Simulizi: Nyumba Iliyojaa Dhambi

Simulizi: Nyumba Iliyojaa Dhambi

SEHEMU YA 44

Siku hiyo ilikuwa ni ya kipekee sana kati yangu na Nurat. Tulitulia ndani kwa zaidi ya saa moja na baada ya kumaliza, akaondoka kuelekea kwao huku akionekana kuwa na furaha mno.
Aliniambia ukweli kwamba tangu azaliwe hakuwahi kukutana na mwanaume aliyekuwa na nguvu kama mimi.

Nilishangaa sana, nikajiuliza maswali mengi mno kuhusu vijana wa Dar, sikujua tatizo lilikuwa nini ndiyo maana biashara ya mchuzi wa pweza ilikuwa kubwa sana Dar es Salaam kwa kuwa hawakuwa siriazi faragha.

Nurat hakuniacha mikono mitupu, akanipa na pesa za matumizi, nakumbuka ilikuwa ni zaidi ya shilingi laki moja ambayo yote nilimtumia Zamaradi kwa kuwa niliona kwangu si kitu kwa kuwa nilikuwa na zaidi ya bilioni.

Maisha yangu yaliendelea, baada ya kuinunua nyumba ya akina Zamaradi nikafanya mpango wa kununua kiwanja tegeta ambapo huko nikaanza kujenga.

Nilitaka kuwa na nyumba kubwa, yenye kila kitu ndani kwa mtu yeyote ambaye angefanikiwa kuingia basi ajue kweli aliingia kwenye moja ya nyumba kali sana hapa Afrika.

Baada ya kukamilisha kununua kiwanja, nikapanga mipango yangu ya kujenga jumba hilo la kifahari, nikanunua ramani ya nyumba yenyewe lakini tatizo moja ni kwamba kiwanja kilikuwa kidogo na nyumba niliyoitaka ni kubwa mno.

“Hiki kiwanja cha nani?” nilimuuliza mwenyekiti wa mtaa ambaye naye alifanya kazi ya udalali wa viwanja huko tegeta. Nilimuulizia kiwanja kilichopakana na changu.

“Kuna mwanamke mmoja hivi anafanyaga biashara za kwenda Dubai, ndiye mwenye kiwanja hiki,” alinijibu.
“Mi nataka nikinunue, anauza kiasi gani?” nilimuuliza.

“Mmh! Sidhani kama atauza, aliniambia kwamba anataka kuja kujenga hapa mwaka huu na mafundi kashatafuta,” alinijibu.

Nilijua tu kwamba ningefanikiwa kununua kiwanja chake kama tu ningeonana naye. Nilimwambia mzee huyo aliyeitwa kwa jina la Hamadi kwamba aniunganishe naye ili nizungumze kwani nilihitaji mno kuwa na kiwanja chake.
 
SEHEMU YA 45

Hilo halikuwa tatizo, akakubali na hivyo kunipa namba yake ya simu. Nilimpigia siku hiyohiyo na kujitambulisha, nilimwambia kwamba nilikuwa na shida ya kuzungumza naye hivyo kama lingekuwa jambo jema basi tukutane sehemu na kuonana.

Hakukuwa na tatizo, baada ya saa moja tukaonana katika Mgahawa wa KFC uliokuwa Mikocheni na kuanza kuzungumza.

Alikuwa mwanamke mtu mzima kidogo lakini kwa jinsi alivyoonekana, alipenda mno mambo ya ujana. Kichwani alikuwa na wigi la Peruvian, vidoleni aliweka kucha za bandia, alivaa viatu virefu huku akiwa na sketi fupi ambayo ilipanda mpaka juu ya mapaja.

Pamoja na ugwadu wangu kwa watoto wa kike lakini huyu mwanamke hakunivutia hata kidogo. Alijitahidi hata kukibusti kifua chake lakini yote hayo yaligonga mwamba mbele yangu.

