Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
- Thread starter
- #41
30
Watu walizidi kukusanyika mahali pale wakiwasikiliza watu hao waliokuwa wakipeana vitisho kwamba yeyote angeweza kumuua mwenzake.
Hakukuwa na mtu aliyeingilia, labda kwa sababu wengi waliyafahamu maisha ya huyu mzee huyu aliyeitwa Hamisi tena huku wengine wakimsonta kidole kijana yule aachane naye lakini hakutaka kuacha, aliendelea kumwambia kwamba angeweza kumuua.
“Kijana anatafuta balaa, huyu mgeni nini?” aliuliza mzee mmoja.
“Si mgeni, ni mwenyeji kabisa.”
“Sasa kwa nini anampiga mkwara huyu mzee, hamjui nini?”
“Anamjua sana, si unajua hivi visifa vya vijana wetu,” alisema mzee mwingine.
Mzee Hamisi hakutaka kuzungumza sana, akaondoka na kuingia ndani huku akiwa amefura kwa hasira.
Kijana yule hakuondoka, alijiona kuwa bingwa na kuona mpinzani wake ameshindwa.
Alitukana na kutukana huku mikwara ikiendelea kusikika mdomoni mwake lakini mzee Hamisi hakurudi nje, aliendelea kubaki mulemule ndani kwake. Nakumbuka kijana yule alichukua zaidi ya dakika tano zaidi kutukana na kisha kuondoka.
Usiku ulipoingia, nikaanza kumuona mzee Hamisi akiwa kwenye mti mmoja mkubwa uliokuwa katikati ya uwanja mmoja mkubwa wa mpira. Mahali hapo alisimama peke yake na baada ya dakika kadhaa, kulikuwa na idadi kubwa ya watu waliofika uwanjani hapo.
Kila mtu alikuwa mtupu, haikujalisha kama ni mtu mzima, mtoto au kijana, uwe mwanaume au mwanamke, unapokuwa hapo ulitakiwa kuwa mtupu. Niliwaona wanawake wawili wakiwa wamebeba chungu kimoja kikubwa na kukipeleka mbele kabisa kisha mwanamke mmoja aliyeonekana kuwa mtu mzima kusogea karibu na kile chungu.
“Leo ni siku ya kuleta mahitaji yenu na kufanyiwa kazi,” alisema mwanamke yule, sauti yake ni kama ililazimishwa iwe ya kutisha.
Ngoja nikwambie kitu. Miongoni mwa mambo mengi niliyoambiwa na Yusnath ni kuhusu siku maalumu ambayo hutumika kwa ajili ya kupeleka mahitaji yao kwa ajili ya kufanyiwa kazi. Wachawi hutenga siku maalumu kwa ajili ya kufanyia kazi matatizo yao.
Watu walizidi kukusanyika mahali pale wakiwasikiliza watu hao waliokuwa wakipeana vitisho kwamba yeyote angeweza kumuua mwenzake.
Hakukuwa na mtu aliyeingilia, labda kwa sababu wengi waliyafahamu maisha ya huyu mzee huyu aliyeitwa Hamisi tena huku wengine wakimsonta kidole kijana yule aachane naye lakini hakutaka kuacha, aliendelea kumwambia kwamba angeweza kumuua.
“Kijana anatafuta balaa, huyu mgeni nini?” aliuliza mzee mmoja.
“Si mgeni, ni mwenyeji kabisa.”
“Sasa kwa nini anampiga mkwara huyu mzee, hamjui nini?”
“Anamjua sana, si unajua hivi visifa vya vijana wetu,” alisema mzee mwingine.
Mzee Hamisi hakutaka kuzungumza sana, akaondoka na kuingia ndani huku akiwa amefura kwa hasira.
Kijana yule hakuondoka, alijiona kuwa bingwa na kuona mpinzani wake ameshindwa.
Alitukana na kutukana huku mikwara ikiendelea kusikika mdomoni mwake lakini mzee Hamisi hakurudi nje, aliendelea kubaki mulemule ndani kwake. Nakumbuka kijana yule alichukua zaidi ya dakika tano zaidi kutukana na kisha kuondoka.
Usiku ulipoingia, nikaanza kumuona mzee Hamisi akiwa kwenye mti mmoja mkubwa uliokuwa katikati ya uwanja mmoja mkubwa wa mpira. Mahali hapo alisimama peke yake na baada ya dakika kadhaa, kulikuwa na idadi kubwa ya watu waliofika uwanjani hapo.
Kila mtu alikuwa mtupu, haikujalisha kama ni mtu mzima, mtoto au kijana, uwe mwanaume au mwanamke, unapokuwa hapo ulitakiwa kuwa mtupu. Niliwaona wanawake wawili wakiwa wamebeba chungu kimoja kikubwa na kukipeleka mbele kabisa kisha mwanamke mmoja aliyeonekana kuwa mtu mzima kusogea karibu na kile chungu.
“Leo ni siku ya kuleta mahitaji yenu na kufanyiwa kazi,” alisema mwanamke yule, sauti yake ni kama ililazimishwa iwe ya kutisha.
Ngoja nikwambie kitu. Miongoni mwa mambo mengi niliyoambiwa na Yusnath ni kuhusu siku maalumu ambayo hutumika kwa ajili ya kupeleka mahitaji yao kwa ajili ya kufanyiwa kazi. Wachawi hutenga siku maalumu kwa ajili ya kufanyia kazi matatizo yao.