SEHEMU YA 35
“Ndiyo! Mwili wako una joto tamu sana, yaani nilivyokukumbatia , nilihisi raha kama nimeona mlango wa pepo.
Zamaradi, unaufanya moyo wangu udunde, ndum ndum ndum....” nilimwambia.
“Jamaniiiiii”
“Wewe u mzuri mno, una tabasamu zuri, una meno mazuri, macho ya goroli, Zamaradi, umeumbika, unajua kucheka, una sura ya kitoto, umejazia, Zamaradi, hakika hakuna mwanaume anayeweza kukuacha akikupata,’ nilimwambia kwa kumchombeza.
“Jamaniiiii! Nasikia aibu huko!” aliniambia kwa kasauti kake ka kubembeleza.
“Zamaradiiiiiiii....nipo radhi nikose kila kitu, yaani pesa, kuingia peponi, nikose furaha lakini nisikukose wewe, ni mwanamke wa kipekee sana, ni mwanamke unayehitaji kuwa na furaha muda wote, unahitaji kutabasamu, kujaliwa, kusikilizwa, ni mwanamke unayetakiwa kuwa kwenye ulimwengu wako wa kipekee, Zamaradi, katika dunia hii hakuna mwanamke mzuri kama wewe,” nilimwambia, nilimsifia sana.
“Jamaniiiiiiiiiii” aliniambia, nahisi muda huo alikuwa aking’ata kidole chake.
“Zamaradi mpenzi, naomba ufungua mikono yako, unikumbatie, nikubusu, nikuonyeshee jinsi ulimwengu wa mapenzi ulivyo, nikaribishe mpenzi, nionje radha ya mate yako kwa mara nyingine,
Zamaradi, kuwa mama wa watoto wangu,” nilimwambia kwa sauti ile tamu kabisa.
“Kwani hujaoa bebi?” “Ningeoaje na wakati sikuwa nimeonana nawe? Zamaradi! Be mine mamiiiiii, unautetemesha moyo wangu....let me love you senyorita,” niliendelea kumchombeza.
Siku hiyo ndiyo nikaamini kwamba na mimi mkali kwenye maneno matamu, nilimfanya Zamaradi ajisikie kuwa mwanamke mzuri kuliko Mila Kunis, nilimwaminisha kwamba moyoni mwangu hakukuwa na yeyote yule.
Siku hiyo nilikesha nikiongea naye tu. Sijui alikuwa na bwana au peke yake, kitu nilichokuwa nikikiangalia ni mimi kuwa naye tu.
Nakumbuka siku hiyo nililala majira ya saa saba na asubuhi nikapanga kwenda benki.
Ilipofika, nikachukua begi langu na kwenda benki kwa lengo la kuchukua pesa hizo. Nilihitaji kuchukua milioni tisini kwani nilijua kungekuwa na dharura.
Sikutaka kwenda na dalali, nilikwenda peke yangu. Niliingia benki nikiwa na begi langu lililokuwa na nguo ndani, unajua kwa nini? Kwa sababu ya kubadilisha.