu kumficha huyo fala, nitakuharibia sasa hivi” alisema yule kijana kwa sauti ambayo ilionyesha ukorofi wa wazi kabisa na kumfanya mzee Frank ashangae, “kijana unamaana gani kusema hivyo mbona sikuelewi?” aliuliza mzee Frank kwa sauti ya mshangao, “utanielewa ukisha muona mwanao amededi, si unajifanya hunielewi” alisema yule kijana, ambae mzee Frank hakuwa anamjua kabisa, “kijana kuwa mstaarabu kidogo, umekuja hapa unahitaji sigara, na kabla hujalipa unaleta fujo za kitoto au ndio….” alisema mzee Frank na kama ilivyo kuwa mwanzo, kijana yule akamkatiza, “sigara ndio nini we mzee, acha mambo ya kijinga, unajuwa huyo choko wako amenipotezea fedha ngapi, tena amevuruga mipango yangu kibao” alisema yule kijana kwa sauti iliyo ashiria ukosefu wa amani, “unasema Higgno amekupotezea fedha nyingi kivipi?” aliuliza Frank, kwa sauti ya mshangao, “we mwambie huyo fala ajiandae nitakuja baadae kumfanyia kitu mpaka ajute kuingilia mambo yasiyo muhusu, yeye si anajifanya anajuwa kupiga, sasa amejiponza mwenyewe” alisema yule kijana, kisha akaanza kuondoka bila kulipia ile sigara.*******
Higgno pasipo kujuwa kuwa alikuwa ametembelewa na mgeni nyumbani kwao alielekea moja kwa moja mpaka matogoro kanisani, ambako ndio mwisho wa daladala na kuanza kutembea kwa miguu kuelekea mahilo, yaani kule shambani kwao, ni mwendo wa kilomita sita hivi toka aliposhukia daladala, akitumia lisaa lizima kwa mguu, njia nzima akiwaza kilicho mtokea, ilikuwa ni vigumu sana kuamini kilicho tokea.
Ukweli Higgno alikuwa na asilimia nyingi sana za kupata kazi, lakini kilichotokea ni kitendo cha ajabu sana kwake, yaani ndoto zake zimezimwa ndani ya sekunde chache tu, “yule mwanamke sijui nimemkosea nini mpaka anifanyie vile, sasa nikimuambia boss wake si anaweza kumfokea” aliwaza Higgno ambae toka mida ile mawazo yalikuwa ni hayo tu hata alipofika nyumbani kwake kule shambani, na akubadili nguo kisha akaingia porini kuanza kukagua mitego yake, ambayo alikuwa ana siku mbili hajaikagua, bahati ilikuwa kwake, Higgno alikuta mitego imenasa mawindo mengi sana kuanzia ile ya Ngolombwe (mnyama waporini mwenye kimo cha chini kidogo ya mbuzi, au swala), kanga, hata sungura na samaki kule mtoni, hivyo akabeba wanyama wake aliowakuta wakiwa na uafadhali, maana wengine alikuta wameshaanza kuharibika kutoka na kukaa muda mrefu kwenye mtego.
Higgno alipofika nyumbani akaanza kuandaa nyama ya Ngolombwe kwa kumchuna na kukata nyama ambazo aliona zinafaa kubanikwa na nyepesi kuziandaa, huku akifukia utumbo, miguu na kichwa, lakini huwezi amini licha ya kuwa busy na kukausha nyama ya Ngolombwe na sungura kadhaa walipo patikana na samaki pia ambao walikuwa ni wengi sana, lakini bado mawazo juu ya kukosa kazi yalimsumbua muda wote alijiuliza maswali yasiyo na majibu kutwa nzima, hata mida ya saa moja akiwa anaendelea na kazi yake, aliendelea kuwaza juu ya mschana yule aliemkosesha nafasi za kazi.
Naam saa mbili na nusu giza likiwa limedhaifishwa na mwangaza wa mbala mwezi angavu, mara akaona mwangaza wa taa za gari zikija barabara ile ya vumbi ya kutokea mjini, na lilipofika usawa wa shamba lao akaona kama gari lile lina sua sua kama vile dereva wa gari lile hakuwa na uhakika na kule anakoenda, mara akaliona gari lile linakata kona kuingia shambani kwake, hapo Higgno akajua kuwa ni wale jamaa wa jana wamekuja kumvamia hivyo akajiandaa kwa lolote.
Msomaji kabla hatujaendelea na kilichomtokea Higgno usiku huu, hebu tuone kwanini Layalah, alimkosesha kazi Higgno.*********
Turudi saa mbili kasoro za asubuhi, Mahamud na binti yake Soraya ambae muda wote akiwa anawaza juu ya kijana mpole, wakiwa ndani ya Nissan patrol lilikuwa linaendeshwa na mschana Laylah waliingia eneo la ofisi za tajiri huyu Mahamud, waliweza kuona watu wengi sana waliokuja pale kwaajili ya maombi ya kazi, “watu wengi hawana ajira” alisema Mahamud aliekuwa amekaa seat ya mbele pembeni ya dereva wake, huku Soraya akiwa amekaa seat ya nyuma peke yake akiwaza juu ya kijana mpole, kijana wa kwanza kumpenda na kuwa tayari kwa lolote, “Soraya inabidi usimamie kampuni kwa umakini ili tueweze kuitanua kampuni yetu na kutoa ajira nyingi zaidi” alisema Mahamud huku anageuka kumtazama mwanae, ambae licha ya kujivika niqab usoni mwake lakini alionekana wazi kuwa amenyongea, “ndiyo baba” aliitikia Soraya kwa kifupi, Mahamud akajuwa bado binti yake hakuwa sawa, hivyo akapeleka macho mbele.
Lakini wakati anapeleka macho mbele ndipo alipo muona kijana ambae kamwe sura yake asingeisahau hata kwa bahati mbaya, “punguza mwendo Laylah” alisema Mahamud huku akitazama kule walikosimama watu wengi waliokuwa wanasubiri ajira, na Laylah akapunguza mwendo, huku wote wakitazama kule alikokuwa anatazama mzee Mahamud.
Naam hapo ndipo moyo wa Soraya ulipolipuka kwa mshangao na mshtuko mkubwa, ni baada ya kumuona kijana mpole akiwa katika kundi la watu wanao subiri kuajiriwa, “unamuona yule kijana alievaa suruali ya kitambaa na shati la kuchomekea” alisema mzee Mahamud kwa sauti ambayo ilionyesha kuwa na shahuku isiyo na kifani, “huyu hata kama jina lake halitasomwa lazima apewe ajira, huyu ndie alienisaidia siku ile nilipo vamiwa na wale majambazi kule Msamala” alisema Mahamud na hapo Laylah akamtazama Soraya, ambae pia alikuwa anamtazama Laylah, kwa macho ya mshangao lakini wa furaha, “hoo! baba huyu ndie yule ambae ulisema anafaa kunioa” aliuliza Soraya kwa sauti ya uchangamfu, ikiwa ni mara ya kwanza toka kumekucha hata mzee Mahamud alifurahi kwa uchangamfu wa Soraya, kwanza alicheka kidogo, “ni kweli nilisema lakini simaanisha kama nitakulazimisha” alisema Mahamud, huku Laylah anakanyaga mafuta kuingiza gari ndani ya geti.
Yap! waliposimama na kushuka toka kwenye gari, mzee mahamud akaingia ofisini na Soraya abaki anamkabidhi Layla majina ya watu waliochagulia kufanyiwa majaribio ya ajira, “Laylah, nadhani umemkumbuka yule kijana mpole” alisema Soraya kwa sauti ya chini iliyojaa kihoro, “tena nimeshangaa kusikia kuwa ndie aliemsaidia boss siku zile” alisema Laylah kwa sauti ya chini pia, lakini bado ikiwa na mshangao, “sasa hakikisha haingii humu ndani, muambie akupatie namba yake ya simu pia hakikisha kama kweli anaishi kule shambani Mahilo” alisema Soraya huku anampatia karatasi zenye majina ya watahiniwa………. ITAENDELEA
Kumbe ni amri agizo kutoka juu🤓 watu walishaanza kumkisia vibaya Laylah
 
Kumbe ni amri agizo kutoka juu🤓
C nilikwambia,
Hana shida huyo, yupo kazini na ukizingatia tokea mwanzo barua ya jamaa ilipita kwa bahati mbaya.

Harafu tuachane na hayo, "jamani natafuta make wa kuoa, sharti awe hajui kusoma"🤣😂🔥😂🔥😂
Kazi Haina kipengele, na Soraya ndio atajileta shamba na mkataba tunasainia hukohuko. 🤣😂😂😂
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA AROBAINI NA SABA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA SITA: Yap! waliposimama na kushuka toka kwenye gari mzee mahamud akaingia ofisini na Sorata akabaki ana mkabidhi Layla majina ya watu waliochagulia, kufanyiwa majaribio ya ajira, “Laylah, nadhani umemkumbuka yule kijana mpole” alisema Soraya kwa sauti ya chini iliyojaa kihoro, “tena nimeshangaa kusikia kuwa ndie aliemsaidia boss siku zile” alisema Laylah kwa sauti ya chini pia, lakini bado ikiwa na mshangao, “sasa hakikisha haingii humu ndani, muambie akupatie namba yake ya simu pia hakikisha kama kweli anaishi kule shambani Mahilo” alisema Soraya huku anampatia karatasi zenye majina ya watahiniwa …….. ENDELEA….
Hapo Laylah akashangaa sio kidogo, “we! Soraya, mwenzio si atakosa kazi na wakati baba amesema tuhakikishe anapata kazi?” aliuliza Laylah kwa sauti ya chini iliyojaa mshangao, “sitaki akutae na baba mpaka niongee nae mimi we fanya kama nilivyo kuambia” alisema Soraya kisha akaanza kuingia ndani akimuacha Laylah amesimama anamtazama kwa macho ya mshangao.
Soraya alipiga hatua kadhaa kisha akasimama na kugeuka nyuma akamuona Laylah amesimama anamtazama kama vile hakuelewa alichotakiwa kukifanya, hapo Sorya akarudi tena kwa Laylah, “usichoelewa nini Laylah?” aliuliza Soraya kwa sauti ya ile ile ya chini lakini iliyoonyesha kulalamika, “da’ Soraya, nayafikiria maisha ya yule kijana kwanini usimuache aingie halafu….” aliongea Laylah, lakini Soraya hakumuachia nafasi ya kumalizia akamadaka juu kwa juu, “Laylah, hii ndiyo nafasi yangu ya pekee ya kutimiza malengo yangu na ndoto yangu, ukikosea huyu kijana akaingia ndani hakika sito kusamehe hata kidogo” alisema Soraya kwa sauti kavu ambayo hata Laylah hakuwahi kuiskia hata siku moja, maana ilikuwa ya ukali na inayo maanisha, kisha akaondoka zake kuelekea ndani ya jengo la ofisi.
Soraya alimkuta baba yake akiwa pamoja na watu wengine watatu, ambao walikuwa na madaraka mbali mbali kwenye kampuni yao, yaani kama waajiriwa, huku kiti kimoja kikiwa kimebakia nae akakaa, “kama nilivyo waambia zingatieni majibu ya maswali mnayo uliza, si munajuwa kuna watu wanaleta janja janja, ameiba cheti cha ndugu yake anakifanya ni cha kwake ili apate kazi, akipata kazi unashangaa kama ni fundi anaharibikiwa na gari wanaanza kupiga piga simu tuwapelekee mafundi wengine wakawasaidie” alisema mze Mahamud kwa msisitizo, wakati wana wanasubiri watu waanze kuingia ili wawatahini, “hakuna shaka boss, tumejiandaa vizuri” walijibu wale watu watatu, huku muda wote Soraya akiwa kimya ametulia akiwaza juu ka kile alichomtuma Laylah, akiombea Laylah asije kufanya kitu tofauti.
Naam Laylah alirudi ndani na zile karatasi, akawaeleza kuwa tayari amesha waita walio hitajika na baada ya hapo akaelezwa kuwa aende akawaite mmoja baada ya mwingine waingie ndani” alisema Mahamud na Laylah akatoka nje, dakika chache baadae akaanza kungia ndani mtu mmoja baada ya mwingine, ambao walihojiwa na kuingia mwingine, huku wakichukuwa majina ya wale waliowakubali kwaajili ya kuingia kwenye awamu ya pili ambayo ingekuwa ni majaribio, ambapo ingefanyika siku mbili mbele.
Watu waliingia huku Soraya na baba yake wakimtazama kwa umakini kila alieingia wakiwa wanamtazamia mtu mmoja kwa mitazamo tofauti, wakati mzee Mahamud anatarajia kuona kijana aliemsaidia siku ile aliyovamiwa na vijana wawili waliokuwa na lengo la kumdhuru na kumpora fedha, huku Soraya alikuwa anaombea kijana huyo huyo asiingie mule ndani, maana hakutaka akutane na baba yake kabla hajakutana nae yeye.*********
Saa tano Talib alienda mwembe chai kwa Zido, na aliwakuta wakina Zido wakiwa pale nyumbani wanauguza majeraha yao waliyo yapata jana kule shambani kwa Soraya, “jamani hee mimi na mchongo, tusikae kuwaza juu ya yule fala” alisema Talib, huku ana sokota bangi, “Talib hebu achana na hizo mambo, unajuwa unapo mzungumzia yule dogo unamzungumzia mtu mwingine kabisa sio wa kipindi kile tupo shule” alisema Vitus ambae ni mmoja kati ya walioumia kidogo na kuwa na afadhari, “we ngoja uone nitakacho mfanyia usiku wa leo, nyie wenyewe mutajua kuwa mimi sio wa pole pole” alisema Talib kwa majisifu huku anawasha ile bangi yake na kuanza kuivuta, “Dah! Hebu achana na hiyo tupe mchongo mpya tuone kama unafaa” alisema Vitus, na hapo Talib akaanza kuelezea kuhusu fedha zilizopo kwenye kabati la ukutani la ofisini kwa baba mjomba wake, “sasa tutaingiaje mpaka ndani ya jumba lile mwanangu” aliuliza Zido kwa mara ya kwanza, “mutaingia mapema halafu mutajibanza chumbani kwangu, kwasasa nitahakikisha ninaiba funguo moja ya mlango wa nyuma wa nyumba kubwa, ambao tutaumia kuingilia na kiukweli mlango wa ofisi huwa haufungwi, hapo ni kazi kwenu kuchukuwa mkwanja na kutambaa zenu” alieleza Talib kwa namna ambayo ungesema ni kitu chepesi sana, “ni hivyo tu!?” aliuliza Vitus, kwa sauti ya mashaka, “kumbe je! unadhani kuna jipya basi, ni kama kumsukuma mlevi” alisema Talib huku akiendelea kuvuta bangi, “basi poa, wacha kwanza tukae sawa halafu tucheze na huo mkwanja” alisema Vitus, huku wenzake pia wakianza kupata matumaini mapya.**********
Naam kule kwenye masailiano ya ajira, Bahati iliangukia upande wa Soraya, maana wali wasaili wale watu walioomba kazi mpaka saa tisa za jioni, ambapo mtu wa mwisho aliingia pasipo kumuona Kijana mpole akiingia mule ndani, “unasema wameshaisha mbona yule kijana sijamuona?” aliuliza mzee Mahamud kwa mshangao, huku anamtazama Laylah aliekuja kutoa taarifa ya kuwa tayari watu wote walishaisha, “boss nadhani alipoona hajaitwa akaamua kuondoka” alisema Laylah huku akitazamaisha kichwa chini, “khaaaa! kwanini lakini, ilifaa umueleze mapema kuwa asiondoke” aliongea mzee Mahamud kwa sauti ya kulalamika, akionyesha wazi kuwa yule kijana kwake ni uhimu sana na hakutakiwa kukosa kazi, “baba wala hauhitaji kuwa na wasi wasi, madhari tumesha muona na kumfahamu basi tukimuona tena tutamueleza aje kukuona” alisema Soraya akionyesha kuwa mwenye furaha tofauti na alivyokuwa asubuhi.
Baada ya kuwa tangazia wale walioomba nafasi wakiwasoma majina wale waliopitishwa kwenye interview, Mzee Mahamud na binti yake wakaondoka pale ofisini huku Laylah akiendesha gari, muda wote Soraya alionyesha mwenye furaha isiyo na kifani, aliongea na kucheka kwa furaha hata wakiwa nyumbani pia alikuwa hivyo hivyo.
Masaa yalikatika huku Laylah, akionekana kusalia pale nyumbani kwa boss wake, na hata walipomaliza kuswali swala ya insha ndipo Mahamud aliposhangaa, “Laylah, hujachoka kwa kazi tuliyoifanya kutwa nzima, ni vyema kama ungeenda kupumzika nyumbani” alisema Mahamud na Soraya akadakia, “samahani baba, nimemueleza mimi abakie kuna jambo nilitaka nikuombe” alisema Soraya na kuwafanya baba yake na mama yake washtuke kidogo, maana haikuwahi kutokea Soraya akatoa ombi kwa msisitizo kama huu, “nini tena mwangu, kuna jambo umepungukiwa?” aliuliza Mahamud, ambae siku zote katika mali au vitu alivyojaaliwa kuwa navyo basi mwanae alikuwa anampenda na kumthamini kuliko utajiri wake wote, “baba… mhhhh! nilikuwa naomba niende kwa kina Laylah” alisema Soraya kwa sauti ya upole yenye mashaka mashaka, “mh! Soraya usiku huu, kuna jambo gani muhimu usiku huu?” aliuliza mzee Mahamud kwa sauti ya mshangao kama alivyoshangaa mke wake, yaani mama Soraya, “hakuna kitu baba, ila… ila tu… ninataka kubadili mazingira maana leo sijikii vizuri” alisema Soraya, ambae toka amepata akili hakuwahi kukataliwa kitu na wazazi wake hasa baba yake ambae alimkingia kifua pale mama yake alipohitaji kumnyima kile alichoomba.
Mzee Mahamud alitulia kidogo akiwaza juu ya ombi la binti yake, alitumia kama dakika mbili nzima huku Soraya ambae alikuwa amevalia gauni lake refu la kushindia pale nyumbani pamoja na Laylah ambae alikuwa kama alivyokuja asubuhi wakisubiri jibu, “sioni ubaya wowote, wacha akaone jinsi mwenzie anavyoishi” alisema mama Soraya baada ya kuona mume wake anakosa jibu, “sijawahi kufika nyumba kwa Laylah, vipi kuhusu usalama wake?” aliuliza mzee Mahamud, ambae alionyesha wazi kutoridhika na ombi la mwanae, huku ana mtazama Laylah, Soraya nae akamtazama Laylah ambae pia alikuwa anamtazama na macho yao yakakutana, “ndiyo boss, usalama upo mkubwa tu, isitoshe mtaani kwetu hakuna fujo wa la vijana wahuni” alisema Laylah ambae alishaanza kuhisi mpango wa Soraya, japo hakuwa amemueleza, “ok! basi kesho saa mbili muwe hapa nyumbani, na kila baada ya muda fulani Soraya utakuwa unapiga simu kunijulisha kama upo salama” alisema Mahamud kisha akaeleka chumbani kwake, akimuacha Soraya anaingia chumbani kwenda kujiandaa.
Hapo ndipo ungejua kuwa kuna jambo Soraya alikuwa amepania, maana alivaa zile nguo alizozi chukuwa kwa kijana mpole akidhania kuwa ni zawadi zake, alivaa gauni jepesi na fupi ndani ya baibui, alichukuwa vitu ambavyo alikuwa anahisi vinge msaidia kwenye safari yake, ikiwa ni pamoja na mswaki na dawa yake, baadhi ya mafuta anayo yatumia kila siku na kiasi flani cha fedha.
“Da’ Layalah, naomba iwe siri yako, nipekele kule Mahilo nataka kufika kwa kijana mpole” alisema Soraya wakati wanatoka kwenye kituo cha mafuta, Laylah akatoa macho kwa mshangao, “Da’ Soraya, nikupeleke Mahilo usiku huu?” aliuliza Laylah kwa mshangao,”ndiyo tukimpata utaenda kuniacha huko utanifuata asubuhi” alijibu Soraya, akionyesha kuwa amedhamiria kufanya vile, “lakini Da’Soraya huogopi kule porini” aliuliza Layla kwa mshangao huku anakanyaga mafuta kuelekea mashariki mwa mji wa songea, “wala siogopi najua yule kijana hawezi kuniacha kwenye matatizo” alisema Soraya kwa kujiamini, akionyesha mwenye shauku ya kukutana na kijana yule, “na kama akikataa usilale kwake?” aliuliza Laylah ikiwa ni kama tahadhari, “hawezi kunifukuza kwasababu wewe tayari utakuwa umeshaondoka” alijibu Soraya na hapo kikapita kimya kifupi, “hivi umesema anaitwa nani vile?” aliuliza Soraya, “anaitwa Higgno” alijibu Laylah, huku anaendelea kukanyaga mafuta.******
Naam hatimae walifika mashambani na kubahatika kukiona kibanda kimoja pembeni mwashamba moja kubwa, huku moto ukiwaka nje yake ikionyesha kulikuwa na mtu, nadhani patakuwa pale maana wale wafanyakazi wa kule shambani walionyesha kuwa anakaa huku” alisema Soraya, “kwahiyo una uhakika kuwa ndiyo pale” aliuliza Laylah huku anapunguza mwendo, hapo tunakumbuka wakati ule tuliomuona Higgno akilitazama gari likiwa lina punguza mwendo barabarani, “twende mpaka pale kama sio pale tutaulizia anapoishi si umesema anaitwa Higgno?” aliuliza Soraya, huku sauti yake ikianza kubadilika na kuwa yenye kihoro, mh! sawa lakini mwenzio naogopa” alisema Laylah, huku anatembeza gari taratibu kutafuta njia ya kuingilia, na alipoipata aka kata kulia na kuanza kufuata njia ile iliyoenda moja kwa moja mpaka kwenye kile kibanda kidogo cha udongo, ambacho nje yake kulikuwa na mtu amekaa karibu na moto huku zikionekana nyama na samaki wengi wakibanikwa juu yake, “ndio yeye” alisema kwa kunong’ona Soraya, huku yeye na Layla wanamtazama kijana mpole ambae sasa alishamjua jina kuwa ni Higno, ambae alikuwa analishangaa gari lile lililopandishwa vioo, lililokuwa linamulika kwa taa zake, “ndiyo ni yeye” alisema Laylah kwa sauti ya kunong’ona pia, “mwenzio naona aibu tushuke kwanza wote halafu utaondoka” alisema Soraya, kwa sauti ya kunong’ona huku anajichekesha kicheko cha chini chini kilichojaa aibu. Hatimae soraya yupo shambani kwa higgno je nini kitajiriiiii? Usikose kufuatilia mkasa huu hapa hapa JamiiForums bila kusahau kuwa talibu nae ana jambo lake usiku nyumban kwa mzee Frank.....ITAENDELEA.
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA AROBAINI NA SABA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA SITA: Yap! waliposimama na kushuka toka kwenye gari mzee mahamud akaingia ofisini na Sorata akabaki ana mkabidhi Layla majina ya watu waliochagulia, kufanyiwa majaribio ya ajira, “Laylah, nadhani umemkumbuka yule kijana mpole” alisema Soraya kwa sauti ya chini iliyojaa kihoro, “tena nimeshangaa kusikia kuwa ndie aliemsaidia boss siku zile” alisema Laylah kwa sauti ya chini pia, lakini bado ikiwa na mshangao, “sasa hakikisha haingii humu ndani, muambie akupatie namba yake ya simu pia hakikisha kama kweli anaishi kule shambani Mahilo” alisema Soraya huku anampatia karatasi zenye majina ya watahiniwa …….. ENDELEA….
Hapo Laylah akashangaa sio kidogo, “we! Soraya, mwenzio si atakosa kazi na wakati baba amesema tuhakikishe anapata kazi?” aliuliza Laylah kwa sauti ya chini iliyojaa mshangao, “sitaki akutae na baba mpaka niongee nae mimi we fanya kama nilivyo kuambia” alisema Soraya kisha akaanza kuingia ndani akimuacha Laylah amesimama anamtazama kwa macho ya mshangao.
Soraya alipiga hatua kadhaa kisha akasimama na kugeuka nyuma akamuona Laylah amesimama anamtazama kama vile hakuelewa alichotakiwa kukifanya, hapo Sorya akarudi tena kwa Laylah, “usichoelewa nini Laylah?” aliuliza Soraya kwa sauti ya ile ile ya chini lakini iliyoonyesha kulalamika, “da’ Soraya, nayafikiria maisha ya yule kijana kwanini usimuache aingie halafu….” aliongea Laylah, lakini Soraya hakumuachia nafasi ya kumalizia akamadaka juu kwa juu, “Laylah, hii ndiyo nafasi yangu ya pekee ya kutimiza malengo yangu na ndoto yangu, ukikosea huyu kijana akaingia ndani hakika sito kusamehe hata kidogo” alisema Soraya kwa sauti kavu ambayo hata Laylah hakuwahi kuiskia hata siku moja, maana ilikuwa ya ukali na inayo maanisha, kisha akaondoka zake kuelekea ndani ya jengo la ofisi.
Soraya alimkuta baba yake akiwa pamoja na watu wengine watatu, ambao walikuwa na madaraka mbali mbali kwenye kampuni yao, yaani kama waajiriwa, huku kiti kimoja kikiwa kimebakia nae akakaa, “kama nilivyo waambia zingatieni majibu ya maswali mnayo uliza, si munajuwa kuna watu wanaleta janja janja, ameiba cheti cha ndugu yake anakifanya ni cha kwake ili apate kazi, akipata kazi unashangaa kama ni fundi anaharibikiwa na gari wanaanza kupiga piga simu tuwapelekee mafundi wengine wakawasaidie” alisema mze Mahamud kwa msisitizo, wakati wana wanasubiri watu waanze kuingia ili wawatahini, “hakuna shaka boss, tumejiandaa vizuri” walijibu wale watu watatu, huku muda wote Soraya akiwa kimya ametulia akiwaza juu ka kile alichomtuma Laylah, akiombea Laylah asije kufanya kitu tofauti.
Naam Laylah alirudi ndani na zile karatasi, akawaeleza kuwa tayari amesha waita walio hitajika na baada ya hapo akaelezwa kuwa aende akawaite mmoja baada ya mwingine waingie ndani” alisema Mahamud na Laylah akatoka nje, dakika chache baadae akaanza kungia ndani mtu mmoja baada ya mwingine, ambao walihojiwa na kuingia mwingine, huku wakichukuwa majina ya wale waliowakubali kwaajili ya kuingia kwenye awamu ya pili ambayo ingekuwa ni majaribio, ambapo ingefanyika siku mbili mbele.
Watu waliingia huku Soraya na baba yake wakimtazama kwa umakini kila alieingia wakiwa wanamtazamia mtu mmoja kwa mitazamo tofauti, wakati mzee Mahamud anatarajia kuona kijana aliemsaidia siku ile aliyovamiwa na vijana wawili waliokuwa na lengo la kumdhuru na kumpora fedha, huku Soraya alikuwa anaombea kijana huyo huyo asiingie mule ndani, maana hakutaka akutane na baba yake kabla hajakutana nae yeye.*********
Saa tano Talib alienda mwembe chai kwa Zido, na aliwakuta wakina Zido wakiwa pale nyumbani wanauguza majeraha yao waliyo yapata jana kule shambani kwa Soraya, “jamani hee mimi na mchongo, tusikae kuwaza juu ya yule fala” alisema Talib, huku ana sokota bangi, “Talib hebu achana na hizo mambo, unajuwa unapo mzungumzia yule dogo unamzungumzia mtu mwingine kabisa sio wa kipindi kile tupo shule” alisema Vitus ambae ni mmoja kati ya walioumia kidogo na kuwa na afadhari, “we ngoja uone nitakacho mfanyia usiku wa leo, nyie wenyewe mutajua kuwa mimi sio wa pole pole” alisema Talib kwa majisifu huku anawasha ile bangi yake na kuanza kuivuta, “Dah! Hebu achana na hiyo tupe mchongo mpya tuone kama unafaa” alisema Vitus, na hapo Talib akaanza kuelezea kuhusu fedha zilizopo kwenye kabati la ukutani la ofisini kwa baba mjomba wake, “sasa tutaingiaje mpaka ndani ya jumba lile mwanangu” aliuliza Zido kwa mara ya kwanza, “mutaingia mapema halafu mutajibanza chumbani kwangu, kwasasa nitahakikisha ninaiba funguo moja ya mlango wa nyuma wa nyumba kubwa, ambao tutaumia kuingilia na kiukweli mlango wa ofisi huwa haufungwi, hapo ni kazi kwenu kuchukuwa mkwanja na kutambaa zenu” alieleza Talib kwa namna ambayo ungesema ni kitu chepesi sana, “ni hivyo tu!?” aliuliza Vitus, kwa sauti ya mashaka, “kumbe je! unadhani kuna jipya basi, ni kama kumsukuma mlevi” alisema Talib huku akiendelea kuvuta bangi, “basi poa, wacha kwanza tukae sawa halafu tucheze na huo mkwanja” alisema Vitus, huku wenzake pia wakianza kupata matumaini mapya.**********
Naam kule kwenye masailiano ya ajira, Bahati iliangukia upande wa Soraya, maana wali wasaili wale watu walioomba kazi mpaka saa tisa za jioni, ambapo mtu wa mwisho aliingia pasipo kumuona Kijana mpole akiingia mule ndani, “unasema wameshaisha mbona yule kijana sijamuona?” aliuliza mzee Mahamud kwa mshangao, huku anamtazama Laylah aliekuja kutoa taarifa ya kuwa tayari watu wote walishaisha, “boss nadhani alipoona hajaitwa akaamua kuondoka” alisema Laylah huku akitazamaisha kichwa chini, “khaaaa! kwanini lakini, ilifaa umueleze mapema kuwa asiondoke” aliongea mzee Mahamud kwa sauti ya kulalamika, akionyesha wazi kuwa yule kijana kwake ni uhimu sana na hakutakiwa kukosa kazi, “baba wala hauhitaji kuwa na wasi wasi, madhari tumesha muona na kumfahamu basi tukimuona tena tutamueleza aje kukuona” alisema Soraya akionyesha kuwa mwenye furaha tofauti na alivyokuwa asubuhi.
Baada ya kuwa tangazia wale walioomba nafasi wakiwasoma majina wale waliopitishwa kwenye interview, Mzee Mahamud na binti yake wakaondoka pale ofisini huku Laylah akiendesha gari, muda wote Soraya alionyesha mwenye furaha isiyo na kifani, aliongea na kucheka kwa furaha hata wakiwa nyumbani pia alikuwa hivyo hivyo.
Masaa yalikatika huku Laylah, akionekana kusalia pale nyumbani kwa boss wake, na hata walipomaliza kuswali swala ya insha ndipo Mahamud aliposhangaa, “Laylah, hujachoka kwa kazi tuliyoifanya kutwa nzima, ni vyema kama ungeenda kupumzika nyumbani” alisema Mahamud na Soraya akadakia, “samahani baba, nimemueleza mimi abakie kuna jambo nilitaka nikuombe” alisema Soraya na kuwafanya baba yake na mama yake washtuke kidogo, maana haikuwahi kutokea Soraya akatoa ombi kwa msisitizo kama huu, “nini tena mwangu, kuna jambo umepungukiwa?” aliuliza Mahamud, ambae siku zote katika mali au vitu alivyojaaliwa kuwa navyo basi mwanae alikuwa anampenda na kumthamini kuliko utajiri wake wote, “baba… mhhhh! nilikuwa naomba niende kwa kina Laylah” alisema Soraya kwa sauti ya upole yenye mashaka mashaka, “mh! Soraya usiku huu, kuna jambo gani muhimu usiku huu?” aliuliza mzee Mahamud kwa sauti ya mshangao kama alivyoshangaa mke wake, yaani mama Soraya, “hakuna kitu baba, ila… ila tu… ninataka kubadili mazingira maana leo sijikii vizuri” alisema Soraya, ambae toka amepata akili hakuwahi kukataliwa kitu na wazazi wake hasa baba yake ambae alimkingia kifua pale mama yake alipohitaji kumnyima kile alichoomba.
Mzee Mahamud alitulia kidogo akiwaza juu ya ombi la binti yake, alitumia kama dakika mbili nzima huku Soraya ambae alikuwa amevalia gauni lake refu la kushindia pale nyumbani pamoja na Laylah ambae alikuwa kama alivyokuja asubuhi wakisubiri jibu, “sioni ubaya wowote, wacha akaone jinsi mwenzie anavyoishi” alisema mama Soraya baada ya kuona mume wake anakosa jibu, “sijawahi kufika nyumba kwa Laylah, vipi kuhusu usalama wake?” aliuliza mzee Mahamud, ambae alionyesha wazi kutoridhika na ombi la mwanae, huku ana mtazama Laylah, Soraya nae akamtazama Laylah ambae pia alikuwa anamtazama na macho yao yakakutana, “ndiyo boss, usalama upo mkubwa tu, isitoshe mtaani kwetu hakuna fujo wa la vijana wahuni” alisema Laylah ambae alishaanza kuhisi mpango wa Soraya, japo hakuwa amemueleza, “ok! basi kesho saa mbili muwe hapa nyumbani, na kila baada ya muda fulani Soraya utakuwa unapiga simu kunijulisha kama upo salama” alisema Mahamud kisha akaeleka chumbani kwake, akimuacha Soraya anaingia chumbani kwenda kujiandaa.
Hapo ndipo ungejua kuwa kuna jambo Soraya alikuwa amepania, maana alivaa zile nguo alizozi chukuwa kwa kijana mpole akidhania kuwa ni zawadi zake, alivaa gauni jepesi na fupi ndani ya baibui, alichukuwa vitu ambavyo alikuwa anahisi vinge msaidia kwenye safari yake, ikiwa ni pamoja na mswaki na dawa yake, baadhi ya mafuta anayo yatumia kila siku na kiasi flani cha fedha.
“Da’ Layalah, naomba iwe siri yako, nipekele kule Mahilo nataka kufika kwa kijana mpole” alisema Soraya wakati wanatoka kwenye kituo cha mafuta, Laylah akatoa macho kwa mshangao, “Da’ Soraya, nikupeleke Mahilo usiku huu?” aliuliza Laylah kwa mshangao,”ndiyo tukimpata utaenda kuniacha huko utanifuata asubuhi” alijibu Soraya, akionyesha kuwa amedhamiria kufanya vile, “lakini Da’Soraya huogopi kule porini” aliuliza Layla kwa mshangao huku anakanyaga mafuta kuelekea mashariki mwa mji wa songea, “wala siogopi najua yule kijana hawezi kuniacha kwenye matatizo” alisema Soraya kwa kujiamini, akionyesha mwenye shauku ya kukutana na kijana yule, “na kama akikataa usilale kwake?” aliuliza Laylah ikiwa ni kama tahadhari, “hawezi kunifukuza kwasababu wewe tayari utakuwa umeshaondoka” alijibu Soraya na hapo kikapita kimya kifupi, “hivi umesema anaitwa nani vile?” aliuliza Soraya, “anaitwa Higgno” alijibu Laylah, huku anaendelea kukanyaga mafuta.******
Naam hatimae walifika mashambani na kubahatika kukiona kibanda kimoja pembeni mwashamba moja kubwa, huku moto ukiwaka nje yake ikionyesha kulikuwa na mtu, nadhani patakuwa pale maana wale wafanyakazi wa kule shambani walionyesha kuwa anakaa huku” alisema Soraya, “kwahiyo una uhakika kuwa ndiyo pale” aliuliza Laylah huku anapunguza mwendo, hapo tunakumbuka wakati ule tuliomuona Higgno akilitazama gari likiwa lina punguza mwendo barabarani, “twende mpaka pale kama sio pale tutaulizia anapoishi si umesema anaitwa Higgno?” aliuliza Soraya, huku sauti yake ikianza kubadilika na kuwa yenye kihoro, mh! sawa lakini mwenzio naogopa” alisema Laylah, huku anatembeza gari taratibu kutafuta njia ya kuingilia, na alipoipata aka kata kulia na kuanza kufuata njia ile iliyoenda moja kwa moja mpaka kwenye kile kibanda kidogo cha udongo, ambacho nje yake kulikuwa na mtu amekaa karibu na moto huku zikionekana nyama na samaki wengi wakibanikwa juu yake, “ndio yeye” alisema kwa kunong’ona Soraya, huku yeye na Layla wanamtazama kijana mpole ambae sasa alishamjua jina kuwa ni Higno, ambae alikuwa analishangaa gari lile lililopandishwa vioo, lililokuwa linamulika kwa taa zake, “ndiyo ni yeye” alisema Laylah kwa sauti ya kunong’ona pia, “mwenzio naona aibu tushuke kwanza wote halafu utaondoka” alisema Soraya, kwa sauti ya kunong’ona huku anajichekesha kicheko cha chini chini kilichojaa aibu. Hatimae soraya yupo shambani kwa higgno je nini kitajiriiiii? Usikose kufuatilia mkasa huu hapa hapa JamiiForums bila kusahau kuwa talibu nae ana jambo lake usiku nyumban kwa mzee Frank.....ITAENDELEA.
Bikra mbili zinaenda kutana litakufa jitu😂
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA AROBAINI NA TISA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA AROBAINI NA NNE: alichokishuhudia kilimshangaza na kumzizimisha mwili mzima, maana alimuona mke wake ana tembea taratibu kama zombie akihesabu hatua moja moja, miguu ametanua, mmoja kushoto mmoja kulia, ungejuwa wazi hakutaka ikutane kana kwamba uvunguni kwake kulikutana na dhahama kubwa, “mama Hilda mama Hilda” aliita mke wa Njogopa, aliekuwa amekaa karibu na mume wake pale kwenye mabenchi waliyo kalia wakina mzee Komba ambae ni kama alikuwa ameshikwa na butwaa, huku akimtazama mke wake ambae alishtuka sana alivyoitwa na mke wa Njogopa …….. ENDELEA….
Mke wa Njogopa aliinuka na kumfuata mke wa Komba ambae bado alikuwa amesimama anatazamana na mume wake, “vipi shoga mbona unatembea hivyo kuna usalama kweli?” aliuliza mke wa Njogopa, huku akimtazama mama Hilda aliesimama miguu pande, zaidi ya miguu pande ile ya kiaskari kwenye gwaride, “mwenzangu yamenikuta, sijui kuna mdudu gani ametambalia, yaani ninawashwa haijawahi kutokea” alidanganya mama Hilda, huku macho yako kwa mume wake, “jamani amekutambalia kwa bibi?” aliuliza mke wa Njogopa kwa sauti iliyojawa na huzuni, akivuta picha ya maumivu ya muwasho anaoupata mama Hilda, yaani mke wa mzee Komba, “yaani penyewe pale pale pamfuleni (mtoni au kisimani, sehemu wachotayo maji)” alijibu mama Hilda huku ana muonyesha ishara mume wake ya kumuita, nae akainuka na kuwasogelea, “jamani pole, basi wacha nikuache uende na shameji akakuangalie” alisema mke wa Njogopa na kuondoka zake, akiwaacha Komba na mke wake wakielekea nyumbani kwao.
“Mke wangu, mbona unatembea hivyo umepatwa na nini?” aliuliza mzee Komba, huku akimkokota mke wake ambae tembea yake ilikuwa ni kwa shida kubwa, “ndugu yangu, wakati wakurudi nilibanwa na mkojo njani, nikaingia kichakani kukojoa sijui amenitambaa mdudu gani, yani hapa mpaka chupi nimevua, haivaliki nina washwa kama upupu, nime jikuta mpaka kum.. yote nyekunduuu” alisema mama Hilda, huku anaingiza mkono wake kwenye sidilia yake na kutoa nguo yake ya ndani akamkabidhi mume wake mkononi nae akaishika na kuitazama halafu akaendelea uibeba, huku wakiendelea na safari, na walipo kuwa wanakatiza kwenye kichaka kimoja pembeni ya barabara mita chache kabla hawajafika nyumbani, mara wakaanza kusikia sauti ya kike ikitokea kichakani, “sio huko bwana” ilikuwa ni sauti ya kulalamika ya kike toka kichakani, “mara moja tu nakojoa haraka, mbona siku ile tulifanya na haukuumia” ilisikika sauti ya kiume ikibembeleza kilevi, “lakini wanasema sio kuzuri kuzoea nitashindwa kuzaa” ilisikika sauti ya kike, ambayo mzee Komba na mke wake walishaijua kuwa ni sauti ya binti yao, “lakini si mpaka ufanye sana halafu siku ile uliniambia tamu au ulinidanganya?” iliuliza ile sauti ya kiume, nadhani kutokana na ulevi hawakujua kama walikuwa wanasikika nje ya kichaka, “hata kama tamu lakini sio vizuri” alisema Hilda, huku wazazi wake wanasikia kila kitu na kushindwa kupita haraka eneo lile kutokana na mwendo mdogo wa mama Hilda, “sasa ndio unanyima” iliuliza sauti ya kiume, “na wewe kwa kung’ang’ania, haya basi ingiza lakini ukichafuka shauri yako” ukweli mzee Komba hakutamani kuendelea kusikiliza zaidi upuuzi wa mwanae ambae alikuwa analipia kwa gharama kubwa sana ulanzi aliounywa jioni ile.
Hawakuelewa kilichoendelea kwasababu hawakusikia sauti nyingine yoyote toka kichakani mpaka walipo toweka eneo lile la kichaka, ikionyesha kuwa binti yao aliweza kuhiimili kile alichokuwa anafanyiwa, “unajua mama Hilda sasa ibidi tuwe tunanywea nyumbani” alisema mzee komba huku wakiingia eneo la nyumbani kwao, “baba Hilda bwana yaani mimi naugulia maumivu wewe una uzungumzia ulanzi” alilalamika mama Hilda, “hapana mama Hilda, we si unaona anachokifanya mwanao, sasa unataka niwe namuona akishikwa shikwa na vijana” alisema mzee Komba na hapo mke wake hakujibu lolote mpaka walipoingia ndani, “chukua ungo njoo nao chumbani”, alisema mama Hilda, huku yeye akiongoza chumbani, na mzee Komba akaigia jikoni ambako alichukua ungo na kuelekea chumbani ambako alimkuta mke wake amelala kitandani akitazama juu, yaani chali amevua nguo zote huku miguu ameitanua kwa nguvu na kuikunja kama anaehitaji kujifungua, japo giza lilikuwa limetanda lakini mzee Komba aliweza kukisia kuwa kitumbua kilikuwa kime achama vibaya sana, “nipepee baba Hilda” alisema mama Hilda na mzee Komba akaanza kupepea kwenye kitumbua cha mke wake, kama vile anapuliza moto wa kuni au mkaa, akiupeleka ungo juu na chini.
Kazi hiyo ilidumu kwa muda wa lisaa lizima mpaka mama Hilda alipopitiwa na usingizi, lakini kazi haikuishia hapo, maana kila mama Hilda alipojiziuka na kubana miguu maumivu yalimlipukia na kumuamsha mume wake akiomba kupepewa kwenye kitumbua chake, na mzee Komba alifanya hivyo pasipo kujua alicho fanyiwa mke wake, na kama angekuwa na taa mule ndani, angeweza kuona vitu vyeupe mfano wa tui zito la nazi likichuungulia kwenye mlango wa kitumbua cha mke wake.
Shughuli iliendelea maraa kwa mara karibia usiku kucha, hata kulipokucha mzee Komba alikuwa na usingizi kama wote, huku mke wake akiamka na unafuu fulani japo alikuwa anatembea kwa kuchechemea.******
Ni kweli ilikuwa siku ya juma tatu, siku ambayo ilikuwa inasubiriwa kwa hamu kubwa na Familia ya bwana Frank, maana ndiyo siku ambayo kijana wao alikuwa anaenda kujaribu bahati yake ya kuomba nafasi ya kazi, na walikuwa na asilimia kubwa ya kijana wao huyo kupata moja ya nafasi za kazi kati ya zilizotolewa, maana alisha ahidiwa na tajiri Mahamud mwenye kamumpuni hiyo ya usafirishaji.
Saa moja kasoro tayari Higgno alikuwa ameshafika nje ya ofisi za Mahamud Trans, eneo la NMC ikiwa ni shirika la kiserikali la kuhifadhi nafaka akiwa mmoja kati ya watu wachache, ambao tayari walikuwa wameshafika eneo lile kwa muda ule, ambao ulikuwa ni mapema sana, maana muda wa kuanza mchakato ulikuwa ni saa mbili kamili za asubuhi, Higgno akajichanganya na wenzake na kuanza maongezi ya hapa na pale, hasa wakizungumzia mabasi mapya mengi waliyokuwa wanayaona mbele yao, ambayo ubavuni yalikuwa yameandikwa SORAYA EXPRESS, “huyu jamaa anamkwanja mrefu, unajua haya mabus ni mpya kabisa yapo kama ishirini hivi” alisema mmoja wao, “hivi kwanini haya mabus amebadili jina hajaandika Mahamud?” aliuliza kijana mwingine huku Higgno akiwa msikilizaji tu!, “hii ni kampuni mpya ya mwanae, anampenda kinyama” alisema yule wa kwanza, “ebwana hee! unamfahamu huyo Soraya mwenyewe, ni demu mkali kinyama, nilimuonaga kitambo wakati anasoma Songea Girls, alisema mwingine akimsifia mtoto wa tajiri mwarabu Mahamud, “namfahamu yule demu ni mkali kinoma, sijui nani atakuwa ana kula ule mzigo” aliongea mwingine wakimfuambua macho kijana Higgno, ambae mwanzo hakujua kama Mahamud alikuwa na mtoto wa kike, yeye alikuwa anamjuwa Talib pekee.****
Soraya aliamka miida ya saa moja na robo na kuanza kujiandaa kwaajili ya kwenda ofisini kuwa hoji na kuwatahini watu waliokuwa wanahitaji kuwaajili, ukweli Soraya muda wote alikuwa anajiandaa mawazo yake yalikuwa ni namna gani atampata kijana mpole, ukweli alitaka kuonana nae haraka sana kwasababu aliona wazi wazazi wake wanaanza kumshuku kijana mpole bila sababu yoyote, “lazima nikutana nae haraka, hata kama watakutana nae tayari mimi nitakuwa nimesha kutana nae” aliwaza Soraya ambae hata mimi sikujua ana maana gani.
Wakati anaendelea kuvaa mara akaingia Subira, ambae humu chumbani ni kama kwake, kwasababu alimlea Soraya katika chumba hiki toka akiwa mdogo, “Soraya unahitaji masaada wowote?” aliuliza Subira, akimaanisha kama Soraya alikuwa anahitaji msaada katika mavazi, “hapana nimesha maliza, alisemema Soraya aliekuwa anajifunga ile niqab yake, yaani kitambaa cha kuzuia uso wake, “sawa ila naona kama baba yupo tayari na Laylah ameshafika” alisema Subira, ambae hakutoka mule chumbani mpaka Soraya alipomaliza kujiandaa, na wakatoka kwa pamoja mpaka Sebuleni, ambapo alimkuta baba yake akipata kifungua kinywa, “assalam alaykum” alisalimia Soraya kwa sauti iliyo pooza, “waalaykum salam, umeamkaje Sor…” kabla hajamalizia tayari Soraya alikuwa amesha ondoka kueleka ofisini, mzee Mahamud akamtazama kwa mshangao, “mh! ana nini huyu, au ni kwasababu jana nilionyesha kumtilia mashaka huyo kijana wake mpole” aliwaza Mahamud, “lakini lazima nimtilie mashaka, kwanini awe yeye tu! usikute ni mmoja kati ya wanao panga haya matukio, bora yule alienisaidia mimi aliomba apate kazi akimaliza chuo……” hapo Mahamud akasita kidogo, kuna kitu alikumbuka, alimkumbuka kijana aliemsaidia lakini hakumkumbuka jina, japo kwa Sura alikuwa na uhakika wa kumtambua, “sijui kama barua yake ilipita kati ya zile tulizo zichagua?” alijiuliza Mahamud huku anatazama upande wa kolido ilipo ofisi, akamuona Soraya anakuja toka ofisini amebabe begi lenye barua za maombi ya kazi, alipo mtazama usoni alimuona wazi kuwa binti yake amekosa amani, “Soraya upo vizuri kweli mwanangu?” aliuliza Mahamud wakati huo mke wake nae anatokea upande wa vyumbani, “unadhani kuna jingine ni lile lile la jana tu!, anamfikiria huyo kijana wake mpole” alisema mama Soraya ambae alikuwa amevalia mavazi ya kushinda nayo pale pale nyumbani” hapo Soraya hakutaka hata kujibu wala kugeuka, akaanza kuongoza kutoka nje, “eti! Soraya” alisema mzee Mahamud, unaweza kusema alikuwa anataka kupima kama binti yake alikosa amani juu ya jambo la jana, bahati nzuri Soraya hakuwa na kiburi na haikuwahi kutokea kuwanunia wazazi wake, alisimama na kugeuka kumtazama baba yake, wakati huo mama yake alikuwa anakaa mezani pamoja na mume wake, “unakumbuka niliwahi kusema kuhusu kijana alienisaidia wakati ule nilipo vamiwa na wale vibaka” alisema mzee Mahamud na Soraya akakumbuka vyema juu ya kijana huyu, “namkumbuka baba” aliitikia Soraya kwa sauti ya upole isiyo changamka kama alivyo siku zote, “hoo! ni yule ulieahidi kumpatia kazi, aliomba nafasi kweli?” aliuliza mama Soraya, “ndio nilitaka kumueleza Soraya kuwa tuweke nafasi moja ya dharula, ili kama ikitokea hatukuipitisha barua yake basi tutampatia nafasi hiyo, maana nakumbuka hatukuchukua barua za mafundi wasio na uzoefu” alisema Mahamud, “ndiyo baba bila shaka” alisema Soraya na wakati huo alitokea Laylah na kusalimia, kisha akapokea begi Soraya na wakaanza kutoka nje.
Mahamud hakuwaacha waondoke, maana bado aliona ishara ya mwanae Soraya kuwa katika hali tofauti, Laylah anadaa gari langu tutatumia hilo kwenda ofisini” alisema Mahamud, hakuwa na lolote zaidi ya kuhitaji kuwa karibu na binti yake pengine angemshawishi kurudi katika hali yake ya uchangamfu, “ndiyo boss” aliitikia Laylah, kisha wakaendelea kutembea kutoka nje, “leo ni kasheshe, bint Mahamud amekataa kunywa chai” alisema Mahamud akimueleza mke wake, “lakini baba Soraya, unajua bado sijaelewa, nikwamba hutaki Soraya aolewe na huyo kijana au kuna jingine?” aliuliza mke wa Mahamud, “mama Soraya, siwezi kusahau kile huyo kijana alichomsaidia Soraya, na nina uheshimu msaada huo, lakini lazima nimuulize swali langu, ambalo akishindwa kulijibu au kama jibu sitoridhika nalo basi hata Soraya akilia machozi ya damu, sitomkubalia” alisema Mahamud, akimalizia kunywa chai na kutoka nje kuungana na wakina Soraya kuelekea ofisini.
Wakati huo Talib, ambae ni mmoja kati ya watu walioamka mapema siku ile alikuwa ana wachungulia dirishani kutokea chumbani kwake, akisubiri waondoke ili na yeye aondoke zake kuelekea Luhila kwakina Higgno, ambako alikuwa ana pafahamu vyema kabisa, lengo lake lilikuwa ni kwenda kumfundisha adabu bwana mdogo huyu kwa kumkosesha fedha nyingi sana alizoishia kuziona kwa macho, “au kwanini nisi fanye mchongo wa kuingiza majambazi humu ndani ili wakavunje lile kabati la fedha ofisini kwa mjomba” aliwaza Talib akiwa bado dirishani awatazama wakina Soraya, ambao walikuwa wanaingia kwenye gari pamoja na mjomba wake, kisha gari linaondoka Laylah akiliendesha taratibu kutoka getini.
Nalilipotokomea nje tu! hapo hapo Talibu akachukua kisu fulani kirefu na kukiweka kiunoni mwake, akikibana na mkanda wa suruali yake akifunika na tishet lake ndefu, kisha akatoka na kuingia nyumba kubwa, akaenda sebuleni kwa shangazi yake ambae alikuwa anamalizia kunywa chai, “shikamoo shangazi” alisalimia Talib, ambae hutumia salamu hii kwa shangazi yake tu!, “marahaba, vipi kuna shida” aliuliza mama Soraya huku anamtazama Talib aliekuwa amesimama anamkodolea macho, “shangazi nilikuwa nahitaji kwenda kutazama biashara inaendaje, sasa niazime elfu tano nitakurudishia nikirudi” alisema Talib na hapo shangazi akaguna kidogo, “mh! mara ngapi nimesha kuazima fedha halafu hukurudisha, we sema naomba elfu tano” alisema shangazi huku anainuka na kuelekea chumbani kwake akimuacha Talib ana waza namna ya kuzipata fedha ofisini kwa mjomba wake, “lazima nipange mpango huo, na jua hiki kibabu tuna kifungia kwenye gunia halafu tuna zama ndani wanakomba mkwanja” aliwaza Talib na wakati huo shangazi yake akaja na elfu tano akamkabidhi na yeye akaondoka zake.*******
Naam! Higgno akiwa pamoja na wale wenzake ambao sasa walianza kuwa kama marafiki pale nje ya eneo la ofisi ya Mahamud Trans, maongezi yaliendelea huku kila muda ulivyosonga ndivyo watu walivyozidi kuongezeka, na mpaka saa mbili kasoro tayari watu zaidi ya mia tatu walikuwa wameshajaa eneo lile, hakika licha ya kuwa alishapewa ahadi ya kupewa kazi mwaka mmoja uliopita lakini kwa uwingi wa watu hawa ulianza kumtia mashaka kijana Higgno.
Naam wakiwa wamezama kwenye maongezi mara wakaliona Nisaan Patrol likiingia, “huyoooo! alisema mmoja wao huku wanatazama gari lile ambalo lilikuwa limepandishwa vioo vya giza, yaani Tinted, ambalo lilikuwa linapita karibu yao, na ghafla likapunguza mwendo na hawakujua kwanini, lakini alikusimama likaelekea moja kwa moja ndani ya geti la uzio mdogo wa ofisi na kuingia ndani kisha geti likafungwa.
Hapo zikapita dakika kumi ndipo mlango mdogo ulio ambatanishwa kwenye lile geti la chuma ulifunguliwa na akatokea mschana mmoja ambae kwa mbali Higgno hakuweza kumfahamu mschana yule alikuwa ameshika karatasi, mkononi mwake akiongozana na mlinzi wa kampuni ya ulinzi, “sogeeni msikilize” alipiga kelele yule mlinzi, na hapo watu kama mia tatu hivi wakamiminika karibu na lile geti, “haya sikilizeni majina yenu, ukiitwa unaingia ndani sitaki vurugu” alisema yule mlinzi, kisha akachukua lile karatasi toka kwa Laylah na kuanza kuita majina, ni majina ya watu ambao barua zao zilishateuliwa, na hapo ndipo Higgno alipoweza kumtambua yule mschana kuwa ni yule mwanamke ambae ni dereva wa yule mschana ambae alimsaidia mara mbili, (ndivyo alivyo mtambua yeye Higgno)
Higgno akiwa makini kabisa anasikiliza jina lake, alisikiliza kwa muda mrefu huku watu wakiitwa na kuingia ndani mpaka alipoona kurasa zote mbili za karatasi la majina lilielekea mwisho na yeye kuanza kukata tamaa, “haya jamani, nitaita majina matatu ya mwisho, kama hautosikia jina lako tutaomba uondoke eneo hili” alisema yule mlinzi nakuanza kusoma tena yale majina, muda wote Laylah alikuwa makini kuangalia waliokuwa wanaingia ndani, na mara kwa mara alilikuwa anamtazama Higgno ambae bado alikuwa anashangaa kuona yule mschana dereva wa yule mschana wa kiarabu yupo hapa kwa Mahamud.
Aliita jina la kwanza na mwenye jina akaitika na kuingia ndani, jina lililofua lilikuwa ni Higgno Frank, “nipooo” aliitikia Higgno kwa sauti ya juu kabisa, huku akijipenyeza kwenye kundi la watu kusogelea geti akiwa na bahasha yake ya vyeti vya chuo cha ufundi, lakini ile anataka kuingia tu! akazuiliwa mlangoni na yule mwanamke dereva, “wewe ndie nani vile?” aliuliza yule dereva huku anapokonya ile bahasha kwa Higgno na kuifungua, “Higgno Frank” alijibu, Higgno kwa sauti ya upole, huku anamtazama yule mwanadada ambae nae uzuri wake sio wa pole pole, aliekuwa anachomoa vyeti vyake na kuanza kuvitazama.
Laylah, alitazama vyeti vile huku mwingine wa mwisho alieitwa aliingia ndani na akimpita Higgno alieanza kushangaa kwanini yeye anakaguliwa vyeti pale mlangoni, “Higgno unaishi wapi kwa sasa?” aliuliza Laylah, huku anarudisha vyeti kwenye bahasha, “naishi mahilo shambani kwetu” alisema Higgno, ambae kudanganya kwake ni mara chache sana, wakati huo watu wengine walikuwa wanaondoka eneo lile, ni baada ya kushindwa kusikia majina yao, “unaweza kunipa namba zako za simu?” aliuliza Laylah, huku akimtazama Higgno, “hapana dada yangu sina namba yoyote ya simu, hata ya baba yangu sijaishika kichwani” alisema Higgno, “kwani baba yako unaishi nae huko shambani?” aliuliza Laylah, “hapana kule naishi mwenyewe” alijibu Higgno kwa sauti ya upole, hapo Laylah, akashusha pumzi ndefu huku anatazama chini, kisha akatulia kwa sekunde kadhaa na kuinua uso wake kumtazama Higgno, “sikia kaka yangu, jina lako liliitwa kwa bahati mbaya, lakini ki ukweli hauna sifa za kuwa mwajiriwa wa kampuni hii, hivyo unaweza kwenda” alisema Laylah, huku anampatia Higgno bahasha yake, kisha akaingia pamoja na mlinzi na kufunga geti huku Higgno akikosa nafasi ya kukumbusha kuwa alikuwa ana ahadi na mwarabu Mahamud…… ITAENDELEA
Higgno huwa ni fala fala tu hata kujielezea hawezagi
 
Ebwanae hatimae nitakuwa nareply. Nimesoma kimya kimya tangu enzi za ASALI HAITIWI KIDOLE kwa minjali ya kutokuwa na acount, leo nimeitengeneza bhana
 
Back
Top Bottom