Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 153,016
- 454,028
Mtunzi: Nyemo Chilongani
Sehemu ya 01
Nilisimama juu ya mlima mmoja mkubwa, mawingu yalitanda angani huku radi zikianza kupiga mfululizo hali iliyoonyesha muda wowote ule mvua kubwa ingenyesha.
Nilikuwa nikiogopa sana, pembeni ya mlima ule mkubwa ambao sikujua nilifikaje, kulikuwa na miti mingi iliyosababisha giza kuwa kubwa kitu kilichoniongezea hofu nzito moyoni mwangu.
Sikuwa na msaada wowote mahali hapo, nilijaribu kuangalia huku na kule nikiamini ningeweza kupata msaada lakini hakukuwa na mtu yeyote. Wakati nikijiuliza nilifikaje hapo, ghafla nikaanza kusikia vishindo vikubwa vikija kule nilipokuwa. Sikujua vilikuwa vishindo vya nani, nikabaki nikitetemeka kwani nilijua huo ndiyo ungekuwa mwisho wa maisha yangu.
Mwili wangu ulikuwa ukitetemeka sana, nilitamani kukimbia kutoka mlimani hapo lakini kitu cha ajabu, sikuweza kukimbia, miguu ilikuwa mizito kuinuka, hivyo nikabaki nikiwa nimesimama tu.
Ghafla, nikawaona watu zaidi ya ishirini wakija mbele yangu, walikuwa ni binadamu wa kawaida ila walikuwa na muonekano wenye kutisha sana. Walikuwa watupu, viunoni walivaa vitu kama ukili, nyuso zao hazikuwa zikionekana vizuri.
Walikuwa wakinisogelea huku wakicheza wimbo ambao sikujua ulitoka wapi. Walikuwa wakiniangalia huku wakichekacheka kama watu wasiokuwa na akili fulani. Walitisha, nilitamani kuyafumba macho ili nisiweze kuwatazama lakini nilipotaka kufanya hivyo, nilishindwa pia.
Nikabaki nikiwa nimesimama, dakika ziliendelea kwenda mbele, cha ajabu, idadi hiyo ya watu haikuishia ishirini tu bali iliendelea kuongezeka mpaka wakafika watu zaidi ya sitini.
Baada ya dakika kama thelathini hivi, nikawaona watu kadhaa wakija pale niliposimama huku wakiwa wameshika beseni kubwa, nilipochungulia ndani, niliona damu nzito za watu, zilikuwa mbichi kabisa na kila aliyekuwa akizingalia, alionekana kuzitamani.
“Umeshawahi kunywa damu wewe?” aliniuliza mwanamke mmoja mtu mzima, alikuwa na umri usiopungua miaka sabini, alikuwa hajiwezi lakini ndiye aliyeonekana kucheza kwa nguvu kuliko wote mahali hapo.
“Sijawahi kunywa damu, na siwezi kunywa,” nilisema kwa sauti tena kwa kujiamini sana.
Sehemu ya 01
Nilisimama juu ya mlima mmoja mkubwa, mawingu yalitanda angani huku radi zikianza kupiga mfululizo hali iliyoonyesha muda wowote ule mvua kubwa ingenyesha.
Nilikuwa nikiogopa sana, pembeni ya mlima ule mkubwa ambao sikujua nilifikaje, kulikuwa na miti mingi iliyosababisha giza kuwa kubwa kitu kilichoniongezea hofu nzito moyoni mwangu.
Sikuwa na msaada wowote mahali hapo, nilijaribu kuangalia huku na kule nikiamini ningeweza kupata msaada lakini hakukuwa na mtu yeyote. Wakati nikijiuliza nilifikaje hapo, ghafla nikaanza kusikia vishindo vikubwa vikija kule nilipokuwa. Sikujua vilikuwa vishindo vya nani, nikabaki nikitetemeka kwani nilijua huo ndiyo ungekuwa mwisho wa maisha yangu.
Mwili wangu ulikuwa ukitetemeka sana, nilitamani kukimbia kutoka mlimani hapo lakini kitu cha ajabu, sikuweza kukimbia, miguu ilikuwa mizito kuinuka, hivyo nikabaki nikiwa nimesimama tu.
Ghafla, nikawaona watu zaidi ya ishirini wakija mbele yangu, walikuwa ni binadamu wa kawaida ila walikuwa na muonekano wenye kutisha sana. Walikuwa watupu, viunoni walivaa vitu kama ukili, nyuso zao hazikuwa zikionekana vizuri.
Walikuwa wakinisogelea huku wakicheza wimbo ambao sikujua ulitoka wapi. Walikuwa wakiniangalia huku wakichekacheka kama watu wasiokuwa na akili fulani. Walitisha, nilitamani kuyafumba macho ili nisiweze kuwatazama lakini nilipotaka kufanya hivyo, nilishindwa pia.
Nikabaki nikiwa nimesimama, dakika ziliendelea kwenda mbele, cha ajabu, idadi hiyo ya watu haikuishia ishirini tu bali iliendelea kuongezeka mpaka wakafika watu zaidi ya sitini.
Baada ya dakika kama thelathini hivi, nikawaona watu kadhaa wakija pale niliposimama huku wakiwa wameshika beseni kubwa, nilipochungulia ndani, niliona damu nzito za watu, zilikuwa mbichi kabisa na kila aliyekuwa akizingalia, alionekana kuzitamani.
“Umeshawahi kunywa damu wewe?” aliniuliza mwanamke mmoja mtu mzima, alikuwa na umri usiopungua miaka sabini, alikuwa hajiwezi lakini ndiye aliyeonekana kucheza kwa nguvu kuliko wote mahali hapo.
“Sijawahi kunywa damu, na siwezi kunywa,” nilisema kwa sauti tena kwa kujiamini sana.