“Naitwa Edward,” nilimwambia huku nikitoa tabasamu, tena kwa kumuonyeshea heshima, kwa kuwa alinikuta hapo, nikasimama na kumpa mkono.

“Naitwa Miss Maria,” aliniambia.
Sikutaka nimwambie moja kwa moja kuhusu mpango wangu, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kuzoeana kwanza ili hata nitakapomgusia suala langu kusiwe na tatizo lolote lile.

“Ila umependeza sana! Unaonekana kama binti wa miaka kumi na nane,” nilimwambia, kwa kifupi nilikuwa nikimpaka mafuta kwa kutumia mgongo wa chupa.

“Ahsante sana! Yaani nimetoka Dubai, nimechoka, nilipanga leo niende kulala pale Serena Hotel lakini daah! Simu yako ikanifanya nije kwanza kuzungumza na wewe,” aliniambia, hapo tu nikapata picha kwamba alikuwa mwanamke wa kupenda sifa, na mimi kumjaza mtu ndiyo zangu, nikaanza kumpampu ili aendelee kujisifia.
“Nilisikia kwamba unafanya biashara!” nilimwambia.

“Yeah! Ofcourse nafanya. Unajua maisha haya ya ajabu sana. First day kwenda Dubai, nilishangaa sana, unajua it was like surprise kwangu, yaani majengo ya kule ni balaa.

It came a time mpaka nikawa najiuliza hivi nilifika peponi ama bado nipo hapa duniani?” alijigamba.
“Duuh! Kwa hiyo hata China ushafika kwenda kuchukua bidhaa?”
 
SEHEMU YA 46

“Yaani huko ndiyo nakwenda kama kariakoo vile, I’m just flying anytime ninayotaka,” aliniambia.

“Hebu niambie kwanza China kupo vipi, yaani nataka nijue bhana,” nilimwambia kwa lengo la kumfanya aendelee kujisifia kama alivyofanya.

Nyie hapa duniani kuna watu wanajua kujisifia, aliniambia mambo mengi, sijui alikwenda China, alifanya biashara nyingi mpaka akakutana na Jack Ma, yule bilionea wa China.

Nilibaki nikizisikiliza tu pingu alizokuwa akinifunga, hakujua kama mimi ni mjanja basi akajiona anajua sana kumbe na mimi nilikuwa na tageti zangu.

“Daah! Kati ya watu waliofanikiwa, wewe ni mwanamke wa chuma,” nilimwambia.
“Yaani usione hivi. Maisha haya nisingepambana hata gari nisingenunua.”

“Naona jitihada zako, umekuja na Verrosa new model.”
“Kuna nyingine nimeiacha nyumbani, ni Range SUV. Niliinunua kwa kuiagiza kutoka Japan, ila siipendi kwa kuwa ipo juu juu sana.

Mimi napenda kama Verrosa. Kuna Hammer moja niliagiza, nikaona kama it is not my type, nikampa my young sister, naye ikamshinda manake inakula sana mafuta, she sold it,” aliniambia.

Kwanza nikashusha pumzi ndefu, nilitamani kucheka lakini nikapiga moyo konde niendelee kumsikiliza. Alinipiga sana fiksi na mwisho wa siku nikaanza kumwambia kuhusu mpango wangu.

Alinisikiliza, kwa jinsi nilivyoonekana tu alinichukulia kawaida sana kwa kuwa nilivalia kikawaida mno. “Unataka kununua kiwanja changu?” aliniuliza.

“Ndiyo! Natamani niwe nacho, kimekaa sehemu nzuri kidogo,” nilimwambia.
“Una hela? Mimi mwenzio Mchaga, pesa mbele kama tai,” aliniambia.

“Sina hela ya kutosha, kwani unakiuza kiasi gani?”
“Milioni kumi!”
“Milioni kumi?” niliuliza kwa mshtuko.
“Ndiyo!”

Kwanza nikabaki kimya, nilikuwa na pesa lakini haikuwa ya kutumia hovyo kiasi hicho, kama kweli alikuwa akikiuza kwa bei hiyo inamaana kwamba nisingeweza kununua kwa sababu tu nilijiandaa kukinunua kwa shilingi milioni tano tu.

Huyu mwanamke aliyeitwa Maria japokuwa alikuwa mtu wa sifa lakini namsifu sana kwa kuwa alikuwa na akili mno. Unajua kwa nini? Ngoja nikwambie kilichotokea hapo baada ya kuona nasitasita kutoa milioni kumi.
 
SEHEMU YA 47

Akapiga simu sehemu na kuanza kuongea na mtu mmoja na kumwambia kwamba alitaka kuonana naye na ingekuwa vizuri kama wangekuja wote wawili, sikujua hao walikuwa akina nani lakini kwa jinsi alivyokuwa akiongea, alionekana kuwa mtu fulani ambaye alizoeana naye sana.

Akanihamisha kabisa kutoka kwenye suala la kiwanja na kuzungumza mambo mengine ya kujifagilia kama kawaida yake.

Tuliendelea na mazungumzo kama nusu saa hivi ndipo nikaona gari fulani aina ya IST ikipaki na milango ilipofunguliwa, aisee waliteremka wasichana warembo ile balaa.

Naweza kusema kwamba hao ndiyo walikuwa mademu wa viwanja, waliofaa kuishi jijini Dar es Salaam na kwenda kwenye Ukumbi wa Element kama ilivyokuwa kwa wengine warembo.

Walitembea kwa mwendo wa maringo mno kana kwamba hii ardhi waliyokuwa wakiikanyaga haijawahi kuchimbiwa choo. Walinata na walikuwa wakali ile kinoma, Maria akasimama na kuwafuata, akawapokea na kuwaleta palepale.

Nilishindwa kubaki kimya, mimi mwenyewe mdhaifu kwa watoto wa kike hivyo kila nilipokuwa nikiwaangalia, moyo wangu uliniambia ‘Hawa unapiga, ukishindwa utakuwa mzembe sana’.
Akanitambulisha.

Mmoja aliitwa Doreen. Huyu alikuwa mwembamba kama Miss Tanzania, mweupe, alipokuwa akitabasamu vishimo viwili vilikuwa vikionekana mashavuni mwake, sura nyembamba na kitovuni alitoboa kipini kitu kilichonichanganya sana.

“Hi Doreen,” nilimsalimia huku nikimshika mkono, ulikuwa lainiiiiiiiiii.
“Hi!”

“Naitwa Edward!” nilijitambulisha.
“Ahsante kwa kukufahamu love,” aliniambia, akanishtua kishenzi, yaani kidogo tu nishaanza kuitwa love.

“Na huyu anaitwa Amanda,” aliniambia.
Huyo Amanda naye alikuwa mkali ile balaa, sura yake ilikuwa pana kidogo lakini alikuwa na sura ya kitoto mno, alijaajaa na huku nyuma ilikuwa si mchezo, yaani yangekuwa yale mambo yetu angewekwa kwenye kipengele cha ‘Big Booty’.

“Hi Amanda!”
“Hi Baby love,” naye akanirudishia.
Mpaka hapo nilishapagawa kinoma. Muda wote huyo Maria alikuwa akiniangalia tu, alikwishajua kwamba nilipagawa hivyo akaanza kuniambia kuhusu ishu ya kiwanja.

“Kwa hiyo bwana mimi kiwanja nauza milioni kumi, upo tayari?” aliniuliza.
 
SEHEMU YA 48

Yaani hili swali nililiona la kitoto sana, mbele ya mademu wakali kama wale, niseme milioni kumi sina si ungekuwa ujinga huo?

Huo ndiyo ujanja alioutumia, aliamini kwamba kama angewaita wanawake hao wauri, kidume mimi ningekubaliana na bei yake kwa sababu nisingetaka kujishusha, na kweli nikakubaliana naye.

Yaani milioni kumi ikanitoka na kukubali kulipana siku hiyohiyo, yaani kila kitu ningemalizana naye siku hiyo. Baada ya kukubaliana, tukaenda benki huku nikiongozana na wote watatu na tulipomaliza tukaenda kwenye kiwanja na kukinunua.

“Aya sasa! Kazi kwako,” aliniambia Maria.
“Kivipi sasa mbona sijakuelewa!”
“Au hutaki niwaambie warudi?” aliniuliza.
Hapo nikapata jibu alimaanisha nini.

Nisingekuwa mjinga kumwambia sikutaka na hivyo warudi. Mshikaji wangu ninapokwambia kwamba nilikuwa na mambo ya kishetani sana niamini tu, kwa sasa nimebadilika kwa sababu tu nimeoa na nina familia yangu nyumbani.

“Kwa hiyo wote wawili?”
“Yeah! Threesome! Au hutaki?” aliniuliza.
“Mbona umeng’ang’ania sitaki tu!”
“Hahaha! Kazi kwako! Ila wanaendaga hotelini tu hao,” aliniambia.

“Hilo pia si tatizo.”
Kuna wakati kipindi hicho nilikuwa najiambia kwamba kwenye ujana wako ndipo ambapo unatakiwa kufanya ujinga wote unaotaka kuufanya ili ukiwa mzee utulie.

Leo unakutana na wazee, vitambi vina vinyweleo mpaka vimeota mvi lakini bado wanataka watoto wadogo, yaani hii inamaanisha kwamba ujana wao hawakuufaidi kwa kufanya ushenzi kama huu na ndiyo maana zama hizo zilianza kujirudi kwao.

Mimi nilitaka nifanye yote ili hata siku moja mtu akinifuata na kuniuliza kama niliwahi kufanya ushenzi huu na huu basi nimwambie nilifanya na sikuona faida yoyote ile.

Wanawake wawili ndani ya kitanda kimoja, mambo hayo niliwahi kuyaona kwa Wazungu tu lakini si huku Tanzania.

Basi nikakubaliana nao, wakaniambia niwapoze tu elfu hamsini kila mmoja, chakula na pesa ya nauli, nikawaambia poa, pesa si tatizo, tatizo ni wao tu kunipa huduma ya kitu moyo inataka.
 
SEHEMU YA 49

Tukaondoka na kuelekea hotelini. Nilijiona Mfalme Mswati. Niliona hotelini mbali, wakati mwingine nilitamani hata kupiga picha na kuwaonyeshea Watanzania wote kwamba si mnaona sasa nilivyo? Si mnaona jinsi ninavyoondoka na watoto wawili?

Tulipofika hotelini tukaingia, sikutaka kuchelewa, mambo yakaanza mara moja huku nikionekana kuwa na kasi kama Hussein Bolt.

Nilitaka kuwaonyeshea kwamba hela ya mwanaume haiendi bure, ilikuwa ni lazima wailipie na ndicho kilichotokea. Ilichukua masaa matatu, wote wakawa hoi.

“Wewe mtu balaa!” aliniambia Doreen huku akiniangalia kwa mshangao, pamoja na mambo yake machafu lakini alikiri kwamba hakuwahi kukutana na mimi.
“Balaa langu lipi sasa?”

“Utadhani siyo mwanaume wa Dar!” alidakia Amanda.
“Kwa hiyo mnaniambiaje? Mmeshakula laki moja yangu na huduma mliyonipa ni ya shilingi elfu sitini tu, kuna ya arobaini imebaki huko kwenu,” nilimwambia.

“We kaka utatuua!”
“Basi nawaongezeni, mimi mpaka niridhike!”
“Kwani hujaridhika tu?”
“Bado hata kidogo!” niliwaambia.

Niliongea kama masihara lakini nilimaanisha, ni masaa matatu lakini ilionekana kama nusu saa kwangu. Filimbi ikapigwa tena na wachezaji kuingia uwanjani.

Watu walikuwa wakihema kama mbwa, mpira wa siku hiyo ilikuwa balaa, viungo walikuwa wakimiliki mpira kwa kasi kubwa, kila ulipokuwa ukitoka, mpira mwingine ulirushwa ndani kuonyesha kwamba siku hiyo ilikuwa ni ya kazi tu, wachezaji wasiokuwa na uwezo wa kumaliza dakika tisini hawakutakiwa kucheza mechi hiyo.

Nakumbuka tuliingia majira ya saa kumi jioni na waliondoka pale saa tano usiku, niliwang’ang’aniza walale, wakakataa kabisa.

“Nitawapeni milioni moja kila mtu!”
“Hapana! Hata ukinipa milioni hamsini silali! Mwanaume gani hutosheki!” aliniambia Doreen.

“Jamaniiiiiiii....”
“Aku! Tena usiniguse,” aliniambia Doreen manake alishaona mkono wangu ulianza kumletea shobo.

Nikaachana nao, wakaondoka na mimi kulala hotelini.

Asubuhi ilipofika, baba yake na Zamaradi akaniambia kwamba siku hiyo ndiyo walitaka kuhama hivyo nilitakiwa kuonana naye.
 
SEHEMU YA 50

Halikuwa tatizo, tukaonana, tukaongea na siku hiyo kuhama na hivyo kuanza kuirekebisha nyumba ile kwa kuvunja baadhi ya sehemu na kuboresha sehemu nyingine kuwa na mvuto zaidi.

Nilikuwa na pesa, niliitengeneza kwa wiki moja tu, ikawa nzuri mno kiasi kwamba kila mtu aliyekuwa akiiangalia aliipenda kupita kawaida kutokana na mapambo yake yaliyokuwa kwa nje.

Kwa ndani niliamua kufanya kufuru, nilitaka nipafanye kuvutie, yaani msichana yeyote ambaye angeingia basi awe anatamani tu kuolewa na mimi ili aishi humo.

Ilitumia siku kadhaa kila kitu kikakamilika.

Nilichokuwa nikihitaji nilikipata, nilichokifanya kingine ni kununua coaster tatu ambazo zilianza kufanya biashara, nikanunua bajaj tano, bodaboda ishirini lakini pia nikaamua kuwekeza zaidi kwenye kilimo ambapo nilisafiri mpaka Mbeya na kununua shamba la hekari ishirini na hivyo kuanza kupanda mpunga.

Haikuishia hapo bali kingine nilichokifanya ni kuwekeza kwenye ardhi, nikajenga nyumba nyingine mbili na kuzipangisha kwa pesa ndefu, ndani niliwawekea kila kitu na malipo yake nilihitaji yafanyike kwa dola kwani niliweka mazingira fulani kama nyumba za Wazungu ambao ndiyo walikuwa lengo langu kuwapata ndani ya nyumba hizo mbili kubwa.

Kwa kila mwezi, kodi yake ilikuwa ni dola elfu moja, zaidi ya milioni mbili na nilianza kupata wateja wengi hasa Wazungu waliokuwa wakija huku kwa mambo yao ya utalii kwa kuwa kiasi hicho kwao kilikuwa kidogo mno. Ndiyo hivyo nikawa naingiza pesa.

“Hii nyumba itajaa dhambi sana! Yaani humu, hata mke wa mbunge akijipindua, tutalaumiana,” nilisema huku nikiwa kitandani.

Watu wa kwanza walionijia kichwani ni Halima na Shamila, sasa zake na Issa, nianze nao halafu niende kwa huyo demu wake, hata kama alikuwa amemuoa, kwanza ilikuwa ni lazima nifanye yangu.
*
*
*
JE, nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom