Simulizi: Sehemu isiyo na jina

bioto

JF-Expert Member
Oct 1, 2017
1,261
2,095
A PLACE WITH NO NAME.
(Sehemu isiyo na Jina)
SEHEMU YA (1)
Mtunzi........hemed mayugu
UTANGULIZI.
Ni Hadithi nzuri iliyoandikwa na Jumanne katika
kitabu chake alichokitoa mwishoni mwa mwaka wa
elfu mbili na kumi na Moja, ni hadithi ambayo watu
wengi waliipenda, hasa vijana wengi wa Tanzania na
hata watu kutoka inchi za Jirani kama Kenya na
Uganda. Vijana wengi waliyoisoma hadithi hii wengi
wao walitokwa na machozi pia wengine wakifurahi
kutokana na visa vilivyo mkuta Jumanne. Kutokana
na matukio kuwa mazito mengine ya ajabu watu
wengi walithubutu kumtafuta Jumanne kupitia simu
na wengine wakituma ujumbe kwa barua pepe
ilimradi tu wapate uhakika juu ya alichokuwa
amekiandika. Wengi walikuwa hawaamini kama ni
kweli alifika eneo hilo, alikutana na visa alivyokuwa
ameviandika kwenye kitabu chake cha A place with
no name, Eneo hilo lipo? Majawabu yake yalikuwa
ya kweli kwani hata ndugu zake walithibitisha hilo
pale walipojumuika naye kwenye vyombo vya habari
ili kuwambia watu kuusu sehemu ambayo aliishi
miezi kadhaa kisha akatokako kwa msaada wa Mtu
wa uko aliko Kuwa. Nyuma ya hilo Jumanne alikuwa
na Siri nzito ambayo hakupaswa kabisa kuisema
kwa Mwanadamu yeyote ambaye anaishi katika
ulimwengu huu baada ya kufanikiwa kutoka katika
sehemu isiyo na jina. Jumanne alionywa na mtu
aliyemsaidia kutoka katika ulimwengu wa ajabu,
ulimwengu ambao alikuwa aamini kama upo katika
uso wa Dunia. Kutokana na kukeleketwa na siri
ambayo hakupaswa kuisema kwa mtu yeyote
Jumanne alishindwa kuvumilia akajikuta anaisema
Siri hiyo nzito. Je nini kilimkuta Jumanne baada ya
kuisema siri ambayo hakupaswa kabisa kukifumbua
kinywa chake kwa ajili ya kuitoa siri hiyo, na ni Siri
gani hiyo, na aliyemwambia asiitoe siri hiyo ni nani,
je viumbe waliyokutana naye walikuwa wa aina gani.
Soma hadithi ya maisha ya Jumanne mwenyewe
akielezea ukweli wa maisha yake katika kitabu
chake cha A place with no Name, kisha Mimi
nitakuendelezea ni nini ambacho kilimkuta Jumanne
baada ya kuitoa siri nzito ambayo alikatazwa asiitoe
kutoka kwa ndugu zake. Hadithi yake inaanza hivi.
""Kwa jina naitwa JUMANNE A. MWAKYOMA Ni
mzaliwa wa mkoa mpya wa RUNGWE. Kwa
wasiojua rungwe ilikuwa wilaya ya mkoa wa mbeya
na ndio ilikuwa makao makuu ya wilaya. Lakini Kwa
sasa ni Mkoa mpya katika mikoa 30 ya Tanzania
pia mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Mbeya
university of science mwaka wa tatu. Hii ni simulizi
inayo nihusu. Isome na ukimaliza kusoma uwache
comment pia share na like page yetu. Ku-like page
bofya Link/maandishi ya bluu hapo Chini.
Nakumbuka ilikuwa tarehe 6/8/2012. Ni siku
ambayo kamwe sitoisahau,
Ilikuwa ni siku ambayo niliaga nyumbani kwenda
kutarii kwenye vivutio vya mkoa wetu wa rungwe.
kama mnavyojua mkowa wetu unavivutio vingi vingi
na vya maajabu yake kama mlima Rungwe, bwawa
la mungu, na ziwa ngozi na vingine vingi.
Siku hio Nakumbuka nilichukua begi langu la
mgongoni nikaweka karanga kama robo, zilikuwa
zimekaangwa, maji ya kunywa pamoja na soda ya
chupa (fanta) niliaga nyumbani na kuondoka
kuelekea polini nia yangu ilikuwa ni kwenda kuliona
ziwa NGOZI, ziwa ambalo watu wanaliogopa
wakirihusisha na imani za kishirikina. Na
inasemekana ziwa ilo ukiingia kuoga utoki, wewe
utaishi huko huko.
Nilifanikiwa kufika sehemu ya ziwa hilo salama japo
ziwa hilo limezungukwa na msitu ambao si wa
kawaida pamoja na milima labda ndo maana watu
wanaogopa, nilipata kuliona ziwa hilo, ni ziwa
dogodogo unaweza kusema bwawa kubwa lakini
ndio hivyo lenyewe ni ziwa. Nilikaa kama masaa
mawili pale kando ya ziwa lile huku nikitafuna
karanga zangu nikishushia na soda. Mazingira ya
pale kwangu yalinivutia kwasababu ilikuwa na upepo
mwanana.
Nilimaliza kula vizuri nikakusanya vitu vyangu na
kurudisha kwenye begi ili nipate kuondoka pale
nirudi nyumbani. Kabla sijatoka pale nilikumbuka
kuwa nina camera ya digital. Hapo nilipata wazo la
kupiga picha eneo hilo ili nipate kumbukumbu na
ushahidi tosha. baada ya hapo niliamka kuondoka
lakini nikakumbuka kuwa sijachukua maji ya ziwa
hilo ili niwe na ushahidi zaidi wa kuwambia watu
waamini Kama nimefika au raha. Nilimwaga maji
yangu ya kunywa kisha nikasogea na kuteka maji ya
ziwa lile, kipindi nateka maji hayo begi langu
nilikuwa nimeliacha pembeni. Nilipo maliza kuteka
maji kugeuka nyuma sikuliona begi langu, nilibaki
nimezubaa Kwa muda huku nikijiuliza Nani
kalichukuwa begi langu na wakati nilikuwa peke
yangu. nikiwa bado najiuliza tena hofu nayo ikiwa
ishaniingia, ghafra Giza nene lilitanda maeneo hayo
ya ziwa ngozi, nilishikwa na uoga ghafra, uoga
wangu uliongezeka zaidi giza lile lilipozidi kuwa
nene, pale nikagundua ndio wakati wangu wa kufa,
niliisi kizunguzungu kwa muda wa sekunde kadhaa
kisha nikaanguka chini, toka hapo sikujua nini tena
kiliendelea.
Baadaye niliisi mtu ananiita kuniamsha kutoka
kwenye usingizi mzito, niliamka lakini nilijikuta
kwenye mji mmoja mdogo wenye nyumba tatu
kubwa Kweli kweli, halafu watu wakiwa wengiii, pia
eneo hilo likiwa limezungukwa na miti mingi
mikubwa na cha kushangaza watu wote walikuwa
awaniangalii wala awataki kusema na Mimi kila mtu
alikuwa Amenyamaza..........
.ITAENDELEA.
 
Sehemu................(02).
WhatsApp......... 0755577488.
ILIPO ISHIA.
Niliamshwa nikajikuta kwenye mji mdogo wenye
nyumba tatu kubwa kubwa halafu watu wengii, eneo
hilo lilikuwa limezungukwa na miti mingi mikubwa,
cha kushangaza watu wote walikuwa awaniangalii
wala walikiwa awataki kusema na Mimi. Kila mtu
alikuwa amenyamaza.
SONGA NAYO.
Nikiwa niko eneo hilo nilijiuliza
"Nimefika je hapa na kwanini na apa ni wapi? Hawa
watu awasemi na mimi wanafanya shughuri zao tu,
halafu nimesikia Kama mtu ananiamsha tena Kwa
kuniita jina langu ni nani huyo".
Baada ya kutafakari mambo hayo, nilisimama na
kumsogelea mtu mmoja ambaye umri ulikuwa
haupungui miaka sabini.
"Shikamoo mzee, naomba kujua mzee wangu hapa
ni wapi?"
Yule mzee aliendelea kukaa kimya tu, wala
hakusema chochote. Baada ya kushindwa kwa
mzee yule nilimfuata mtu mwingne, huyu alikuwa ni
mwanamke. Nilimuuliza swali lile lile baada ya
kumfikia, lakini naye hakusema chochote. Baada ya
kuona kuwa hakuna hata dalili za kusemeshwa na
kundi lile la watu, ambao walikuwa wamekaa kama
wanaongea wao lakini maneno hayasikiki, kwa
haraka utaweza kusema kuwa walikuwa hawasemi.
Lakini nilipowachunguza makini jikagundu kuwa
wanasema. Kwa mtazamo wao wa kukaa kimya
niliamua kupiga kelele kwa maneno haya
"HAPA NI WAPI, MBONA AMNAMBII NA NANI
KANILETA HUKU NIRUDISHENI NILIKOTOKA"
Baada ya kusema maneno hayo, ghafura kilitokea
kimbunga kikubwa na kunizoa, kimbunga hicho
kilinirusha mpaka juu kabisa, chini sikuweza
kupawaona tena na sikujua nini kiliendelea tena
kwangu.
Nilishituka usingizini baada ya kuiota ile ndoto ya
ajabu, nilikaa kitandani kama dakika ishirini
nikiitafakari sana ile ndoto ilimaanisha nini, kwanza
ziwa Ngozi nilikuwa naliogopa na sikuwahi
kulikaribia hata mala moja kwasababu historia yake
ilikuwa inatisha.
Nikiwa na mawazo nilisimama na kutoka chumbani
kwangu kwa ajiri ya kuelekea bafuni kuoga na
kupiga mswaki, Nikiwa bafuni nilishitushwa na
mabadiliko ya Ghafra ya bafu lile, lilibadilika na
kuwa bafu liingine kabisa, seheme ambao huwa
naweka mswaki wangu ulikuwepo mswaki wa mti!
Nilipoinua macho juu ya kilechumba cha bafu
niliona vitu vya kumetameta Kama nyota halafu
vikizunguka mule bafuni huku kama vinanisogolea.
Nilipiga kelele na kukimbia kurudi chumbani
kwangu, Nikiwa nakimbia kurudi chumbani nilisikia
sauti ya mwanamke akinisemesha.
"We kaka mbona unakimbia hivyo kunanini ambacho
unaogopa? "
Sauti ile ilinisitusha sana, nikageuka kuangalia ni
nani anayenisenesha. Kwakweli nilikutana na sura ya
Bint mrembo sijui kama niliwahi kumuona katika
Dunia hii.
"Tafadhali naomba unambie hapa ni wapi?"
Nilimuuliza swali hata kabla sijamjibu la kwake.
"Hapa sisi tunakaa tu lakini hatujui ni wapi, na
tulifikaje!"
"Amjui mlifikaje!?"
Nilimuuliza tena. kwakweli jawabu lake
lilinichanganya sana.
"Kweli kaka sisi hapa hatupajui, na wala hatukuwahi
kutoka tangu tufike na leo ni mwezi wa tatu!"
"Mh! Mwe....mwezi....wa..wa tatu?"
"Ndiyo"
Baada ya kuambiwa hivyo niliamua kurudi chumbani
kwangu. Sikutaka tena kuuliza maana nilishituka
sana, lakini nilipogeuka niliona kana kweli sipo
sehemu sitahiki yaani nyumbani. Pale kulikuwa
pengine kabisa. Hilo sikutaka kujaji bali niilingia
ndani ya Chumba changu ambacho nilitokea,
kwasababu nilikiacha kiko kama nilichokizoea.
Tauro langu lilikuwa kiunoni mwangu, kama
kawaida, lakini nilipoingia ndani mlango ulijifunga
wenyewe. Sikuamini macho yangu, nilikuta kitanda
kingine tena cha miti, godoro la pamba limeshonwa
kwa magunia, hata kiononi nilijikuta na gunia sio
tena tauro, begi langu la nguo alipo, kila kitu
kilibadilika kikawa kipya kwa muda wa dakika tano
ambazo nilitoka kwenda bafuni. Nikiwa bado
nashangaa nilisikia kelele za watu wakilia huku
wakinitaja jina langu.
"Juma! Juma!"
Bado kelele zikiwa zinaendelea niliisikia sauti ya
mama akiniita huku akilia.
"Jumanne mwanangu umeondoka bila kunambia
chochote, bila kuniaga. kwanini mwanangu
umenifanyia hivyo"
Kelele zile zilizidi kuwa nyingi masikioni mwangu,
tena zikaongezeka zikawa nyingi mpaka nikakosa
nguvu kabisa na kuanguka chini...........
 
Sehemu ya (3)
WhatsApp. 0755577488.
ILIPO ISHIA
"Juma! Juma!"
Bado kelele zikiwa zinaendelea niliisikia sauti ya
mama akiniita huku akilia.
"Jumanne mwanangu umeondoka bila kunambia
chochote, bila kuniaga. kwanini mwanangu
umenifanyia hivyo"
Kelele zile zilizidi kuwa nyingi masikioni mwangu,
tena zikaongezeka zikawa nyingi mpaka nikakosa
nguvu kabisa na kuanguka chini...........
ENDELEA.
Sikujua tena kilichoendelea ila niliamka nikakuta
wasichana wawili wamesimama Pembezoni mwa
kitanda changu, nilibaki kuwatazama huku
nikiwashangaa, kumbe hata wao pia walikuwa
wakinishangaa. Tuliendelea kutazamana bila
kusemeshana hivyo hivyo, mpaka ukapita muda
Kama wa dakika mbili ndiyo mmoja katika wale
wasichana wawili akaniuliza
"vip hali yako kaka?"
"Safi tu"
Niliitika kinyonge.
"Mh wewe unadanganya, hauko sawa, unaonekana
kabisa kama mgonjwa"
Binti Mwingine tena alisema.
"Mbona unasema siko sawa?"
Nami nilimuuliza tena Binti yule swali.
"Muonekano wako tu unaonesha, maana toka
umelala leo ni siku ya tatu ndio umepata kuamka"
"Siku ya tatu?!!"
Niliuliza kwa kushangaa.
"Ndiyo siku tatu umelala, kila tulipo kuwa tukijaribu
kukwamsha ulikuwa uoneshi hata dalili za kuamka"
Bint Mwingine tena alinisema.
Kwa Maelezo yao ilinibidi niamini kuwa ni kweli,
kwasababu nilikuwa na njaa ya hatari. Baada ya
kuligundua hilo sikutaka kuongea maneno mengi
zaidi niliomba Chakula, njaa niliokuwa nao ilikuwa
aisimuliki.
"Naombeni chakula maana Nina njaa kweli"
Nilisema.
Baada ya kusema hivyo Binti mmoja kati ya wale
wawili alitoka, hali ya chumba hicho ilikuwa vilevile
ya kushangaza. Hazikupita hata dakika mbili yule
Binti alirudi huku kabeba bakuri la chakula mkononi,
mkono mwingine alikuwa kabeba kibeseni kidogo
kilichokuwa na maji ya kunawa.
Chakula kile kilikuwa ni wali na nyama, sijui
walijuaje kuwa mimi napenda sana wali na na
Nyama, nilikipokea chakula na kuanza kukifakamia
haraka haraka mpaka wale wasichana
walinishangaa. Ilikuwa kidogo nile hata bila kunawa.
"Kaka usile Kwa pupa utapaliwa! kula taratibu"
Binti mmoja alisema baada ya kuishangaa sipidi
yangu ya kula.
Japo chakula kilikuwa wali nyama lakini kilikuwa
tofauti kabisa na jinsi nilivyo kizoea, ladha yake
ilikuwa nzuri ajabu, kwakweli sikuwahi kuisikia ladha
kama ya chakula kile, ladha hio iliniongezea hamasa
ya kukila chakula kile kwa pupa hatari. Nilimaliza
kula Chakula, nikaletewa maji nikanywa maji mengi.
Baada ya kula na kunywa hapo sasa nilijisikia ni
Mimi.
Baada ya kumaliza zoezi la kula nilitaka kujua
kwanini nilikuwa eneo lile, kwanini nilisikia makelele
ya watu wakinililia na kwanini vitu vilibadilika?
Baada ya kujiuliza niliwauliza moja kwa moja
mabinti wale.
Maswali yangu hayakujibiwa, zaidi walibaki
wakiniangalia tu basi. Kwakweli wale mabinti
walipendeza sana, walikuwa wanavutia, maumbo
yao utafikiri Jennifer Lopez, midomo yao mizuuri
kama Angelina Julie, sura zao za mvuto na za upole
kama Nadia Bukhari. Mavazi yao kwakweli yalikuwa
tofauti kabisa, yalikuwa yanavutia yaliyokuwa
yamewakamatilia vizuri mwilini na kuwachora
maumbo yao, halafu yalikuwa na mng'ao bila shaka
yalikuwa ya khariri na dhahabu. Kweli walikuwa
wakisitaajabisha sana, kila nilipozidi kuwatazama
ndio mvuto wao uliongezeka. Udenda wa
matamanio ulianza kunitoka, nilitamani niwambie tu
kweli kuwa nimewapenda ila niliogopa kwasababu
sikuwajua niwa aina gani.
Nilipozidi kuwangalia nao pia walizidi kunikazia
macho, ghafra mmoja akainama, kama vile
ananisogezea midomo yake, nami nilijikuta
natamani kufanya kama alivyotaka, kumbe hapana
hakuwa na lengo la kunipiga busu bali alinishika
mkono na kuninyanyua.
Walinizoa kwenye kile chumba na kunipeleka
sehemu nyingine kabisa ndani ya jumba hilo,
sehemu hiyo ulikuwa ni ukumbi mkubwa wa kukaa
ambao ulikuwa na viti vya aina ya sofa, zilikuwa ni
sofa za kipekee na ambazo kwa mazingira ya
kawaida kwakweli sikuwahi kuziona. Meza ya pale
ilikuwa ya aina yake, ilikuwa imetengenezwa kwa
dhahabu tupu, kila kitu cha pale ukumbini kilikuwa
cha thamani ya hali ya juu na kilikuwa
kimetengenezwa kwa Vito vya thamani tupu.
"Kaa kwenye kiti hapo"
Niliambiwa na mmoja wa mabinti wale.
Nami nilikaa, lakini wasiwasi ulianza kunitanda sana
moyoni mwangu uoga nao ukaniingia, wale mabinti
walikuwa wanajiamini sana, mavazi yao yale
yalinifanya niamini kuwa labda ni majini tena majini
wabaya ambao wanakula watu. Yote yakiwa
yanaendelea Mimi bado nilikuwa na tauro langu
kiunoni, tauro la Gunia ambalo lilikuwa limenikaa
vizuri hata namna ya kufunguka ilikuwa haiwezekani.
Mabinti wale wazuri walizidi kuniangalia kwa macho
ya kutamanisha kweli kweli huku wakiwa wamekaa
kwenye kochi jingine upande Mwingine.
"Wewe unaitwa nani?"
Wasichana wale waliniuliza kwa kujiamini kweli
kweli.
"Jumanne"
Nilisema kwa upore.
"Mh! Jumanne jina zuri kweli kweli. Lakini Jumanne
mbona unaonekana una wasiwasi hivyo,
unatuogopa?"
Bint mmoja aliuliza tena.
"Hapana"
"Kama ni hapana mbona unaonekana kuogopa
kabisa au unaisi baridi kwakuwa umevaa hivyo?"
"Hapana"
Nilijibu tena baada ya kuulizwa swali lingine, mule
ndani hata baridi halikuwemo kabisa, ila mazingira
Yale Mimi sikuyaelewa kabisa, ukiongezea na gunia
kiunoni ndio kabisa pozi lilizidi kunishia na nikazidi
kuisi nangoja kufa tu.
"Haya bhna, kama jibu lako ni moja tu, Mimi naitwa
RAULATI, na Mimi Naitwa JAMILA"
Mabinti wale walijitambulisha kwangu, majina yao
yalinipendeza lakini sikuwajibu chochote kwasababu
ya hofu niliyokuwa nayo.
"Umeuliza kuusu hapa ni wapi, ulifikaje na umekuja
kufanya nini. Ilo swali lako kwakweli hatujui namna
ya kukujibu, na labda tukwambie tu kuwa kama
alivyokwambia Raulati pale mwanzo hata sisi hatujui
tulifikaje hapa, hatujui hapa ni wapi? Na wala hatujui
tuliletwa kufanya nini? Cha kuzingatia ni kwamba
hata sisi tunaishi bila kuelewa tuko ulimwengu wa
aina gani Jumanne, wala usituogope sisi ni
Binadamu kama wewe, na tulifika hapa bila kujua
kama wewe, tena ujio wako hapa umetufanya na
sisi tuwe na nguvu na moyo zaidi kwakuwa
tumempata mwanaume wa kuishi naye kwahio
tutaishi kwa kujiamini"
Wasichana wale walizungumza hivyo, walikuwa
wanazungumza kwa kupokezana. Baada ya
kunambia hivyo kidogo sasa nilipata ujasiri wa
kuuliza.
"Kama ni hivyo mnaishije hapa? Chakula mnakitoa
wapi, na maji pamoja mavazi?"
Niliuliza hivyo maswali yangu yalikuwa yanalenga
muonekano wao, kwani walikuwa wamenawili vizuri
sana. Halafu Mimi waliniletea chakula
nilipowaomba, kwahio nilitaka kujua chakula
walikitoa wapi.
"Kuusu swala la Chakula, mavazi, manukato, na
vingine vya muhimu unavyovijua katika maisha ya
Mwanadamu, vipo tu hapa, labda tukwambie tu
kuwa sisi huu hapa ni mwezi wa tatu tuko hapa,
tuna kula hapa hapa na huwa hatupiki, Bali ni kula,
kujisaidia na kulala"
Mabint wale walisema. Maelezo yao bado yalikuwa
hayajanipa jibu halisia japo kuwa yalinitisha zaidi.
"Sasa hicho chakula kinaletwa na nani?"
"Unataka kujua chakula kinaletwaje? Subili uje uone
jinsi kinavyopatikana"
Bint aliyejitambulisha kwa Jina ka JAMILA alisema.
"Je vipi kuusu hivi Vito vya Thamani nimetoka
wapi?"
"Hivyo tulivikuta Jumanne, unavyoona vyote humu
tulivikuta kasoro mavazi tu, na chakula pamoja na
manukato na mafuta, hivyo huwa vinapatikana kwa
njia ambao utaona mwenyewe ukishazoea"
RAULATI alinijibu.
Majawabu yake yalikuwa yananichanganya sana,
Jinsi walivyokuwa wanaongea kwa kujiamini
niliamini wananidanganya hakuna ukweli ndani ya
Maelezo ambayo walikuwa wananipa.
Bado tukiwa pale JAMILA alitoka na kumwacha
RAULATI.
"Samahani hivi ninyi ni Mapacha?"
Nilijikuta namuuliza swali hilo RAULATI.
"Mbona umeuliza hivyo Jumanne?"
Binti yule naye alinirudishia jawabu kama swali.
"Kwasababu mnanichanganya ndiyo maana, yaani
kila nikizidi kuwataza ndiyo taswira ya kuonekana
kuwa ninyi ni Mapacha inanijia, mnafanana kweli
Kweli"
Nilisema.
"Ni kweli kabisa sisi ni Mapacha"
RAULATI alinijibu. Ni kweli kabisa jinsi walivyokuwa
wanatazamika wote walifanana kabisa. Nikiwa
nataka niulize swali lingine JAMILA alirejea tena,
mkononi alikuwa ameshikilia linguo lizito kama koti,
lilikuwa ni nguo zito lililokuwa na manyoya
manyoya, manguo hayo wanapenda kuyavaa
wakitaka kulala au wanapotoka kuoga, mala nyingi
wanayavaa ni watu wanaoishi sehemu za baridi
kama Urusi na Uingereza.
JAMILA alinikabizi vazi lile huku akinambia nilivae
nikaoge na kupiga mswaki.
"Kwani sasa hivi ndiyo kumekucha?"
Niliuliza, kwani nilistaajabu sana kuniambia nikapige
mswaki wakati niliamka muda mrefu na nilikaa nao.
"Muda ushaenda sana na sasa ni saa tatu na dakika
35 za asubuhi"
JAMILA alisema.
Baada ya kunambia hivyo bado tena walinishangaza,
walijuaje ni saa tatu na dakika 35 wakati wamo tu
ndani ya jumba hilo hakuna mwanga wa Jua zaidi ni
mwangaza wa kawaida tu.
"Mbona saa siioni mmejuaje kama sasa ni saa tatu
na Dakika 35?"
Niliuliza tena, sasa nilitamani kujua mengi kuusu
sehemu hiyo.
ITAENDELEA.
 
