Simulizi: Namchukia Mama Yangu

Sehemu ya 19

Tuliagana na mganga na kwenda kutafuta usafiri. Kwa vile tulikuwa hatujala tulitafuta sehemu kupata kifungua kinywa cha haja na kisha nilimpeleka da Suzy kwake na kurudi zangu kwangu. Kutokana na uchovu nilipofika nyumbani nilipanda kitandani na usingizi mzito ulinichukua.
****
Nilitumia zile dawa kwa siku tatu kwa umakini mkubwa na kumaliza. Baada ya kumaliza kutumia makombe na dawa za kunywa nilikaa kusubiri matokeo ya dawa zile japokuwa sikuwa na uhakika wa kushika ujauzito kama nilivyoahidiwa na mganga.

Baada ya siku nne mzee Sambi alirudi, niliamini ule ulikuwa muda muhimu kutega mtoto. Usiku kabla ya kukutana naye mwili nilinawa dawa kwa bi mkubwa kabla ya kukutana na mwenzangu.

Nilifanya vile kisha nilikwenda kukutana na mwenzangu, niliendelea kufanya vile kwa wiki nzima huku nikiwa na matumaini madogo ya kushika ujauzito.

Mwezi ulikatika huku duka langu likiwa tayari limejazwa vitu vyote vya muhimu na kuanza kulifanyia matangazo ya kwenye magazeti na kwenye baadhi ya redio nchini.
***
Kupitiliza kuziona siku zangu kulinishtua lakini bado sikuamini kwa vile hali kama ile iliishawahi kunitokea hata nilipokuwa na mume wangu kwa kupitiliza miezi miwili, lakini mwezi wa tatu niliziona siku zangu na ziliendelea kama kawaida.

Mabadiliko ya hali yangu yalinishtua kidogo, nilimweleza mwenzangu ambaye alinishauri twende hospitali kuangalia afya yangu.

Nilikwenda hospitali na kufanya vipimo, tena nakumbuka siku ile nilikuwa na mzee Sambi. Baada ya daktari kuangalia majibu ya vipimo alivyonieleza nikapime alisema:

“Vipimo vinaonesha upo sawa, ila...”
Alishusha pumzi na kututazama usoni na kutabasamu kitu kilichonifanya nijiulize mbona anatabasamu ameona nini.

“Ila nini dokta?” mzee Sambi aliuliza wakati huo nilikuwa nimemuegemea begani.
“Hongereni.”

“Hongera ya nini?” mzee Sambi aliuliza.
“Inaonekana mambo si mabaya.”
“Kivipi?” safari ile niliuliza mimi.

“Inaonesha wewe ni mjamzito.”
“Nooo...nooo,” nilijikuta nikitikisa kichwa kukataa kama vile dokta ni muongo.
“Kwa nini unakataa?” aliniuliza akinishangaa.
“Hata siamini.”

“Kwa nini huamini.”
“Nimeitafuta sana mimba, siamini kama kweli Mungu kasikiliza maombi yangu.”
“Basi mama hongera sana kweli una ujauzito.”

“Nashukuru Mungu,” Nilisema kwa sauti ya kilio, furaha ya ujauzito ilinifanya niangue kilio cha kwikwi.

“Basi mpenzi, tumshukuru Mungu kwa kila jambo,” mzee Sambi alinibembeleza.
Baada ya maelezo ya daktari jinsi ya kuitunza mimba changa tulirudi nyumbani.

Njiani nilibakia na maswali ujauzito ule ni kudra ya Mungu au dawa za mganga mama Amina ambaye naye alimuomba Mungu?
Lakini kwa upande mwingine nilikubaliana na mama Amina ni mganga wa kweli kwa jinsi alivyonieleza ndivyo ilivyokuwa.

Nilipanga kumpelekea zawadi kubwa kwa ujauzito ule pia zawadi nyingine kama nikijifungua.

Kwa kweli ilikuwa furaha kubwa moyoni mwangu kushika ujauzito. Nilipofika nyumbani nilimjulisha da’ Suzy naye alifurahi sana, nilimsikia akipiga vigelegele upande wa pili kuonesha naye alifurahia shoga yake kupata ujauzito.

Ujauzito wangu ulifanya nigeuke malkia kwa mzee Sambi muda mwingi alihakikisha yupo karibu yangu huku akihakikisha sifanyi kazi yoyote ngumu mpaka nitakapojifungua.
Nilimfikishia taarifa mama kuhusiana na ujauzito wangu, mama alifurahi sana mwanaye kupata ujauzito. Furaha ya mama ilinifariji na kujisikia faraja moyoni mwangu.

“Mwaija angalie usirudie makosa ya awali wa kupoteza ujauzito wako,” mama alinionya.
“Mama sasa hivi nazingatia maelekezo ya madaktari ili kuifanya mimba yangu ikue vizuri.”

“Kama hivyo ni vizuri, mama yako nina hamu ya mjukuu.”
“Najua mama, tumuombe Mungu akupe mjukuu.”

“Inshaallah.”
Ukaribu wa mzee Sambi uliongezeka, muda mwingi hakucheza mbali na mimi huku akiniahidi ujauzito ukifika miezi minne angenipeleka Afrika Kusini na kukaa huko mpaka nitakapojifungua.

“Mwaija, katika kitu ambacho nilikiomba usiku na mchana basi ni hiki cha wewe kubeba ujauzito. Ujauzito ukifikisha miezi minne nakupeleka South Africa (Afrika Kusini) ambako utakaa mpaka utakapojifungua.”
“Kwani hapa kuna nini?”

“Katika kitu chenye thamani chini ya jua, ni hilo tumbo lako ambalo nataka nilitunze kuliko hata mboni za macho yangu.”

“Mpenzi unataka mtoto gani?”
“Japokuwa nataka wa kiume lakini yeyote atakayezaliwa ni zawadi yangu.”

Ukaribu wa mzee Sambi ilinifanya nikose muda wa kurudi kwa mganga kumueleza matokeo ya dawa aliyonipa ilinisaidia kushika ujauzito. Sikupenda kumweleza bwana yangu kuhusu ujauzito wangu ulipatikana kupitia kwa mganga.

Wakati huo mzee Sambi alikuwa ameninunulia Toyota Rav 4 kwa ajili ya kunipeleka popote kama hayupo. Kwa vile nilikuwa sijajua gari vizuri alinitafutia dereva kijana mmoja jirani yetu.

Muda mwingi alikuwa kijiweni nikiwa na shida nilimpigia na kuja mara moja kunisikiliza. Niliendelea kuona neema ya Mungu ikinifungukia kwa mambo yangu kuninyookea.

Miezi miwili ilikatika huku maendeleo kwenye ujenzi wangu yakipungua kasi japokuwa ilikuwa kwenye hatua za kumalizia. Mzee Sambi alinieleza nisiwe na wasiwasi muda si mrefu nyumba yangu itaisha.

Hali yangu ya ujauzito ilifanya niwe mtu wa kupumzika nyumbani hata kwenye super market yangu nilichelewa kuifungua mpaka hali yangu itakapokuwa vizuri, lakini kwa shauku ya mtoto aliyokuwa nayo mzee Sambi niliona mpaka nitakapojifungua.

Tatizo la kuchoka sana hospitali walisema tatizo la kuchoka sana litaisha baada ya ujauzito kukua, ile hali ilikuwa ya mpito. Pamoja na kuwa nachoka lakini nilipata huduma zote muhimu.

Mzee Sambi alihamia kwangu kwa wiki mbili akinieleza ameaga kwa mkewe amesafiri kikazi. Mtoto wa kike nilinenepa mbona nilideka nini nilichokitaka nikakosa.

Siku moja nikiwa nimejipumzisha nyumbani msichana wangu wa kazi alinieleza kuna mgeni nje.

“Dada kuna mgeni.”
“Mwanaume au mwanamke?”
“Mwanamke wa makamo.”
“Mwambia aingie.”

Baada ya muda aliingia mama mmoja aliyekuwa amevaa gauni la kitenge na kitenge kingine alijifunga chini na juu alitengeneza kilemba cha kitenge pia.
Vazi lile lilikuwa limempendeza sana yule mama ambaye alikuwa umri wa dada zangu.
“Karibu dada,” nilimkaribisha nikiwa nimejilaza kwenye kochi.

“Asante,” alijibu na kwenda kukaa kwenye kochi lililokuwa likitazamana na kochi langu.
“Shikamoo,” nilimwamkia huku nikijitahidi kukaa kitako.

“Marahaba, za hapa?”
“Mmh! Nzuri, karibu.”
“Asante, mzee Sambi nimemkuta?”
“Ametoka.”

“Ametoka saa ngapi?” aliniuliza huku akitembeza macho kila kona ya nyumba kama anakagua kitu.

“Asubuhi lakini hachelewi kurudi.”
“Samahani mama unatumia kinywaji gani?” msichana wangu wa kazi alimuuliza mgeni.
“Asante, situmii kitu,” mgeni alishukuru.

Nilipomuangalia kwa chati mkononi alikuwa ameshika ufunguo wa Land Cruiser VX, pia alikuwa na mkufu na hereni za dhahabu na mkononi alikuwa na pete vidole vitatu, hakika yule mama alikuwa anaonekana ni mtu mwenye maisha mazuri.

“Mama yangu ungekunywa hata juisi basi,” nilimbembeleza mgeni.

“Usihofu, siku nyingine.”
“Ulikuwa na shida gani?”
“Aah! Basi nitaonana naye.”
“Kwa hiyo akija nimwambie nani aliyekuja?”
“Nitamuona tu wala usihofu, naomba niwakimbie.”

“Japokuwa hukutaka kutuambia wewe ni nani, nikuruhusu dada yangu.”
Yule mama alinyanyuka na kutoka na kuniacha nikimsindikiza kwa macho. Baada ya kutoka nilijiuliza yule ni nani aliyekuja kumuuliza mzee Sambi.

Alikuwa mtu wa kwanza kuja kumuulizia mzee Sambi toka nihamie pale, wazo la haraka lilikuwa labda mwenye nyumba ambaye nilielezwa ni mwanamke alikuwa hakai maeneo yale.

Nilijiuliza alikuwa na shida gani ikiwa kodi yake alilipwa ya mwaka mzima. Niliachana naye na kuendelea na yangu.
Muda mfupi baada ya yule mama kuondoka, aliingia mzee Sambi. Kama kawaida nimpokea kwa kujilazimisha huku akinikataza kunyanyuka.

“Aah! Tulia unaenda wapi mpenzi?”
“Mpenzi unafikiri nisipofanya mazoezi nitalemaa si ulimsikia daktari.”
“Asubuhi si ulifanya, pumzika sitaki uteseke.”
“Sawa, lakini kukupokea ni moja ya mazoezi siyo mateso.”

“Haya mpenzi.”
Baada ya kupumzika nilimweleza ugeni uliofika kumuuliza muda mfupi kabla hajarejea.
“Mpenzi kuna mtu alikuja kukuulizia.”

“ Mtu?”
“Ndiyo.”
“Alikuja kuniulizia hapa?”
“Ndiyo.”
“Mmh! Mtu gani aliyekuja kukuuliza hapa?”
“Kuna mama mmoja alikuja kukuuliza inawezekana ni mwenye nyumba wako.”

“Mmh! Ana shida gani namba yangu ya simu si anayo!”
“Mi nitajuaje.”
“Amesemaje?”
“Amesema mtaonana baadaye.”

“Akuacha ujumbe wowote?”
“Hakuacha.”
“Kwani yupo vipi?”
“Mrefu mweusi amevaa kitenge kuanzia juu mpaka chini.”
“Ana mwanya?”
“Ndiyo.”

“Na ana meno mawili ya dhahabu?”
“Ndiyo, una mfahamu?”
“Ndiyo.”
“Ni nani?”
“Achana naye ni mwenye nyumba.”
“Sasa mbona amekuja bila taarifa?”
“Nitaonana naye, kama ana shida lazima atanipigia tu.”

“Mmh! Inaonekana mwenye nyumba hanajipenda sana.”
“Kawaida, baada ya kuniuliza ukamjibu sipo alisema kitu gani kingine?”
“Amesema mtaonana.”

“Basi hilohilo tu?”
“Ndiyo.”
“Mmh! Sawa.”
“Kwani vipi mbona kama umeshtuka?”
“Kawaida tu.”

Sikutaka kumuuliza sana niliamini yule ni mama mwenye nyumba wake. Usiku wa siku ile aliniaga kurudi kwake japokuwa alipanga kurudi kwake siku ya pili jioni.
“Vipi mbona ghafla,” nilimuuliza.
“Hapana kesho nitarudi.”

Pia sikutaka kumzuia kwa vile nilikuwa naye kwangu kwa wiki moja na nusu kitu ambacho kilikuwa hakijatokea, siku za nyuma alikuwa akilala mara mojamoja na kuondoka siku ya pili.
***
Aisee story tamu sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sehemu ya 20

Pia sikutaka kumzuia kwa vile nilikuwa naye kwangu kwa wiki moja na nusu kitu ambacho kilikuwa hakijatokea, siku za nyuma alikuwa akilala mara mojamoja na kuondoka siku ya pili.
***
Ilikuwa ajabu baada ya mzee Sambi kuondoka ilipita wiki bila kufika kwangu kitu ambacho hakikuwa kawaida yake. Baada ya wiki moja ndipo alikuja. Vilevile sikutaka kumuuliza niliamini ni mihangaiko pia nilizingatia ni mume wa mtu.

Siku aliyokuja tulikutana kimwili usiku majira ya saa tano aliondoka kwenda kwake. Nilala vizuri mpaka asubuhi wakati huo nilikuwa nalala na msichana wa kazi kwa ajili ya msaada wa usiku.

Siku ya pili nilipoamka nilipokwenda kuoga nilishtuka kukuta kwenye nguo ya ndani kuna damu kidogo. Haikunishtua sana japokuwa nilijiuliza damu ile inatokana na nini.
Sikutaka kukaa kimya nilimjulisha mzee kuhusiana na hali niliyojikuta asubuhi.

“Mmh! Au jana nimetumia sana nguvu?”
“Walaa, kawaida, mbona nipo sawa tu ila kilichonishtua ni damu kidogo kwenye nguo ya ndani.”
“Unasikia mabadiliko yoyote mwilini?”
“Nipo sawa.”

“Fanya hivi fika hospitali mara moja mi nitakuja baadaye ila nijulishe maendeleo yako.”
“Hakuna tatizo.”
“Basi fanya hivyo.”

Baada ya kuzungumza na mzee wangu nilioga na kumpigia dereva aliyekuwa akisaidia kunipeleka popote kwa vile nilikuwa sijajua vizuri gari pia hali yangu ya ujauzito.

Baada ya kufika nilimweleza anipeleke hospitali. Sele alinipeleka mpaka hospitali ya Madona iliyopo Tabata Aroma. Nilipofika nilimweleza daktari hali niliyokutana nayo asubuhi ambaye alishtuka sana.

Lakini baada ya kunifanyia vipimo ilionesha hakukuwa na athari zozote kwenye ujauzito wangu.

Alinipa dawa na kunieleza nisifanye kazi yoyote ngumu kwa kipindi kile. Nilimshukuru Mungu kukuta ujauzito wangu upo salama. Jioni alipokuja mzee Sambi nilimweleza niliyo elezwa hospitali kuhusu ujauzito wangu.
“Nina wasiwasi jana labda nilitumia nguvu bila kujua.”

“Mmh! Labda, sasa tutafanyaje?”
“Itabidi tuvumilie mpaka hali itakapokuwa sawa.”

Tulikubaliana kutokutana kimwili kwa kipindi kile. Kwa vile muda wake wa kuwepo kwangu uliisha saa nne usiku aliondoka. Kama kawaida niliendelea kulala na msichana wangu wa kazi ambaye alikuwa mtu muhimu sana kwangu hasa kwa kipindi kile.

Siku ya pili nilipoamka kabla ya yote niliangalia nguo yangu ya ndani na kukuta tena damu kidogo. Lakini ya siku ile ilizidi kidogo ya jana yake.

Nilishtuka sana na kumpigia simu daktari mmoja shoga yangu aliyekuwa serikalini pia alikuwa akifanya kwenye hospitali ya ‘private’ ambaye tulianza naye urafiki nilipokuwa dukani.

Baada ya kuita kwa muda ilipokelewa upande wa pili, nilimweleza hali yangu, naye alishtuka baada ya kumweleza mi’ ni mjamzito lakini natoka damu kidogo hasa usiku nikilala na ninapoamka asubuhi hukuta hali ile.

“Unataka kuniambia baada ya kuiona hiyo damu huendelea kutoka kama upo kwenye siku zako?”

“Hapana, ikitoka mara moja basi mpaka siku ya pili asubuhi kitu ambacho sikielewi.”
“Unasema ya leo imezidi kidogo tofauti na ya jana?”

“Ndiyo.”
“Mmh! Itakuwa nini? Mtu uwe na ujauzito damu zitoke, kuna kitu chochote ulichokifanya ambacho kinaweza kusababisha hali hiyo?”
“Juzi usiku nakumbuka nilikutana kimwili na mwenzangu.”
“Hamkutumia nguvu katika tendo?”
“Wala kawaida tu.”

“Tumbo unalisikiaje?”
“Lipo kawaida tu.”
“Haliumi?”
“Haliumi.”
“Hebu njoo hospitali mara moja tufanye uchunguzi wa kina.”

“Sawa nakuja.”
Nilikata simu na kumueleza msichana wangu wa kazi hali iliyonitokea, ambaye jana yake sikumweleza ile hali. Baada ya kumweleza alishtuka.

“Dada kuwa makini damu itatoka vipi ikiwa tayari una ujauzito, tumbo linauma?” naye aliniuliza kama daktari.

“Walaa.”
“Sasa kitakuwa nini?”
“Hata najua naona maluweluwe tu.”
“Unasema jana ulikwenda hospitali na kusema hakuna tatizo, basi hebu isikilizie hali na leo kama itazidi basi urudi hospitali,” alinipa ushauri.

“Hapana kuna daktari wangu mmoja alinieleza niende leo.”
“Dada kama kurudi si ungerudi kwa daktari aliyekutibu jana kuliko kubadili daktari?”
“Siyo mbaya siendi kwenye tiba bali kufanya uchunguzi wa kina ili kujua hali hii inasababishwa na nini.”

“Kama ni hivyo hakuna tatizo.”
“Wacha nimjulishe shemeji yako”
“Bado hujamwambia?”
“Bado nilitaka kwanza kupata maelezo ya kitaalamu kwa vile ilinitisha.

Kwa vile natoka nitampigia na Sele aje anichukue.”
Nilimpigia simu mzee Sambi na kumweleza hali iliyonitokea asubuhi alishtuka na kunieleza nirudi hospitali.
“duh! Sasa ni nini hicho?”
“Yaani hata mwenyewe nashangaa.”

“Tumbo linauma?”
“Lipo kawaida.”
“Basi ungerudi Madona.”
“Nakwenda kwa Dokta Hindu.”
“Si mbaya inabidi afanye vipimo vya kina ili tujue tatizo nini na tiba yake ifanyike haraka.”

“Sawa mpenzi.”
Nilikata simu na kumpigia dereva anifuate asubuhi ile. Nilikwenda kuoga na kujiandaa kwenda hospitali. Baada ya kufungua kinywa nilielekea kwa dokta Hindu aliyekuwa mtaalamu wa magonjwa ya wanawake.

Nilisahau kuwaeleza kitu kimoja kuhusu da’ Suzy wakati huo alikuwa amepata bwana na kuamua kuacha kazi pale super market. Kitu kingine kilichosababisha aache kazi kilikuwa ugomvi kati yake na Meneja Emma bwana yake wa zamani waliyeachana.

Kutokana na habari nilizopewa Meneja Emma baada kujua da’ Suzy ana bwana mwingine tena mwenye uwezo ambaye alikuwa akimpitia baada ya kazi kama mwanzo wangu na mzee Sambi roho ilimuuma.

Kitendo kile kilimuumiza sana Emma na kutaka kutumia ubosi wake kurudisha uhusiano wa zamani kitu kilichosababisha usumbufu kwa da’ Suzy na kuamua kuacha kazi.

Hata baada ya kuacha kazi bado aliendelea kupata usumbufu toka kwa Emma wa kupigiwa simu bila kuzingatia yupo wapi na nani. Pia alikuwa akimtumia ujumbe wa vitisho kitu kilichosababisha kubadili namba yake ya simu ambayo mimi sikuwa nayo.

Taarifa hizo nakumbuka nilipewa na mmoja ya wasichana tuliokuwa tunafanya kazi pamoja aliyekuwa akiendelea na kazi.

Kwa kipindi kile sikuwa na shida naye kwa vile nilijua ana namba yangu lazima angenipigia na kunipa michapo mizima. Niliamini alichokifanya kilikuwa na maslahi kwake.

Baada ya dereva kuja alinichukua na kunipeleka hospitali. Nilipofika nilikuta wagonjwa wengi nilisubiri kwa saa nzima ndipo nilipopata nafasi ya kuonana na dokta Hindu.
 
Sehemu ya 20

Pia sikutaka kumzuia kwa vile nilikuwa naye kwangu kwa wiki moja na nusu kitu ambacho kilikuwa hakijatokea, siku za nyuma alikuwa akilala mara mojamoja na kuondoka siku ya pili.
***
Ilikuwa ajabu baada ya mzee Sambi kuondoka ilipita wiki bila kufika kwangu kitu ambacho hakikuwa kawaida yake. Baada ya wiki moja ndipo alikuja. Vilevile sikutaka kumuuliza niliamini ni mihangaiko pia nilizingatia ni mume wa mtu.

Siku aliyokuja tulikutana kimwili usiku majira ya saa tano aliondoka kwenda kwake. Nilala vizuri mpaka asubuhi wakati huo nilikuwa nalala na msichana wa kazi kwa ajili ya msaada wa usiku.

Siku ya pili nilipoamka nilipokwenda kuoga nilishtuka kukuta kwenye nguo ya ndani kuna damu kidogo. Haikunishtua sana japokuwa nilijiuliza damu ile inatokana na nini.
Sikutaka kukaa kimya nilimjulisha mzee kuhusiana na hali niliyojikuta asubuhi.

“Mmh! Au jana nimetumia sana nguvu?”
“Walaa, kawaida, mbona nipo sawa tu ila kilichonishtua ni damu kidogo kwenye nguo ya ndani.”
“Unasikia mabadiliko yoyote mwilini?”
“Nipo sawa.”

“Fanya hivi fika hospitali mara moja mi nitakuja baadaye ila nijulishe maendeleo yako.”
“Hakuna tatizo.”
“Basi fanya hivyo.”

Baada ya kuzungumza na mzee wangu nilioga na kumpigia dereva aliyekuwa akisaidia kunipeleka popote kwa vile nilikuwa sijajua vizuri gari pia hali yangu ya ujauzito.

Baada ya kufika nilimweleza anipeleke hospitali. Sele alinipeleka mpaka hospitali ya Madona iliyopo Tabata Aroma. Nilipofika nilimweleza daktari hali niliyokutana nayo asubuhi ambaye alishtuka sana.

Lakini baada ya kunifanyia vipimo ilionesha hakukuwa na athari zozote kwenye ujauzito wangu.

Alinipa dawa na kunieleza nisifanye kazi yoyote ngumu kwa kipindi kile. Nilimshukuru Mungu kukuta ujauzito wangu upo salama. Jioni alipokuja mzee Sambi nilimweleza niliyo elezwa hospitali kuhusu ujauzito wangu.
“Nina wasiwasi jana labda nilitumia nguvu bila kujua.”

“Mmh! Labda, sasa tutafanyaje?”
“Itabidi tuvumilie mpaka hali itakapokuwa sawa.”

Tulikubaliana kutokutana kimwili kwa kipindi kile. Kwa vile muda wake wa kuwepo kwangu uliisha saa nne usiku aliondoka. Kama kawaida niliendelea kulala na msichana wangu wa kazi ambaye alikuwa mtu muhimu sana kwangu hasa kwa kipindi kile.

Siku ya pili nilipoamka kabla ya yote niliangalia nguo yangu ya ndani na kukuta tena damu kidogo. Lakini ya siku ile ilizidi kidogo ya jana yake.

Nilishtuka sana na kumpigia simu daktari mmoja shoga yangu aliyekuwa serikalini pia alikuwa akifanya kwenye hospitali ya ‘private’ ambaye tulianza naye urafiki nilipokuwa dukani.

Baada ya kuita kwa muda ilipokelewa upande wa pili, nilimweleza hali yangu, naye alishtuka baada ya kumweleza mi’ ni mjamzito lakini natoka damu kidogo hasa usiku nikilala na ninapoamka asubuhi hukuta hali ile.

“Unataka kuniambia baada ya kuiona hiyo damu huendelea kutoka kama upo kwenye siku zako?”

“Hapana, ikitoka mara moja basi mpaka siku ya pili asubuhi kitu ambacho sikielewi.”
“Unasema ya leo imezidi kidogo tofauti na ya jana?”

“Ndiyo.”
“Mmh! Itakuwa nini? Mtu uwe na ujauzito damu zitoke, kuna kitu chochote ulichokifanya ambacho kinaweza kusababisha hali hiyo?”
“Juzi usiku nakumbuka nilikutana kimwili na mwenzangu.”
“Hamkutumia nguvu katika tendo?”
“Wala kawaida tu.”

“Tumbo unalisikiaje?”
“Lipo kawaida tu.”
“Haliumi?”
“Haliumi.”
“Hebu njoo hospitali mara moja tufanye uchunguzi wa kina.”

“Sawa nakuja.”
Nilikata simu na kumueleza msichana wangu wa kazi hali iliyonitokea, ambaye jana yake sikumweleza ile hali. Baada ya kumweleza alishtuka.

“Dada kuwa makini damu itatoka vipi ikiwa tayari una ujauzito, tumbo linauma?” naye aliniuliza kama daktari.

“Walaa.”
“Sasa kitakuwa nini?”
“Hata najua naona maluweluwe tu.”
“Unasema jana ulikwenda hospitali na kusema hakuna tatizo, basi hebu isikilizie hali na leo kama itazidi basi urudi hospitali,” alinipa ushauri.

“Hapana kuna daktari wangu mmoja alinieleza niende leo.”
“Dada kama kurudi si ungerudi kwa daktari aliyekutibu jana kuliko kubadili daktari?”
“Siyo mbaya siendi kwenye tiba bali kufanya uchunguzi wa kina ili kujua hali hii inasababishwa na nini.”

“Kama ni hivyo hakuna tatizo.”
“Wacha nimjulishe shemeji yako”
“Bado hujamwambia?”
“Bado nilitaka kwanza kupata maelezo ya kitaalamu kwa vile ilinitisha.

Kwa vile natoka nitampigia na Sele aje anichukue.”
Nilimpigia simu mzee Sambi na kumweleza hali iliyonitokea asubuhi alishtuka na kunieleza nirudi hospitali.
“duh! Sasa ni nini hicho?”
“Yaani hata mwenyewe nashangaa.”

“Tumbo linauma?”
“Lipo kawaida.”
“Basi ungerudi Madona.”
“Nakwenda kwa Dokta Hindu.”
“Si mbaya inabidi afanye vipimo vya kina ili tujue tatizo nini na tiba yake ifanyike haraka.”

“Sawa mpenzi.”
Nilikata simu na kumpigia dereva anifuate asubuhi ile. Nilikwenda kuoga na kujiandaa kwenda hospitali. Baada ya kufungua kinywa nilielekea kwa dokta Hindu aliyekuwa mtaalamu wa magonjwa ya wanawake.

Nilisahau kuwaeleza kitu kimoja kuhusu da’ Suzy wakati huo alikuwa amepata bwana na kuamua kuacha kazi pale super market. Kitu kingine kilichosababisha aache kazi kilikuwa ugomvi kati yake na Meneja Emma bwana yake wa zamani waliyeachana.

Kutokana na habari nilizopewa Meneja Emma baada kujua da’ Suzy ana bwana mwingine tena mwenye uwezo ambaye alikuwa akimpitia baada ya kazi kama mwanzo wangu na mzee Sambi roho ilimuuma.

Kitendo kile kilimuumiza sana Emma na kutaka kutumia ubosi wake kurudisha uhusiano wa zamani kitu kilichosababisha usumbufu kwa da’ Suzy na kuamua kuacha kazi.

Hata baada ya kuacha kazi bado aliendelea kupata usumbufu toka kwa Emma wa kupigiwa simu bila kuzingatia yupo wapi na nani. Pia alikuwa akimtumia ujumbe wa vitisho kitu kilichosababisha kubadili namba yake ya simu ambayo mimi sikuwa nayo.

Taarifa hizo nakumbuka nilipewa na mmoja ya wasichana tuliokuwa tunafanya kazi pamoja aliyekuwa akiendelea na kazi.

Kwa kipindi kile sikuwa na shida naye kwa vile nilijua ana namba yangu lazima angenipigia na kunipa michapo mizima. Niliamini alichokifanya kilikuwa na maslahi kwake.

Baada ya dereva kuja alinichukua na kunipeleka hospitali. Nilipofika nilikuta wagonjwa wengi nilisubiri kwa saa nzima ndipo nilipopata nafasi ya kuonana na dokta Hindu.
Mmh jmn nini tena nlipata furaha kama mimba ninayo mie!

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom