Simulizi: Sitasahau Tanga

Simulizi: Sitasahau Tanga

bioto

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2017
Posts
1,261
Reaction score
2,099
IMEANDIKWA NA : ATUGANILE
MWAKALILE
*********************************
*********************************
***************
Simulizi : Sitasahau Tanga
Sehemu Ya Kwanza (1)
Nikiwa kwenye mishe zangu za
research kwenye mji wa Tanga,
ilikuwa ni research ya siku kumi
na nne. Jioni ya siku ya pili
nikakatisha sehemu flani hivi
mjini hapo kuangalia na
kutembea tembea, lahaula
nikakutana na binti mmoja wa
kuvutia sana kwakweli nikajikuta
nikivutiwa naye alikuwa mweupe
sana na nywele ndefu na umbo
kama la mamiss hivi dah nikaona
hapa ndio penyewe yani kwani
alikuwa na ugonjwa wangu
mkubwa unaonivutia kwa
wadada nao ni rangi nyeupe.
Sikutaka kupoteza wakati mtoto
wa kiume ikanibidi nimsogelee ili
niweze kumsabahi, tukasalimiana
pale na kujuana majina na
tukabadilishana namba. Basi
ikawa kila jioni nakutana na yule
binti, pesa yote namalizia kwake.
Kwakweli nikampenda kwani
alikuwa ni binti mzuri sana kama
malaika aliyeshushwa hata demu
wangu niliyemwacha Dar
nikamsahau kabisa kwani
hakuwa na mvuto kama huyu
dada wa kitanga.
Baada Ya kumaliza ile research ya
siku kumi na nne sikutamani
kurudi Dar ila ilinibidi nirudi ili
nikakabidhi kazi ya watu na
nikasake mavumba ya ziada ya
kunifaa kumchumbia yule binti
wa kitanga.
Niliporudi Dar sasa ndio nilielewa
ule wimbo wa "Tanga kunani
pale".
Siku hiyo nikiwa kwenye chumba
changu nimetoka kuoga mara
simu ikaita kuichek ni yule binti
wa kitanga.
MIMI: Hallow mpenzi
BINTI: Ndio mpenzi, mbona
hujajisugua vizuri umeacha povu
sikioni?
MIMI: (Nikachukua kidole na
kugusa sikioni kukitoa kikatoka
na povu), haa umejuaje mpenzi?
BINTI: Nimekuona hapo mpenzi
wangu.
MIMI: (Nikiangalia kushoto na
kulia), umenionaje?
BINTI: Usijari mpenzi, chukulia
kawaida tu.
Baada ya simu kukatika, Dah
nilikaa nikawaza na kuwazua
nikaamua kupotezea tu. Nikavaa
fastafasta, halafu nikaenda
kununua msosi nikachukua na
kilimanjaro moja nikashushia ili
nilale vizuri. Mara simu ikaita,
BINTI: Mpenzi si nilikukataza
wewe kunywa pombe?
MIMI: (Nikiwaza kichwani,
majanga haya) mbona mi
sijanywa pombe!
BINTI: Nimekuona mpenzi
umekunywa bia moja.
MIMI: (Nikashtuka na kuangalia
kushoto na kulia), aaah sijui eeeh
kwani umejuaje?
BINTI: Fanya yote ila tambua
hakuna utalofanya nisijue.
Halafu akakata simu, nikaanza
kuwaza tena amejuaje kama
nimekunywa? Au kasikia harufu
ya pombe kwenye simu. Mara
sms ikaingia kwenye simu yangu,
kuangalia ni yule binti, sms
iliandikwa "usiwaze sana mpenzi"
Nikiwa chumbani nimejiinamia
mara demu wangu wa Dar
akanipigia simu na kuniambia
kuwa nimempotezea siku hizi
kwani tangu nimerudi sijaonana
nae, sikutaka kuongea mengi ila
nikamwambia asijari nitaonana
nae tu. Wakati najiandaa kulala
binti wa Kitanga naye akanipigia,
BINTI: Mpenzi ulikuwa unaongea
na nani kwenye simu?
MIMI: Ni rafiki yangu wa kawaida
tu mpenzi.
BINTI: Niambie ukweli tafadhari.
MIMI: Huo ndio ukweli mpenzi.
BINTI: Sawa ila nitakachofanya
usinilaumu badae.
MIMI: Jamani mpenzi unataka
kufanya nini tena?
BINTI: Si nilikukataza kuongea na
wanawake wewe, na kwanini
unanidanganya?
MIMI: Aaah samahani mpenzi,
sitarudia.
Akakata simu, nikawaza sana bila
ya kupata jibu nikaamua kulala
tu.
Asubuhi nikashtushwa na simu
yake,http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
BINTI: Mbona hukushusha
chandarua usiku?
MIMI: Umejuaje mpenzi?
Nilisahau bhana.
BINTI: Usijari mpenzi.
Basi nikaamka na kwenda zangu
kuoga, nikarudi na kuvaa ili
nijiandae kwenda kwenye mishe
zangu. Mara simu ikaita.
BINTI: Mpenzi hiyo tisheti
uliyovaa siipendi.
MIMI: (Nikiangalia ile tishirt
yangu), umejuaje kama nimevaa
tishirt usiyoipenda?
BINTI: Nimejua tu mpenzi,
unajua mi nakupenda kwahiyo
mambo mengi unayofanya
yanakuja kwangu kwa hisia.
MIMI: Asante kwa upendo wako
mpenzi basi nitaibadili usijari.
Nikakata simu na kwenda
kwenye mishe zangu. Ila
nikawaza sana kama yale mambo
ni upendo kweli au kuna vitu vya
ziada katikati hapa, nikaamua
kupotezea na kufanya mambo
mengine.
Nikarudi home nikiwa
nimejichokea hata nikaona uvivu
kwenda kutafuta msosi.
Nilipofika nikajilaza kitandani na
kujikuta nikipitiwa na usingizi
hapo hapo.
Nikaanza kuota nipo sehemu
nzuri sana na mchumba angu
huyo wa kitanga, tukienjoy na
kula raha tu.
Kulivyokucha nikaamka na
kwenda kuoga kama kawaida,
nakumbuka jana jioni nilikuwa
na elfu themanini kwenye wallet,
nikaichukua na kuicheki ile pesa
nakuta imebaki elfu thelathini
nikaanza kujiuliza elfu hamsini
imekwenda wapi. Mara yule binti
akawa anapiga simu,
BINTI: Mpenzi jana tulienjoy
eeh!!
MIMI: Aaaah, eeeh wapi tena?
BINTI: Si ndotoni mpenzi!!
MIMI: Kivipi mpenzi?
BINTI: Yani ndoto uliyoota wewe
usiku na mimi nimeota hivyo
hivyo.
Akakata simu bado nikawa
najiuliza juu ya upotevu wa pesa
yangu. Mara akanitumia sms
"usijari mpenzi, hiyo pesa
tumeitumia ndotoni"
Nikawaza sana juu ya upotevu wa
pesa yangu, nikajiuliza inakuwaje
mtu ufanye matumizi ya pesa
ndotoni? Likanijia wazo kuwa
yule binti si mtu wa kawaida.
Nikajishauri kwenda kupata
ushauri kwa rafiki yangu wa
karibu. Wakati natoka kwenye
chumba changu kuna sms
ikaingia kwenye simu yangu ila
nikaipotezea sikuisoma wala nini.
Nikaenda kwenye shughuli
zangu, badae nikaenda kwa
mshikaji wangu kumweleza kama
nilivyowaza. Nikamkuta na
tukapiga story mbili tatu badae
nikamweleza mambo yote.
MIMI: Ndio hivyo bhana.
RAFIKI: Aaah pole sana mshikaji
wangu ila nilikwambia kuwa
makini na Tanga, hata hivy
usipende kuwatongoza mademu
hovyohovyo sehemu yoyote ile.
MIMI: Sasa nishauri ndugu cha
kufanya.
RAFIKI: Cha msingi tumtafute
mtaalam twende, haya mambo ya
kishirikina kaka.
MIMI: Dah umenitisha kaka hata
kurudi kwangu naogopa.
RAFIKI: Usiogope wangu, wee
nenda tu ukiogopa atakushtukia
mapema.
MIMI: Dah sijui kama nitalala leo
kaka.
RAFIKI: Usijari kaka, cha msingi
potezea kama hujui kitu vile
halafu kesho twende kwa
mtaalam kaka.
MIMI: Poa kaka nashukuru
maana nishapagawa hapa.
Tukaagana pale halafu nikarudi
kwangu.
Nikiwa chumbani nikachukua
simu yangu kuikaguakagua
nikakuta missed call kibao na
sms moja nikashangaa hata
ilikuwaje sikusikia wakati inaita,
kumchek aliyekuwa anapiga ni
demu wangu wa Dar na ile sms
ni kutoka kwa binti wa kitanga,
iliandikwa "usijaribu kumweleza
yoyote juu ya habari zangu"
nikashtuka sana, ni hii sms
niliyoipotezea wakati naondoka
asubuhi. Mara simu ikaanza
kuita, kuangalia ni dada yangu
anapiga
MIMI: Hallow dada,http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
DADA: Mbona umekuwa na akili
fupi sana wewe? Unajua matatizo
aliyoyapata mchumba ako huku?
MIMI: Kwani kafanyeje tena
dada?
DADA: Muda wote amekupigia
simu hupokei, mwenzio yupo hoi
huku ule ujauzito umetoka.
MIMI: (Hata nilisahau kama
demu wangu wa Dar alikuwa na
mimba yangu) nini dada mbona
sikuelewi?
DADA: Huwezi kunielewa kwa
simu, kama unaweza njoo
hospitali au njoo nyumbani.
MIMI: Poa dada ngoja nijiandae.
Nikakata simu, nikaenda kuoga
na kuvaa fastafasta niondoke,
wakati nataka kutoka simu yangu
ikaanza kuita, kuitoa na
kuiangalia ni yule binti wa
kitanga.
BINTI: Unataka kwenda wapi?
MIMI: Aaah hapana siendi
popote.
BINTI: (Akacheka kidogo),
unataka kwenda wapi?
MIMI: Eeeh aaah nataka kwenda
kutafuta chakula.
BINTI: Haya rudi kakae, chakula
nitakuletea leo.
MIMI: (Huku nikiwa na hofu
moyoni), utaniletea kivipi?
BINTI: Kwani shida yako ni
chakula au ni nini? Kama ni
chakula sasa mashaka ya nini si
nimekwambia nitakuletea au?
MIMI: (nikaamua kujigeresha
kidogo), aaah Acha utani bhana
mpenzi wangu, unajua wazi upo
mbali sasa chakula utakiletaje?
BINTI: Nitakileta kwa hisia na
utashiba kabisa kwahiyo usitoke.
Akakata simu, nikaanza kuwaza
itakuwaje sasa na vipi kuhusu
kwenda hospitali nikawaza cha
kufanya, au niende halafu akipiga
nimwambie sijaenda? Bado
nikawa na utata moyoni.
Nikainuka pale nilipokaa na
kujipa moyo kuwa naenda tu hata
iweje. Nikaenda mpaka mlangoni
ile nataka kufungua mlango tu
sms ikaingia kwenye simu yangu,
kuangalia ni demu wa kitanga
"nimekwambia usitoke"
http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Nikakosa raha kabisa, nikarudi na
kukaa kitandani nikaamua
kujilaza nikitafakari, mara sms
ikaingia kwenye simu yangu
kuangalia ni yule binti wa
kitanga "angalia mezani
nimekuletea chakula"
Loh nikainuka kama nimepigwa
shoti vile, kuangalia naona juisi
ya Azam mango na biskuti,
nikawaza kuwa ameletaje vitu
vile nikaanza kupata mashaka,
mara sms nyingine ikaingia
"usiogope mpenzi, kula tu"
Nilikosa amani kwakweli,
nikasogelea ile juisi na kuiangalia
kama ni juisi kweli ndio ilikuwa
Azam mango kabisa na ndio juisi
niipendayo, mmh nikaziangalia
na zile biskuti zilikuwa biskuti za
ukweli kabisa zile zenye
mchanganyiko wa chokleti,
kutokana na njaa yangu nikaanza
kuvifakamia huku bado niliwaza
ameletajeletaje.
Nilipomaliza tu, akapiga simu.
BINTI: Vipi mpenzi umeshiba?
MIMI: Ndio nimeshiba, kwani
umeviletaje?
BINTI: Hata kushukuru hujui?
MIMI: Samahani mpenzi
nilijisahau.
Akakata simu, nikakaa na
mawazo pale kitandani. Mara
simu ikaita kuangalia ni dada
anapiga tena.
DADA: Vipi wewe yani huna hata
hofu na mwenzio?
MIMI: Aaah dada samahani.
DADA: Kwahiyo unakuja au huji?
MIMI: Aaah sijui dada.
DADA: Hujui nini? Nipe jibu
moja, unakuja au huji?
MIMI: Sitaweza kuja kwa leo
dada, nitakuja kesho.
DADA: Nilijua tu, mxyuuuu
(akanisonya na kukata simu).
Nikawa pale kitandani
nimejiinamia tu huku kichwani
mawazo mengi yamenitawala,
mara sms ikaingia kwenye simu
yangu
"si ulale mpenzi wangu jamani"
Nikaamua kujilaza huku nikijiona
bonge la boya maana nipo kama
vile mtu anayeongozwa na
rimote.
Mara usingizi ukanipitia pale
kitandani, nililala hadi
nikajisahau nikaja kushtushwa na
mlio wa simu.
RAFIKI: Vipi kaka mbona leo
hujatokea maeneo?
MIMI: Kivipi ndugu wakati ndo
kumekucha!
RAFIKI: (huku akinicheka),
kumekucha wakati saa kumi na
moja jioni hii?
MIMI: (nikafungua pazia na
kuchungulia dirishani, kumbe
kijua cha jioni ndio kipo
ukingoni), acha masikhara bhana
saa mbili hii (huku nikiangalia
saa yangu ya ukutani).
RAFIKI: (Akinicheka tena), wee
boya saa kumi na moja hii labda
kama leo una kazi ya ulinzi ndio
mida ya kujiandaa hii (akinicheka
tena).
MIMI: (Nikiangalia vizuri ile saa
ya ukutani, iliyoonyesha mshale
mdogo kwenye tano na mkubwa
kwenye nane), daah
nilichanganya mida kaka.
Nikakata simu na kuanza kuwaza
imekuwaje nimelala hadi
kujisahau vile, ni usingizi wa
namna gani ulinipata dah!! Mara
rafiki yangu akaanza kupiga tena.
RAFIKI: Kaka, vipi ule mpango
wa kwenda kwa mtaalam au
umepotezea?
MIMI: Hapana sijapotezea kaka,
nataka sana unipeleke itakuwaje
sasa?
RAFIKI: Wewe tu, nilitaka
nikupeleke leo au unaona yale
majanga yako ya kawaida kaka?
Kabla sijamjibu simu ikakatika,
na kuanza kuita tena kuangalia ni
binti wa kitanga.
BINTI: Ulikuwa unaongea na
nani?
MIMI: Rafiki tu mpenzi
wangu.http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
BINTI: Ulikuwa unaongea nae
kuhusu nini?
MIMI: Hamna kitu ni salamu tu.
BINTI: Unanificha sio?
MIMI: Hapana sijakuficha huo
ndio ukweli.
BINTI: Wee ni muongo eeh!! Haya
njia ya muongo fupi na mi naijua.
Akakata simu, nikabaki kwenye
maswali na viulizo vya kila aina.
Kwanza nikawaza juu ya usingizi
niliolala hadi kusahau kuamka
kwenda popote pia kusahau kula.
Nikajiuliza inamaana sijala
chochote tangu nilipokula juisi na
biskuti usiku. Mara sms ikaingia,
"usijari mpenzi kula na kuoga na
vyote vya muhimu umefanya
ndotoni"
Aaah majanga haya!!
ITAENDELEA
 
Sehemu Ya Pili (2)
Nikabaki nimeduwaa tu na
macho yamenitoka hata nisijue
cha kufanya kwa wakati ule.
Nikaamua kuinuka pale kitandani
na kujinyoosha nyoosha ila cha
kunishangaza sikuwa na njaa
kabisa.
Nikawa nimesimama huku
nikitafakari yale majanga, mara
simu yangu ikaita,
RAFIKI: Vipi wewe mbona
umenikatia simu bhana?
MIMI: Hapana sijakata, imejikata
yenyewe.http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
RAFIKI: Halafu wewe naona akili
yako imepinda. Haya vipi
itakuwaje, nikupitie kesho
asubuhi?
MIMI: (nikiwa bado sijiamini
amini kama siku imeisha kweli),
aaah eeh haya poa basi.
RAFIKI: Mbona hueleweki
unajiumauma tu, au hutaki?
Niambie bhana.
MIMI: Hapana sio kama sitaki.
RAFIKI: Ila nini sasa? Ongea
bhana mtoto wa kiume acha
kujiumauma hapo.
MIMI: Aah sijui bhana
Nikajikuta nimekata ile simu,
hata nilikuwa sijielewi kabisa.
Mara dada akawa anapiga
DADA: Yani mdogo wangu siku
hizi kweli umekuwa shetani, toka
asubuhi hadi muda huu
unashindwa hata kutujulia hali?
Yaonyesha umefurahishwa sana
na yaliyo mpata mwenzio.
MIMI: Samahani dada, naomba
mnisamehe sana sio kusudio
langu.
DADA: Ila ni kusudio la nani?
MIMI: Sijui dada.
DADA: Hivi wewe una kichaa au?
Nikakata simu kwani naona
wananichanganya tu na wakati
sijielewi kabisa.
Nikakaa chini na kujiinamia huku
nikipanga mipango kuwa
niondoke mahali hapo hata
nikalale nje ili nisipitilize tena.
Mara simu ikaita,
BINTI: Mambo mpenzi,
nimekumiss.
MIMI: (hapo natamani hata
kumtukana), poa tu hata nami
nimekumiss pia.
BINTI: Unaonaje leo twende
tukatembee mpenzi?
MIMI: (huku nimejawa na
hasira), unajua usinichanganye
wewe! Tukatembee vipi wakati
tuko mbali mbali?
BINTI: Ndio unanikaripia eeh!
MIMI: (Nikawa mpole tena),
hapana mpenzi nisamehe.
BINTI: Sijazoea kukaripiwa,
umeniudhi sana.
Akakata simu, dah nikapagawa
zaidi. Nikainuka tena na kwenda
hadi mlangoni ili nifungue
mlango nitoke. Mara simu ikaita,
BINTI: Unaenda wapi?
MIMI: Aaaah eeeh mmh!
BINTI: Unakwenda wapi?
MIMI: Aah maswali gani tena
hayo?
BINTI: Wewe kiburi eeh!
MIMI: (nikiwa na hasira na
mimi), niache bhana nikapunge
upepo nje.
BINTI: Kumbe wewe ni kiburi na
jeuri!!
MIMI: Ndio mambo gani hayo
jamani mpenzi?
Akakata simu, nikiwa bado
nimesimama pale mlangoni
akanitumia sms
"huendi popote"
Nikajikuta nikiwaza mambo
mengi, mara dada akaanza
kupiga tena.
DADA: Vipi na leo unakuja au
huji?
MIMI: Aaah daah sijui bhana.
DADA: Hivi mdogo wangu una
nini wewe?
MIMI: Sielewi kitu dada.
DADA: Uko wapi sasa hivi?
Ile nataka kumjibu simu
ikakatika, kuichek eti imeisha
chaji nikaamua kwenda
kuichomeka kwenye chaji, huku
mawazo mengi kichwani yakiwa
yamenitawala. Nilipokaa kidogo
nikaiwasha tena na hapo
nikakutana na sms kutoka kwa
binti wa kitanga,
"nimekwambia leo huendi
popote, utakula jeuri yako"
http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Nilikosa raha kwakweli
nikatamani hata nipae
niondokane na hayo majanga.
Nikajiuliza kuwa huyu binti ana
mamlaka gani ya kunizuia mimi
nisitoke? Nikajipa moyo na
kujipigapiga kifuani huku
nikisema, mimi kidume bhana
nitatoka tu. Mara akanipigia simu
tena, nikaitoa pale kwenye chaji
na kupokea.
BINTI: Unasemaje mpenzi?
MIMI: Mbona sijasema chochote.
BINTI: (Akacheka sana halafu
akakata simu).
Nikaamua kuirudisha simu
kwenye chaji, huku kichwa
changu kikiwa kama
kimevurugika.
Nikainuka na kwenda kufungua
mlango ila ukawa mgumu
kufunguka, nikasikia mlio wa sms
nikarudi kuisoma,
"hivi nilivyokwambia kuwa leo
huendi popote ulijua masikhara?"
Nikaiangalia ile sms mara tatu
tatu, nikaona huyu mwanamke
anacheza na akili yangu sasa.
Nikiwa nimejawa hasira
nikachukua simu na kumpigia ila
haikupokelewa, nikapiga tena
haikupokelewa na tangu
nimerudi Dar huyu binti
amekuwa na kawaida ya
kutokupokea simu zangu.
Nikachukia sana, hasira
zikanizidi. Nikainuka tena kwa
hasira nikaenda mlangoni na
kuusukuma mlango lakini
haukufunguka. Nikawa
nimepatwa na joto la hasira huku
jasho jingi likinitoka, nikarudi na
kukaa kitandani mara sms
ikaingia kwenye simu,
"pole kwa joto mpenzi"
Nikazidi kupandwa na hasira hata
nisijue cha kufanya, nikachukua
tena simu ili nimpigie rafiki
yangu kabla sijapiga simu yangu
ikaanza kuita.
BINTI: Unataka kumpigia nani?
MIMI: Nimekupigia simu
hujapokea ila nikitaka kumpigia
mtu ndio unajua?
BINTI: Nijibu kwanza unataka
kumpigia nani?
MIMI: Rafiki yangu tu.
BINTI: Ulitaka kumwambia nini?
MIMI: (Nikiwa na hasira), unajua
nimechoshwa na maswali yako?
BINTI: Umechoshwa na maswali
sasa ulipokuwa unanipigia ulitaka
nini?
Akakata simu, dah huyu binti
nilitamani hata kumtukana
matusi yote ya dunia.
Njaa ikanianza, nikawa nawaza
sasa nitatoka vipi kwenda
kununua chakula. Simu ikaita,
BINTI: Vipi una njaa eeh!!
MIMI: (Hapo natamani
kumtukana), unauliza majibu?
BINTI: Kwahiyo unatakaje?
MIMI: Nataka kwenda nje
kununua chakula.
BINTI: Leo hutoki ila chakula
nitakuletea.
MIMI: Dah!! Kwanini unanifanyia
hivyo lakini?
Akakata simu, nikawa ni mtu
mwenye mawazo. Nikainuka tena
na kwenda kufungua mlango
bado ulikuwa mgumu, mara dada
nae akaanza kupiga simu
DADA: Uko wapi lakini? Si
ulisema utakuja leo yani huwezi
amini mwenzio kazidiwa vibaya
sana huku.
MIMI: (nikajikuta naropoka tu),
Sasa jamani dada, kwani mi ndio
daktari?
DADA: Unasemaje wewe?
MIMI: Aah samahani dada ulimi
umeteleza.
DADA: Endelea na hiyo tabia
yako tu.
Akakata simu. Nikawaza sana
kuwa imekuwaje hadi nimemjibu
dada vile. Mara sms ikaingia
"umemjibu vizuri sasa dada yako,
hongera mpenzi"
Aah nikazidi kupatwa na hasira,
mara akanipigia simu
BINTI: Nikuletee chakula gani leo
mpenzi wangu?
MIMI: Niletee chakula kizuri cha
kushiba.
BINTI: Haya usijari, nitakuletea
mpenzi.
Akakata simu nikashangaa
imekuwaje hata nikamjibu vizuri
vile wakati nina hasira nae.
Nikawa bado na mawazo nikaona
sms kwenye simu,
"angalia mezani mpenzi"
kuangalia, dah kaniwekea
vyakula vya kila aina, kutokana
na njaa yangu uroho ukanijaa.
Nikasogea pale mezani na kuanza
kula, nilipomaliza akanipigia
simu.
BINTI: Hata kunikaribisha
mpenzi?
MIMI: Aah mmh nilisahau
mpenzi, samahani.
BINTI: Usijari sana, vipi
umeridhika nacho lakini?
MIMI: Ndio nimeridhika mpenzi,
ila umekiletaje?
BINTI: Nimekileta kwa hisia
mpenzi, vipi unataka kuoga?
MIMI: Ndio nataka kuoga mpenzi.
BINTI: Haya ngoja kidogo
mpenzi.http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Akakata simu, Nikawa kama mtu
aliyepigwa bumbuwazi nilikuwa
nikingoja huko kuoga kwa hisia
nako kutakuwaje.
Nikawaza pale ndani huku
nikingoja huko kuoga kwa hisia.
Mara akanipigia simu,
BINTI: Mpenzi upo tayari kuoga?
MIMI: Ndio mpenzi nipo tayari.
BINTI: Haya vua nguo zako zote.
Akakata simu, hofu kubwa
ikanitanda moyoni nikawaza
kama nivue kweli nguo au la,
nikiwa bado naendelea kuwaza
akanitumia sms "vua basi ukaoge
mpenzi"
Bado nikawa nawaza tu,
akanipigia simu
BINTI: Kwani unaogopa nini
mpenzi?
MIMI: Hapana siogopi kitu ila
naomba kesho ndio nioge kwa
hisia mpenzi.
BINTI: (Akacheka sana), kwanini
umeghairi mpenzi?
MIMI: Hapana mpenzi ila
sijajisikia kuoga usiku huu.
BINTI: Haya usijari mpenzi.
Akakata simu, nikawa nimekaa
huku nikipanga mipango ya
kesho tu kwenye kichwa changu.
Nikiwa ndani ya mawazo rafiki
yangu akinipigia tena simu,
RAFIKI: Kesho nitakuja kukufata
hapo kaka twende ile sehemu.
MIMI: Poa kaka.
Alipokata tu simu nyingine
ikaingia
BINTI: Mwambie huyo rafiki yako
aache kabisa kujihusisha na
mambo haya atapotea.
MIMI: Mbona sikuelewi?
Akakata simu, nikazidi kupagawa
kwa mawazo hata nisijue cha
kufanya kwa wakati huo. Mara
taa ya chumbani kwangu
ikazimwa kukawa na giza na
utulivu uliopitiliza, nikaanza
kuogopa huku nikitamani kupiga
kelele lakini nikashindwa
kufanya hivyo nilikiona chumba
kikiwa kikubwa sana, jasho la
uwoga likaanza kunitoka nililowa
mwili mzima kama
nimemwagiwa maji. Mara taa
ikawashwa tena na simu ikaanza
kuita,
BINTI: Kumbe wewe ni muoga
sana eeh!
MIMI: Aaah mmh kiasi tu sio
sana.
BINTI: Kukuzimia taa tu jasho
limekutoka kama unakimbizwa,
nikikufanyia mengine je?
MIMI: hapana usinifanyie vibaya
mpenzi.
Akakata simu na kupiga tena,
BINTI: Ooh mpenzi nimesahau, je
utapenda tukatembee leo?
MIMI: Aah hapana mpenzi,
tutaenda siku nyingine.
BINTI: Kwanini jamani mpenzi?
http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
MIMI: Hamna sababu mpenzi ila
tutaenda siku nyingine. Naomba
kesho uniamshe mpenzi.
BINTI: Sawa usijari, umekuwa
muelewa sasa mpenzi
nimefurahi. Ila nakuomba
tukatembee.
Akakata simu ilinibidi niwe
mpole na nijifanye kuwa
nafurahia vyote anavyonifanyia
huku akili yangu kichwani
ikiwaza mambo mbali mbali
ikiwemo namna ya kumuepuka
binti huyo.
Nilikuwa nikijigeuza geuza tu
pale kitandani huku mawazo
mengi yakinitawala.
Mara simu yangu ikaita,
BINTI: Mpenzi leo hulali?
MIMI: Nitalala tu mpenzi si
utanishushia neti?
BINTI: Dah nafurahi umenikubali
mpenzi, nitakushushia usijari.
Akakata simu, nami nikajilaza
pale kitandani. Nikaota ndoto
kuwa nipo sehemu nzuri sana na
yule binti.
Asubuhi kulipokucha, yeye akawa
wa kwanza kunipigia simu.
Nikaamka na kwenda kuoga
nikarudi na kujiandaa ili nitoke,
mara dada akaanza kunipigia,
DADA: Mdogo wangu tafadhari
tunahitaji pesa kidogo kwaajili ya
kuongezea kulipia hospital na
vitu vingine.
MIMI: Hakuna shida dada, kwani
mnataka kiasi gani?
DADA: Ungetuma kama elfu
thelathini hivi.
MIMI: Sawa natuma sasa hivi
kwa njia ya simu.
Nikakata simu na kuanza kutuma
pesa, nikafata muamala mzima ila
badae naletewa sms kuwa salio
halitoshi kuhamisha kiasi cha
pesa ninachotaka.
Nikaamua kuangalia salio duh
nikakuta eti imebaki mia tano.
Nikajisemea 'hata sikubali hawa
wendawazimu washaniibia hela
yangu kwenye simu yani laki
mbili na nusu imebaki mia tano
sikubali lazima niwafatie huko
makao makuu'http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
nilikuwa naongea kwa jazba
huku nikiangalia lile salio mara
mbili mbili bila hata ya kuamini
kama hela yangu imekatwa na
mtandao kama kawaida ya wizi
wao au ni vipi.
Nikaanza kutoka ndani nikiwa na
jazba za mtandao ule, mara
akanipigia simu
BINTI: Mbona una hasira sana
mpenzi?
MIMI: Si hawa wapumbavu wa
mtandao wameniibia pesa yangu.
BINTI: Hawajakuibia bhana.
MIMI: Kama hawajaniibia pesa
yangu yote imekwenda wapi?
BINTI: Ngoja nitakwambia.
Akakata simu, nikiwa bado
nimesimama pale mlangoni huku
nina uchungu na hasira ya pesa
yangu, mara akanitumia sms
"mpenzi, ulivyoshinda ndani jana
na juzi ulifikiri unahudumiwa
kwa pesa ya nani? Na tulipoenda
kutembea usiku je? Pesa yako
imetumika kwenye kukuhudumia
kwahiyo usilaumu mtandao, hiyo
pesa umeitumia mwenyewe"
 
Sehemu Ya Tatu (3)
Nikiwa bado na mawazo,
nikasikia sauti ya mama na dada
nje ina maana nao wamefika
kwangu. Nikajihisi baridi
ikipenya mwilini mwangu,
nilikuwa nikitetemeka balaa.
Sikuwa na raha wala furaha.
Mara sms ikaingia kwenye simu
yangu,
"yote yale yalikuwa ni majaribio
sasa picha kamili itaanza."
Nikapatwa na hofu kubwa
moyoni, sikuwa na furaha
kwakweli. Nikahisi mama na
dada wakizidi kusogelea mlango
wangu, wakaanza kubisha hodi
huku wakiniita jina langu
sikutamani kuitika kwakweli
nilijiona na mtu mwenye mkosi
pale ndani, mama alizidi kubisa
kuwa nifungue na nisipofanya
hivyo atapiga kelele ili watu waje
kubomoa mlango, aliposema
hivyo nikahisi kupagawa kabisa
kwani yule binti alinambia kuwa
nikipiga kelele basi atauondoa
kabisa uhai wa wale waliopoteza
fahamu mule ndani, nilipofikiria
hayo nikaenda mlangoni na
kuwafungulia mlango. Baada ya
kuwafungulia tu wakaingia moja
kwa moja ndani nami
nikaurudishia mlango,
MAMA: Mungu wangu,
umemfanya nini kaka yako?
(huku akimfata pale chini na
kumtingishatingisha).
MIMI: (Huku nikitetemeka),
hapana mama sijamfanya
chochote.
DADA: Hivi una akili wewe? Yani
wenzio wanatapatapa humu
ndani na wewe umetulia kabisa
kana kwamba hakuna
kilichotokea.
MIMI: Dada sielewi kitu.
Mama akiendelea kumwamsha
kaka pale chini huku akijisemea,
"jamani mwanangu, sijui
amekufa".
Mama ndio alikuwa hajielewi
kabisa bora hata ya dada, mara
yule binti akanipigia simu,
BINTI: Mwambie mama asilie.
MIMI: Usinichanganye ujue!
Wewe ndio umesababisha yote
haya.
BINTI: Mpe simu mama
nimueleweshe tafadhari.
MIMI: Hapana, naogopa nae
utamfanya kama hawa.
BINTI: Unampenda mama yako?
MIMI: Ndio nampenda.http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
BINTI: Ok mpe simu niongee
naye.
Nikiwa bado sina maamuzi sahihi
nikawa nimeganda na ile simu
sikioni, dada akauliza
DADA: Kwani nani huyo?
MIMI: Eti anataka kuongea na
mama.
DADA: Mpe basi mama aongee
naye.
Nikampa mama simu, naye
akaweka sikioni akiwa kakaa pale
chini nikamwonga akiangukia
pale pale, dada akapiga ukelele
wa ajabu huku akimwita mama
"mama mama mamaaaa".
Ilikuwa ni kitendo cha gafla dada
nae akaichukua ile simu na
kuiweka sikioni nahisi alitaka
kujua ni nani huyo aliyeongea na
mama, kufumba na kufumbua
nae akawa chini akitapatapa.
Nilizidi kuchanganyikiwa
kwakweli, na mimi nikachukua
ile simu na kuiweka sikioni labda
na mimi kinipate kilichowapata
wenzangu ili nisiwe na ufahamu
tena, ila nilipoiweka sikioni
nikimsikia yule binti wa kitanga
akicheka sana,
MIMI: Umewafanya nini ndugu
zangu?
BINTI: Unataka kujua
nilichowafanya?
MIMI: Ndio niambie umewafanya
nini?
BINTI: Haya tazama hapo chini.
Halafua akakata simu, kuangalia
pale chini hakuwepo mtu yeyote,
wote walitoweka. Nikapagawa
hakuna mfano nikahisi kurukwa
na akili mule ndani, nikataka
kwenda nje na kukimbia, simu
ikaita tena,
BINTI: Usithubutu kwenda
popote kama bado unawapenda
ndugu zako.
MIMI: Unajua sikuelewi wewe?
Yani sikuelewi kabisa, unamaana
gani kunifanyia mambo haya?
BINTI: (Akacheka sana), maana
yangu utaijua tu ila Kama
unawapenda ndugu zako hawa,
usiende popote pale.
Akakata simu, nikazidi kurukwa
na akili mule ndani.
nakufa jamani, ama aliyesema
kufa hufi ila chamoto utakiona
wala hakukosea. Niliungua sana
mule pipani, mara kuna mtu
akaja kuniopoa kumwangalia ni
yule yule mtoto wa kitanga,
akawa anacheka sana.
BINTI: Vipi umejisikiaje hapo?
Nikataka kumjibu ila nashangaa
sikuweza kufanya hivyo kwani
mdomo ulikuwa mzito sana,
akaniambia tena,
BINTI: Nina uhakika kama
ukipona na haya nikufanyiayo
hutorudia tena kubeba mizigo
ovyo ovyo. (akacheka sana na
kutoweka).
Nikawa natetemeka mahali pale
ila kilichonishangaza ni kuwa
nimechemka kwenye lile pipa
halafu sijababuka mwili, mara
akaja yule mtu aliyeniongoza
mwanzo na kunishika tena
mkono kunipeleka sehemu
nyingine.
Tukaingia chumba ambacho
akaniacha mimi peke yangu na
yeye akatoka, yani chumba
kilikuwa na siafu wengi sana
walining'ata kila sehemu ya
mwili wangu hadi nikajihisi
mwili unakufa ganzi kwakweli ni
maumivu yaliyopitiliza.
Baada ya muda akaja na
kunifungulia nikatoka mule ndani
nikiwa na madonda ya kila aina.
Akaniuliza,
"unapenda sana
wasichana?"http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Nikatikisa kichwa nikiashiria
hapana. Akanichukua na
kunipeleka sehemu nyingine.
Tulifika sehemu ambayo mbele
yake kuna wasichana wazuri sana
tena wa kuvutia, yule mtu
akanigeukia na kuniambia,
"kijana chagua mmoja hapo"
Nikakataa kwa kichwa kuwa
simtaki yeyote, sikuwa na hamu
na msichana yeyote kwakweli,
yule mtu akaniambia tena,
"inamaana huwaoni walivyo
warembo wale mabinti?"
Nikatingisha tena kichwa
kuonyesha kwamba siwataki wale
wasichana.
Tukaondoka mahali hapo,
nikapelekwa sehemu ambayo
nilikuta wanaume wenzangu
wamepanga foleni halafu kuna
mtu mmoja mbele ana panga
kubwa sana yani ukimkaribia
anakuchinja kama kuku dah
nilihisi kupagawa nikatamani
kukimbia ila sikuweza, yani yule
mtu hakuwa na huruma kabisa
kila aliyemfikia alimchinja kama
kuku na mimi nikawekwa
kwenye huo mstari.
Niliona mwisho wangu
umekaribia, nikamaliza sala zote
kimoyomoyo nikajikuta nikitubu
kila aina ya dhambi niliyotenda,
machozi yalinibubujika kila hatua
niliyomsogelea yule mtu,
nilijikuta nikilia kama mtoto
mdogo sikuwa na jinsi zaidi ya
kujisogeza ili nikabidhi kichwa
changu iwe halali yao.
Nikakosa raha kwakweli,
nikachukia moyoni na kuwaza
mwisho wa mambo haya ni lini.
Mara dada akanipigia,
DADA: Vipi tena mbona hutumi
hiyo pesa?
MIMI: Aaah mmmh kuna tatizo
kidogo dada ngoja nitatuma
badae.
DADA: Nilijua tu mxyuuuu
(akanisonya).
Akakata simu, bado akili yangu
haikuwa sawa hadi pale mlango
wangu ulipogongwa, nikaenda
kufungua kumbe ni rafiki yangu
alikuja kama alivyoniahidi jana.
RAFIKI: Vipi upo tayari
tuondoke?
MIMI: Ndio nilikuwa nataka
kutoka hapa kaka.
RAFIKI: Basi twende.
Mara simu yangu ikaita, nami
nikaipokea,
BINTI: Mwambie rafiki yako
aache kufatilia mambo yangu.
MIMI: Kivipi jamani mpenzi?
BINTI: Inamaana hujui rafiki yako
amefata nini?
MIMI: Hapana sijui.
BINTI: Hivi unajua kama
ninaouwezo wa kuwazuia
msitoke hapo?
MIMI: Kwani vipi mpenzi mbona
sikuelewi?
BINTI: Mpe rafiki yako simu
nimuulize kitu.
Nikampa rafiki yangu simu ili
aongee na yule binti, kilikuwa ni
kitendo cha kufumba na
kufumbua yani baada ya
kumkabidhi simu rafiki yangu ili
aongee naye nikashtukia rafiki
yangu akianguka chini na povu
jingi likimtoka mdomoni, moyo
ukanipasuka kwakweli nilijikuta
nikitetemeka na kuona baridi ila
jasho jingi likinitoka. Kwakweli
nilichanganyikiwa nilitamani
ardhi ipasuke nidumbukie.
Nilimwangalia rafiki yangu pale
chini akiwa katulia tuli hata
nisijue cha kufanya, nikatamani
kupiga yowe la msaada.
Nilipotaka kufanya hivyo, simu
yangu ikaita
BINTI: Usithubutu kupiga kelele
kama unapenda kumuona rafiki
yako akiendelea kupumua.
MIMI: Nihurumie tafadhari
nakuomba nihurumie.
BINTI: (Akacheka sana).
Akakata simu, mapigo ya moyo
yalikuwa yananienda kwa kasi
balaa.
Sikujua msaada gani nimpe rafiki
yangu pale chini. Nikainama na
kujaribu kumuinua ili nimuweke
kitandani ila alikuwa mzito kama
jiwe tena alizidi kukoroma na
povu jingi likimtoka mdomoni.
Hofu ikazidi kutanda moyoni
mwangu na mawazo mengi
yakinitawala huku nikiomba sala
zote ili nikomboke na lile janga.
Nikakaa pale chini karibu na
rafiki yangu, nikatamani
nichukue simu na kuwapigia
watu ili niombe msaada ila
nikasita kufanya hivyo.
Nikajifikiria tena, ikabidi
nichukue simu nimpigie kaka.
MIMI: Hallow kaka nina matatizo
tafadhari njoo nyumbani kwangu.
KAKA: Kwani vipi tena mdogo
wangu?
MIMI: Tafadhari kaka njoo.
KAKA: Poa nakuja mdogo wangu.
Nikawa na matumaini ya kupata
msaada sasa.
Mara kidogo yule binti akanipigia
BINTI: Aliyekutuma umpigie kaka
yako simu nani?
MIMI: Aaah eeh sijui hata sielewi.
BINTI: Unampenda kaka yako?
MIMI: Ndio nampenda.
BINTI: Kama unampenda mpigie
tena simu sasa mwambie asije.
MIMI: Itakuwaje sasa?
BINTI: Fanya kama
nilivyokwambia.
Akakata simu, hata sikujielewa
kwakweli nikachukua simu na
kumpigia tena kaka lakini namba
yake ikawa inaita tu bila ya
kupokelewa.
Baada ya muda kupita kupita,
kaka akanipigia simu.
KAKA: Nakaribia kufika mdogo
wangu, naona missed call yako
hapa vipi ulikuwa unasemaje?
MIMI: Nilikuwa nakwambia basi
tena usije.
KAKA: Hebu acha ujinga wako
huo, nimetoka haraka haraka
nyumbani halafu unasema nisije
tena! Mi nakuja.
MIMI: Dah usije kaka, tafadhari
usije.
KAKA: Kwani kuna nini wewe?
Nakuja bhana.
Akakata simu, nikawa ni mtu
mwenye mawazo hata nisijue cha
kufanya tena muda ule huku
nikihofia maisha ya kaka yangu.
Nikamwangalia tena rafiki yangu
pale chini, nikamfikiria na kaka
yangu anaekuja nguvu ziliniisha
kabisa. Mara akanipigia simu,
BINTI: Umeshindwa kabisa
kumzuia kaka yako kuja hapo?
MIMI: Nimeshindwa, nihurumie
tafadhari.
BINTI: Nitakachokifanya
usinilaumu badae.
MIMI: Jamani nihurumie,
nihurumie nakuomba.
BINTI: Huruma yangu utaiona
akifika kaka yako mahali hapo.
Akakata simu, nikawa kama mtu
aliyepagawa. Nikachukua simu na
kumpigia dada,
MIMI: Tafadhari dada nakuomba
umzuie kaka asije kwangu.
DADA: Kwani kuna nini?http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
MIMI: Hamna kitu ila mzuie.
DADA: Una matatizo gani wewe??
Na mimi nakuja huko nijue
kinachoendelea.
MIMI: Mungu wangu, dada
nakuomba usije.
DADA: Khaaa, nakuja sasa.
Akakata simu, nikazidi
kuchanganyikiwa nilitamani hata
nipae nitokana na haya
maswahibu.
Yule binti akanitumia sms,
"ndugu zako wanacheza na moto"
ITAENDELEA
 
Sehemu Ya Nne (4)
Nikajihisi kama kupagawa hivi na
wala sikujua cha kufanya kwa
muda ule. Mara mlango
ukagongwa,
MIMI: Nani wewe?
KAKA: Mimi hapa kaka yako.
MIMI: Kaka si nimekwambia usije
tena jamani!
KAKA: Acha masikhara wewe,
hebu nifungulie mlango.
MIMI: Hapana kaka, wee nenda
tu.
KAKA: Kwani una nini wewe?
Hebu fungua huko.
Kaka akawa anasukuma sukuma
mlango, ikabidi niinuke na
kwenda kufungua mlango, kaka
akaingia ndani moja kwa moja
nami nikaurudishia mlango.
KAKA: Hiki ndicho ulichokuwa
unanikataza nisiingie ndani,
umemfanyaje mwenzio?
MIMI: Sijamfanya kitu kaka.
KAKA: Sema ukweli mdogo
wangu, umemfanyaje huyu?
MIMI: Sijui kaka ameanguka
mwenyewe.
KAKA: Aaah acha masikhara
bhana, ataangukaje mwenyewe?
Fanya fasta tumpeleke hospitali.
MIMI: Haitawezekana kaka.
KAKA: Haitawezekana kivipi
bhana? Hebu njoo tuite msaada
hapo nje tumbebe tumpeleke
hospitali.
MIMI: Unajua nini kaka....(kabla
sijajibu vizuri, simu yangu
ikaanza kuita)
Nikaipokea ile simu,
BINTI: Kaka yako anataka kujua
kilichompata rafiki yako?
MIMI: Ndio.
BINTI: Mpe simu nimweleze
mwenyewe.
Nikampa simu kaka ili aongee
nae ila kabla ya kuongea
akaniuliza,
KAKA: Kwani ni nani?
MIMI: Wee ongea naye tu.
KAKA: Nitaongea vipi na mtu
nisiyemfahamu?
MIMI: Ongea naye tu kaka.
Kaka akachukua ile simu, ikawa
ni kitendo cha sekunde tu kwani
kaka alianguka chini kama gunia
huku jasho jingi likimtoka na
macho akiwa ameyatoa tu,
nikaanza kupatwa na uoga kwani
kaka hakuongea chochote.
Nikajiuliza yule binti kawafanya
nini wale hadi hawajitambui
tena. Roho ikawa inaniuma sana
hata sikujua cha kufanya kwa
muda ule kwakweli nilihisi
kuchanganyikiwa kabisa
nikatamani nichimbe shimo
nijifukie.
Nikiwa bado natafakari yale
yaliyopo, mlango wangu
ukagongwa tena kwa nguvu.
MIMI: Nani wewe unagonga kwa
nguvu hivyo?
DADA: Mimi hapa
MIMI: Wewe nani ndio? (kana
kwamba nimeisahau sauti yake)
DADA: Dada yako ina maana
huijui sauti yangu?
MIMI: Nenda tu dada.
DADA: Vipi tena jamani?
MIMI: Weee nenda tu bhana.
DADA: Niende wapi jamani
mdogo wangu wakati nimekuja
kwako?
MIMI: Nenda bhana, sitaki
mgeni.
DADA: Kwani kaka yuko wapi?
MIMI: Sijui bhana, wee nenda.
DADA: Unajua unanichanganya
wewe, unachogoma kunikaribisa
humo ndani ni nini?
MIMI: Nenda bhana mbona
huelewi wewe?
DADA: Ok, ngoja nikamchukue
mama nije nae ili tujue
unachoficha humo.
MIMI: Usifanye hivyo dada, dada
dada (kimya alikuwa
ameshaondoka).
Nikazidi kupagawa sasa dada
ameenda kumchukua mama si
balaa hili litanipata jamani mimi
dah.
Yule binti akanipigia tena simu,
BINTI: Ndugu zako wanajua
kufatilia mambo eeh?
MIMI: Sikuelewi jamani
sikuelewi.
BINTI: Hunielewi eeh!! Ngoja
utanielewa wakifika hao ndugu
zako.
MIMI: Tafadhari usiwatende
vibaya.
BINTI: Wameyataka wenyewe, na
watanijua vizuri mtoto wa
kitanga.
MIMI: Jamani jamani nakuomba
tafadhari usinifanyie hivyo.
BINTI: Si nilikwambia uwakataze
umeshindwa? Sasa ndio utajua
vizuri leo.
Akakata simu nikabaki kupagawa
tu na wala nisijue la kufanya.
Nilijihisi kama vile mtu
aliyechanganyikiwa.
Usiku ukawa umeingia na masaa
nayo yakizidi kuyoyoma. Ikawa
saa sita usiku mara simu yangu
ikaita kuangalia imeandikwa
shemeji1, kumbe ni mke wa kaka
ananipigia maana yeye ndiye
nilimsave shemeji1.
MKE WA KAKA: Shemeji, kaka
yako alisema anakuja huko, vipi
mbona hajarudi hadi sasa?
MIMI: Aaah mmh shemeji
kulikuwa na tatizo kidogo ila
atarudi tu.
MKE WA KAKA: Atarudi muda
gani jamani shemeji, ujue hii ni
saa sita jamani.
MIMI: Atarudi tu.
MKE WA KAKA: Nakuja
hukohuko, hata msinitanie kwa
kufichiana maovu.
MIMI: Usije bhana atarudi.
MKE WA KAKA: Nakuja.
Akakata simu, baada ya muda
kidogo nikasikia muungurumo
wa boda boda nje. Mara mlango
ukaanza kugongwa kuwa
nimfungulie. Sikuwa na jinsi
nikamfungulia,
MKE WA KAKA: Eeh mume
wangu yupo wapi? Nilijua tu
kuna mambo mnanificha nyie
bora nimekuja kuyashuhudia
mwenyewe.
MIMI: Hapana shemeji sio hivyo
unavyofikiria.
MKE WA KAKA: Wee usinitanie
kabisa, niambie ukweli. Yani
unamwona kaka yako akitenda
ufirauni halafu unajifanya
kumtetea.
Mara simu yangu ikaita,
BINTI: Anataka nini nae huyo?
MIMI: Anamtaka mumewe.
BINTI: Mpe simu niongee naye.
MIMI: Hapana siwezi kukupa
uongee naye.
Mara mke wa kaka akadakia,
MKE WA KAKA: Kwani nani
huyo?
MIMI: Eti anataka kuongea na
wewe.
MKE WA KAKA: Sasa si unipe
niongee nae jamani.
MIMI: Hapana shemeji, siwezi
kukuruhusu uongee naye.
Shemeji akanipora ile simu na
kuiweka sikioni ili aongee nae,
muda huo huo nae akaanguka
chini na kutapatapa, ikawa sasa
kama yale matukio
nimeshayazoea.
Yule binti akanipigia tena simu,
BINTI: Unaupenda mchezo
wangu?
MIMI: Aah usinichanganye
bhana.
BINTI: (Akacheka sana), angalia
tena chini.
Akakata simu, kuangalia akawa
amewarudisha wale watu wote,
nikazidi kutetemeka hata nisijue
cha kufanya.
Ilikuwa hakuna kulala wala kula
wala kufanya chochote.
Kulipokucha nikashtuliwa na
simu ya mke wa rafiki yangu.
SHEMEJI: Vipi shemeji jana
hamkufanikiwa?
MIMI: Kumbe alikwambia jamaa,
hatukufanikiwa.
Mara akakata simu, nikasikia
simu ya rafiki yangu ikiita kwa
mara ya kwanza toka mfukoni
mwake. Nikaichukua ile simu
alikuwa ni yule yule shemeji.
SHEMEJI: Nasikia kuna matatizo
huko.
MIMI: Aaah hapana, kwani nani
kakwambia?
SHEMEJI: Nina mdogo wangu ana
marhani ndio kasema.
MIMI: Aaah kakudanganya huyo.
SHEMEJI: Unajua kwanini
nimekata ile simu yako na kupiga
huku?
MIMI: Kwanini?
SHEMEJI: Ngoja tuje
tutakwambia.
MIMI: Tafadhari msije jamani
sitaki matatizo mengine.
Akakata simu, nikiwa bado ni
mtu mwenye mawazo, mara yule
binti akapiga simu yangu.
BINTI: Umenikera sana, nani
kakutuma upokee simu nyingine?
MIMI: Jamani kwani na hilo
siruhusiwi?
BINTI: Ngoja nikuonyeshe tena.
Akakata simu, nikawa
nimeshikwa na bumbuwazi kuwa
yule binti anataka kunionyesha
mbwembwe gani hizo tena...
Nikawa sijielewi kabisa nikajihisi
akili yangu kama ikiniruka hivi,
nikazidi kuwaza na kuwazua bila
ya kupata jibu la maana.
Mara gafla giza nene likatanda
pale chumbani, nikazidi kukosa
amani moyoni mwangu, mara
kuna kitu kikaja na kunikaba
kooni nikaanza kutapatapa na
kuhangaika kama kwa dakika
kadhaa ile hali ikatoweka na
mwanga ukarudi tena mule
ndani. Mara yule binti akanipigia
simu,
BINTI: Unajisikiaje mpenzi?
MIMI: Najisikiaje nini wakati
umeniumiza wewe?
BINTI: Pole mpenzi.
MIMI: (Nikamjibu kwa ukali),
pole yako haisaidii bhana.
BINTI: Kwahiyo unanikaripia eeh!
MIMI: Hapana sijakukaripia
bhana.
Akakata simu, nikazidi kupatwa
na hasira kila nikiwaangalia wale
ndugu zangu pale chini nakosa
raha na pia nazidi kukosa amani.
Nikakaa nikajifikiria nikachukua
simu na kumpigia yule binti ila
hakupokea baada ya muda
akanipigia yeye,
BINTI: Eeh unasemaje?
MIMI: Tafadhari kuwa na
huruma japo kidogo jamani, ona
umetufungia humu toka jana na
hatujala chochote.
BINTI: Kwahiyo shida yako ni
chakula tu?
MIMI: Hapana sio chakula tu ila
nataka uwazindue hawa watu.
BINTI: (Akacheka sana), chakula
utakipata ila kuwazindua hao sio
kazi yangu.
MIMI: Nihurumie tafadhari.
BINTI: Fumba macho.
MIMI: (Nikafumba kama
alivyoniamuru)
BINTI: Haya fumbua macho yako.
Halafu akakata simu, Mungu
wangu sikuamini kabisa
nilichokiona mbele yangu, kwani
nilikuwa chumbani ila cha
kushangaza chumbani mule
kulikuwa na shughuli mbalimbali
zikiendelea, mara kuna watu
wakiuza chakula na wengine
wakiuza vinywaji tena walikuwa
makini na shughuli zao tu, hofu
kubwa ikanitanda moyoni, mara
nikapokea sms,
"nenda ukajinunulie chakula
sasa"
Nikahisi kupagawa kabisa na
wala sikujielewa na sikuweza
kuwasogelea kabisa, nilijihisi
kuchanganyikiwa kwakweli, mara
simu yangu ikaita,
BINTI: Unaogopa nini sasa?
MIMI: Aaah sijui hata naogopa
nini?
BINTI: (Akacheka), wewe si
umetaka chakula jamani,
nimekusaidia kukuletea wauzaji
nakushangaa huendi kununua,
kwanini sasa?
MIMI: Aaah mmmh kwani aah
sikuelewi.
BINTI: Inamaana hutaki chakula
tena? Niwaondoe?
MIMI: Mmmh eeeh nini sijui
kitu.
BINTI: (Akacheka sana), ukome
kuchukua mizigo usiyoweza
kubeba.
Akakata simu, ikawa ni kitendo
cha kufumba na kufumbua wale
wauzaji sikuwaona tena.
Nikashikwa na bumbuwazi tu
hata sikujielewa.
Nikiwa mule ndani sijielewi
chochote nikasikia watu wawili
wakiongea pale nje, sauti ya
mmoja wao niliitambua ni mke
wa rafiki yangu. Wakaanza
kugonga mlango, nami nikaenda
na kuwafungulia nao wakapitiliza
moja kwa moja ndani.
Yule mke wa rafiki yangu
alikimbilia moja kwa moja pale
chini alipolala mumewe huku
akimtingishatingisha aamke ila
kama kawaida hakuamka, yule
mwingine ambaye alikuwa
mdogo wa mke wa rafiki yangu
alikuwa pembeni akiangalia tu na
wala hakusema chochote.
Mara simu yangu ikaita,
BINTI: Hao nao wamefata nini?
MIMI: Sijui wamefata nini.
BINTI: Mpe simu mmoja
nizungumze naye.
Nikataka kumpa yule mke wa
rafiki yangu ile simu lakini ile
anataka kuichukua mdogo wake
akamkataza na kumwambia
kuwa asiichukue ile simu. Mimi
nikabaki nawashangaa tu, mara
yule mdogo mtu akaniamuru
niikate ile simu nami nikafanya
hivyo. Akamgeukia dada yake na
kumwambia kuwa atoe ubani
kwenye mkoba na akaombe moto
nje, ikabidi nimuulize,
MIMI: Samahani mdogo wangu
mbona unataka kuniletea mambo
ya mashetani humu ndani?
Nikaona kanigeukia na sura yote
imebadilika, nikaanza kupatwa
na uoga.
Akaniambia jambo moja tu kuwa
inapaswa nikubali kumtoa ndugu
yangu mmoja kama kafara ili
niokoe maisha ya wale wengine
au wote wapotee, akaniambia
kuwa nichague kati ya wale
watatu ambao ni mama, kaka na
dada.
Kwakweli nguvu ziliniishia
nikajihisi kujisaidia haja kubwa
na ndogo kwa wakati mmoja
kwani bado sikujua niamue lipi
kumtoa ndugu yangu mmoja
kama kafara au wote wapotee, na
je ndugu huyo nitamtoa nani kati
ya mama, kaka na dada bado
sikupata jibu kwakweli.
Nikashindwa kujielewa kwa
wakati huo niamue jambo gani,
yule mdogo mtu akawa
amenikazia macho huku
yakiashiria kuwa anangoja jibu
langu. Sikujielewa kabisa na wala
sikuelewa niwaambie kitu gani.
Yule mdada akaniambia kuwa
niamue moja. Nikajikuta macho
yakinitoka nilitia huruma sana na
nilisononeka mno, mara yule
aliyekwenda kuleta moto akarudi
na ubani ukawashwa.
Yule mdogo mtu bado
akaniashiria kuwa nichague
ndugu yangu mmoja kwa kafara,
MIMI: Tafadhari nawaomba,
ndugu zangu wasitendwe vibaya.
Mimi ndio chanzo cha haya yote,
naomba sana kama itawezekana
basi hiyo kafara nitolewe mimi.
Nilijikuta nikiropoka kwani
nilipatwa na mfadhaiko mkubwa
yani atolewe ndugu yangu kafara
kwa makosa yangu! Hapana
huruma ilinijaa.http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Yule dada akanikazia macho tena,
mara akaanza kuungurumisha
kama simba nikawa naogopa
huku jasho jingi likinitoka, mara
yule mdada akaanza kuongea na
mimi tena kwa sauti ya
mtetemesho.
MDADA: Kwahiyo upo tayari
kafara utolewe wewe
mwenyewe?
MIMI: Ndio nipo tayari.
MDADA: Nipe sababu kubwa
iliyokufanya kuamua hivyo.
MIMI: Sababu mimi ndio chanzo
cha yote haya, ndugu zangu
hawahusiki.
MDADA: Upo tayari kweli?
MIMI: (Huku nikitetemeka), ndio
nipo tayari.
MDADA: Kweli kabisa kabisa upo
tayari!
MIMI: (Nikizidi kutetemeke, huku
nikitamka kwa sauti ya chini),
ndio.
MDADA: Ngoja nikuonyeshe
kwanza.
Nikiwa nimekaa chini huku
natetemeka, nikamuona yule
dada akichukua kama unga unga
kwenye mkoba wake na
kunipulizia, nikajikuta nikianguka
chini.
Niliposhtuka ilikuwa ni mahali
pengine kabisa, kwanza kabisa
ilikuwa kama porini tena
kumetulia kabisa ni sauti za
ndege tu zilizosikika, nikainuka
mahali hapo na kuanza kutembea
bila ya kujua ninapoelekea, mara
akatokea mtu mbele yangu na
kunishika mkono huku
akinipeleka ninapotakiwa
kwenda.
ITAENDELEA
 
Sehemu Ya Tano (5)
Tukafika mahali kuna nyumba ila
ukiziangalia ni kama vichuguu,
nikaingizwa chumba cha kwanza
humo nilikuta maji yakitokota
kwenye pipa kubwa na yule
aliyenipeleka akaniamuru
nidumbukie kwenye lile pipa ila
nikasita huku nikiomba
msamaha, ila wala haikusaidia
nilimshuhudia yule mtu
akinibebea juu juu na
kunitumbukiza kwenye hilo pipa
linalochemka maji kwakweli
nilijua hapo ndio
Nikawa nimenyong'onyea kupita
maelezo, nikaanza kujisogeza
pale alipo yule mtu mwenye
panga. Huku nikizidi kutetemeka.
Nilipofika pale nikajilaza chini
yani tayari kwa kuchinjwa,
nikashangaa muda unapita bila
ya kusikia panga likipita kwenye
shingo yangu, mara gafla
nikashikwa kichwa kugeuka
nakutana uso kwa uso na
mwanamke mrembo sana,
akaniamuru niinuke pale
machinjioni nami nikainuka
akaniamuru nimfate nami
nikafanya hivyo.
Nilienda naye mpaka kwenye
chumba ambacho hakikuwa na
kitu chochote ndani, akaniuliza,
"unajua kwanini nimekuleta
humu?"
Nikatikisa kichwa nikiashiria
kwamba sijui sababu ya mimi
kuwa humo, mara gafla yule
mwanamke akayeyuka na
kupotea nikabaki peke yangu
kwenye kile chumba.
Nikawa natetemeka kwani
chumba chenyewe
hakikueleweka mara kiwe na
rangi nyekundu mara blue mara
nyeusi ila ilikuwa ikija rangi
nyeusi mule ndani kunatisha
sana.
Nikiwa bado sijielewi elewi akaja
yule binti wa kitanga na kuanza
kuniongelesha,
BINTI: Je unajutia kuwa na mimi?
Nikaonyesha ishara ya ndio kuwa
najutia.
BINTI: Unadhani unaweza
kuniepuka maishani mwako?
Sikujua kama nikubalia au
nikatae nikabaki kutoa macho tu.
Akanishika mkono nikatoka nae
nje, akanipeleka mahali kwenye
dimbwi ila dimbwi hilo lilijaa
damu, akaonyesha kwa kidole,
"umeona juisi ninayopenda?"
Nikatikisa kichwa kuwa nimeona,
basi akanishika mkono na
tukarudi tulipotoka, akaniambia,
"nataka ukaniletee ile juisi
ninywe"
Akanikabidhi kikabu nikabebee
ile juisi, akanionyesha ndoo
iliyokaribu nae kuwa niijaze,
sikuweza kuhoji zaidi ya kubeba
kile kikapu hadi kwenye lile
dimbwi, nikataka kuchota
nikakutana na tangazo,
"HAIRUHUSIWI KUANGUSHA
HATA TONE MOJA CHINI"
Nikawaza sasa nitabebaje na kile
kikapu maana kila nikikijaza na
kukiinua juu damu ile ambayo
ilikuwa nyepesi kama maji
ilimwagika.
Nikaamua kurudi na hata kikapu
nikakiacha hapo kwa kuogopa
kuangusha hayo matone.
Nilipofika kwa yule binti
akachukia sana,
"mbona hujaleta nilichokuagiza?"
Nilimuangalia tu na ukizingatia
mahali hapo sikuwa na uwezo wa
kuzungumza, gafla mambo hapo
hapo yakabadilika kwani
nikajikuta nipo peke yangu
sehemu yenye giza nene sina pa
kwenda wala kupapasa wakati
nashangaa hayo mara
kukabadilika tena nikamuona
mmama mbele yangu akipika
chakula ila mkono wake ndio
aliutumia kama mwiko wa
kupikia chakula, nikawa nimetoa
macho naye akaniuliza,
"unashangaa nini? Jishangae
wewe unaetaka kujitoa kafara
mwenyewe"
Bado nilikuwa nikishangaa laiti
kama ningekuwa na uwezo wa
kuongea hapo ningesema mengi.
Nikamwona yule mama akiwa
makini na kazi zake na wala
hakuogopa moto, akaniuliza,
"unahitaji chakula?"
Nikaitikia kwa kichwa kuwa
nahitaji, akaenda na kuniletea
sinia ambalo limejaa minyoo,
mmh nilipatwa na kinyaa cha
ajabu huku nikijisemea moyoni
mmh hadi minyoo ni chakula!
Sikuweza kula kwakweli.
Yule mama akawa anacheka sana,
akaniuliza tena,
"unapapenda huku?"
Nikatikisha kichwa kuashiria
kuwa kule sipapendi, yule mama
akacheka sana, na akauliza tena
"unataka kurudi ulipotoka?"
Nikaonyesha ishara kuwa nahitaji
kurudi, akaniambia tena,
"nikuonyeshe njia?"
Nikaonyesha ishara ya ndio.
Akauliza tena,
"je utaweza kukwepa
vishawishi?"
Nikaonyesha ishara kuwa
naweza, akachukua yale mavitu
anayopika na kunimwagia usoni,
nilihisi kama vile sura inatoka,
maumivu niliyoyapata
hayaelezeki nilijikuta nikigalagala
chini kama mtoto mdogo. Nililia
sana huku yule mmama akicheka
sana.
Maumivu yalipopungua yule
mmama alinishika mkono na
kunipeleka mpaka pale kwenye
dimbwi la damu akaniamuru
ninawe ile damu usoni nami
nikafanya hivyo kuja kushtukia
nilijikuta nipo kwenye chumba
na yule mdada mrembo
aliyeniokoa kwenye kuchinjwa.
Nikiwa naye mule ndani, akawa
ananifanyia visa kama vile
mwanamke afanyavyo mitego
kwa mwanaume kwakweli
sikutamani hata mwanamke wa
aina yoyote, alifanya vitu vingi ila
nilimwangalia tu.
Akanisogelea na kuniuliza,
"unanienda au hunipendi?"
Nikabaki nimemkodolea macho
tu hata nisijue cha kumwambia.
Naye akazidi kuniangalia nahisi
alikuwa akiipima akili yangu,
akaniuliza tena,
"unanipenda?"
Nikamwangalia tu, nikaamua
kutikisa kichwa nikiashiria
simpendi, mara yule mdada
akageuka kuwa joka kubwa,
nikaanza kuogopa na kukimbia,
nikakimbia sana ila kila
nikiangalia nyuma lile joka nalo
lilizidi kunikimbiza, nilikimbia
hadi nguvu ziliniishia nikaanguka
kuangalia naona lile joka
limekuwa na vichwa saba tena
likizidi kunikaribia.
Nikiwa nimechoka kukimbia,
nikaanguka chini na lile joka
likanisogelea karibu kabisa
nilikuwa natetemeka sana.
Lilipofika karibu yangu
likabadilika tena na kuwa
mwanamke mzuri sana tena
mwenye kuzidi mvuto na
urembo kushinda yule wa
kwanza, nikawa naogopa sana,
yule mwanamke akanishika
mkono na kunisimamisha,
akaniangalia sana kisha nae
akaniuliza tena kwa sauti ya
kubembeleza,
"vipi mimi unanihitaji?"
Nikawa nimetoa mimacho na
kutikisa kichwa, gafla niliona
yule mwanamke amegeuka na
kuwa simba nikaanza kukimbia
tena yani nilikimbia sana, ila
nikigeuka nyuma naona ni bonge
la simba likinikimbiza.
Nilizidi kukimbia ila mbele
nikakutana na mto ile wakati
nauvuka nikiwa nimejawa na
uoga tela nikajikwaa na kuanguka
chini ila niliangukia jiwe kubwa
kwahiyo nikapoteza fahamu.
Kwa matumaini yangu nilijua
nikishtuka pale basi nitakuwa
duniani yani kwenye ardhi yenye
watu wa kawaida kama mimi.
Ila niliposhtuka nilijikuta
nimewekwa kitandani tena
nimevuliwa nguo zote na kubaki
mtupu kabisa, pembeni yangu
alikuwepo mwanamke mrembo
sana nae akiwa mtupu kabisa
alikuwa ananipaka vitu kama
mafuta ya maji ila ni malaini
sana, akawa ananisiliba na
kufanya kama vile
ananikandakanda mwili mwangu.
Mmh nikawa natetemeka sana,
nikamwomba Mungu anipe
ujasiri mkubwa kwa wakati huo
tena ikiwezekana basi niwe kama
mwanaume asiye na nguvu za
kiume tena.
Yule mwanamke alizidi
kunikandakanda kwa mtindo wa
kupapasa mwili wangu, alishuka
hadi sehemu zangu za siri,
nilizidi kutetemeka tena
niliogopa sana ni kweli sikupatwa
na hisia zozote kwa wakati ule
najua Mungu alinisaidia.
Yule mwanamke kuona kuwa
hata sionyeshi dalili yoyote ya
mshtuko wa hisia akachukia
sana, akaanza kunifanyia mambo
ya ajabu ajabu hata hayafai
kuelezea, nilikuwa kama
kifaranga cha kuku kilichoachwa
na mamaye, kwakweli nilikuwa
mpweke na mwenye huzuni
kubwa.
Yule mwanamke akaniamuru
niinuke pale, nami nikainuka,
akiwa vile vile mtupu akatangulia
mbele ili nimfate nyuma,
nilijitahidi kukwepesha macho
yangu maana haya macho haya
ndio yanayotutia majaribuni
vijana wengi sana.
Nikaongozana nae hadi kwenye
kisima, kile kisima kilikuwa cha
maajabu kwani maji yake
yalikuwa yakitokota sana.
Nikiwa nae pale kisimani,
akaniuliza,
"unanihitaji?"
Nikazidi kutetemeka mahali pale,
nikawa nimemkodolea macho tu,
akasema tena,
"nijibu, unanihitaji?"
Niliogopa kujibu kwani nilijua
wazi ni jambo gani lingefatia,
nilizidi kutetemeka, yule
mwanamke akanikazia macho
kuashiria kuwa anahitaji jibu,
nami nikatikisa kichwa kuashiria
kuwa simuhitaji, akachukia sana
na pale pale akanitumbukiza
kwenye kile kisima kwakweli
niliiva tena sana nilitokota kama
vile napikwa ili niliwe, nililia
mule kisimani hadi nikapoteza
tena fahamu.
http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kuja kushtuka nilijikuta nipo
Tanga tena eneo lile lile ambalo
nilikutana na yule binti, na tena
mbele yangu alikuwepo yule yule
binti wa kitanga.
Akanishika mkono na kunipeleka
eneo lile lile ambalo mimi na
yeye tulikuwa tukikutana na
kupiga story nyinginyingi, nikawa
natetemeka kwani sikujua ni nini
anachotaka kunifanyia.
Alikuwa na mkoba, mara akatoa
boxer kwenye ule mkoba wake,
akaniuliza
BINTI: Unaikumbuka hii?
(akinionyeshea ile boxer).
MIMI: (Nikashangaa gafla
nimepata uwezo wa kuongea),
ndio naikumbuka.
BINTI: Uliiacha wapi?
MIMI: (Nikijaribu kuvuta
kumbukumbu ya sehemu
nilipoiacha ile boxer).
BINTI: Hakikisha uwe sawa na
majibu utakayo toa kwani jibu
lako linaweza kukuokoa au
kukuangamiza, na pia usinipe
jibu la kubuni nataka jibu la
ukweli na uhakika. Ninazo hapa
kama hizi tano na zote ni za
kwako kwahiyo uwe na majibu
ya uhakika.
Nikawa nimemtumbulia mimacho
tu huku nikifikiria cha kumjibu.
Nikiwa sina kumbukumbu nzuri
juu ya ile boxer nikawa nimetoa
macho tu hata nisijue cha kujibu.
Akaniuliza tena,
BINTI: Inamaana hukumbuki
uliiacha wapi?
MIMI: (Nikiwa nasua sua cha
kujibu), eeh ndio sikumbuki.
BINTI: Unamkumbuka Penina?
MIMI: (Nilishtuka sana na hata
sikujua huyu binti wa kitanga
amemjulia wapi Penina), aah eeh
ndio namkumbuka.
BINTI: Haya niambie
unamkumbuka kivipi?
Hapo nikakumbuka wazi kuwa ile
boxer niliisahau kwa Penina,
nikamwambia yule binti wa
kitanga kuwa nimemkumbuka
penina sababu ya ile boxer.
BINTI: Kwanini uliacha hii boxer
kwa penina?
MIMI: Penina alikuwa mke wa
mtu, siku hiyo hatukujua kama
mumewe anarudi katika
purukushani ya kukimbia baada
ya kufumaniwa ndio nikasahau
boxer yangu.
BINTI: Nini kilifuata baada ya
kufumaniwa?
MIMI: Penina alifukuzwa na
mumewe na hivyo akaja kwangu
na kudai kuwa ana mimba yangu
kwa kuogopa msala na mimi
nikamfukuza.
BINTI: Je unajua kilichompata
Penina baada ya wewe
kumfukuza?
MIMI: Hapana sijui.
BINTI: Penina alilazimika kwenda
kutoa ile mimba na huko ndiko
akapatwa na umauti. Je nikikupa
lawama juu ya kifo cha Penina
nitakuwa nimekuonea?
MIMI: (Nikiwa nimetumbua
mimacho tu kama mtu
nisiyejielewa), aaah mmh sijui.
BINTI: Na kwanini ulitembea na
Penina wakati ulijua ni mke wa
mtu? Je ulikuwa na lengo la
kumuharibia ndoa yake?
MIMI: (Bado nilijiumauma wala
sikuwa na jibu la moja kwa
moja).
Yule binti wa kitanga aliniangalia
kwa macho makali sana hadi
nikaanza kuogopa, akaingiza
mkono tena kwenye mkoba wake
na kutoka na boxer nyingine,
akaniuliza tena.
BINTI: Na hii je uliiacha wapi?
MIMI: (Nikiwa na mshangao
mkubwa kuwa amezipata wapi
zile boxer, ambazo hata mimi
mwenyewe sina kumbukumbu ya
mahali nilipoziacha. Nikabaki
kutumbua mimacho tu.), mmh
sijui.
BINTI: Unamkumbuka Aisha?
MIMI: Ndio nimemkumbuka, hiyo
boxer niliiacha kwake wakati
baba yake ametubamba kwahiyo
nilivyokimbia nikaisahau.
BINTI: Baada ya wewe kukimbia
nini kilifuata?
MIMI: Aisha alikuja nyumbani na
kudai kuwa ana mimba yangu
kwavile sikutaka makubwa
ikabidi nikimbie ila hata
niliporudi sikupata tena habari
zake.
BINTI: Haya, Aisha naye alienda
kutoa ujauzito wako ili arudi
kwao akiwa mtoto safi kwa
bahati mbaya umauti ukamshika.
Je na yeye hujasababisha wewe
kifo chake?
MIMI: (Nikiwa natetemeka kuwa
vipi mimi nikawa vile hadi hao
wakapatwa na umauti).
Nikiwa natafakari, akatoa tena
boxer nyingine,
BINTI: Na hii uliiacha kwa Nana,
naye alikuwa mke wa mtu.
Kwanini uliiacha?
MIMI: Niliogopa mumewe
angenifumania.
BINTI: Sasa boxer hii ndio
ilimfanya Nana apigwe na
mumewe hadi mauti ikampata. Je
nimlaumu mume au wewe?
MIMI: Hata sijui kitu.
BINTI: Siku zote hujui kitu,
inamaana wewe hutambui
uyafanyayo?
MIMI: Natambua.
BINTI: Je adhabu ulizopata
umeonewa?
MIMI: Hapana sijaonewa.
Akaingiza tena mkono kwenye
mkoba,
BINTI: Na hii uliiacha kwa Salma
kwanini?
MIMI: Salma alikuwa ni demu wa
rafiki yangu ili mwenyewe
asigundue katika harakati
nikaiacha hiyo boxer.
BINTI: Unajua kilichofuata?
MIMI: Rafiki yangu alipoikuta,
Salma akamwambia ukweli ila
Salma alipokuja kwangu
nikalazimika kumtimua kwani
sikutaka kugombana na rafiki
yangu sababu ya mwanamke.
BINTI: Na Salma alikosa
mwelekeo akanywa vidonge na
kujiua kwaajili yako.
MIMI: (Nikiwa nashangaa sana,
kwani sikujua kama Salma alijiua
kwaajili yangu).
BINTI: Mabinti wengi wametoa
mimba kwaajili yako na hiyo ni
sababu tosha ya mimi kwenda
kuivuruga mimba ya demu wako
wa dar.
MIMI: (hapo ndio nikaelewa
kwanini mimba ya demu wangu
wa dar ilitoka), haaa kumbe!!
Akaingiza mkono tena na kutoa
boxer nyingine,
BINTI: Hii pia uliiacha kwa
Tamari, niambie kuhusu Tamari.
MIMI: Tamari alikuwa ni rafiki
wa demu wangu, nakumbuka ni
yeye alinilazimisha niache boxer
kwake.
BINTI: Vipi alipokwambia
anaujauzito wako?
MIMI: Nilijua ni mbinu zake za
kuniachanisha na mpenzi wangu,
kwahiyo nikamkana.
BINTI: Naye akaenda kutoa
mimba na kufa. Je unajua
kwanini wasichana wengi
wanakufa wakienda kutoa
ujauzito wako?
MIMI: Hapana sijui.
BINTI: Nitakwambia sababu.
Akaniangalia na kunikazia macho
sana, safari hii alitoa boxer na
kuongea kwa ukari,
BINTI: Katika boxer zote na
matendo yake machafu, hii ndio
boxer iliyonikera na ndiyo
itakayofanya upate adhabu tena.
Akainuka na kuniambia kuwa
nimuandalie majibu
yanayoeleweka juu ya ile boxer.
Bado sikujielewa kwanini
nilikuwa naacha zile boxer na
kwanini ziniletee matatizo kila
sehemu nilipo ziacha. Na bado
nikajiuliza kwanini hao wadada
walikufa wakati wanatoa ujauzito
wangu, bado sikuwa na jibu ila
nikangoja majibu kwa huyu binti
wa kitanga ambaya hadi muda
huo sikuelewa ni jini au ni
mchawi au ni mzimu au ni mtu
wa aina gani kwani bado
alinichanganya sana.
Nikiwa sijielewi elewi kabisa na
huku nikijiuliza maswali mengi
mengi.
Yule binti wa kitanga akarudi na
kunishtua,
BINTI: Haya niambie ni wapi
uliacha hii boxer?
MIMI: Samahani, niliacha kwako
kwa bahati mbaya.
BINTI: (Akacheka sana), bahati
mbaya! Ulikuwa na maana gani?
MIMI: Sikuwa na maana yeyote
ile nilijisahau tu.
BINTI: Ulijisahau tu au ulitaka
kuonyesha jinsi gani wanipenda?
MIMI: Aaah mmh sijui.
BINTI: (Akacheka tena), kwahiyo
hukunipenda?
MIMI: Naam!
BINTI: Kwani nimekuita au
nimekuuliza, kwahiyo
hukunipenda?
MIMI: Mmmh Sijui.
BINTI: Wewe una matatizo sana,
yani hujui kama ulinipenda au
la?
MIMI: Mmmh ndio sijui.
Akaniangalia kwa macho makali
sana kama vile anasoma kitu
kwenye ubongo wangu. Nikawa
na mawazo ya uoga kichwani
mwangu, akanigeukia na
kuniuliza tena.
BINTI: Unamjua Leila?
MIMI: Ndio namjua.
BINTI: Eeh kwanini ulimdanganya
yeye na familia yake kuwa
unaenda kutoa mahari?
Nikabaki natoa mimacho tu na
kushangaa huyu binti ameyajuaje
yote hayo, maana nilipokuwa na
Leila nikapenda niwe nae karibu
zaidi kwahiyo nikaenda kupeleka
barua kwao ili nitambulike ila
ilipofika kipindi cha mahari hapo
ndio utata ulianza maana sikuwa
na jinsi zaidi ya kuwadanganya
kuwa nitaenda ila
nikawapotezea. Nikashangaa sana
huyu binti amejuaje.
Akaniuliza tena,
BINTI: Kwanini hukumfatilia tena
Leila?
MIMI: Ujana tu ndio ulinisumbua
dada.
BINTI: Heeee, nishakuwa dada
yako tena?
MIMI: Mmmh aaah sijui.
Akacheka sana na kuniangalia
kwa dharau,
BINTI: Haya unajua kwanini
wanakufa wakitoa mimba zako?
MIMI: Sijui chochote.
BINTI: Wanakufa kutokana na
zindiko ulilofanyiwa ukiwa
mdogo, mama yako ukimuuliza
atakwambia.
MIMI: Mmmmh
BINTI: Je unajua hatma ya Leila
ilikuwaje?
MIMI: Sijui.
BINTI: Leila alichanganyikiwa
sana kwa aibu uliyompa kwao,
akaamua kujiua. Tatizo
umetembea na wanawake wengi
ndiomana ukimwacha mmoja
humfatilii tena.
Bado nikawa sijielewi na mawazo
lukuki juu ya huyu binti wa
kitanga.
Akaniambia nimuulize swali
nitakalo.
MIMI: Vipi mchumba angu wa
dar, je ni mzima?
Akacheka sana, kisha akaniambia
nimfuate. Nikainuka na kuanza
kumfuata, mara gafla nikamuona
Leila amesimama mbele yangu,
nikaanza kutetemeka na kuogopa
sana, nikiwa sijielewi nilistukia
nikichapwa viboko kila sehemu.
Mbele yangu alikuwepo Leila na
yule binti wa kitanga, nilichapwa
sana hadi nikapoteza fahamu.
http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Niliposhtuka nilikutana na giza
nene yani sioni chochote cha
mbele yangu. Nilipoinuka mahali
pale, nikaanza kutembea kwa
kupapasa ila kila nilipokanyaga
nilikanyaga mwiba kumbe pale
chini palijaa miba mitupu.
Kwahiyo ikanipasa kutembea
kwa tahadhari, nilipofika mbele
nikakutana na yule binti wa
kitanga, akaniambia "njoo huku"
nikawa namfata, kufika mbele
gafla akatokea binti mmoja
niliyemjua kwa jina la Salma,
huyu alikuwa ameshika gongo
kubwa sana akanibamiza nalo
kichwani, nikaanguka na
kupoteza fahamu.
Kuja kushtuka nilikuwa kwenye
mto mkubwa tena katikati,
nilitetemeka sana mwili ulipatwa
na baridi ya ajabu, nikaogopa
sana pale katikati ya mto.
Nikaanza kujikongoja taratibu ili
niweze kutoka kwenye ule mto,
wakati nafika juu yani
nimeshatoka mtoni akatokea mtu
na kunisukuma tena gafla mtoni
nikawa natapatapa na
kuhangaika, kumwangalia vizuri
yule mtu ni yule binti wa kitanga,
nikabaki natahamaki na
nikaamua kumuuliza.
MIMI: Je hizi ndio adhabu zangu?
BINTI: (Akacheka sana), hapana
hapa tunacheza tu kama
kombolela, adhabu yenyewe ni
moja tu utaipata.
Nikanyong'onyea gafla kwani
mwili wote ulikuwa una niuma
yani kila sehemu ni maumivu
tupu.
Nikawa natetemeka sana ndani ya
ule mto na yule binti wa kitanga
alizidi kunicheka pale juu.
Nikaanza tena kujitoa kwenye ule
mto, nikajitahidi kutoa na
kujikongoja tena hadi juu,
nikawa namfata yule binti wa
kitanga cha kustaajabisha
akatoweka, nikaanza kuogopa na
hofu kubwa ikanitanda moyoni.
Mara mvua kubwa ya gafla
ikaanza kunyesha, nikaamua
kukimbilia mti uliokaribu ili
nijikinge na ile mvua, nilipofika
pale chini ya mti, mara upepo
mkubwa ukaanza kuvuma na
kusababisha ule mti kudondoka,
nilitoka mbio na kuwa mbali na
ule mti wakati unaanguka.
Mvua nayo iliendelea kunyesha
tena kwa wingi kabisa, nikawa
kama mnyama porini,
nilitetemeka sana na hata nisijue
cha kufanya kwani nilikuwa
natembeatembea bila uelekeo wa
maana, mvua iliendelea kunyesha
na kufanya nizidi kutetemeka
kwa baridi.
Mara gafla likaanza kuwaka jua
kali sana tena lile jua la kuchoma
utosini, nikazidi kushangaa na
kustaajabu.
Mbele yangu ikatokea nyumba,
nikaanza kujiuliza mbona ile
nyumba sikuiona mwanzoni.
Nikaamua kuisogelea ile nyuma
na kujaribu kubisha hodi ila
hakuna aliyeniitikia.
Nikaamua kuingia ndani
hivyohivyo, nikakutana na mbibi
akiwa anaota moto hata
nikamshangaa kwa jua lile
anaotaje moto, ikabidi nianze
kwa kumsalimia
MIMI: Bibi shikamoo.
BIBI: Marahaba, nilijua tu ukiona
nyumba utakuja.
MIMI: Na mbona unaota moto
wakati kuna joto?
BIBI: Unajua mara nyingine
inabidi tufanye vitu kinyume
chake, usipende kuishi kwa
mazoea.
MIMI: Kivipi bibi?
BIBI: Ndio kama hivi, mimi naota
moto wakati ni joto. Wewe
umezoea nini maishani?
MIMI: Nimezoea maisha ya
kawaida bibi.
BIBI: Kwahiyo maisha unayoishi
sasa ni ya kawaida?
MIMI: Hapana, naona majanga tu.
BIBI: Najua mambo yameenda
kinyume, hukutarajia jambo hili.
Ngoja nikwambie.
MIMI: Niambie bibi.
BIBI: Siku zote katika maisha
unapofanya jambo kinyume
huwa linaumiza wengine, au
mimi sikuumizi wewe hapa
ninavyoota moto wakati ni joto?
MIMI: Kweli naumia bibi.
BIBI: Basi unapofanya jambo
kinyume na ukalizoea linakuwa
kawaida ingawa linawaumiza
wengine, ndio hivyo na wewe
unapopatwa na kinyume cha
uliyozoea lazima utaumia.
Umejifunza nini hapo?
MIMI: Nimejifunza kuwa
kinyume nilichofanya mazoea
ndio kimekuwa kinyume changu
sasa.
BIBI: (Akacheka), unapenda
wasichana wazuri na wakuvutia,
kila uwaonapo macho yako
hayakuishi hamu. Mjukuu wangu,
hii ni Tanga, mji mzuri wenye
matunda ya kupendeza na
mabinti wazuri.
MIMI: Unamaana gani bibi?
BIBI: Nina mabinti wengi sana
tena ni wazuri sana kazi yao ni
kuwapata vijana wenye tamaa
kama nyie.
MIMI: (Nikiwa nimetoa mimacho
tu), sielewi bibi.
BIBI: Damu za wengi zimekulilia
wewe ila mabinti zangu
wanafanya kazi nzuri sana kwani
mwanaume yeyote mwenye
tamaa kama yako awaonapo
lazima ashtuke. Ngoja nikuitie
watano uwaone.
Yule bibi akanyosha mkono juu
kama ishara ya namba tano, mara
wakatokea mabinti wazuri sana
na wenye mvuto wa kipekee,
nikabaki kuwaangalia tu.
BIBI: Unamtaka yupi kati yao?
MIMI: Hapana bibi sihitaji
mwanamke yeyote.
Yule bibi na wale mabinti wote
wakacheka sana halafu wale
mabinti wakatoweka.
BIBI: Sogea karibu nami ili tuote
moto vizuri, (huku akiendelea
kuchochea kuni zake).
Nikawa nasita kuusogelea moto
ule, akaniamuru tena nimsogelee
pale. Duh kufika karibu ni kama
jehanamu ndogo maana ule moto
unaunguza taratibu mmh!! Yule
bibi akaniangalia, yani ingawa ni
mzee ila alionyesha kuwa na sura
nzuri sana. Akaniuliza,
BIBI: Unajisikiaje sasa?
MIMI: Naungua bibi.
BIBI: Basi hii ni raha ya kufanya
vitu kinyume mjukuu wangu.
Nikabaki nikimwangalia yule bibi
na hata nisimmalize, mara
akachukua glasi na kumimina
kitu ndani yake na kunikabidhi,
BIBI: Karibu maziwa mjukuu
wangu.
MIMI: (Nikapokea huku
nikiangalia na kustaajabu), bibi
mbona hii ni damu?
BIBI: Mbona unakuwa si
muelewa mjukuu wangu?
Nimekwambia kuwa hapa
tunafanya vitu kinyume, sasa
unashangaa nini kunywa!
Nikiwa bado nimeishika ile glasi
na kuendelea kutafakari, mara
yule bibi akasema,
BIBI: Na usistaajabu
utakapotakiwa kutembelea
kichwa badala ya miguu,
(akacheka sana).
Bado nilikuwa kama mtu
niliyepigwa na bumbuwazi bila
ya kuwa na majibu na pale ule
moto ulizidi kunichoma tu.
Mara yule bibi akainuka ila
akawa anatembea
kinyumenyume huku akicheka,
na akarudi akitembea
kinyumenyume vilevile.
BIBI: Hata ukitaka kuyarudia
maisha ya kawaida utakubidi
utembee kinyumenyume hadi
utakapofika.
MIMI: Nionyeshe njia basi bibi.
BIBI: Kunywa maziwa kwanza.
Akatoa na bakuri na kunikabidhi,
BIBI: Tafuna na hizo karanga, ni
tamu sana na hayo maziwa.
MIMI: Jamani bibi, mbona ni
mavi ya mbuzi?
BIBI: Jifunze kuwa muelewa
utashinda.
Nikawa nimeshika kile kibakuli
chenye mavi ya mbuzi na ile glasi
yenye damu hata nisielewe
nakula vipi vitu hivi.
BIBI: Unapotumia kitu kinyume
na wewe fanya kinyume chake
utajikuta umekizoea na kuona
cha kawaida.
MIMI: Jamani bibi, ndio nile mavi
ya mbuzi na damu kweli?
BIBI: Bora ule maana
nitakapokuletea maji ya kunywa
hapa ushushie utakuwa umepata
uzoefu kidogo.
MIMI: Khaaaa kama damu ndio
maziwa na mavi ya mbuzi ndio
karanga je hayo maji ni nini?
BIBI: (Akacheka sana), na hata
nikikwambia hiyo damu ni damu
gani utazidi kupagawa ni kheri
ule ushibe hicho
nilichokuandalia.
Bado maswali mengi
yaliniandama, je hii damu ni
damu ya nini? Bado sikupata jibu
nikawa najipanga kumuuliza
huyu bibi aniambie ukweli
vyovyote vile sina jinsi.
MIMI: Samahani bibi, niambie hii
ni damu ya nini?
BIBI: Unataka kujua kweli?
MIMI: Ndio nataka kujua bibi.
BIBI: Kunywa kwanza nikwambie.
Bado moyo wangu ulisita kunywa
ile damu na kula yale mavi ya
mbuzi.
Nikawa bado naiangalia ile damu
na kuitafakari, bibi akaendelea
kuniamuru kuwa ninywe.
BIBI: Uzima wako upo humo, ni
bora unywe tu kwa hiyari yako.
Nikajaribu kunywa ile damu ila
kinyaa kilizidi kunishika.
Bibi akaniangalia kwa jicho kali
sana na kusome.
BIBI: Nimeshakwambia
unapokula vitu hvyo weka
kinyume chake utaona ni
kawaida tu. Narudia tena, uzima
wako upo humo.
Ikabidi nifanye kama alivyosema
kuwa damu ni maziwa na mavi
ya mbuzi ni karanga. Ila nikala
kidogo tu na kumrudishia,
MIMI: Asante bibi nimeshiba.
BIBI: Hapana, hutakiwi kubakisha
unatakiwa umalize vyote na
kikombe ukilambe kuonyesha
kuwa umeridhika na ladha yake.
MIMI: Bibi ila vimenishinda
kwakweli.
BIBI: Hiyo ni lazima ule, yani
utake usitake. Je ungependa
nikwambie hiyo damu ni ya nini?
MIMI: Ndio niambie.
BIBI: Mwanamke akiwa kwenye
siku zake huwa anatoa uchafu, na
uchafu huo huwa kwenye mfumo
wa nini?
MIMI: Huwa ni damu.
BIBI: Basi hiyo ni damu ya
mwanamke akiwa kwenye siku
zake.
MIMI: Aaargh mbona umenipa
uchafu jamani?
BIBI: (Akacheka sana), haya
kunywa sasa.
MIMI: Hapana, siwezi kunywa
uchafu.
Mara yule bibi akanipulizia kitu,
nikawa kama nimepumbazika
nikajikuta nikiyala yale mavi ya
mbuzi na kuinywa ile damu, ila
nilipomaliza tu nikawa kawaida,
nilitamani kutapika kabisa yani.
Mara akanipa glas nyingine na
kuniambia,
BIBI: Chukua na maji ya kunywa
ushushie.
MIMI: (Yani ile kuangalia hadi
kichefuchefu), jamani bibi mbona
ni mate tena yamechanganyika
na makohozi.http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
BIBI: Inakupasa unywe na hapo
utajifunza kuona kinyaa cha yale
uliyoyafanya.
MIMI: Aaah bibi, siwezi kunywa
mate kwakweli.
Akanifanyia kama mwanzo,
nikajikuta nikinywa ile galsi
yenye mate hadi kuimaliza,
halafu nikawa kawaida. Yule bibi
akawa ananiangalia na kusema,
BIBI: Kuna juice pia inapaswa
unywe, ngoja nikupe.
Akachukua glasi na kunikabidhi.
MIMI: Loh bibi jamani ndio
usaha kweli?
BIBI: Ndio, kunywa juisi hiyo.
MIMI: Siwezi bibi yani ninywe
usaha kweli dah!
Akafanya kama mwanzo, na ule
usaha nao nikanywa. Mara gafla
nikaanza kuumwa na tumbo hadi
nikawa nalia na kugalagala chini,
yule bibi alikuwa akicheka sana,
na mimi nilizidi kuugulia.
Wakati nalia vile, wakaja
wasichana wazuri na
kunizunguka mahali pale,
kwakweli sikuona hata uzuri wao
kwa maumivu yale ya tumbo,
niliugulia sana na hakuna
aliyenisaidia.
Baada ya kuugulia kwa muda
mrefu, bibi akanipa glasi na
kuniambia.
BIBI: Kunywa hii ni juisi ya
machozi itapoza maumivu yako
ya tumbo.
Kunywa machozi haikuwa shida
kwangu kwani nilishakunywa
vingi visivyonywewa,
nikaichukua ile glasi ya machozi
na kunywa, ilikuwa ina ladha
kama ya chumvichumvi hivi.
Nilipomaliza kunywa tu na yale
maumivu yakakatika.
BIBI: Unajua kwanini umeumwa
na tumbo?
MIMI: Sijui bibi.
BIBI: Kwasababu ulikuwa
unakataa kula chakula chetu.
MIMI: Nahitaji kurudi kwenye
maisha ya kawaida, nirudisheni
tafadhari.
BIBI: Unadhani ni kazi rahisi?
MIMI: Sijui kwakweli.
BIBI: Je unaweza kuifanya jana
kuwa leo?
MIMI: Siwezi.
BIBI: Lazima ifanyike kazi ya
ziada ili uwe kawaida na si
kinyume tena.
MIMI: Basi bibi nisaidie.
Bibi akaniangalia tu, mara
akawaita tena wale mabinti wa
tano.
BIBI: Chagua mmoja uwe nae kila
utakapokwenda.
MIMI: Hapana bibi, sitaki
mwanamke.
BIBI: Sasa wewe unataka nini?
MIMI: Nataka niwe kwenye
maisha ya kawaida.
BIBI: Ngoja uone kwanza.
Akanionyesha mahali kwenye
watoto wengi wakilia na mahali
pengine wanawake wengi
wakilia. Halafu akaniuliza.
BIBI: Upande upi unaonyesha
huruma zaidi?
MIMI: Pande zote zaonyesha
huruma ila zaidi Ni ule upande
wa watoto.
BIBI: Umewaonea huruma
watoto, ni sawa kabisa. Na
kwanini hukupenda
kuwahurumia wakiwa tumboni
ili nao watoke wakiwa kama
wewe?
Nikakaa kimya kwani sikuwa na
la kujibu.
Bibi yule akanichukua na
kunifungia kwenye chumba, kile
chumba kilikuwa na sisimizi na
siafu wengi nao wakaning'ata
sana hadi vidonda vikanijaa.
Baada ya muda akanifungulia na
kuniuliza,
BIBI: Umejisikiaje wakati wale
wadudu wanakung'ata?
MIMI: Nimeumia sana na
maumivu yake hayaelezeki.
Akachukua majivu na kunipaka
mwilini, huku akiniambia,
BIBI: Ukitaka tusiendelee
kukufatilia fata kile
watachokwambia.
MIMI: Nitafanya vyote bibi,
sitapuuza hata kimoja.
Akachukua na damu nayo
akanipaka mwili mzima, kisha
akasema,
BIBI: Umependeza sana mjukuu
wangu.
Nikabaki namtazama tu huku
macho yangu yamejawa na
huruma tupu na yakionyesha
kuwa nahitaji msaada na
kuhurumiwa.
Kufumba na kufumbua, sikuwa
tena kwenye ile nyumba na wala
yule bibi hakuwepo ila nilijikuta
niko peke yangu chini ya mti, cha
kushangaza ule mti ulikuwa na
mdomo na macho. Nilitetemeka
sana. Kila nilipouangalia nao
ulinichekea, nikatetemeka sana
mahali pale na kuanza kurudi
kinyumenyume, wakati nafanya
hivyo uli mti ulikuwa ukizidi
kucheka huku nao ukinifata.
Kwakweli mkojo ulinitoka, wakati
narudi vile kinyumenyume kuna
kitu nikakigonga kwa nyuma kwa
haraka kabisa nikageuka na
kuangalia, Mungu wangu,
alikuwa mtu mrefu sana mbele
yangu sikuweza hata kumtazama,
akachukua mkono wake na
kushika shingo yangu huku
akinining'iniza juu juu nikawa
natetemeka huku ninalia sana.
Alichokifanya sasa ni kunitupa
toka kule juu hadi chini, na hapo
hapo nikapoteza fahamu.
Kuja kushtuka, Mungu wangu
sikutegemea nilichokiona mbele
yangu.
Sikutegemea nilichokiona,
niliposhtuka nikajikuta nipo
kitandani, nikamwona mpenzi
wangu akiwa pembeni yangu
pale kitandani, nikawa nashangaa
shangaa tu.
Nikamwona yule mpenzi wangu
akifurahi sana kuwa nimeamka
na akaharakisha kwenda nje,
kurudi ndani akawa
ameongozana na yule mdada
aliyekuja na mke wa rafiki yangu,
yule mdada mwenye maruhani.
Nikawa bado nashangaa shangaa
tu. Bado sikuelewa kitu, nikazidi
kushangaa shangaa tu. Kitu cha
kwanza kabisa nikawaambia,
MIMI: Naombeni maji ya kunywa.
Kabla sijajibiwa, mara simu
yangu ikaanza kuita muda ule ule
niliposhtuka, nikawa napapasa ili
niipokee, mara yule mdada wa
mwanzo akaniamuru nimpatie ile
simu, nilipompatia akaniambia,
MDADA: Hii ndio
imekusababishia mambo yote.
Nikashangaa kivipi simu
imenisababishia mambo yote
yale. Na alipoichukua yule dada
ile simu ikaacha kuita.
Kwanza nikawa sielewi wala
siamini kama nipo kwenye
ulimwengu wa kawaida.
Nikaanza kuwashangaa tu yule
mdada na mpenzi wangu, huku
nikijiuliza maswali mengi mengi
imekuwaje wakawa pamoja na
wengine wako wapi. Pia
nikashangaa kile chumba kwani
kilikuwa ni chumba tofauti
kabisa na chumba changu.
MIMI: Mbona humu sio
chumbani kwangu? (huku
nikizidi kushangaa).
MDADA: Ipo sababu kubwa ya
kukuondoa mule kwenye chumba
chako.
MIMI: Mbona sielewi?
MDADA: Ndio huwezi kuelewa
mpaka utakapoeleweshwa.
MIMI: Niambieni kwanza, nipo
dunia ya kawaida au dunia ya
kinyumenyume?
MDADA: (Akacheka), upo
kawaida, na upo salama sasa. Ila
usalama wako utaongezeka pale
utakapoamua kuinuka hapo ili
twende baharini ukaoge maji ya
bahari, na hii simu(akionyesha
ile simu yangu aliyoshika),
tunaenda kuitupa baharini.
Sikuweza kubisha wala kupinga,
nikainuka pale nikiwa mimi yule
mdada na mpenzi wangu.
Tukakodi kibajaji kikatupeleka
hadi baharini.
http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kufika pale baharini,
nikajishangaa nimekuwa mzito
sana kuitupa ile simu, nikajikuta
nikisita kufanya hivyo. Yule
mdada akaniambia,
MDADA: Unapenda kuishi maisha
ya kawaida?
MIMI: Ndio napenda.
MDADA: Basi tupa hiyo simu.
MIMI: Ila simu yangu ni ya
gharama sana jamani.
MDADA: We itupe tena uirushe
mbali kama unayapenda maisha
yako, nitakupa sababu ya kufanya
hivyo.
Roho iliniuma sana kila
nikiangalia ile simu, nilizidi
kuumia moyoni. Yule mdada
akaniangalia tena kwa macho
makali na kusema,
MDADA: Tupa hiyo simu.
MIMI: Ujue nilinunua laki tano
hii simu!
MDADA: Haya, laki tano na
maisha yako kipi bora?
MIMI: Bora maisha yangu.
MDADA: Basi itupe hiyo simu.
Bado nikawa nasitasita,
nilimtazama mpenzi wangu naye
aliniangalia kwa jicho la huruma
sana, nikapatwa na mfadhaiko
wa moyo nikakumbuka yote
niliyowatenda wadada kwa tamaa
zangu. Nikakumbuka mateso
niliyopata kwenye dunia ya
kinyumenyume.
Hapo nikaamua kuchukua
maamuzi magumu na kuirusha
ile simu katikati ya maji, mara
gafla nikashtuka,
MIMI: Aaah laini yangu!!
MDADA: Imefanyaje?
MIMI: Nimeitupa nayo.
Kabla hajaniambia kitu tena mara
gafla tukaona moshi mwingi
ukitokea pale nilipoirusha ile
simu, nikaanza kutetemeka kwa
uoga. Yule dada akaniambia
kuwa niingie kwenye maji ili
niweze kujisafisha zile nuksi na
mabalaa. Ila bado sikujua wale
ndugu niliowaacha ndani ni nini
kimewapata, je ni wazima au
wamekufa, nikaamua kumuuliza
yule dada,
MIMI: Na ndugu zangu je ni
wazima au wamekufa?
MDADA: Hilo swali niulize baada
ya kujisafisha ndio nitakupa jibu.
Nikamwangalia tena yule mpenzi
wangu bado alionyesha huruma
sana na hata sikumwelewa kuwa
ananihurumia mimi au
anaonyesha huruma ya nini.
Nikaangalia tena pale
nilipoirusha simu yangu bado
palikuwa panafuka moshi.
Yule mdada akaniamuru tena
kuwa niende kwenye maji
nikaoge, ila nikawa nasita
kufanya hivyo na yule mpenzi
wangu alizidi kunyong'onyea na
pia alizidi kuonyesha huruma.
Nikaamua kwenda kuoga hayo
maji ya bahari, yule dada
akanielekeza sehemu ya kwenda
kuoga ilikuwa ni mbali kidogo na
pale nilipoitupa ile simu yangu
na pia akanionya kuwa nisifike
pale nilipoitupa simu
yangu.http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Nikiwa ndani ya maji ya bahari,
wazo likanijia kuwa nisogee
karibu zaidi na nilipoitupa ile
simu labda nitaiona tena.
Nikawa nimesogea karibu huku
nikiwa kama naogelea kumbe
najaribu kupapasapapasa, ili
kama nikiipata basi niitoe ile
laini yangu tu. Mara gafla maji
yakawa ya moto sana mule
baharini hadi yakawa
yananiunguza, wakati nataka
nikimbilie nchi kavu, nikakuta
kuna mtu amenishika bega kwa
nyuma ile kugeuka ni macho kwa
macho na binti wa kitanga,
amefikaje na anataka nini sijui.
Nilipogeuka nyuma nikakutana
macho kwa macho na binti wa
kitanga, nilianza kutetemeka kwa
hofu na uoga, akawa ananiangalia
huku anacheka nikazidi
kutetemeka. Nilipoangalia kule
nchi kavu nilimwona yule mdada
akininyoshea mkono kama ishara
ya kuniita, nikawa najitahidi
nitoke ila yule binti wa kitanga
alining'ang'ania na hadi nafika
nchi kavu yeye alikuwa nyuma
yangu.
Yule mdada akaniuliza tena kwa
ukali,
MDADA: Umefanya vitu gani
wewe?
MIMI: Sijui.
MDADA: Hujui nini? Unadhani
angekufuata huyo bila sababu?
MIMI: Naomba nisaidie basi,
nilienda kule nilipoitupa ile simu.
MDADA: Yani wewe umeharibu
kila kitu.
Nikamwona yule dada akichukua
kiwembe na kuja karibu yangu,
akanichana kwenye mkono,
nilipatwa na maumivu makali
akanizuia kusogea popote mpaka
pale aliponichana pakikauka
damu.
Nikiwa naugulia yale maumivu,
nikamwona yule dada akienda
pembeni na kuongea kitu na
mpenzi wangu, mara wote
wakanisogelea pale.
Nikamwona yule dada akichukua
tena kiwembe na kumchana
mpenzi wangu mkononi halafu
akachukua ile damu iliyokuwa
inamtoka mpenzi wangu na
kunipaka shingoni halafu yeye na
yule mpenzi wakasogea mbali.
Kwa muda mchache nilihisi kama
nataka kukata roho kwani
maumivu yaliyonipata pale
shingoni yalikuwa makubwa
sana, hadi nikajikuta nikianguka
kwenye maji na kuanza
kutapatapa.
Ninachokumbuka nilipoteza
fahamu.
http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Niliposhtuka nilijikuta nipo
nyumbani, nimelala kwenye
jamvi na wote ninaowafahamu
wakiwa wamenizunguka, hadi
yule mdada nilimwona pale
kasoro mpenzi wangu tu ndiye
hakuwepo pale.
Wote niliwakuta wamefurahi na
nilikuwa kama mtu niliyepoteza
dira.
Wakaniacha nipumzike bila
kuniuliza chochote.
Baada ya siku mbili, ikabidi
niongee nao kwani nilikuwa
sielewi chochote.
MIMI: Mama mbona sielewi
chochote, ilikuwaje kwani?
MAMA: Ni vigumu kuelezea ila
umetufanya kupata majeraha
yasiyosahaulika kamwe.
MIMI: Na kile chumba changu
imekuwaje mama?
MAMA: Kile chumba
tulikirudisha kwa mwenye
nyumba kwani ungeendelea
kukaa pale kungekuwa na
makubwa zaidi.
MIMI: Ila mama, inaniwia
vigumu kukuelewa.
Basi mama akamwita yule mdada
ili nipate kuzungumza naye pia.
MDADA: Sikia, janga ulilolipata ni
kubwa sana. Mimi nisingeweza
kukusaidia ila babu yangu ni mtu
wa huko na anajua vitu vingi.
MIMI: Kwahiyo watu
walioanguka chumbani kwangu,
waliamkaje?
MDADA: Kuna dawa niliwapaka
wakaamka, ile dawa
iliwezakufanya kazi baada ya
wewe kukubali kujitoa kafara.
MIMI: (Kuna kitu nikajifikiria na
kuamua kuuliza), mbona wakati
nipo kwenye ulimwengu usio wa
kawaida simu yangu sikuiona
halafu niliposhtuka kawaida
ikaanza kuita?
MDADA: Simu yako haikuwa
simu ya kawaida, yule dada
alikubadilishia simu muda mrefu
sana ndiomana kila jambo
ulilotaka kufanya ukiwa na ile
simu aligundua kwa haraka.
Nikawa nawaza amebadilishaje,
na mbona nilikuwa naiona
kawaida.
MIMI: Ila ndugu zangu ni
wazima?
MDADA: Ndio ni wazima ila...
MIMI: (Nikadakia), ila nini na
yuko wapi mpenzi wangu?
MDADA: Ndio huyo ninayetaka
kumuongelea.
MIMI: (Huku mapigo ya moyo
yakienda mbio), kafanyaje?
MDADA: Amejitoa kwaajili yako.
MIMI: Sikuelewi, unamaanisha
nini?
MDADA: (akainamisha kichwa
chini na kuniambia), kwa bahati
mbaya tumeshindwa kumwokoa
kwahiyo amekufa.http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Nilihisi utumbo ukijisokoto na
tumbo likaanza kuniuma gafla.
MIMI: Hapana hapana sitaki
kuamini.
MDADA: Huo ndio ukweli.
Niliona machozi yakinitoka,
nilijisikia vibaya kujua yule
msichana ambaye ni mpenzi
wangu amekufa kwaajili yangu.
Roho iliniuma sana.
Wakawepo watu pale kunifariji
na kunipa moyo. Nikajiona
nimepata kovu ambalo
sitalisahau tena.
Rafiki yangu akaja pale na kunipa
moyo.
RAFIKI: Pole sana ila yote ni
mapito tu.
MIMI: Asante ila nimeumia sana.
RAFIKI: Hata sisi hatuelewi, na je
sikuzote ulizopoteza fahamu
ulikuwa wapi? Maana yule dada
alituambia kwamba upo eneo la
hatari sana.
MIMI: Ni kweli tena yalikuwa
majanga sana ila ninachoweza
kusema hadi sasa ni kuwa
SITAISAHAU TANGA.
MWISHO
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni http://www.equatorstory.com/
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 
Sehemu Ya Tano (5)
Tukafika mahali kuna nyumba ila
ukiziangalia ni kama vichuguu,
nikaingizwa chumba cha kwanza
humo nilikuta maji yakitokota
kwenye pipa kubwa na yule
aliyenipeleka akaniamuru
nidumbukie kwenye lile pipa ila
nikasita huku nikiomba
msamaha, ila wala haikusaidia
nilimshuhudia yule mtu
akinibebea juu juu na
kunitumbukiza kwenye hilo pipa
linalochemka maji kwakweli
nilijua hapo ndio
Nikawa nimenyong'onyea kupita
maelezo, nikaanza kujisogeza
pale alipo yule mtu mwenye
panga. Huku nikizidi kutetemeka.
Nilipofika pale nikajilaza chini
yani tayari kwa kuchinjwa,
nikashangaa muda unapita bila
ya kusikia panga likipita kwenye
shingo yangu, mara gafla
nikashikwa kichwa kugeuka
nakutana uso kwa uso na
mwanamke mrembo sana,
akaniamuru niinuke pale
machinjioni nami nikainuka
akaniamuru nimfate nami
nikafanya hivyo.
Nilienda naye mpaka kwenye
chumba ambacho hakikuwa na
kitu chochote ndani, akaniuliza,
"unajua kwanini nimekuleta
humu?"
Nikatikisa kichwa nikiashiria
kwamba sijui sababu ya mimi
kuwa humo, mara gafla yule
mwanamke akayeyuka na
kupotea nikabaki peke yangu
kwenye kile chumba.
Nikawa natetemeka kwani
chumba chenyewe
hakikueleweka mara kiwe na
rangi nyekundu mara blue mara
nyeusi ila ilikuwa ikija rangi
nyeusi mule ndani kunatisha
sana.
Nikiwa bado sijielewi elewi akaja
yule binti wa kitanga na kuanza
kuniongelesha,
BINTI: Je unajutia kuwa na mimi?
Nikaonyesha ishara ya ndio kuwa
najutia.
BINTI: Unadhani unaweza
kuniepuka maishani mwako?
Sikujua kama nikubalia au
nikatae nikabaki kutoa macho tu.
Akanishika mkono nikatoka nae
nje, akanipeleka mahali kwenye
dimbwi ila dimbwi hilo lilijaa
damu, akaonyesha kwa kidole,
"umeona juisi ninayopenda?"
Nikatikisa kichwa kuwa nimeona,
basi akanishika mkono na
tukarudi tulipotoka, akaniambia,
"nataka ukaniletee ile juisi
ninywe"
Akanikabidhi kikabu nikabebee
ile juisi, akanionyesha ndoo
iliyokaribu nae kuwa niijaze,
sikuweza kuhoji zaidi ya kubeba
kile kikapu hadi kwenye lile
dimbwi, nikataka kuchota
nikakutana na tangazo,
"HAIRUHUSIWI KUANGUSHA
HATA TONE MOJA CHINI"
Nikawaza sasa nitabebaje na kile
kikapu maana kila nikikijaza na
kukiinua juu damu ile ambayo
ilikuwa nyepesi kama maji
ilimwagika.
Nikaamua kurudi na hata kikapu
nikakiacha hapo kwa kuogopa
kuangusha hayo matone.
Nilipofika kwa yule binti
akachukia sana,
"mbona hujaleta nilichokuagiza?"
Nilimuangalia tu na ukizingatia
mahali hapo sikuwa na uwezo wa
kuzungumza, gafla mambo hapo
hapo yakabadilika kwani
nikajikuta nipo peke yangu
sehemu yenye giza nene sina pa
kwenda wala kupapasa wakati
nashangaa hayo mara
kukabadilika tena nikamuona
mmama mbele yangu akipika
chakula ila mkono wake ndio
aliutumia kama mwiko wa
kupikia chakula, nikawa nimetoa
macho naye akaniuliza,
"unashangaa nini? Jishangae
wewe unaetaka kujitoa kafara
mwenyewe"
Bado nilikuwa nikishangaa laiti
kama ningekuwa na uwezo wa
kuongea hapo ningesema mengi.
Nikamwona yule mama akiwa
makini na kazi zake na wala
hakuogopa moto, akaniuliza,
"unahitaji chakula?"
Nikaitikia kwa kichwa kuwa
nahitaji, akaenda na kuniletea
sinia ambalo limejaa minyoo,
mmh nilipatwa na kinyaa cha
ajabu huku nikijisemea moyoni
mmh hadi minyoo ni chakula!
Sikuweza kula kwakweli.
Yule mama akawa anacheka sana,
akaniuliza tena,
"unapapenda huku?"
Nikatikisha kichwa kuashiria
kuwa kule sipapendi, yule mama
akacheka sana, na akauliza tena
"unataka kurudi ulipotoka?"
Nikaonyesha ishara kuwa nahitaji
kurudi, akaniambia tena,
"nikuonyeshe njia?"
Nikaonyesha ishara ya ndio.
Akauliza tena,
"je utaweza kukwepa
vishawishi?"
Nikaonyesha ishara kuwa
naweza, akachukua yale mavitu
anayopika na kunimwagia usoni,
nilihisi kama vile sura inatoka,
maumivu niliyoyapata
hayaelezeki nilijikuta nikigalagala
chini kama mtoto mdogo. Nililia
sana huku yule mmama akicheka
sana.
Maumivu yalipopungua yule
mmama alinishika mkono na
kunipeleka mpaka pale kwenye
dimbwi la damu akaniamuru
ninawe ile damu usoni nami
nikafanya hivyo kuja kushtukia
nilijikuta nipo kwenye chumba
na yule mdada mrembo
aliyeniokoa kwenye kuchinjwa.
Nikiwa naye mule ndani, akawa
ananifanyia visa kama vile
mwanamke afanyavyo mitego
kwa mwanaume kwakweli
sikutamani hata mwanamke wa
aina yoyote, alifanya vitu vingi ila
nilimwangalia tu.
Akanisogelea na kuniuliza,
"unanienda au hunipendi?"
Nikabaki nimemkodolea macho
tu hata nisijue cha kumwambia.
Naye akazidi kuniangalia nahisi
alikuwa akiipima akili yangu,
akaniuliza tena,
"unanipenda?"
Nikamwangalia tu, nikaamua
kutikisa kichwa nikiashiria
simpendi, mara yule mdada
akageuka kuwa joka kubwa,
nikaanza kuogopa na kukimbia,
nikakimbia sana ila kila
nikiangalia nyuma lile joka nalo
lilizidi kunikimbiza, nilikimbia
hadi nguvu ziliniishia nikaanguka
kuangalia naona lile joka
limekuwa na vichwa saba tena
likizidi kunikaribia.
Nikiwa nimechoka kukimbia,
nikaanguka chini na lile joka
likanisogelea karibu kabisa
nilikuwa natetemeka sana.
Lilipofika karibu yangu
likabadilika tena na kuwa
mwanamke mzuri sana tena
mwenye kuzidi mvuto na
urembo kushinda yule wa
kwanza, nikawa naogopa sana,
yule mwanamke akanishika
mkono na kunisimamisha,
akaniangalia sana kisha nae
akaniuliza tena kwa sauti ya
kubembeleza,
"vipi mimi unanihitaji?"
Nikawa nimetoa mimacho na
kutikisa kichwa, gafla niliona
yule mwanamke amegeuka na
kuwa simba nikaanza kukimbia
tena yani nilikimbia sana, ila
nikigeuka nyuma naona ni bonge
la simba likinikimbiza.
Nilizidi kukimbia ila mbele
nikakutana na mto ile wakati
nauvuka nikiwa nimejawa na
uoga tela nikajikwaa na kuanguka
chini ila niliangukia jiwe kubwa
kwahiyo nikapoteza fahamu.
Kwa matumaini yangu nilijua
nikishtuka pale basi nitakuwa
duniani yani kwenye ardhi yenye
watu wa kawaida kama mimi.
Ila niliposhtuka nilijikuta
nimewekwa kitandani tena
nimevuliwa nguo zote na kubaki
mtupu kabisa, pembeni yangu
alikuwepo mwanamke mrembo
sana nae akiwa mtupu kabisa
alikuwa ananipaka vitu kama
mafuta ya maji ila ni malaini
sana, akawa ananisiliba na
kufanya kama vile
ananikandakanda mwili mwangu.
Mmh nikawa natetemeka sana,
nikamwomba Mungu anipe
ujasiri mkubwa kwa wakati huo
tena ikiwezekana basi niwe kama
mwanaume asiye na nguvu za
kiume tena.
Yule mwanamke alizidi
kunikandakanda kwa mtindo wa
kupapasa mwili wangu, alishuka
hadi sehemu zangu za siri,
nilizidi kutetemeka tena
niliogopa sana ni kweli sikupatwa
na hisia zozote kwa wakati ule
najua Mungu alinisaidia.
Yule mwanamke kuona kuwa
hata sionyeshi dalili yoyote ya
mshtuko wa hisia akachukia
sana, akaanza kunifanyia mambo
ya ajabu ajabu hata hayafai
kuelezea, nilikuwa kama
kifaranga cha kuku kilichoachwa
na mamaye, kwakweli nilikuwa
mpweke na mwenye huzuni
kubwa.
Yule mwanamke akaniamuru
niinuke pale, nami nikainuka,
akiwa vile vile mtupu akatangulia
mbele ili nimfate nyuma,
nilijitahidi kukwepesha macho
yangu maana haya macho haya
ndio yanayotutia majaribuni
vijana wengi sana.
Nikaongozana nae hadi kwenye
kisima, kile kisima kilikuwa cha
maajabu kwani maji yake
yalikuwa yakitokota sana.
Nikiwa nae pale kisimani,
akaniuliza,
"unanihitaji?"
Nikazidi kutetemeka mahali pale,
nikawa nimemkodolea macho tu,
akasema tena,
"nijibu, unanihitaji?"
Niliogopa kujibu kwani nilijua
wazi ni jambo gani lingefatia,
nilizidi kutetemeka, yule
mwanamke akanikazia macho
kuashiria kuwa anahitaji jibu,
nami nikatikisa kichwa kuashiria
kuwa simuhitaji, akachukia sana
na pale pale akanitumbukiza
kwenye kile kisima kwakweli
niliiva tena sana nilitokota kama
vile napikwa ili niliwe, nililia
mule kisimani hadi nikapoteza
tena fahamu.
http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kuja kushtuka nilijikuta nipo
Tanga tena eneo lile lile ambalo
nilikutana na yule binti, na tena
mbele yangu alikuwepo yule yule
binti wa kitanga.
Akanishika mkono na kunipeleka
eneo lile lile ambalo mimi na
yeye tulikuwa tukikutana na
kupiga story nyinginyingi, nikawa
natetemeka kwani sikujua ni nini
anachotaka kunifanyia.
Alikuwa na mkoba, mara akatoa
boxer kwenye ule mkoba wake,
akaniuliza
BINTI: Unaikumbuka hii?
(akinionyeshea ile boxer).
MIMI: (Nikashangaa gafla
nimepata uwezo wa kuongea),
ndio naikumbuka.
BINTI: Uliiacha wapi?
MIMI: (Nikijaribu kuvuta
kumbukumbu ya sehemu
nilipoiacha ile boxer).
BINTI: Hakikisha uwe sawa na
majibu utakayo toa kwani jibu
lako linaweza kukuokoa au
kukuangamiza, na pia usinipe
jibu la kubuni nataka jibu la
ukweli na uhakika. Ninazo hapa
kama hizi tano na zote ni za
kwako kwahiyo uwe na majibu
ya uhakika.
Nikawa nimemtumbulia mimacho
tu huku nikifikiria cha kumjibu.
Nikiwa sina kumbukumbu nzuri
juu ya ile boxer nikawa nimetoa
macho tu hata nisijue cha kujibu.
Akaniuliza tena,
BINTI: Inamaana hukumbuki
uliiacha wapi?
MIMI: (Nikiwa nasua sua cha
kujibu), eeh ndio sikumbuki.
BINTI: Unamkumbuka Penina?
MIMI: (Nilishtuka sana na hata
sikujua huyu binti wa kitanga
amemjulia wapi Penina), aah eeh
ndio namkumbuka.
BINTI: Haya niambie
unamkumbuka kivipi?
Hapo nikakumbuka wazi kuwa ile
boxer niliisahau kwa Penina,
nikamwambia yule binti wa
kitanga kuwa nimemkumbuka
penina sababu ya ile boxer.
BINTI: Kwanini uliacha hii boxer
kwa penina?
MIMI: Penina alikuwa mke wa
mtu, siku hiyo hatukujua kama
mumewe anarudi katika
purukushani ya kukimbia baada
ya kufumaniwa ndio nikasahau
boxer yangu.
BINTI: Nini kilifuata baada ya
kufumaniwa?
MIMI: Penina alifukuzwa na
mumewe na hivyo akaja kwangu
na kudai kuwa ana mimba yangu
kwa kuogopa msala na mimi
nikamfukuza.
BINTI: Je unajua kilichompata
Penina baada ya wewe
kumfukuza?
MIMI: Hapana sijui.
BINTI: Penina alilazimika kwenda
kutoa ile mimba na huko ndiko
akapatwa na umauti. Je nikikupa
lawama juu ya kifo cha Penina
nitakuwa nimekuonea?
MIMI: (Nikiwa nimetumbua
mimacho tu kama mtu
nisiyejielewa), aaah mmh sijui.
BINTI: Na kwanini ulitembea na
Penina wakati ulijua ni mke wa
mtu? Je ulikuwa na lengo la
kumuharibia ndoa yake?
MIMI: (Bado nilijiumauma wala
sikuwa na jibu la moja kwa
moja).
Yule binti wa kitanga aliniangalia
kwa macho makali sana hadi
nikaanza kuogopa, akaingiza
mkono tena kwenye mkoba wake
na kutoka na boxer nyingine,
akaniuliza tena.
BINTI: Na hii je uliiacha wapi?
MIMI: (Nikiwa na mshangao
mkubwa kuwa amezipata wapi
zile boxer, ambazo hata mimi
mwenyewe sina kumbukumbu ya
mahali nilipoziacha. Nikabaki
kutumbua mimacho tu.), mmh
sijui.
BINTI: Unamkumbuka Aisha?
MIMI: Ndio nimemkumbuka, hiyo
boxer niliiacha kwake wakati
baba yake ametubamba kwahiyo
nilivyokimbia nikaisahau.
BINTI: Baada ya wewe kukimbia
nini kilifuata?
MIMI: Aisha alikuja nyumbani na
kudai kuwa ana mimba yangu
kwavile sikutaka makubwa
ikabidi nikimbie ila hata
niliporudi sikupata tena habari
zake.
BINTI: Haya, Aisha naye alienda
kutoa ujauzito wako ili arudi
kwao akiwa mtoto safi kwa
bahati mbaya umauti ukamshika.
Je na yeye hujasababisha wewe
kifo chake?
MIMI: (Nikiwa natetemeka kuwa
vipi mimi nikawa vile hadi hao
wakapatwa na umauti).
Nikiwa natafakari, akatoa tena
boxer nyingine,
BINTI: Na hii uliiacha kwa Nana,
naye alikuwa mke wa mtu.
Kwanini uliiacha?
MIMI: Niliogopa mumewe
angenifumania.
BINTI: Sasa boxer hii ndio
ilimfanya Nana apigwe na
mumewe hadi mauti ikampata. Je
nimlaumu mume au wewe?
MIMI: Hata sijui kitu.
BINTI: Siku zote hujui kitu,
inamaana wewe hutambui
uyafanyayo?
MIMI: Natambua.
BINTI: Je adhabu ulizopata
umeonewa?
MIMI: Hapana sijaonewa.
Akaingiza tena mkono kwenye
mkoba,
BINTI: Na hii uliiacha kwa Salma
kwanini?
MIMI: Salma alikuwa ni demu wa
rafiki yangu ili mwenyewe
asigundue katika harakati
nikaiacha hiyo boxer.
BINTI: Unajua kilichofuata?
MIMI: Rafiki yangu alipoikuta,
Salma akamwambia ukweli ila
Salma alipokuja kwangu
nikalazimika kumtimua kwani
sikutaka kugombana na rafiki
yangu sababu ya mwanamke.
BINTI: Na Salma alikosa
mwelekeo akanywa vidonge na
kujiua kwaajili yako.
MIMI: (Nikiwa nashangaa sana,
kwani sikujua kama Salma alijiua
kwaajili yangu).
BINTI: Mabinti wengi wametoa
mimba kwaajili yako na hiyo ni
sababu tosha ya mimi kwenda
kuivuruga mimba ya demu wako
wa dar.
MIMI: (hapo ndio nikaelewa
kwanini mimba ya demu wangu
wa dar ilitoka), haaa kumbe!!
Akaingiza mkono tena na kutoa
boxer nyingine,
BINTI: Hii pia uliiacha kwa
Tamari, niambie kuhusu Tamari.
MIMI: Tamari alikuwa ni rafiki
wa demu wangu, nakumbuka ni
yeye alinilazimisha niache boxer
kwake.
BINTI: Vipi alipokwambia
anaujauzito wako?
MIMI: Nilijua ni mbinu zake za
kuniachanisha na mpenzi wangu,
kwahiyo nikamkana.
BINTI: Naye akaenda kutoa
mimba na kufa. Je unajua
kwanini wasichana wengi
wanakufa wakienda kutoa
ujauzito wako?
MIMI: Hapana sijui.
BINTI: Nitakwambia sababu.
Akaniangalia na kunikazia macho
sana, safari hii alitoa boxer na
kuongea kwa ukari,
BINTI: Katika boxer zote na
matendo yake machafu, hii ndio
boxer iliyonikera na ndiyo
itakayofanya upate adhabu tena.
Akainuka na kuniambia kuwa
nimuandalie majibu
yanayoeleweka juu ya ile boxer.
Bado sikujielewa kwanini
nilikuwa naacha zile boxer na
kwanini ziniletee matatizo kila
sehemu nilipo ziacha. Na bado
nikajiuliza kwanini hao wadada
walikufa wakati wanatoa ujauzito
wangu, bado sikuwa na jibu ila
nikangoja majibu kwa huyu binti
wa kitanga ambaya hadi muda
huo sikuelewa ni jini au ni
mchawi au ni mzimu au ni mtu
wa aina gani kwani bado
alinichanganya sana.
Nikiwa sijielewi elewi kabisa na
huku nikijiuliza maswali mengi
mengi.
Yule binti wa kitanga akarudi na
kunishtua,
BINTI: Haya niambie ni wapi
uliacha hii boxer?
MIMI: Samahani, niliacha kwako
kwa bahati mbaya.
BINTI: (Akacheka sana), bahati
mbaya! Ulikuwa na maana gani?
MIMI: Sikuwa na maana yeyote
ile nilijisahau tu.
BINTI: Ulijisahau tu au ulitaka
kuonyesha jinsi gani wanipenda?
MIMI: Aaah mmh sijui.
BINTI: (Akacheka tena), kwahiyo
hukunipenda?
MIMI: Naam!
BINTI: Kwani nimekuita au
nimekuuliza, kwahiyo
hukunipenda?
MIMI: Mmmh Sijui.
BINTI: Wewe una matatizo sana,
yani hujui kama ulinipenda au
la?
MIMI: Mmmh ndio sijui.
Akaniangalia kwa macho makali
sana kama vile anasoma kitu
kwenye ubongo wangu. Nikawa
na mawazo ya uoga kichwani
mwangu, akanigeukia na
kuniuliza tena.
BINTI: Unamjua Leila?
MIMI: Ndio namjua.
BINTI: Eeh kwanini ulimdanganya
yeye na familia yake kuwa
unaenda kutoa mahari?
Nikabaki natoa mimacho tu na
kushangaa huyu binti ameyajuaje
yote hayo, maana nilipokuwa na
Leila nikapenda niwe nae karibu
zaidi kwahiyo nikaenda kupeleka
barua kwao ili nitambulike ila
ilipofika kipindi cha mahari hapo
ndio utata ulianza maana sikuwa
na jinsi zaidi ya kuwadanganya
kuwa nitaenda ila
nikawapotezea. Nikashangaa sana
huyu binti amejuaje.
Akaniuliza tena,
BINTI: Kwanini hukumfatilia tena
Leila?
MIMI: Ujana tu ndio ulinisumbua
dada.
BINTI: Heeee, nishakuwa dada
yako tena?
MIMI: Mmmh aaah sijui.
Akacheka sana na kuniangalia
kwa dharau,
BINTI: Haya unajua kwanini
wanakufa wakitoa mimba zako?
MIMI: Sijui chochote.
BINTI: Wanakufa kutokana na
zindiko ulilofanyiwa ukiwa
mdogo, mama yako ukimuuliza
atakwambia.
MIMI: Mmmmh
BINTI: Je unajua hatma ya Leila
ilikuwaje?
MIMI: Sijui.
BINTI: Leila alichanganyikiwa
sana kwa aibu uliyompa kwao,
akaamua kujiua. Tatizo
umetembea na wanawake wengi
ndiomana ukimwacha mmoja
humfatilii tena.
Bado nikawa sijielewi na mawazo
lukuki juu ya huyu binti wa
kitanga.
Akaniambia nimuulize swali
nitakalo.
MIMI: Vipi mchumba angu wa
dar, je ni mzima?
Akacheka sana, kisha akaniambia
nimfuate. Nikainuka na kuanza
kumfuata, mara gafla nikamuona
Leila amesimama mbele yangu,
nikaanza kutetemeka na kuogopa
sana, nikiwa sijielewi nilistukia
nikichapwa viboko kila sehemu.
Mbele yangu alikuwepo Leila na
yule binti wa kitanga, nilichapwa
sana hadi nikapoteza fahamu.
http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Niliposhtuka nilikutana na giza
nene yani sioni chochote cha
mbele yangu. Nilipoinuka mahali
pale, nikaanza kutembea kwa
kupapasa ila kila nilipokanyaga
nilikanyaga mwiba kumbe pale
chini palijaa miba mitupu.
Kwahiyo ikanipasa kutembea
kwa tahadhari, nilipofika mbele
nikakutana na yule binti wa
kitanga, akaniambia "njoo huku"
nikawa namfata, kufika mbele
gafla akatokea binti mmoja
niliyemjua kwa jina la Salma,
huyu alikuwa ameshika gongo
kubwa sana akanibamiza nalo
kichwani, nikaanguka na
kupoteza fahamu.
Kuja kushtuka nilikuwa kwenye
mto mkubwa tena katikati,
nilitetemeka sana mwili ulipatwa
na baridi ya ajabu, nikaogopa
sana pale katikati ya mto.
Nikaanza kujikongoja taratibu ili
niweze kutoka kwenye ule mto,
wakati nafika juu yani
nimeshatoka mtoni akatokea mtu
na kunisukuma tena gafla mtoni
nikawa natapatapa na
kuhangaika, kumwangalia vizuri
yule mtu ni yule binti wa kitanga,
nikabaki natahamaki na
nikaamua kumuuliza.
MIMI: Je hizi ndio adhabu zangu?
BINTI: (Akacheka sana), hapana
hapa tunacheza tu kama
kombolela, adhabu yenyewe ni
moja tu utaipata.
Nikanyong'onyea gafla kwani
mwili wote ulikuwa una niuma
yani kila sehemu ni maumivu
tupu.
Nikawa natetemeka sana ndani ya
ule mto na yule binti wa kitanga
alizidi kunicheka pale juu.
Nikaanza tena kujitoa kwenye ule
mto, nikajitahidi kutoa na
kujikongoja tena hadi juu,
nikawa namfata yule binti wa
kitanga cha kustaajabisha
akatoweka, nikaanza kuogopa na
hofu kubwa ikanitanda moyoni.
Mara mvua kubwa ya gafla
ikaanza kunyesha, nikaamua
kukimbilia mti uliokaribu ili
nijikinge na ile mvua, nilipofika
pale chini ya mti, mara upepo
mkubwa ukaanza kuvuma na
kusababisha ule mti kudondoka,
nilitoka mbio na kuwa mbali na
ule mti wakati unaanguka.
Mvua nayo iliendelea kunyesha
tena kwa wingi kabisa, nikawa
kama mnyama porini,
nilitetemeka sana na hata nisijue
cha kufanya kwani nilikuwa
natembeatembea bila uelekeo wa
maana, mvua iliendelea kunyesha
na kufanya nizidi kutetemeka
kwa baridi.
Mara gafla likaanza kuwaka jua
kali sana tena lile jua la kuchoma
utosini, nikazidi kushangaa na
kustaajabu.
Mbele yangu ikatokea nyumba,
nikaanza kujiuliza mbona ile
nyumba sikuiona mwanzoni.
Nikaamua kuisogelea ile nyuma
na kujaribu kubisha hodi ila
hakuna aliyeniitikia.
Nikaamua kuingia ndani
hivyohivyo, nikakutana na mbibi
akiwa anaota moto hata
nikamshangaa kwa jua lile
anaotaje moto, ikabidi nianze
kwa kumsalimia
MIMI: Bibi shikamoo.
BIBI: Marahaba, nilijua tu ukiona
nyumba utakuja.
MIMI: Na mbona unaota moto
wakati kuna joto?
BIBI: Unajua mara nyingine
inabidi tufanye vitu kinyume
chake, usipende kuishi kwa
mazoea.
MIMI: Kivipi bibi?
BIBI: Ndio kama hivi, mimi naota
moto wakati ni joto. Wewe
umezoea nini maishani?
MIMI: Nimezoea maisha ya
kawaida bibi.
BIBI: Kwahiyo maisha unayoishi
sasa ni ya kawaida?
MIMI: Hapana, naona majanga tu.
BIBI: Najua mambo yameenda
kinyume, hukutarajia jambo hili.
Ngoja nikwambie.
MIMI: Niambie bibi.
BIBI: Siku zote katika maisha
unapofanya jambo kinyume
huwa linaumiza wengine, au
mimi sikuumizi wewe hapa
ninavyoota moto wakati ni joto?
MIMI: Kweli naumia bibi.
BIBI: Basi unapofanya jambo
kinyume na ukalizoea linakuwa
kawaida ingawa linawaumiza
wengine, ndio hivyo na wewe
unapopatwa na kinyume cha
uliyozoea lazima utaumia.
Umejifunza nini hapo?
MIMI: Nimejifunza kuwa
kinyume nilichofanya mazoea
ndio kimekuwa kinyume changu
sasa.
BIBI: (Akacheka), unapenda
wasichana wazuri na wakuvutia,
kila uwaonapo macho yako
hayakuishi hamu. Mjukuu wangu,
hii ni Tanga, mji mzuri wenye
matunda ya kupendeza na
mabinti wazuri.
MIMI: Unamaana gani bibi?
BIBI: Nina mabinti wengi sana
tena ni wazuri sana kazi yao ni
kuwapata vijana wenye tamaa
kama nyie.
MIMI: (Nikiwa nimetoa mimacho
tu), sielewi bibi.
BIBI: Damu za wengi zimekulilia
wewe ila mabinti zangu
wanafanya kazi nzuri sana kwani
mwanaume yeyote mwenye
tamaa kama yako awaonapo
lazima ashtuke. Ngoja nikuitie
watano uwaone.
Yule bibi akanyosha mkono juu
kama ishara ya namba tano, mara
wakatokea mabinti wazuri sana
na wenye mvuto wa kipekee,
nikabaki kuwaangalia tu.
BIBI: Unamtaka yupi kati yao?
MIMI: Hapana bibi sihitaji
mwanamke yeyote.
Yule bibi na wale mabinti wote
wakacheka sana halafu wale
mabinti wakatoweka.
BIBI: Sogea karibu nami ili tuote
moto vizuri, (huku akiendelea
kuchochea kuni zake).
Nikawa nasita kuusogelea moto
ule, akaniamuru tena nimsogelee
pale. Duh kufika karibu ni kama
jehanamu ndogo maana ule moto
unaunguza taratibu mmh!! Yule
bibi akaniangalia, yani ingawa ni
mzee ila alionyesha kuwa na sura
nzuri sana. Akaniuliza,
BIBI: Unajisikiaje sasa?
MIMI: Naungua bibi.
BIBI: Basi hii ni raha ya kufanya
vitu kinyume mjukuu wangu.
Nikabaki nikimwangalia yule bibi
na hata nisimmalize, mara
akachukua glasi na kumimina
kitu ndani yake na kunikabidhi,
BIBI: Karibu maziwa mjukuu
wangu.
MIMI: (Nikapokea huku
nikiangalia na kustaajabu), bibi
mbona hii ni damu?
BIBI: Mbona unakuwa si
muelewa mjukuu wangu?
Nimekwambia kuwa hapa
tunafanya vitu kinyume, sasa
unashangaa nini kunywa!
Nikiwa bado nimeishika ile glasi
na kuendelea kutafakari, mara
yule bibi akasema,
BIBI: Na usistaajabu
utakapotakiwa kutembelea
kichwa badala ya miguu,
(akacheka sana).
Bado nilikuwa kama mtu
niliyepigwa na bumbuwazi bila
ya kuwa na majibu na pale ule
moto ulizidi kunichoma tu.
Mara yule bibi akainuka ila
akawa anatembea
kinyumenyume huku akicheka,
na akarudi akitembea
kinyumenyume vilevile.
BIBI: Hata ukitaka kuyarudia
maisha ya kawaida utakubidi
utembee kinyumenyume hadi
utakapofika.
MIMI: Nionyeshe njia basi bibi.
BIBI: Kunywa maziwa kwanza.
Akatoa na bakuri na kunikabidhi,
BIBI: Tafuna na hizo karanga, ni
tamu sana na hayo maziwa.
MIMI: Jamani bibi, mbona ni
mavi ya mbuzi?
BIBI: Jifunze kuwa muelewa
utashinda.
Nikawa nimeshika kile kibakuli
chenye mavi ya mbuzi na ile glasi
yenye damu hata nisielewe
nakula vipi vitu hivi.
BIBI: Unapotumia kitu kinyume
na wewe fanya kinyume chake
utajikuta umekizoea na kuona
cha kawaida.
MIMI: Jamani bibi, ndio nile mavi
ya mbuzi na damu kweli?
BIBI: Bora ule maana
nitakapokuletea maji ya kunywa
hapa ushushie utakuwa umepata
uzoefu kidogo.
MIMI: Khaaaa kama damu ndio
maziwa na mavi ya mbuzi ndio
karanga je hayo maji ni nini?
BIBI: (Akacheka sana), na hata
nikikwambia hiyo damu ni damu
gani utazidi kupagawa ni kheri
ule ushibe hicho
nilichokuandalia.
Bado maswali mengi
yaliniandama, je hii damu ni
damu ya nini? Bado sikupata jibu
nikawa najipanga kumuuliza
huyu bibi aniambie ukweli
vyovyote vile sina jinsi.
MIMI: Samahani bibi, niambie hii
ni damu ya nini?
BIBI: Unataka kujua kweli?
MIMI: Ndio nataka kujua bibi.
BIBI: Kunywa kwanza nikwambie.
Bado moyo wangu ulisita kunywa
ile damu na kula yale mavi ya
mbuzi.
Nikawa bado naiangalia ile damu
na kuitafakari, bibi akaendelea
kuniamuru kuwa ninywe.
BIBI: Uzima wako upo humo, ni
bora unywe tu kwa hiyari yako.
Nikajaribu kunywa ile damu ila
kinyaa kilizidi kunishika.
Bibi akaniangalia kwa jicho kali
sana na kusome.
BIBI: Nimeshakwambia
unapokula vitu hvyo weka
kinyume chake utaona ni
kawaida tu. Narudia tena, uzima
wako upo humo.
Ikabidi nifanye kama alivyosema
kuwa damu ni maziwa na mavi
ya mbuzi ni karanga. Ila nikala
kidogo tu na kumrudishia,
MIMI: Asante bibi nimeshiba.
BIBI: Hapana, hutakiwi kubakisha
unatakiwa umalize vyote na
kikombe ukilambe kuonyesha
kuwa umeridhika na ladha yake.
MIMI: Bibi ila vimenishinda
kwakweli.
BIBI: Hiyo ni lazima ule, yani
utake usitake. Je ungependa
nikwambie hiyo damu ni ya nini?
MIMI: Ndio niambie.
BIBI: Mwanamke akiwa kwenye
siku zake huwa anatoa uchafu, na
uchafu huo huwa kwenye mfumo
wa nini?
MIMI: Huwa ni damu.
BIBI: Basi hiyo ni damu ya
mwanamke akiwa kwenye siku
zake.
MIMI: Aaargh mbona umenipa
uchafu jamani?
BIBI: (Akacheka sana), haya
kunywa sasa.
MIMI: Hapana, siwezi kunywa
uchafu.
Mara yule bibi akanipulizia kitu,
nikawa kama nimepumbazika
nikajikuta nikiyala yale mavi ya
mbuzi na kuinywa ile damu, ila
nilipomaliza tu nikawa kawaida,
nilitamani kutapika kabisa yani.
Mara akanipa glas nyingine na
kuniambia,
BIBI: Chukua na maji ya kunywa
ushushie.
MIMI: (Yani ile kuangalia hadi
kichefuchefu), jamani bibi mbona
ni mate tena yamechanganyika
na makohozi.http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
BIBI: Inakupasa unywe na hapo
utajifunza kuona kinyaa cha yale
uliyoyafanya.
MIMI: Aaah bibi, siwezi kunywa
mate kwakweli.
Akanifanyia kama mwanzo,
nikajikuta nikinywa ile galsi
yenye mate hadi kuimaliza,
halafu nikawa kawaida. Yule bibi
akawa ananiangalia na kusema,
BIBI: Kuna juice pia inapaswa
unywe, ngoja nikupe.
Akachukua glasi na kunikabidhi.
MIMI: Loh bibi jamani ndio
usaha kweli?
BIBI: Ndio, kunywa juisi hiyo.
MIMI: Siwezi bibi yani ninywe
usaha kweli dah!
Akafanya kama mwanzo, na ule
usaha nao nikanywa. Mara gafla
nikaanza kuumwa na tumbo hadi
nikawa nalia na kugalagala chini,
yule bibi alikuwa akicheka sana,
na mimi nilizidi kuugulia.
Wakati nalia vile, wakaja
wasichana wazuri na
kunizunguka mahali pale,
kwakweli sikuona hata uzuri wao
kwa maumivu yale ya tumbo,
niliugulia sana na hakuna
aliyenisaidia.
Baada ya kuugulia kwa muda
mrefu, bibi akanipa glasi na
kuniambia.
BIBI: Kunywa hii ni juisi ya
machozi itapoza maumivu yako
ya tumbo.
Kunywa machozi haikuwa shida
kwangu kwani nilishakunywa
vingi visivyonywewa,
nikaichukua ile glasi ya machozi
na kunywa, ilikuwa ina ladha
kama ya chumvichumvi hivi.
Nilipomaliza kunywa tu na yale
maumivu yakakatika.
BIBI: Unajua kwanini umeumwa
na tumbo?
MIMI: Sijui bibi.
BIBI: Kwasababu ulikuwa
unakataa kula chakula chetu.
MIMI: Nahitaji kurudi kwenye
maisha ya kawaida, nirudisheni
tafadhari.
BIBI: Unadhani ni kazi rahisi?
MIMI: Sijui kwakweli.
BIBI: Je unaweza kuifanya jana
kuwa leo?
MIMI: Siwezi.
BIBI: Lazima ifanyike kazi ya
ziada ili uwe kawaida na si
kinyume tena.
MIMI: Basi bibi nisaidie.
Bibi akaniangalia tu, mara
akawaita tena wale mabinti wa
tano.
BIBI: Chagua mmoja uwe nae kila
utakapokwenda.
MIMI: Hapana bibi, sitaki
mwanamke.
BIBI: Sasa wewe unataka nini?
MIMI: Nataka niwe kwenye
maisha ya kawaida.
BIBI: Ngoja uone kwanza.
Akanionyesha mahali kwenye
watoto wengi wakilia na mahali
pengine wanawake wengi
wakilia. Halafu akaniuliza.
BIBI: Upande upi unaonyesha
huruma zaidi?
MIMI: Pande zote zaonyesha
huruma ila zaidi Ni ule upande
wa watoto.
BIBI: Umewaonea huruma
watoto, ni sawa kabisa. Na
kwanini hukupenda
kuwahurumia wakiwa tumboni
ili nao watoke wakiwa kama
wewe?
Nikakaa kimya kwani sikuwa na
la kujibu.
Bibi yule akanichukua na
kunifungia kwenye chumba, kile
chumba kilikuwa na sisimizi na
siafu wengi nao wakaning'ata
sana hadi vidonda vikanijaa.
Baada ya muda akanifungulia na
kuniuliza,
BIBI: Umejisikiaje wakati wale
wadudu wanakung'ata?
MIMI: Nimeumia sana na
maumivu yake hayaelezeki.
Akachukua majivu na kunipaka
mwilini, huku akiniambia,
BIBI: Ukitaka tusiendelee
kukufatilia fata kile
watachokwambia.
MIMI: Nitafanya vyote bibi,
sitapuuza hata kimoja.
Akachukua na damu nayo
akanipaka mwili mzima, kisha
akasema,
BIBI: Umependeza sana mjukuu
wangu.
Nikabaki namtazama tu huku
macho yangu yamejawa na
huruma tupu na yakionyesha
kuwa nahitaji msaada na
kuhurumiwa.
Kufumba na kufumbua, sikuwa
tena kwenye ile nyumba na wala
yule bibi hakuwepo ila nilijikuta
niko peke yangu chini ya mti, cha
kushangaza ule mti ulikuwa na
mdomo na macho. Nilitetemeka
sana. Kila nilipouangalia nao
ulinichekea, nikatetemeka sana
mahali pale na kuanza kurudi
kinyumenyume, wakati nafanya
hivyo uli mti ulikuwa ukizidi
kucheka huku nao ukinifata.
Kwakweli mkojo ulinitoka, wakati
narudi vile kinyumenyume kuna
kitu nikakigonga kwa nyuma kwa
haraka kabisa nikageuka na
kuangalia, Mungu wangu,
alikuwa mtu mrefu sana mbele
yangu sikuweza hata kumtazama,
akachukua mkono wake na
kushika shingo yangu huku
akinining'iniza juu juu nikawa
natetemeka huku ninalia sana.
Alichokifanya sasa ni kunitupa
toka kule juu hadi chini, na hapo
hapo nikapoteza fahamu.
Kuja kushtuka, Mungu wangu
sikutegemea nilichokiona mbele
yangu.
Sikutegemea nilichokiona,
niliposhtuka nikajikuta nipo
kitandani, nikamwona mpenzi
wangu akiwa pembeni yangu
pale kitandani, nikawa nashangaa
shangaa tu.
Nikamwona yule mpenzi wangu
akifurahi sana kuwa nimeamka
na akaharakisha kwenda nje,
kurudi ndani akawa
ameongozana na yule mdada
aliyekuja na mke wa rafiki yangu,
yule mdada mwenye maruhani.
Nikawa bado nashangaa shangaa
tu. Bado sikuelewa kitu, nikazidi
kushangaa shangaa tu. Kitu cha
kwanza kabisa nikawaambia,
MIMI: Naombeni maji ya kunywa.
Kabla sijajibiwa, mara simu
yangu ikaanza kuita muda ule ule
niliposhtuka, nikawa napapasa ili
niipokee, mara yule mdada wa
mwanzo akaniamuru nimpatie ile
simu, nilipompatia akaniambia,
MDADA: Hii ndio
imekusababishia mambo yote.
Nikashangaa kivipi simu
imenisababishia mambo yote
yale. Na alipoichukua yule dada
ile simu ikaacha kuita.
Kwanza nikawa sielewi wala
siamini kama nipo kwenye
ulimwengu wa kawaida.
Nikaanza kuwashangaa tu yule
mdada na mpenzi wangu, huku
nikijiuliza maswali mengi mengi
imekuwaje wakawa pamoja na
wengine wako wapi. Pia
nikashangaa kile chumba kwani
kilikuwa ni chumba tofauti
kabisa na chumba changu.
MIMI: Mbona humu sio
chumbani kwangu? (huku
nikizidi kushangaa).
MDADA: Ipo sababu kubwa ya
kukuondoa mule kwenye chumba
chako.
MIMI: Mbona sielewi?
MDADA: Ndio huwezi kuelewa
mpaka utakapoeleweshwa.
MIMI: Niambieni kwanza, nipo
dunia ya kawaida au dunia ya
kinyumenyume?
MDADA: (Akacheka), upo
kawaida, na upo salama sasa. Ila
usalama wako utaongezeka pale
utakapoamua kuinuka hapo ili
twende baharini ukaoge maji ya
bahari, na hii simu(akionyesha
ile simu yangu aliyoshika),
tunaenda kuitupa baharini.
Sikuweza kubisha wala kupinga,
nikainuka pale nikiwa mimi yule
mdada na mpenzi wangu.
Tukakodi kibajaji kikatupeleka
hadi baharini.
http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kufika pale baharini,
nikajishangaa nimekuwa mzito
sana kuitupa ile simu, nikajikuta
nikisita kufanya hivyo. Yule
mdada akaniambia,
MDADA: Unapenda kuishi maisha
ya kawaida?
MIMI: Ndio napenda.
MDADA: Basi tupa hiyo simu.
MIMI: Ila simu yangu ni ya
gharama sana jamani.
MDADA: We itupe tena uirushe
mbali kama unayapenda maisha
yako, nitakupa sababu ya kufanya
hivyo.
Roho iliniuma sana kila
nikiangalia ile simu, nilizidi
kuumia moyoni. Yule mdada
akaniangalia tena kwa macho
makali na kusema,
MDADA: Tupa hiyo simu.
MIMI: Ujue nilinunua laki tano
hii simu!
MDADA: Haya, laki tano na
maisha yako kipi bora?
MIMI: Bora maisha yangu.
MDADA: Basi itupe hiyo simu.
Bado nikawa nasitasita,
nilimtazama mpenzi wangu naye
aliniangalia kwa jicho la huruma
sana, nikapatwa na mfadhaiko
wa moyo nikakumbuka yote
niliyowatenda wadada kwa tamaa
zangu. Nikakumbuka mateso
niliyopata kwenye dunia ya
kinyumenyume.
Hapo nikaamua kuchukua
maamuzi magumu na kuirusha
ile simu katikati ya maji, mara
gafla nikashtuka,
MIMI: Aaah laini yangu!!
MDADA: Imefanyaje?
MIMI: Nimeitupa nayo.
Kabla hajaniambia kitu tena mara
gafla tukaona moshi mwingi
ukitokea pale nilipoirusha ile
simu, nikaanza kutetemeka kwa
uoga. Yule dada akaniambia
kuwa niingie kwenye maji ili
niweze kujisafisha zile nuksi na
mabalaa. Ila bado sikujua wale
ndugu niliowaacha ndani ni nini
kimewapata, je ni wazima au
wamekufa, nikaamua kumuuliza
yule dada,
MIMI: Na ndugu zangu je ni
wazima au wamekufa?
MDADA: Hilo swali niulize baada
ya kujisafisha ndio nitakupa jibu.
Nikamwangalia tena yule mpenzi
wangu bado alionyesha huruma
sana na hata sikumwelewa kuwa
ananihurumia mimi au
anaonyesha huruma ya nini.
Nikaangalia tena pale
nilipoirusha simu yangu bado
palikuwa panafuka moshi.
Yule mdada akaniamuru tena
kuwa niende kwenye maji
nikaoge, ila nikawa nasita
kufanya hivyo na yule mpenzi
wangu alizidi kunyong'onyea na
pia alizidi kuonyesha huruma.
Nikaamua kwenda kuoga hayo
maji ya bahari, yule dada
akanielekeza sehemu ya kwenda
kuoga ilikuwa ni mbali kidogo na
pale nilipoitupa ile simu yangu
na pia akanionya kuwa nisifike
pale nilipoitupa simu
yangu.http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Nikiwa ndani ya maji ya bahari,
wazo likanijia kuwa nisogee
karibu zaidi na nilipoitupa ile
simu labda nitaiona tena.
Nikawa nimesogea karibu huku
nikiwa kama naogelea kumbe
najaribu kupapasapapasa, ili
kama nikiipata basi niitoe ile
laini yangu tu. Mara gafla maji
yakawa ya moto sana mule
baharini hadi yakawa
yananiunguza, wakati nataka
nikimbilie nchi kavu, nikakuta
kuna mtu amenishika bega kwa
nyuma ile kugeuka ni macho kwa
macho na binti wa kitanga,
amefikaje na anataka nini sijui.
Nilipogeuka nyuma nikakutana
macho kwa macho na binti wa
kitanga, nilianza kutetemeka kwa
hofu na uoga, akawa ananiangalia
huku anacheka nikazidi
kutetemeka. Nilipoangalia kule
nchi kavu nilimwona yule mdada
akininyoshea mkono kama ishara
ya kuniita, nikawa najitahidi
nitoke ila yule binti wa kitanga
alining'ang'ania na hadi nafika
nchi kavu yeye alikuwa nyuma
yangu.
Yule mdada akaniuliza tena kwa
ukali,
MDADA: Umefanya vitu gani
wewe?
MIMI: Sijui.
MDADA: Hujui nini? Unadhani
angekufuata huyo bila sababu?
MIMI: Naomba nisaidie basi,
nilienda kule nilipoitupa ile simu.
MDADA: Yani wewe umeharibu
kila kitu.
Nikamwona yule dada akichukua
kiwembe na kuja karibu yangu,
akanichana kwenye mkono,
nilipatwa na maumivu makali
akanizuia kusogea popote mpaka
pale aliponichana pakikauka
damu.
Nikiwa naugulia yale maumivu,
nikamwona yule dada akienda
pembeni na kuongea kitu na
mpenzi wangu, mara wote
wakanisogelea pale.
Nikamwona yule dada akichukua
tena kiwembe na kumchana
mpenzi wangu mkononi halafu
akachukua ile damu iliyokuwa
inamtoka mpenzi wangu na
kunipaka shingoni halafu yeye na
yule mpenzi wakasogea mbali.
Kwa muda mchache nilihisi kama
nataka kukata roho kwani
maumivu yaliyonipata pale
shingoni yalikuwa makubwa
sana, hadi nikajikuta nikianguka
kwenye maji na kuanza
kutapatapa.
Ninachokumbuka nilipoteza
fahamu.
http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Niliposhtuka nilijikuta nipo
nyumbani, nimelala kwenye
jamvi na wote ninaowafahamu
wakiwa wamenizunguka, hadi
yule mdada nilimwona pale
kasoro mpenzi wangu tu ndiye
hakuwepo pale.
Wote niliwakuta wamefurahi na
nilikuwa kama mtu niliyepoteza
dira.
Wakaniacha nipumzike bila
kuniuliza chochote.
Baada ya siku mbili, ikabidi
niongee nao kwani nilikuwa
sielewi chochote.
MIMI: Mama mbona sielewi
chochote, ilikuwaje kwani?
MAMA: Ni vigumu kuelezea ila
umetufanya kupata majeraha
yasiyosahaulika kamwe.
MIMI: Na kile chumba changu
imekuwaje mama?
MAMA: Kile chumba
tulikirudisha kwa mwenye
nyumba kwani ungeendelea
kukaa pale kungekuwa na
makubwa zaidi.
MIMI: Ila mama, inaniwia
vigumu kukuelewa.
Basi mama akamwita yule mdada
ili nipate kuzungumza naye pia.
MDADA: Sikia, janga ulilolipata ni
kubwa sana. Mimi nisingeweza
kukusaidia ila babu yangu ni mtu
wa huko na anajua vitu vingi.
MIMI: Kwahiyo watu
walioanguka chumbani kwangu,
waliamkaje?
MDADA: Kuna dawa niliwapaka
wakaamka, ile dawa
iliwezakufanya kazi baada ya
wewe kukubali kujitoa kafara.
MIMI: (Kuna kitu nikajifikiria na
kuamua kuuliza), mbona wakati
nipo kwenye ulimwengu usio wa
kawaida simu yangu sikuiona
halafu niliposhtuka kawaida
ikaanza kuita?
MDADA: Simu yako haikuwa
simu ya kawaida, yule dada
alikubadilishia simu muda mrefu
sana ndiomana kila jambo
ulilotaka kufanya ukiwa na ile
simu aligundua kwa haraka.
Nikawa nawaza amebadilishaje,
na mbona nilikuwa naiona
kawaida.
MIMI: Ila ndugu zangu ni
wazima?
MDADA: Ndio ni wazima ila...
MIMI: (Nikadakia), ila nini na
yuko wapi mpenzi wangu?
MDADA: Ndio huyo ninayetaka
kumuongelea.
MIMI: (Huku mapigo ya moyo
yakienda mbio), kafanyaje?
MDADA: Amejitoa kwaajili yako.
MIMI: Sikuelewi, unamaanisha
nini?
MDADA: (akainamisha kichwa
chini na kuniambia), kwa bahati
mbaya tumeshindwa kumwokoa
kwahiyo amekufa.http://
deusdeditmahunda.blogspot.com/
Nilihisi utumbo ukijisokoto na
tumbo likaanza kuniuma gafla.
MIMI: Hapana hapana sitaki
kuamini.
MDADA: Huo ndio ukweli.
Niliona machozi yakinitoka,
nilijisikia vibaya kujua yule
msichana ambaye ni mpenzi
wangu amekufa kwaajili yangu.
Roho iliniuma sana.
Wakawepo watu pale kunifariji
na kunipa moyo. Nikajiona
nimepata kovu ambalo
sitalisahau tena.
Rafiki yangu akaja pale na kunipa
moyo.
RAFIKI: Pole sana ila yote ni
mapito tu.
MIMI: Asante ila nimeumia sana.
RAFIKI: Hata sisi hatuelewi, na je
sikuzote ulizopoteza fahamu
ulikuwa wapi? Maana yule dada
alituambia kwamba upo eneo la
hatari sana.
MIMI: Ni kweli tena yalikuwa
majanga sana ila ninachoweza
kusema hadi sasa ni kuwa
SITAISAHAU TANGA.
MWISHO

Tanga kunani... Story nzuri...

Chapter Closed...


Cc: mahondaw
 
Back
Top Bottom