Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,076
- 463,978
- Thread starter
- #21
12
Kanisa lilianza kama utani, nakumbuka kipindi kile kulikuwa na washirika kama wanne, watu wengi waliokuwa wakipita karibu na kanisa lile, walishangaa ilikuwaje mchungaji awe na nguvu ya kutoa huduma na wakati watu walikuwa wachache sana.
Watu tulipuuzia, mchungaji yule ambaye alipenda sana kujiita mtume akaanza kuchapisha matangazo na kuyabandika mitaani kwamba alikuwa akiponya magonjwa mbalimbali, wanawake waliokuwa tasa waliitwa pia kwa ajili ya kuwekewa mikono na kupokea uponyaji.
Hilo halikuwafanya watu kulisogelea kanisa lile kwani kitu walichohitaji ni kuona miujiza ili waamini. Baada ya mwezi mmoja, watu walewale wanne waliokuwa ndani ya kanisa lile wakaanza kuwaambia watu wengine kwamba kulikuwa na miujiza ilikuwa ikitendeka hivyo watu wawapeleke wagonjwa kwa mchungaji yule.
Kama unavyojua binadamu kuna kitu kujaribu. Kuna mwanamke aliyekuwa akiishi karibu na mtaa uliokuwa na kanisa lile, miaka nenda rudi alikuwa na kibiongo. Watu walimuonea huruma lakini baada ya kusikia kile kilichozungumziwa kuhusu mchungaji na miujiza aliyotarajiwa kuitoa, mwanamke yule akaingia.
Sijui nini kilitokea kanisani lakini siku moja baadae nilipomuona mwanamke yule, hakuwa na kibiongo. Hapo ndipo watu walipoanza kuamini kwamba ile miujiza iliyokuwa ikitangazwa kweli ilikuwa ikifanyika, kanisa likaanza kujaza watu.
“Nilifahamu hilo tu, hebu niambie kingine nisichokijua,” nilimwambia Yusnath.
“Subiri,” aliniambia na kunipeleka sehemu iliyokuwa na kitu kikubwa kama televisheni na kuanza kunionyeshea maisha halisi ya mchungaji yule.
Lile kanisa halikuwa kanisa kama tulivyokuwa tukiliona, lilikuwa pango kubwa ambalo lilikuwa na muonekanao wa kichwa cha paka, mlangoni kulikuwa na miti mikubwa iliyokuwa imesimikwa huku juu yake kukiwa na mafuvu mawili ya binadamu na mafuvu mengine ya mnyama nisiyemfahamu.
Mlangoni hapo kulikuwa na mtungi mkubwa wa damu, kila mshirika aliyekuwa akiingia kanisa, ilikuwa ni lazima kuinama mlangoni kisha kuingia. Unapoinama pale mlangoni, unauinamia ule mtungi bila kujua na katika hali ambayo sikuifahamu, kuna kiasi kidogo cha damu unachangia katika mtungi ule.
Kanisa lilianza kama utani, nakumbuka kipindi kile kulikuwa na washirika kama wanne, watu wengi waliokuwa wakipita karibu na kanisa lile, walishangaa ilikuwaje mchungaji awe na nguvu ya kutoa huduma na wakati watu walikuwa wachache sana.
Watu tulipuuzia, mchungaji yule ambaye alipenda sana kujiita mtume akaanza kuchapisha matangazo na kuyabandika mitaani kwamba alikuwa akiponya magonjwa mbalimbali, wanawake waliokuwa tasa waliitwa pia kwa ajili ya kuwekewa mikono na kupokea uponyaji.
Hilo halikuwafanya watu kulisogelea kanisa lile kwani kitu walichohitaji ni kuona miujiza ili waamini. Baada ya mwezi mmoja, watu walewale wanne waliokuwa ndani ya kanisa lile wakaanza kuwaambia watu wengine kwamba kulikuwa na miujiza ilikuwa ikitendeka hivyo watu wawapeleke wagonjwa kwa mchungaji yule.
Kama unavyojua binadamu kuna kitu kujaribu. Kuna mwanamke aliyekuwa akiishi karibu na mtaa uliokuwa na kanisa lile, miaka nenda rudi alikuwa na kibiongo. Watu walimuonea huruma lakini baada ya kusikia kile kilichozungumziwa kuhusu mchungaji na miujiza aliyotarajiwa kuitoa, mwanamke yule akaingia.
Sijui nini kilitokea kanisani lakini siku moja baadae nilipomuona mwanamke yule, hakuwa na kibiongo. Hapo ndipo watu walipoanza kuamini kwamba ile miujiza iliyokuwa ikitangazwa kweli ilikuwa ikifanyika, kanisa likaanza kujaza watu.
“Nilifahamu hilo tu, hebu niambie kingine nisichokijua,” nilimwambia Yusnath.
“Subiri,” aliniambia na kunipeleka sehemu iliyokuwa na kitu kikubwa kama televisheni na kuanza kunionyeshea maisha halisi ya mchungaji yule.
Lile kanisa halikuwa kanisa kama tulivyokuwa tukiliona, lilikuwa pango kubwa ambalo lilikuwa na muonekanao wa kichwa cha paka, mlangoni kulikuwa na miti mikubwa iliyokuwa imesimikwa huku juu yake kukiwa na mafuvu mawili ya binadamu na mafuvu mengine ya mnyama nisiyemfahamu.
Mlangoni hapo kulikuwa na mtungi mkubwa wa damu, kila mshirika aliyekuwa akiingia kanisa, ilikuwa ni lazima kuinama mlangoni kisha kuingia. Unapoinama pale mlangoni, unauinamia ule mtungi bila kujua na katika hali ambayo sikuifahamu, kuna kiasi kidogo cha damu unachangia katika mtungi ule.
niacheee