Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
- Thread starter
- #81
SEHEMU YA 64
Mzee Hamisi hakuwa na jinsi, kama ni maji, tayari aliyavulia nguo na wakati huo alitakiwa kuyaoga, alichokifanya ni kuanza kupiga hatua kwenda mbele, alipofika karibu na mlango ule, vikapu vitatu vikaonekana mbele yake na ndani vilikuwa na majina ya watu watatu ambao alikuwa akiwapenda sana.
Hakujua ni kikapu gani kilikuwa na jina gani, alichotakiwa ni kuchagua tu kikapu pasipo kujua ndani kulikuwa na jina gani. Mapigo yake ya moyo yakaanza kudunda, alikuwa kwenye mtihani mgumu mno.
Watu wote watatu ambao alitajiwa alikuwa akiwapenda mno, ila hakuwa na jinsi kwa wakati huo, alitakiwa kuchagua kapu moja na mtu mmoja kufariki dunia, hivyo alitakiwa kufanya hivyo ili geti lifunguke.
Akakishika kikapu kimoja ambacho hakujua kulikuwa na jina gani, ghafla akahisi akianza kububujikwa na machozi ya uchungu, alipochungulia ndani, akakutana na jina la mama yake.
Akajikuta akipiga magoti na kuanza kukipiga kifua chake kwa maumivu makali.
“Uwiiiiiiiiiiii.....” alijikuta akianza kulia kwa sauti kubwa.
.
.
Je, nini kitaendelea?
Mzee Hamisi hakuwa na jinsi, kama ni maji, tayari aliyavulia nguo na wakati huo alitakiwa kuyaoga, alichokifanya ni kuanza kupiga hatua kwenda mbele, alipofika karibu na mlango ule, vikapu vitatu vikaonekana mbele yake na ndani vilikuwa na majina ya watu watatu ambao alikuwa akiwapenda sana.
Hakujua ni kikapu gani kilikuwa na jina gani, alichotakiwa ni kuchagua tu kikapu pasipo kujua ndani kulikuwa na jina gani. Mapigo yake ya moyo yakaanza kudunda, alikuwa kwenye mtihani mgumu mno.
Watu wote watatu ambao alitajiwa alikuwa akiwapenda mno, ila hakuwa na jinsi kwa wakati huo, alitakiwa kuchagua kapu moja na mtu mmoja kufariki dunia, hivyo alitakiwa kufanya hivyo ili geti lifunguke.
Akakishika kikapu kimoja ambacho hakujua kulikuwa na jina gani, ghafla akahisi akianza kububujikwa na machozi ya uchungu, alipochungulia ndani, akakutana na jina la mama yake.
Akajikuta akipiga magoti na kuanza kukipiga kifua chake kwa maumivu makali.
“Uwiiiiiiiiiiii.....” alijikuta akianza kulia kwa sauti kubwa.
.
.
Je, nini kitaendelea?

