Simulizi: Nyumba Iliyojaa Dhambi

SEHEMU YA 37

Siku hiyohiyo nikamtafuta dalali na kumwambia kuhusu mzigo niliokuwa nimechukua, hakukuwa na kitu cha kupoteza kwani siku zote pesa ni mwanaharamu kwa sababu unaweza kujiona tajiri asubuhi lakini wakati wa adhana ya Magharibi ukawa masikini wa kutupwa.

Tulipofika nyumbani kwa akina Zamaradi, baba yake akaitwa na kumlipa pesa zake na hatimaye kuinunua nyumba hiyo. Kiukweli haikuwa nzuri sana kama nilivyowaeleza lakini niliamini kwamba baada ya kuwa nayo basi ningeweza kuirekebisha na kuwa moja ya nyumba nzuri sana hapa Dar es Salaam.

Wakati hayo yote yakiendelea sikuwa nimemuona Zamaradi, wakati mwingine nilijiongelesha kwa sauti kubwa ilimradi tu anisikie na kama alikuwa chumbani aje sebuleni lakini wapi.

Tulifanya biashara kwa amani kabisa na hivyo kuhitaji mwezi mmoja kwa ajili ya kujiandaa kuondoka mahali hapo. Hilo halikuwa tatizo lakini pia nikamwambia dalali kwamba nilihitaji kununua kiwanja maeneo ya Goba kwani pia nilitaka nishushe mjengo mkubwa wa kuanza maisha yangu.

Ngoja nikwambie kitu. Nilikuwa na pesa, tena nyingi mpaka wakati mwingine nilitamani sana kuombwa na mademu hivyo hii nyumba ya Sinza nilitaka niirekebishe ili iwe inatumika kwa ajili ya kulala na warembo tu, halafu ile ya Goba ambayo ningeijenga iwe ya mwanamke mmoja tu ambaye angekuja na kuwa mke wangu.

Tulipoondoka tu, nikampigia simu Zamaradi na kuongea naye, nilimwambia kwamba nilitoka kwao, aliniambia kuwa alikwenda kwa mama yake mdogo aliyekuwa akiishi Temeke ila angerudi muda si mrefu.

“Nije nikufuate?” nilimuuliza.
“Wapi? Huku Temeke?”
“Yaap!”
“Nimetoka! Sasa hivi nipo hapa Veta!” alinijibu.
“Hebu naomba uteremke hapo Ilala Boma mamii!”
“Wewe upo hapo?”

“Hapana ila nitafika kabla yako!” nilimwambia harakaharaka.
“Halafu!”
“Nataka tukae hapo Lamada tuongee kidogo,” nilimwambia.

“Sawa love.”
Akakata simu, nilihisi mwili wangu kama ukimwagiwa maji ya baridi, sikuamini mtoto angenikubalia kirahisi namna ile, nguvu ya pesa ilikuwa kubwa kupita kawaida.
 
SEHEMU YA 38

Haraka sana nikaelekea kwenye kijiwe cha bodaboda na kutaka kuchukua moja ya kuniwahisha haraka sana kwani kutoka hapo Veta mpaka Ilala hakukuwa mbali, kazi kwangu kutoka huku Sinza mpaka hapo Ilala.

“Oya! Nataka unipeleke Ilala Boma,” nilimwambia dereva mmoja.
“Haina noma! Pakia!”
“Unajua kuendesha kwa kasi? Nataka niwahi!”
“Wewe tu braza!”

“Basi kama vipi, hakikisha hii pikipiki inapaa,” nilimwambia sentensi ambayo ilimaanisha nilikuwa na haraka kupita kawaida.

Nilichomwambia ndicho alichokifanya, alikuwa na haraka kupita kawaida. Aliendesha pikipiki mpaka huku nyuma nikahisi kwamba huo ndiyo ungekuwa mwisho wangu, na pesa zangu ningeziacha benki.

Baada ya dakika tano hivi tukafika Ilala Boma, nikateremka, nikamlipa elfu kumi na kumwambia abaki na chenji wakati mimi nikiingia ndani ya Hoteli ya Lamada ambapo nikaelekea mapokezi na kuchukua chumba.

“Nataka kile cha bei ya juu kabisa. Si mna VIP hapa?” niliuliza.
“Ndiyo!”
“Naomba,” nilimwambia.

Haraka sana nikapewa, wakati nikielekea juu, Zamaradi akanipigia simu na kuniambia kwamba tayari alifika hapo Ilala Boma, nikamwambia aje hapo hotelini wakati nikiandaa mazingira.

Nikaingia ndani ya chumba hicho, nilipokiangalia kitanda tu, nikasisimka ile kishenzi, sikuamini kama siku hiyo nilikuwa nammaliza huyu Zamaradi kiwepesi namna ile.

Nikakilalia kwanza ili nijue kina uwezo gani, nikakukuruka hapo kitandani nikaona uwezo wake mzuri hivyo nikamsubiri.

Baada ya dakika kadhaa simu ikapigwa kwa kuwa niliacha maelekezo kuhusu yeye pale mapokezi, nikaipokea na kuhitaji niletewe mpaka chumbani, nikaletewa.

Nilipomuona Zamaradi akiingia, mapigo yangu ya moyo yakaanza kudunda kwa nguvu, nilipagawa, niliweweseka kupita kawaida. Kwa jinsi alivyokuwa amefungasha nikaona leo ilikuwa ni shida mahali hapo.

Kwanza kwa mbwembwe nikamfuata na kumshika kiuno, nikamvutia kwangu na kuupeleka mdomo wangu sikioni kwake na kumnong’oneza.

“Leo ndiyo leo! Yaani itakuwa kama nilifungwa jela miaka kumi,” nilimwambia kwa sauti ndogo na ya kunong’oneza sikioni kwake.
“Una uhakika?”
“Una pumzi za mbio ndefu?” na mimi niliuliza.
 
SEHEMU YA 39

“Zinatosha za kukimbia kutoka hapa mpaka Mlandizi!” alinijibu kwa sauti ndogo pia sikioni mwangu.

“Tuongeze mpaka Chalinze! Yaani leo mpaka zile chipsi uziite chishiiiii....na pepsi uiite peshiiiii...” nilimwambia na wote kuanza kucheka.

Kabla ya kitu chochote kile ilikuwa ni lazima umfanye msichana kuwa rafiki yako, ni kweli tulikuwa tumechati, tena sana tu lakini kulikuwa na uhitaji wa kumfanya kuwa rafiki zaidi.

Sikutaka kukurupuka, nilikuwa bingwa wa kufanya makosa sehemu zote lakini chumbani halikuwa mojawapo. Nilijua jinsi ya kutafuta urafiki kwanza, kuzungumza kana kwamba sikuwa nikihitaji kitu chochote kutoka kwake.

Tulikuwa kama marafiki wa muda mrefu, nilijitahidi alijue tabasamu langu, ajue jinsi lipsi zangu zilivyokuwa zikicheza, yaani kwa kifupi nilitaka ajue kila kitu kutoka kwangu, na auzoee mwili wangu pia.

Pale kitandani, huku tukiwa tunapiga stori, nikasimama na kuvua fulana yangu na suruali yangu kisha kuelekea bafuni kuona.

Mapenzi yalikuwa ni usafi wa hali ya juu, wakati mwingine watu waliyachukia kwa sababu wengine walitaka kuyafanya kuwa uchafu.

Nilijua kabisa kwamba mapenzi ni uchafu lakini si wa kunuka jasho wala mdomo, ilikuwa ni lazima ujiandae, ujisafishe kote halafu ndiyo uje ule uchafu wa kwenye sita kwa sita.

Hakuna siku ambayo nilioga kwa umakini kama siku hiyo, nilitoka nikiwa msafi mno na nilihisi kwamba kama ningekuwa naoga hivyo kila siku basi hata taulo lisingekuwa linachafuka.

“Vipi? Maji yapo tayari!” nilimwambia.
Akasimama na kuvua nguo zake, akabaki na ile ya ndani tu.

Nilishtuka sana, nilimwangalia huku nikiwa namtamani kupita kawaida. Wakati mwingine nilitamani hata kumrukia kwani nilichanganyikiwa kupita kawaida.

Akafungua mkoba wake na kuchukua khanga na kujifunga kisha kunigeukia na kuanza kutoa tabasamu pana.

“Kwa hiyo hapo umevaa khanga moko?” nilimuuliza huku nikitabasamu.
“Hahah! Fala sana wewe...” aliniambia huku akitoa tabasamu la mbali.
 
SEHEMU YA 40

Akaondoka na kuelekea bafuni. Kitu cha kwanza nikazima simu yangu, sikutaka nisumbuliwe, katika tukio kama hilo ulitakiwa utulie kama unanyolewa, halikutakiwa kuingiliwa na kitu chochote kile.

Alipomaliza kuoga, akatoka, akakaa kitandani na kilichotokea hapo, hakifai kuandikika mahali hapa.

Tulichukua masaa mawili, tukamaliza na kuelekea bafuni. Kila mmoja wetu alikuwa na furaha tele, sikuamini kama ningempata Zamaradi kirahisi namna hiyo, yaani kuniona jana tu, kupata sifa kwamba nilikuwa na pesa basi leo alijirahisisha na kulala naye.

Tulipomaliza kuoga tukaondoka zetu huku mtu mzima nikijisikia mwepesiiiii kiasi kwamba niliona wepesi wangu ungenifanya hata kupaa angani kama ndege.

*** Nisikilize! Mimi na Zamaradi tukawa wapenzi, alinipenda sana lakini wakati huo nilikuwa nikifikiria mambo mengine kabisa.

Alikuwa akinipigia sana simu na kuzungumza naye, alihitaji niwe na mapenzi fulani hivi ambayo sikuwa nayo kwa sababu nilijua kwamba alipenda pesa zangu na si jinsi nilivyo.

Hivyo naye nikapelekana naye kipesapesa kama alivyotaka. Wakati huo nilikuwa nikifanya mambo yangu na nyumba ile kuanza kubadilishwa taratibu.

Mpaka wakati huo siku nimemwambia Nurat ukweli, tulikuwa tukionana na kuzungumza mambo mengine lakini mambo ya kumwambia kuhusu pesa, hayakuzungumziwa kabisa.

Nilichokuwa nikimpendea Nurat ni kwamba alinithamini sana. Nilipokuwa sina pesa, alikuwa akinisaidia sana na hata siku hiyo ambayo tulionana, alijua kwamba sina pesa hivyo alinipa shilingi elfu hamsini.

Moyo wangu ukahisi kabisa kwamba huyu ndiye alikuwa msichana pekee ambaye nilitakiwa kuishi naye.

Unapompata msichana ambaye anakujua ulivyo, huna kitu, anakusaidia, huyo ni mtu muhimu sana ambaye unatakiwa kuishi naye, haijalishi wangapi watakuja mbele yako, mtu wa kwanza kabisa awe huyo anayekusaidia unapokuwa na shida.

“Edward! Hivi kwa nini tusifanye Friends With Benefits?” aliniuliza huku akiniangalia machoni kwa macho ambayo yalionyesha kabisa kunipenda na kunihitaji.
“Ndiyo nini hiyo?”
 
SEHEMU YA 41

“Yaani tunakuwa marafiki, siku nikiwa na hamu ya kufanya mapenzi, nakupigia simu, tunaonana na kufanya, hata wewe ukiwa na hamu, unanipigia nakuja na kufanya.

Tukiwa na shida tunasaidiana, tusiwe wapenzi, ukipata mpenzi, nitambulishe, sitojisikia wivu, hiyo ndiyo maana yake,” aliniambia.

Unajua nilishtuka sana! Sikuamini kama duniani kulikuwa na kitu kama hicho. Yaani uwe na msichana, awe rafiki yako halafu ukitaka kuduu naye, unampigia simu, anakuja na kumalizana halafu hamjuani mpaka siku ambayo mwingine angekuwa na hamu.

Nilimwangalia Nurat, sikummaliza hata kidogo, maneno yale hakutakiwa kuniambia mrembo kama yeye, kwa nini tufanye hivyo na wakati nilikuwa nampenda?

“Mbona umekaa kimya?” aliniuliza.
“Unajua nakupenda sana, sasa unaposema tuwe hivyo, kwa nini usinipe nafasi tu ya kuwa nawe?” nilimuuliza.

“Edward! Mimi ni Mwarabu, najua unajua matatizo yetu! Kuwaambia kwamba nimepata mpenzi, mweusi, halafu hauna pesa, hawawezi kunielewa. Tuwe kama nilivyokwambia,” aliniambia.

Nilijifikiria sana kwa sekunde kadhaa, nikajiona ni mjinga sana kama nisingekubaliana kuwa kama alivyoniambia.

Basi nikatingisha kichwa changu na kumwambia nilikuwa radhi kuwa kama alivyosema, akaniambia twende sehemu kutembea.
“Wapi?”
“Wewe twende tu.”

Kuanzia hapo nilimuona Nurat akiwa kwenye hali ya kawaida, alikuwa na mhemko kupita kiasi.

Niliogopa, mimi na Mwarabu wapi na wapi, halafu nilishasikia kwamba watu wahivyo walikuwa wabaridi, hawakuwa kama ngozi nyeusi, hivyo niliamini hata siku ambayo tungekuwa faragha nisingeweza kufurahia kabisa.

Wakati tukitembea, alikuwa akinishika mkono, nilijitahidi kuukwepesha lakini wapi. Akakodi Bajaj, tukapanda na kuondoka mahali hapo.

Humo ndani ilikuwa balaa, yaani ndiyo niliamini kwamba siku hiyo ingekuwa ni ya kwanza kulala na msichana wa Kiarabu. Mara aniegemee, mara anishike huku na kule, yaani akaanza kuuchaji mwili wangu hata kabla hatujafika huko.

Wakati mwingine nilitamani tu ghafla bin vuu tuwe chumbani kwani nilizidiwa nguvu na kuona muda wowote ule ningemwambia dereva Bajaj atupishe na mimi ningemlipa kiasi chochote alichotaka.
 
SEHEMU YA 42

Tuliondoka mpaka tulipofika chaka fulani hivi lililokuwa Sinza Kwa Remmy, tunateremka na kuelekea kwenye hiyo loji. Sikuwa nikiamini kilichokuwa kikienda kutokea, nikaanza kumkumbuka mshikaji wangu fulani ambaye kila siku alikuwa akiniuliza hivi:

“Edward! Hivi ni bora ulale na mwanamke mwenye shepu nzuri ila sura mbovu au ulale na mwanamke mwenye sura nzuri ila mbaumbau?”

Jibu langu nililokuwa nikimpa ndiyo siku hiyo nilikutana nalo kwa Nurat. Alikuwa mzuri mno lakini dada wa watu alikuwa kama kapigwa pasi nyuma.

Hii ingenisaidia mno kwa sababu wakati mwingine baada ya kuchafua sana shuka unaonekana kuchoka, sasa kama mtu sura mbaya utainjoi vipi kurudi tena, hivyo niliamini kwamba msichana akiwa na sura nzuri anakuhamasisha kukurudisha mchezoni.

Basi tukaingia, akachukua chumba na kwenda huko. Tulipofika, akakaa kitandani na kuniangalia. Nilikuwa najua sana kuigiza hasa eneo kama hilo, nilijifanya mshambuliaji nisiyelijua goli kumbe upande wa pili nilikuwa mfungaji mzuri kama Messi.

“Mbona umesimama huko. Njoo huku basi,” aliniambia, nikajifanya nyoka wa maonyesho kumbe hakujua kama nilikuwa kobra mwenye sumu kali.

“Naogopaaaa...” nilimwambia huku nikitabasamu.
“Sasa unaogopa nini? Hebu njoo,” aliniambia na kunivuta mpaka kitandani.

Kwenye mapenzi nilijifunza hivi: Hata kama ulikuwa konkodi, uwezo wa kumiliki hata wanawake watatu au wanaume watatu faragha lakini ukitaka kumdatisha mwenzio ni lazima ujifanye muoga flani, ukiguswa huku unashtuka, mara hutakitaki, mara hivi na vile.

Hiyo itamfanya hata mwenzako kuwa na hamu ya kutaka kufanikisha lengo lake, ndivyo nilivyomfanyia Nurat kiasi kwamba akahisi kama vile sikuwahi kuwa na msichana faragha.

“Baby! I just need you right now!” aliniambia kwa Kizungu, bado nikajifanya kama boya fulani hivi.

“Lakini.......”
“Shiiiiiiii...I just need you right now. I’ve been waiting for this moment, please, just give me what you’ve got,” aliniambia huku akianza kunipapasa.

“Nurat...lakiniiiiiiiii....” nilijifanya kama kujitetea.
 
SEHEMU YA 43

Mtoto wa Kiarabu hakutaka kunisikiliza, yaani alichanganyikiwa kabisa. Akaniona kuwa mgeni, akahitaji kunifundisha hesabu za 3+6 lakini cha ajabu nikamuonyesha ni jinsi gani naweza kuifanya 5y+8x na kumtafutia thamani ya x na y.

“What do you know about? Doggie?” aliniuliza huku akiniangalia.
“No! I know many of them. The 69, The Ship, variation, the pillow lift, the bum lift, over the edge, The jumping frog, legging....na nyingine nyingi,” nilimwambia huku nikimwangalia usoni.

“How do you know all of this?” aliniuliza kwa mshangao.
“I am a big fan of Kamasutra,” nilimjibu huku nikimwangalia usoni kwa macho yauliziayo ‘Nianze mimi ama wewe?’ *
*
*
*

Je, nini kitaendelea?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom