Simulizi: Nyumba Iliyojaa Dhambi

Simulizi: Nyumba Iliyojaa Dhambi

SEHEMU YA 36

Nilijua kwamba unapotoka kuchukua pesa nyingi benki na unapotoka, huwa kuna watu wanakufuata kwa ajili ya kukuua na kukuibia pesa, sasa kwa sababu nilikuwa mjanja, nilitaka niwachezee mchezo mpaka washangae.

Nilihitaji kiasi hicho cha pesa, niliambiwa nisubiri wakati wakiendelea kufanya process za mimi kupata kiasi hicho cha pesa. Baada ya saa moja, nikapewa na kuanza kuondoka.

Hapo benki, unapotoka, kwa kuwa ipo kwenye ghorofa refu, kabla ya kwenda nje kuna lifti, hivyo nilichokifanya ni kwenda kwenye lifti kama ninataka kwenda juu, humo ndani, nikabadilisha nguo zangu na kuchukua zilizokuwa kwenye begi, nikavaa na kofia kabisa kisha kuteremka kutoka kwenye lifti na kuchukua nyingine, nikaanza kushuka.

Nilitoka huku nikiwa na muonekano mwingine kabisa.

Kwa kawaida sehemu hiyo si ya kupaki bodaboda, ila kwa mbali niliwaona vijana wawili, walikuwa na elementi, walisimama pembeni ya bodaboda yao huku wakiangalia kule kwenye jengo lile la benki, nikajua tu kwamba walitonywa kuna mtu ametoa milioni tisini hivyo walitakiwa kunifanyia uninja, kumbe hawakujua kama mimi mwenyewe nilikuwa ninja.

Nikawaacha wakiendelea kumsubiri mtu aliyevalia suruali ya kitambaa na fulana nyekundu, kumbe huyu aliyetoka ambaye alivalia pensi ya jinsi, fulana ya bluu na kofia nyeusi na kubeba begi ndiye mtu ambaye walitakiwa kumfuata, ila kwa kuwa hawakugundua kutokana na maelekezo waliyopewa kuwa tofauti na jinsi nilivyokuwa, nikawa huru kuondoka bila kufuatwa na yeyote yule.
Nimejifunza kitu hapa,,, asante mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom