Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,081
- 464,013
- Thread starter
- #101
77.
Alizidi kuyatamka maneno yale, alipoona kwamba hayatoshi tu, akaanza kuchukua karatasi zenye maneno yale, akachukua na unga fulani kisha kuuweka katika karatasi ile na kuanza kumpulizia Ramadhani kitu kilichomchanganya vilivyo, hapohapo akaanguka chini na mapovu kuanza kumtoka mdomoni na puani.
Huo ulikuwa ushindi mkubwa ambao hakutarajia kuupata kabla, mtu ambaye alimsumbua kwa kipindi klirefu, leo hii, tena usiku huu alikuwa hoi pale chini. Kwake, hiyo iliendelea kuwa furaha, kubwa, alichokifanya ni kupotea, na ghafla akaibukia katika uwanja wa wachawi wenzake, wote waliomuona, wakaanza kutetemeka akiwemo mkubwa wao.
Nguvu alizokuja nazo mzee Hamisi zilikuwa kubwa mno, uwanjani hapo walikuwa na kiongozi wao lakini naye alipomuona mzee Hamisi akiingia, akajikuta akitetemeka, hofu ikamjaa na mwisho wa siku, wote kwa pamoja akiwemo yeye kiongozi wakapiga magoti chini kama ishara ya kumpa heshima.
Huo nao ukawa ushindi mkubwa, kule kuzimu alipokwenda, alipewa nguvu za ajabu ambazo hakuamini kama angeweza kuzipata katika maisha yake.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kila kitu, mzee Hamisi akawa kiongozi wa wachawi lakini huyohuyo ndiye alikuwa hakosi msikitini. Alikuwa mtu wa swala tano, aliheshimika mno pasipo watu kujua kwamba mtu huyo alikuwa mkubwa wa wachawi na alikuwa na nguvu mno za kichawi.
Hiyo ndiyo stori ya mzee Hamisi niliyotaka kukupa, alikuwa miongoni mwa watu niliokutana nao kule kuzimu. Walikuwa watu wengi sana, wote hao walikuwa wakimuabudu shetani ambaye alikuwa mbele yao.
Ukiachana na mzee Hamisi, yule mchungaji na mwanasiasa ambao wote niliwapeni sifa zao, kulikuwa na msichana mmoja hivi, msichana mrembo kwa kumwangalia, aliyekuwa na figa matata sana, naye huo alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa humo.
Kwa kumwangalia, mwanaume yeyote aliye rijali asingeweza kumuacha, alivutia, alikuwa na umbo namba nane, sura nyembamba na kifuani alionekana kama msichana aliyetoka kuvunja ungo siku si nyingi.
Sikuwa nikimfahamu, sikuwahi kumuona kabla lakini Yusnath aliniambia kwamba msichana huyo aliitwa Esta.
Alizidi kuyatamka maneno yale, alipoona kwamba hayatoshi tu, akaanza kuchukua karatasi zenye maneno yale, akachukua na unga fulani kisha kuuweka katika karatasi ile na kuanza kumpulizia Ramadhani kitu kilichomchanganya vilivyo, hapohapo akaanguka chini na mapovu kuanza kumtoka mdomoni na puani.
Huo ulikuwa ushindi mkubwa ambao hakutarajia kuupata kabla, mtu ambaye alimsumbua kwa kipindi klirefu, leo hii, tena usiku huu alikuwa hoi pale chini. Kwake, hiyo iliendelea kuwa furaha, kubwa, alichokifanya ni kupotea, na ghafla akaibukia katika uwanja wa wachawi wenzake, wote waliomuona, wakaanza kutetemeka akiwemo mkubwa wao.
Nguvu alizokuja nazo mzee Hamisi zilikuwa kubwa mno, uwanjani hapo walikuwa na kiongozi wao lakini naye alipomuona mzee Hamisi akiingia, akajikuta akitetemeka, hofu ikamjaa na mwisho wa siku, wote kwa pamoja akiwemo yeye kiongozi wakapiga magoti chini kama ishara ya kumpa heshima.
Huo nao ukawa ushindi mkubwa, kule kuzimu alipokwenda, alipewa nguvu za ajabu ambazo hakuamini kama angeweza kuzipata katika maisha yake.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kila kitu, mzee Hamisi akawa kiongozi wa wachawi lakini huyohuyo ndiye alikuwa hakosi msikitini. Alikuwa mtu wa swala tano, aliheshimika mno pasipo watu kujua kwamba mtu huyo alikuwa mkubwa wa wachawi na alikuwa na nguvu mno za kichawi.
Hiyo ndiyo stori ya mzee Hamisi niliyotaka kukupa, alikuwa miongoni mwa watu niliokutana nao kule kuzimu. Walikuwa watu wengi sana, wote hao walikuwa wakimuabudu shetani ambaye alikuwa mbele yao.
Ukiachana na mzee Hamisi, yule mchungaji na mwanasiasa ambao wote niliwapeni sifa zao, kulikuwa na msichana mmoja hivi, msichana mrembo kwa kumwangalia, aliyekuwa na figa matata sana, naye huo alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa humo.
Kwa kumwangalia, mwanaume yeyote aliye rijali asingeweza kumuacha, alivutia, alikuwa na umbo namba nane, sura nyembamba na kifuani alionekana kama msichana aliyetoka kuvunja ungo siku si nyingi.
Sikuwa nikimfahamu, sikuwahi kumuona kabla lakini Yusnath aliniambia kwamba msichana huyo aliitwa Esta.