Sehemu ya (4),
Simu;...........0755577488.
"Kwani sasa hivi ndio kumekucha?"
Niliuliza, kwani nilistaajabu sana kuniambia nikapige
mswaki wakati niliamka muda mrefu na nilikaa nao.
"Muda ushaenda sana na sasa ni saa tatu na dakika
35 za asubuhi"
JAMILA alisema.
Baada ya kunambia hivyo bado tena walinishangaza,
walijuaje ni saa tatu na dakika 35 wakati wamo tu
ndani ya jumba hilo hakuna mwanga wa Jua zaidi ni
mwangaza wa kawaida tu.
"Mbona saa siioni mmejuaje kama sasa ni saa tatu
na Dakika 35?"
Niliuliza tena, sasa nilitamani kujua mengi kuusu
sehemu hiyo.
SONGA NAYO.
Unataka kujua tumejuaje, tazama kule uone nini
kinafanyika.
Niligeuka nami kutazama upande ambao
nilioneshwa, kweli nilikuta saa, pale pale kwenye
saa kulikuwa na kalenda, maana yake ni kwamba
ilikuwa imejigawa kalenda na saa.
Niliendelea kuikodolea ile saa ya aina yake, lakini
ghafra ilibadilika, jina langu likatokea kwenye ile
saa ya ajabu iliyokuwa imebandikwa ukutani.
"JUMANNE MWAKYOMA, UMEZALIWA MWAKA
1887, TAREHE 17 MWEZI WA 4. BADO
UMAESALIWA NA SIKU 7560 AMBAZO NI SAWA NA
MASAA 456700"
Nilishituka sana baada ya kuona vile kwa Hesabu ya
haraka haraka siku hizo ni sawa na Miaka kumi na
miwili inamaana hakukuwa tena na Nyongeza ya
siku.
"Sasa ndiyo inamaanisha nini?"
Nilijikuta nauliza, maana ilinishangaza sana.
"Jumanne usiwaze, mbona kufa kawaida tu, we
unaogopa kufa"
Jamila alisema.
"Hapana siogopi"
Nilisema.
"Wewe unamiaka 12 ya kuishi Ongera wengine
hawatazifikisha hata miaka hizo wanakufa wewe
unaogopa!"
Raulati alisema. maneno yake yalikuwa kama pilipili
ndani ya kichwa changu. Badala ya kunishauli sasa
yeye aliongea kama vile anataka kunila.
Niliogopa sana hata kuwa karibu na wale
wasichana. Yaani mpaka hapo nilijua nimekaa na
majini Bali sio wanadamu kama walivyojitambulisha
kwangu kuwa ni wanadamu wa kawaida kama
nilivyokuwa Mimi. Kilicho nitisha zaidi ni siku zangu
za kuishi zilizokuwa zimesalia, kwa kawaida mtu
unaweza kuona kama ni Miaka Mingi lakini unaweza
kufa hujafanya chochote, na kawaida Mwanadamu ni
Bora usiijue tarehe yako wala siku yako ya kufa,
utaishi kwa wasiwasi wakati wote, utaishi bila
kujiamini kabisa, Basi ndicho kilinikuta Mimi kabisa
ndani ya Jumba lile lililokuwa na ufahari lakini
nilikuwa sijui liko sehemu gani hapa Duniani.
Pozi la kuoga lilinishia kabisa, nikaendelea kukaa
huku nimeinamisha kichwa pale kwenye kiti
nilipokuwa nimekaa.
"Jumanne unaweza nini twende ukaoge?"
Sauti ya Jamila ilisikika ikinisemesha. Sikujali hata
alichosema mawazo yalikuwa mbali sana.
"Jumanne kwa kifupi hupaswi kabisa kuwaza kiasi
hicho, haya ni maisha ambayo yakupaswa uyazoee,
mbona sisi tushachukulia kawaida, kama ni kufa
kupo wala si jambo la kujiuliza na kuwaza kiasi
hicho utajiumiza tu"
Raulati alisema.
Kwakweli maneno ya mabint wale yalikuwa ya kutia
moyo kama ningekuwa katika mazingira ya kawaida
ambao nimeyazoea, lakini kwa mazingira Yale
walikuwa kama vile wanazidi kuniogopesha halafu
na kuwatilia shaka zaidi kuwa wao si binadamu Bali
ni majini wabaya.
"Jumanne unapajua mwanza?"
Niliulizwa na Jamila.
Swali hili lilinishitua sana, nikainua uso wangu,
kuwaangalia mabinti wale.
"Napajua; kwahio hapa tupo mwanza?"
Niliuliza kwa hamasa ili kama ni mwanza nitafute
namna ya kutoroka katika eneo hilo, uzuri mwanza
nilikuwa naijua vizuri tu.
"Ha ha ha ha haaa! Jumanne yani unawaza kuwa
upo Mwanza, wazo hilo ondoa kabisa sisi tumeisha
kwambia kuwa hapa sisi hatupajui......... labda
tuipe sisi Jina, kwamaana hiyo Is A place with no
name.......Sehemu isiyo na Jina.....
........Kweli ni sehemu isiyokuwa na Jina kabisa
Jamila umesema"
Mabint wale walisema walijisikia Furaha sana.
kiukweli. jinsi walivyokuwa wanazungumza kwa
Kejeli Mimi niliumia sana, nilitamani niwapige hata
makofi lakini namna na Ujanja nilikuwa sina.
Kwanza niliogopa, Pili nilikuwa naamini kuwa wale
mabinti watakuwa ni mashetani.
"Jumanne ngoja tukusimulie kisa cha maisha yetu
labda unaweza ukaishi kwa kujiamini na yakupaswa
uizoee sehemu hii kama sisi"
Jamila alisema.
Kwakweli nilikuwa kama sanamu au katuni mbele
yao, kwasababu ya vile walivyokuwa wanavionesha
mbele yangu, hata waliponiambia kuwa wanisimulie
kisa cha maisha yao sikutamani hata iwe hivyo,
naningeweza ningezuia lakini nilikuwa naogopa hata
kutamka maneno yenye ukari kwa mabinti wale,
kwahio ilinilazimu kuwasikiliza.
"Jumanne sisi tunakupenda sana, yani kipindi
umelala pale tulikuwa tunatamani uwamke,
tulijivunia kumpata mwanaume ndani ya jumba hili,
kwakweli kwa mazingira haya utalazimika uwe
mume wetu sisi sote wawili. Mwezi wa tatu tupo
sisi hapa hatukuwahi kuona mtu Mwingine hata
kipepeo wala kiumbe kingine labda cha kushukuru
ni kwamba sisi hali kama yako haikutukuta, Bali
tulijikuta humu, na mambo mengine yakaendelea.
Usihofu kuusu kufa hata sisi tutakufa na tulioneshwa
kama wewe"
Jamila alizungumza, alichokisema kwa mbaali
kilianza kuniingia na nikatamani aendelee
kuzungumza ingawa bado walikuwa hawajinishawish
i kuwa wao ni Binadamu. Nilipenda kila
alilozungumza lakini la kuusu Mimi kuwa mume
wao aaaaa! Bado nilikuwa sijashawishika kabisa.
"Sisi ni wenyeji wa Mwanza, na ndiko tulikozaliwa.
Wazazi wetu walifariki kwa ajali mbaya ya gari, ajali
ambayo ilitokea wakiwa wanatoka Hospitali ya
wilaya ya Nyamagana. Gari lao lilipata ajali baada
ya kugongwa na gari kubwa la mafuta na kuangukia
mtaroni mwa Barabara. Ajali hio ndiyo iliwaua
wazazi wetu, sisi pia tulikuwa kwenye gari hilo,
lakini hatukuweza kudhurika kwa chochote.
Sisi tumelelewa na Mjomba wetu mpaka kufikia
hapa tulipo"
Raulati alielezea historia yao. Bado Mimi nilitamani
wanambie walifika Je pale, labda wangenishawishi
nipate kuamini kuwa wao ni Binadamu.
"Tulifikaje hapa Jumanne. Kwanza kabisa siku moja
tumelala usiku tuliota ndoto moja wote wawili,
ndoto yetu ilifanana, na tuliiota ndoto hiyo siku ya
Alhamisi. Ndoto hiyo lilenga siku ya ijumaa.
Kawaida siku ya Ijumaa huwa ni siku ya michezo
kwa ratiba za mashule.
Ndoto ilionesha kuwa kulikuwa na mchezo wa mpila
wa miguu kwa wavulana baina ya shule yetu ya
mkuyuni na shule ya secondary ya Kapripont. Shule
hizi ni majirani sana na huwa zinaupinzani mkubwa
sana katika michezo, na hakuna Mwanafunzi
ambaye alikuwa anatamani kuikosa mechi hiyo ya
aina yake hata kwa kushangalia tu. Mapema saa
sita tuliondoka na kwenda msikitini kwenda kusali.
Saa saba na nusu tulitoka msikitini tukarudi shuleni
kwa ajili ya kuitazama mechi ya shule yetu na
wapinzani wetu wa shule Jirani. Saa nane na Nusu
ndiyo wachezaji waliingia uwanjani na mpila
ukaanza kuchezwa, tulikuwa na shamra shamra za
kushangalia kwa nguvu zote, pande zote mbili
zilikuwa na ushindani wa nguvu katika kushangilia.
Ndani ya Dakika tano toka mpila kuanza mala
kilitokea kimbunga kidogo tu katikati ya uwanja,
baada ya kimbunga hicho kutokea shangwe
ziliongezeka sana kwetu sisi washangiliaji. Lakini
ghafra kimbunga hicho kilibadiliaka ikawa ni
kimbunga kikubwa kweli kweli. Hapo tukapoteana
vumbi tu ndizo zilitawala eneo hilo, hatukuona tena
kuwa kuna madarasa karibu na uwanja ule, sisi
tulikimbilia upande ambao hatukujua ni wapi
tunaelekea mwisho kabisa tulijikuta tumo ndani ya
pango.
Ndoto ile ilitushitua wote usingizini na kuanza
kusimuliana ile ndoto sisi kwa sisi, nilichosimulia
Mimi ndicho jamila alinisimulia kwahio hakukuwa
na utofauti wa ndoto hiyo.
Tulibaki na maswali mengi sana, kwanini ndoto
tuliyoiota ilifanana? na ilikuwa na maana ipi kwetu?
tulijiuliza lakini hatukupata majibu zaidi ya kuamua
kujisaulisha kuwa ni ndoto kama ndoto za kawaida.
Tuliamua kujisaulisha kwasababu ya kuona kuwa ni
ndoto kama ndoto zingine za kawaida.
Wiki hiyo ilikatika na kwa bahati mbaya Wiki hiyo
shule yetu haikuwa na michezo ya haina yeyote
kwahio Ijumaa ya wiki hiyo ilipita free.
Siku ya Jumanne ya wiki mpya mapema kabisa
tulitangaziwa kuwa Ijumaa ya wiki hio kutakuwa na
mechi ya mpila wa miguu kwa wavulana, tena shule
ya ushindani tulitangaziwa kuwa ni majilani wetu wa
kapripoiti. Sisi hatukuamini kabisa kama ni kweli
maana hata kumbukumbu ya ndoto ilianza kujirudia
vichwani mwetu.
Tulianza kujadiliana sisi kwa sisi kuwa hatutaudhulia
katika mchezo huo, tena tulipanga hata siku hiyo ya
Ijumaa tusiende shule kwasababu tuliogopa
tuliamini kabisa kuwa ndoto ile huwenda ikatimia
kwasababu hatukuwahi kuota ndoto ya
kufanana..........
 
Sehemu ya (05),
WhatsApp 0755577488.
ILIPOISHIA.
Sisi hatukuamini kabisa kama ni kweli maana hata
kumbukumbu ya ndoto ilianza kujirudia vichwani
mwetu.
Tulianza kujadiliana sisi kwa sisi kuwa hatutaudhulia
katika mchezo huo, tena tulipanga hata siku hiyo ya
Ijumaa tusiende shule kwasababu tuliogopa
tuliamini kabisa kuwa ndoto ile huwenda ikatimia
kwasababu hatukuwahi kuota ndoto ya
kufanana..........
SONGA NAYO.
Basi tuliendelea kukaa mpaka siku hiyo ya Ijumaa,
lakini cha kushangaza tulipata hamasa ya kwenda
shule, na tulisoma vizuri kabisa. ulipofika wakati wa
kwenda msikitini hatukwenda kabisa, hatukwenda
msikitini, na hiyo ndiyo ilikuwa mala yetu ya kwanza
kutoenda msikitini siku ya Ijumaa. Kilichokuwa
vichwani mwetu tulikuwa tunawaza muda wa
michezo ufike twenda kushangilia, ndani ya muda
mfupi tulijikuta tunasahau kabisa ndoto ambayo
tuliiota wiki iliyopita siku ya alhamisi.
Hatimaye wakati wa michezo ulifika siku hiyo ya
ijumaa, wanafunzi wote tulikusanyika kwenye uwanja
wa michezo. Saa nane na nusu mpila ulianza
kuchezwa lakini mpila ulipoanza tu hivi mapigo yetu
ya moyo yakaenda mbio, wasiwasi ukazidi
kututawala, tukajishauri tuondoke, maana sasa
tunakoelekea ni kutukuta kilichotukuta kwenye
ndoto. Bado tukiwa tunaangalina na kushauliana
mala wanafunzi wa upande wetu walishangilia, kwa
maana hiyo timu yetu ya shule ilikuwa ishapata gori.
Aaaa! Nasi tukajiunga kushangalia tukasahau kabisa
kuwa lazima ile ndoto ilikuwa na maana yake, basi
tulipomaliza kushangalia tulitulia mpila ukaendelea
lakini dakika mbili tu, kilitokea kimbuka kama kile
kile cha kwenye ndoto, hapo sasa ndipo tulishikwa
Bumbuwazi.
"Tuondoke haraka lazima ni lazima"
Tulijikuta tunasema, lakini tulipogeuka nyuma
ulizuka tena upepo mkari kutokea nyuma yetu,
upepo huo ulichanganyikana na vumbi zito,
tukageuka tena upande wa uwanjani napo hatukuona
kitu vumbi ndilo lilikuwa limeisha tawala sehemu
yote. Hatukua na ujanja tulijisemea tu ngoja litimie
ambalo lilikuwa linakusudiwa kwenye ile ndoto.
Lakini sasa hali ile hatukuweza kuivumilia, tulianza
kukimbia hovyo huku tumeshikana mikono, harafu
sasa cha ajabu tulikuwa hatugongani na Mwanafunzi
yeyote, ilikuwa kama tupo njiani peke yetu.
Tulikimbilia tusikokujua ghafra tuliona pango Dogo
kwenye lile vumbi tukatamani kuingia humo kungoja
upepo utulie ndiyo tuchukue hatua nyingine.
Tukiwa mule ndani ya pango hilo dogo tulisikia
kelele nyingi azieleweki watu si watu mbwa si
mbwa tena Kama vile zinatufuata. Tuliamua kutoka
tukimbie lakini atukuweza. Badala yake lile pango
lilikua kubwa, pana halafu ndani ikawa Kama kuna
vitu vya kung'aa.
Tuliogopa sana ila atukujua tutokee wapi. Tukiwa
wenye hofu, ghafra walitokea watu wawili wazee;
Mwanamke na mwanamume wakatwambia
"Karibuni katika makao yenu mapya".
"Makao yetu mapya!? Tuliuliza Kwa mshangao sana,
swali letu halikujibiwa. Badala yake wale wazee
walipotea.
Baada ya wazee wale kupotea hatukujua ni nini
kiliendelea Bali nasi tulijikuta humu humu ndani ya
Jumba la A place with no name. Hatukuwahi kutoka
inje ya jumba hili na tunaishi kama kawaida, kama
ndiyo Dunia nyingine basi tushafika inatubidi
kukubali. kwanza toka tufike hapa hatukuwahi
kuuona mlango wa kutokea inje ya Jumba hili, lakini
Tunashukuru kwakuwa kila kitu tunapata"
Raulati alizungumza hivyo. Kisa chao kweli hata
Mimi kilinishangaza sana, lakini sikukiamini kabisa.
Nilijiuliza kirahisi tu hivyo, haiwezekani kimbunga
kivume harafu kiwapoteze watu kwa njia kama ya
kwao, japo kuwa kweli walianza kwa kuota ndoto
kama Mimi nilivoota ndoto, lakini ndoto yangu
ilikuwa kama ukweli kwasababu sikupewa nafasi ya
kuitafakari nikiwa nyumbani, Bali nilijikuta nimo
ndani ya Jengo lile la ajabu.
"Jumanne bado utuamini sisi?"
Jamila aliniuliza.
"Nawamini"
Niliwajibu kwa upole.
"Basi amka ukaoge na kupiga mswaki kama
uogopi"
Jamila alinambia tena, nilikuwa nashindwa hata
kusimama, lakini nilishangaa tu Raulati anasimama
na kunishika mkono huku akiniangalia usoni. Macho
yangu na yake yalikuwa yamepishana kama futi
moja tu, hakika yule Binti alikuwa Mzuri kabisa
alikuwa mzuri. Macho yangu yenyewe yalijikuta
yanamuogopa hata kumwangalia kwa Aibu.
"Twende ukaoge, siku tatu ujaoga tangu ufike hapa"
Raulati alisema.
Sikuwa na ujanja baada ya kushikwa na Binti yule
nilijikuta nasimama mwenyewe kisha wakaniongoza
njia ya kuelekea bafu lilipo.
Walinionesha halafu Mimi nikaingia bafuni kuoga,
kiunoni bado nilikuwa na tauro langu. Bafuni nilipo
ingia nilikuta bafu ni lingine kabisa tofauti na la
mwanzo. Palikuwa ni pasafi tu wala hakukuwa na
vitu kama nilivyovikuta mwanzo. Bafuni kulikuwa na
kila kitu kizuri unachokijua katika vyumba hivyo,
muonekano wake ulikuwa wa Kibillionare, kwakweli
mazingira ya mule yalipendeza sana, chumba kile
kilikuwa ni kikubwa tu na kilikuwa kimejitosheleza
kila kitu, kama ni maisha yalikuwa ni maisha
yanayoitajika kabisa, Bafu lile nashindwa hata
kulielezea labda kwasababu mazingira yangu
niliyokuwa nimeyazoea hayakukaribia kabisa.
Nilioga nikamaliza nikajifuta vizuri na taulo lingine
kabisa ambalo lilikuwa ndani ya Bafu lile
nimendaliwa, baada ya kumaliza nililivaa koti
ambalo Jamila alinipa kwa ajili ya kulivaa baada ya
kuoga. Taulo la gunia niliacha huko huko.
Nilitokea bafuni mule nikawakuta mabinti wale wote
wamesimama huku wakiniangalia kwa matamanio
kweli, Tabasamu ndilo lilikuwa limetawala ndani ya
nyuso zao.
"Tunakupenda Jumanne wetu"
Sauti nzuri ya mahaba iliwatoka mabinti wale. Kwa
Jinsi nilivyokuwa na mashaka Juu yao sikutaka
kabisa kuwajibu ila niliwaoneshea Tabasamu tu
basi.
"Chumba chako unakikumbuka?"
Jamila aliniuliza.
"Hapana"
"Kile pale nenda kila kitu kipo safi"
Nilioneshwa baada ya kukataa kuwa sikikumbuki.
Nilisogea kwenye Chumba nilichooneshwa,
nikaushika mlango na kuufungua, nilisitaajabu sana
baada ya kukuta chumba si kile cha hawali na
kilipendeza sana kile Chumba hakiamungu
nilipendezwa sana na maadhari ya Chumba kile,
nilijikuta natamani kuingia haraka. Lakini Kabla
sijaingia ndani niligeuka Nyuma na kuangalia kama
Raulati na Jamila wananiangalia, lakini sikuwaona
pale walipokuwa wamesimama, kidogo wasiwasi
ulianza kuniingia tena. Basi niliingia ndani ya
Chumba hicho, nilipoingia kabisa ndani nilikuta nguo
safi zimekunjwa vizuri ziko juu ya kitanda,
nilizichukua na kuzivaa. zilikuwa ni nguo za kawaida
tu lakini zilinipendeza sana.
Baada ya kumaliza kuvaa nguo zile nilishitukia
mlango unagongwa, Sauti ilikuwa ya wale Mabinti
ikiliita jina langu.
"Hawa wamejuaje kama nimeisha maliza kuvaa"
Nilijisemea mwenyewe, maana wale mabint Mimi
nilikuwa siwaamini kabisa, nilijua wale ni majini tu,
kwa mazingira yale kwakweli Mimi walinitisha sana,
Fikra zangu zoote ziliamini kuwa lazima watakuwa
ni majini tu, lazima. Kwasababu hata mazingira Yale
sikuyaona kama ni ya kawaida, halafu kipindi hicho
nilikuwa nishasoma hadithi nyingi kuusu maisha ya
majini kutoka kwa watunzi tofauti kama akina
Mavugo, Rais wa Iramba zilizokuwa zinahusu majini
majini, hadithi zote zilionesha kuwa maisha ya
majini huwa yapo vizuri na ya kifahari, uthamani wa
Vitu vyao huwa mala nyingi vya dhahabu tu. Kingine
kilichonitisha ni ndoto nilio iota, kwani ndoto ile
nilikuwa kwenye ziwa Ngozi, ziwa ambalo historia
yake huwa inaogopesha, kwahio moja kwa moja
mabinti wale Mimi sikuwaamini kabisa lazima
walikuwa ni majini. Hilo tu ndilo lilikuwa wazo langu
kuu Juu yao, hata kisa chao walichonisimulia
niliamini si cha kweli Bali cha kutunga tu kama
hadithi zingine ambazo nilikuwa nishazisoma.
Nilitoka Chumbani mule kwa unyonge sana.
"Jumanne mbona ujiamini wewe.........Ebu jiamini
basi utaishi je kwa mashaka muda wote huu,
mbona sisi tushazoea wala hatuwazi kiasi hicho"
Mabinti wale walisema. Kweli walijitahidi sana kwa
nguvu zao kunishawishi lakini kwangu walikuwa
hawana mafanikio kabisa.
Nilitoka nao tukarudi sehemu ya kukaa tukaendelea
kuongea mambo mengine. Nilijaribu hata
kuwadadisi walizaliwa mwaka gani wakanambia
kuwa wao walizaliwa mwaka 1990 inamaana kwa
muda huo walikuwa na umri wa miaka kumi na
saba tu, walikuwa ni mabinti wabichi hasa.
Tukiwa tushaongea mengi mwisho nilianza kuhisi
njaa, nilipoiangalia saa nilikuta ni kama saa nane na
nusu, basi nikajikuta nasema kuwa"Nahisi njaa"
Ndivyo nilivyosema tu hivyo wale Mabinti wote
walisimama na kunifuata kisha wakanisogelea na
kunishika kwa pamoja.
"Jumanne mpenzi wetu twende tukale"
"Mh!"
Niliguna tu, nilishindwa hata kuuliza maana sikujua
chakula hicho kiliandaliwa muda gani. Nami
nilinyanyuka nilipokuwa nimekaa nikaongozana nao.
Jumba lile lilikuwa limekamilia na Dyaning
ilikuwepo, huwezi amini nilipofika Dyning sikuamini
kabisa sijui walikuwa wanatembea na mawazo
yangu, nilikuta mezani kuna ugari na hotpot ya
nyama ya kuku tena alikuwa kuku mzima kabisaa
aliyekuwa kakatwakatwa vipandevipande kama
tulivyozoea, kabisa sikumbuki kama kulikuwa na
kipande kilichokuwa kimesalia katika yule mnyama
tena alikuwa Jogoo ambaye kwa kipimo alikuwa na
kilo zaidi ya tano.
"Jumanne utapasuka ukicheza na maisha ya huku,
yani huku ni television tu ndiyo hatuna, lakini vingine
vyote Burudani sana"
Wale mabinti walisema.
"Kwa maana hiyo hata Disko lipo?"
Nilijikuta nauliza swali hilo.
"Subili kama unalitaka wewe mwenyewe utafurahi tu,
lakini mpaka ukubali kuwa mpenzi wetu, ndiyo
vingine ivijue"
Nilijibiwa hivyo, Nilijikuta nacheka kwanza kwenye
ile meza ya chakula.
Tulizungumza vingi sana pindi tunakula, nao
walipata fursa ya kuniuliza jinsi nilivyifika pale, ni
nini kilinikuta Mpaka kufika pale? Bila kusita
niliwasimulia. Mchana wa siku hiyo uliisha kwa
kuongea tu na mabinti wale.
Baada ya stori zote za mchana hatimaye usiku
uliingia tukala tena chakula cha nguvu, wakati huu
tulikula wali na maharage pamoja na mboga za
majani. Baada ya zoezi la kula usiku kuisha,
niliagana na Mabinti wale nikaelekea chumbani
kwangu, nao pia wakaelekea Chumbani kwao.
Chumba cha mabinti wale sikujua kilikuwa upende
upi katika Jumba lile ambalo nilikuwa siijui hata
ramani yake.
Baada ya kuingia Chumbani nilikaa tu kitandani
huku nikuwaza. Nilijiuliza maswali mengi sana, vipi
nilifika pale, nilifanya kosa gani mpaka kufika pale?
Jumba hilo liko wapi Duniani hapa?"
Madirisha ya Jumba lile yalikuwa juu kabisa, yani
huwezo wa kulifikia ili kuchungulia inje ilikuwa si
rahisi kuyafikia na kuchungulia. Japokuwa ilikuwa ni
siku ya nne ndani ya Jumba lile, lakini niliona Kama
ndio siku ya kwanza kwangu, kwani siku tatu
nilizitumia kwenye usingizi mzito wa bila
kujitambua. niliwaza mengi sana, hata mabinti wale
nao nilianza kuwajaji mwenyewe, Yaani Jamila na
Raulati ambao walikuwa na mvuto wa ajabu, katika
kutafakari sana kuusu mabinti hawo, kidogo
niilijikuta nikifarijika moyoni. Nilijiona Kama vile
kwenye Jumba lile panaweza kuwa pahara sahihi
kabisa kwani nitaishi dunia ya peke yangu iliyojaa
furaha ya mapenzi kutoka Kwa mapacha wawili
wenye mvuto wa pekee. Mvuto wa wale watoto
wakike kwakweli sikuwahi kuona mwanamke wa
kuwafananisha nao toka kuzaliwa kwangu. Baada ya
kutafakari mambo mengi, sikujua usingizi ulinipitia
vipi ila nilishituka baada ya kusikia nagongewa
mlango. Tena mgongaji alikuwa akigonga kwa
nguvu sana.
"Nani anayegonga hivyo mlango wakati Mimi
nimelala"
Nilisema Kwa sauti ya uchovu.
"AMKA HARAKA HATUNA MUDA WA KUPOTEZA."
Ilisikiska sauti nzito ya mwanaume ikisema, sauti
hiyo ilitokea mlangoni, kwamaan hiyo kulikuwa na
Mwanaume ndiye kasimama mlangoni. Sauti hiyo
ilinifanya niogope na kujawa na wasiwasi mwingi.
"FANYA HARAKA TUONDOKE"
Bado nikiwa hata sijafikilia cha kufanya sauti ile
ilisikika tena ikisema. .........................
 
Sehemu no (6)
WhatsApp.. 0755577488
ILIPOISHIA.
"AMKA HARAKA HATUNA MUDA WA KUPOTEZA."
Ilisikika sauti nzito ya mwanaume ikisema, sauti
hiyo ilitokea mlangoni, kwamaana hiyo kulikuwa na
Mwanaume ndiye kasimama mlangoni. Sauti hiyo
ilinifanya niogope na kujawa na wasiwasi mwingi.
"FANYA HARAKA TUONDOKE"
Bado nikiwa hata sijafikilia cha kufanya sauti ile
ilisikika tena ikisema. .........................
SONGA NAYO.
Sauti ile ilizidi kusikika mala nyingi tena ikijirudia
rudia. AMKA! AMKA! AMKA! HARAKA! HARAKA!
HARAKA! AMKA HARAKA WEWE. FANYA FANYA
HARAKA! MUDA UMETUACHA. Niliogopa tena
nilizidi kuogopa. Sikuweza kuusogelea tena mlango
badala yake nilitafuta mahara pa kujificha. Zilipita
kama dakika tano pakawa kimya ile sauti sikuisikia
tena. Nilirudi kitandani kwangu nikakaa huku Nikiwa
na hofu kubwa na mawazo mengi nisijue nini cha
kufanya. Haikupita muda mrefu
Tangu tukio la sauti za kutisha zisisike, mala
nilisikia sauti ya Raulati akiniita.
"Wewe Jumanne wewe amka bhna uje tunywe chai
unalala mpaka tunasahu kama tuna mtu Mgeni
humu ndani"
Sauti ya Raulati ilinisemesha.
"Tunywe chai!"
Nilijisemea kimoyo moyo.
"Haya nakuja"
Nilisema kwa nguvu.
"Haya jitahidi kuwahi sasa, kwani sisi hatuwezi kula
bila uwepo wako"
Sauti ya Jamila nayo ilisikika, Sauti zao zilikaribiana
sana kufanana. Japo kuwa walikuwa wanafanana,
lakini kwenye sauti kidogo zilitofautiana.
"Amna lazima hawa wasichana ndio wananichezea
mchezo huu, hawa hawa ndio wananiletea vitisho
hivi vya ajabu, haiwezekani nimesikia makelele ya
kutisha muda si mrefu na sizani kama Nusu saa
limepita halafu wao ndiyo wanajitokeza, Hakika
hawa ni majini"
Nilijisemea ndani ya Chumba kile, na si kwamba
nilikuwa nasema kwa sauti ya chini, hapana nilikuwa
nasema kwa Sauti ya juu sana, sikujali niko wapi,
nilijikuta naupata ujasiri wa kuzungumza hivyo kwa
nguvu. Baada ya kusema hivyo niliusogelea mlango
na kuufungua.
Nilipoufungua mlango nilikutana na nyuso za wale
mabinti wote wawili wakiniangalia kwa unyonge
sana, hii alimaanisha kwamba nilicho kizungumza
muda mfupi walikisikia.
"Sawa Jumanne, lakini sisi tunajijua ni akina nani,
ila tunaomba utusamehe kama tunakuuzi, na tangu
sasa hakika hutosikia tukikusemesha tena"
Raulati alisema, mpaka hapo wote wawili walikuwa
wanatokwa na machozi.
Baada ya kusema hivyo waligeuka na kurudi zao.
Hata Mimi roho iliniuma kabisa, Mabint wazuri wale
kuwauzi nilijisikia vibaya kabisa japo kuwa nilikuwa
nikiwahofia.
"Ebu ngoja nione itakavyo kuwa"
Nilisema hivyo. Nilijiona kidogo Jasiri. Lengo
lilikuwa ni kuhakiki kuwa kweli mabinti wale ni
Binadamu kweli kama nilivyokuwa mimi. Niliondoka
chumbani kwangu na kuelekea sitting room kukaa
hata kabla sijaupiga mswaki, wala kuoga asubuhi.
Nilipofika hapo cha kwanza nilitupia macho kwenye
saa nikakuta ni saa tatu kasoro dakika kumi na
moja.
"Kha! Kumbe muda ushaenda kiasi hiki" nilijisemea
mwenyewe kimoyo moyo. Niliendelea kukaa pale
peke yangu, Hakuwa Jamila wala Mwenzake Raulati
alijitokeza. Nilikaa pale toka hiyo saa tatu mpaka
saa tano peke yangu, muda huo nilikuwa sijanywa
chai, wala kuoga, wala kupiga mswaki.
Baada ya kuona hakuna mabadiliko nilijiongoza
mwenyewe tu nikaenda kupiga mswaki, sikuoga
hata, nipipomaliza nilirudi chumbani kwangu, nikaa
tena, nilikuwa nahisi njaa lakini namna ya kuongea
na Mabinti wale nilikuwa sina nilikaa na njaa yangu
mpaka mida ya saa saba ndani ya Chumba changu,
nilitoka chumbani mule na kurudi sebuleni, kipindi
nafika pale sebuleni tu, Raulati na Jamila walikuwa
wanatoka Dyning kula. Nilisimama na kuangalia
vizuri nao pia wakasimama kuniangalia, macho yetu
yakakutana. Tuliangaliana sana pale sebuleni
mwisho nikatamani kuwambia wanisaidie chakula.
Lakini nilishindwa kabisa kusema baada ya kuwaona
mabinti wale machozi yakiwatoka, hapo nikatamani
niwapigie magoti niwaombe msamaha kwa
nilichowafanyia nikawa kama nimewachelewa
kwasababu wakati huo huo walishikana mikono na
kuelekea chumbani kwao. Chumba chao nilikuwa
sijui ni wapi kilipo ndani ya Jumba lile. Walipokuwa
wanatembea Mimi niligeuka kuwaangalia, nikajikuta
napata ujasiri wa kuwafuata kwa nyuma ilimradi tu
nipate kujua chumba chao kiko upande upi ndani ya
Jumba lile la ajabu. Kweli nilifanikia kuwakuta
wanaingia ndani ya Chumba chao na kuufunga
mlango. Baada ya kuona hivyo nilitamani nijue ni
Binadamu ukweli au ni majini tena ambayo yalikuwa
yakinipigia kelele malangoni kwangu. Nilisogea
karibu kabisa na mlango wao, na uzuri mlango
ulikuwa na kufuri lenye tudu, nililiweka jicho langu
kwenye tundu la kupitishia funguo katika mlango,
nikachungulia ndani.
"Kwanini tusimuhurumie tu!"
Niliisikia sauti ya Jamila inasema na mwenzake.
"Kwanini Jamila?"
Raulati aliuliza.
"Kwasababu kipindi tunakuja huku chumbani kwetu
yeye alikuwa akitufuata nyuma, huwenda anatamani
kutuomba msamaha lakini anashindwa"
Jamila alisema tena.
"Kumbe kaniona kipindi nawafuata"
Nilijisemea kimoyo moyo.
"Ni kweli Jamila lakini tumwache kwanza kwa siku
ya leo Ajifunze
Hata Mimi najua ni ngumu sana yeye kutuamini sisi
kama ni Binadamu wa kawaida kwasababu
ametukuta eneo hili ambalo hatulijui hata hata sisi
lakini yeye haelewi. Naomba tumwache kwanza
halafu tuone hatafanya nini"
Raulati alisema. Kauli yake Jamila aliipokea kwa
uzuri kabisa kisha wakapiga makofi ya
kupongezana, niliwaona wakaanza na kutabasamu
kwa Furaha. Ujasiri wa kujiona kichwa ulishindwa
baada ya kugundua kuwa kweli mabinti wale
walikuwa ni Binadamu kama Mimi wala si Majini
kama nilivyokuwa nafikiria.
"Jamila na Raulati!"
Nilijikuta nasema kwa nguvu huku nikiuwachia
mlango na kuanza kupiga hatua kurudi sebuleni.
"Jumanne!"
Nilisikia sauti ikiniita. Niligeuka nyuma kwa haraka
sana, nilimkuta Jamila kasimama mlangoni mwa
chumba chao ananiangalia kwa Uzuni.
"Unatupenda sisi Jumanne?"
Mala Raulati naye alifika na kunisemesha.
Sikuwajibu chochote kwanza kabla ya kupiga magoti
mbele yao kwa ajili ya msamaha.
"Naombeni mnisamehe"
Nilijikuta nasema hivyo baada ya kupiga magoti.
"Jumanne hauna sababu ya kutuomba msamaha,
kwakuwa ulikuwa ukihisia, hata sisi tunajua kabisa
ni sababu ya kufika katika eneo usilolijua"
Raulati alisema tena, muda huo huo Jamila
alinisogelea na kunishika kisha akaninyanyua.
"Pole Jumanne kwa kuteseka muda wote huo"
Alinambia Binti yule.
"Jumanne usijali, tunajua toka asubuhi ujala
chochote, una njaa basi twende ukale"
Raulati alisema wakanishika mikono yangu kila
mmoja mkono wake Tukarudi sebuleni, hatukukaa
tulipitiliza Mpaka Dyningi. Mezani hatukukuta kitu,
tulikuta meza nyeupe tupu.
"Jumanne Furahi kwanza halafu ndiyo tukwambie
ufanye nini"
Jamila alisema.
Nilijikuta natabasamu Mimi mwenyewe, hali ya
kuona aibu Kwa mabinti wale kwa kile ambacho
nilikuwa nishawakosea sikuwa nayo tena.
"Haya sema unataka chakula Gani?"
Raulati aliniuliza.
"Ninyi si mnatoka mwanza?"
Nami pia niliwauliza.
"Ndiyo"
Waliitikia wote,
"Sasa natamani Ugari na Samaki mzuuri ambaye
ninyi mnamjua ndani ya Ziwa Victoria, tena awe
hajaungwa mafuta wala nyanya awe amepikwa
chukuchuku wa chumvi na limao halafu mchuzi wa
kutosha"
Kipindi nasema hivyo mawazo yangu yote yalikuwa
kwenye sato, samaki ambaye niliwahi kumla mala
moja katika maisha yangu yote mpaka kufikia umri
wangu niliokuwa nao.
"Bila shaka unamuwaza Sato wewe"
Jamila alisema.
"Ndiyo mwenyewe, Jumanne anamuwaza Sato"
Raulati naye aliongezea.
Baada ya Raulati kusemau nisikufiche,
Kwakweli ilikuwa nikimbie pale mezani wale mabinti
wakanizuia kwani walikuwa wameniweka katikati
yao.
 
SEHEMU (07).
Usinianguashe Share tafadhali nakuomba.
ILIPOISHIA,
"Bila shaka unamuwaza Sato wewe"
Jamila alisema.
"Ndiyo mwenyewe, Jumanne anamuwaza Sato"
Raulati naye aliongezea.
Baada ya Raulati kusema hivyo, nisikufiche,
Kwakweli ilikuwa nikimbie pale mezani wale mabinti
wakanizuia kwani walikuwa wameniweka katikati
yao.
ILIPOISHIA,
Pale mezani yaliporomoka mahotipoti mawili sijui
hata yalitokea wapi? Wale mabint wao hawa
kushituka kabisa.
"Jumanne haya ndiyo maisha ya huku, Kwahiyo
yazoee tu basi, maji ya kunawa kama kawada
unajua tunako nawa, maji ya Kunywa hayo hapo
kwenye kabati"
Jamila alisema.
Ni kweli mule ndani ya Dyning kulikuwa na kabati
kubwa la vyombo vyote, maji kulikuwa na masiki ya
kunawia ndani ya Chumba hicho. Kwa ujasiri kabisa
Jamila aliushika mfuniko wa Hotpot na kuutoa,
hotpot lile ndilo lilikuwa na mboga, weee! Kama
nilivyokuwa nawaza vipande kama vitano vya
Samaki tena Sato mkubwa kanona mchuzi ukiwa
ndani yake wa kutosha, kwa macho tu ulikuwa ni
mchuzi mzito hatari tena ambao ulikuwa hujaungwa
mafuta wala nyanya.
Amka unawe Ule Jumanne"
Raulati alisema.
"Na nyinyi"
"Sisi tushakula tayari wewe tu ndio ujala"
Jamila alinijibu.
Nilichoka hata pozi la kula peke yangu lilinikosa
njaa ilikatika pale pale kabisa. Chakula kilikuwa ni
Chenyewe lakini sikujua kiliko toka, kingine wale
mabinti walikataa kula pamoja nami, sasa
walimaanisha nini kukataa. Hicho nacho kilizidisha
wasiwasi tena kwangu, mala nikaanza kuwaza tena
lazima kuna mchezo wa kichawi ndiyo unachezwa.
Haiwezekani ndani ya dakika mbili useme halafu
unachokihitaji kitokee. Afadhali kingekuwa kitu
kingine lakini chakula! Aaa! kilipikwa saa ngapi?
Yote ilikuwa ni migogoro ndani ya moyo wangu.
"Jumanne usiwaze haya mbona ni maisha unapaswa
uyazoee, usiogope kabisa, mbona kila siku ndivyo
unavila"
Raulati alisema.
Maneno yake kwangu hayakuwa na msaada, nilikaa
nikakiangalia chakula kwa dakika tatu kabisa lakini
sikuthubu kusimama kwenda kunawa.
"Unataka nini Jumanne kama ndio hivyo?"
Raulati aliniuliza.
Si kumjibu. Niliendelea kunyamaza.
Baada ya kuona kuwa Mimi nimenyamaza Jamila
alisimama na kulifungua kabati kisha akatoka na
Chombo kama kibeseni kidogo, akasogea kwenye
bomba akateka maji kisha akarudi nayo mezani.
Walinishika mikono yangu na kuninawisha kisha na
wao wakanawa na kuanza kula kama tonge mbili
mbili, huku wakimla na samaki.
Jumanne haya tumekutangulizia kama uwamini, kula
sasa hivi huwezi kuwa chochote"
Jamila alisema.
"Nimeshiba"
Nilijibu.
"Jumanne unachekesha sana, utakufa wewe, chakula
ndicho hichi hichi unakila kila siku, usiku na mchana
toka ufike hapa bado unaogopa! Kipi unataka
tukusaidie, dah! Wewe Ni mwanaume lakini umezidi
Jumanne, afadhali hata sisi tulikuwa Jasiri
kidogo............ Mbali na Hilo Jamila hii ni sehemu
ambayo hatuijui, hatujui tulikuja kufanya nini,
hatuelewi nani alituleta hapa, hasa kwa lengo lipi?
Sasa kipi tunaogopa kama anampango wa kutuua
au ni majini wanashida ya kutula nyama basi na
iwe. Kama ni kufa tutakufa tu, kama tupo huku kwa
kazi maalumu napo pia itajulikana tu, unaogopa
kufa Leo kwenye chakula wakati sehemu uijui, hata
chumbani kwako unaweza kuuliwa au hata
kubadilishwa na kuwa jitu tu. Cha ajabu na cha
kushangaza unakula vyakula unavyotaka, bado
unaogopa. Haya Subili kufa!"
Jamila alisema kisha Raulati naye akongezea. Kama
ni akili mabinti wale walikuwa na Akili za kutosha
maneno yao yalinipa ujasiri wa kuanza kukila
chakula kile. Ni kweli kabisa walichokiongea pale
sikufika kwa kutaka nilishitukia nipo, mpaka hapo
nilikuwa nishajiuliza mwenyewe pale nilifika kufanya
nini? Aliyenipereka anamakusudio yapi? Kumbe
kukiogopa chakula ilikuwa haina maana kuwa kama
kuna kifo basi siwezi kukuepuka lazima nife tu,
Nilikula hata wale mabint wakanipongeza, na wao
sasa kila mmoja akatamani kunilisha. Samaki yule
alikuwa mzuri, vipande vitano vya kunona halafu
supu yenyewe ya nguvu, ugari wenyewe ulikuwa
unaojitosheleza, nilikula Ugali nikauwacha nguvu
iliishia kwenye samaki, nilikuwa vipande vitatu vya
samaki yule halafu Jamila na Raulati wakala kimoja
kimoja. Kabla hatujanawa baada ya kumaliza kula
ugali na samaki, sikuamini mala matunda ndizi na
Tikitiki maji vilitua kwenye meza, niliwaangalia wale
mabinti usoni kwa mshangao, wao walikuwa
wanatabasamu tu.
"Shushia matunda Jumanne, usiogope hii ndiyo
sehemu yetu huwenda tutaishi huku milele ni bahati
sana. Kuishi maisha ya pekee kama haya"
Jamila alisema.
"Kabisa, huu ni ulimwengu wa pekee, ulimwengu wa
kujivunia, hata kama ni nyama tunaandaliwa ili waje
watule tumenona ni poa tu ngoja nasi tuvifaidi vya
kwao"
Raulati aliongezea, maneno ya Raulati Mimi kidogo
yalikuwa yananitisha, maana sasa kama yalikuwa
yanaendana na uwalisia. Kuwa huwenda kula kule
lengo ni kunona halafu niliwe nikiwa na nyama za
kutosha na mafuta mengi. Nilikuwa nakula matunda
Yale kifuani nikiwa nishaanzisha mgogoro Mwingine
ambao tena uliwahusu mabinti wale, Pengine
nilikuwa nahisi kuwa huwenda ni majini ukweli
labda ndio maana Raulati anasema vile kwasababu
wananiandaa; katika swala hili nilijiuliza kwanini
wale wasichana wawe pale kama sio majini.
Kingine ilikuwa najipa matumaini kuwa huwenda
kweli nao ni Binadamu, kama walivyosema kuwa
hatuna haja ya kuogopa kwasababu hatujui ukweli
tuliperekwa pale kwa lengo lipi?
Hiyo miwili ndiyo ilikuwa migogoro mikubwa
kwangu, niliendelea kula matunda na mabinti wale
lakini kwa taadhali kubwa sana, hio ni kwasababu
walianza tena kunijaza wasiwasi kwa maneno yao
wenyewe. Wasiwasi wangu sikutaka kuwaoneshea
ili wasije kuwa na mashaka juu yangu. Kama ni
kucheka nilicheka sana kwenye meza ile ya Chakula.
Tulipo maliza kula Mimi nilitaka nijue vyombo huwa
vinatoka vipi pale mezani; hivyo ni kwasababu
vipindi vingine vya chakula tulikuwa tukimaliza kula
tunaondoka tunaviacha pale, sasa siku hiyo nilitaka
nijue vyombo huwa vinatolewa na nani, meza nayo
inasafanyiwa je?.
"Hicho tu ndicho unataka kujua jumanne?"
Jamila aliniuliza baada ya kuwaeleza kuwa nataka
kuona vyombo vinavyotokaje kwenye meza.
"Toka usimame huku"
Tulisogea pembeni kidogo ya meza ile ili nishuudie.
Haikupita hata sekunde kama Chakula kilivyo shuka
ndivyo vyombo vilipotea kwenye meza ile, meza
yenyewe niliona tu inakuwa safi, chini ya meza napo
palikuwa safi viti vikajipanga vizuri Lakini aliyekuwa
anafanya hayo yote alikuwa aonekani.
"Umeona Jumanne?"
Jamila aliniuliza.
"Kweli nimeona kabisa"
Nilisema.
Basi huku tunaishi kifalme kwahio hakuna haja ya
kuogopa"
Jamila alisema tena.
Jumanne, Umeisha oga?"
Raulati aliniuliza.
"Bado sijaoga!"
"Basi twende ukaoge kwanza halafu ndiyo mambo
mengine yaendelee"
Raulati alisema. Kisha wakanishika mikono yangu
kama kawaida tukaongozana kurudi chumbani
kwangu, nililazimika kuwazoea wale wasichana
lakini bado nilikuwa na migogoro miwili juu yao.
Mgogoro hasi na chanya.
Chumbani kwangu wao walibaki mlangoni Mimi
nikaingia chumbani kisha nikitoka na lile koti la
manyoa huku nimelivaa mwilini, Taulo nilijua liko
huko bafuni nemeandaliwa kama kawaida.
"Sasa si naenda kuoga peke yangu!"
Nilisema ili kujiwekea taadhali.
"Ndiyo wewe nenda uwoge wala usijali; ukimaliza
kuoga na kuvaa kila kitu utatugongea chumbani
kwetu tutakuja tupige stori"
Raulati alisema kisha Mimi nikaongoza kuelekea
bafuni, wao nao wakaongoza kuelekea Chumbani
kwao. Bafuni nilifika nikaliweka lile linguo sehemu
maalumu ambayo ilikuwa imeandaliwa kwa ajili ya
kuanika taulo na nguo zingine. Kisha nikalifungua
bomba la maji ya mvua na kuanza kuoga. Bila
habari nilishangaa tu mlango wa bafu unafunguliwa.
Nilishituka sana nikalikimbilia taulo lakini nilikuwa
nimechelewa Jamila na Raulati walikuwa
washauteka mlango wa bafu tayari. Mwilini
walikuwa wamevalia nguo nyepesi halafu zimelowa
kabisa, nguo hizo zilikuwa zimegandana mwilini
mwao hatari.
"Aah! Sasa ndiyo mnafanya nini?"
Nilisema kwa utaratibu, nilianza kuogopa.
"Jumanne unaogopa nini, inamaana bado
unatuogopa tu"
Jamila alisema.
"Siwaogopi lakini......"
"Lakini nini Jumanne, sisi niwanawake wewe
mwanaume, itawezekana vipi tukae watatu tu,
sehemu kama hii kama mtu na Dada zake"
Raulati naye alisema.
"Jumanne, unaogopa nini sasa, makusudio ya sisi
kuwepo hapa na wewe lazima yanamaana kubwa,
huwenda hata ili nalo ni miongoni mwa makusudio
hayo. Tafadhali kuwa mwanaume"
Jamila alisema tena.
"Jumanne ebu tuangalie kwa muonekano wetu huu
bahati nzuri akajitokeza Mwanaume Mwingine
akatutimizia haja zetu wewe utajisikiaje, tafadhali
ndiyo wakati wako wa kutufanya utakavyo"
Raulati naye alisema.
Mabinti wale walikuwa wanaongea maneno mazito
ya kumtoa nyoka pangoni halafu kwa sauti laini
iliyopikwa ikapikika nao ikakubali kisha ikatamkwa
utafikiri mwanamziki JLo yupo kwenye chujio la
Sauti pindi anaimba nyimbo. Kilichonikosesha Uhuru
wa kuongea hawakunipa nafasi kabisa ya kuwajibu
hata neno moja. Hata Mimi nilianza kuhisi
mabadiliko ya hali ya juu, Nyoka alianza kujichomoa
pangoni.
"O oooh!" Nilisema huku nikilichukua taulo na
kujifunga, Sasa hapo ndipo ilikuwa kama nawatibua,
walianza kunisogelea huku wakiniita kwa madeko ya
hali ya Juu.
"Jumanne!......Jumanne! .....Jumanne!"
Sasa hapo Mimi nilizidi kusogea mpaka kwenye
ukuta kabisa wa bafu, kusema kweli kuta zile
zilikuwa safi sana, nilikosa pa kukimbilia, sasa huku
nyoka naye alikuwa kaisha jionesha(kujichora)
kabisa kuwa anataka kung'ata. Taulo lenyewe
lilidondoka lenyewe hata kabla wale mabinti
hawajanifikia.
 
SEHEMU YA (08).
Tafadhali Msiniangushe Share tafadhali nipate nguvu
ya kuzidi kuandaa hadithi zuuri kila mala, Share
share.
ILIPOISHIA.
Sasa hapo Mimi nilizidi kusogea mpaka kwenye
ukuta kabisa wa bafu, kusema kweli kuta zile
zilikuwa safi sana, nilikosa pa kukimbilia, sasa huku
nyoka naye alikuwa kaisha jionesha(kujichora)
kabisa kuwa anataka kung'ata. Taulo lenyewe
lilidondoka lenyewe hata kabla wale mabinti
hawajanifikia.
SONGA NAYO,
"Jumanne, tufanye tufurahi bhna, tafadhali tupo kwa
ajili yako, tupe tunachokihitaji, tunakupenda sana"
Sauti ya ajabu ilipenya Masikioni mwangu kutoka
kwa Raulati, bila shaka yeye ndiye alikuwa kulwa.
"Tupe utamu, tupe raha, tufanye tutabasamu kila
tutakapokuwa tunakuangalia, tufanye tusikuchukie,
tufanye tuyafurahie mazingira haya tuliyopo"
Jamila naye aliongezea. Neno tufanye tusikuchukie
ndilo lilinimaliza kabisa, kawaida Mtoto wa kike
akifikia hatua hiyo ukamwacha tu bila kufanya
chochote, basi jua kabisa kuwa wewe nayeye
mmekuwa maadui mpaka kufa. Kipindi
wanayaongea hayo walikuwa wamesimama karibu
kabisa wakiniangalia kwa macho ya matamanio,
Mimi tayari nilikuwa nahisi washaanza kunishika
kwa mikono yao milaini. Bado niliendelea
kusimama kwa kuegemea ukuta lakini nilikuwa
nikitamani wanianze wao nami niwaoneshe
mautundu ya ajabu. Nyoka yeye sasa alinipeleka
vibaya alitamani shimo ambalo lina ladha nyingine
kabisa kuliko zote Dunia, shimo ambalo linajoto la
pekee joto ambalo halipatikani sehemu nyingine
Duniani.
Watoto walinisogelea wakaanza kunishika shika
kifuani nguo zao wakaziachia nao wakabaki kama
ndio wamezaliwa yani watoto wachanga ambao
hawajui hata aibu iko wapi Duniani, vifuwa vyao
vikiwa vimetunga embe Dodo zilizokuwa zimeiva
vizuri tayari kwa kukamuliwa kwa ladha ya utamu.
Wakiwa wanafanya yao Mimi niliendelea kuushikilia
ukuta uku ladha nzuri ambayo sizani kuna mtu
ambaye uwa anaweza kuisimulia ikinitesa huku
nikiisi napaa hivi, sasa ladha ilizidi pale
niliposhikwa nyoka yangu kwa mikono laini ya wale
mabinti. Kwakweli niliisi kuzimia kwa ukari wa
kushikwa kwa mikono ile. Nilianza kuhemea juu juu,
nami nikaanza kuitumia mikono yangu, sasa kwa
ajili ya kuonesha mautundu yangu kwa mabinti wale
wazuri Duniani.
Hakiamungu mtu mmoja kushindana na watu wawili
ni ngumu, kabisa nilizidiwa nikabaki wa kuhema,
Jamila na Raulati wakaendelea kuniperekesha kwa
mikono yao laini. Mambo yalipozidi mimi
mwenyewe nilijikuta natamka.
"A place with no name, A place with no name!"
Mambo yaliponiwia magumu sasa, nilimkamata
mmoja nikambenjua sikuelewa nyoka aliiona vipi
shimo lilipo akaingia weee maumbo yao kwakweli
walijua kuyatumia ndani ya bafu mchezo ulichezeka,
kilichokuwa kinafanyika pale ni kubadilisha mpila tu,
Mapacha si kila sehemu wanafanana, hakiamungu
wale watoto hawakuzidiana kitu lakini kila mmoja
alikuwa na ladha yake. Mchezo ulikwenda kwa
dakika arobaini na tano ndani ya uwanja wa bafuni,
mapumziko tuliyamishia uwanja Mwingine,
tulikokotana tukaingia chumbani kwao, weee! Uko
ndiko hapakufaa kabisa. Tuliucheza mchezo karibu
masaa mawili na nusu ndiyo mambo yakapoa.
"Hapo ndipo maisha yanakwenda vizuri, eee!
Jumanne........A place with no name. Ha ha ha ha
ha!"
Mabinti wale walisema kisha wakacheka, waliirudia
kauli yangu, ambayo nilisema bafuni baada ya
kuzidiwa.
"Haya bhana, twende tukaoge sasa"
Nami nilisema. Nilisahu kabisa kuwa nilikuwa na
mgogoro juu ya mabinti wale, yani sikutaka tena
kuyaweka mawazo Yale ya ajabu nilibaki na wazo
moja tu la wapenzi basi.
"Nawapenda sana"
Nilijikuta nasema
Kipindi tuko bafuni tunaoga kutoa janaba.
"Hata sisi tunakupenda sana,............hautuogopi
tena Jumanne?"
Raulati aliuliza.
"Ni kweli siwaogopi kabisa ninyi wapenzi wangu"
"Tunashukuru sana mpenzi wetu,............ Kwahio
sasa tumekuwa wapenzi wako?"
Jamila naye aliuliza.
"Ndiyo"
Nilisema.
"Kwanini"
Waliniuliza tena.
"Kwasababu mumenionjesha ladha tamu"
Nilisema.
"Mh! Jumanne! Kweli tumekuonjesha tu, kwahio
bado unataka"
"Hapana, sitaki tena"
Nilisema.
"Basi usiseme kuwa tumekuonjesha, sema kuwa
tumekupa ladha nzuri"
Jamila alisema.
"Haya nashukuru kwa chakula kizuri mlichonipa"
Nilisema.
"Mh! Kumbe uko vizuri Jumanne, umeweza
kutuhimili wawili wote"
Raulati alisema.
"Ndiyo kwasababu lazima nikomae ili kila mmoja
wenu ajisikie kuwa kupata ladha ambayo anahitaji"
Nilisema. Kisha wote wakacheka.
"Haya asante bhna"
Raulati alisema.
Tuliendelea kuoga kipindi hiki tulikuwa ndani ya
Chumba chao mule mule nako kulikuwa na Bafu
pamoja na Choo kilikuwa ni Master room.
Tulimaliza kuoga vizuri wakanifuta maji kisha
tukatoka ndani ya Bafu. Tulipofika kitandani, tulikuta
mabadiliko makubwa, kwa mala nyingine
nilistaajabu sana; kitandani tulikuta nguo nyingine,
nzuri zaidi tena zilikuwa zimetengenezwa kwa
madini, yaani zile nguo zilipendeza sana tena sana,
kulikuwa na manukato tofauti kabisa manukato hayo
sikuwahi hata kuyasikia.
"Jumanne bado hujapata picha ya sisi kuwepo
hapa?"
Raulati aliniuliza.
"Hapana! Sijajua chochote"
Nilisema.
"Kuna sababu kubwa sana, hata kwa macho, yani
kitendo cha kufanya mapenzi sisi na wewe tayari
kabisa inaonesha dhairi kuwa kuna makusudio
makubwa ndiyo maana humu pamebadilika, huoni
hata shuka la kitanda limebadilika, nguo zenyewe
zilizokuja nizingine kabisa, yaani haya mavazi toka
tuwe hapa leo mwezi wa tatu hatukuwahi kuyaona,
hatukuwahi kupata manukato hata mala moja zaidi
ya nguo za kawaida, na nguo nzuri zaidi ni zile za
Jana tu"
Raulati alisema tena.
"Labda kwakuwa sisi ni Mabinti wa Kiislam
haturuhusiwi kupulizia manukato"
Jamila alisema.
"Kwa ulimwengu wa sasa Mh! ni ngumu sana, Mimi
nilikuwa naona watu huko nilikotoka walikuwa
wanapulizia tu, hata wanawake walio olewa tena hao
ndiyo wamepigwa marufuku kabisa kugusa hayo
manukato isipokuwa kwa waume zao"
Nilisema.
"Safi Jumanne nimepata wazo. Kwamaana hiyo sisi
na wewe tushakuwa wapenzi, inamaana sisi ni wake
zako?"
Raulati alisema.
"Ndiyo"
Nami nilikubali,
"Na uzuri sisi tunakaa Dunia ya peke yetu, kwahio
tutaishi hapa kama mume na wake zake
hakutokuwa na maneno maneno"
Raulati alisema tena.
Mazungumzo yetu yaliambatana na vitendo vingine
kama kupakaana mafuta, mafuta ambayo
tuliyatumia hayakuwa na manukato kabisa.
"Umeona Jumanne haya ndiyo mafuta ambayo huwa
sisi tunapaka, lakini ni mazuri kweli Kweli
yanazitunza Ngozi zetu hadi raha"
Jamila alisema.
Mabinti wale walinipamba vizuri sana na vazi lile
lilinipendeza sana, hakika lilinipendeza hata
nilipojiangalia kwenye kioo kikubwa kilichokuwa
ndani ya Chumba kile nilitaka kujikataa kuwa siye
Mimi, nilikuwa kama mfalme wa Dunia ya peke
yangu.
Wale mabinti nao walipendeza sana baada ya
kuyavaa mavazi yao yaliyofanana. Ndani mwanga
ulikuwemo, kutokea Juu ya madirisha yaliyokuwa
juu kabisa ya Jumba lile. Baada ya kumaliza zoezi
zima la kuvaa tulitoka chumbani na kwenda
sebuleni kukaa.
"Mlinambia kuwa huku kuna kila kitu isipokuwa
terevisheni tu, lakini Burudani ya Disco ipo"
Nilisema.
"Burudani ya Disco tumeisha icheza vizuri tu, huko
bafuni mpaka chumbani kwetu, ukumbuki
ulivyocheza Jumanne?"
Raulati alisema kisha wakacheka, hata Mimi
mwenyewe nilijikuta nacheka.
"Haya nashukuruni sana"
Nilisema, maneno yao yalimaanisha kuwa hakuna
Disco lakini wao ndio Disco kwangu. Kweli yani
kitendo cha kufanya nao mapenzi wale Mabinti
kwangu walibaki kuwa Disco. kwa penzi la wale
mabinti mapacha sikupenda niliache Jumba lile
mwenyewe nilipenda tu niendelee kukaa mule mule
ndani ya Jumba la A place with no Name.
"Nimependa hata tusitoke humu, Tuishi humu humu
ndani ya Jumba hili"
Nilisema.
Baada kusema hivyo, wale mabinti waliniangalia
huku wakitabasamu, kisha wakanambia.
"Hata sisi tunapenda tuendelee kuwa humu humu"
Mabinti wale walisema kwa pamoja.
Maisha ya jumba lile kwakweli nilianza kuyaona ya
pekee kwangu, kila kitu chenye Furaha nilikipata
kutoka kwa mabinti wale.
Mwezi sasa uliisha nikiwa ndani ya Jumba lile,
Sitarehe zilizidi kuwa nyingi kila kulipokuwa
kunakucha, Raulati na Jamila walizidi kunipa ladha
ya penzi la pekee ambalo sikuwahi kulipata Hapa
Duniani. Kwakweli wale wasichana Mimi
sitowasahau kamwe katika maisha yangu. Tukiwa
Katika mwezi wa Pili ndani ya Jumba lile, mabinti
wale walianza kusikia mabadiliko makubwa ndani
ya miili yao, Dalili hizo zilionesha kuwa ni za mimba
zilizo anza kutunga matumboni mwao, nilijisikia
Furaha sana baada ya wale mabinti kupata mimba.
Ndani ya Jumba lile ilikuwa kula, kuoga kujisaidia
kisha mnapiga story mnangoja kwenda kulala.
Siku moja tulikuwa tumekaa sebuleni tukiendelea
kupiga sitori kama kawaida Mimi na wapenzi wangu
(jamila na Raulati). Tukiwa hatuna hili wala lile
tulishangaa sehemu ya Jumba hilo inafunguka,
lilikuwa ni lango kubwa kweli kweli. Inje ya mlango
huo palionekana kama ni sehemu ya mji kabisa.
Tulishangaa sana hata hatukuamini, tulichokuwa
tunakiona. Tukiwa tunashangaa mala alitokea mzee
mmoja na mwanamke mmoja, halafu nyuma yake
kulikuwa na wanaume watano. Sijui niseme nini
kuusu wale wanaume, vilikuwa ni vidume virefu
hasa, na uzuri wa Jengo lile lilikuwa ni reefu, kwa
mkubwa wa viumbe wale Mimi nilikuwa najiunga
mala tano. Labda nilahisishe kwa kusema kuwa
kama uliwahi kuuiona movie ya JACK THE GIANT
mfano wake ni sawa na wale viumbe. Mapanga
mikononi yalikuwa makubwa labda Mimi nililingana
na ukubwa wa mapanga yao.
 
SEHEMU YA (09).
Naomba ku-share sana. Ku-share kwako kunanipa
matumaini ya kufika mbali. Nisaidieni bhna mtunzi
wenu kama mnanikubali.
ILIPOISHIA.
Jengo lile lilikuwa ni reefu, kwa mkubwa wa viumbe
wale Mimi nilikuwa najiunga mala tano. Labda
nilahisishe kwa kusema kuwa kama uliwahi kuiona
movie ya JACK THE GIANT mfano wake ni sawa na
wale viumbe. Mapanga mikononi yalikuwa
makubwa labda Mimi nililingana na ukubwa wa
mapanga yao.
SONGA NAYO,
Richa ya kuwa viumbe wakubwa usoni walikuwa
wamejichora kwa langi ambazo ziliwafanya kutisha,
kwakweli waliogopesha kabisa wale watu, ujasiri wa
kuendelea kukaa pale ulinikosa kabisa, nilijua huo
ndiyo wakati wangu wakufa. Nilipowageukia
wapenzi wangu(jamila na Raulati) wao niliwakuta
tayari wameisha zirai na kuzirai.
Akiwa na wale wanadamu wakubwa yule mzee na
mwanamke yule walisogea wakakaa kwenye moja
ya kiti katika jumba lile. Wale viumbe au wanadamu
wakubwa walisimama kama walinzi.
"Hongera Jumanne!"
Mzee yule alianza kwa kusema hivyo. Sikumuelewa
hongera yake ilimaanisha nini. Muda huo anaongea
Mimi mawazo yote yaliishia kwa wale magiant(watu
wakubwa) nilizani nitakufa siku hiyo.
"Jumanne usiwe na hofu mbona kawaida tu, hawa ni
watu wa kawaida na hawana madhala yoyote kwako,
ishi kwa kujiamini"
Mzee yule alisema, kisha akasimama pamoja na
Mwanamke aliyekuja naye kisha akanambia na
Mimi nisimame nimfuate, tulienda upande Mwingine
wa Jumba lile tukafika ukutani ambako kulikuwa
hakuna kitu chochote, akashika sehemu ya ukuta
huo ukafunguka mlango Mwingine tofauti na
alioingilia, kisha tukatoka inje, wale Magiant
walikuwa nyuma yetu wakitufuata, tulipo fika inje ya
Jumbe lile sikuona kitu chochote hakukuweko na
miti wala nyumba, ilikuwa kama ni jangwa kubwa
lakini Ardhi yake ilikuwa tambalale haina hata
mabonde. Kilikuwa ni eneo kubwa sana, ambalo
hata sikuweza kuona mwisho wake. Kwa inje Jumba
lile lilikuwa refu sana, na lilionekano lilijengwa
zamani sana.
"Tazama vizuri lakini bado siku mbili tu, na huu
ndiyo mlango Lakini eneo lote hili lina ulinzi
mkubwa sana wewe uoni"
Yule mzee alisema. Alinichanganya na kunitisha
zaidi aliposema bado siku mbili.
"Samahani mzee unamaanisha nini kusema kuwa
bado siku mbili?"
Ilinibidi nimuulize.
"Siku mbili za wewe kuendelea kuwemo ndani ya
Jumba hili la kifahari, jumba ambalo liko pasiko
julikana"
Mzee yule alisema.
"Kwamaana hiyo unamaanisha Mimi nitakufa?"
"Hapana hutokufa lakini bado siku mbili"
Yule mzee alisema kisha akasimama kama anaaga,
Mwanamke aliyekuwa naye akiwa sambamba naye,
ilionekana alikuwa ni mke wake, wale Magiant nayo
yakasogea karibu yake, pale pale wakapotea
nikabaki peke yangu pale inje ya Jumba lile.
Alinitesa sana kwa maneno yake kuwa Bado siku
mbili za kuendelea kuwepo kwenye Jumba lile
ambalo Mimi niliamini linastarehe kuliko mahara
kokote ambako niliwahi kufika.
Nilirudi ndani ya Jumbe lile bila kutarajia mlango
ule ulijifunga wenyewe, sikulijali hilo nilirudi pale
Sitting room kuwangalia wapenzi wangu wako
Katika hali gani. Cha ajabu nilipofika tu nao
wakaamka huku wakitabasamu, hapo ndipo
walinichanganya zaidi.
"Kwa maana hiyo mlikuwa mnajua kila kilichokuwa
kinaendelea?"
Nilijikuta nauliza.
"Unauliza nini mpenzi wetu?"
Raulati uliuliza ilionesha kabisa hakunielewa.
"Nauliza hivi kilichotokea hapa muda mfupi
mnakijua?"
Niliuliza tena.
"Mbona hatukuelewi kabisa unamaanisha nini,
maana sisi tuko sawa kama tulivyokuwa hapo
hawali hakuna jambo jipywa ambalo tumeliona"
Walinijibu.
"What...khaaa acheni basi, inamaana tumeanza
kuigiziana hapa?"
Niliuliza tena, maana walinichanganya nikajikuta
natumia nguvu kuwauliza.
"Kwanza tunaomba utusamehe mpenzi wetu, kabisa
hatujui chochote sisi hatuwezi kukuficha wewe
wakati wewe ndiye mume wetu na tunakaa sisi na
wewe tu humu hakuna Mwingine ambaye tunaweza
kumwekeza siri yetu zaidi ya wewe"
Mabint wale walisema kweli maneno yao yalinigusa
sana, japo kuwa tukio lile kidogo lilileta utata na
kunichanganya sana, nikaanza hata kukumbuka
matukio ya mwanzo ya sauti ambayo yalikuwa
yashaisha hayatokei tena.
"Jumanne hatuna Mwingine tena ambaye anaweza
kutufanya tufurahi katika maisha yetu yote zaidi
yako, tunakupenda sana"
Jamila alisimama na kusema.
"Kweli Jumanne tazama sasa dalili za mimba
zishajionesha kabisa katika matumbo yetu,
itakuwaje tukufiche kitu wakati wewe ndiwe mfalme
wetu"
Raulati naye alisimama na kusema.
"Okey kaeni chini kwanza tuzungumze taratibu"
Niliwambia nao kwa unyenyekevu kabisa wakakaa.
Sifa ya pekee ya wale wasichana kwangu kabisa
siwezi kuisahau waliyajua mapenzi kuliko kiasi
ambacho niliwahi kufikiri kama kuna wanawake wa
aina hiyo katika ulimwengu wa sasa, toka nianzishe
nao mahusiano ndani ya Jumba lile hawakuwa
wakubishana na Mimi, hawakuwa wa kuongea
ambacho kingeniuzi, walikuwa ni wacheshi, hata
pale nilipokuwa nawakosea wao walianza kwa
kuzungumza kwa kutanguliza masamaha halafu
ndiyo wanayatoa yaliyokuwa moyoni mwao. Kabisa
kwa vigezo hivyo kwangu ilikuwa si ngumu
kujishusha kwao.
"Sawa amjamuona mzee mmoja na mwanamke
halafu walikuwa na mamtu marefu makubwa
kabisa?"
Niliwauliza,
"Jumanne mpenzi wetu, we ulikuwa unaota he!"
Walinijibu, kiujumla walinishangaa nini nilikuwa
nakizungumza.
"Ni kweli kabisa amekuja hapa Mzee na Mke wake
pamoja na hao Binadamu wakubwa Mimi najiumba
mala tano. Hamjaona?"
"Ni kweli hatujui kabisa"
Walinijibu.
"Huu ukuta mnaouona huu ndiyo ulifunguka lango
kubwa, halafu kwa inje ikawa kama kuna mji kabisa
mpaka magari yalikuwa yanatembea. Hamjaona
hata hilo?"
Niliuliza tena kwa msisitizo.
"Ukweli hatujui kitu Jumanne mpenzi wetu, hatujui
kabisa"
Mabinti wale Walinijibu, niliisi kuchanganyikiwa
kabisa kwasababu lile lango linafunguka niliamini
kabisa kuwa hata wao walikuwa wanaona ingawa
sikuwa na hakika kwasababu nilikuwa nimezubalia
maeneo ya inje ya lango hilo.
"Basi sawa huwenda ni kweli hamkuona. Naombeni
mnisamehe na Mimi kwa kuwafanya muwe na
wasiwasi. Lakini jueni kuwa Mimi zimesalia siku
mbili ambazo si sizijui zinamaanisha nini katika
maisha yangu haya"
Nilisema kwa Uzuni.
"Jumanne tafadhali usizungumze hivyo, utatuumiza
sisi wapenzi wako"
Jamila alisema huku akionekana kabisa ni mwenye
maumivu moyono, hata Raulati naye alionekana vile
vile.
"Please Jumanne mpenzi wetu, kama kuna jambo
jipya tafadhali naomba utuweke wazi tujue namna ya
kutafuta suruhisho maana ushatutisha tayari wenzio.
Kumbuka tunakupenda sana, tunaamini maisha yetu
bila wewe hayaendi Jumanne"
Raulati alisema.
Maneno yao yalinitoa machozi nilikosa kabisa ujasiri
wa kiume. Iliniuma hata Mimi kwakweli japokuwa
nilikuwa sijui bado siku mbili ilimaanisha nini.
Ilinibidi niwasimulie kisa kizima Jinsi yule mzee
alipotokea na Mke wake pamoja na Magiant(mamtu
makubwa) wakanitoa inje na kunambia maneno
"Bado siku mbili".
"Sawa Jumanne hizo siku mbili ni zako, lakini
tunakuomba ni Bora tufe wote lakini haiwezekani
kabisa wewe hutuache humu, eiza kwa kufa au kwa
kuondoka........ Wewe ni mwanaume wa pekee
kwetu Jumanne tambua tunakupenda kuliko
chochote"
Mabinti wale walisema. Maumivu yao yalikuwa ni
makubwa kabisa, ingawa hata Mimi nilikuwa na
maumivu lakini nilijikuta najilaumu kwanini
nililisema jambo lile kwao, niliwaonea huruma sana
wapenzi wangu, walikuwa wananipenda sana, tena
sana. Upendo ambao walikuwa nao kwangu sizani
kama kuna uwezekano wa kuusimulia, labda jua tu
kuwa upendo ambao ukimwacha mwenzako kwa
muda wa masaa mawili tu, unaona kama vile
umekosa kitu kikubwa sana katika maisha yako,
kuna mapenzi jamani, Duniani kuna mapenzi ambayo
kwakweli yanaweza yakakufanya ujisahau kama kuna
majukumu mengine labda tuseme ni kwasababu
nilikuwa ndani ya Jumba lile la ajabu.
"Msijali okey naombeni mjipe Ujasiri nawependa
sana"
Niliwambia wote kwa pamoja walisimama
wakanikumbatia.
"Twende tukale muda umeenda sana"
Niliwambia wapenzi wangu. Kweli muda ulikuwa
ushaenda sana, ilikuwa kama ni saa nane na nusu
za mchana.
"Haya"
Walisema kisha wakasimama. Kidogo Furaha
iliwarejea moyoni mwao. Tulipofika mezani kila
tulicheza mchezo mzuri ambao hatukuwahi
kuucheza, mchezo huo ulikuwa kila mmoja
anamuombea mwenzake chakula ambacho
anakupenda bila hata kuangalia ni kikubwa kiasi
gani, vyakula vilirundikana kwenye meza hatari, kula
sasa napo ukawa mchezo ambao ulituacha hoi,
kwani tulikuwa tunakula kwa Style ya pekee,
ulipokuwa unashiba unamchagua mwenzako ale
chakula badala yako, hata kama ulikuwa ushashiba
mwenzio akikuchagua nawe unakula badala yake.
Sikuwahi kufurahia kama siku hiyo, tulikuwa hata
kuamka kwenye meza ikawa mtihani, tulikuwa
tunacheka tu, yani japo kuwa tulikuwa tumeshiba
sana. Mambo yalipotuwiya magumu tufikiri ni
namna gani tunaweza kupunguza shibe.
"Ningepata kitu cha kupunguzia shibe ningekula tena
halafu nikakwambia Jumanne uongezee badala
yangu tuone itakuwaje"
Raulati alisema.
"Mh! We Raulati usiseme hivyo usijekumfanya
mpenzi wangu akapasuka wakati anatembea na
moyo wangu"
Jamila naye alisema. Ilikuwa Furaha sana kwenye
meza ya Chakula. Muda huo huo tulishangaa
ikashuka Juice yenye muonekano kama embe. "Sisi
tushashiba bila shaka hii ni dawa ya kupunguza
shibe"
Nilisema.
Huku nikipereka mikono kwenye ile Chupa iliyokuwa
na Juice hiyo. Hata kabla sijaishika Jamila
aliipokonya akaifungua na kunywa yeye.
 
SEHEMU YA (10).
Naomba nifikishe Share 100 kama unaipenda
hadithi hii tafadhali Share.
ILIPOISHIA.
Ilikuwa Furaha sana kwenye meza ya Chakula. Muda
huo huo tulishangaa ikashuka Juice yenye
nuonekano kama embe.
"Sisi tushashiba bila shaka hii ni dawa ya
kupunguza shibe"
Nilisema.
Huku nikipereka mikono kwenye ile Chupa iliyokuwa
na Juice hiyo. Hata kabla sijaishika Jamila
aliipokonya akaifungua na kunywa yeye.
SONGA NAYO.
Kweli kama mawazo yangu yalivyokuwa, baada ya
kuinywa ile Jamila alijisikia vizuri kama hajala kitu,
chakula chote tumboni kiliyeyuka. Baada ya jamila
kuwa vizuri wote tuliinywa Juice ile matumbo
yakawa safi. Siku hiyo kwetu hali ilibadilika na kuwa
safi kabisa.
Usiku nikiwa kitandani mawazo yalianza kujirudia
kichwani mwangu. Maneno aliyoyazungumza mzee
yule yalianza kujirudia na kukitawala kichwa kizima.
"Kwanini kanambia vile? alimaanisha nini?
Kwasababu gani?"
Nilijikuta najiuliza mwenyewe nikiwa kitandani.
Safari ya kujiuliza haikuishia pale nilianza
kukumbuka Jinsi nilivyofika ndani ya Jumba lile
ambalo tulilipa jina la A place with no Name. Hapo
ndipo uoga kwangu uliongezeka zaidi.
"Kwanini nisiwatoroke hawa wasichana, kwani hata
hivyo Mimi niliwakuta humu, siwajui hawanijui,
tulijuana humu humu. Japo kuwa nawapenda lakini
nitafanya nini, amna namna lazima niwaache
niondoke kabisa ndani ya jumba hili la ajabu"
Niliwaza usiku huo nikiwa kitandani nimekaa.
Wapenzi wangu Jamila na Raulati walikuwa
wamelala Fo fo fo hawajitambui, hata hivyo masaa
yalikuwa yashaenda sana, kwa kufikiri ilikuwa kama
saa kumi za usiku. Baada ya kuwaza sana niliamka
kitandani nikavaa nguo zangu, Suruali na tisheti
kisha nikatoka chumbani mule, sikuwaza tena
kingine zaidi ya kuwatoroka wasichana wale, maana
niliisi alichonambia yule mzee kitakuwa ni kifo tu,
hakuna kitu kingine zaidi ya kifo.
Maajabu ya Jumba lile yalikuwa mengi sana.
Mengine ni kwamba ukiamka usiku kama unashida
ya Chooni kulikuwa kuna switch za kuwasha taa
kabisa kama tanesco lakini mchana taa hizo
zilikuwa hazionekani lakini usiku ndio taa zilikuwa
zinaonekana. Yani kwa kulitafakari jumba lile lazima
uogope sana. Chumbani mule nilitoka Giza, huku
sebuleni ndio niliwasha hio taa ya ajabu, kisha
nikausogelea ukuta mahara aliposhika yule mzee
ukuta ukafunguka. Nilipofika nikashika kama
alivyoshika yeye kweli ukuta ule ulifunguka kama
kawaida. Sikutaka kuangalia nyuma nilitoka inje ya
Jumbe lile, mazingira yalikuwa Yale Yale kama
jangwa. Hapo nilianza kuwaza wapi niende ili nipate
kutoka katika lile eneo la A place with no name
nirudi nyumbani.
Nikiwa ndio nimepiga hatua kama saba kutoka
karibu ya Jumba lile, niliisi kama kuna makelele
mengi ya watu wenye mapanga wananifuata, watu
wale nilikuwa siwaoni kabisa. Niligeuka huku na
kule kuangalia ni wapi makelele Yale yanatokea
sikufanikiwa kuona kwani yalikuwa kama vile
yananizunguka, nilizidi kuogopa pale inje ya lile
jumba, nikatamani nirudi ndani, ya jumba lile kwani
mlango hata sikuufunga niliuwacha wazi. Nilipiga
hatua kulisogelea jumba lile lakini cha ajabu
nilikuwa silifikii, kila hatua yangu niliyokuwa naipiga
ilikuwa kama nalipushi jumba lile kusogea mbele
mala saba ya hatua zangu, au nilikuwa nakua kama
narudi nyuma kama hatua saba kutoka lilipokuwa
jumba lile la pekee katika Dunia hii. Mpaka
kunaanza kupambazuka vizuri nilikuwa sijalikaribia
Jumba lile, ingawa nilikuwa nakimbia lakini
sikufanikiwa kulifikia, hata kelele nilizokuwa
nazisikiliza zilikata kabisa. Jumba lile sikuliona tena
machoni mwangu. Nikiwa nimechoka niliamua
kusimama, pembeni yangu kulikuwa na mti
mkubwa, akili zikanituma nisogee pale
nikajipumzishe kwa uchovu niliokuwa nao. Mti ule
ulikuwa pekee ndani ya jangwa lile, sikujua kabisa
lilitokea wapi kwani kwa umri wangu sikuwahi
kusikia kuwa kuna mti mkubwa ndani ya jangwa
kama ule mti. Nilisogea na kukaa pale chini ya mti,
nikiwa pale mala niliisi usingizi ghafra, nilijikaza
nisinzie kwasababu nilikuwa maeneo ambayo siyajui
kwahio nilikuwa nahofu. Richa ya kujikaza lakini
sikufanikiwa kujizuia niliijikuta nazama ndani ya
usingizi. Nikiwa katikatika kabisa ya usingizi mzito
niliota ndoto. Ndoto ili nilikuwa ndani ya Jumba
nililotoroka mbele ya Wapenzi wangu Raulati na
Jamila wakinililia.
"Jumanne usiondoke, usituache sisi peke yetu
tutakufa.........Tafadhali Jumanne tunakupenda
sana"
Mabinti wale walizidi kunililia ndani ya ndoto, walilia
mpaka wakawa wanagaa gaa chini na mimba zao,
lakini Mimi bado nilishikilia msimamo wangu wa
kutowasikiliza, ila nilitamani kuliacha jumba lile
kama nilivyolikuta.
"Jumanne huku hupajui, huwenda unakoelekea ndiko
kubaya, ujui yule mzee alimaanisha nini, huwenda ni
kufunga ndoa yetu"
Tena Sauti ya Raulati ilisema. Mabinti wale walilia
sana lakini sikuelewa kabisa, kabisa sikuelewa
walichokuwa wananiambia. Baada yakuona kelele
zao zilipozidi niliamua kuondoka na kuwaacha ndani
ya Jumba lile, lakini mabinti wale walinifuata nyuma
wakidai ni Bora tuondoke wote ndani ya Jumba lile.
Nilifika mlangoni nikaufungua mlango na kutoka
inje, hata kabla Raulati na Jamila hawajatoka inje ya
jumba lile mlango ulijifunga, Mimi nilikuwa
nimewageukia nikiwaangalia, huruma iliniingia Sana,
nikatamani niushike mlango nirudi tena ndani lakini
nijisemea.
"Potelea mbali"
Nilisema kisha nikageuka kuondoka zangu.
Nilipogeuka tu hivi, macho yangu yalikutana na jitu
la ajabu tena linatisha, sikuwahi kuona kiumbe cha
vile hata kwenye movies. Mwenyewe niligeuka
haraka kurudi ndani ya Jumba lakini Sikuweza
kuufungua ukuta ule.
Kile kiumbe cha ajabu kilinua mkono wake mlefu
kwa ajili ya kunikamata, pale pale nilishituka
usingizini. Baada ya kushituka niliitafakari ile ndoto.
Nilianza kuogopa mwenyewe baada ya kuitafakari
ile ndoto ya kuogopesha.
Niliamua kusimama ili niondoke pale chini ya mti.
Lakini kumbe mazingira hayakuwa Yale tena
nilijikuta niko ndani ya msitu mkubwa. Hapo ndipo
nilizidi kuogopa zaidi ya hawali.
"Mungu wangu niokoe!"
Nilisema ndani ya msitu huo. Kila nilipokuwa
nageuka huku na kule sikuweza kabisa kuona
mwisho wa msitu ule. Mala niliisi kabisa kuna kundi
la watu linanifukuza kutoka nyuma yangu, niligeuka
nyuma kwa haraka, kuona kama kweli kuna kundi la
watu. Kweli niliona kundi kubwa la watu nyuma
yangu, watu wale walikuwa wameshikilia mapanga
mikononi mwao. Watu wale dhairi walionesha kuwa
wanakuja kwangu, niliogopa Sana, nguvu za uoga
zenye kunisukuma kukimbia zilinijia, pale pale
nikaanza kukimbia ili kukoa Uhai wangu. Moyoni
nilikuwa nauimba wimbo wa Miguu nisaidie moyo
hauna Duka.
Nilikimbia sana, tena sana lakini lile kundi lilizidi
kunifuata nyuma. Lilikuwa ni kundi kubwa sana, kila
nilipokuwa naongeza spidi ya kukimbia basi ilikuwa
kama nawaongeza nao spidi ya kukimbia. Watu
wale walionekana kama jeshi la zamani kabisa kwa
jinsi walivyokuwa wanatazamika. Nyusoni mwao
walikuwa wamejichora kwa marangi maupe.
Walionekana kutisha sana, japo kuwa nilikuwa
nakimbia sana lakini nilikuwa sijui wapi nilikuwa
naelekea kwasababu ndani ya msitu ule kulikuwa
apaeleweki mwanzo ni wapi na mwisho ni wapi,
maana ilikuwa kama tunazunguka tu ndani ya msitu
ule wa kutisha. Nakumbuka nilikimbia umbali mrefu
sana, nikajikwaa na kuanguka chini, sikupata
kuamka tena baada ya kuanguka.
Bali nilishitushwa na kitu cha Baridi kikinigusa
mwilini mwangu, nilishituka sana lakini nilichokutana
nacho kilinishitua zaidi na nilitamani kufa hata kabla
ya siku zangu, nilitamani hata Ardhi ipasuke niingie
basi nife.
Wakati huo hata maneno ya Raulati ya kwenye
ndoto yalianza kujirudia tena, nikaanza kujilaumu
kwanini nilichukua maamuzi ya kuondoka ndani ya
Jumba lile nikawaacha wapenzi wangu, tena niliishi
kwa Furaha kila kitu nilikipata. Muda huo mbele
yangu kulikuwa na joka kubwa ambalo sizani kama
niliwahi kuliona katika mazingira ya ulimwengu huu,
ni Joka ambalo lilikuwa na uwezo wa kunimeza
halafu bado nisitoshe tumboni mwake nikabaki
nemeelea yaani lisishibe kabisa. Nilitetemeka mwili
mzima pale chini nilipokuwa mpaka mkojo
ukanitoka, halafu muda huo nilikuwa na njaa na
masaa yalionesha ni Jioni kwenye masaa ya Saa
kumi na mbili.
Lile Joka lilizidi kuniangalia Kama linanitamani
Sana. Baada ya kuona mambo yamekuwa magumu
nilifumba macho yangu hata kama linanimeza basi
nisione jinsi ambavyo lingenimeza. Nilifumba
macho kama dakika tano kisha nikafumbua.
Nilipofumbua macho yangu sikulikuta lile Joka
nilijikuta niko pekee maeneo Yale.
ITAENDELEA.
 
SEHEMU YA (11).
ILIPOISHIA.
Lile Joka lilizidi kuniangalia Kama linanitamani
Sana. Baada ya kuona mambo yamekuwa magumu
nilifumba macho yangu hata kama linanimeza basi
nisione jinsi ambavyo lingenimeza. Nilifumba
macho kama dakika tano kisha nikafumbua.
Nilipofumbua macho yangu sikulikuta lile Joka
nilijikuta niko pekee maeneo Yale.
SONGA NAYO.
Nilibaki pale nikijiuliza kuusu joka lile la aina yake
bila majibu, nguvu za kusimama kutoka pale
nilipokuwa zliniishia kabisa sikuwa na uwezo hata
wa kusimama kwa ajili ya kuondoka eneo lile.
Bado nikiwa nimekaa pale pale mala nilisikia sauti
ya mwanamke ikinita jina langu.
"Jamanne! Jumanne! Jumanne!"
Nilishituka sana maana sauti tu ndio ilikuwa
ikisikika bila kumuona aliyekuwa ananiita, labda
kwakuwa giza lilikuwa lishaanza kutanda ndio
maana sikuweza kumuona mtu yule. Richa ya hivyo
pia niliogopa sana, maana kulikuwa ni msituni
kabisa, mahala ambapo naweza kusema palikuwa
panatisha sana.
"Jumanne mbona uko huku nani kakufikisha huku?"
Sauti ile ilizidi kusikika. Tena wakati huu ndio
ilisikika ikinisemesha tena msemaji alikuwa Jirani
yangu kabisa.
"We nani mbona sikuoni?"
Nilijikuta nasema kwa uwoga.
"Nimekuja kukusaidia na sijui ni Kwanini umetoka
ulipokuwa?"
Sauti ile ilisema tena.
"Sijui Kwanini nimetoka huko, lakini ungejitokeza
hata nikuone maana unaniogopesha ukiendelea
kujificha!"
Nilisema tena.
"Ha ha ha ha! Unaogopa nini Jumanne wakati
nemekwambia nimekuja kukusaidia?"
Sauti ile ilisikika tena. Ilikuwa ni Sauti ya kike,
Mwanamke tena ailionekana ni msichana tu.
"Basi naomba unisaidie kama umekataa kujitokeza"
Nilisema.
Ghafra alijitokeza Binti mzuuri mweupe halafu
mavazi yake ya mng'ao hata nywele zake zilikuwa
ziking'aa kabisa. Moyoni nikajikuta najihakikishia
kuwa.
"Bila shaka huyu ni malaika wa mungu, mungu
kakisikia kilio changu"
Nilibaki kumzubalia Mwanamke yule(malaika) kama
nilivyoazania, yeye naye akaniangalia sana tu,
macho yetu yakakutana sana.
"Kwa maana hiyo malaika wa mungu ndio wazuri
hivyo. Je na wale wanawake wa peponi ambao
mwenyezi Mungu katuahidi nawenyewe wako kama
wewe?"
Nilijikuta naropoka kabisa, uoga ulinishia kabisa,
kusema kuwa amekuja kunisaidia na kumuona mtu
mwenyewe kweli nilijikuta najiamini kuwa nimeisha
pata usalama.
"Ha ha ha ha haaa! Jumanne unanishangaza sana.
Mimi sio Malaika kama uzaniavyo, Malaika wana
mabawa Mimi sina, malaika hawana Jinsia lakini
wanamajina ya kiume wote"
Mwanamke yule alisema.
"Sasa kama siyo malaika ni nani sasa?"
Nilimuuliza mwanamke yule mzuuri.
"Naomba unifuate utajua Mimi ni nani?"
Mwanamke yule alisema, kauli hiyo kidogo ilinitisha
nikaanza kumuhofia Mwanamke yule tena.
"Huwenda ni Jini ndio linaenda kunimaliza kabisa"
Niliwaza huku mwanamke yule akizipiga hatua
kusonga mbele Mimi bado niliendelea kusimama
kumwangalia.
"Jumanne mbona amesimama njoo"
Mwanamke yule alisema. Nami nilianza kupiga
hatua kumfuata, alisimama akinisubili.
"Unaitwa nani?"
"Naitwa Fiona"
"Fiona!"
Nilirudia jina lake kwa mshangao maana jina hilo
siyo hata la kitanzania na wala si katika Afrika, Asiri
yake ni Ulaya hasa Ugiriki huko ndiko majina ya
hivyo yako.
"Unanikumbuka?"
Aliniuliza.
"Nakukumbuka! Hapana na nitakukumbuka Vipi
wakati sikuwahi hata kukuona"
"Aaa! Sawa twendelee na safari yetu"
Mwanamke yule alisema. Tukaendelea kutembea
kuelekea alikokuwa anakujua yeye. Muda wote Mimi
nilitamani kumuuliza maswali basi, maana nilikuwa
na maswali yasiyopungua mia moja kuusu eneo hilo
halafu na Mimi nilifikaje eneo hilo.
"Samahani Fiona, naomba kujua eneo hili liko
wapi?, na linaitwaje? Na watu wa huku mnaishi je?"
Nilijikuta nauliza maswali hayo.
"Jumanne huku ni sehemu ambayo hakuna kiumbe
chochote kinachojua kunaitwaje? Hakuna
Mwanadamu au Jini anaye jua eneo hili liko wapi,
kuusu kuishi tunaishi kama kawaida tu. Mbona
umeniuliza maswali hayo?"
Fiona naye aliniuliza baada ya kunijibu.
"Aaaa! Kwasababu nilitaka kujua tu"
Nilimjibu.
"Mh! Jumanne hivyo tu basi"
Fiona alisema.
"Ndiyo hivyo tu basi"
Nilisema.
"Ngoja Mimi nikuulize, wewe umetokea wapi mpaka
kufika hapa?"
Fiona aliniuliza swali hilo ambalo Mimi mwenyewe
nilitamani nimuulize anisaidie.
"Sijui hata nilikotokea na sijui nilifika vipi hapa"
Nilisema. Maneno yangu yalimfanya Fiona acheke.
"Mbona unanicheka"
Nilijua ni Mimi tu, ambaye anaishi sehemu ambayo
haina Jina kumbe hata wewe ulikuwa ukiishi
Sehemu ambayo haikuwa na jina pole sana
Jumanne"
Fiona alisema, nilichoka nakuchoka kabisa.
Nikasimama tena kuendelea kumtafarakari Fiona.
"Usisimame Jumanne tunakoenda ni mbali sana
kwahio jikaze kabla Giza alijawa Nene zaidi maana
tutalazimika kutumia taa". Fiona alisema.
Kweli tuliendelea kutembea hata Mimi mwenyewe
nilikaza mwendo kidogo ili tuwahi kufika.
Tulitembea sana mpaka usiku ukaingia kama mida
ya saa mbili na nusu bado nilikuwa sijaona
muelekeo wa pale tunapoelekea.
Njiani tulikuwa tunazungumza mengi ya kawaida.
"Fiona mbona hatufiki Mimi nimeisha choka!"
Nilisema.
"Jumanne wewe ni mwanaume utachoka vipi
mapema hivi, sasa utawezaje kulifanikisha lengo
lako kama ukiwa legelege"
Fiona alisema.
Kauli yake ilinishitua sana.
"Kwahio unajua nini ambacho kimo ndani ya akili
zangu?"
Nilimuuliza.
"Ndio maana nilikuuliza unanikumbuka?"
"Hapana"
Nilisema.
"Haya twendelee"
Fiona alisema kisha tukaendelea na safari yetu,
usiku huo. Msituni mule kulikuwa na mwanga wa
mbala mwezi ukimulika kwahio kidogo tulikuwa
tunaona vizuri. Lakini tulifikia mahala pakawa Giza
sehemu yote, Giza hilo lilisababishwa na kivuli cha
miti ambayo ilikuwa imepangana kwa kurundikana.
"Gizani hapa huogopi Fiona?"
Niliuliza.
"Kama unaogopa Mimi Niko kwa ajili yako, ngoja
nikuwashie taa"
Fiona alisema mala ghafula mwanga angavu
ukatokea kwenye mikono yake, mikononi alikuwa
kama kashikilia kitu cha mng'ao ambacho
kilisababisha mwanga huo.
"Haya jiamini twende sasa"
Fiona alisema.
Tuliendelea na Safari yetu, lakini sasa Mimi bado
nilibaki najiuliza kwanini Fiona ananiuliza kuusu
kumkumbuka wakati Mimi sikuwahi hata kumuona,
sikuwahi hata kumuwaza.
"Sawa nimekumbuka"
Nilisema.
Muda huo nilikumbuka kuwa niliwahi kuota ndoto
toka nikiwa mdogo bado nasoma Darasa la Tano.
Ndoto hiyo ilikuwa ya kutisha kweli kweli, nimo
ndani ya msitu mkubwa halafu nafukuzwa na watu
wa kutisha kama wachawi, nikiwa nakimbia ndio
alitokea mtu akaniokoa mtu huyo alikuwa ni kama
Fiona vile vile mpaka umri.
"Nashukuru kama umenikumbuka"
Fiona alisema.
"Sasa.....!
"Usizungumze chochote tena, nyamaza tukifika
tunakoelekea tutazungumza kwa mengi mpaka
mengine utaacha ya ziada"
Fiona alinikatisha nilichokuwa nataka kuzungumza,
nikabaki kimya huku tukiendelea, nilikuwa bado na
mambo mengi ya kuzungumza naye ila ilinibidi
nikae kimya ili kutekeleza wajibu.
Kwakweli sikuwahi kutembea safari ndefu kama ile
toka kuzaliwa kwangu, safari ile ilikuwa ya kwanza
kwa urefu katika maisha yangu, ilikuwa ni safari
ndefu sikuwahi pata, naamini muda ule ulikuwa
tayari ni saa 3 za usiku bado tulikuwa ndani ya
msitu tukitembea, niliisi kuchoka sana lakini Fiona
alizidi kunipa matumaini kuwa bado kidogo
usichoke, nami nilizidi kujikaza, lakini ilifikia kipindi
nikakata tamaa kabisa ya kuendelea kutembea
ndani ya mstu ule, nikachoka nikakaa chini kabisa.
"Jumanne nikuache niondoke zangu?"
Fiona aliniuliza.
"Nimechoka Fiona, nimechoka sana, maana hatufiki
naamini mpaka sasa nimasaa manne tumeisha
tumia tunatembea tu, kwani huu ni Msitu wa aina
gani ambao haufiki mwisho, toka tuanze kutembea
tumo humu tu, hatutoki kabisa Mimi nimechoka
sana aisee"
Nilisema.
"Kwahio unataka nikubebe"
Fiona alisema.
Swali lake nilikosa namna ya kulijibu.
"Mimi nakuacha utajua wewe utakako elekea Mimi
nataka kukusaidia wewe unakuwa mchovu kwani
Mimi sitembei kama wewe!"
Fiona alisema.
"Sawa Fiona lakini Mimi nimechoka sana,
nisikudanganye na isitoshe nina njaa kwani sijala
toka asubuhi"
"Najua unanjaa na sikwamba Mimi ndio sababu
hayo umeyataka wewe mwenyewe hakuna
aliyekukimbiza katika Jumba la Kifalme. Hivi
unazani Mimi nisingakuja kukusaidia ungekuwaje
wewe, kama si kufa si bado ungekuwa unateseka
huku Msituni usijue wapi pa kwenda, na hiyo njaa
yako si ungekuwa nayo au chakula unakiona kama
unakiona chukua ule"
Fiona alisema kwa sauti ya ukakamavu.
Maneno yake yaliniumiza sana, kumbe kule
nilikotoka kulikuwa ni Ufalme ndio maana nilikuwa
na kula vizuri navaa vizuri.
"Kwahio yule mzee alimaanisha nini kusema bado
siku mbili"
Nijikuta nageuza maada tena.
"Nimekwambia usiniulize swali lolote mpaka tufike
tunakoelekea. Hata hivyo nikuache tuone utafanya
nini ndani ya msitu huu maana ungekuwa peke yako
mpaka sasa"
Fiona alisema kisha akatoweka muda huo huo.
 
SEHEMU YA (12)
Na HEMED MAYUGU.
ILIPOISHIA.
"Kwahio yule mzee alimaanisha nini kusema bado
siku mbili"
Nijikuta nageuza maada tena.
"Nimekwambia usiniulize swali lolote mpaka tufike
tunakoelekea. Hata hivyo nikuache tuone utafanya
nini ndani ya msitu huu maana ungekuwa peke yako
mpaka sasa"
Fiona alisema kisha akatoweka muda huo huo.
SONGA NAYO.
Nilibaki pale bila kujua nifanye nini zaidi ya
kuogopa. Kila nilipokuwa napiga jicho kule na huku
sikuona Chochote kwasababu ya mwanga hafifu wa
mbala mwezi, nilizidi kuogopa na kuogopa,
nikashindwa kutoka pale hata kulitamka Jina la
Fiona niliogopa maana nilihofia kuwa kama kuna
jitu la ajabu lingenisikia na kuja kunila.
"Mungu wangu nisaidie, niokoe katika janga hili
zito"
Nilijikuta nainua mikono yangu na kuomba huku
nimesimama. Bado nikiwa nawaza na kujiuliza nini
cha kufanya nilisikia kama vile kuna kitu kinatikisa
tikisa miti harafu kama kinakoroma, mapigo ya
moyo yaliniripuka paa! Pale nguvu ziliniishia nikakaa
chini kabisa, sijui kwanini hali ile kilinikuta, na
ukiongezea na njaa tumbo lote lilikuwa linatetemeka
utafikiri tetemeko la Ardhi ndilo limepita ndani ya
tumbo langu.
Muda huo huo machozi yalianza kunitoka
nikatamani kufa kabisa maana siyo mateso
kwakweli. Bado nikiwa najililia peke yangu mala
mbele yangu niliona vitu viwili vya mng'ao halafu
vikubwa kweli kweli, vitu hivyo vilikuwa
vinanisogelea, na kila nilipokuwa vinafika sehemu ya
kivuli vilififia, moja kwa moja nikajua bila shaka ni
Joka tena bonge la Joka. Toka hapo nisikufiche
nilikuja kuamka kumekucha asubuhi nipo kitandani.
Nilianza kuyachunguza mazingira ya kitanda kile
kidogo yalikuwa yatofauti kabisa hata Chumba
chenyewe kilionekana kichakavu kabisa, mashuka ya
kitanda yalikuwa ya ajabu ajabu tu, bado nikiwa
nimezubaa Mala ndani ya Chumba hicho aliingia
Fiona.
"Jumanne ushaamka?"
Fiona aliniuliza.
"Ndiyo"
Nilimjibu kwa unyonge.
"Vipi! unajisikiaje?"
"Kawaida tu"
Nilimjibu Fiona.
"Haya amka ukaoge halafu ndio mambo mengine
yafuate"
Fiona alisema kisha namimi nikaamka Fiona
akaniongoza kuelekea sehemu ya Kuoga. Tulitoka
inje ya jumba ambalo Fiona alikuwa anaishi, lilikuwa
ni Jumba lililochoka, lilionekana kama Jumba
lililojengwa miaka amsini likatelekezwa, lakini
lilikuwa ni Jumba kubwa sana.
"Jumanne mbona unaizubalia Nyumba yangu, humu
ndimo tutakuwa tunakaa Mimi na wewe"
Fiona alisema.
"Mimi na wewe wawili tu?"
Nilimuuliza swali hilo.
"Ndiyo"
"Lakini Mimi sipendi kuishi huku nahitaji kurudi
nyumbani kwetu"
"Ha ha ha ha haaa! Jumanne unawaza kurudi
nyumbani kwenu, unapajua kwenu nikuache
uwende?"
Fiona alicheka kwanza kisha akaniuliza. Sikupata
hata jawabu la kumjibu maana ule mkiki wa Jana
ambao nilikumbana nao ulinitisha sana, kiherehere
kilinitoka kabisa.
Muda huo tulikuwa tumesimama. Jumba lile lilikuwa
lipo polini kabisa na lilikuwa limezungukwa na miti
kama kawaida. Fiona alinishika mkono mpaka
sehemu ambao kulikuwa na bwawa kubwa ambalo
maji yake yalikuwa yanatiririka.
"Hapa ndipo huwa naoga Mimi. Kwahio vua uoge"
Fiona alisema.
"Na wewe ukiwa hapa hapa nivue nioge?"
Nilimuuliza Fiona.
"Jumanne sasa unaogopa nini wakati umelala bila
kujitambua, umeamka bila njaa, unajua nimekufanyia
nini? Wewe oga wala huna Chochote cha kunificha
kwanza kila kitu nakiona hata kama umevaa nguo"
Fiona alisema.
Kwakweli maneno yake yalinitisha na kunifanya
nianze kumuogopa.
Kibishi tu nilivua nguo nikaingia kwenye maji na
kuoga. Fiona yeye alikuwa amekaa huku
akiniangalia na kutabasamu.
Nilioga kihoga hoga kisha nikatoka kwenye maji na
kujifuta kwa Taulo la ajabu ajabu ambalo alinipatia
Fiona.
"Umemaliza?"
Fiona aliniuliza Baada ya kumaliza kujifuta maji.
"Ndiyo"
"Haya vaa nguo zako turudi ndani"
Fiona alisema. Nguo zangu zilikuwa ni zile zile
nilizotoroka nazo kutoka kwenye Jumba la A PLACE
WITH NO NAME, kama tulivyolitungia jina Jumba
hilo.
"Jumanne unakumbuka kitu gani kizuri toka uwe
kwenye haya mazingira ambayo huyajui kabisa?"
Fiona aliniuliza.
"Msaada wako tu ndio mzuuri kuliko vyote"
Nilimjibu nami hivyo, nilitamani nimjibu kuwa penzi
la Raulati na Jamila ndilo kitu kizuri ambacho
nakikumbuka kuliko vyote lakini nilisita kwasababu
hata Fiona naye alikuwa mwanamke kwahio niliisi
kungetokea jambo.
"Kumbe! Basi Nashukuru sana. Kwahio naomba
tusogee kurudi ndani"
Fiona alisema kisha tukaanza kusogea taratibu
kurudi ndani huku tukizungumza.
"Jana nilipokuuliza kuwa unakikumbuka mala ya
mbili ulikataa lakini baadaye ukasema
ushanikumbuka, tuliwahi kuonana wapi Mimi na
wewe?"
Fiona aliniuliza.
"Nakumbuka siku za nyuma kabisa, yaani miaka
kama saba hivi ishapita niliwahi kuota ndoto ya
Kutisha halafu akatokea mtu kama wewe hivyo
hivyo akaniokoa, hicho tu ndicho kimenifanya
niseme nakukumbuka"
"Ni kweli, lakini ushagundua kitu kuusu maisha
yako?"
Fiona aliniuliza tena.
"Hapana kwani yakoje?"
Nilimuuliza Fiona.
"Wewe Uliandaliwa toka zamani kuja kuishi huku na
upaswi kabisa kurudi katika mazingira uliyotoka, na
kosa lako ni kwamba ulitoroka kwenye Jumba la
Ufalme na ulipaswa uwe mfalme na wale mabinti
walikuwa ni Malkia wako. Kwa kosa lako ulistahili
kufa tu, lakini huruma yangu tu ndio inakufanya
mpaka sasa unaishi, na unavyoona Mimi ndiye
huwa Mlinzi wa Mwisho kabisa katika eneo hili kwa
yeyote yule anaye fika huku na kujaribu kutafuta
namna ya kuondoka. Lakini hakuna mlango wa
kutokea huku haupo zaidi ya kufa, Lazima ufe
Jumanne lakini nakuhurumia na Mimi ndiye muuaji
wa Mwisho kabisa"
Fiona alisema, hapo ndipo alinitisha zaidi kabisa,
kumwogopa kukazidi kuwa kukubwa moyoni
mwangu.
"Usiniogope Mimi, lakini nakuonya hupaswi kabisa
kutoka hapa, lakini pia kuna koo za watu wengine
huko ambao nao ni wabaya zaidi. Kuna mpaka
ambao unatutenganisha nao, kule ulipokuwa
unaelekea jana ndiko hukohuko. kule ukifika sizani
kama kutakuwa na msamaha zaidi ya kufa"
Fiona alisema tena, maneno yake bado kwangu
yalikuwa mtihani vile vile, kwanza yeye mwenyewe
nilimuogopa, halafu pia ananimbia hakuna eneo
lenye usalama, bado nahitajika kufa lakini kwa
msamaha wake tu ndio maana naendelea kuishi.
Yeye ni nani kwangu nilijikuta nawaza hivyo ikanibidi
nimuulize.
"Fiona wewe ni nani kwangu?"
Nilimuuliza.
"Kwasababu nakupenda na kwasababu toka hawali
ulishawahi kuniota basi ndiyo maana, sio wewe tu
uliiota ndoto hiyo hata Mimi niliiota kuwa kuna Mtu
atakuja nitamuhurumia na huyo ni zawadi kwangu,
nakupenda sana Jumanne"
Fiona alisema, pale Mimi nilishituka sana, kama
Fiona kanipenda halafu nilikuwa simjui asili yake, ni
Jini au Binadamu, halafu bado ni muuaji "si
anaweza kunigeuka hata Mimi siku moja na kuniua"
yalikuwa ni mawazo yangu kichwani mwangu.
Kipindi hicho tulikuwa tumesimama tukiangalina,
Mimi nilikuwa namwangalia kwa Hofu.
"Nitakuonyesha mambo mengi sana Jumanne, we
usijali naamini hata baadaye utazoea utakuwa
unatembea maeneo haya, lakini pia nitakuonyesha
mpaka wetu uko wapi ili usije ukavuka na kwenda
sehemu ya pili Ukauliwa"
Fiona aliendelea kusema.
Nikiwa na mawazo nilikuwa nakubali tu ilimradi
lakini Mimi bado nilitamani hata nipate sehemu ya
kuondokea eneo hilo kwani hata Fiona mwenyewe
sikumwamini tena.
"Tusogee tukae pale ndiyo tuzungumze vizuri"
Fiona alisema. Tulisogeo mahala aliposema kukaa,
tulipofika tulikaa pale tukaendelea na mazungumzo
kama kawaida, kichwani tayari nilikuwa nishaandaa
maswali mengi sana ya kumuuliza Fiona.
"Jumanne naomba sasa uniulize maswali yako yote
nitakujibu halafu baadaye tutaenda kula"
Fiona alisema, kama vile alikuwa kwenye akili
zangu.
"Kwanza naomba unambie kwanini nilifika huku?"
Nilimuuliza. Lakini Bado nilikuwa simwamini yeye
hata kidogo.
"Kwasababu uliitajika kuwa Mfalme katika koo hii,
Mfalme wa uku alishafariki miaka miwili nyuma"
"Sasa Mimi nilipaswa vipi kuwa mfalme wakati
Mimi siyo wa huku"
Nilimuuliza Fiona.
Ni Hadith ndefu sana kuusu maisha yako, kama
ulikuwa ujui ngoja nikusimulie mwanzo mpaka
mwisho.
Kwenu mpo wavulana wawili na wasichana watano,
na wewe ndiye mdogo katika kizazi cha Baba na
Mama yako. Kuzaliwa kwako ni sawa na Bahati
mbaya Labda hata usingezaliwa na Kuzaliwa kwako
kuliambata na maombi maalumu ya mizimu. Kipindi
Mama yako anajifungua Dada yako unayemfuata
kulitokea msiba katika Ukoo wenu, Mke wa Baba
yako mkubwa alifariki na kumwacha Mtoto
mchanga.............
 
SEHEMU YA (13)
WhatsApp 0755577488.
Naomba kushare Tafadhali. Nawaomba ku-share
Tafadhali.
ILIPOISHIA.
Kwenu mpo wavulana wawili na wasichana watano,
na wewe ndiye mdogo katika kizazi cha Baba na
Mama yako. Kuzaliwa kwako ni sawa na Bahati
mbaya Labda hata usingezaliwa na Kuzaliwa kwako
kuliambata na maombi maalumu ya mizimu. Kipindi
Mama yako anajifungua Dada yako unayemfuata
kulitokea msiba katika Ukoo wenu, Mke wa Baba
yako mkubwa alifariki naye akiwa na Mtoto
mchanga kabisa..............
SONGA NAYO,
Kifo cha Mama yako huyo kilisababisha mtoto
aliyemwacha kunyonyweshwa na Mama yako mzazi,
katika mila zenu kwa kawaida mama ambaye
alikuwa amemnyonyesha mtoto Mwingine ambaye
hakumzaa yeye, Mama huyo hakupaswa kuzaa tena
mtoto Mwingine zaidi ya kukifunga kizazi chake,
hizo ni mila na tamaduni ndizo zilikataza.
Kilichofanyika ni nini? Baada ya kuona kuwa Mama
yako ana Mtoto mmoja wa kiume ambaye ni kaka
yako, ndugu zake na Baba yako pamoja na ndugu
zake na Mama yako waliona kuwa sio Busara
mama yako azae Mtoto mmoja wakiume kisha
afunge kizazi wakati uwezo wa kuzaa Bado alikuwa
nao, kwahio baada ya maoni hayo kupitishwa na
kukubaliwa kwa pande zote mbili, wote
walikubaliana kwenda kuomba mizimu kwanza
iwape ruhusa Ndiyo azaliwe mtoto huyo, mchana
waliondoka na kwenda katika mzimu yenu ambayo
imo katika vichaka na mapori yanayorizunguka ziwa
Ngozi, wakaomba msamaha kisha wakaomba
ruhusa kwa ajili ya Mama yako apate mimba ya
Mtoto wa kiume kupitia mizimu. Baada ya maombi
Ishara Fulani ya kushangaza ilitokea katika eneo
hilo, Ishara hiyo ilionesha kuwa Maombi
yamekubaliwa kuwa Mama yako apate mimba ya
Mtoto wa kiume na atakapo zaa mtoto huyo
atakuwa na ulinzi mkubwa wa mizimu kwahio ni
Mali ya mizimu ya Ukoo.
Isingekuwa mizimu Jumanne usingezaliwa, na
mimba yako ilikuwa kwa ajili ya zawadi ya Mtoto wa
kiume kwa mizimu. Wewe usingekuwepo wala
usingefika katika eneo hili, tusema labda
tusengekuwa tunaongea hapa.
Kisa chako cha kufika huku kinakuja ikiwa ni baada
ya kufariki Mfalme wa huku, alikosekana ni nani wa
kumrithi, walitafuta ni nani atasitahili kuwa Mfalme
akakosekana katika jamii ya uku. Mfalme alifariki
bila kuacha mtoto yeyote wakiume au wa kike
ambaye angeongoza Ufalme kama malkia. Baada ya
majadiliano ya muda Mrefu wazo lilikuja kuwa Yupo
ambaye anasitahili kuwa mfalme kutoka katika ukoo
wa Mizimu ya Ziwa Ngozi ni nani huyo Mfalme ni
Jumanne, huyo alizaliwa kutoka katika mizimu na
alizaliwa akiwa chini ya mizimu, labda nikuthibitishie
kuwa toka Mtoto Jumanne hukuwahi kuugua hata
Ugonjwa wowote ule, kama na hilo hakuwahi
kusimuliwa basi ndivyo ilivyo......"
"Ni kweli niliwahi kuambiwa na Mama yangu kuwa
sikuwahi kuugua toka kuzaliwa kwangu, lakini swala
la mizimu niliwahi kusikia lakini sikuwahi kuupata
ukweli wa jambo hilo kama ulivyonieleza wewe"
Nilisema baada ya Fiona kunisimulia, kwakweli
nilistaajabu sana.
"Nazani umeelewa uhalisia wako kwa maana hiyo
hakuna haja ya kuendelea zaidi kwasababu wewe
hupaswi tena kurudi ulikotoka Bali wewe utaishi
huku huku kwasababu umeteuliwa kuwa Mfalme wa
kuongoza koo ya Mababu na mizimu yenu. Bado
nafasi yako ipo na ndiyo maana Hujafa mpaka sasa.
Akikosekana Mwingine wewe utalazimika kuwa
Mfalme tena, wewe Jumanne ulikuwa hauna hata
Chembe ya uwezo wa kufika kwangu, ungekuwa
ishauliwa njiani huko, yaani ni maombi yangu kama
mtu muhimu katika Koo hii ndiyo maana ulifika
kwangu, na hivyo ni kwasababu ya ndoto zetu mbili
kufanana"
Fiona alisema. Kwakweli nilistaajabu sana, Maelezo
yake yalinitisha kwanza, halafu pili yalininyima haki
ya Mimi kurudi katika mazingira ambayo
nimeyazoea. Kwa kisa chake hicho alijikuta
anayafukia baadhi ya maswali yangu mengine, kama
nilifikaje hapo? kwanini iwe Mimi tu asiwe
mwingine?
"Sawa Fiona Kwahio Raulati na Jamila wao
watafanywa nini?"
Ilinibidi nimuulize kuusu wapenzi wangu, maana
waliniuma sana na niliwakumbuka baada ya kuona
uwelekeo wangu ni wakufa tu.
"Usiwaze ukipata nafasi ya kurudi kule basi hawo
watakuwa wake zako kama Malkia, lakini ukikosa
bahati ya kurudi wale watabaki watu wa kawaida
katika Ufalme huu wa ajabu, tena Jumanne ulikuwa
na Bahati ya pekee kuwa na wanawake wawili
wenye kufanana na Mapacha sijui niseme nini ili
nikusifu, na kwa bahati zaidi ulikuwa
ushawabebesha wote wawili mimba, kwahio hata
kama ungefariki wewe, bado watoto wako
wangekuja kulithi Ufalme, umenisikitisha
sana.....Lakini huwenda kuna makusudio makubwa
ndiyo maana umefika kwangu"
Fiona alisema huku akitabasamu. Kwa mazungumzo
yake nilimgundua tu kuwa tayari alikuwa na elemeti
za mapenzi juu yangu ndio maana alisema hayo.
Baada ya kuligundua hilo niliwaza kuwa
akijichanganya tu akazama katika hali ya kutaka
mapenzi na Mimi basi nitatumia udhaifu wake wa
mapenzi ili anisaidie kutoka katika eneo hilo, hilo
ndilo wazo langu ambalo nililiwaza na nikaliamini.
"Jumanne naomba usiniogope kwanzia sasa kwa
hali yeyote utakayo niona nayo hata kama inatisha
kwasababu ndivyo nilivyo, kwahio vumilia tu
kwasababu ndio ishatokea na mpaka hapa nimeisha
amini lazima Mimi na wewe tungakutana tu,
kwakuwa tayari tulikuwa tushaota ndoto ambazo
ziliendana kwa kiasi kikubwa"
Fiona alisema, maneno yake yalikuwa makari lakini
namna ya kuyakwepa nilikuwa sina zaidi ya kuwa
mpole kama maji yaliyotohama.
"Nazani ushanijua kabisa kuwa Mimi sio Binadamu
wa kawaida kama ulivyo wewe, lakini nilazima Mimi
na wewe tuwe wapenzi kwasababu nakupenda
ikimbukwe toka kuzaliwa kwangu sikuwahi kukutana
na mwanamume yeyote hata wa huku, nilipofikisha
miaka kumi na mitano tu nilikabiziwa kazi yangu ya
mpakani kabisa, hakuna ambaye anavuka eneo hili
na kuna mahala au mwisho ambao mtu yeyote
akifika Mimi najua kuwa kuna mtu au kitu ambacho
yanipaswa nikizuie, Mimi nina uwezo wa kupigana
na watu zaidi ya elfu moja. Kwahio ninautofauti
mkubwa na wengine wote halafu pia ninao uwezo
wa kujigeuza zaidi ya sura mia za viumbe tofauti
ambavyo unavijua na usivyo vijua"
Fiona alisema tena, hakika nilikuwa katika mateso
makari sana kipindi nilipokuwa nazungumza na
Mwanamke yule ambaye alikuwa ni mzuuri utazani
malaika wa Mungu ndiye niliyekuwa naye. Hata
kipindi alipokuwa anazungumza nilikuwa
namuogopa mwili mzima ulikuwa unatetemeka kwa
hofu, maana angeweza hata kunigeukia Mimi pale
nisingekuwa na cha kujitetea labda ningezimia.
niliwaza huwenda hata Joka lile kubwa alikuwa ni
yeye labda ndiyo maana liliniangalia tu bila
kunifanya Chochote.
"Jumanne bado unawasiwasi kuusu Mimi?"
Baada ya kunieleza mfumo wake aliniuliza.
"Ha!.....hapana!"
Nilisema kwa kusicratch. "Haya amka mpenzi
wangu twende ndani ukale maana nahisi unanjaa
isiyopimika"
Fiona alisema, muda huo nazani kwa kukadilia
ilikuwa kama mida ya saa tatu za asubuhi kwahio
alikuwa anazungumzia chakula cha Asubuhi(chai)
Niliongozana naye mpaka ndani mwa jumba lake la
Ajabu, Jumba ambalo lilikuwa kubwa, refu halafu
limechakaa hasa. Ndani ya Jumba tulifikia kwenye
meza ya chakula, yani mazingira ya pale yalikuwa
kama kule kule, Mimi nilikuwa nawaza chai na
mkate kweli navyo vilifika kama nilivyowaza.
"Bado na hili utashangaa Jumanne?"
Fiona aliniuliza tena.
"Hapana, nimeisha zoea"
"Haya kula sasa ushibe eti mpenzi wangu"
Fiona alisema. Kitendo cha kuniita Mimi mpenzi
wake nilikuwa sikipendi lakini ningefanya nini wakati
nilikuwa ndani ya mdomo wa mamba au tumbo la
Chatu kwahio nilikuwa sina ujanja wa kukataa zaidi
ya kukubali tu.
"Sasa mbona wewe uli?"
Nami nilipata kumuuliza.
"Mimi vyakula kama hivyo huwa sili hivyo ninyi ndio
mnavila tu"
"Mh!"
"Ndiyo na ndio maana nilikwambia toka hawali
kuwa utakachokiona kwangu usikishangae maana
ninauwezo wa kujigeuza na kuwa kiumbe Mwingine
tofauti ambaye unamjua au usiyemjua. Hivyo
nilikupa tahadhari ili hata ikitokea ujue ni kawaida
yangu, pia itasaidia kuishi kwa kujiamini......
Jumanne Mimi nakupenda sana ndiyo maana
nimekupa tahadhari mapema"
Fiona alisema tena bhana. Ilinibidi nizidi kuwa
mpole kwake, lakini kwakweli Fiona alikuwa mzuri
na kwajinsi alivyokuwa anaongea kwa taratibu, sauti
yake ikiwa inaongezea uzuri wake na utaratibu wa
maneno yake alitazamika kama ni bonge moja la
Mwanamke ambaye Duniani hayupo kabisa kabisa,
na kweli sizani Duniani yupo kwasababu nilipokuwa
Mimi sio Dunia hii ile ni Dunia ambayo haina Jina
na ndio maana hadithi au kisa changu hiki nilikipa
Jina hilo hilo la A place with no name. Kweli ndugu
msomaji wa kisa hiki, sijui kama kinakupendeza au
kinakusikitisha au kukufurahisha lakini huu ndio
ukweli kwamba nimekaa kule miezi kumi lakini
Sikuwahi kulijua jina la sehemu hio kabisa,
nilijitahidi sana kulitafuta kwa kuwaulizia lakini
sikufanikisha kabisa kulijua jina halisi la eneo hilo.
Basi naomba tuendelee na kisa hiki cha kweli
kilichonikuta Mimi.
 
A PLACE WITH NO NAME,_14.
(Sehemu isiyo na Jina)
NA HEMED MAYUGU,
Tell; 0755577488. WhatsApp.
Share share tafadhali, Usiashau Ku-share.
ILIPOISHIA.
Kweli ndugu msomaji wa kisa hiki, sijui kama
kinakupendeza au kinakusikitisha au kukufurahisha
lakini huu ndio ukweli kwamba nimekaa kule miezi
kumi lakini Sikuwahi kulijua jina la sehemu hio
kabisa, nilijitahidi sana kulitafuta kwa kuwaulizia
lakini sikufanikisha kabisa kulijua jina halisi la eneo
hilo.
Basi naomba tuendelee na kisa hiki cha kweli
kilichonikuta Mimi.
SONGA NAYO.
Niliendelea kunywa chai hivyo kwa kujing'ang'aniza
kwasababu nilikuwa Nina hofu sana.
"Jumanne naamini bado unahofu kabisa,.....usi
niogope bhna Mimi nitakulinda na nitaishi na wewe
mpaka watakapo kuhitaji lakini kabisa sitokubali ufe
endapo akipatika Mtu mwingine wa kuwa Mfalme,
nitakulinda mpaka labda Mimi ndio nife"
Fiona alizidi kujifungisha na kujiapisha kwangu
ambaye Mimi nilikuwa sina hata chambe ya moyo
wa mapenzi kwake japo kuwa nilitamani ajiingize
kwangu ilimradi nimtumie ili anisaidie kutoka
sehemu ile ya kutisha.
"Sawa Fiona lakini lakini naomba nikuulize tena"
Nilisema.
"Uliza tu Jumanne, uliza chochote nitakujibu sahivi"
Fiona alisema, ilikuwa tayari kanipa Uhuru wa
kuzungumza chochote ambacho ningependa
kumuuliza.
"Kwahio hata Raulati na Jamila walikuwa ni
Binadamu kam nilivyo Mimi?"
Niliuliza hivyo makusudio ili kujua maana hata wale
wasichana japo kuwa nilithubutu kufanya nao
mapenzi lakini bado nilikuwa sina hakika sana kama
walikuwa Binadamu japo kuwa walinisimulia kisa
cha maisha yao.
"Ni kweli Jumanne wale ni Binadamu kama wewe
tu, na kuzaliwa kwao kuliendana na wewe kwa kiasi
kikubwa. Mama yao aliwahi kuolewa na wanaume
watatu na wote akadumu nao miaka mitatu lakini
wote hakufanikiwa kupata Mtoto, lakini baada ya
kukutana na Baba yao walithubutu kwenda katika
matambiko kwa ajili ya mtoto, waliitambikia mizimu
ya kwao na mwanaume ambaye pia chimbuko lake
alitokea katika koo hii kwahio yule alikuwa ni ndugu
yenu moja kwa moja hawa mabinti wametoka ndani
ya ukoo wenu, naamini kwasababu Mama yao
alikuwa na Shida ya watoto Ndiyo maana walizaliwa
wawili"
"Kumbe!...........basi sawa"
Nilisema baada ya Fiona kunisimulia kisa cha
wapenzi wangu, moyo uliniuma sana kwanini
niliwaacha Mabinti wazuri wale waliokuwa
wanapendeza, wacheshi, wenye mapenzi ya dhati
kwangu, walikuwa wamejitolea kwa hali yoyote ile
kwa ajili yangu.
"Kwanini sikuwamini Jamila na Raulati.........Mungu
wangu sijui sasa wako katika hali ipi"
Nilijikuta nasema hivyo mbele ya Fiona.
"Jumanne usiwawaze nitakusaidia utawarudia
wapenzi wako, wao sasa hivi wapo Japo wanaumia
kwanini uliwaacha lakini haina budu, wameambiwa
wavumilie na wameahidiwa wewe kurudishwa ndani
ya Jumba lile. Hata hivyo Jumanne ulifanya makosa
sana kuondoka mule, kwanza Wenzako walikuwa
washajitoa kuwa hawatarudi tena kwenye maisha ya
Duniani kwasababu mlipokuwa kila aina ya Furaha
mlikuwa nayo"
Fiona alisema, maneno yake yalikuwa ya kweli na
yaliniuma sana, ukiongezea kuwa uwezekano wa
Mimi kufa upo hapo ndipo nilichanganyikiwa zaidi
na zaidi. Nilikuwa na Maswali mengi bado ya
kuuliza kuusu kila kitu ambacho nilikutana nacho
kabla ya kufika kwenye Jumba lile, Visa vya ajabu
baada ya kufika ndani ya Jumba lile na hata kuusu
vyakula na mavazi pia vilitoka wapi, yote hayo
yalikuwa ni maswali nimeyaandaa kumuuliza Fiona
kwasababu alionekana kunijali ingawa nilikuwa
namuhofia. Kwa wakati huo nilishia hapo na
maswali yangu niliyatunza, nikasema nisubili mpaka
siku ambayo akijiingiza kwenye mtego wa mapenzi
nitamuuliza vizuri kwani muda huo akili zangu
zilikuwa zishavurugwa.
Nilipomaliza kunywa chai Fiona alinishika mkono
tukatoka mpaka sting room yake, kweli mazingira
ya Jumba lile yalikuwa yakizamani tu, hata viti vya
kukalia vilikuwa nimechoka.
"Jumanne unashangaa mazingira haya zoea tu, hapa
si kama kule lakini nikivitaka vinakuja, ila sitaki na
mazingira yangu haya hapa hupaswi kuyajua yote
kwasababu utaishi kwa kuogopa wakati wote"
Fiona alisema. Maisha Yale Mimi yalinitisha sana,
basi kwakuwa nilikuwa nishakamatika ilinilazimu
kuyakubali. Tukiwa tumekaa na tunaangaliana Fiona
alisimama na kunifuata nilipokuwa nimekaa
akanishika kichwani kisha akachuchumaa huku
macho yake yameishia kwangu, kwa mtazamo wake
wa kuangalia ilionesha bayana kuwa alikuwa
anahitaji penzi langu.
"Jumanne kwanza niwie radhi kwa hiki lakini ni
kwasababu nakupenda sana"
Fiona alisema kwa sauti ya madeko, Aisee ingawa
akina Jamila na Raulati niliwaaminia kwa madeko
lakini kwa Fiona ilikuwa nyingine kabisa, sauti ile
ilikuwa kama inanigonga kwenye moyo wangu,
yaani ilikuwa kama inaniimbia wimbo mzuuri wa
mapenzi.
"Kama kiumbe huyu hajui Chochote kuusu mapenzi
mbona anamadeko ya ajabu kiasi hiki, na hii ni sauti
tu je akinipa si ndio nitakufa kabisa na kulisahau
lengo langu la kurudi nilikotoka"
Nilijeseme mwenyewe kimoyomoyo.
"Jumanne naomba unifundishe namna ya kufanya
mapenzi?"
Fiona alisema, yani kama vile switch alikuwa
anaiswtch on taa inawaka halafu anaiswitch off taa
inazima na ndivyo ilivyokuwa sauti ya Fiona kwa
upande wangu, Sauti yake ile ilikuwa ya ajabu kweli
kweli, yaani hata nyoka pangoni alikuwa anaanza
kufurukuta kutoka ili aingie shimoni.
Sikumjibu nilibaki kimya tu.
"Jumanne utanifundisha namna ya kufanya
mapenzi?"
Mtoto alizungumza tena.
Haki ya mungu niliisi kama vile napagawa kabisa
sijielewi, nilijikuta nasema.
"Ndiyo nitakufundisha halafu kidume tayari nilikuwa
nishasimama, Nyoka pangoni kule kakiinua kichwa
mpaka pango lenyewe lilikuwa kidogo libomoke,
Fiona alishituka sana, akaniuliza.
"Na Hicho ni nini Jumanne"
Badala ya kumjibu Mimi nilimtoa nyoka pangoni
kisha nikamwabia.
"Wewe mwenyewe umenambia kuwa unaona kila kiti
hata kilichojificha"
Nilisema. Yani kuzungumza kwa Fiona
kulinipagawisha Mimi mpaka mwisho wa kupagawa,
yaani kama ni kuzimia ilibakia kidogo, kwakweli
ilikuwa imesalia kidogo nimbake Fiona nguvu
iliyokuwa inanisukuma ilikuwa kama nimemeza
mavidonge ya kuongeza nguvu za kiume.
"Kumbe ndio hivyo Jumanne Mh ni hatari sasa"
Fiona alisema tena. Mimi kwakuona kama
ananichelewesha nilimshika sikujua hata nguo yake
niliichomoka je mwilini mwake, kama sikosei
nilishitukia nguo haipo mwilini mwake baada ya
kuishika.
Mtoto alikuwa amesimama naye ameiva kweli kweli
halafu akiniangalia kwa macho ya mahaba
yaliyokuwa yamejaa Huruma ya mahaba. Yaani
kalegea lege lege kama chapati ambayo
ijakaangwa.
Yani niligundua tu huyu haitaji maandalizi Bali
nikumpa taratibu tu kwasababu yeye mwenyewe
alikuwa kaisha iva nilimulaza pale pale kwenye viti
vyake nikampa kitu roho inapenda, kwakuwa
nilikuwa najua kabisa hakuwahi kujihusha yaani kitu
kibichi kabisa nilikuwa naenda mwendo wa Pole
pole kwa kiitarunya wanasema Despacito.
"Taratibu Jumanne unaniumiza"
Fiona alianza kulalamika maumivu, nilijihakikishia
sifa kwa Fiona. Nilimtungua kisha nikamla taratibu
Mwisho nikamwacha.
"Tayari nishakufundisha jinsi wanavyofanya mapenzi"
Nilisema baada ya kumaliza mchezo wa kikubwa.
"Asante Jumanne, Nashukuru sana ingawa kuna
maumivu ila Raha sana"
Fiona alisema.
"Usijali Fiona hio ni mala ya kwanza ndio maana
ukizoea hakika hutopata shida kabisa yaani kuna
Raha yake acha tu"
Nilisema kwa mbwembwe kumbe sikujua kua
nilikuwa najichimbia shimo la Giza kwa Fiona.
"Kweli"
"Ndiyo"
Nilimjibu kisha tukafuta damu damu zile halafu
tukaenda kuoga.
Baada ya kutoka kuoga Fiona alionekana mwenye
Uzuni sana. Nakumbuka aliniambia hivi.
"Jumanne ukiisi njaa utafanya kama ulivyozoea!"
Alivyo sema hivyo aliondoka na kuelekea sehemu
nyingine kabisa ya Jumba hilo. Siku nzima mpaka
usiku sikumuona tena Fiona, lakini nilistaajabu taa
inawaka ndani ya Jumba lile taa ilikuwa kama
kidude alichokuwa ameshikilia usiku wa Jana
tuliokuwa tunatembea msituni.
Nilikaa kwa mawazo sana pale sehemu ya kukaa
chakula cha usiku sikukila kabisa, nilikuwa na Hofu
kwanini Fiona aliondoka akionekana mwenye Uzuni
ndani ya Jumba lile alielekea wapi? Niliwaza sana.
"Au ndio anaandaa maandalizi ya Kunila Mimi"
Niliwaza peke yangu Usiku nikiwa nimekaa, sikujua
hata usingizi ulinipitia vipi Bali nilishituka usiku
baada ya kusikia sauti za ajabu ajabu ndani ya
Jumba lile Sauti zilikuwa zinatisha sikuwahi kusikia
sauti za ajabu kiasi kile kabisa. Sauti hizo
ziliniogopesha sana. Nikaanza kujivuta kuelekea
sehemu ambayo niliisi labda nitajificha nisionekane.
Kwakuwa mazingira ya Jumba Yale nilikuwa siyajui
niliona sehemu ambayo mwanga ulikuwa upenyezi
nikajificha hapo, kelele zile zilizidi kuwa nyingi sana,
halafu ghafra zikakata. Mimi niliendelea kujificha ili
nione kama kuna kitu ambacho kingetokea.
Mala nikiwa pale niliona kivuli kikubwa cha Mtu na
kama alikuwa Mtu basi ni yale Magiant(Mtu
mkubwa )
 
ILIPOISHIA.
1Nikaanza kujivuta kuelekea sehemu ambayo niliisi
labda nitajificha nisionekane. Kwakuwa mazingira ya
Jumba lile nilikuwa siyajui niliona sehemu ambayo
mwanga ulikuwa upenyezi nikajificha hapo, kelele
zile zilizidi kuwa nyingi sana, halafu ghafra zikakata.
Mimi niliendelea kujificha ili nione kama kuna kitu
ambacho kingetokea.
Mala nikiwa pale niliona kivuli kikubwa cha Mtu na
kama alikuwa Mtu basi ni yale Magiant(Mtu
mkubwa )
SONGA NAYO.
Kivuli kile kilikuwa kinasogea kutoka mafichoni.
Nilichoka nilipokuta ni Fiona anatembea kwa uchovu
sana, alionekana hana nguvu kabisa. Nilimuonea
huruma nikatoka pale nilipokuwa nimejificha na
kwenda kumsaidia.
"Fiona umekuwa je?"
Nilimuuliza baada ya kumfikia na kumshika.
Baada ya kusema Hivyo Fiona alinitazama Macho
yake jinsi yalivyokuwa yaliniogopesha nikajikuta
namwachia na kusogea pembeni huku Nikitetemeka.
Nilijua ule ndio mwisho wangu, macho yake
yalikuwa yamebadilika yamekuwa ya langi nyeusi
kama ya wale Nyoka weusi.
"Jumanne naomba usiniogope nisaidie"
Fiona alisema. Pale niligundua kuwa ndio Yale
aliyoniambia kuwa akibadilika kwa hali yoyote
nisimuogope kwasababu ndivyo alivyo. Nilipojaribu
kumchunguza vizuri mpaka miguuni, mikono
haikuwa ya Binadamu, miguu ilikuwa kama ya
ndege na kucha kabisa.
Nilijipa Ujasiri tu nikamshika kisha akanionesha
wapi nimpeleke. Nilimuongoza na kumpeleka
kwenye chumba alichonionesha. Kilikuwa ni
Chumba kile kile ambacho nililala Mimi usiku wa
Jana.
Nilipomfikisha nilimuomba nimuache.
"Usiondoke Jumanne tulale wote hapa hapa hakuna
tena sehemu nyingine ya kulala zaidi ya hapa"
Fiona alisema. Kwa Jinsi alivyokuwa Duh! Kweli
ilikuwa ishu nzito kwangu, kulala na kiumbe cha
ajabu kile, nilivumilia sana, kwa Maelezo yake na
ukiongezea jinsi nilivyokuwa namnyari sikubisha
nami nilijitupia pale pale kitandani.
"Jumanne mpenzi wangu Nakupenda sana, haya
yote yametokea kwasababu yako, nimepokea
mabadiliko ambayo yamenisisimua mpaka basi,
Penzi lako limenisisimua sana kwakuwa mwili
wangu hujawahi kufanya kitendo hiki ndio maana
nimekuwa hivi, kwahio usijali nitazoea tu mwisho
tutafurahi wote kwa pamoja"
Fiona alisema tena. Hapo nilimwelewa nikajua
kabisa kumbe hata Yale makelele yalikuwa ya
kwake. Mmmh! Kwa hali ile hakika kama ni
maajabu ya ulimwenguni omba usimuliwe kama hivi
lakini yasikukute Fiona alikuwa ni kiumbe sijui
niseme Viumbe vya ajabu! vya ajabu! vya ajabu
nilivumilia sana kumstahimili kwani ilikuwa inafikia
kipindi mpaka natamani ni Bora nife tu kuliko kuishi
na kiumbe wa ajabu kiasi kile.
"Usijali Fiona, kawaida tu"
Nilimjibu na Mimi ili kumfanya naye ajisikie furaha,
lakini Mimi moyoni nilikuwa siko naye kabisa.
"Nilikuwa sijui mapenzi yanavyofanywa japokuwa
nilikuwa napata hamu ya kufanya kitendo hicho,
halafu pia nilikuwa nasikia tu mapenzi kwahio
nilikuwa nahamu sana ya kufanya mapenzi. Kuna
Raha sana kufanya mapenzi, kesho tutafanya tena
Jumanne!"
Fiona alisema tena Usiku huo kwa sauti ya madeko,
sauti yake ile Mimi ilikuwa inaniripua hasa maana
ilikuwa ya aina yake. Yaani kama vile ilikuwa kama
inaniongezea nguvu za kufanya kile kitendo.
"Usijali tutafanya tena kesho ndio itakuwa vizuri
utosikia maumivu yaani ni Raha tu"
Nilimjibu Fiona. Si kwamba ndani ya chumba kile
kulikuwa Giza hapana, Bali taa ilikuwemo, kwahio
tulikuwa tunaongea kwenye mwanga na muda huo
Fiona alikuwa kaisha badilika na kuwa katika Sura
ya Binadamu wa kawaida. Yani alipokuwa
anabadilika kuwa Binadamu alikuwa mzuuri kweli
kweli, hapo ndipo nilikuwa napata uthibitisho kuwa
kumbe Majini wanakuwa na Sura nzuri kwa ajili ya
kuficha asiri yao lakini yenyewe ni mabaya hatari.
Tuliongea mengi usiku huo, hata hivyo masaa
yalikuwa yashaaenda sana, ilikuwa kama mida ya
saa tisa ndio tulilala. Nililala kwa shida sana kwani
sauti ya madeko ya Fiona aliniumiza sana.
Asubuhi kulipokucha, Mimi na Fiona tulitoka
tukaenda kuoga tena kama mtu na Mpenzi wake,
huko huko kwenye maji mambo yaliivia huko,
mchezo wa kikubwa ulichezewa huko siku hio.
Hakika sikuwahi kupata kufanya mapenzi na kiumbe
mwenye joto la mahaba kama Fiona, kwakweli sijui
niusifie vipi mwili wake lakini ndio hivyo nilikuwa
nafanya mapenzi na viumbe wa tofauti ndani ya
mwili mmoja. Tulifanya mapenzi karibu masaa
matatu, bila kuchoka cha ajabu sikupata hata
kupumzika hata mala moja kila nilipokuwa nafunga
bao, labda kwasababu ya Joto la mwili wake
pamoja na sauti yake iliyokuwa inanibusti katika
kulifanya tendo lile la pekee katika Raha za
Mwanadamu. Siku hii ndio Fiona aliifurahia kuliko
siku zote katika maisha yake alijiapiza sana
kwangu.
"Jumanne mpenzi wangu, hakika umenigusa hasa
katika moyo wangu, utanifanya dhaifu mahala
popote kwa ajili yako. Sikuwahi kupata Raha kama
hii katika Maisha yangu, labda ndio maana
walinificha huku. Hakika wengine wanafaidi sana.
Jumanne usiniache mpenzi wangu, usiniache kweli
hata Mimi sizani kama nitakuruhusu kuniacha ni
bora nife! nife lakini nisikuache wewe"
Fiona alijiapiza kiapo kizito sana kwangu, kiapo
ambacho kilinikumbusha wapenzi wangu
niliowaacha ndani ya Jumba la ufahari Jumba
lililokuwa na Furaha tele. Kwa maneno yake Fiona
alinitesa sana kwasababu Mimi sikumpenda kiasi
hicho japokuwa sikuwahi kupata radha ya mapenzi
na yenye kusisimua kama penzi la Fiona, ila sasa
alikuwa si kiumbe wa kawaida alikuwa ni Binadamu
sijui Jini aliyekuwa na uwezo wa kugeuka geuka na
kuwa kiumbe mwingine kabisa. Yaani kwa
kurahisisha alikuwa hana sifa ya upekee ya kiumbe
maalumu Bali alikuwa ajulikani amegemea wapi,
ingawa kiasi kikubwa alionekana katika muonekano
wa kibinadamu lakini alikuwa ali kabisa vyakula
ambavyo Mimi nilikuwa navila, kwa bahati mbaya
sikupata hata kujua alikuwa anakula nini, huwenda
alikuwa ananiacha usiku kitandani ndio anaenda
kutafuta chakula chake. Mchana nyingi nilishinda
naye pale pale kwenye Jumba lake isipokuwa
alipokuwa anahisi hatari ndio aliniacha na kwenda
kukabiliana nayo.
Niliishi na Fiona kwa Shida sana kwa upande
wangu, kwani kila baada ya siku mbili aliitaji penzi
langu, nilimpa tu ili afurahie na nashukuru hata Mimi
mwenyewe nguvu zilikuwa aziniishii kwani nilikuwa
nakula chakula vya kuongeza nguvu za mambo
hayo. Kuusu swala la Chakula kwangu ilikuwa sio
Shida kabisa, yaani ilikuwa nikuagiza chakula cha
aina yoyote nacho kilikuja, nini nilikihitaji kisije,
kilikuwa hakipo ambacho nilikikosa. Kuusu hili
nilimuuliza Fiona akanambia kuwa kila ambacho
Binadamu anakiandaa katika maisha yake huwa
kinachukuliwa kinaletwa katika mazingira Yale,
vyakula vya mahotelini vilichukulia mala nyingine,
vingine viliandaliwa kule kule ukiwa na njaa ukiomba
vinakuja kwa haraka sana kama mazingira Yale vipo,
lakini vitacheleweshwa kidogo kama kule havipo
vimefuatwa katika mazingira ya Dunia yetu hii.
Yeye ndiye alikuwa anajua kuwa kimechelewa au
Raha lakini Mimi sikuwahi kuchunguza kama
kilikuwa kinachelewa au hapana, kwasababu
nilikuwa naona kama vile ni sawa. Nilimuuliza
mengi sana mpaka kuusu yule mzee aliyekuja ndani
ya lile Jumba na Mke wake alinijibu kuwa huyo
ndiye mwenye mamlaka baada ya mfalme kufariki,
na kuusu wale watu wakubwa Kama Magiant
alinambia ndio asilimia kubwa ya watu wa uko watu
wa Uko mala nyingi ni watu wa zamani zamani.
Yaani Mizimu! Mizimu ya mababu ndio inaishi
huko.
Nilipomuuliza kuusu kwenda huko kwenye mji wa
kifalme nikapaone, alinambia haiwezekani kabisa
mimi kufika huko kwasababu sipaswi kujua nini
kilichopo huko kama sijawa Raia wa kule rasimi.
Nilimuuliza maswali mengi sana yakiwemo kuusu
watu niliwaona kwenye ndoto baada ya kupotea pale
ziwa Ngozi. Kuusu hawo alinambia kuwa ilikuwa ni
njia ya kuondoka na zile zilikuwa ni mizimu ya
mababu zangu ambao walikuwa wakinipokea. kuusu
hilo sikutaka kuuliza sana kwasababu nilikuwa
nishafika huko tayari kwahio sikuwa na haja ya
kupeleleza sana.
Siku zilizidi kukatika. Nakumbuka siku moja Fiona
alinichukua tukaongozana naye ili kwenda kuiona
mwisho wa mipaka ya eneo lao ambalo yeye
aliishia katika kudumisha ulinzi. Tulifika huko
mpakani tunakaa huku tukipiga story. Mazungumzo
mengi ya Fiona yalikuwa ni Viapo vya mapenzi
yangu tu kwake, mwanamke yule alikuwa hana wazo
kubwa zaidi ya kuliwaza penzi langu tu.
"Sasa Fiona wewe kama unanipenda kiasi hiki,
ikitokea Mimi nimechaguliwa tena kuwa mfalme
itakuwaje?"
Nilimuuliza swali hilo.
"Jumanne kwakweli Mimi nitakufa na kama
wanataka nipaache huku basi siku moja waje
wazungumzie habari za kukuacha wewe, Tutakosana
nao. Mpaka sasa wanajua Mimi na wewe tuko
pamoja lakini hawajui kama sisi ni wapenzi, yaani
hawajui kabisa kuwa nimeisha Fanya mapenzi na
wewe. Na wakijua sijui itakuwaje, wananiamini sana
Jumanne yaani mpaka hapa wanajua Mimi siwezi
kufanya mapenzi kabisa kwasasa mpaka watakapo
niruhusu baadaye huko na muda huo atabadilishwa
mtu mwingine kwasababu wanajua kabisa mapenzi
yanasababisha udhaifu kwetu. Huwa ni vigumu sana
sisi kujua kuusu mapenzi, na ndio maana
nilikwambia kuwa huwa nasikia tu kuusu mapenzi,
lakini nilikuwa sijui yanafanywaje ila sasa mihemuko
ya mwili nilikuwa naipata nikawa nazania ni
mabadiliko ya kimwili tu, hata damu zile zanazotoka
nilielekezwa tu namna ya kupambana nazo lakini
sikuambiwa ni kwasababu gani. Huwa napata shida
sana damu zile zilipokuwa zinakaribia kunitoka siku
nne au tatu kabla, mihemuko inakuwa mingi sana"
 
ILIPOISHIA,
Huwa ni vigumu sana sisi kujua kuusu mapenzi, na
ndio maana nilikwambia kuwa huwa nasikia tu
kuusu mapenzi, lakini nilikuwa sijui yanafanywaje ila
sasa mihemuko ya mwili nilikuwa naipata nikawa
nazania ni mabadiliko ya kimwili tu, hata damu zile
zanazotoka nilielekezwa tu namna ya kupambana
nazo lakini sikuambiwa ni kwasababu gani. Huwa
napata shida sana damu zile zilipokuwa zinakaribia
kunitoka siku nne au tatu kabla, mihemuko inakuwa
mingi sana"
SONGA NAYO.
Fiona alisema.
Ni kweli Fiona na usijali kwahilo, ila naomba
uwelewe kuwa; kuna wakati ambao wewe
mwenyewe hutakaraika na kuyachukia mapenzi
kabisa wala hutoona raha yoyote kwenye mapenzi"
Nilisema, lengo langu ili kumpunguza matumaini
yake ya kuwa na Mimi.
"Jumanne unanidanganya, haiwezekani kabisa uweze
kuichukia ladha ya mapenzi labda kuachana lakini
umtafute mwingine wala sio kuichukia na kuisahau
ladha ya mapenzi, ladha nzuri yenye Raha na
msisimko wa mwili kuliko vingine vyote"
Fiona alisema, tena alikuwa anaongea kwa msisitizo
kweli kweli utafikiri alikuwa anayajua mapenzi toka
zamani.
Bado tukiwa pale mala Fiona aliisi kama kuna kundi
la watu wanakuja katika maeneo hayo, Mwanamke
yule alisimama muda huo huo alibadilika akawa
mrefu mpaka usawa wa kimo cha miti mirefu kabisa
katika msitu ule. We niliogopa nikataka kukimbia
akanikamata kwa mkono wake, niliishia ndani ya
kiganja chake, yaani umbo zima lilibadilika likawa
kubwa, kwa Jinsi nilivyokuwa kwenye kiganja cha
Mwanamke yule mfano wake ni sawa na ushike
Chapati iliyokunjwa tayari kwa kuliwa. Nilikuwa
kama sisiminzi tu kwa yule mwanamke.
"Usipige kelele kuna watu wanakuja"
Fiona alinambia, sauti yake ilikuwa ya kawaida tu.
Watu aliokuwa anawasema mimi sikufanikiwa
kuwaona kwasababu nilikuwa chini kabisa hata
akuniinua kuona, basi ilinibidi nipoe nisikilize ni nini
kitatokea pale. Baada ya kuona na kujiridhisha
aliniachia mimi harafu akalijirudi katika umbo
ambalo nililipenda.
"Jumanne mpenz wangu bado hujanizoea tu,
usinigope bhna, Mimi siwezi kukudhuru wewe hata
siku moja, nikifanya ubaya kwako kwanza utachukia,
hutonipa penzi lako ambalo Mimi nalipenda au hata
nikisema nikuue bado nitaishi kwa mateso ambayo
yataperekea Mimi mwenyewe kufa. Hakika wewe ni
sawa na Moyo wangu, wewe ni sawa na hewa
ambayo naipumua hapa, harufu yako iko kwenye
mwili wangu imegandana. kukuacha wewe kwakweli
Kiujumla siwezi hata kwa nyundo labda waniue
kwanza"
Fiona alisema.
Maneno ya mwanamke yule yalikuwa yananipa
kuwaza sana, hata namna ya kuanza kumuomba
anisaidie kutoka mahala kule nilishindwa, ujasiri wa
kumuomba ulikosekana. Ningeanzia wapi kwanza na
hata kama ningesema wala asingekubali kabisa.
Kilichokuwa kimesalia sasa moyoni mwangu ni
kuomba nichaguliwe kurudi katika Jumba lile
ambalo nilikuwa siku kadhaa nyuma labda
ingenisaidia nakuachana naye.
"Haya nimekuelewa Fiona Mpenzi wangu. Lakini vipi
kuusu hawo watu uliokuwa unawasema wameishia
wapi?"
Nilimuuliza.
"Bado wapo mbali inaonekana wanamapanga bila
shaka ni watu wa Vita"
Fiona alisema.
"Ni wengi sana?"
"Hapana wala sio wengi sana, ni kama miambili
hivi, maana niwachache sana"
Fiona alisema kwa kujiamini.
Bado tukiwa hatuna hili wala lile alizuka kiumbe
huyo.
"Mungu wangu!"
Nilijisemea huku nikiwa nimesimama na Fiona.
"Usiwaze Jumanne wewe tulia Mimi nikuoneshe
Jinsi ambavyo huwa naifanya kazi yangu"
Mwanamke alinambia kisha akakimbilia nyuma ya
Mti na kuniacha Mimi nikionekana mbele ya macho
ya kiumbe kile cha ajabu, chenye kutisha halafu
kikubwa sana. Mimi nilizani Fiona kaenda kujificha
ili asionekane kwani nilipopiga macho kumwangalia
alipokimbilia sikuomuona tena, wasiwasi
uliongezeka nikatoka eneo lile mbio kuitafuta
sehemu ambayo ingeulinda usalama wangu,
nakumbuka sehemu ambayo lilikuwa Jengo la Fiona
ilikuwa ni mbali sana kutoka pale Mpakani
tulipokuwa, kwa mwendo wangu Fiona alinambia ni
masaa kama saba ndio nafika lakini kwa uwezo
wake ni sekunde kwahio kule nisingeweza kwenda.
Nilijificha maeneo Yale Yale ili pia nishuudie nini
ambacho kingeendelea. Ghafla lile likiumbe
lilianguka chini, tayari kichwa alikuwa hana. Wakati
huo huo nikamuona Fiona kashikilia Jambio mbili
mikononi mwake zote zikiwa na damu, kumbe yeye
ndiye aliyeifanya kazi ya kulilarua lile likiumbe
ambalo sikuwahi kuliona.
"Jumanne!"
Fiona aliniita baada ya kumaliza kuifanya kazi yake,
nilijitokeza mbele ya macho yake, yeye
akanisogelea.
"Naomba nikurudishe kwanza ndani maana hapa ni
hatari halafu Mimi nitarudi kuwashughurikia hawa"
Fiona alinambia, kwa Jinsi nilivyokuwa ninaogopa
nilikubali moja kwa moja lakini hata kabla hajafanya
lolote sijui ni nini ambacho kilimkuta Fiona
nilishitukia anaanguka chini. Nilipotupa macho
yangu mbele nilikutana na Mwanamke mwingine
ambaye kimtazamo alikuwa kama Fiona.
Mwanamke yule alikuwa ameshikilia upinde halafu
hata mishale hakuwa nayo. Lakini pia sikuona
mshale wowote ambao ulikuwa kwenye mwili wa
Fiona.
Niliinama kumsaidia Fiona ambaye alikuwa chini
akiangaika.
"Kimbia Jumanne, kimbia ujisifiche usije
ukadhurika"
Fiona alisema, ilikuwa kama ndio kauli au neno la
mwisho kutoka kwake, nilishangaa mtu anayeyuka
na kuniacha Mimi mwenyewe. Nilisimama kwa
majonzi kwasababu sikuwa na msaada huku
nikiamini ndio wakati wangu wa kufa, niliamini hivyo
kwasababu Fiona aliwahi kunambia kuwa kazi yake
huwa ni kuuwa, sasa kumuona Mwanamke
mwingine kama yeye hapo fikira ziliniepereka mbali,
nikafikiri washajua kuwa Fiona kashindwa kuniua,
kwahio walimtuma yule Mwanamke mwingine kuja
kutuua, ndio maana alimuua Fiona kwanza halafu
animalizie na Mimi. Macho yangu yaliishia kwa yule
mwanamke aliyekuwa mbele yangu, hata yeye
alibaki kuniangalia tu, tulikaziana macho pale kama
dakika moja kisha akageuka na kurudi zake.
Nilibaki pale peke yangu nimesimama nikiwaza
sana, nilijiuliza maswali mengi kwanini mwanamke
yule aliniacha bila kuniua. Lakini pia hata pa
kwenda nilikuwa sipaelewi kabisa. Nilijipa moyo wa
Ujasiri mwanaume nikaufuata uwelekeo wa yule
Mwanamke aliyekuwa anafanana na Fiona nikiamini
huko huwenda kukaweko na msaada. Kwanza
kwanini aliniacha kama wao ni wauaji lazima
kulikuwa na kitu ambacho alikifikiria juu yangu.
Hicho nilikifikiria nacho kikaniongezea ujasiri wa
kumfuata mwanamke yule. Nilianzisha safari ya
kumfuata kule Alipokuwa anaelekea bado alikuwa
anaonekana kabisa kwenye upeo wa macho yangu
kwa mbaali japo kuwa kulikuwa ni msituni.
Mwanamke yule aliuvuka mpaka.........mpaka
ambao Fiona alinionesha hawali kuwa ni sehemu
ambayo sipaswi kwenda ni kwa maadui zao, ni
upande ambao hawana hata Chembe ya huruma
ukifika maeneo hayo lazima ni kufa tu basi.
Nilisimama baada ya kufikiria hayo.
"Lakini mbona huyu Mwanamke yupo kama Fiona
na anafanana na Fiona kabisa, inamaana hizi
sehemu kila upande wake una mtu wa kufanana na
Fiona ambaye analinda mipakani. Lakini hapana
ingekuwa kweli wasingekuwa maadui lazima kuna
kitu hapa, huwenda Fiona alinidanganya"
Niliwaza wazo ambalo nililiamini.
"Potelea mbali kama nikufa poa na kama ingekuwa
kufa mwanamke yule angeniua na Mimi baada ya
kumuua Fiona"
Niliwaza tena kisha nikaiendeleza safari ya kumfuata
yule Mwanamke huko huko upande wa pili. Lakini
bado nilikuwa na wasiwasi kwanini Fiona kauliwa
kama ni watu wamoja. Huwenda kweli ni maadui
lakini wazo lililokuwa linanilinda Mimi ni kwanini
sikuuliwa pamoja ma Fiona, wakati huo niliamini
kabisa Fiona alikuwa amepotezwa kabisa hawezi
kurudi katika Uhai wake. Nilizidi kusonga mpaka
nikafika mpakani ambapo Fiona alinionesha, pale
mpakani kulikuwa na miti mitatu mikubwa
imepangana, ile miti ndio ilichukuliwa kama
milango ya kuvuka upande wa pili bila kupita
katikati ya miti ile ulikuwa uvuki kwenda kokote Bali
utabaki wakuzurula katika sehemu hiyo hiyo, hayo
yote Fiona alinieleza baada ya kunionesha Jinsi
mpaka ulivyo tenganishwa. Nilipofika pale
nilisimama nikafikiria niende huko au hapana.
"Lakini hata nikirudi kule Fiona kaisha fariki kwahio
nikirudi kule sitopata msaada wowote" niliwaza
nikiwa pale mpakani, kumbukumbu ya maisha ya
ndani ya Jumba la mala ya kwanza kwa wapenzi
wangu Raulati na Jamila ikajirudia kichwani
mwangu, nikakumbuka Jinsi walivyokuwa
wananiomba nisiwaache niendelee kukaa nao.
Kilichoniuma zaidi ni kwamba niliwaacha wote
wakiwa wajawazito, wamebeba mimba za watoto
wangu halafu kumbe hawakuwa Mashetani kama
nilivyokuwa nawazania walikuwa Binadamu kama
Mimi.
"Daah! Basi tu maisha yangu yangekuwa raha
msatarehe sana lakini ona ninavyoangaika na nisiko
kujua"
Nilijiseme mwenyewe kisha nikaegemea mti mmoja
katika ile miti ya mpakani. Nikiwa nimeuwegemea
usingizi ulinipitia pale kwenye mti. Ndani ya ule
usingizi niliota ndoto ambayo nilikuwa naifikilia,
ndoto ya wapenzi wangu wakinilalamikia, wakinililia
kwanini niliyachukua maamuzi ya kuondoka na
kuwaacha. Ndoto hiyo ilikuwa ndefu sana,
ilihusanisha mambo mengi, kwani katika hiyo ndoto
niliona niko na Fiona halafu kuna mgogoro mkubwa
katika ule ufalme Chanzo ikiwa ni kwanini Fiona
alifanya nami mapenzi na kwanini alikubali kufanya
mapenzi. Hilo ndilo lilikuwa linaleta ugomvi katika
Ufalme ule. Baada ya mambo hayo kutokea Fiona
alipewa adhabu ambao niliona kama vile itauondoa
Uhai wake. Baada ya hapo nilishituka usingizini bila
kutarajia nilijikuta niko sehemu nyingine ndani ya
Jumba la ajabu kama la Fiona ila mbele yangu
kukiwa na sanamu kubwa la Joka lililojikunja.
 
Baada ya mambo hayo kutokea Fiona alipewa
adhabu ambao niliona kama vile itauondoa Uhai
wake. Baada ya hapo nilishituka usingizini bila
kutarajia nilijikuta niko sehemu nyingune ndani ya
Jumba la ajabu kama la Fiona ila mbele yangu
kukiwa na sanamu kubwa la Joka lililojikunja.
SONGA NAYO,
Niliogopa sana kuona vile, nikajiuliza Fiona karudi
tena na kuja kunichukua lakini Yale mazingira
sikuwahi kuyaona toka nimeishi na Fiona.
Nilisimama na kuangalia vizuri eneo lile lakini
haikuwa kabisa lile la nyumbani kwa Fiona.
"Jumanne karibu"
Sauti ilisikika ikinisemesha. Sauti ile sikujua
inatokea upande upi lakini ilisikika kama vile
msemaji yuko mbele yangu, lakini sikumuona, hata
nilipogeuka nyuma si kumuona mzungumzaji. Kila
upande nilitazama pia sikumuona mzungumzaji.
Niligeuka mala kadhaa kuangaza kama nitamuona
kwani Sauti ilikuwa akijirudia rudia kuzungumza.
"Tafadhali naomba ujitokeze mbele yangu nikuone
maana unanitisha"
Nilisema baada ya hali kuniwia ngumu, mazingira
Yale kwangu yalikuwa ni mengine kwahio ilinipasa
niwe mpole na msitaharabu.
"Usijali Jumanne Mimi Niko hapa"
Sauti ile ilisikika tena mbele yangu. Nilipokuwa
niliisi kujikojolea maana kilichokuwa kinazungumza
lilikuwa ni Joka kubwa kweli kweli, Joka lile liliinua
kichwa chake likawa kama linanisogelea. Muda huo
Mwenzenu miguu ilikufa ganzi kabisa, yaani
nilishuka mwenyewe mpaka chini, huku nikilia
kuomba msaada. We kweli kufa jamani ni kugumu
ukiwa kwenye matatizo. Ukisikia kifo cha mateso ni
kigumu basi amini nikigumu kweli kweli, Mimi
mwenyewe nilitamani kufa pale pale maana niliisi
naenda kumezwa.
"Jumanne kumbe wewe ni muoga hivyo! Kwamaana
hiyo Fiona hakukwambia Tabia zetu jinsi tulivyo
sisi!"
Muda huo huo lile Joka liligeuka na kuwa
mwanamke mzuuri kama Fiona halafu akasema
hivyo.
Nilibaki kumwangalia yule Mwanamke huku bado
nikiwa chini natetemeka.
"Mimi naitwa Sofia, ni sawa sawa na Fiona ndio
maana tunafanana. Ila usiniogope nimesha jua kuwa
Fiona hakukwambia kuusu Sifa na Tabia zetu.
Nakuomba kuanzia sasa ujue kwamba ninauwezo
wa kubadilika na kuwa kiumbe mwingine tofauti
kabisa. Nina uwezo wa kujigeuza sura na
muonekano mwingine wa viumbe zaidi ya mia moja.
Kwahio naomba inizoee hata kama ikitokea
nimebadilika na kuwa kiumbe kingine cha
kukutisha"
Mwanamke yule alisema, wote walikuwa ni
wanawake ambao Umri wao hukuzidi miaka 25.
"Jumanne"
Mwanamke yule aliniita.
"Naam"
Nami niliitika.
"Mimi ninaitwa nani?"
Aliniuliza tena.
"Unaitwa Sofia"
"Nimependa sana, yaani vizuri sana"
Sofia alisema.
Muda huo Mimi nilikuwa na hofu kweli kweli maana
ilikuwa sio kawaida mwanamke yule alinitisha sana.
Nikiwa hivyo hivyo na mashaka alinichukua na
kuniingiza ndani kabisa ya Jumba lake lile,
majumba yao kwa kiasi kikubwa yalikuwa
yanafanana tu, ila ili la kwa Sofia kidogo lilikuwa na
uwafadhali halikuwa la zamani kama la Fiona.
"Jumanne kaa hapo, na najua unanjaa sana, lakini
utaratibu wa huku si unaujua, kwahio unaweza
kuomba unachokihitaji, ningekuwa nakula chakula
kama chenu ningekuombea chakula kipi kwasababu
wewe ni Mgeni kwangu leo"
Sofia alisema. Alionekana mkarimu kweli kweli.
Mpaka hapo Mimi nilikuwa sijaongea Chochote
kuusu maisha ya Sofia.
Jumanne natamani azungumze jambo maana nahisi
Faraja sana kuwa na wewe Leo.
Sofia alisema tena.
Baada ya kunambia hivyo nilijikuta anapata ujasiri
wa kumuuliza.
"Kwanini Umemuua Fiona?"
"Ha ha ha haa! Jumanne sijamuua Fiona na
huwenda mpaka sasa kaisha amka anakutafuta"
Sasa kwanini usinirudishe kwa Fiona wangu"
Nilisema tena kwa Uzuni.
"Jumanne Mfalme ambaye umekimbia bila kutarajia
unawaza nini, hapa pia upo sehemu salama, tena
huwenda hapa pakawa salama zaidi kuliko kwa
Fiona, na unabahati sana wewe ulikuwa wa kufa!"
Sofia alisema. Alinishitua sana, nikatamani sasa
kujua mengi kutoka kwake maana sasa niligundua
kuwa huwenda kuna mchezo Ambo Fiona alikuwa
anaufanya kwangu"
"Kwanini umesema ningekuwa nisha kufa!"
Nilimuuliza Sofia.
"Huku huwa ni vigumu sana kumsamehe mtu
ambaye umekuwa msaliti huwa tunauwa tu, tena
unabahati sana mpaka kufika mikononi Mwa Fiona
lazima kuna kitu kilifanyika na huwenda Fiona
mwenyewe alikusaidia mpaka kufika pale. Kuna
askari ambao wanaua bila kujua wamekuuwa vipi"
Sofia alisema. Maneno yake yalinikumbusha kwa
Fiona Jinsi alivyonambia nikiwa kwake, Fiona naye
alinambia hivyo hivyo kama alivyosema Sofia.
"Sawa nimekuelewa, taarifa zangu wewe
umezijuaje?"
Nilimuuliza tena hivyo kwasababu Fiona alinambia
kuwa wao ni maadui wakubwa halafu umekuwaje
Sofia azijue habari zangu.
"Umeuliza vizuri, nauwenda Fiona alikuwa kaisha
kwambia Jinsi sisi na wao tulivyo. Sisi ni maadui
wakubwa sana, lakini uadui wetu hautufanyi tuache
kushilikiana kwenye maswala mengine, kuna
wawakilishi ambao huwa wanaudhulia kwenye vikao
vya ushirikiano. Kwahio taarifa huwa tunazipata na
kule kuna ubarozi wetu pia"
Sofia alisema.
Nilitamani kujua mengi sana kutoka kwake.
"Unaweza kunambia hata historia ya maisha yako,
halafu unacho jua kuusu hizi koo zenu mnavyoishi?"
Nilimuuliza Hivyo Sofia ili niipate kumjua kiujumla.
"Sawa Jumanne nitakusimulia lakini ningeomba
uombe chakula chako ule kwanza kisha ukaoge
halafu tukae nitakusimulia mfumo mzima wa huku
na historia"
Sofia alisema.
"Lakini samahani unaweza kuniambia sehemu hii
inaitwaje?"
Nilimuuliza tena swali lingine.
"Huku hapajulikani lakini tunaishi kwa
Koo........Kula kwanza nitakusimulia vizuri vyote
utavijua tu"
Sofia alisema tena. Ilinilazimu niombe chakula nile
kwanza halafu ndio tuulizane vizuri. Njaa kweli
nilikuwa nao na niliagiza ugari na samaki kweli
vikaja, maisha ya kule kuusu chakula na mavazi kwa
Mwanadamu ni ya Raha sana. Mavazi yalikuwa
yanaletwa tu, nilikuwa nayakuta kitandani kazi yangu
ilikuwa ni kuvaa tu na kula full Stop.
Nilikula chakula nikashiba vizuri kisha akanichukua
na kunipereka tena sehemu iliyokuwa na Maji ya
kutiririka(ya mto), ilikuwa ni sehemu nzuri tu japo
kuwa ilitofautiana sana na kule kwa Fiona. Mambo
ya pale yalikuwa kama yale yale ya Fiona, hata
nilipomwabia Sofia anipishe nioge yeye alinambia
vile vile.
"We Oga kwani unajua nimekukuta wapi,
nimekufanyia nini. Hata hivyo kila kitu nakiona
katika mwili wako. Kwahio hamna haja ya
kuondoka"
"Lakini Sofia Mimi ni Mwanaume wewe ni
Mwanamke haipendezi Mimi nioge wewe ukiwa
hapa. Naona aibu"
Nilisema lengo langu kumfanya aondoke.
"Mwanamke, mwanaume, na aibu! mbona bado
ujaniweka wazi. Kwani kuna nini katika hivi vitu
vitatu. Wanaume mbona wengi huwa nawapiga
wengine wakiwa hawajavaa kabisa lakini hakuna
madhara yoyote ambao huwa yanatokea, aibu labda
Mimi nikifanya kosa ndio huwa naona aibu
kumweleza mfalme wetu. Kwani kuna aibu nyingine
kati ya mwanaume na mwanamke?"
Sofia alisema. Hapo niligundua kuwa nilichowahi
kuambiwa na Fiona ni cha kweli kuwa wao
walikuwa hawaruhusiwi kufanya mapenzi kabisa na
hawajui namna mapenzi yanavyofanywa. Baada ya
kugundua hivyo ilinibidi nikae kimya na kuzivua
nguo zangu kisha nikaingia kwenye maji na kuoga.
"Lakini Sofia eti ninyi huwa amfanyi mapenzi?"
Nikiwa kwenye maji nilijikuta naropoka.
Sofia aliniangalia sana kwa mshangao kweli.
"Ni kweli Jumanne na tulikatazwa kabisa kujihusisha
ma mapenzi hata kama ikitokea tukajua jinsi ya
kuyafanya. Walinipa vitisho sana. Lakini kuna muda
ambao hata Mimi huwa nawaza kujua mapenzi
yanavyofanywa, natamani nijue Jinsi mapenzi
yanavyofanywa lakini nisifanye"
Sofia alisema.
"Haya"
Nami nilitikia tu hivyo kwani tayari nilikuwa nishaaza
kujilaumu kwanini nilimuuliza kitu hicho. Maana
angeweza hata kusema nimfundishe Jinsi mapenzi
yanavyofanywa.
Nilikuwa naongea kwa kujiamini kwasababu
nilikuwa nishawazoea sana. Baada ya kumaliza
Kuoga tulirudi tena ndani, tulipofika ndani
nilimuomba anisimulie historia ya kule katika hizo
Jamii zao.
"Nashukuru Jumanne kwa kuonekana Jasiri,
kwakweli Fiona alikuwa kaisha kufundisha vingi, na
huwenda alikuwa kaisha kwambia kabisa kuwa
huwa anabadilika na kuwa kitu kipya maana
unajiamini sana. Ongera sana japo kuwa hapo
hawali nilijua kabisa kuwa ujawahi kujua kitu kuusu
sisi labda ndio maana uliniogopa"
Sofia alisema.
"Sawa lakini Fiona alikuwa kaisha nambia kila kitu,
kwahio usijali. Mwanzo niliogopa kwasababu
nilikuwa sitambui kama ni wewe Mimi nilizani ni
Joka la kweli"
Nilisema, maneno yangu yalimfanya Sofia kuguna
kisha kutabasamu na kusema.
"Haya bhna, navutiwa sana na Jinsi unavyojiamini"
Sofia alisema.
 
ILIPOISHIA.
"Sawa lakini Fiona alikuwa kaisha nambia kila kitu,
kwahio usijali. Mwanzo niliogopa kwasababu
nilikuwa sitambui kama ni wewe Mimi nilizani ni
Joka la kweli"
Nilisema, maneno yangu yalimfanya Sofia kuguna
kisha kutabasamu na kusema.
"Haya bhna, navutiwa sana na Jinsi unavyojiamini"
Sofia alisema.
SONGA NAYO.
Sophia alisema tena. Nilipokuwa Mimi nilikuwa
nangoja anisimulie tu kisa cha maisha ya huko.
"Najua una hamu ya kujua mengi kuusu huku"
Sofia alizungumza tena.
"Ni kweli kabisa nina hamu ya kujua, kwasababu
Fiona hakuwahi kunisimulia kiundani zaidi ya
kunambia kuwa ninyi ni maadui wakubwa sana"
Nilisema nami pia ili kumfanya awe mwepesi zaidi
katika jambo nililotaka kujua.
"Kwanza kabisa Mimi na Fiona ni Mtu na Mdogo
wake na ndio maana unaona tunafanana kiasi hiki,
Mimi ni mkubwa Fiona ni Mdogo, tulizaliwa wawili
tu katika kizazi cha mama Baba na Mama yetu,
tulikulia mazingira ya pamoja. Kama Fiona
ajakwabia huwa kuna watu maalumu ambao wao ni
kwa ajili ya kudumisha ulinzi katika koo hizi. na
watu hao wanalisishana kama Ufalme unavyokuwa.
Kwa mfano tayari huko kuna Mtoto kaisha zaliwa
kwa ajili ya kulithi hapa Mimi nikiachia nafasi hii,
haijarishi watakuwa wangapi katika kuzaliwa kwao
lakini atachukuliwa mmoja tu ndiye atakuwa Mlinzi.
Ni nafasi ya pekee sana katika hizi koo zetu kupewa
nafasi ya kuwa mlinzi wa mwisho. Ni kweli huwa
hatuna huruma kabisa, na sisi huwa tunapambana
na viumbe vizito sana. Ilikuwa vipi Mimi na Fiona
Mdogo wangu wote tukawa walinzi..........hapo
hawali hizi koo zilikuwa pamoja na aliyekuwa mlinzi
kama sisi alikuwa ni mmoja tu, lakini kulitokea
kutoelewana baina ya hizi koo mbili wakaanza
kubaguana sana, ugomvi huo ukaletezea kutengana
ndio ikawa hivi kwa watu wa Ukoo wetu na Ukoo
ule mwingine. Koo hizi zote ni koo za kimila katika
Ziwa Ngozi. Koo hizi ziliungana zamani sana enzi
za mababu zenu, zamani kabisa huko wakawa kitu
kimoja katika kuisimamia mizimu yao. Hio ilitokea
kwasababu wote walilitumia ziwa Ngozi, na
ilipendeza sana sana. Lakini kutokana na
mabadiliko basi ndio mgogoro mkubwa ukatokea
baina ya koo hizi mbili na sio huku tu hata huko
Duniani tayari muunganiko ule ulikufa katika koo
zenu ambazo zilikuwa zimeungana na ndio maana
huku palikuwa hivyo. Maisha ya uku huwa
yanachukuliwa kama mungu na utegemewa sana na
wanadamu katika maswala yao ya muhimu. Baada
ya Vita hio kuwa nzito Baba na mama yangu
walikuwa wametoka kila mmoja koo yake, Baba
alikuwa katoka katika Koo hii na Mama Yetu
alikuwa katoka katika ukoo ule ambao wanahitaji
Mfalme kwa ajili ya kuwaongoza baada ya Mfalme
kufariki miaka miwili nyuma. Mgogoro huo
ulisababisha na sisi tukatenganishwa na
kugawanywa kila mmoja upande wake. Sofia Mimi
upande wa Baba na Fiona upande wa Mama"
Sofia alinisimulia vizuri sana kisa chao na kweli
kabisa hata nilivyoajaribu kufuatilia niligundua
kabisa kuliwahi kuwa na Ugomvi mkubwa katika
Ukoo wetu na mgogoro mkubwa ambao uliletezea
kutoelewana kabisa na watu Fulani, mpaka
nakiandika kitabu hiki cha kweli kuusu maisha
yangu bado hatukuwahi kuelewana lakini kuna
baadhi ya vitu tunashirikiana sana tu. Kwahio
alichokuwa anakizungumza Sofia kilikuwa cha kweli
kabisa.
"Sawa Sofia sasa ni nini kilichosababisha ugomvi
huo mkubwa?"
Niliuliza tena.
"Jamanne nishakwambia mabadiliko tu, unajua
tuseme muda mwingine kuna tamaa za hapa na
pale kwahio ndio maana ulitokea ugomvi mkubwa
kiasi hicho, tunauwana hovyo hovyo lakini
namshukuru mungu Mimi na Fiona mdogo wangu
tunajaliana sana, muda mwingine tunakutana
tunazungumza lakini si kuuana, na ndio maana
sijamuua. Yani kiujumla anajua ukweli wa maisha
yangu nami pia najua ukweli wa maisha yake. kuna
kitu ambacho sijakwambia lakini ni Cha muhimu
sana, Ziwa Ngozi hilo ziwa ni sawa na kiota chetu
pande zote mbili, lakini huwa aliendewi hivi hivi
ukienda hovyo kwa papara wanadamu wanakusahau
hio pia ni kwasababu ya Ugomvi huo ndio
ulisababisha mambo hayo, hapo lilipo lipo katika
msimamo wa koo tu basi, akienda mtu ambaye
hausiki na koo hizi ni Vigumu sana kupona, yaani
huwa ni mala chache sana, na wakiwa kikundi cha
watu mala nyingi mmoja wao lazima amezwe, hata
kama muhusika katoka katika koo hizi mbili awe
msitaharabu sana hakutokuwa na vita vyovyote.
Lakini akiwa mkorofi naye pia anaweza kusahurika,
Watu wote ambao wanafariki huwa wanakuja kuwa
watumwa huku"
Sofia alisema tena, yaani ilikuwa kama ndio
kaniongezea maswali mengine ya kumuuliza japo
kuwa kwenye upande wa Ziwa Ngozi alikuwa sahihi
kabisa wala hakukosea. Ziwa Ngozi kama
mnavyolijua watu wa mbeya, na kama wewe siyo
mtu wa mbeya hakuwahi Kujua historia ya ziwa hilo
nakuomba uulize utasimuliwa kuusu ziwa Ngozi.
"Umesema kuusu watu wanao fariki wanakuja huku,
kwahio hata Mimi nishafariki"
Nilimuuliza ili kujua maana mwanzo kipindi nafika
kwenye lile Jumba la ufahari nilisikia kelele za watu
wananiita na kulitaja jina langu kana kwamba
nishafariki. Tena Mama yangu mzazi ndiye alikuwa
akilia sana.
"Wewe umechukuliwa Jumanne na usizani wewe
ulizaliwa kwa kawaida hapana wewe ulizaliwa kwa
maombi maalumu kwahio ndio maana
umechukuliwa lakini kule ipo kama umekufa na hata
ikatokea umerudi kule watakushangaa na huwenda
wakakukimbia, na ndio maana nilikwambia huku
kufa kawaida ukisha kuwa msaliti"
Sofia alisema tena kwa msisitizo. Wee hapo hapo
sikupenda tena kuulizia habari zangu tena, kifo
kilinitisha sana, mpaka nilianza kuomba ili
nifanikiwe kurudi katika lile Jumba nililowaacha
wapenzi wangu Jamila na Raulati, lakini nilipata
kumuomba Sofia kama kuna namna ya kunisaidia
anitoe huko nikisha fika Duniani itajulikana mbele
kwa mbele, lakini alinyamaza tu hakunijibu. Hapo
niliamua nibadili niulize tena swali lingine kabisa
ambalo lilimuhusu yeye, maana kunyamaza kwakwe
niligundua kabisa kuwa huwezekano wa Mimi
kutoka kule upo ila kuna kitu alikihofia.
"Samahani tena Sofia! Kama Fiona ni ndugu yako
mbona ulimemfanyia vile?"
Nilimuuliza tena Sophia.
"Pole sana Jumanne, pia naomba unisamehe sana.
Jumanne wewe ni kijana mzuri sana, pia huwenda
ukawa mfalme kweli kwasababu umepewa nafasi
nyingine ya kuishi huku akitafutwa mtu mwingine,
lakini akikosekana itabidi wewe uwe mfalme tena.
Hongera sana lakini Omba Asije akapatikana mtu
mwingine ambaye atakuwa Mfalme maana wewe
utalazimika kufa"
Sofia alisema tena.
Alipokuwa anagusia swala langu la kufa Mimi
nilikuwa naogopa sana.
"Lakini bado ujanambia kwanini ulimemfanyia Fiona
ubaya ule?"
Nilimuuliza tena ili kumfanya abadili maada.
"Jumanne najua kabisa kuwa Wewe na Fiona
mmeanzisha mahusiano ya kimapenzi na Fiona yeye
mwenyewe ndiye alinambia hayo yote, kwahio
nilifanya vile kwa ajili ya kumuokoa Mdogo wangu,
najua ambacho kitamkuta ni kifo kibaya. Mpaka
hapo alikuwa kaisha athirika sana mdogo wangu na
ndio maana nimemuweza kirahisi na hata hivyo yeye
ajui kuwa Mimi ndiye nimemfanyia hivyo. Kiujumla
nimemuokoa mdogo wangu, Ngoja akae kwanza
peke yake halafu ajipange upya ila atakuja kwangu
kuniuliza kwasababu anajua kabisa ni vigumu mtu
mwingine kumuweza tofauti na Mimi"
Sofia alisema. Maneno yake yaliniumiza sana, tena
sana kwa Jinsi ninavyojua maumivu ya mapenzi
halafu Fiona alivyokuwa anajiapiza kwangu sikuwa
na Imani na alichokifanya Sofia kwa mdogo wake.
"pole sana Fiona, naamini unaangaika sana huko
uliko"
Nilijikuta nasema maana maneno aliyokuwa Fiona
anayasema kwangu, viapo vile vya nguvu, hasa
aliponambia kuwa Mimi ni sawa na pumzi
aliyokuwa anaivuta. Kiukweli niliumia sana sana.
 
ILIPOISHIA.
"pole sana Fiona, naamini unaangaika sana huko
uliko"
Nilijikuta nasema maana maneno aliyokuwa Fiona
anauasema kwangu, viapo vile vya nguvu, hasa
aliponambia kuwa Mimi ni sawa na pumzi
aliyokuwa anaivuta. Kiukweli niliumia sana sana.
SONGA NAYO.
"Unayajua Mapenzi?
Nilimuuliza Sofia.
"Sitaki hata niyajue Jumanne maana kwa jinsi nilivyo
haswa ni mtihani sana kwetu kujihusisha na
mapenzi"
"Sawa"
Nilisema kisha nikatulia.
"Kwanini umeniuliza Hivyo Jumanne?"
"Kwasababu sina hakika kabisa na kile ambacho
umekifanya kama ni sahihi, ni bora ungemuua kuliko
kumwacha anaishi maana naamini ndio umemtesa
kabisa zaidi ya mateso yaani anaweza hata kufa
kabisa"
Nilisema.
"Jumanne kweli unacho kizungumza?"
"Sahihi kabisa, Mimi ndiye namjua Fiona, Nimekaa
naye sana"
Nilisema tena.
"Naomba usitoke humu; nitarudi muda si mrefu"
Sofia alisema. Kisha akapotea pale pale.
Nilibaki mule ndani peke yangu, nilikuwa najiamini
sana kwasababu nilikuwa nimewazoea, kawaida
yangu nilikuwa nikibaki ndani ya majumba Yale
peke yangu, nilikuwa napenda kuagiza karanga
mbichi kwa ajili ya kutafuna, maana wale viumbe
walikuwa si wa mchezo katika swala zima la
kujamiana. Nilihofia pia Sofia naye anaweza
akageuka nae akataka tufanye mapenzi. Niliendelea
kukaa kumsubili Sofia arudi huku nikitafuna karanga
zangu. Haikupita Robo saa Sofia akawa amerudi.
Alionekana mwenye hasira sana.
Alinifuata akanizoa kwenye kiti nilichokuwa nimekaa
na kunitupa nikajipigiza kwenye ukuta na kutua
Chini.
Sofia alianza kubadilika macho yakawa meusi kama
ya joka.
"Tafadhali Sofia naomba usiniue!"
Nilisema hivyo. Muda huo tayari nilikuwa nishajua
kabisa ni wakati wangu wa kufa.
"Jumanne! Napenda nikuue lakini ngoja nikuache
kwanza nione nini kitaendelea........ila hupaswi tena
kuwa Mfalme katika Koo ile kwasababu Mdogo
wangu kaisha Athirika kabisa"
Sofia alisema. Muda huo machozi yalikuwa
yanamtoka hata hasira zilimpungua.
"Alinilazimisha yeye kufanya Mapenzi"
Nilisema, kulikuwa hakuna namna ya kujitetea zaidi
ya kuzungumza hivyo.
"Simama uje ukae hapa tuzungumze vizuri"
Sofia alisema.
Nilisimama nikasogea aliponiambia niende kukaa.
Nilifika nikakaa kwenye kiti Jirani na alipokuwa
amesimama tayari hali yake ilikuwa amerudi katika
usawa.
"Jumanne naomba unifundishe mapenzi, nataka
namimi nijue jinsi hayo mapenzi yalivyo, ili
nihakikishe kama kweli hali niliyomkuta nayo Fiona
niyakweli!"
Sofia alisema. Kauli yake Mimi ilinishitua sana.
"Sofia hupaswi kufanya mapenzi maana ni hatari,
utamuua mdogo wako ukifanya mapenzi na Mimi?"
Nilisema. Lengo langu ili kuilinda heshima na
huruma iliyokuwepo baina ya Sofia na Fiona, viumbe
ambao walikuwa ni Mtu na mdogo wake.
"Utaki?"
Sofia alisema kwa ukari huku akiniangalia Usoni.
Niliogopa nikajua ndio mwisho wangu wa kuishi
endapo nitagoma kufanya naye.
"Sawa nitafanya lakini naomba tukimaliza kufanya
mapenzi unisaidie kurudi nilikotoka!"
Nilisema hivyo makusudi maana nilijua kabisa
nikisha Fanya mapenzi na Sofia naye lazima
anogewe kwahio ambacho kingefuata huko ni
uwadui na kuuana.
"Kama ni hivyo naomba unifundishe jinsi ya kufanya
mapenzi"
Sofia alisema tena. Nilisimama nikamwambia
aondoe vazi lake. Bila kusita naye alifanya hivyo
hivyo, kisha nikamwambia ajilaze kwenye kiti
ambacho kilikuwa kama kochi la futi tatu, naye
akafanya hivyo hivyo, alikuwa aogopi kabisa.
Alipojilaza Mimi nilimsogelea kisha nikaanza
kumchezea ili kumwandaa. Nilimshika shika
kiufasaha kabisa nikamuona akaanza kuguna
miguno ya kafara, sauti zao za mahaba ndizo
zilikuwa zinanitisha Mimi, Sauti zile zilikuwa si za
kawaida kabisa nazani hazikuwa hata za Binadamu
maana kila alipokuwa anazidi kulia kwa madeko
ndio nami nilizidi kupandisha mizuka.
Nilimtoa nyoka pangoni kisha nikamzamisha
shimoni, shimo ambalo nyoka mwenyewe alikuwa
anaenda kulifungulia kwa mala ya kwanza ili
kurekebisha kipimo kabisa. Nilimpa Sofia kile
ambacho alikuwa anakitaka. Baada ya kumaliza
yeye mwenyewe alipoa kisha nikamwambia tukaoge
kwanza halafu mambo mengine yaendelee. Kweli
naye alitii na kwenda kuoga,.... nilioga naye
tukamaliza tukarudi ndani. Sielewi wale viumbe
wakoje, hata dakika kumi hazikuisha Sofia alitoka
na kukimbia mbio kuelekea sehemu ambayo alijua
yeye.
Kama ilivyokuwa kwa Fiona ndivyo hivyo hivyo kwa
Sofia. Wakati huu sikushituka kabisa kwasababu
nilikuwa nishawaozea jinsi walivyo. Afadhali hata
kwa Sofia yeye aliwahi kurudi. Yeye alirudi nyakati
za saa moja hivi. Hata kurudi kwake kulikuwa
tofauti na Fiona huyu alikuwa kawaida.
"Naomba unisamehe Jumanne mpenzi wangu"
Sofia alisema. Hapo tu ndipo Mimi walikuwa
wananiuzi, tayari Sofia naye ailianza kuniita mpenzi,
jambo ambalo Mimi nilikuwa silitaki.
"Mapenzi ni mazuri Sana kuna raha sana. Kwahio
kesho tutarudia"
Vile vile kama alivyosema mdogo wake.
"Hapana Sophia kesho hatutakiwi kufanya tena,
tukifanya unakuwa kama Fiona"
Nilisema. Nilivyosema hivyo akapoa.
"Jumanne kwahio unataka nikurudishe kwa Fiona.
"Hapana, naomba unisaidie kutoka katika inchi hii
nirudi nyumbani"
"Ni kweli Jumanne maana kwa Jinsi nilivyomuona
mdogo wangu, sina hakika kama wewe unaweza
kuwa mfalme maana watagundua tu kuwa
alijihusisha kimapenzi iwe isiwe, ni bora Mimi
ambaye sijaathirika sana nibaki niwe naenda
kumliwaza"
Sofia alisema. Hapo kidogo alinipa matumaini ya
kurudi nyumbani habari za Ufalme watajua wao.
"Utanisaidia Sofia kutoka huku?"
Niliuliza.
"Usijali nitafanya kila mbinu kesho nikuondoe,
hakuna anaye Jua kuwa wewe uko na Mimi ila
wanajua uko kwa Fiona. Na hata siku ikitokea
wanakuhitaji ukawe mfalme nitamwambia Fiona
awadanganye kuwa ulimtoroka yeye akiwa vitani na
haikujulikana ulienda wapi"
Sofia alisema.
"Hilo litakuwa wazo zuri lakini ningeomba msisubiri
wao wajue bora umwambie Fiona ndiye aende
akariport kabla ili iwe rahisi kwao kumtafuta mtu
mwingine"
Nilisema, hapo niliongezea ushauri.
"Hilo ni wazo zuri Jumanne"
Sofia alisema.
"Haya, Sofia hawatojua kuwa Mimi nimerudi katika
ulimwengu wangu?"
Nilimuuliza.
"Hawatokufuatilia hata usijali"
Sofia alinijibu jawabu zuri ambalo lilinipa matumaini
zaidi. Tuliongea mengi sana siku hio nikampa
ushauri kuusu mapenzi yalivyo endapo akizama
sana na kuyazoea. Kiujumla aliupenda ushari wangu
akaridhika nao sana.
Usiku sikulala naye kama nilivyo lala na Fiona siku
ya kwanza, nililala kwenye godoro zuri tu halafu
chumba kingine tofauti na alichoingia yeye, maisha
ya pale yalikuwa tofauti kidogo na ya nyumbani kwa
Fiona. Kweli asubuhi mapema kabisa kama
tulivyokuwa tumepanga Sofia aliniamsha na
kunichukua kisha akanambia nifumbe macho kama
ilivyokuwa Imepangwa, kweli nilijikuta ndani ya poli
inje kidogo ya ziwa Ngozi.
"Jumanne naomba uondoke ila nitalikumbuka sana
penzi lako umenitamanisha kuendelea kufanya
mapenzi, siku moja usishangae naweza hata
kutoroka na kuja huku kwa ajili yako, nitajua jinsi ya
kukupata. Nimeamua kukutoa kule kwasababu ya
kuilinda heshima yangu na Mdogo wangu. Nenda!"
Sofia alisema. Kisha akapotea huwezi amini muda
ambao Sofia alitoweka sauti ya Fiona alisikika
Masikioni mwangu akiniita huku akisema.
"Jumanne umeamua kuniacha nife?"
Sauti hiyo ilinishitua sana. Lakini nilishindwa kuijibu
ikanibidi nitafute namna ya kurudi nyumbani.
Niliianza safari ya kulikatiza pori lile ambalo
limelizunguka Ziwa Ngozi kuelekea nyumbani. Kwa
bahati nzuri nilikutana na watu wakiwa mashambani
huko nikawaomba msaada wa kurudi nyumbani.
Sauti ya Fiona iliendelea kunisindikiza lakini
sikuthubutu kuijibu. Jioni kabisa ndio nilifika
nyumbani lakini njiani huko nilikuwa nishakumbana
visanga kibao kutoka kwa watu, kila mmoja alikuwa
akidai kwamba, nilishafariki na kuzikwa. Kauli hizo
sikuzijali kwasababu nilikuwa najua watu
watanikimbia na kunisema hivyo, ni kweli watu
walinikimbia wengine wakawa wananifuata ili
kuhakiki kama kweli au ni mzimu wangu.
Hata nilipofika nyumbani Mama alizimia, ndugu
zangu wengine walikimbia.
Nilijitahidi sana kuwashawishi mpaka kuamini,
niliwasimulia mengi niliyokutana nayo kipindi niko
huko. Walipokuja kuamini ni pale nilipowasimulia
Habari za kuzaliwa kwangu ndipo waliamini kabisa
kuwa Mimi nilichukuliwa na mizimu ya ziwa Ngozi.
Hicho ndicho kisa cha maisha yangu. Sijatunga Bali
ni chakweli.
ILIPOISHIA.
Walipokuja kuamini ni pale nilipowasimulia Habari
za kuzaliwa kwangu ndipo waliamini kabisa kuwa
Mimi nilichukuliwa na mizimu ya ziwa Ngozi.
Hicho ndicho kisa cha maisha yangu. Sijatunga Bali
ni chakweli.
SONGA NAYO.
Baada ya kutoka katika maisha hayo Jumanne
aliishi kwa mawazo sana, ndugu zake walipokuwa
wanajaribu kumuuliza ni kitu gani ambacho alikuwa
anakiwaza yeye alikuwa akiwajibu kuwa; anawaza
kwasababu ya kuwaacha wasichana wawili Raulati
na Jamila katika mazingira Yale, jumanne alikuwa
akiwapenda sana Raulati na Jamila, mabinti ambao
walikuwa ni Mapacha. Ndugu zake walijitahidi sana
kumuweka sawa kwa kumshauli asahau habari za
Jamila na Raulati kwani wale walikuwa ni mabinti
Mapacha, ndugu wawili waliozaliwa pamoja kwahio
hata kama wangetoka naye, bado ingemlazimu
awaowe wote wawili jambo ambalo lingekuwa
gumu sana. Na hata kama angemchagua mmoja
angemchagua nani ambaye angekubali aolewe peke
yake na mwenzake abaki au nani angekubali abaki
halafu mwenzake aolewe. Kwahio ilikuwa ngumu
sana katika swala hilo. Baada yakupokea ushauri
mwingi ndipo walipomshauli asimulie Kisa cha
maisha yaliyomkuta huko. Kisa hicho ambacho
umemaliza kukisoma. Mwanzo ilikuwa ngumu sana
kwa Jumanne kukubali kukisimulia kisa hicho cha
ajabu katika maisha yake, alikuwa anadai kuwa kuna
vitu ambayo hakupaswa kabisa kuviweka bayana
kwasababu alipewa Onyo kubwa sana na kiumbe
aliyemsaidia kutoka kule kuwa endapo tu atathubutu
kuuzungumza baadhi ya vitu ambavyo alimkataza
basi angerudi katika maisha Yale Yale ya uko
alikokuwa. Kwa maana hiyo kutokana na kisa chake
Sofia alimkataza Jumanne asitamke baadhi ya vitu
ambavyo alikumbana navyo huko. Hapo hawali
Jumanne alisimulia kisa chake lakini baadhi ya
vipengere alikuwa avisemi kabisa, lakini kila
alipokuwa anazidi kukaa mawazo yalizidi kumtuma
auseme ukweli wa kila jambo ambalo alikutana nalo
huko, jambo zito sana ambalo alikatazwa ni kuusu
kufanya mapenzi na wale Binadamu wa Ajabu yaani
Sofia na mdogo wake Fiona, halafu jambo lingine
alikuwa amekatazwa ni kwamba hakupaswa kabisa
kuijibu sauti ya Fiona ambayo ilizidi kumfuata hata
pale alipofika nyumbani na kuishi, Sauti ile
ilimshinda Jumanne akajikuta anaijibu sauti ile
kuwa; amwache asimfuatilie. Siku ambayo Jumanne
alitamka hivyo alilia siku mzima kwasababu ya
maagano ambayo waliwekeana na Sofia. Maagano
hayo Jumanne aliyasema kwa ndugu zake kuwa
aliambiwa kuwa akithubutu kuusema ukweli ule na
kuijibu sauti ya Fiona lazima arudi kule na adhabu
yake ni kuishi kwa mateso mpaka pale Ambako
angefariki. Baada ya ndugu zake kujua hivyo
walijaribu kumtembeza Jumanne kwa waganga
mbali mbali ili waifunge mizimu isiendelee
kimfuatilia. lakini kila mganga alishindwa na
alikuwa anakumbana na vipigo vya kuumiza sana.
Baada ya kushindwa kwa waganga walimfanyia
maombi ya Dini wakaamini kabisa kuwa hatopata
matatizo tena, toka hapo jumanne hakusikia wala
kupata dalili zozote kuusu mizimu kumwandama.
Miezi miwili tangu kuombewa ndipo alipoanza
kuongea kwa uhuru katika vyombo vya Habari Vitu
ambavyo alikutana navyo huko alikokuwa. Mwisho
alishauliwa kukitoa kitabu ili kibaki kama
kumbukumbu kwa wasikilizaji na watanzania wote
wajue kuusu swala la Mizimu. Ushauri huo Jumanne
aliufanyia kazi ndipo alikaa chini na kuiandika
hadithi yake kamili. kitu cha pekee alichokiacha ni
kuusu Sauti ya Fiona aliyoijibu, baadaye kitabu
chake kiliingia sokoni watu wakakiona na kukisoma.
Ingawa kilikuwa na page chache lakini kilivutia sana
kwa wasomaji.
Kwakuwa alikuwa ni Mwanafunzi katika Chuo kikuu
cha Sayansi cha mbeya Jumanne alianza kufanya
taratibu za kurudi chuo kwa ajili ya kuendelea na
masomo yake. Siku moja kabla ya kwenda chuo,
kulipokucha Jumanne hakuwepo ndani, ndugu zake
walitafuta sana sana lakini hawakufanikiwa kumpata,
baaye waliamini Jumanne alirudi tena alikokuwa
kwa maana hiyo alichukuliwa tena na mizimu ya
ziwa Ngozi, baada ya kujua hivyo walienda kufanya
tambiko katika mizimu yao lakini hawakufanikiwa
ndipo walipoamua kumsahau Jumanne kwa namna
hiyo.
Mwisho wa hadithi hii ya kuvutia.
Imetungwa na Hemed Mayugu.
Kama ikitokea Jumanne akirudi msimu wa Pili wa
Hadithi hii utakuijia hapa hapa, nazani atatwambia
vingi vingi vya mambo ambayo yanaendelea
kumkuta. Tumuombee na Tuombe Jumanne apate
kurudi ili Hadithi yetu nzuri iendelee. Asanteni sana
kwa Ushirikiano wenu katika kuifuatilia Hadithi hii ya
kusisimua.

-MWISHO-
 
Back
Top Bottom